Huu ni utenzi maarufu uliokuwa ukisomwa na Sheikh Said bin Ahmed katika miaka ya sitini
baada ya kila akimaliza mawaidha yake katika
kipindi chake cha dini katika Idhaa
ya wilaya ya pwani ya
Kenya Broadcasting Service -
DUA
Twakuomba mtukufu - Aso kijana na kufu
Mola wetu maarufu - Allahu ulo Karima
Mikono tumeinuwa - Mola wetu watujuwa
Taqabali zetu dua - Utupe lilo
na wema
Mola matozi yatoka - Hakika yabubujika
Tumetubu kwa
hakika - Waja wako tumekoma
Ya Rabbi tupe elimu - Utupe njema
fahamu
Ya kutambua vigumu
- Vya dini yako Karima
Utupe matunda yake - Tuisome tusichoke
Mola elimu iweke - Moyoni mahala pema
Rabbi
ijapo hukumu
- Isiwe kwetu ni ngumu
Tusiweze kudhulumu - Tukuche wewe Karima
Utupe na
kupendana - Sisi na wetu vijana
Mapenzi yaso khiana - Yalo mazuri
daima
Tutuze mijini mwetu - Tuqidhie deni zetu
Kabila ya kuja
kwetu - Mjumbe wa mauti
mwema
Kula
ajae na
shari - Waijua yake siri
Ivunde yake dhamiri - Asiweze kusimama
Rabbi
sala na
salamu - Zimfikie hashimu
Na
swahabaze kiramu - Na aali na kila mwema
Amina Rabbi amina
- Amina Rabbi amina
Amina Rabbi amina
- Ya Rabbi watusikia