Assalaam Alaykum,
Shairi lifuatalo linaloitwa
TUJITAHIDI NA SUNNA ni katika jumla ya
mashairi yaliyotungwa na Sh. Khamis
bin Nassor Al-Nabhany, Mola amrehemu.Shairi hili alilitunga baada ya kuona
kijijini kwao vijana wengi wameshiriki
ulevi
TUJITAHIDI NA SUNNA
Wazee na
as-habu, Akh-wa na ukhtina
Nimeandika kitabu, Kiasi kukumbushana
Kidogo nimekutubu, Si ila kuambizana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Faradhi iwe kamili, Tujitahidi na sunna
Tufunge tena tusali, Kwa usiku
na mchana
Na tukimiliki
Tujitahidi na
sunna, Tukamilisha faradhi
Aidha zaka tutowe, Kwa amri
ya Rabbana,
Walokhusika wapewe, Bila ya kupendeleana
Kwa kipimo wagawiwe, Pasi kudhulumiana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Tukae tukikumbuka, Kua uhai hapana
Wengi waliotutoka, Wala hawarudi tena
Jambo jema la kushika, Ni kumtii Rabbana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Tunyanyueni mikono, Tukisikia adhana
Tusali na
sala tano, Na dua kuombeana
Tuombe masikizano, Jamii muuminina
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Tujitahidi na
dini, Ndio jambo la maana
Na sadaka
tutoweni, Ina ubaya khiyana
Tumlaani shetani, Laanahul mal-una
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Tuitambuwe dunia, Kua si kubwa
ni duna
Hii dunia ni njia,
Twapita si maskana
Dunia yatuzomea, Na
huku yatutafuna
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Pana safari lazima,
Kubwa mfano haina
Sote inatuandama, Aasi na msalihina
Habakii mtu nyuma, Babu na baba na
mwana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Soteni lazima kwenda, Mbele yake Subhana
Kila tuliyoyatenda,
Wenyewe tutayaona
Mwenye
Tujitahidi na sunna, Tukamilishe faradhi
Dhalimu na
madhulumu, Walo wakikopeshana
Wakae wakifahamu, Siku ya kwenda
kutana
Wanaekewa zakumu, Chakula cha kulishana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Wako wapi
watukufu, Walokuwa na majina
Ambao ni
maarufu, Na sote tukiwaona
La mwisho
ni udhaifu,
Hali zao hairana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Waliokuwa na
raha, Wanangiwa na mahana
Wote wapiga siyaha, Kina wakiambiana
Hayupo mwenye furaha, Jamii wanadangana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Tuwatazame wazuri, Walio wakijivuna
Maringo na
ujeuri, Fedhuli na kujiona
Unakwisha uhodari, La kulifanya hawana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Wako wapi
maridadi, Wa
vikoi na fulana
Kwenda huku wakirudi, Na kujiona wapana
Sasa hawajisafidi,
Unawapata mdhana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Iwapi ile suhuba, Watu kutemebleana
Kila wendapo washiba, Karamu kupikiana
Jamii wapiga toba, Na wote ni mahuzuna
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Tuwatazame walevi, Waliowakilevyana
Na ukali
Unawishia ujuvi, Khatima wachukiana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Ndugu zangu nawambia,
Ni kali mno dunia, Yauma
tena yabana
Atakaeichezea, Ajuwe watapambana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Kuna adhabu
akhera, Ya
namna kwa namna
Toba ya Rabbi sitara, Allahu
mustaana
Tuombeni maghfira, Kwa Rabbil-aalamina
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Niliyowahadithiya, Ni ya kweli si ya
dhanna
Kwa maneno yangu haya, Ni kama kuzinduana
Na iwapo
ni mabaya,
Nawaomba samahana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
Tammati sina la kwamba, Ni bora tatulizana
Lakini radhi naomba, Kwa wazee
na vijana
Musije mukanigomba, Ikawa kununiana
Tujitahidi na
sunna, Tukamilishe faradhi
.