RAMADHANI HUFUTA MADHAMBI YALIYOTANGULIA
Suleyman
Mohammad Said
Amesema Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam);
“Mwenye kufungaRamadhani kwa imani na
kwa kutaraji kupata thawabu, husamehewa madhambi yake yaliyotangulia”.
Pia amesema Mtume
(Swallah Llahu alayhi wa sallam);
“ Mwenye kusimama ramadhani (kwa
kusali ) kwa imani na kwa kutaraji kupata thawabu husamehewa madhambi yake
yaliyotangulia”.
Na amesema Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam);
“ Mwenye kusimama (kwa kusali ) usiku
wa Laylatul Qadri kwa imaani na kutaraji kupata thawabu basi atasamehewa
madhambi yaliyotangulia”.
Pia amesema Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) katika hadithi tofauti kuwa mwezi huu
wa Ramadhani ni mwezi ambao hufunguliwa milango ya pepo na hufungwa milango ya
moto na mashetani hufungwa, pia hufunguliwa milango ya rehma na milango ya
msamaha.
Hizi ni baadhi ya fadhila za mwezi huu na kila
muislam anatakiwa ajihimu katika msimu huu wa kheri ili aingie katika wale
watakaopata rehma na kusamehewa madhimbi
Na sababu za kusamehewa kama tulivyo
elezwa katika hadithi za Bwana Mtume Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam), kwa mwenye kufunga na
kusali usiku, na sala inayokusudiwa hasa ni sala ya Tarawehe, hivyo watu
wajihimu kusali sala hii adhimu ambayo ni zawadi kwetu na haipatikani fursa ya
kuisali sala hii isipokuwa katika Ramadhani na rakaa zake kwa ukamilifu ni
ishirini na kadri mtu anapoozisali sala za usiku nyingi iwe tarawehe kisha
akasali tahajudi na witri basi fadhila za mtu huyo huzidi na mtu huyo
huhesabika ameifahamu maana ya Ramadhani.
Ama yule anayelala tu baada ya futari
na sala zote za usiku kumpita, basi ni mwenye kupata khasara kubwa, kwani
amejiharamishia mwenyewe fadhila za mwezi huu.
Jambo la mazingatio zaidi ni kuhusu nia
ya huyo anayefanya ibada hizi kwani katika hadithi tulizokwisha zizungumza
zimeweka bayana juu ya atakayepata atayetimiza suna mbali mbali na kumwekwa
sifa za huyo anayefanya ibada hizi kisha akasemehewa madhamb iyake, na sifa
zenyewe ni :
Kuamini Mwenye kufanya hayo kwa
kumuamnini Mola wake nayo ni kuzifanya amali hizo kwa ajili ya Allah tu si kwa sababu
watu wamuone na kumzungumza kuwa fulani nimcha Mungu basi atakapoepukana na
riya ndipo ataingia katika wale watakaosamehewa. Zaidi ya hayo ni kule
kujiepusha na maasi, kwa sababu kadri mja anapomuasi Mola wake ndipo anapokuwa
mbali nae katika kukubaliwa maombi yake
Kutaraji kulipwa thawabu.
Muumini wa kweli ni yule anayefanya
ibada hali ya kuwa moyo wake umetulizana
na kuwa na yakini kuwa ile ibada
aifanyayo atalipwa na Mola wake thawabu wala kutokuwa na shaka atapata malipo
ama hapati? Hivyo mja anatakiwa ataraji kupata malipo kutokana na ibada
azifanyazo hata zikiwa ni ndogo na khasa
katika mwezi
Mja vile vile atatakiwa afuate shuruti
za toba nazo ziko nyingi, na kwa ufupi asifanye tena madhambi yake na anuwie
kuacha kabisa, vile vile awe na unyenyekevu na kuonyesha kujuta kwake mbele ya
Mola wake juu ya yale madhambi aliyoyafanya na
Ewe Mola tusamehe madhambi
yetu na turehemu kwa hakika wewe ni mwenye kurehemu waja wako. “Amin”