Assalaam
Alaykum,
Ufuatao
ni
utenzi unaoeleza kisa
cha mtume wa
Mwenyezi Mungu,
Seyyidna Ayyub ALAYHIS
SALAAM. Utenzi huu
umetungwa
na:
Mwinyi
Muhammad Abdulla Shatry
wa
Lamu.
UTENZI WA KISA CHA
NABII AYYUB (A.S.)
1.
Bismillahi Qadimu,
Arrahmani Rahimu,
Mwenye enzi
ya kudumu,
Muumba ndiwe
Jalia
2.
Uloumba ulimwengu,
Arshi juu
ya mbingu,
Ukapanga
na mafungu,
Waja kuwamiminia
3.
Aridhi ukatandika,
Ziumbe ukawaweka,
Hukuwa na
mshirika, Ni kazi
yako Moliwa
4.
Ukanyesha
na mivua,
Ukalitowa na
jua, Miti
nayo ikamea,
Ikanawiri dunia
5.
Hakuna mtenda
kazi, Ila
ni wewe
muyuzi, Mwenye
mkubwa uyuzi,
Ndiwe wa
kutegemewa
6.
Ukaumba majabali,
Makubwa yaso
mithali, Ndani
yake muna
7.
Ukakusnaya milima,
Ya
mitanga ilokwima,
Meupe ukiiona, Na raha
kuyangalia
8.
Yote ni
kazi ya
Mola, Asokula
asolala, Na kwake
huna muhula,
Popote utarejea
9.
Katengeza
kwa udongo, Na
tope zenye mavundo,
Mwanadamu lake umbo,
Quruani yatwambia
10.
Ukayaweka mauti,
Kwetu sisi
ni
sharuti, Huja pasi
na wakati,
Siku zikisikilia
11.
Tahadhari mwanadamu,
Yataka ujifahamu,
Siku zikishakutimu,
Budi huna
nakwambia
12.
Ewe mja usojali,
Kumbuka huna
mahali, Mauti
hayako mbali,
Popote hukungilia
13.
Ghafula hukukabili,
Mauti hayako
mbali, Na jina
likabadili, Wendo
wakakulilia
14.
Nakuomba ndugu
yangu, Tafadhali
nisikia, Roho
si ya
ulimwengu, Hakuna cha
kubakia
15.
Wawapi wanazuoni,
Matajiri masikini, Na
wenye nguvu
wendani,
16.
Wako wapi wenye
nguvu, Akili
na
uwerevu, Hawakuwa
watukivu, Leo wameshika
ndia
17.
Mamako alihajali,
Mimba yako
kahimili, Uzito
kama
jabali, Hakushindwa
katukuwa
18.
Kwa kite kaitukuwa,
Henenda akijishuwa, Na
mangi akiongowa,
Kwa kazi
yake Karima
19.
Ukazawa mwanadama,
Huna mbele
wala nyuma,
Kakuyeya wako mama,
Kwa uwezo
wa
Karima
20.
Ulimwengu si
makazi, Kwa
kila alomuyuzi, Ni
mapito ya
wemuzi,
Ya kwenenda mui
mwema
21.
Baada haya
kunena, Nina kiswa
waungwana, Cha Ayubu
tumwa mwema,
Nimependa kukitowa
22.
Nimependa kufasiri,
Niwape zake
khabari, Nimeona
ni
uzuri, Mupate
kumuelewa
23.
Babake alitajiri,
Alina
24.
Alipokufa babake,
Kayashika
25.
Alitajiri ajabu,
Wa
majumba na dhahabu,
Na wana wenye
adabu, Mola
memruzukia,
26.
Alikuwa
na hekima, Za
fahamu ya
ilima, Na akili
zilo tama, Yote
kampa Jalia
27.
Alikuwa mahabubu,
Kwa watu
na
maswahibu, Akipendeza
Ayubu, Kwa watu
ni maridhia
28.
Uli na
nguvu muili, Na
sura zake
jamali, Na biashara
amali, Ndio
alokifanyia
29.
Kamuoa mwana
mwema, Rahama
binti Fartima,
Babu yake
nitasema, Ndie
Yusufu nabiya
30.
Ayyubu alioa, Wake
watatu sikia,
Wawili wakakimbia,
Rahama akabakia
31.
Riwaya ilopokewa,
Watoto walozaliwa, Ni
kumi kuongezewa,
na
wanane kutimia
32.
Kawaeya wake zake,
Pamoja na
wana wake, Hawakumuata
pweke, Kwa
raha na
mazowea
33.
Mkubwa mtoto wake,
Kawalika ndugu
zake, Harimala
jina
lake, Kwake akawatukua
34.
Kawapikia chakula,
Ndugu
35.
Balaa zikawafika,
Kwa msiba
ulotuka,
Ya ukuta
kuanguka, Wanawe
wakajifia
36.
37.
Ali na
mengi majumba,
bustani na
mashamba, Na wanyama
wa kutunga,
Wote hawakubakia
38.
Maradhi yalimshika,
Siku nyingi
na
miaka, Hakuwa
akipunguka. Ila
kuzidi nabiya
39.
Maradhi ya
kiajabu, Yalompata
Ayubu, Hakusaza
matibabu, Na wanaojua
dawa
40.
Mabombwe yalikitoka,
Na ngozi ikatanika,
Mkewe akashutuka,
Kamba unani
nabiya
41.
Muili hukushanuka, Na
mabombwe hukutoka,
Nawe umebadilika, Na
wazidi kwendelea
42.
Hata naona
ajabu, Yalonipata
muhibu, Ni kazi
yake Wahabu,
Ilahi yamueleya
43.
Kamba wewe
hufahama, Yalonipata
Rahama, Mitihani
ya Karima,
Nami taisubiria
44.
Maradhi ya
miujiza,
Ya ngozi yake
kuoza, Wadudu
wakitapuza, Muilini
kwa nabiya
45.
Hakuona la sahali,
Ugonjwa kauhimili,
Mkubwa ulo
thaqili, Mola
aloqadiria
46.
Rahama kamuhimili,
Kenda nae
huko mbali,
Nti yenye
majabali, Kibanda
kamjengea
47.
Kenda nae
taratibu, Kamueka
kwa
adabu, Hakusikia
dharubu, Za
mikukuto ya
ndia
48.
Kali chakula hakuna,
Wala maji
ya kunwa,
Ndaa ilipowabana,
Rahama hakungojea
49.
Kateremka mjini,
Rahama katumaini,
Tapata mwema
mwendani, Riziki
kumpatia
50.
Watu walipomuona,
Kwa umoya
wakanena, Ndoo
kwetu wata bwana,
Shere wakimtezea
51.
Rahama hakukubali,
Waloyasema rijali,
Kaomba Mola
Jalali, Amlinde
na
mabaya
52.
Ayyubu akamwita,
Kamba wewe
huniata, Ni gani wenda
tafuta, Nambiya
nipate juwa
53.
Kamba wewe
mume wangu,
Nakuapia
kwa Mungu,
Sitakutupa bwanangu,
Wala sibadili nia
54.
Kanena na
moyo wake, Ni wapi
mimi nifike,
Kakumbuka mwanamke,
Upesi akamwendea
55.
Mlango akaubisha,
Akataka kukopesha,
Nikipata tarejesha,
Kanena wangu
nabiya
56.
Mwanamke
kwa umbeja,
Kishipa kikampija,
Akanena kwani ngoja,
Lilokueta nambiya
57.
Hukuya nyumbani
kwangu,
Ila kunipa
matungu, Akuone mume
wangu, Apate
kukuridhia
58.
Rahama akamjibu,
Mwanamke
kwa ghadhabu, Nina
wangu Ayyubu,
Nilopewa na
Jaliya
59.
Mimi sitokukiridhi, Kwani
mimi
meniudhi, Una
kitu chenye
hadhi, Ukitaka
niatia
60.
Ali na
nyele safira,
Rahama zalikin'gara,
Mwanamke kwa
hasira, Makasi
kamuetea
61.
Kazikata nyee
zake, Akampa
mwanamke, Kabeba
mikate yake,
Mumewe kampekea
62.
Rahama akadhahabu,
Akafika
kwa Ayubu,
Mumewe kataghadhabu,
Maneno kimwelezea
63.
Mumewe likamkera,
Kutoa nyee
safira, Zilikua
nyee bora, Ni
ndefu zikin'garia
64.
Akamwapia Jalali,
Mbee za wake
rasuli, Si
haramu ni
halali, Chakula
nilokwetea
65.
Mla wewe
mume wangu,
Nimeuza nyee
zangu, Nimekwapia
kwa
Mungu, Maovu
kukutendea
66.
Kanena tahakikisha, Na
hadi taipitisha,
Mboko mia
takutwesha, Ninapopata
afiya
67.
Kiwa na
afiya yangu,
Tachunguza mke
wangu,
68.
Rahama akamjibu,
Kwa sitaha
na
adabu, Kwamba uovu
Ayubu, Siwezi
kukufanyia
69.
Rahama ayatamke,
Amwambie mume wake,
Amuombe Mola wake,
Mateso kumwondolea
70.
Kamwambia mke
wangu, Naona
haya kwa
Mungu, Mestarehe
na wanangu,
Ashara wa
thamania
71.
Tasubiri Mola
wangu, Na balaa
za matungu,
Maadamu moyo
wangu, Na ulimi
mebakia
72.
Na ulimi nibakishe,
Ilahi nikukumbuke,
Dudu usimuoneshe,
Ulimini kuningia
73.
Walitoka
kwa muili,
Wadudu wote wawili,
Tiati wamekabili,
Ayyubu changaliya
74. Wa
kwanza katumbukia, Mtoni
akaingia, Mai yakamtukua,
Ayyubu kionea
75.
Wa pili
kapanda
bara, Kwenye
jangwa la sahara,
Akawa mnyama bora,
Asali yake
ni dawa
76.
Hapohapo Jibrili,
Kwa Ayubu
kawasili, Yali
mikono miwili,
Kudhumani metukua
77.
Metukua kudhumani,
Metoka nayo
peponi, Amepewa
na
Manani, Ayyubu
kumwetea
78.
Ayubu katakauli,
Kamwambia Jibirili,
Menikumbuka Jalali,
Kunipa yangu
afiya
79.
Jibirili kamjibu,
Menipa Mola
Wahabu, Dawa
yako kukutibu,
Matunda ya
jannatia
80.
Akamwambia simama,
Ayyubu tumwa
mwema, Kwa
amri ya
Karima, Inshalla
utatulia
81.
Mimi nimetumwa kwako,
Nipoze ugonjwa
wako, Piga
tini guu
lako, La upande
wa
kulia
82.
Yakatoka maji
moto, Meupe
yalo mazito,
Akapowa tumwa
wetu, Maradhi
yakapungua
83.
Kamwambia Jibirili,
Upige nao
wa
pili, Wa kushoto
sikuvuli, Maji
yakaitokea
84.
Mabaridi ya
kutosha, Jibrili
kamnwesha, Mola
akamrejesha,
85.
Maradhi yake
kapona, Tumwa
akawa mzima,
Akarudi kama
zama, Kwa
uwezo wa
Jaliya
86.
Ayyubu akanawiri,
Kan'gara
87.
Riwa nyengine
hunena, Alibaki
na
Rahima, Kazaa wangine
wana, Na
88.
Haya yaliyomsibu,
Kumpata Ayyubu,
Mitihani ya
Wahabu, Nae
kaisubiria
89.
Mola anatufundisha,
Kutaka kutuonesha,
Maana ukiondeshwa,
Sibabaike sikia
90.
Uyatie akilini,
Usubiri
kwa Manani,
Ndake Mola mitihani,
Quruani yatwambia