|
|
|
|||
Utulivu
(Tumaaniyna) ni nguzo muhimu sana katika nguzo za Swala, na bila ya utulivu Swala
haiwi kamilifu.
Siku moja Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) alikuwa amekaa msikitini, akaingia mtu mmoja na kuswali. Baada ya
kumaliza akainuka na kwenda kumsalimia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam). Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
akamuambia:
“Rudi kaswali tena, wewe bado hujaswali.”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
alimrudisha mtu huyo mara tatu, na kila anapomaliza kuswali alikuwa akimuambia:
“Rudi kaswali tena, wewe bado hujaswali”.
Yule mtu akamuambia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam):
“Sijuwi kuswali vizuri kuliko hivi, (bora) nifundishe”.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
akamuambia:
“Unapotaka kuswali tia udhu, kisha elekea kibla, kisha soma
utakachoweza kusoma katika Qurani, kisha ruku-u mpaka utulie (Tumaaniyna)
na uwe na uhakika kuwa umerukuu (sawa), kisha inuka usimame sawa sawa(Tumaaniyna),
kisha usujudu mpaka utulie (Tumaaniyna) na uwe na uhakika kuwa umesujudu
sawa, kisha kaa vizuri mpaka utulie katika kikao chako(Tumaaniyna),
kisha sujudu na utulie (Tumaaniyna) mpaka uwe na uhakika kuwa umesujudu
sawa, kisha ufanye hivyo hivyo mpaka umalize kuswali”
Bukhari,
Muslim, AbuDaud, Attirmidhy, Annasai na Ibni Majah
Hadithi
hii na nyingi kama hizi zinatujulisha kuwa Swala haiwi kamili bila ya utulivu (Tuma
– aniyna). Nako ni kutulia katika kila kitendo cha Swala. Mtu anatakiwa
atulie mpaka awe na uhakika kuwa ametulia.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amempa jina la ‘Mwizi’ mtu
anayeswali bila utulivu.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Katika wezi wabaya kabisa ni wale wanaoiba katika Swala zao,
hawarukuu kwa ukamilifu wala hawasujudu kwa ukamilifu na hawawi na khushuu.”
Na
katika riwaya nyingine amesema juu ya ‘Mwizi wa Swala’:
“Na wala haunyoshi mgongo wake sawa pale anaporukuu na
anaposujudu.”
Imam
Ahmad, Al Hakim na imesahihishwa na Imam Al Dhahabi.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amekataza kudokoadokoa katika Swala.
Kwa sababu anayeswali kwa pupa bila ya utulivu anakuwa mfano wa kuku anayedokoa
mtama, na huwa haipi haki yake Swala, wala hakipi kila kitendo haki yake. Bali
hampi Mola wake haki Yake.
Kumbuka kuwa
ndani ya Swala yanapita mazungumzo baina yako na Mola wako Subhanahau wa Taala.
Katika
hadithi ambayo sehemu ya mwanzo yake ni Hadith Al Qudusiy, Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenyezi Mungu anasema;
‘Nimeigawa Swala baina yangu na baina ya mja wangu sehemu mbili, na mja wangu
(ninampa) anachoniomba’. Mja anaposema:
“ÇáúÍóãúÏõ
ááøåö ÑóÈøö ÇáúÚóÇáóãöíäó”
,MwenyeMungu Husema: “Mja wangu amenishukuru”.
Na anaposema:
“ÇáÑøóÍúãÜäö
ÇáÑøóÍöíãö”,
Mwenyezi Mungu Husema:“Mja wangu amenipa sifa yangu”.
Na anaposema:
“ãóÜáößö
íóæúãö ÇáÏøöíäö”,
Mwenyezi Mungu Husema:
“Mja wangu amenitukuza”, au Husema:“Mja
wangu amejisalimisha kwangu ”.
Na anaposema;
“ÅöíøóÇßó
äóÚúÈõÏõ æÅöíøóÇßó äóÓúÊóÚöíäõ ”,
Mwenyezi Mungu Husema:
“Haya
ni baina yangu na baina ya mja wangu na mja wangu atapata atakachoniomba.”
Na anaposema:
“ÇåÏöäóÜÜÜÜÇ
ÇáÕøöÑóÇØó ÇáãõÓÊóÞöíãó. ÕöÑóÇØó ÇáøóÐöíäó ÃóäÚóãÊó Úóáóíåöãú ÛóíÑöÇáãóÛÖõæÈö
Úóáóíåöãú æóáÇó ÇáÖøóÇáøöíäó”.
Mwenyezi Mungu husema:
“Hii ni ya mja wangu na mja wangu atapata anachoniomba”
Mtu
anapozungumza na mzee wake au mkubwa wake wa kazini au anapozungumza na mfalme
katika wafalme wa dunia, huzungumza naye kwa heshima na utulivu kubwa.
Mwenyezi
Mungu Subhanahu wa Taala anastahiki zaidi heshima na utulivu huo kuliko viumbe
hao dhaifu.
Mmoja
katika maulama amemfananisha anayeswali kwa pupa bila ya utulivu kuwa ni sawa
na mwenye kunywa dawa chungu anapoweka chungwa lake tayari apate kula mara
baada ya kunywa dawa kwa ajili ya kuuondoa uchungu wa dawa. Lakini yule
anayestarehe ndani ya Swala yake, mfano wake ni mfano wa mtu anayekunywa
kinywaji kitamu. Anakunywa taratibu, akistarehe nayo huku akitamani kinywaji
hicho kismalizike.
Mtu
anapomjuwa Mola wake, na kuzijuwa neema alizopewa, kisha akaujuwa uwezo wa Mola
wake juu yake, huyo ndiye anayemjuwa Nani anayemuabudu, na anampa heshima
anayostahiki.
Ibni l
Qayim amepiga mfano wa mtu anayemuabudu Mola wake bila ya kumpa heshima
anayostahiki kuwa ni mfano wa panya aliyemouwa ngamia, kisha akamchukuwa ngamia
huyo na kumpeleka penye tundu lake (tundu la panya) na kumtaka mkewe (ngamia)
aingie ndani humo.
Ngamia
akamwambia panya:
“Sikiliza bwana, nitafutie nyumba kiasi changu, au tafuta mke
kiasi chako”
Ibni l
Qayim alimaliza kwa kusema:
“Na hivi ndivyo ilivyo, mtu ama amuabudu Mwenyezi Mungu kama
Anavyostahiki kuabudiwa, au atafute kijiungu chake akiabudu kama anavyotaka yeye.”
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema juu ya wenye
kuichelewesha Swala ya Alasiri na kuiswali karibu na Magharibi:
“Hiyo ni Swala ya wanafiki. Anasubiri, analitegea jua mpaka
linapokuwa baina ya pembe mbili za shetani, hapo huinuka na kuzidokoa (rakaa)
nne, (ndani yake) hamtaji Mwenyezi Mungu isipokuwa kidogo sana.”
Muslim,
Attirmidhy na Annasai
Baadhi
ya watu wanao mtindo huu wa kuichelewesha Swala ya Alasiri. Wanaiacha mpaka jua
linapokaribia kutuwa, ndipo wanapoinuka na kuzidokoa raka nne za Alasiri haraka
haraka kabla ya kuadhini Magharibi kwa muda mchache sana, ili abaki na udhu
wake apate kuuswalia Magharibi.
Kumbuka
kuwa unapokuwa ndani ya Swala, unazungumza na Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu,
wakati wewe ni dhaifu. Mwenyezi Mungu Mwenye kutowa, wakati wewe ni masikini,
muhitaji. Mwenyezi Mungu Mwenye funguo zote za hazina za mbinguni na ardhini.
Kwa hivyo swali katika wakati wake na kuwa na utulivu ndani yake huku
ukimshukuru na kumuomba, kwani mlango Wake uko wazi wakati wote.
Kuzikosa
jamaa mbili hizi ni kujikosesha kheri nyingi sana. Watu wengi baada ya machofu
ya kazi ya mchana kutwa huona tabu kuinuka juu ya kiti au mbele ya television
na kujikokota kwenda msikitini kuswali Swala ya Isha jamaa pamoja na Waislam
wenzake. Hii inatokana na kutokujuwa umuhimu wa kuswali jamaa, pamoja na
kutokujuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema nini
kuhusu wale wasioziswali Swala hizo katika jamaa na nini wanachokikosa.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Swala nzito kwa wanafiki kuziwsali jamaa ni Swala za Isha na
Alfajiri, na lau wangelijuwa faida iliyomo basi wangelikuja hata kwa kusota”.
Muslim,
Imam Ahmad, Attabarani, Annasaiy, Ibni Majah na wengine
Na
akasema:
“Na atakayeswali Isha katika jamaa, anaandikiwa thawabu ya
aliyeswali nusu ya usiku, na atakayeziswali zote mbili katika jamaa (Magharibi
na Isha), anaandikiwa thawabu za aliyeswali usiku kucha”.
Muslim,
Ibni Hibban, Al Jamia al Kabiyr.
Katika
makosa yanayofanywa na baadhi ya wanaoswali ni kule kukimbia wanapokwenda
msikitini kwa ajili ya kuiwahi raka-a isiwapite.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amekataza kitendo
hicho pale aliposema:
“Mnaposikia Iqamah, ziendeeni Swala zenu (nendeni msikitini) kwa
utulivu na kwa uchaMungu (msiende mbio). Raka-a mtakazoziwahi swalini na
mtakazozikosa kamilisheni”.
Bukhari
na Muslim
Baadhi
ya watu wanapoingia msikitini na Imamu amesujudu au amekaa, huwa hawafungi Swala
na kuingia katika jamaa moja kwa moja. Husubiri mpaka Imamu ainuke ndipo
wanapofunga Swala na kujiunga na jamaa.
Kitendo
hicho kimekatazwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mmoja wenu anapoingia (msikitini) akamkuta Imamu amesujudu au
amekaa basi naye amfuate Imamu huyo kwa kujiunga naye katika kile kitendo
alichomkuta nacho.”
Attirmidhy
Katika
kitendo asichokipenda Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
na kilichokuwa kikimchukiza sana ni kumtangulia Imamu katika kurukuu au
kusujudu au kuinuka nk.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amemfananisha mwenye kitendo
hicho kuwa sawa na punda.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Haogopi mmoja wenu anapomtangulia Imamu akageuzwa kichwa chake
kuwa sawa na kichwa cha punda?”
Addarimy
na Ibni Majah
Na
akasema:
“Imamu amewekwa ili afuatwe. Akisema: “Allahu akbar” na nyinyi
semeni kama yeye. Anaposoma na nyinyi mumsikilize. Anaporukuu nanyi murukuu.
Anaposema: “Samia llahu liman hamidah”, semeni: “Rabana laka l hamd”. Na
anapokua amekaa nanyi nyote kwa pamoja pia kaeni (kama yeye)”.
Maimamu
wote watano isipokuwa Attirmidhiy
Na
akasema:
“Hakika mimi ni Imamu wenu. Msinitangulie
katika kurukuu wala kusujudu wala kusimama wala kutoa salamu”.
Muslim
– Ibni Khuzayma – Al Bayhaqi na wengineo
Maulamaa
wanasema kwa vile Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
katika hadithi hii ametumia neno la kiarabu ‘Idhaa’ katika kuunganisha
utaratibu wa kumfuata Imamu (FAIDHA kabbara fakabbiru wa idhaa qara-a
faansitu), akitufahamisha kuwa ni lazima tuufuate utaratibu huu bila kuchelewa.
Unapomaliza
kusoma Tahiyatu na Imamu bado hajamaliza, badala ya kukaa kimya ni bora mtu asome
baadhi ya dua alizotufundisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam).
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipoulizwa nini mtu afanye
anapomaliza kusoma tahiyatu na Imamu bado hakumaliza, akasema:
Çááøóåõãøó Åäí ÙóáóãúÊõ äóÝúÓöí ÙõáúãÇð ßóËöíÑÇð æó áÇ íóÛúÝöÑõ ÇáÐøõäõæÈó
ÅöáÇøó ÃóäúÊó¡ ÝÇÛúÝöÑú áöí ãóÛúÝöÑóÉð ãöäú ÚöäúÏößó æóÇÑúÍãúäöí Åäøóß ÃóäúÊó ÇáÛóÝõæÑõ
ÇáÑøóÍöíã"
“Sema; “Allahumma inniy dhalamtu nafsiy
dhulman kathiyraa, walaa yaghfiru dhunuuba illaa anta. Fa- aghfirliy
maghfiratan min indika warhamniy, innaka anta l ghafuwru rrahiym”
Bukhari
na Muslim
Na maana
yake ni;
“Mola wangu mimi nimejidhulumu nafsi yangu dhulma nyingi sana,
na hapana anayesamehe madhambi isipokuwa wewe, kwa hivyo nighufirie maghfira
kutoka kwako na nirehemu, hakika Wewe ni Mwenye Kusamehe, Mwenye Huruma.”
Na
katika hadithi nyingine akasema:
“Mtu anapomaliza kusoma tahiyatu na Imamu bado hajamaliza na
asome:
Çááøóåõãøó Åöäí ÃÚõæÐõ Èößó ãöäú ÚóÐóÇÈö Ìóåóäøóãó¡ æóãäú
ÚóÐóÇÈö ÇáÞóÈúÑö¡ æóãöäú ÝöÊúäóÉö ÇáãóÍúíÇ
æÇáãóãÇÊö¡ æóãöäú ÔóÑøö ÝöÊúäóÉ ÇáãóÓöíÍö ÇáÏøóÌøóÇáö"
“Allahumma inni audhu bika min adhaabi jahannam, wamin adhaabi l
qabri, wa min fitnatil mahyaa wa l mamaat, wamin sharri fitnatil masiyhi
ddajaal”
Muslim
Na maana
yake ni
“Mola wangu najikinga kwako kutokana na adhabu ya Jahannam na
kutokana na adhabu ya kaburi na kutokana na mitihani ya uhai na ya kifo na (na
najikinga kwako kutokana na) shari ya mitihani ya Masiyhi Dajjaal”
Na katika
hadithi nyingine akasema:
“Mmoja wenu anapomaliza kusoma Tahiyatu na Imamu bado hajamaliza,
basi na ajichagulie katika dua nzuri nzuri.”
Katika
hadithi iliyosimuliwa na Al Bara-a (Radhiya Llahu anhu) anasema:
“Alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
anaporukuu akiunyosha mgongo wake sawa sawa.”
Na
katika riwaya nyingine:
“Alikuwa hainami sana kuelekea chini wala hainuki sana kuelekea
juu.”
Al
Baihaqi
Imepokelewa
katika sifa za kurukuu kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) alikuwa anaporukuu akiunyosha mgongo wake sawa sawa, hata kama mtu
atamwaga maji juu ya mgongo wake basi maji hayo yangetulia.
(Kitabu
cha Sifatu Salaatu Nnabiy- Sh. Al Albaniy na Sahih Al Jami-a al Saghiry -
hadithi nambari 4732)
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Nimeamrishwa kusujudu juu ya mifupa saba;
Mikono miwili (viganja). Magoti mawili. 'Matumbo ya vidole vya
miguu. Kipaji pamoja na pua.”
Na
riwaya nyingine inasema; Alikuwa akigusisha kipaji
chake na pua yake juu ya ardhi.
Na
alikuwa akisema:
“Haifai Swala ya mtu ikiwa hajaimakinisha pua yake juu ya ardhi
sawa sawa pamoja na kipaji chake”.
Addaraqutniy
na Attabarani – Abu Daud na Imam Ahmad
Na
alikuwa pia akiyamakinisha magoti yake juu ya ardhi pamoja na matumbo ya vidole
vya miguu yake na akivielekeza vidole kibla.
Bukhari
– Abu Daud – Al Baihaqi
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akikataza kula vyakula
venye harufu ya kukirihisha kabla ya kwenda msikitini.
Alikuwa
akisema:
“Aliyekula kitunguu thomu au kitunguu maji au ‘Kurratha’ (mfano
wa vitunguu vidogo au majani yake), asiingie ndani ya misikiti yetu na (bora)
akae nyumbani kwake mpaka itakapoondoka harufu. Kwa sababu Malaika wanaudhika
kwa harufu yoyote inayowaudhi wanadamu.”
Muslim
Mtu
anapotaka kumkabili mfalme wa kidunia, au mkuu wake wa kazini basi hukakikisha
kuwa amevaa vizuri na ananukia vizuri na utamuona kabla ya kuonana naye kila
mara akijitizama penye kiyoo ili ahakikishe kuwa amependeza. Lakini anapokwenda
kukabiliana na Mola wake, Mfalme wa wafalme, hayo hayamshughulishi hata kidogo.
Mwenyezi
Mungu anasema:
íóÇ Èóäöí ÂÏóãó
ÎõÐõæÇú ÒöíäóÊóßõãú ÚöäÏó ßõáøö ãóÓúÌöÏò
“Enyi wanadamu chukueni mapambo yenu wakati
wa kila Sala."
Al
Aaraf – 31
Sitra
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa anaposwali hujiwekea Sitra
mbele yake. Na Sitra ni kitu chochote kisafi utakachoweka mbele yako
wakati wa kuswali umbali wa mahali pa kusujudia kwa ajili ya kuwazuwia watu
wasipite mbele yako.
Jambo
hili si fardhi lakini Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
alikuwa akilihimiza sana, na alikuwa akifanya hivyo na akausia.
Unaposwali
na Imamu haina haja ya kuweka sitra, kwa sababu sitra ya Imamu ndiyo sitra
yako, na hata kama mtu atapita mbele yako nawe unaswali, ikiwa Imamu keshaweka
sitra huko mbele basi haidhuru.
Imepokelewa
katika hadithi nyingi kuwa Masahaba wakubwa kama vile Ibni Abbas (Radhiya Llahu
anhu) walikuwa wakipita mbele ya safu za nyuma wakati Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) akiswalisha na hakuwakataza wala kuwaambia kitu. Hii ikimaanisha
kuwa inajuzu mtu kupita mbele ya wanaoswali ikiwa huko mbele Imamu keshaweka
sitra.
Kupita
mbele ya mtu anayeswali peke yake (baina yake na sitra) ikiwa amejiwekea sitra,
au hata kama hakujiwekea, hiyo ni haramu na haijuzu.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Angelijuwa yule anayepita mbele ya mtu anayeswali atalipwa nini
(kwa dhambi yake hiyo), basi angehiari asubiri arubaini kuliko kupita mbele
yake.”
Aliyesimulia
hadithi anasema:
‘Sielewi Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam))
alisema siku arubaini au miezi au miaka arubaini’.
Imepokelewa
na Maiamu wote wa hadithi
Na
katika hadithi ilipokelewa na Bukhari na Muslim, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) alisema:
“Mmoja wenu anaposwali akiwa kieshajiwekea kitu kinachomsitiri, basi
anapotaka mtu kupita baina yake na baina ya sitra yake, amsukume. Na kama
atashikilia kutaka kupita, basi apigane naye, kwa sababu huyo ni shetani”.
Bukhari
na Muslim
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) anaposima mbele baada ya
kuqimiwa Swala alikuwa akisema:
“Simamisheni msitari sawa, kwani kuusimamisha sawa ni katika
ukamilifu wa Swala”.
Bukhari
na Muslim
Na
akisema:
“Wallahi mtasimamisha sawa msitari ama sivyo Mwenyezi Mungu
atazifanya nyoyo zenu zikhitilafiane”.
Baadhi
ya watu huchelewa kufika msikitini, kisha utawaona wakati watu washaanza kuswali
wao ndio wanaswali Sunnah ya kabla ya Swala ya Alfajiri au hufanya hivyo wakati
Swala inaqimiwa.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema juu ya Sunna hiyo ya
kabla ya Swala ya Alfajiri:
“Ninaipenda kuliko dunia na kila kilichokuwemo ndani yake”.
Lakini
wakati huo huo Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
amekataza mtu kuswali Swala za Sunnah wakati Swala ya fardhi inaqimiwa au
ishaqimiwa.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Inapoqimiwa Swala, basi hapana kuswali Swala nyingine isipokuwa
(ile) iliyofaradhishwa.”
Bukhari
– Muslim
Kwa
hivyo tujaribu kuwasili mapema msikitini kwa ajili ya kuziwahi rakaa mbili hizo
tusije tukakosa kheri nyingi zilizomo ndani yake, au tuziswali nyumbani kabla
ya kwenda msikitini kwa ajili ya kuzipata kheri hizo pamoja na kuingiza nuru
ndani ya nyumba zetu.
Kutojishughulisha
na kumtaja Mwenyezi Mungu baada ya kumaliza Swala ni kujikosesha kheri nyingi
sana.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Anayemsabbihi Mwenyezi Mungu (Subhanallah) baada ya kila Swala
ya Fardhi mara 33 Na kumhimidi mara 33 (Alhamdulillah) na kumkabbir mara 33
(Allahu Akbar), hizo ni tisini na tisa, kisha ili kuitimiza idadi ikawa mia
moja akasema:
áÇó Åöáóåó ÅöáÇø Çááå æóÍúÏóåõ áÇó ÔóÑöíßó áóåõ¡ áóåõ Çáãõáúßõ æóáóåõ
ÇáúÍóãúÏõ æóåõæó Úóáóì ßáø ÔóíúÁò ÞóÏöíÑ
”Laa ilaaha illa Llahu wahdahu laa shariyka lahu, lahu l mulku
walahu l hamdu wahuwa ala kulli shay in qadiyr,”, basi ataghufiriwa madhambi
yake hata yakiwa mengi mfano wa povu la bahari”
Muslim –
Abu Daud – Imam Ahmad
Unapomkuta
Imamu amerukuu ukataka kujiunga na Swala ili uiwahi Raka-a ile, unatakiwa
kupiga takbira mbili, moja ya kuingia katika Swala na ya pili ya kujiunga na
Imamu katika kurukuu.
Unaporukuu
lazima uhakikishe kuwa umemkuta Imamu akiwa bado amerukuu. Imamu akianza kuinua
mgongo wake kwa ajili ya kusimama kabla wewe kurukuu, basi huhesabiwi kuwa
umeiwahi raka-a ile.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amekataza mtu kuswali akiwa
ameshikwa na haja kubwa au ndogo.
Katika
hadithi sahihi, anasema Abu Umama (Radhiya Llahu anhu):
“Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) akisema:
“Mmoja wenu asiswali akiwa ameshikwa na haja mpaka akajisaidie
(kwanza), na asiingie mmoja wenu katika nyumba ya watu bila ya kuruhusiwa, na
Imamu asije akaswalisha watu kisha akajihusisha peke yake kwa dua.”
Muslim
- Ibni Majah – Abu Daud – Ahmad
Mwenyezi
Mungu Anasema:
ÞóÏú ÃóÝúáóÍó
ÇáúãõÄúãöäõæäó. ÇáøóÐöíäó åõãú Ýöí ÕóáÇÊöåöãú ÎóÇÔöÚõæäó
“Hakika wamefuzu Waislam. Ambao katika Sala
zao huwa ni wanyenyekevu.”
Al
Muuminun 1-2.
Katika
kuifasiri aya hii, mfasiri maarufu wa Qurani Ibnu Kathiyr anasema:
“Ibni Abbas (Radhiya Llahu anhu) amesema: “Khaashiuun, -
maana yake, ‘Wanaoswali wakiwa na uoga pamoja na utulivu.”
Aliy (Radhiya Llahu anhu) amesema: “Khashiuun, - maana yake ni
unyenyekevu wa moyo”.
Ibnu
Kathiyr akaendelea kusema:
“Hapo
mwanzo Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
walikuwa wanaposwali wakinyanyua macho yao juu. Lakini baada ya kuteremka aya
hii (ÞóÏú ÃóÝúáóÍó ÇáúãõÄúãöäõæäó. ÇáøóÐöíäó åõãú Ýöí ÕóáÇÊöåöãú
ÎóÇÔöÚõæäó), wakawa wanateremsha macho yao
chini na kuangalia mahala wanaposujudu”.
Na Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:
“Waache (kufanya hivyo) wale watu wanaonyanyua macho yao
kutizama juu ndani ya Swala. Yatapofolewa macho yao”
Bukhari
– Muslim na wengineo.
Na
katika kukataza huku, wanaingia pia wale wanaotizama huku na kule wakiwa ndani
ya Swala.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenyezi Mungu anaendelea kumtizama mja wake (kwa rehma)
anapokuwa akiswali mpaka pale anapoanza kugeuka na kutizama pengine.
Anapougeuza uso wake, na Mwenyezi Mungu huacha kumtizama”.
Ahmad
– Annasai – Abu Daud
Na Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipoulizwa juu ya
kugeukageuka katika Swala akajibu:
“Huo ni wizi. Shetani anaiba kwa ujanja katika Swala ya mja”.
Bukhari
- Imam Ahmad – Attirmidhiy na wengine
Baadhi
ya watu wanapotoa salam, huashiria upande wa kulia kwa kiganja cha mkono wa
kulia na upande wa kushoto kwa kiganja cha mkono wa kushoto.
Kufanya
hivyo ni makosa.
Kutoka
kwa Jabir (Radhiya Llahu anhu) anasema: “Tulipokuwa
tukiswali pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam),
tulikuwa pale tunaposema: ‘Assalaam aleikum wa Rahmatullahi’, tukiashiria
mikono yetu pande mbili. Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) akasema: ”Mbona nakuoneni mnanyanyua mikono yenu mfano wa wadudu
wanaotembea bila kutulia?”
Watu wakaacha kuashiria.
Muslim
Kosa
lingine linalofanywa katika kutoa salam, ni pale mtu anapokitingisha na
kukipeleka kichwa chake juu na chini wakati anapougeuza uso wake upande wa
kushoto baada ya kusalimia upande wa kulia.
Njia
sahihi ya kutoa salam ni kugeuka kulia kisha kushoto bila kukinyanyua wala
kukishuka kichwa.
Wallahu
taala aalam
Wassalaam
alaykum wa rahmatullahi wa Barakatuh