Makosa ndani ya Swala

Imekusanywa na Muhammad Faraj Al Saiy

Utulivu.. 1

Kudokoa.. 1

Kuichelewesha

Isha na Alfajiri

 

Kuikimbilia

 

Kumsubiri Imamu.. 3

Kushindana na Imamu.. 3

Unapomaliza Tahiyatu.. 3

Kuunyosha mgongo. 4

Kusujudu.. 4

Vyakula vyenye harufu.. 4

Nguo nzuri 4

Sitra.. 5

Msitari 5

Sunna ya Alfajiri 5

Baada ya Swala.. 6

Kuiwahi Rakaa.. 6

Kwenda haja.. 6

Kunyanyua macho. 6

Kutoa salam... 7

 

Utulivu (Tumaaniyna)

Utulivu (Tumaaniyna) ni nguzo muhimu sana katika nguzo za Swala, na bila ya utulivu Swala haiwi kamilifu.

Siku moja Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa amekaa msikitini, akaingia mtu mmoja na kuswali. Baada ya kumaliza akainuka na kwenda kumsalimia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam). Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akamuambia:

“Rudi kaswali tena, wewe bado hujaswali.”

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alimrudisha mtu huyo mara tatu, na kila anapomaliza kuswali alikuwa akimuambia:

“Rudi kaswali tena, wewe bado hujaswali”.

Yule mtu akamuambia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam):

“Sijuwi kuswali vizuri kuliko hivi, (bora) nifundishe”.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuambia:

“Unapotaka kuswali tia udhu, kisha elekea kibla, kisha soma utakachoweza kusoma katika Qurani, kisha ruku-u mpaka utulie (Tumaaniyna) na uwe na uhakika kuwa umerukuu (sawa), kisha inuka usimame sawa sawa(Tumaaniyna), kisha usujudu mpaka utulie (Tumaaniyna) na uwe na uhakika kuwa umesujudu sawa, kisha kaa vizuri mpaka utulie katika kikao chako(Tumaaniyna), kisha sujudu na utulie (Tumaaniyna) mpaka uwe na uhakika kuwa umesujudu sawa, kisha ufanye hivyo hivyo mpaka umalize kuswali”

Bukhari, Muslim, AbuDaud, Attirmidhy, Annasai na Ibni Majah

 

Hadithi hii na nyingi kama hizi zinatujulisha kuwa Swala haiwi kamili bila ya utulivu (Tuma – aniyna). Nako ni kutulia katika kila kitendo cha Swala. Mtu anatakiwa atulie mpaka awe na uhakika kuwa ametulia.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amempa jina la ‘Mwizi’ mtu anayeswali bila utulivu.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Katika wezi wabaya kabisa ni wale wanaoiba katika Swala zao, hawarukuu kwa ukamilifu wala hawasujudu kwa ukamilifu na hawawi na khushuu.”

 

Na katika riwaya nyingine amesema juu ya ‘Mwizi wa Swala’:

“Na wala haunyoshi mgongo wake sawa pale anaporukuu na anaposujudu.”

Imam Ahmad, Al Hakim na imesahihishwa na Imam Al Dhahabi.

 Rudi juu

Kudokoa

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amekataza kudokoadokoa katika Swala. Kwa sababu anayeswali kwa pupa bila ya utulivu anakuwa mfano wa kuku anayedokoa mtama, na huwa haipi haki yake Swala, wala hakipi kila kitendo haki yake. Bali hampi Mola wake haki Yake.

Kumbuka kuwa ndani ya Swala yanapita mazungumzo baina yako na Mola wako Subhanahau wa Taala.

Katika hadithi ambayo sehemu ya mwanzo yake ni Hadith Al Qudusiy, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

 “Mwenyezi Mungu anasema; ‘Nimeigawa Swala baina yangu na baina ya mja wangu sehemu mbili, na mja wangu (ninampa) anachoniomba’. Mja anaposema:

ÇáúÍóãúÏõ ááøåö ÑóÈøö ÇáúÚóÇáóãöíäó

,MwenyeMungu Husema: “Mja wangu amenishukuru”.

Na anaposema:

ÇáÑøóÍúãÜäö ÇáÑøóÍöíãö”,

Mwenyezi Mungu Husema:“Mja wangu amenipa sifa yangu”.

Na anaposema:

ãóÜáößö íóæúãö ÇáÏøöíäö,

 Mwenyezi Mungu Husema:

“Mja wangu amenitukuza”, au Husema:“Mja wangu amejisalimisha kwangu ”.

Na anaposema;

ÅöíøóÇßó äóÚúÈõÏõ æÅöíøóÇßó äóÓúÊóÚöíäõ,

 Mwenyezi Mungu Husema:

“Haya ni baina yangu na baina ya mja wangu na mja wangu atapata atakachoniomba.”

Na anaposema:

ÇåÏöäóÜÜÜÜÇ ÇáÕøöÑóÇØó ÇáãõÓÊóÞöíãó. ÕöÑóÇØó ÇáøóÐöíäó ÃóäÚóãÊó Úóáóíåöãú ÛóíÑöÇáãóÛÖõæÈö Úóáóíåöãú æóáÇó ÇáÖøóÇáøöíäó”.

Mwenyezi Mungu husema:

“Hii ni ya mja wangu na mja wangu atapata anachoniomba”

 

Mtu anapozungumza na mzee wake au mkubwa wake wa kazini au anapozungumza na mfalme katika wafalme wa dunia, huzungumza naye kwa heshima na utulivu kubwa.

Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala anastahiki zaidi heshima na utulivu huo kuliko viumbe hao dhaifu.

 

Mmoja katika maulama amemfananisha anayeswali kwa pupa bila ya utulivu kuwa ni sawa na mwenye kunywa dawa chungu anapoweka chungwa lake tayari apate kula mara baada ya kunywa dawa kwa ajili ya kuuondoa uchungu wa dawa. Lakini yule anayestarehe ndani ya Swala yake, mfano wake ni mfano wa mtu anayekunywa kinywaji kitamu. Anakunywa taratibu, akistarehe nayo huku akitamani kinywaji hicho kismalizike.

Mtu anapomjuwa Mola wake, na kuzijuwa neema alizopewa, kisha akaujuwa uwezo wa Mola wake juu yake, huyo ndiye anayemjuwa Nani anayemuabudu, na anampa heshima anayostahiki.

 

Ibni l Qayim amepiga mfano wa mtu anayemuabudu Mola wake bila ya kumpa heshima anayostahiki kuwa ni mfano wa panya aliyemouwa ngamia, kisha akamchukuwa ngamia huyo na kumpeleka penye tundu lake (tundu la panya) na kumtaka mkewe (ngamia) aingie ndani humo.

Ngamia akamwambia panya:

“Sikiliza bwana, nitafutie nyumba kiasi changu, au tafuta mke kiasi chako”

Ibni l Qayim alimaliza kwa kusema:

“Na hivi ndivyo ilivyo, mtu ama amuabudu Mwenyezi Mungu kama Anavyostahiki kuabudiwa, au atafute kijiungu chake akiabudu kama anavyotaka yeye.”

 Rudi juu

Kuichelewesha Swala

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema juu ya wenye kuichelewesha Swala ya Alasiri na kuiswali karibu na Magharibi:

“Hiyo ni Swala ya wanafiki. Anasubiri, analitegea jua mpaka linapokuwa baina ya pembe mbili za shetani, hapo huinuka na kuzidokoa (rakaa) nne, (ndani yake) hamtaji Mwenyezi Mungu isipokuwa kidogo sana.”

Muslim, Attirmidhy na Annasai

 

Baadhi ya watu wanao mtindo huu wa kuichelewesha Swala ya Alasiri. Wanaiacha mpaka jua linapokaribia kutuwa, ndipo wanapoinuka na kuzidokoa raka nne za Alasiri haraka haraka kabla ya kuadhini Magharibi kwa muda mchache sana, ili abaki na udhu wake apate kuuswalia Magharibi.

Kumbuka kuwa unapokuwa ndani ya Swala, unazungumza na Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu, wakati wewe ni dhaifu. Mwenyezi Mungu Mwenye kutowa, wakati wewe ni masikini, muhitaji. Mwenyezi Mungu Mwenye funguo zote za hazina za mbinguni na ardhini. Kwa hivyo swali katika wakati wake na kuwa na utulivu ndani yake huku ukimshukuru na kumuomba, kwani mlango Wake uko wazi wakati wote.

 Rudi juu

Isha na Alfajiri katika jamaa

Kuzikosa jamaa mbili hizi ni kujikosesha kheri nyingi sana. Watu wengi baada ya machofu ya kazi ya mchana kutwa huona tabu kuinuka juu ya kiti au mbele ya television na kujikokota kwenda msikitini kuswali Swala ya Isha jamaa pamoja na Waislam wenzake. Hii inatokana na kutokujuwa umuhimu wa kuswali jamaa, pamoja na kutokujuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema nini kuhusu wale wasioziswali Swala hizo katika jamaa na nini wanachokikosa.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Swala nzito kwa wanafiki kuziwsali jamaa ni Swala za Isha na Alfajiri, na lau wangelijuwa faida iliyomo basi wangelikuja hata kwa kusota”.

Muslim, Imam Ahmad, Attabarani, Annasaiy, Ibni Majah na wengine

 

Na akasema:

“Na atakayeswali Isha katika jamaa, anaandikiwa thawabu ya aliyeswali nusu ya usiku, na atakayeziswali zote mbili katika jamaa (Magharibi na Isha), anaandikiwa thawabu za aliyeswali usiku kucha”.

Muslim, Ibni Hibban, Al Jamia al Kabiyr.

 Rudi juu

Kukimbilia Swala

Katika makosa yanayofanywa na baadhi ya wanaoswali ni kule kukimbia wanapokwenda msikitini kwa ajili ya kuiwahi raka-a isiwapite.

Mtume wa Mwenyezi Mungu wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amekataza kitendo hicho pale aliposema:

“Mnaposikia Iqamah, ziendeeni Swala zenu (nendeni msikitini) kwa utulivu na kwa uchaMungu (msiende mbio). Raka-a mtakazoziwahi swalini na mtakazozikosa kamilisheni”.

Bukhari na Muslim

 Rudi juu

Kumsubiri Imamu

Baadhi ya watu wanapoingia msikitini na Imamu amesujudu au amekaa, huwa hawafungi Swala na kuingia katika jamaa moja kwa moja. Husubiri mpaka Imamu ainuke ndipo wanapofunga Swala na kujiunga na jamaa.

Kitendo hicho kimekatazwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Mmoja wenu anapoingia (msikitini) akamkuta Imamu amesujudu au amekaa basi naye amfuate Imamu huyo kwa kujiunga naye katika kile kitendo alichomkuta nacho.”

Attirmidhy

 Rudi juu

Kushindana na Imamu

Katika kitendo asichokipenda Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na kilichokuwa kikimchukiza sana ni kumtangulia Imamu katika kurukuu au kusujudu au kuinuka nk.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amemfananisha mwenye kitendo hicho kuwa sawa na punda.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Haogopi mmoja wenu anapomtangulia Imamu akageuzwa kichwa chake kuwa sawa na kichwa cha punda?”

Addarimy na Ibni Majah

 

Na akasema:

“Imamu amewekwa ili afuatwe. Akisema: “Allahu akbar” na nyinyi semeni kama yeye. Anaposoma na nyinyi mumsikilize. Anaporukuu nanyi murukuu. Anaposema: “Samia llahu liman hamidah”, semeni: “Rabana laka l hamd”. Na anapokua amekaa nanyi nyote kwa pamoja pia kaeni (kama yeye)”.

Maimamu wote watano isipokuwa Attirmidhiy

 

Na akasema:

“Hakika mimi ni Imamu wenu. Msinitangulie katika kurukuu wala kusujudu wala kusimama wala kutoa salamu”.

Muslim – Ibni Khuzayma – Al Bayhaqi na wengineo

 

Maulamaa wanasema kwa vile Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) katika hadithi hii ametumia neno la kiarabu ‘Idhaa’ katika kuunganisha utaratibu wa kumfuata Imamu (FAIDHA kabbara fakabbiru wa idhaa qara-a faansitu), akitufahamisha kuwa ni lazima tuufuate utaratibu huu bila kuchelewa.

 Rudi juu

Unapomaliza Tahiyatu

Unapomaliza kusoma Tahiyatu na Imamu bado hajamaliza, badala ya kukaa kimya ni bora mtu asome baadhi ya dua alizotufundisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipoulizwa nini mtu afanye anapomaliza kusoma tahiyatu na Imamu bado hakumaliza, akasema:

Çááøóåõãøó Åäí ÙóáóãúÊõ äóÝúÓöí ÙõáúãÇð ßóËöíÑÇð æó áÇ íóÛúÝöÑõ ÇáÐøõäõæÈó ÅöáÇøó ÃóäúÊó¡ ÝÇÛúÝöÑú áöí ãóÛúÝöÑóÉð ãöäú ÚöäúÏößó æóÇÑúÍãúäöí Åäøóß ÃóäúÊó ÇáÛóÝõæÑõ ÇáÑøóÍöíã"

“Sema; “Allahumma inniy dhalamtu nafsiy dhulman kathiyraa, walaa yaghfiru dhunuuba illaa anta. Fa- aghfirliy maghfiratan min indika warhamniy, innaka anta l ghafuwru rrahiym”

Bukhari na Muslim

 

Na maana yake ni;

“Mola wangu mimi nimejidhulumu nafsi yangu dhulma nyingi sana, na hapana anayesamehe madhambi isipokuwa wewe, kwa hivyo nighufirie maghfira kutoka kwako na nirehemu, hakika Wewe ni Mwenye Kusamehe, Mwenye Huruma.”

 

Na katika hadithi nyingine akasema:

“Mtu anapomaliza kusoma tahiyatu na Imamu bado hajamaliza na asome:

Çááøóåõãøó Åöäí ÃÚõæÐõ Èößó ãöäú ÚóÐóÇÈö Ìóåóäøóãó¡ æóãäú ÚóÐóÇÈö ÇáÞóÈúÑö¡ æóãöäú ÝöÊúäóÉö ÇáãóÍúíÇ

æÇáãóãÇÊö¡ æóãöäú ÔóÑøö ÝöÊúäóÉ ÇáãóÓöíÍö ÇáÏøóÌøóÇáö"

“Allahumma inni audhu bika min adhaabi jahannam, wamin adhaabi l qabri, wa min fitnatil mahyaa wa l mamaat, wamin sharri fitnatil masiyhi ddajaal”

Muslim

 

Na maana yake ni

“Mola wangu najikinga kwako kutokana na adhabu ya Jahannam na kutokana na adhabu ya kaburi na kutokana na mitihani ya uhai na ya kifo na (na najikinga kwako kutokana na) shari ya mitihani ya Masiyhi Dajjaal”

 

Na katika hadithi nyingine akasema:

“Mmoja wenu anapomaliza kusoma Tahiyatu na Imamu bado hajamaliza, basi na ajichagulie katika dua nzuri nzuri.”

  Rudi juu

Kuunyosha mgongo

Katika hadithi iliyosimuliwa na Al Bara-a (Radhiya Llahu anhu) anasema:

“Alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) anaporukuu akiunyosha mgongo wake sawa sawa.”

 

Na katika riwaya nyingine:

“Alikuwa hainami sana kuelekea chini wala hainuki sana kuelekea juu.”

Al Baihaqi

 

Imepokelewa katika sifa za kurukuu kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa anaporukuu akiunyosha mgongo wake sawa sawa, hata kama mtu atamwaga maji juu ya mgongo wake basi maji hayo yangetulia.

(Kitabu cha Sifatu Salaatu Nnabiy- Sh. Al Albaniy na Sahih Al Jami-a al Saghiry - hadithi nambari 4732)

 Rudi juu

Kusujudu

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Nimeamrishwa kusujudu juu ya mifupa saba;

Mikono miwili (viganja). Magoti mawili. 'Matumbo ya vidole vya miguu. Kipaji pamoja na pua.”

 

Na riwaya nyingine inasema; Alikuwa akigusisha kipaji chake na pua yake juu ya ardhi.

 

Na alikuwa akisema:

“Haifai Swala ya mtu ikiwa hajaimakinisha pua yake juu ya ardhi sawa sawa pamoja na kipaji chake”.

Addaraqutniy na Attabarani – Abu Daud na Imam Ahmad

 

Na alikuwa pia akiyamakinisha magoti yake juu ya ardhi pamoja na matumbo ya vidole vya miguu yake na akivielekeza vidole kibla.

Bukhari – Abu Daud – Al Baihaqi

 Rudi juu

 

Vyakula vyenye harufu

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akikataza kula vyakula venye harufu ya kukirihisha kabla ya kwenda msikitini.

Alikuwa akisema:

“Aliyekula kitunguu thomu au kitunguu maji au ‘Kurratha’ (mfano wa vitunguu vidogo au majani yake), asiingie ndani ya misikiti yetu na (bora) akae nyumbani kwake mpaka itakapoondoka harufu. Kwa sababu Malaika wanaudhika kwa harufu yoyote inayowaudhi wanadamu.”

Muslim

 Rudi juu

Kuvaa nguo nzuri

Mtu anapotaka kumkabili mfalme wa kidunia, au mkuu wake wa kazini basi hukakikisha kuwa amevaa vizuri na ananukia vizuri na utamuona kabla ya kuonana naye kila mara akijitizama penye kiyoo ili ahakikishe kuwa amependeza. Lakini anapokwenda kukabiliana na Mola wake, Mfalme wa wafalme, hayo hayamshughulishi hata kidogo.

Mwenyezi Mungu anasema:

íóÇ Èóäöí ÂÏóãó ÎõÐõæÇú ÒöíäóÊóßõãú ÚöäÏó ßõáøö ãóÓúÌöÏò

“Enyi wanadamu chukueni mapambo yenu wakati wa kila Sala."

Al Aaraf – 31

  Rudi juu

Sitra
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa anaposwali hujiwekea Sitra mbele yake. Na Sitra ni kitu chochote kisafi utakachoweka mbele yako wakati wa kuswali umbali wa mahali pa kusujudia kwa ajili ya kuwazuwia watu wasipite mbele yako.

Jambo hili si fardhi lakini Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akilihimiza sana, na alikuwa akifanya hivyo na akausia.

 

Unaposwali na Imamu haina haja ya kuweka sitra, kwa sababu sitra ya Imamu ndiyo sitra yako, na hata kama mtu atapita mbele yako nawe unaswali, ikiwa Imamu keshaweka sitra huko mbele basi haidhuru.

 

Imepokelewa katika hadithi nyingi kuwa Masahaba wakubwa kama vile Ibni Abbas (Radhiya Llahu anhu) walikuwa wakipita mbele ya safu za nyuma wakati Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akiswalisha na hakuwakataza wala kuwaambia kitu. Hii ikimaanisha kuwa inajuzu mtu kupita mbele ya wanaoswali ikiwa huko mbele Imamu keshaweka sitra.

 

Kupita mbele ya mtu anayeswali peke yake (baina yake na sitra) ikiwa amejiwekea sitra, au hata kama hakujiwekea, hiyo ni haramu na haijuzu.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Angelijuwa yule anayepita mbele ya mtu anayeswali atalipwa nini (kwa dhambi yake hiyo), basi angehiari asubiri arubaini kuliko kupita mbele yake.”

 

Aliyesimulia hadithi anasema:

‘Sielewi Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)) alisema siku arubaini au miezi au miaka arubaini’.

Imepokelewa na Maiamu wote wa hadithi

 

Na katika hadithi ilipokelewa na Bukhari na Muslim, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alisema:

“Mmoja wenu anaposwali akiwa kieshajiwekea kitu kinachomsitiri, basi anapotaka mtu kupita baina yake na baina ya sitra yake, amsukume. Na kama atashikilia kutaka kupita, basi apigane naye, kwa sababu huyo ni shetani”.

Bukhari na Muslim

  Rudi juu

Kuusimamisha msitari

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) anaposima mbele baada ya kuqimiwa Swala alikuwa akisema:

“Simamisheni msitari sawa, kwani kuusimamisha sawa ni katika ukamilifu wa Swala”.

Bukhari na Muslim

 

Na akisema:

“Wallahi mtasimamisha sawa msitari ama sivyo Mwenyezi Mungu atazifanya nyoyo zenu zikhitilafiane”.

 Rudi juu

Sunna ya Alfajiri

Baadhi ya watu huchelewa kufika msikitini, kisha utawaona wakati watu washaanza kuswali wao ndio wanaswali Sunnah ya kabla ya Swala ya Alfajiri au hufanya hivyo wakati Swala inaqimiwa.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema juu ya Sunna hiyo ya kabla ya Swala ya Alfajiri:

“Ninaipenda kuliko dunia na kila kilichokuwemo ndani yake”.

 

Lakini wakati huo huo Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amekataza mtu kuswali Swala za Sunnah wakati Swala ya fardhi inaqimiwa au ishaqimiwa.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Inapoqimiwa Swala, basi hapana kuswali Swala nyingine isipokuwa (ile) iliyofaradhishwa.”

Bukhari – Muslim

 

Kwa hivyo tujaribu kuwasili mapema msikitini kwa ajili ya kuziwahi rakaa mbili hizo tusije tukakosa kheri nyingi zilizomo ndani yake, au tuziswali nyumbani kabla ya kwenda msikitini kwa ajili ya kuzipata kheri hizo pamoja na kuingiza nuru ndani ya nyumba zetu.

 Rudi juu

Baada ya Swala

Kutojishughulisha na kumtaja Mwenyezi Mungu baada ya kumaliza Swala ni kujikosesha kheri nyingi sana.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Anayemsabbihi Mwenyezi Mungu (Subhanallah) baada ya kila Swala ya Fardhi mara 33 Na kumhimidi mara 33 (Alhamdulillah) na kumkabbir mara 33 (Allahu Akbar), hizo ni tisini na tisa, kisha ili kuitimiza idadi ikawa mia moja akasema:

áÇó Åöáóåó ÅöáÇø Çááå æóÍúÏóåõ áÇó ÔóÑöíßó áóåõ¡ áóåõ Çáãõáúßõ æóáóåõ ÇáúÍóãúÏõ æóåõæó Úóáóì ßáø ÔóíúÁò ÞóÏöíÑ

”Laa ilaaha illa Llahu wahdahu laa shariyka lahu, lahu l mulku walahu l hamdu wahuwa ala kulli shay in qadiyr,”, basi ataghufiriwa madhambi yake hata yakiwa mengi mfano wa povu la bahari”

Muslim – Abu Daud – Imam Ahmad

  Rudi juu

Kuiwahi Rakaa

Unapomkuta Imamu amerukuu ukataka kujiunga na Swala ili uiwahi Raka-a ile, unatakiwa kupiga takbira mbili, moja ya kuingia katika Swala na ya pili ya kujiunga na Imamu katika kurukuu.

Unaporukuu lazima uhakikishe kuwa umemkuta Imamu akiwa bado amerukuu. Imamu akianza kuinua mgongo wake kwa ajili ya kusimama kabla wewe kurukuu, basi huhesabiwi kuwa umeiwahi raka-a ile.

 Rudi juu

 

Kujizuwia kwenda haja

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amekataza mtu kuswali akiwa ameshikwa na haja kubwa au ndogo.

Katika hadithi sahihi, anasema Abu Umama (Radhiya Llahu anhu):

“Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akisema:

“Mmoja wenu asiswali akiwa ameshikwa na haja mpaka akajisaidie (kwanza), na asiingie mmoja wenu katika nyumba ya watu bila ya kuruhusiwa, na Imamu asije akaswalisha watu kisha akajihusisha peke yake kwa dua.”

Muslim - Ibni Majah – Abu Daud – Ahmad

 Rudi juu

Kunyanyua macho

Mwenyezi Mungu Anasema:

ÞóÏú ÃóÝúáóÍó ÇáúãõÄúãöäõæäó. ÇáøóÐöíäó åõãú Ýöí ÕóáÇÊöåöãú ÎóÇÔöÚõæäó

“Hakika wamefuzu Waislam. Ambao katika Sala zao huwa ni wanyenyekevu.”

Al Muuminun 1-2.

 

Katika kuifasiri aya hii, mfasiri maarufu wa Qurani Ibnu Kathiyr anasema:

“Ibni Abbas (Radhiya Llahu anhu) amesema: “Khaashiuun, - maana yake, ‘Wanaoswali wakiwa na uoga pamoja na utulivu.”

Aliy (Radhiya Llahu anhu) amesema: “Khashiuun, - maana yake ni unyenyekevu wa moyo”.

 

Ibnu Kathiyr akaendelea kusema:

“Hapo mwanzo Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) walikuwa wanaposwali wakinyanyua macho yao juu. Lakini baada ya kuteremka aya hii (ÞóÏú ÃóÝúáóÍó ÇáúãõÄúãöäõæäó. ÇáøóÐöíäó åõãú Ýöí ÕóáÇÊöåöãú ÎóÇÔöÚõæäó), wakawa wanateremsha macho yao chini na kuangalia mahala wanaposujudu”.

 

Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

“Waache (kufanya hivyo) wale watu wanaonyanyua macho yao kutizama juu ndani ya Swala. Yatapofolewa macho yao”

Bukhari – Muslim na wengineo.

 

Na katika kukataza huku, wanaingia pia wale wanaotizama huku na kule wakiwa ndani ya Swala.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenyezi Mungu anaendelea kumtizama mja wake (kwa rehma) anapokuwa akiswali mpaka pale anapoanza kugeuka na kutizama pengine. Anapougeuza uso wake, na Mwenyezi Mungu huacha kumtizama”.

Ahmad – Annasai – Abu Daud

Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipoulizwa juu ya kugeukageuka katika Swala akajibu:

“Huo ni wizi. Shetani anaiba kwa ujanja katika Swala ya mja”.

Bukhari - Imam Ahmad – Attirmidhiy na wengine

 Rudi juu

Kutoa salam

Baadhi ya watu wanapotoa salam, huashiria upande wa kulia kwa kiganja cha mkono wa kulia na upande wa kushoto kwa kiganja cha mkono wa kushoto.

Kufanya hivyo ni makosa.

Kutoka kwa Jabir (Radhiya Llahu anhu) anasema: “Tulipokuwa tukiswali pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), tulikuwa pale tunaposema: ‘Assalaam aleikum wa Rahmatullahi’, tukiashiria mikono yetu pande mbili. Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema: ”Mbona nakuoneni mnanyanyua mikono yenu mfano wa wadudu wanaotembea bila kutulia?”

Watu wakaacha kuashiria.

Muslim

 

Kosa lingine linalofanywa katika kutoa salam, ni pale mtu anapokitingisha na kukipeleka kichwa chake juu na chini wakati anapougeuza uso wake upande wa kushoto baada ya kusalimia upande wa kulia.

Njia sahihi ya kutoa salam ni kugeuka kulia kisha kushoto bila kukinyanyua wala kukishuka kichwa.

Wallahu taala aalam

Wassalaam alaykum wa rahmatullahi wa Barakatuh

 Rudi juu