Kwa nini Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu)?
Kwa
nini Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu)?
Haider: Katika
mazungumzo yaliyopita ulitaka tuzungumze juu ya uadilifu wa Masahaba, ukasema
kuwa watu hawa hawasemi uongo. Utasemaji nikikuuliza juu ya Sahaba ambaye zimepokelewa
kutoka kwake hadithi nyingi kupita kiasi. Kupita hata uwezo wake?
Khalid: Kama kwamba unataka tuzungumze juu ya
hadithi za Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) zilizopokelewa kutoka kwa
baadhi ya Masahaba (Radhiya Lllahu anhu)?
Haider: Ndiyo, tuzungumze juu ya Masahaba wanaohusika na elimu ya
hadithi.
Khalid: Si
bora tuzungumze juu ya aalim wa hadithi mashuhuri kupita wote katika Masahaba?
Haider: Nani unayemkusudia ?
Khalid: Namkusudia Abdul Rahman bin Sakhar al
Dousiy, yule Sahaba aliyejitolea kuifanya kazi ya elimu hii ya hadithi.
Haider: Mara
ya mwanzo leo nalisikia jina hili.
Khalid: Hulaumiki, kwa sababu Sahaba huyu
anajulikana zaidi kwa umaarufu wake kuliko kwa jina lake. Nakusudia Abu
Hurairah (Radhiya Lllahu anhu).
Haider: Nishamkumbuka!
mwanachuoni wetu maarufu aitwae Hussein Sharafuddin Al Mousawiy alizungumza juu
yake katika kitabu kizuri sana kiitwacho ‘Abu Hurairah’, na akabainisha ndani
yake udhaifu wa riwaya zake mtu huyu.
Khalid: Kabla sijasema lolote kuhusu kauli yako
hii, ningependa kukuuliza suali moja. Umewahi kusoma chochote juu ya Sahaba
huyu mtukufu (Radhiya Lllahu anhu) katika vitabu vya Masunni?
Haider: Kusema
kweli sijapata kusoma chochote, isipokuwa nimekwishasikia mengi sana juu yake
mtu huyu kutoka kwa wanavyuoni wetu, na wote wanasema kuwa hadithi
zilizopokelewa kutoka kwake zote si sahihi. Hata hivyo na tuzungumze juu yake,
lakini kwa utulivu, na suali langu la mwanzo nataka kujua ; mtu huyu
amesilimu mwaka gani?
Khalid: Inajulikana kuwa Abu Hurairah (Radhiya
Lllahu anhu) amesilimu mwaka wa saba baada ya Mtume (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) kuhajiri kwenda Madina na umri wake wakati ule ulikuwa miaka
thelathini, na alikuwa akiishi al Suffah (mtaa ulioshikamana na nyumba ya Mtume (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) mahali walipokuwa wakiishi masikini na wacha Mungu, na
alikuwa daima pamoja na Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam), hambanduki,
kila anapokwenda alikuwa naye mpaka siku ile Mtume (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) alipofariki dunia.
Haider: Lakini
kinachostaabisha ni ule uwezo wake wa kuhifadhi hadithi hata akaweza kuhifadhi
hadithi nyingi kuwapita Masahaba wote.
Khalid: Hii inatokana na dua aliyoombewa na
Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) pale Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu)
alipomuendea Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kumshitakia udhaifu wake wa
kuhifadhi, na Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akamwambia; ‘‘Itandaze
nguo yako’’, na alipoitandaza (Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
akamuombea dua) kisha akamwambia; ‘Sasa jifunike nayo kifuani pako’,
akajifunika na tokea siku hiyo hakusahau tena hadithi.
Haider: Hadithi
hii ngeni kwangu, je umewahi kuifanyia tahakiki ewe ndugu Khalid ?
Khalid: Hadithi hii imesimuliwa na Bukhari na
wengineo kwa hivyo ni sahihi Alhamdulillah, na hadithi hii haimo ndani ya
vitabu vya maulamaa wa Kisunni peke yao, bali imo hata ndani ya vitabu vya
hadithi vya Kishia.
Imeandikwa katika kitabu cha ‘Al Kharaij’
(1/75) na katika ‘Bihar al Anwar’ (18/913) mlango wa ‘Miujiza ya Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) na kukubaliwa kwa dua zake’ kuwa; Abu Hurairah
alimwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam); ‘Mimi
nasikia kutoka kwako hadithi nyingi kisha nazisahau’ Mtume (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) akamwambia; ‘Tandaza guo lako lote’, akatandaza kisha Mtume
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) akauweka mkono wake ndani yake kisha
akamwambia; ‘Jifunike nalo’, ‘nikajifunika’ anasema Abu Hurairah; ‘na tokea
siku hiyo sijasahau tena hadithi’.
Haider: Lakini
kinachoshangaza ni kuwa Abu Hurairah huyu amesimuliwa hadithi nyingi zisizoweza
kulingana na muda wake mfupi tokea aliposilimu.
Khalid: Kwa kuanzia ndugu Haider, ningependa
kukuuliza iwapo unazijuwa idadi ya hadithi alizozisimuliwa Abu Hurairah?
Haider: Maelfu kwa maelfu ya hadithi.
Khalid: Jaribu
kunipa idadi sahihi, kwani katika vitabu sita maarufu vya Masunni na katika
Muwata-a cha Imam Malik hadithi za Abu Hurairah zilizopokelewa ndani yake idadi
yake ni 2218 zilizokubaliwa na katika vitabu vya Sahih Bukhari na Sahih Muslim
mna hadithi 609 tu za Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu) na walizokubaliana juu
yake Bukhari na Muslim ni 326, ziko wapi sasa hizo hadithi maelfu kwa maelfu?
Haider: Si
mimi ninayesema hivyo, haya ni maneno ninayowasikia maulamaa wetu wengi
wanapozungumza juu ya mtu huyu.
Khalid: Masahaba wengi na maulamaa wengi pia
wamemsifia sana Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu) na wameisifia elimu yake
pia, mfano wa Abu Saeed al Khudary (Radhiya Lllahu anhu) aliposema;
‘Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema kuwa ‘Abu Hurairah
ni chombo cha elimu.’
Imam
Shafi naye alisema; “Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu) hodari wa kuhifadhi
kupita wote wenye kuhifadhi hadithi katika wakati wake”.
Ama
Imam Bukhari yeye amesema yafuatayo juu ya Abu Hurairah; “Maulamaa wapatao mia
nane wamepokea hadithi kutoka kwake, na alikuwa hodari wa kuhifadhi kupita watu
wote wa elimu ya hadithi wa zama zake.”
Haider: Lakini
anacholaumiwa Abu Hurairah ni kuwa hapana mtu yeyote duniani aliyewahi
kusimulia hadithi nyingi kuliko yeye. Hapana mwanadamu yeyote anayeweza
kuhifadhi hadithi nyingi kama hizo.
Khalid: Kwanza kabisa uwezo wake mkubwa wa
kuhifadhi unatokana na baraka za ile dua aliyoombewa na Mtume (Swallah Llahu
alayhi wa sallam).
Pili
Mtu aliyekiwishajitolea kutafuta elimu na kusikiliza hadithi za Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) ataweza kweli kushindwa kukusanya idadi hiyo ya
hadithi?
Tatu
Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu) alikuwa na wanafunzi wengi waliopokea kutoka
kwake hadithi hizo.
Nne
Hadithi alizozisimuliwa Abu Hurairah zimo ndani yake maneno ya Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) na zingine ni juu ya matendo ya Mtume (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) na nyingine ni juu ya matendo ya baadhi ya Masahaba
yaliyokubaliwa na Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Tano Zipo hadithi ambazo Abu Hurairah
amesimulia juu ya aliyoyasikia kutoka kwa Masahaba (Radhiya Lllahu anhu) yale
ambayo Masahaba hao waliyasikia kutoka kwa Mtume (Swallah Llahu alayhi wa
sallam).
Sita zipo hadithi nyingi pia zisizosihi
isnadi, yaani hadithi alosingiziwa tu Abu Hurairah kuwa amesimulia wakati yeye
hakuzisimulia hadithi hizo.
Saba kupania kwake Abu Hurairah (Radhiya
Lllahu anhu) kwa ajili ya kuifanya kazi hii tu. Yaani kuzikusanya hadithi
za Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Nane
Ulizungumza juu ya uwezo wake wa kuhifadhi hadithi ukasema kuwa hapana
mwanadamu anayeweza kuhifadhi namna hiyo. Sasa mimi nitakuuliza suali; Uwezo
upi unaoshangaza zaidi, ule wa Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu) kuhifadhi
hadithi elfu chache alizozisikia kutoka kwa Mtume (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) kwa muda wa miaka mitano au ule wa yule aliyehadithia maelfu kwa maelfu
ya hadithi?
Haider: Pengine
unawakusudia Maimamu wetu!
Khalid: Wala
si katika Maimamu, bali hawa ni watu wa kawaida tu na hawaifikii hata chembe
daraja ya Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu), na mmoja wao ni Aban Bin Taghalab
ambaye Jaafar Al Sadeq amesema juu yake; “Hakika
Aban Bin Taghalab amesimulia hadithi zangu 30,000, kwa hivyo na nyinyi
zisimulieni”.
Na
mwengine Muhammad bin Muslim bin Rabah, huyu amesema juu yake An Najashi katika
kitabu chake kiitwacho Al Rijal ukurasa wa 163 kuwa; ‘Muhammad
amepokea kutoka kwa Al Baqer hadithi 30,000 na amepokea kutoka kwa Al Sadiq
hadithi 16,000.’
Na
mwengine Jaber bin Yazid al Juafiy aliyesimulia hadithi nyingi
Na Al
Hurr al Amiliy ameandika katika hitimisho la kitabu chake kiitwacho ‘Wasael’
(20/151) kutoka kwa Jabir yafuatayo; “Kuwa yeye
amehadithiwa hadithi 70,000 kutoka kwa Al Baqer na amehadithia hadithi
zipatazo140,000.
Sasa
tukirudia suali lako; Je hadithi alizozisimulia Abu Hurairah zinaweza hata
kukaribia idadi ya hadithi alosimulia mtu huyu? Kwa kukupa habari tu, Abul
Hussein huyu ameandika kitabu kiitwacho ‘Al Muraja-at’ ambacho ndani
yake amewasifia sana na kuwatetea watu hawa waliohadithia maelfu kwa maelfu ya
hadithi, kwa nini basi asingefanya uadilifu angalau kidogo akamtetea na Abu
Hurairah (Radhiya Lllahu anhu) pia?
Haider: Lakini wapokeaji wa hadithi wa madhehebu ya Kishia
Mwenyezi Mungu awarehemu wanajulikana kuwa ni watu wema na waadilifu na
wanajulikana pia kwa uwezo wao mkubwa wa kuhifadhi. Tafadhali usizikanushe
fadhila hizi ewe Khalid.
Khalid: Ama kuhusu uwezo wa kuhifadhi, jambo
hili halina haja hata kuzungumza juu yake, kwani hadithi zilizoandikwa ndani ya
vitabu vyenu vya asili zinagongana na kupingana. Ama kuhusu wema wao lau kama ungesoma
kidogo tu katika vitabu vya kishia mfano kitabu kiitwacho ‘Rijal al Koshy’, nk.
ungeujuwa vizuri wema wao watu hawa waliohadithia hadithi kwa maelfu. Na hapa nakunukulia riwaya iliyoandikwa katika
kitabu hiki cha ‘Rijal al Koshy’ uk. 95 inayomzungumzia juu ya mmoja wa watu
hao aitwae al Uqaili. Anasema Al Koshy: “Al Uqaili
alikuwa miongoni mwa masahaba wa Amiri l Muuminin, na alikuwa mlevi wa kutupwa
lakini alikuwa akihadithia hadithi kama alivyokuwa akizipokea.”
Na
Abu Hamza al Thamali Thabit bin Dinar naye pia alikuwa mlevi kama ilivyoandikwa
katika kitabu hicho cha Al Koshy uk. wa 76.
Ali
bin Hamza al Batainiy alikuwa akiiba pesa za Al Maasum na khums wanazolipa
maimamu wa kishia, na hata amefikia kulaaniwa na kuambiwa kuwa ni muongo. Yote
haya yanapatikana katika kitabu kiitwacho ‘Al Waqifiyah dirasah tahaliyliyah
(1/418)’. Na wengi wengineo. Kwa hivyo katika vitabu vya Mashia si muhimu kwao
uadilifu wa msimuliaji wa hadithi, inatosha tu msimuliaji huo awe ni mtu
anayewapenda Ahli l Bayt basi hadithi zake zitakubalika na si muhimu hata kama
atakuwa muongo au mlevi au mwizi au awe fasiqi namna gani.
Haider: Juu
ya yote uliyosema ewe ndugu Khalid, lakini hizi riwaya za Abu Hurairah
hazikubaliwi na maulamaa wetu na hii ndiyo sababu huwezi kuziona ndani ya
vitabu vyetu.riwaya za mtu huyu.
Khalid: Ndugu Haider naona bora nimalize
mazungumzo haya mazuri baina yetu kwa kukujulisha kuwa Mashia waliotangulia
walikuwa wakiziandika na kuzifanyia kazi hadithi za Abu Hurairah (Radhiya
Lllahu anhu), na pia maneno yake na fatwa zake zote hizo zilikuwa zikiandikwa
na maulamaa wengi wa mwanzo wa Kishia na walikuwa wakizifanyia kazi pia na
utazikuta kwa mfano katika kitabu cha Mirza Hussein Nuri al Tubrusi katika
kitabu chake kiitwacho Mustadrak al Wasael. Ndani ya kitabu hicho ameandika
hadithi nyingi za Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu) katika mlango wa ‘Al
Ijarah’ (14/28), bali Sheikh al Mufiyd pia ameandika hadithi nyingi za Abu
Hurairah (Radhiya Lllahu anhu) katika kitabu chake kiitwacho Al Amaliy na
utazikuta katika ukurasa 111-112-113.
Na
Sheikh Al Saduq naye pia katika kitabu cha ‘Maaniy al akhbar’ ukurasa wa 80-90
ameandika hadithi zake, na pia katika kitabu ‘Ikmal al din’, ukurasa wa 136, na
katika kitabu cha Al Khiswal wa thawab al aamal pia na katika vitabu vingi
vinginevyo. Kwa nini basi unakanusha tu kabla ya hata kuangalia
kwanza ndani ya vitabu? Daima mimi husema kuwa tatizo la vijana wa Kishia wenye
kupenda kheri huwa hawapendi kusoma vile vitabu vya asili vya Kishia na pia
hawaulizi dalili kutoka kwa mashekhe wao, bali wao wanasema tu kila
wanachoambiwa na wale mashekhe wanaopenda kuzungumza bila dalili.
Haider: Unataka kuniambia kuwa yote wanayosema wanavyuoni wetu juu
ya mtu huyu si ya kweli?
Khalid: Ndiyo
ewe ndugu Haider, kwani maulamaa wote wa Ahlu Sunnah wamekubaliana juu ya
ukweli wa riwaya zake Sahaba huyu mtukufu (Radhiya Lllahu anhu), na pia
maulamaa wa Kishia waliotangulia nao pia wamezikubali riwaya zake, na kama
utasoma vitabu vyenu vilivyoandikwa na maulamaa wa zamani basi hutamuona yeyote
kati ya maulamaa wenu mwenye kumchukia au mwenye kuzikataa riwaya zake
isipokuwa mtu mjinga ambaye Mwenyezi Mungu hakumfungua kifua chake apate
kunufaika na elimu iliyo sahihi. Na lau
Haider: Lakini
anayezitoa makosa hadithi za Abu Hurairah hufanya hivyo kwa ajili ya kuitakia
kheri elimu hii ya hadithi isije ikaingia ndani yake hadithi zisizo sahihi.
Khalid: Wanaojaribu kumtia ila Abu Hurairah
(Radhiya Lllahu anhu) kusudi lao hasa ni moja tu; nalo ni kuitia ila Sunnah
iliyotahirika ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam). Na
kwa vile hawakupata njia nyingine ya kuitia ila, wakaona bora wawatie ila
waliotunukulia Sunnah hiyo, na kwa vile Abu Hurairah (Radhiya Lllahu anhu)
ndiye mashuhuri kupita wote na ndiye aliyesimulia riwaya nyingi zaidi kupita
wote ndiyo sababu wakawa wanajaribu kumtia ila.
Ijulikane kuwa watu kama Abu Hurairah
(Radhiya Lllahu anhu) na walio mfano wake katika Masahaba watukufu (Radhiya
Lllahu anhu), Mwenyezi Mungu ndiye aliyewajaalia kuifanya kazi hii ya
kutufikishia Sunnah hii tukufu ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam). Sunnah ambayo ndani yake yamo mafundisho na sheria anayoipenda
Mwenyezi Mungu na kuridhika nayo. Na sisi tunawapenda kwa ajili hiyo na kwa
ajili ya mengi mema waliyo nayo.