UZAZI WA MPANGILIO NA KUZUWIA UZAZI
Sheria ya Kiislamu inatilia nguvu kuongezeka kwa vizazi
na inahesabu kuongezeka huko kuwa ni neema
itokayo kwa Mwenyezi Mungu.
Mwenyezi Mungu anasema;
"Na
Mwenyezi Mungu amekuumbieni wake katika jinsi yenu, na akakujaalieni kutoka kwa wake zenu watoto wa
na wajukuu."
An Nahl – 72
Na
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (SAW) amesema;
"Oweni wenye kupendeza,
wenye kuzaa, kwa sababu
mimi nitajifaharisha kupitia kwenu (kwa kuwa na
watu wengi) kupita uma zote."
Ahmed
na Abu Daud
na Annasai
Ipo
tofauti baina ya 'uzazi wa
mpangilio' na 'kuzuwia uzazi'.
Uzazi wa mpango ni halali iwapo
utatumika kwa njia za kisheria,
ama kuzuwia uzazi ni haramu
isipokuwa kwa udhuru unaokubalika.
Inapohitajika kuzaa kwa mpangilio
kutokana tabu anayopata mzazi anayezaa mfululizo, inaruhusiwa kutumia njia walizokuwa wakitumia Masahaba (RA)
Imepokelewa katika Bukhari na
Muslim kutoka kwa Jabir (RA) kuwa amesema;
"Tulikuwa tukimwagia nje (maji ya
uzazi) wakati wa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (SAW) na qurani ilikuwa ikiteremka."
Akimaanisha kuwa ingelikuwa ni
haramu, basi ingeteremshwa aya ya kukataza au kuharamisha kufanya hivyo.
Na
inajuzu pia kutumia njia nyingine
Ama kuzuwia uzazi
moja kwa
moja kwa kisingizio cha kuogopa umasikini au kutoweza kulea vizuri, hiyo
ni haramu.
Ifuatayo ni Fatwa iliyotolewa na kamati ya
kudumu ya maulamaa katika mkutano wake wa nane wa kamati
ya maulamaa wakubwa uliofanyika katika mwezi wa
Shaaban mwaka 1396H;
"Shukrani ni za Mwenyezi
Mungu peke Yake, na sala
na salamu zimfikia yule ambaye
hapana Mtume baada yake.
Kwa vile sheria ya
Kiislamu inatilia nguvu kuongezeka kwa vizazi,
kwa hivyo tunaona kuwa vizazi
ni neema kubwa katika neema
za Mwenyezi Mungu alizowapa waja wake, na dalili
nyingi zilizomo ndani ya kitabu
cha Mwenyezi Mungu na ndani ya
mafunzo ya Mtume wake (SAW) zimepitiwa na kamati ya
kudumu. Na kwa vile kuzuwia uzazi kunapingana
na maumbile ya kibinadamu ambayo
Mwenyezi Mungu amewaumba kwayo, na kwa vile ni
kinyume cha sheria ya Kiislamu ambayo
Mwenyezi Mungu amewaridhia nayo waja wake, na kwa
vile wanaolingania watu katika kuzuwia uzazi lengo lao
kubwa ni kupunguza idadi na kuudhoofisha umma wa Kiislamu
ili wawe na uwezo wa
kuzitawala nchi zao na kuwatawala
watu wake.
Na
kwa vile kuyakubali
hayo ni katika
matendo ya wakati wa ujahilia,
na katika kuwa na dhanna
mbaya juu ya Mwenyezi Mungu
Subhanahu wa Taala, na katika
kuudhoofisha uhuru wa Waislamu. Kwa
ajili ya yote hayo, kamati
imeamua kuwa haijuzu kabisa kufunga uzazi wala
kuzuwia uzazi ikiwa kusudi
Mwenyezi Mungu anasema;
"Na
hakuna nyama yoyote (yaani kiumbe
chochote) katika ardhi ila
riziki yake iko juu ya
Mwenyezi Mungu."
Ama ikiwa kuzuwia
huko ni kwa
dharura isiyoepukika kama vile mwanamke hawezi kuzaa isipokuwa
kwa njia ya opreshen (operation), au kuchelewesha uzazi kwa ajili ya
sababu maalum (zenye kukubalika kisheria)walizoziona wazazi, hapo hapana
ubaya kuzuwia au kuchelewesha uzazi, na hii inatokana
na hadithi mbali mbali zilizopokelewa
kutoka kwa Masahaba (RA) kuwa walikuwa wakiyatupa nje maji ya
uzazi, na kama walivyoeleza maulamaa mbali mbali katika kuruhusu
kutumia dawa za kuzuwia uzazi
au kuitowa mimba kabla ya kutimia
siku arubaini, bali kuzuwia uzazi
wakati mwingine huwa lazima inapothibiti
kuwa mzazi atadhurika."
Wallahu taala aalam