KUVAA CHUMA AU SHABA KUNABATILISHA
SALA:?
Suali
Assalaam
Aleykum Warahmatullah,
Kuuliza si ujinga na njia mojawapo ya kupata kujua.
Ni hadith gani ya Mtume inayokataza kuvaa chuma au shaba kwenye swala
? Je impeokewa na nani hadith hiyo ?
Tunaomba kujua kwani tunaona
masheikh wengi wanaswali wamevaa saa.
Jawabu
Kutoka
kwa Abu Obeida kutoka kwa Jabir bin Zaid kutoka kwa Ibn
Abass kasema, amekataza Mtume wa Mwenyezi Mungu kusali na "Al Anuk
wa
Shabah",Na Al Anuk tafsiri yake ni madini ya tin, na Shabah
tafsiri yake ni shaba nyekundu. Na madini yaliyobakia yameingizwa
hapa kwa njia ya kiasi (analogy), Na kiasi ni msingi katika misingi
ya sharia.
Hadith kaipokea Al Imam Rabii al jameh al sahih hadithi namba 294.
Juma
Al Mazrui
----------------------------------------------------------------------------
Majibu:
Sheikh, wa'alaykum salaam warahmatullah,
Suala la kukatazwa kuvaa saa katika Swala
halijasemwa wazi pahala popote kwa upekuzi wangu.
Inavyoonyesha kuwa makatazo hayo yametukia
kwa kufasiriwa na kufahamika maana ya pamoja ya maelezo yanayosemekana kuwa ni
ya hadithi ambayo imesimuliwa na Rabii Ibn Habiib, katika wasimulizi
wanaotegemewa na Maibadhi, kuwa Mtume (rahma na amani za Allah zimwelee yeye)
alikataza kuswali na madini ya risasi (au chuma) na shaba. Kama
alivyofasiri Rabii katika kitabu chake. Na katika kufafanua hayo mmoja wa
Masheikh wa Kiibadhi As Ssalimy akasema kukatazwa huko ni kwa sababu hayo ni
mavazi ya watu wa motoni. Akiegemeza maelezo yake hayo kutokana na hadithi kuwa
mtu alimwendea Mtume rahma na amani za Allah ziwe naye. akiwa amevaa pete ya
shaba, Mtume akamwambia kuwa anasikia harufu ya Masanamu kutoka kwake, yule mt!
u akaitupa pete ile. Na mara nyingine akavaa pete ya dhahabu na Mtume rahma na
amani za Allah ziwe naye akamwambia kuwa naona kwako pambo la watu wa motoni,
yule mtu kusikia hivyo akaitupa vilevile…
Inaonyesha kutokana na haya maelezo
yanayohusiana na Mtume rahma na amani za Allah ziwe naye ambayo yametajwa
hapo juu, ndipo baadhi ya wanachuoni wa Kiibadhi wakapatia hoja ya kukatazika
kuvaa saa au kitu chenye madini katika swala. Na wakasema baadhi yao kuwa ni
haramu na wengine kuwa ni makruhu.
Hata hivyo, hadithi hiyo imedhoofishwa na
baadhi ya wanachuoni katika kitabu cha Fat-hul Baari, sasa tuangalie je, saa
kukatazwa kwake kuvaliwa katika Swala ni nini mantiki yake? Inavyoelekea
waliokataza ni kwa sababu kuna aina ya chuma katika saa, na chuma imekatazwa
kwa mujibu wa hadithi hiyo iliyotajwa huko juu.
Sasa kitu cha kuzingatia ni kuwa chuma kwa
sababu ni katika vitu au mapambo ya motoni, ndiyo maana ikakatazwa kwa mtu
kutumia katika Swala. Lakini je, hiyo chuma yenyewe ni kitu najisi? Na je,
hukumu ya kidunia inalingana na hukumu za akhera? Tutazame maelezo yafuatayo;
Ingawa chuma imetajwa kuwa ni katika mambo
ya motoni, kwa mujibu wa hadithi juu, lakini tunaona katika sehemu tofauti
katika Qur’an Mwenyeezi Mungu anatuonyesha manufaa ya matumizi ya vyuma hapa
duniani. Mifano ni kama aya zifuatazo:nataja baadhi tu;
1 1- {{
(Tukamwambia Daud) “Tengeneza
(nguo za chuma) pana, na upime vizuri katika kuunganisha; na fanyeni
vitendo vizuri; bila shaka Nayaona (yote) mnayoyatenda}} Suratu Saba’,
11
2 2- {{ Na Tukamfundisha (Daud) matengenezo ya mavazi kwa ajili yenu ili yakuhifadhini katika mapigano yenu. Je, mtakuwa katika
wanaoshukuru?}} Suratul Anbiyaa,
80
3 3- {{
Kwa hakika Tuliwapeleka Mitume Wetu kwa dalili waziwazi na Tukaviteremsha
Vitabu na uadilifu pamoja nao, ili watu wasimamie uadilifu. Na Tumekiteremsha
(Tumekiumba) chuma,
chenye nguvu nyingi na manufaa
kwa watu; na ili Mwenyeezi Mungu ajulishe anayemnusuru na Mitume wake, na hali
ya kuwa hawamuoni Mwenyeezi Mungu. Kwa yakini Mwenyeezi Mungu ni Mwenye
nguvu, Mwenye kushinda.}} Suratul Hadiyd, 25
Shahidi hizo ni kuthibitisha kuwa hizo ni
hukmu za kidunia ambazo Mwenyeezi Mungu katoa ruhsa na kuelekeza kuwa mna
manufaa katika vyuma kwa wanaadam.
Suala laja kuhusu unajisi au ubaya wa
chuma katika Swala. Iko wazi kuwa chuma na shaba si vitu najisi na haviwezi
kuharibu Swala ya mtu, na kuhusu vitu vilivyokatazwa na Mtume rahma na amani za
Allah katika Swala vimetajwa waziwazi na sababu zake ziko wazi kuhusiana na
ibada hiyo. Mfano makatazo ya kuswali kwenye kaburi; Hekima ni makatazo ya kufanya
ibada katika sehemu isiyo safi au kwa kutaka msaada kwa asiye Mwenyeezi
Mungu. Na makatazo ya kuswali katika nyakati zilizokatazwa kama wakati wa
kuchomoza jua na kushuka maana pamoja na makatazo hayo, pia baadhi ya riwaya
zinasema hu! enda zikafananisha ibada zetu na ibada za wale waliokuwa wakiabudu
vingine asiye Allah. Au makatazo ya kuswali na hali umebanwa na haja
ndogo/kubwa; kwani hali hiyo itashughulisha moyo wa mtu katika Swala yake na
kumuondolea utulivu kwenye Swala. Vilevile makatazo ya kuswali sehemu zenye
vinyago, picha n.k. kwani kutaondosha kumakinika kwa mtu kwenye Swala
yake.
Kisha baada ya kuona makatazo hayo
yaliyotajwa katika hadithi mbalimbali, tunapata uchambuzi ufuatao ambao
tunaugawa katika mafungu yafuatayo:
1- Kutoshughulika au kushughulishwa na kitu katika
swala.
2- Kutoswali sehemu yenye uchafu/najisi.
3- Kutoswali katika maeneo ambayo hupelekea ile swala
kuwa ni kwa ajili ya kuomba au kutaka msaada kingine kisicho Mwenyeezi Mungu.
Kutokana na hayo tuliyotaja, tunaona
kwamba hiyo hadithi ya makatazo ya kuswali na chuma au shaba:
a- Haiwezi kuchukuliwa kuwa vitu hivyo ni mapambo watu
wa motoni moja kwa moja.
b- Haiwezi kuchukuliwa kuwa chuma au shaba ni vitu
vilivyo najisi au uchafu na kutoweza kutumika wakati wa Swala.
3 c- Haiyumkiniki kuwa kuvaa chenye chuma au shaba
kwenye Swala au penginepo kutasababisha kumpelekea mtu kuhisi awe anaabudu
asiye Allah.
d- Haiwezi kusemwa hapa kuwa makatazo hayo yaliyotajwa
ni ya kiibada katu (ambayo hayahitaji rai wala muono) kwani kwa ujumla wa
maelezo yaliyokuja ni yale yenye kupimika kiakili na kuweza kuyalinganisha na
shahidi zingine. Ama hayo masuala ya kiabada katu yasiyohitaji uchambuzi wala
kupimwa kiakili ni kama masuala ya kutayamamu, kuoga janaba au idadi ya rakaa
za swala na mfano wa hivyo ambavyo vimekuja katika maandiko yaliyothibiti tena
kwa mitiririko mingi tofauti na maelezo kama hayo tuliyoyaona yenye kukataza
kuvaa chuma au shaba ambayo yamekuja katika simulizi moja lisilo na mitiririko
mingi na lisilowafikiana na maandiko sahihi yaliyothibiti kwenye Kitabu na
Sunnah.!
Ama inavyoonesha katika mtazamo
unaostahiki wa kisheria na makusudio sahihi yaliyomo katika
makatazo katika hadithi hiyo ambayo kama ni sahihi, huenda yakawa kwa
makusudio ya kumkataza mtu kutopatikana mishughuliko katika Swala.
Na hivyo, hukumu kama hiyo ya kukataza mtu
kuvaa saa katika Swala, hakutolazimu hali ya aina moja kwa watu wote, kuna
wanaovaa na haiwashughulishi hata chembe wala hata kuihisi chochote, na kuna
watakaohisi na ikawashulisha kiasi, na kuna wanaovaa na ikawashughulisha sana
kwa kuitizama; ima kujua wakati au kuistaajabia uzuri au vilivyomo ndani yake.
Na kutokana na hali hizo basi, na hukumu
pia hutofautiana baina ya hali za hao wavaaji, kuna itakayokuwa kuvaa kwao ni
sawa hakuna ubaya, kuna ambao itakuwa ni makruhu na kuna itakayokuwa haifai. Na
kila mmoja anaijua nafsi yake zaidi.
Pia kwa nini ikatazwe saa tu kwa sababu
inadaiwa ina chuma, na isikatazwe mikanda ya suruali ambayo ina chuma tena
kikubwa kuliko cha saa? Na nguo ngapi zenye vifungo vya chuma na
havijapewa hukumu kama hiyo ya saa? Na kama suala hapa ni uharamu wa
chuma, basi tumeona katika aya mbalimbali kuwa hakupatikani uharamu huo. Ama
ikiwa ni kwa sababu ya kumshughulisha mvaaji katika Swala, basi ijulikane si
chuma tu au saa bali ni kitu chochote kile kinachomshughulisha mtu katika Swala
yake na kumuondoshea utulivu na mawazo yake, moja kwa moja kitakuwa hakifai na
bora kiepukwe.
WA ALLAHU A’ALAM