|
|
|
|
Kutoa Zaka ni nguzo
ya tatu ya Islam. Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"Nguzo
za Islam ni tano. Shahada kuwa hapana Mola anayestahiki kuabudiwa isipokuwa
Allah, na kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na Kusimamisha Swala, na
Kutoa Zaka, na Kufunga mwezi wa Ramadhan na Kuhiji Makka kwa mwenye uwezo wa
kufika huko".
Kufaridhishwa kwa Zaka
ni jambo muhimu na tukufu sana kwa Waislam kwa sababu ya wingi wa faida yake na
kwa ajili ya haja kubwa ya kuwepo kwa jambo hilo, kutokana na masikini na mafakiri
wanaohitajia sana msaada wa ndugu zao wenye uwezo, kwani katika Kutoa Zaka
uhusiano mzuri unajengeka baina ya Waislam matajiri na Waislam masikini, na hii
ni kwa sababu siku zote moyo wa mtu huelekea na kumpenda yule anayemfanyia wema
na ihsani. Zaka inasaidia pia katika kuzisafisha na kuzitakasa nyoyo.
Mwenyezi Mungu Anasema:
ÎõÐú
ãöäú ÃóãúæóÇáöåöãú ÕóÏóÞóÉð ÊõØóåøöÑõåõãú æóÊõÒóßøöíåöã ÈöåóÇ
"Chukuwa Sadaka katika mali zao, uwasafishe na kuwatakasa
kwa ajili ya hizo (sadaka zao)".
At Tawba - 103
Katika kutoa Zaka au
Sadaka kunaizoesha nafsi katika kuwapendelea kheri watu wenye haja na katika
kuwaonea huruma na pia kunaipatia nafsi baraka nyingi kutoka kwa Mwenyezi Mungu
Subhanahu wa Taala.
Mwenyezi Mungu öAnasema:
æóãóÇ
ÃóäÝóÞúÊõã ãøöä ÔóíúÁò Ýóåõæó íõÎúáöÝõåõ æóåõæó ÎóíúÑõ ÇáÑøóÇÒöÞöíäó
"Na chochote mtakachotoa, basi Yeye Atakilipa; naye ni
Mbora wa wanaoruzuku".
Saba-a - 39
Na Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"Mwenyezi
Mungu anasema: 'Ewe mwanadamu, toa na sisi tutakupa"
Anasema Ibni
Uthaimiyn:
"Kutoa
Zaka ni jambo liliofaradhishwa katika Uislam, na ni nguzo muhimu sana baada ya
Shahada mbili na Swala, na dalili ya kuwajibika kwake imo ndani ya Qurani na
pia katika mafundisho ya Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam), pamoja na ijmai
ya Waislam, na yeyote anayeikanusha nguzo hii anakuwa Kafir aliyertadi katika
Uislam, na hukumu yake ni kutubishwa, na akitubu anasamehewa. Ama akikataa
kutubu na akaendelea kuikanusha basi hukmu yake ni kuuliwa.
Ama
anayeifanyia ubakhili au akapunguza katika Zaka yake, huyo anakuwa miongoni mwa
madhalimu wanaostahiki adhabu ya Mwenyezi Mungu.
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóÇáøóÐöíäó
íóßúäöÒõæäó ÇáÐøóåóÈó æóÇáúÝöÖøóÉó æóáÇó íõäÝöÞõæäóåóÇ Ýöí ÓóÈöíáö Çááøåö
ÝóÈóÔøöÑúåõã ÈöÚóÐóÇÈò Ãóáöíãò. íóæúãó íõÍúãóì ÚóáóíúåóÇ Ýöí äóÇÑö Ìóåóäøóãó
ÝóÊõßúæóì ÈöåóÇ ÌöÈóÇåõåõãú æóÌõäæÈõåõãú æóÙõåõæÑõåõãú åóÜÐóÇ ãóÇ ßóäóÒúÊõãú
áÃóäÝõÓößõãú ÝóÐõæÞõæÇú ãóÇ ßõäÊõãú ÊóßúäöÒõæäó
"Na
wale wakusanyao dhahabu na fedha wala hawazitoi katika njia ya Mwenyezi Mungu,
wape habari za adhabu inyoumiza inayowangoja.
Siku
(mali yao) yatakapotiwa moto katika moto wa Jahanamu, na kwa hayo vikachomwa
vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, (na huku wanaambia);
"Haya ndiyo (yale mali) mliyojilimbikia (mliyojikusanyia) nafsi zenu, basi
onjeni (adhabu ya) yale mliyokuwa mkikusanya."
At Tawba - 34 - 35
"Miongini
mwa faida za kutoa Zaka anazozipata mtu katika dini yake" anaendelea kusema
Sh. Ibin Uthaimiyn, "Ni kuitimiza nguzo katika
nguzo za Kiislam, jambo litakalomletea mtu furaha katika dunia yake na katika
akhera yake, na pia inazidi kumkaribisha mja kwa Mola wake na kumuongezea
Imani, kama ilivyo katika mambo yote ya kumtii Mwenyezi Mungu Subhanahu wa
Taala."
Zaka
ni ile haki Aliyoifaradhisha Mwenyezi Mungu kwa Muislam katika mali yake
anayotakiwa kuwapa wanaostahiki. Neno Zaka, katika lugha (katika kamusi ya
lugha ya kiarabu) maana yake ni 'Kujitakasa', kwa sababu anayetoa Zaka
anataraji kuitakasa mali yake, nafsi yake na kupata baraka kutoka kwa Mola
wake.
Mwenyezi Mungu
Anasema:
ÎõÐú
ãöäú ÃóãúæóÇáöåöãú ÕóÏóÞóÉð ÊõØóåøöÑõåõãú æóÊõÒóßøöíåöã ÈöåóÇ
"Chukuwa
Sadaka katika mali zao, uwasafishe na kuwatakasa kwa ajili ya hizo (sadaka
zao)".
At Tawba - 103
Zaka ni nguzo ya tatu
ya Uislam iliyofaradhishwa katika Qurani tukufu na katika mafundisho ya Mtume
mtukufu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), na kwa sababu ya umuhimu wake,
Mwenyezi Mungu ameitaja mara themanini na mbili katika Qurani kwa kuifuatanisha
pamoja na Swala.
Imepokelewa kutoka
kwa Ibni Abbas (Radhiya Llahu anhu) kuwa amesema:
"Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipomteua Muadh bin Jabal (Radhiya Llahu anhu)
kuwa gavana wa nchi ya Yemen na kadhi wao alimwambia:
"Unakwenda
katika nchi ya watu wa Ahlul Kitab, kwa hivyo (kwanza) walinganie katika
shahada ya Laa ilaaha illa Llah na kwamba mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu,
wakitii juu ya hilo, wafundishe kuwa Mwenyezi Mungu amewafaradhishia Swala tano
mchana na usiku, wakitii juu ya hilo, wafundishe kuwa Mwenyezi Mungu
amewafaradhishia Sadaka (Zaka) za mali zao, zichukuliwe kutoka kwa matajiri wao
na kurejeshewa masikini wao, na kama wakitii juu ya hilo, usije ukachukuwa mali
zao zenye thamani, na uiogope dua ya aliyedhulumiwa, kwani hapana kizuizi baina
yake (dua hiyo) na baina ya Mwenyezi Mungu".
Imesimuliwa na
Maimamu wote wa hadithi
Imesimuliwa pia na
Attabarani kutoka kwa Aliy (Radhiya Llahu anhu) kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) amesema:
"Mwenyezi
Mungu amewafaradhishia matajiri wa Kiislam katika mali zao kiasi cha kuwatosha
masikini wao. Na (masikini) wasingepata tabu ya njaa na mavazi isipokuwa
kutokana na ubakhili wa matajiri wao. Jueni kuwa Mwenyezi Mungu atawahesabia
hesabu nzito sana na atawapa adhabu iumizayo".
Zaka imefaradhishwa
wakati Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipokuwa Makka katika siku za
mwanzo za Uislam, lakini hapakuwekwa Nisaab, (kiwango cha mali ambacho
mtu akiwa nacho kwa muda wa mwaka analazimika kuitolea Zaka), wala kiasi cha
kulipa, isipokuwa waliachiwa Waislam wenyewe kukisia kiasi cha kutoa.
Katika mwaka wa Pili
baada ya Hijra, ilifaradhishwa kiasi chake katika kila aina ya mali na
kubainishwa vizuri.
Katika Qurani tukufu na
katika Mafundisho ya Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam), yamo mafunzo mengi
yanayopendekeza Kutoa Zaka na yanayowakemea wale wasioitoa.
Katika Qurani
Mwenyezi Mungu Anasema:
ÎõÐú
ãöäú ÃóãúæóÇáöåöãú ÕóÏóÞóÉð ÊõØóåøöÑõåõãú æóÊõÒóßøöíåöã ÈöåóÇ
"(Ewe
Mtume) Chukuwa Sadaka katika mali zao, uwasafishe na kuwatakasa kwa ajili ya
hizo (sadaka zao)".
At Tawba - 103
Na maana yake ni
"Chukuwa ewe Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) Sadaka maalum kutoka
katika mali za Waislam na uwape wanaostahiki ili wenye mali 'wasafike' kutokana
na uchafu wa ubakhili na tamaa, na kutokana na ubaya wa kuwanyima masikini haki
zao na pia 'uwatakase' nafsi zao kwa sadaka hizo na wapate baraka za Mola wao
ili waweze kupata furaha za hapa duniani na za huko akhera.
Na Akasema:
Åöäøó
ÇáúãõÊøóÞöíäó Ýöí ÌóäøóÇÊò æóÚõíõæäò. ÂÎöÐöíäó ãóÇ ÂÊóÇåõãú ÑóÈøõåõãú Åöäøóåõãú
ßóÇäõæÇ ÞóÈúáó Ðóáößó ãõÍúÓöäöíäó. ßóÇäõæÇ ÞóáöíáðÇ ãøöäó Çááøóíúáö ãóÇ
íóåúÌóÚõæäó. æóÈöÇáúÃóÓúÍóÇÑö åõãú íóÓúÊóÛúÝöÑõæäó. æóÝöí ÃóãúæóÇáöåöãú ÍóÞøñ
áøöáÓøóÇÆöáö æóÇáúãóÍúÑõæãö
"Hakika wachamungu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi.
Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
Walikuwa wakilala kidogo tu nyakati za usiku.
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye
omba".
Adhariyaat 15-19
Katika aya hiÆi Mwenyezi anatuelezea juu ya wale
atakaowaingiza katika bustani Zake na chemchem, kwa sababu walipokuwa huko
duniani walikuwa wenye kulala muda mfupi sana nyakati za usiku, na sehemu kubwa
ya usiku, walikuwa wakiswali, na nyakati za kabla ya kuingia alfajiri walikuwa
wakiomba maghfira huku wakijikurubisha kwake Subhanahu wa Taala.
Walikuwa pia watu
wenye kutoa katika mali zao kuwapa fakiri na maskini, wenye kuomba na wasiyo omba
huku wakiwaonea huruma.
Na Mwenyezi Mungu Akasema
pia:
æóÇáúãõÄúãöäõæäó
æóÇáúãõÄúãöäóÇÊõ ÈóÚúÖõåõãú ÃóæúáöíóÇÁ ÈóÚúÖò íóÃúãõÑõæäó ÈöÇáúãóÚúÑõæÝö
æóíóäúåóæúäó Úóäö ÇáúãõäßóÑö æóíõÞöíãõæäó ÇáÕøóáÇóÉó æóíõÄúÊõæäó ÇáÒøóßóÇÉó
æóíõØöíÚõæäó Çááøåó æóÑóÓõæáóåõ ÃõæúáóÜÆößó ÓóíóÑúÍóãõåõãõ Çááøåõ Åöäøó Çááøåó
ÚóÒöíÒñ Íóßöíãñ
"Na
Waumini wanaume na Waumini wanawake wao kwa wao ni marafiki walinzi. Huamrisha
mema na hukataza maovu, na hushika Sala, na hutoa Zaka, na humtii Mwenyezi
Mungu na Mtume wake. Hao Mwenyezi Mungu atawarehemu. Hakika Mwenyezi Mungu ni
Mtukufu Mwenye nguvu, Mwenye hikima".
At Tawba – 71
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Mambo
matatu naapa juu yake na nakuhadithieni hadithi muihifadhi (vizuri).
Mali
haipungui kwa kutoka sadaka, na mtu anapodhulumiwa akasubiri, basi Mwenyezi
Mungu humuongezea utukufu, na mtu anapojifungulia mlango wa kuombaomba, basi
Mwenyezi Mungu humfungulia mlango wa ufakiri".
Attirmidhy kutoka kwa
Abi Kabsha al Anmaary (Radhiya Llahu anhum)
Na kutoka kwa Abu
Huraira (Radhiya Llahu anhu) amesema kuwa; Mtume (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) amesema:
"Hakika
Mwenyezi Mungu anazikubali Sadaka na anazipokea kwa mkono wake wa kuume na
anailea kama mmoja wenu anavyomlea nyumbu wake mpaka tonge (anayoitoa sadaka)
inafikia ukubwa wa jabali Uhud".
Ahmed - Attirmidhiy
na ameisahihisha
Hadithi hii
inatujulisha kuwa mtu anapotoa Zaka au Sadaka, basi Zaka hiyo inaingia mikononi
mwa Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala kwanza, kabla haijaingia mikononi mwa
masikini anayepewa, ikitufahamisha jinsi gani Mwenyezi Mungu anavyoitukuza
ibada hii ya Kutoa Zaka na jinsi anavyompenda mja wake mwenye kutoa Zaka au
Sadaka hata akaipokea kwa mikono yake Mwenyewe Subhanahu wa Taala kwanza,
akaizidisha jaza yake na kuifanya iwe na ukubwa wa Jabali Uhud.
Anasema Waki’i:
"Hadithi hii pia
inasadikisha kauli yake Subhanahu wa Taala katika Qurani pale Aliposema:
íóÚúáóãõæÇú
Ãóäøó Çááøåó åõæó íóÞúÈóáõ ÇáÊøóæúÈóÉó Úóäú ÚöÈóÇÏöåö æóíóÃúÎõÐõ ÇáÕøóÏóÞóÇÊö
"Je!
Hawajui kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba za waja Wake na kuzipokea
Sadaka?"
At Tawba - 104
Na öAliposema:
íóãúÍóÞõ
Çááøåõ ÇáúÑøöÈóÇ æóíõÑúÈöí ÇáÕøóÏóÞóÇÊö
"Mwenyezi
Mungu huyafutia (baraka mali ya) riba, na huyatia baraka (mali inayotolewa)
Sadaka".
Al Baqarah - 276
Imepokelewa kuwa Anas
(Radhiya Llahu anhu) amesema:
"Mtu mmoja
kutoka katika kabila la Bani Tamim alimwendea Mtume (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) na kumwambia:
"Ewe
Mtume wa Mwenyezi Mungu, mimi nina mali nyingi na nina jamaa wengi na wageni
huja kwangu kwa wingi. Kwa hivyo nijulishe nini nifanye na vipi nitowe?"
Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:
"Utoe
Zaka kutoka katika mali yako, kwa sababu hiyo ni tohara itakayokutahirisha, na
uwaendee watu wako (ndugu zako wa nasaba), na uijue haki ya masikini na ya
jirani na ya muombaji".
Ahmed
Na Kutoka kwa Bibi
Aisha (Radhiya Llahu anha) kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"Mambo
matatu naapa juu yake, Mwenyezi Mungu hawezi kumfanya aliye na sehemu yake
katika Uislam akawa sawa na yule asiye na sehemu. Na sehemu za Uislam ni tatu.
Swala, Funga na Zaka. Na Mwenyezi Mungu anapokuwa pamoja na mja wake hapa
duniani, basi huko akhera hamuachi akawa na mwengine asiyekuwa Yeye. Na mtu
anayewapenda watu hapa duniani, basi siku ya Kiama Mwenyezi Mungu Atamjaalie
awe pamoja nao…."
Ahmed
Na kutoka kwa Jabir (Radhiya
Llahu anhu) amesema:
"Mtu
mmoja alimuuliza Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam);
"Ewe
Mtume wa Mwenyezi Mungu; Unasemaje juu ya mtu anayetoa Zaka ya mali yake?"
Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:
"Atakayetoa
Zaka ya mali yake, keshaiondoa shari yake".
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóÇáøóÐöíäó
íóßúäöÒõæäó ÇáÐøóåóÈó æóÇáúÝöÖøóÉó æóáÇó íõäÝöÞõæäóåóÇ Ýöí ÓóÈöíáö Çááøåö
ÝóÈóÔøöÑúåõã ÈöÚóÐóÇÈò Ãóáöíãò. íóæúãó íõÍúãóì ÚóáóíúåóÇ Ýöí äóÇÑö Ìóåóäøóãó
ÝóÊõßúæóì ÈöåóÇ ÌöÈóÇåõåõãú æóÌõäæÈõåõãú æóÙõåõæÑõåõãú åóÜÐóÇ ãóÇ ßóäóÒúÊõãú
áÃóäÝõÓößõãú ÝóÐõæÞõæÇú ãóÇ ßõäÊõãú ÊóßúäöÒõæäó
"Na
wale wakusanyao dhahabu na fedha wala hawazitoi katika njia ya Mwenyezi Mungu,
wape habari za adhabu inyoumiza inayowangoja.
Siku
(mali yao) yatakapotiwa moto katika moto wa Jahanamu, na kwa hayo vikachomwa
vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, (na huku wanaambia);
"Haya ndiyo (yale mali) mliyojilimbikia (mliyojikusanyia) nafsi zenu, basi
onjeni (adhabu ya) yale mliyokuwa mkikusanya."
At Tawba - 34 - 35
Na akasema:
æóáÇó
íóÍúÓóÈóäøó ÇáøóÐöíäó íóÈúÎóáõæäó ÈöãóÇ ÂÊóÇåõãõ Çááøåõ ãöä ÝóÖúáöåö åõæó
ÎóíúÑðÇ áøóåõãú Èóáú åõæó ÔóÑøñ áøóåõãú ÓóíõØóæøóÞõæäó ãóÇ ÈóÎöáõæÇú Èöåö
íóæúãó ÇáúÞöíóÇãóÉö æóáöáøåö ãöíÑóÇËõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖö æóÇááøåõ ÈöãóÇ
ÊóÚúãóáõæäó ÎóÈöíÑñ
"Wala
wasione wale ambao wanafanya ubakhili katika yale aliyowapa Mwenyezi Mungu
katika fadhila Zake kuwa ni bora kwao (kufanya ubakhili huko). La, ni vibaya
kwao. Watafungwa kongwa (madude ya kunasa shingoni) za yale waliyoyafanyia
ubakhili - siku ya Kiyama. Na urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu.
Na Mwenyezi Mungu ana khabari za yote mnayoyafanya."
Aali Imran - 180
Katika aya hii,
Mwenyezi Mungu amesema 'Sayutawwaquwna' na maana yake ni
(Watafungwa kongwa) badala ya 'Sawfa yutawwaquna'. (Watakuja kufungwa
kongwa).
Ameacha kutumia neno Sawfa’ akaiunganisha moja
kwa moja kwa kusema:
'Sayutawwaquwna' kwa ajili ya
kutujulisha ukaribu wa mtu kukumbana na adhabu hizo. Kwa sababu mtu akeshakufa
tu kiama chake kishasimama, na kuanzia hapo mpaka siku ya Kiama ataanza
kukumbana na baadhi ya adhabu kutokana na yale maovu aliyoyatenda.
Wangapi wametoka
majumbani mwao kwa miguu yao wenyewe, wakarudishwa wakiwa wamebebwa. Wangapi
walifunga wenyewe vifungo vya suruali zao, wakaja kufunguliwa na waoshaji
maiti.
Mwanadamu
anapotafakari juu ya wale wanaobebwa juu ya majeneza kila siku na kupelekwa
makaburini wakiacha mali zao nyingi nyuma yao, mali zitakazokuja kufaidiwa na
warithi, ataona namna gani yeye alivyohangaika kuichuma mali hiyo na nani
atakayekuja kufaidika nayo, na nani atakayehesabiwa juu ya mali hiyo.
Ikiwa mali
imepatikana kwa njia zisizokuwa za halali au ikiwa mali hiyo haikutolewa ndani
yake haki ya Mwenyezi Mungu, basi mali hizo watasatarehe nayo warithi, na yule
aliyechuma ndiye atakayeulizwa na Mwenyezi Mungu na kuhesabiwa.
Mwenyezi Mungu Subhanahu
wa Taala Akamaliza aya hii kwa kusema:
æóáöáøåö
ãöíÑóÇËõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖö æóÇááøåõ ÈöãóÇ ÊóÚúãóáõæäó ÎóÈöíÑñ
"Na
urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ana khabari
za yote mnayoyafanya."
Na maana yake ni kuwa
hata kama utawaachia mali hiyo watu wako, wao pia watakuja kufa na watakaokuja
baadaye nao watakufa, na mwisho kabisa hapana atakayebaki isipokuwa Mwenyezi
Mungu Subhanahu wa Taala, siku atakayozirithi mbingu na ardhi na kila kilicho
juu yake.
Imepokelewa kutoka
kwa Abu Huraira (Radhiya Llahu anhu) kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
amesema:
"Atakayepewa
mali kisha asitoe Zaka yake, basi mali hiyo Siku ya Kiama itageuzwa kuwa joka
dume lenye upara, mwenye madoa mawili machoni pake (kutokana na wingi wa sumu
aliyonayo), atajizungusha katika mwili wa mtu huyo, kisha atamkaba shingoni
pake huku akimwambia:
"Mimi
ndiyo hazina yako uliyokuwa ukiikusanya, mimi ndiyo mali yako", kisha
Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akaisoma aya hii:
æóáÇó
íóÍúÓóÈóäøó ÇáøóÐöíäó íóÈúÎóáõæäó ÈöãóÇ ÂÊóÇåõãõ Çááøåõ ãöä ÝóÖúáöåö åõæó
ÎóíúÑðÇ áøóåõãú
"Wala
wasione wale ambao wanafanya ubakhili katika yale aliyowapa Mwenyezi Mungu
katika fadhila Zake kuwa ni bora kwao (kufanya ubakhili huko)".
Bukhari na Muslim
Na kutoka kwa
Abdillahi bin Umar bin Khattab - Radhiyallahu anhuma amesema kuwa; "Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"Enyi
watu wa Madina, mambo matano mkija mkapewa mtihani juu yake na kuteremshiwa -
Najikinga kwa Mwenyezi Mungu yasije yakakukuteni - Hautoenea uzinzi katika
kaumu mpaka wakafikia kujitangazia, (isipokuwa) yatakuja kuenea kwao maradhi
(aina mpya) ambayo hayajakuwepo kwa waliowatangulia, na hawatopunjwa watu
katika vipimo na katika mezani isipokuwa wataletewa umasikini na shida ya
kupatikana vitu, na dhulma ya ufalme. Na watakapoacha (watu) kutoka Zaka ya
mali zao, watanyimwa mvua, na lau kama si kwa ajili ya wanyama, basi
isingenyesha mvua. Na watakapovunja ahadi ya Mwenyezi Mungu na ahadi ya Mtume
wake, watasalitishiwa adui asiyekuwa mwenzao achukuwe baadhi ya vilivyo
mikononi mwao. Na ikiwa viongozi wao hawatahukumu kwa kitabu cha Mwenyezi
Mungu, basi vitafanywa vita vyao viwe baina yao"
Ibni Majah - Al
Bazaar na Al Bayhaqi
Kutoa Zaka ni fardhi,
na ni katika mambo waliyokubaliana maulamaa wote kuwa yeyote anayeikanusha
fardhi hii anakuwa kesha toka katika dini akiwa ni kafiri aliyertadi, isipokuwa
kama mtu huyo ni Muislam mpya, na kwa ajili hiyo husameheka kutokana na
kutoelewa kwake.
Ama yule anayeacha kutoa
Zaka lakini wakati huo huo hakanushi kuwajibika kwake, huyo anapata dhambi ya
kuacha kuitoa, lakini kuacha huko hakumtoi katika dini, isipokuwa ikiwa anaishi
katika nchi inayohukumiwa na sheria ya Kiislam, basi anayehukumu atatakiwa
aichukuwe Zaka hiyo kwa nguvu.
Ipo hitilafu baina ya
maulamaa iwapo anayeacha kutoa Zaka atozwe gharama kwa kuacha kwake huko kwa
ajili ya kumtia adabu, na gharama yenyewe ni kuchukuliwa nusu ya mali yake, na
hii inatokana na hadithi iliyotolewa na Imam Ahmad na Annasaiy na Abu Daud na
Al Haakim na Al Bayhaqiy kutoka kwa Bahza bin Hakim kutoka kwa baba yake kutoka
kwa babu yake kuwa amesema:
"Nilimsikia
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akisema:
"…Atakayekataa
(kutoa Zaka) tutaichukuwa (kwa nguvu, na pia tutachukua) pamoja na nusu ya mali
yake haki katika haki ya Mola wetu Mtukufu na watu wa Aali Muhammad si halali
kwao kuchukuwa chochote katika hiyo (Zaka)".
Amesema Imam Ahmed
kuwa isnadi ya hadithi hii ni sahihi na amesema Al Hakim kuwa hii ni hadithi
sahihi.
Hata hivyo wapo
baadhi ya maulamaa walioidhoofisha hadithi hii na wengine wakasema kuwa hukmu
hii ilifutwa baadaye, wakiegemea baadhi ya hadithi zinazoelezea juu ya baadhi
ya watu waliochelewa kulipa Zaka na Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
hakuwachukulia nusu ya mali zao.
Ama ikiwa watu
watakataa kutoa Zaka wakiwa wanaelewa kuwa ni jambo la wajibu, na ikiwa zipo
nguvu za kuweza kupambana nao, basi watapigwa vita mpaka wakubali kuitoa. Na
hii inatokana na hadithi iliyosimuliwa na Bukhari na Muslim kuwa Abdillahi bin Umar
(Radhiya Llahu anhu) amesema kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
amesema:
"Nimeamrishwa
nipambane na watu mpaka watowe shahad ya; Laa ilaaha illa Llah Muhammadan
Rasulu Llah, na wasimamishe Swala na watowe Zaka. Wakishafanya hivyo, damu yao
na mali zao zitakingika kwangu isipokuwa katika kulipa haki za Kiislam, na
hesabu yao iko kwa Mwenyezi Mungu".
Imeelezwa na Abu
Huraira (Radhiya Llahu anhu) kuwa; Alipofariki Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) na Abubakar akawa (Khalifa), baadhi ya waarabu walikataa
kutoa Zaka, na Abubakar (Radhiya Llahu anhu) alitayarisha jeshi akupambana nao.
Umar akasema
(kumuuliza Abubakar):
"Vipi
unataka kupigana vita na watu (Waislam), wakati Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) alisema:
"Nimeamrishwa
nipambane na watu mpaka watowe shahada ya; Laa ilaaha illa Llah na atakayetamka
hayo itakingika kwangu mali yake na nafsi yake isipokuwa katika haki yake
(anayodaiwa au kisasi kwa makosa aliyofanya), na hesabu yake iko kwa Mwenyezi
Mungu?”
Abubakar (Radhiya
Llahu anhu) akasema:
"Wallahi
nitampiga vita yeyote atakayetenganisha baina ya Swala na Zaka, kwa sababu Zaka
ni katika 'haki yake' (shahada hiyo). Wallahi lau kama wataacha kunipa mbuzi
mdogo (na katika riwaya nyingine 'Kamba') iliyokuwa ikilipwa wakati wa Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam), ningewapiga vita kwa kukataa kwao
kuitoa".
Umar (Radhiya Llahu
anhu) akasema:
"Wallahi
nilipoona kuwa Mwenyezi Mungu amemfungulia Abubakar kifua chake aamue kuwapiga
vita, nikajuwa kuwa yuko katika haki".
Muslim - Abu Daud -
na Attirmidhy na maimamu wengine wa hadithi.
·
Muislam anayemiliki Niswaab, nacho ni
'Kiwango maalum cha mali kilichowekwa na sheria katika aina yoyote ile ya mali
inayowajibika kuitolea Zaka.
·
Niswaab hiyo lazima iwe ishatolewa
ndani yake mahitajio ya dharura ya lazima kama vile chakula, mavazi, makazi,
vyombo vya nyumbani, chombo cha usafiri na vyombo vyake vya kufanyia kazi,
madeni nk.
·
Lazima kiwango hicho kiwe kimemilikiwa
kwa muda wa mwaka mzima (mwaka wa Kiislam) bila kupungua katika wakati wowote
ule ndani ya mwaka huo, na kama kitapungua katika wakati wowote ule kabla ya
kutimia mwaka, basi hesabu nyingine mpya itaanzwa kuanzia pale kinapokamilika
tena Kiwango hicho.
Amesema Imam An
Nawawiy:
"Madhehebu
yetu na madhehebu ya Maimam Malik na Ahmad na ya maulamaa walio wengi ni kuwa;
Mali inayotolewa Zaka kwa ajili yake, kama vile dhahabu, fedha na wanyama wa
kufugwa, lazima kiwango chake kibaki kwa muda wa mwaka mzima bila kupungua. Na
wakati wowote ule kitakapopungua, basi mwaka wake unakatika, na wakati wowote
ule kitakapotimia tena, unaanza kuhesabiwa mwaka mwingine".
Abu Hanifa anasema:
"Kinachotakiwa
ni kuwepo kwa Kiwango (Niswaab) mwanzo wa mwaka na mwisho wake, na haidhuru
iwapo kitapungua katikati ya mwaka, hata kama mtu alikuwa nazo Dirham mia mbili
kisha zikapotea zote katikati ya mwaka na akabakiwa na dhirham moja tu, au kama
alikuwa na kondoo arubaini wakapungua na akabaki mmoja tu, kisha mwisho wa
mwaka akaweza kumiliki (Dirham) mia mbili kamili au (kondoo) arubaini kamili,
basi itawajibika Zaka kwa vyote".
Masharti haya
hayahusiani na Zaka za mazao na matunda, kwa sababu vitu hivyo Zaka yake
inatolewa siku ya mavuno.
Mwenyezi Mungu
anasema:
ÃóËúãóÑó
æóÂÊõæÇú ÍóÞøóåõ íóæúãó ÍóÕóÇÏöåö
"Na toeni haki yake siku ya kuvuna kwake".
Al An-am – 141
Inamuwajibikia
aliyekabidhiwa mali ya yatima au ya mtu mwenye upungufu wa akili kuitolea Zaka
mali hiyo ikifikia kiwango chake.
Kutoka kwa Abdillahi
bin Amru (Radhiya Llahu anhu), anasema kuwa; Mtume (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) amesema:
"Mwenye
kumlea yatima mwenye mali, basi aifanyie biashara mali hiyo na asiiache mpaka
ikamalizika kwa kuliwa na Sadaka (Zaka)".
Anasema Sh. Sayed
Sabeq katika Fiqhis Sunnah kuwa; Isnadi yake ina udhaifu ndani yake. Akaendelea
kusema:
“Anasema
Al Hafidh kuwa hadithi hii ina ushahidi kuwa ni 'Mursal' iliyorushwa moja kwa
moja mpaka kwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) bila ya kutaja isnadi. Ama
Imam Shafi ameikubali (hadithi hii) kwa sababu zipo hadithi nyingi zinazoelezea
juu ya kuwajibika kwa Zaka katika mali yoyote ile. Anasema Imam
Attirmidhiy kuwa wanavyuoni wamekhitalifiana juu ya kuwajibika kuitolea Zaka
mali ya yatima,” amemaliza kusema Sh. Sayed Sabeq.
Mwenyezi kumiliki
kiwango kinachomwajibisha kutoka Zaka, na wakati huo huo anadaiwa, kwanza
anatoa kiasi cha deni analodaiwa, kisha anailipia Zaka mali iliyobaki ikiwa
bado inafikia kiwango cha kutolewa Zaka. Ama ikiwa mali iliyobaki haifikii
kiwango, basi hatoi Zaka, kwa sababu wakati huo anahesabiwa kuwa ni mtu fakiri,
na Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) anasema:
"Hatoi
Sadaka (Zaka) isipokuwa mtu tajiri".
Ahmad
Na amesema:
"Ichukuliwa
(mali ya Zaka) kutoka kwa matajiri wao na kurudishiwa mafakiri wao".
Anasema Sayyid Sabeq
katika Fiqhis Sunnah kuwa, katika madhehebu ya Imam Shafi na Ahmad na Abu
Thour, ni kuwa mtu akifarki na akaacha deni la Zaka, basi inawajibika katika
mali yake kwanza kutolewa deni la Zaka hata kabla ya kutimizwa wasia aloacha na
kabla ya kupewa warithi.
Mwenyezi Mungu
anasema:
ãöä
ÈóÚúÏö æóÕöíøóÉò íõæÕöí ÈöåóÇ Ãóæú Ïóíúäò
"Baada ya kutoa aliyoyausia au kulipa deni".
An Nisaa - 11
Na Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"Deni
la Mwenyezi Mungu linastahiki zaidi kulipwa".
Na Zaka ni deni la
Mwenyezi Mungu.
Kutoka kwa Ibni Abbas
(Radhiya Llahu anhu) kuwa amesema:
“Mtu mmoja alikuja kwa Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) akasema:
"Mama
yangu amefariki na anadaiwa saumu ya mwezi mzima, je nimlipie?"
Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuuliza:
"Mama
yako angelikuwa na deni ungemlipia?"
Akasema:
"Naam,
ningemlipia".
Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:
"Basi
deni la Mwenyezi Mungu linastahiki zaidi kulipwa".
Bukhari na Muslim
Zaka ni ibada, na kwa
ajili hiyo Kutia Nia ni jambo muhimu kama ilivyo katika ibada yoyote ile. Na
nia ni kitu cha moyoni na hakina uhusiano na ulimi, na kusudi lake ni kuwa mtu
anapotoa Zaka akusudie kuitoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Hakika
ya amali yoyote ni kutokana na nia, na mtu hulipwa kutokan na nia yake".
Inawajibika kuitoa Zaka
pale wakati wake unapowadia, na haijuzu kuichelewesha isipokuwa kwa dharura
inayokubalika.
Kutoka kwa Bibi Aisha
(Radhiya Llahu anha) amesema kuwa; Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
amesema:
"Haichanganyiki
mali pamoja na Zaka isipokuwa itaiangamiza", na katika riwaya nyingine;
"Inakuwa
ishakuwajibikia katika mali yako kuitolea Zaka, kisha usiitoe, kwa hivyo (mali
ya) haramu (isiyotolewa Zaka) inaiangamiza (mali ya) halali".
Shafi na Bukhari
katika 'Attariykh'
Inajuzu kuitanguliza
na kuitoa kabla ya kufikia wakati wake hata kabla ya miaka miwili.
Anasema Al Shoukani
katika kitabu chake 'Naylu l Awtaar';
"Maulamaa
wengi kama vile Azzuhriy na Al Hassan al Basriy na Maimam Shafi na Ahmad na Abu
Hanifa wamejuzisha kuitanguliza Zaka kabla ya kufikia wakati wake".
Ama Imam Malik na
Sufyan al Thouriy na baadhi nyingine ya maulamaa wameona kuwa haijuzu
kuitanguliza kabla ya wakati wake, wao wameziegemea zile hadithi
zinazowajibisha kutoa Zaka baada ya kukamilika mwaka.
Anasema Ibni Rushd:
"Hitilafu
iliyopo baina ya maulamaa ni kuwa - Zaka ni Ibada au haki iliyowajibishwa kupewa
masikini. Wanaosema kuwa Zaka ni Ibada, wao wameifananisha na Swala na wakasema
kuwa haiwezekani kutolewa kabla ya kufikia wakati wake.
Ama
wale wenye kuona kuwa ni haki iliyowajibika, wamejuzisha kuitoa kabla ya
kufikia wakati wake ikiwa mtu mwenyewe amejitolea kufanya hivyo".
Ama Imam Shafi
ameegema madai yake katika hadithi inayosema kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) aliwahi kuchukuwa katika mali ya Al Abbas (Radhiya Llahu anhu) na
kuitolea Zaka kabla ya kufikia wakati wake.
Inapendeza kumuombea
dua mtoaji Zaka, pale anapoitoa.
Mwenyezi Mungu Anasema:
ÎõÐú
ãöäú ÃóãúæóÇáöåöãú ÕóÏóÞóÉð ÊõØóåøöÑõåõãú æóÊõÒóßøöíåöã ÈöåóÇ æóÕóáøö
Úóáóíúåöãú Åöäøó ÕóáÇóÊóßó Óóßóäñ áøóåõãú
"Chukua
sadaka katika mali zao, uwasafishe na kuwatakasa kwa ajili ya hizo (sadaka zao)
na kuwataja kwa vizuri (mbele yangu) na uwaombee dua. Hakika kuwaombea kwako
kutawapa utulivu. "
At Tawba - 103
Kutoka kwa Abudullahi
bin Abi Aufiy amesema:
“Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa pale anapoletewa mali ya Zaka akisema: "Allahumma
salliy alayhim". Na baba yangu siku moja alimpelekea mali ya Zaka akasema:
"Allahumma salliy alaa aali Abi Aufiy".
Ahmad na wengineo.
Imepokelewa kutoka
kwa Wail bin Hajar kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alimuombea mtu
mmoja aliyeleta ngamia wa Zaka akasema:
"Allahumma
barik fiyhi wa fiy Ibilihi". (Mwenyezi Mungu mbariki yeye na ngamia
wake)
Anasema Imam Shafi:
"Ni
Sunnah kwa Imam anapopokea mali ya Zaka kumuombea dua mtoaji kwa kumwambia: "Aajaraka
Llahu fiyma aatayta, wa baarik laka fiyma abqayta".
(Mwenyezi Mungu akupe
ujira mwema katika ulichotoa na akubarikie katika kilichobaki).
2.
Mazao na Matunda
3.
Mali ya Biashara
4.
Wanayama wa kufugwa
5.
Dhahabu na Fesha
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóÇáøóÐöíäó
íóßúäöÒõæäó ÇáÐøóåóÈó æóÇáúÝöÖøóÉó æóáÇó íõäÝöÞõæäóåóÇ Ýöí ÓóÈöíáö Çááøåö
ÝóÈóÔøöÑúåõã ÈöÚóÐóÇÈò Ãóáöíãò. íóæúãó íõÍúãóì ÚóáóíúåóÇ Ýöí äóÇÑö Ìóåóäøóãó
ÝóÊõßúæóì ÈöåóÇ ÌöÈóÇåõåõãú æóÌõäæÈõåõãú æóÙõåõæÑõåõãú åóÜÐóÇ ãóÇ ßóäóÒúÊõãú
áÃóäÝõÓößõãú ÝóÐõæÞõæÇú ãóÇ ßõäÊõãú ÊóßúäöÒõæäó
"Na
wale wakusanyao dhahabu na fedha wala hawazitoi katika njia ya Mwenyezi Mungu,
wape habari za adhabu inayoumiza inayowangoja.
Siku
(mali yao) yatakapotiwa moto katika moto wa Jahanamu, na kwa hayo vikachomwa
vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, (na huku wanaambia);
"Haya ndiyo (yale mali) mliyolimbikia (mliyojikusanyia) nafsi zenu, basi
onjeni (adhabu ya) yale mliyokuwa mkikusanya."
At Tawba - 34 - 35
Kwa hivyo mwenye
kumiliki viwili hivyo (Dhahabu au Fedha) ikiwa ni katika mfumo wa pesa au
mikufu au vipande (vinoo), ikitimia nisabu yake na kukamilisha mwaka na akawa
hana deni, wala shida yoyote, anawajibika kuitolea Zaka yake.
Wakati wa Mtume
Muhammad (Swalla Llahu alayhi wa sallam), watu wa Bara Arabu walikuwa wakifanya
biashara zao kwa njia ya kubadilishana bidhaa, na hawakuwa wakitumia pesa
isipokuwa wachache sana walioweza kumiliki pesa za dhahabu na za fedha
zilizokuwa zikitumika katika nchi za jirani.
Pesa zilizotengenezwa
kwa dhahabu zilikuwa zikiitwa Dinari, na zilikuwa zikiletwa kutoka nchi za
Warumi kama vile Byzantine na nyenginezo, na walikuwa pia wakitumia pesa
zilizotengenezwa kwa fedha zilizokuwa zikiitwa Dirham na hizi zilikuwa zikitoka
nchi ya Wafursi - Iran.
Kwa vile pesa hizo
zilikuwa zikiwafikia zikiwa na uzito mbali mbali, na kiasi mbali mbali,
nyengine ndogo ndogo na nyengine kubwa kubwa, na hazikuwa na kiasi maalum wala
uzito maalum, kwa hivyo watu wa Makka hawakuwa wakizitumia kama zinavyotumiwa
pesa za kawaida, bali walikuwa wakizipima na kuzipa thamani maalum waliyokubalina.
Miongoni mwa vipimo
walivyokuwa wakitumia ilikuwa ratili, ambayo wakati huo ilikuwa na uzito wa
wakia kumi na mbili na walikuwa pia wakitumia vipimo vya Mithqaal.
Kutokana na kipimo
cha Mithqaal, Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:
"Haitolewi
Zaka ikiwa dhahabu haikutimia Mithqaal ishirini ".
Karatasi za benki
(Bank notes) zinazopigwa chapa na serikali tofauti ulimwenguni, hupigwa chapa
kulingana na Dhahabu na Fedha inayomiliki serikali hizo, ama sivyo serikali
yoyote masikini au yenye madeni ingelipiga chapa idadi ya noti yenye thamani
kubwa kuliko dhahabu waliyo nayo na kuweza kulipa madeni yao na kujitajirisha.
Dhahabu hailipiwi
kitu mpaka ifikie Nisabu yake na imilikiwe (nisabu hiyo) kwa muda wa mwaka
(Mwaka wa Kiislam).
Nisabu ya dhahabu ni
mithqaal 20 au gramu 92 au Tola71/2 au wakia 3. (Baadhi ya maulamaa
wanasema kuwa Nisabu yake ni gramu 85 au Tola 5 au wakia 2), na hii inatokana
na ugumu wa kuweza kukisia bei ya vipimo vilivyokuwa vikitumika wakati wa Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) na vinavyotumika wakati wetu huu. Hapana
hitilafu juu ya kiwango cha Mithqaal 20 isipokuwa hitilafu ipo katika
kuifasiri Mithqaal katika vipimo vya kisasa.
Inapofikia kiwango hicho,
na kubaki muda wa mwaka, unaichukua na kuipeleka kuipima kwa sonara au kwa
wajuzi, na baada ya kuijua thamani yake unailipia 2.5% (mbili unusu katika mia)
ya thamani ya dhahabu yote.
Nisabu ya dhahabu
ndiyo Nisabu ya pesa za kawaida.
Kwa mfano katika nchi
ya UAE, bei ya gramu tisini na mbili ya dhahabu ni Dh. 2575/-
Kwa hivyo hicho
ndicho kiwango cha kuanzia kulipia Zaka. Na dhahabu yako inapofikia kiwango
hicho unailipia Dh. 64 /- ambayo ni mbili unusu katika mia ya thamani hiyo. Dhabu
inapozidi, na Zaka yake inaongezeka.
Unailipia thamani ya
dhahabu tu bila kuhesabu ujira wa mfuo au kazi ya mkono au thamani ya nakhshi
zake. (Gharama za ufulishaji hazimo).
Nisabu ya fedha ni
mithqaal 140 au Tola 36 au wakia 141/2.
Ikifikia kiwango
hicho na ikamilikiwa muda wa mwaka, inalipiwa moja katika arubaini au mbili
unusu katika mia ya thamani yake.
Maulamaa wameigawa
deni katika hali mbili.
1-
Ikiwa
anayedaiwa ni mtu tajiri au mtu muaminifu, deni hilo litachukuliwa mfano wa
pesa zilizowekwa dhamana katika benki ambapo wakati wowote mtu anaweza kuzipata
au ana uhakika wa kulipwa deni lake.
Katika hali hii zipo
rai tatu.
a)
Ya kwanza ni kuwa mwenye kudai
anatakiwa ailipie mali hiyo Zaka yake, juu ya kuwa halazimiki kuilipia mpaka
pale atakapozipata na wakati huo atailipia pamoja na Zaka ya siku zote za
nyuma.
b)
Ya pili ni kuwa analazimika kuilipia Zaka
yake kila unapotimia mwaka, kwa sababu pesa hizo zitahesabiwa mfano wa pesa
zilizowekwa benki, na hii ni kwa sababu aliyekopeshwa ni mtu tajiri au
muaminifu kiasi cha kuwa ana uhakika wa kulipwa au wa kuzipata pesa zake hizo
wakati wowote ule anapozitaka.
c)
Rai ya tatu ni kuwa hazilipii mpaka
pale atakapolipwa deni hilo, na hapo atazilipia Zaka ya mwaka ule mmoja tu.
Anasema Sheikh
Mohammad bin Uthaymiyn:
"Rai
ya mwanzo, nayo ni kuilipia Zaka ya miaka yote pale atakapozipata pesa zake ni
bora zaidi na inakubalika zaidi".
2-
Ikiwa
anayedaiwa ni mtu masikini au mtu asiyekuwa muaminifu, haimuwajibikii mwenye
kudai kuzitolea Zaka pesa hizo mpaka pake atakapozipata na kubaki nazo muda wa
mwaka mzima kisha atazilipia Zaka ya mwaka huo tu, ambao mali yake hiyo ilibaki
kwake kama kawaida ya utoaji wa Zaka.
Anasema Sheikh Bin
Uthaimiyn:
"Haijuzu kumdai
au kumlazimisha mtu masikini au kumshitaki na hatimaye kumuingiza jela na
kumtenganisha na watu wake ikiwa mtu huyo hana kweli uwezo wa kulipa deni, na
ikiwa mtu huyo hafanyi ujanja wa kuchelewesha makusudi, na badala yake
tunatakiwa tumsitahamilie mpaka pale Mwenyezi Mungu atakapomfariji.
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóÇÊøóÞõæÇú
íóæúãðÇ ÊõÑúÌóÚõæäó Ýöíåö Åöáóì Çááøåö Ëõãøó ÊõæóÝøóì ßõáøõ äóÝúÓò ãøóÇ
ßóÓóÈóÊú æóåõãú áÇó íõÙúáóãõæäó
"Na
kama (mkopi) ana dhiki, basi (mdai) angoje mpaka afarijike, na kama nyinyi
(mnaodai mkizisamehe deni zenu) mkazifanya sadaka, basi ni bora kwenu. Ikiwa
mnajua haya (basi fanyeni).
Na
iogopeni Siku ambayo mtarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, kisha viumbe wote
watalipwa kwa ukamiliyote waliyoyachuma, nao hawatadhulumiwa".
Al Baqarah - 280 -
281
Mtu akisema:
"Pesa
zangu kwanini nisizidai?", Anaendelea kusema Sh. Bin Uthaimiyn,
"Tunamwamia:
Ni
kweli pesa zako, lakini wewe mwenyewe ndiye uliyemkopesha pesa hizo. Pale alipokujia
kutaka kukukopa ungelimtafutia udhuru wowote ule, kisha ukampa kiasi chochote
cha mali ikiwa kama ni msaada tu kutoka kwako, basi yansingekukuta haya. Lakini
umkopeshe na hali unajuwa kuwa mtu huyu ni masikini, kisha akishindwa kukulipa
ukamshitaki, umtie jela na kumtenganisha na mke na watoto wake, jambo hilo ni
haramu kabisa na haijuzu kwa Muislam kulitenda".
(Mwisho wa maneno ya
Sheikh Ibni Uthaimiyn).
Maulamaa
wamekhitalifiana katika kuzitolea Zaka dhahabu na fedha za mapambo.
Wapo waliosema kuwa
dhahabu au fedha ya kujipamba inapofikia Nisabu yake lazima itolewe Zaka yake,
na hawa wameegemeza hadithi ya Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliposema
kumwambia mwanamke mmoja aliyemvisha mwanawe mkufu wa dhahabu akamwambia:
"Unailipia
Zaka yake?"
Akasema:
"La,
hatuilipii"
Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:
"Huogopi
Mwenyezi Mungu akakuvalisheni mikufu ya Moto? Zilipie Zaka yake".
Imam Ahmad
Na pia hadithi
iliyosimuliwa na Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha) aliposema:
"Aliingia
chumbani kwangu Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
akaniona nimevaa pete za fedha. Akaniuliza:
"Nini
hiki Ewe Aisha?"
Nikamwambia:
"Nimezitengeneza
ili nijipambe kwa ajili yako ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu".
Akasema:
"Unazilipia
Zaka yake?"
Nikasema:
"Hapana."
Akasema:
"Hiyo
inatosha kwa (kukupatia adhabu ya) Moto".
Abu Daud -
Addaraqutni na Al Baihaqi
Ama wale wanaosema
kuwa Dhahabu ya mapambo hailipiwi Zaka, wao wameegemeza hoja zao katika hadithi
iliyosimuliwa na Al Baihaqiy inayosema:
"Jabir
bin Abdillah (Radhiya Llahu anhu) aliulizwa juu ya mapambo:
"Yanatolewa
Zaka?
Akasema:
"La,
hayatolewi"
Akaulizwa:
"Hata
kama thamani yake itafikia Dinari elfu moja?'
Akasema:
"Zaidi"
(hata
kama zaidi ya thamani hiyo)
Na pia hadithi
iliyomo katika Muwataa, kitabu cha Imam Malik inayosema:
"Bibi
Aisha alikuwa akiwalea wana wa kaka yake mayatima na walikuwa na mapambo na
hakuwa akiyatolea Zaka.”
Atakayezichunguza
hadithi hizi na zile, ataona kuwa zile zinazolazimisha kuitolea Zaka dhahabu au
fedha ya mapambo ndizo zenye nguvu zaidi na zenye uhakika zaidi kuliko
zisizolazimisha - Wallahu Taala Aalam.
Hukmu yake
Wapo baadhi ya
maulamaa ambao ni wachache sana wanaosema kuwa hapana dalili ya kuwa mali ya
biashara inatolewa Zaka, lakini dalili zilizomo ndani ya Qurani na Sunnah
zinaleta maana kinyume na rai zao.
Mwenyezi Mungu Anasema:
ÎõÐú
ãöäú ÃóãúæóÇáöåöãú ÕóÏóÞóÉð ÊõØóåøöÑõåõãú æóÊõÒóßøöíåöã ÈöåóÇ æóÕóáøö
Úóáóíúåöãú Åöäøó ÕóáÇóÊóßó Óóßóäñ áøóåõãú
"Chukua
sadaka katika mali zao, uwasafishe na kuwatakasa kwa ajili ya hizo (sadaka zao)
na kuwataja kwa vizuri (mbele yangu) na uwaombee dua. Hakika kuwaombea kwako
kutawapa utulivu."
At Tawba - 103
Aya hii inaleta maana
ya ujumla kuwa Zaka inatakiwa itolewe kutoka katika mali zao (Matajiri), mali
ya aina yoyote ile ikiwemo mali ya biashara, bila kufafanua aina ya mali hiyo.
Na Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"Ichukuliwe
kutoka kwa matajiri wao na kurudishiwa mafakiri wao".
Kwa hivyo dalili hizi
zinatujulisha kuwa mali yoyote ile, ikiwemo mali ya biashara, lazima itolewe Zaka,
na kwamba Zaka hiyo ichukuliwe kutoka kwa matajiri, na bila shaka wafanya
biashara ni matajiri, na kwamba irudishwe kwa masikini. Muhimu mali hiyo iwe
imekifikia kile kiwango cha kutolewa Zaka (Niswabu) na imekamilisha muda wa
mwaka.
Mwenye kumiliki mali
ya biashara iliyofikia Niswabu, akishakamilisha mwaka anatakiwa ahesabu mali
yake yote aliyokuwa nayo kwa ajili ya biashara. Kama ni mfaya biashara wa
nyumba, basi azihesabu nyumba zake (zile tu alizozitayarisha kwa ajili ya
biashara), au ardhi au vyombo vya nyumbani, magari au nguo au biashara ya aina
yoyote ile. Atavihesabu vitu alivyokuwa navyo kwa ajili ya biashara pamoja na
kuzihesabu pesa zote alizonazo kwa ajili ya biashara kisha atazitolea Zaka
yake, nayo ni mbili unusu katika mia au moja katika arubaini.
Atafanya hesabu hiyo
bila kujali kama wakati wowote ule ndani ya mwaka ule pesa hizo zilipungua au
kuongezeka.
Ikumbukwe kuwa
vitakavyohesabiwa ni vitu vilivyotayarishwa kwa ajili ya biashara tu.
Kwa mfano mtu
anamiliki magari hata yakifikia idadi ya magari kumi au zaidi, au atataka kuuza
gari lake mwenyewe kwa ajili ya kulibadilisha tu na kununua gari jengine au
ardhi au nyumba au chochote kile, ikiwa anataka kuuza kwa ajili ya kutaka
kununua kingine badala yake au kwa ajili ya mahitajio mengine yasiyokuwa ya
kibiashara, basi mali hiyo haitolei Zaka ya biashara, na hii ni kwa sababu nia
ya kuviuza vitu hivyo si kwa ajili ya biashara.
Kumbuka pia kuwa Zaka
inatolewa kutokana na asili ya chochote kilichoongezeka kutokana mali hiyo
wakati wowote ule katika mwaka. Ama kile kilichoongezeka kutokana na asili
nyingine, basi mwaka wake unaanza kuhesabiwa kuanzia siku ile iliyoongezeka
mali hiyo.
Kwa mfano;
Mfanya biashara
alikuwa akiendela kupata faida katika biashara yake na kufikia kiasi cha
Shilingi laki kumi, kisha katika mwezi wa mwisho au hata katika siku ya mwisho
kabla ya kutimia mwaka, akapata faida kiasi cha Shilingi laki saba, pesa zote
hizo ZITAHESABIWA pamoja na Zaka ya biashara ya mwaka huo, kwa sababu asili
yake (faida iliyopatikana) inatokana na biashara hiyo anayoitolea Zaka.
Mfano mwingine:
Mfanya biashara
alikuwa akiendelea kupata faida katika biashara yake na kufikia kiasi cha
shilingi laki kumi, kisha katika mwezi wa kumi na mbili au katika siku ya
mwisho au siku yoyote ile ya mwaka huo kabla ya kuingia muda wa kulipa Zaka ya
mwaka ule, mtu huyo akarithi pesa kutoka kwa jamaa yake aliyefariki kiasi cha
Shilingi milioni moja.
Pesa hizo alizorithi HAZITOHESABIWA
katika Zaka ya mwaka huo, bali ataanza kuzihesabia mwaka wake mpya kuanzia siku
ile alizozipata pesa hizo. Kwa sababu asili ya pesa hizo hazitokani na biashara
ile anayoitolea Zaka, bali inatokana na asili nyingine, ambayo ni urithi.
Kwa kawaida mwenye
kupokea mshahara pesa zake huongezeka na kupungua katika miezi mbali mbali. Kwa
vile itakuwa vigumu kwake kuweka hesabu ya kila mwezi pale zinapokamilisha Niswabu
au kuongozeka pale zinapopungua, wanavyuoni wakasema kuwa mtu huyo ataanza
kuuhesabu mwaka wake kuanzia siku ile aliyoweza kutimiza Nisabu, na kuanzia
mwezi huo, atakuwa akiitolea Zaka mali yake kila anapotimiza mwaka.
Mwenyezi Mungu
amewajibisha kuyatolea Zaka mazao Aliposema:
æóåõæó
ÇáøóÐöí ÃóäÔóÃó ÌóäøóÇÊò ãøóÚúÑõæÔóÇÊò æóÛóíúÑó ãóÚúÑõæÔóÇÊò æóÇáäøóÎúáó
æóÇáÒøóÑúÚó ãõÎúÊóáöÝðÇ Ãõßõáõåõ æóÇáÒøóíúÊõæäó æóÇáÑøõãøóÇäó ãõÊóÔóÇÈöåðÇ
æóÛóíúÑó ãõÊóÔóÇÈöåò ßõáõæÇú ãöä ËóãóÑöåö ÅöÐóÇ ÃóËúãóÑó æóÂÊõæÇú ÍóÞøóåõ
íóæúãó ÍóÕóÇÏöåö
"Naye
(Mwenyezi Mungu) ndiye alyeiumba miti inayoegemezwa na isiyoegemezwa, na
mitende na mimea yenye matunda mbali mbaIi, na (akaumba) mizaituni na
mikomamanga inayofananana na isiyofanana. Kuleni matunda yake inapotoa matunda
na toeni haki yake siku ya kuvuna kwake".
Al An-am - 141
Katika kuifasiri aya
hii amesema Ibni Abbas (Radhiya Llahu anhu):
'Haki
yake, ni Zaka yake iliyofaradhishwa".
Wakati wa Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam), Zaka ya mazao ilikuwa ikitolewa katika Mahindi, Ngano,
Mtama, Tende na Zabibu na wengine wakaongeza 'Mchele' na wengine wakasema kuwa Zaka
ya mazao inatolewa katika chakula chochote kile kinachoweza kubaki muda mrefu
kama vile mwaka au zaidi bila kuharibika.
Matunda, hayakuwa
yakitolewa Zaka isipokuwa Tende na Zabibu. Matunda mengine hayakuwa yakitolewa Zaka
isipokuwa kama matunda hayo ni kwa ajili ya biashara, basi hapo itatolewa Zaka
ya biashara na si Zaka ya Mazao.
Zaka ya Mazao
inatolewa siku ya kuvuna na kabla ya kuuzwa wala kuliwa na si lazima itimie
mwaka.
Mazao hayatolewi Zaka
mpaka yatimie Wiski tano yakiwa safi bila magamba. Kama hayajasafishwa, basi
lazima yatimie wiski kumi.
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Chini
ya Wiski tano haitolewi Zaka".
Imam Ahmad na Al Bayhaqiy
Wiski 5 ni sawa na
pishi 300, kwa sababu wiski moja ni sawa na pishi sitini kwa pishi iliyokuwa
ikitumika wakati wa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam), na pishi sitini mara
tano ni sawa na pishi mia tatu.
Kwa vipimo vya
kisasa, anasema Ustadh Said Abdullah Seif Al Hatimiy katika kitabu chake 'Kutoa
Zaka':
"Niswaab
ya mazao ni Wisqi 5. Moja ni kilo 60 yaani kilo 300. Kilo moja ni ratili 13/4
(ratili mbili kasorobo) (300 mara 13/4 = ratili 525).
Kilo
karibu ni sawa na pishi ya mbao (vibaba vinne)."
Mwisho wa maneno ya Ustadh
Said Al Hatimiy.
Kwa hivyo mazao
yakifikia pishi 300 au ratili 525 yanakuwa yamefikia Niswaab yake (kiwango
chake) na yatatolewa Zaka yake ambayo ni moja juu ya kumi (one tenth),
hii ikiwa mazao hayo yanapata maji yake bila kuyahangaikia, yaani kama vile
kunyeshewa na mvua au maji ya mito au chemchem nk.
Ama ikiwa mkulima anayatilia
maji yeye mwenyewe kwa kuyahangaikia maji hayo, basi Zaka yake itapungua na
itakuwa ni nusu ya moja juu ya kumi.
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Kilichonyeshewa
na mvua au maji yanayopita (waadi) au yaliyotwama (Zaka yake ni) moja katika
kumi na kilichomiminiwa maji nusu ya moja katika kumi".
Bukhari na wengineo.
Mwenyezi Mungu
ameamrisha kuitoa Zaka ya mazao; "Siku ya
kuvuna kwake", na maana yake ni; kabla hakijaliwa wala kugawiwa
chochote kile ndani yake, na ikiwa mtu amekwishafanya hivyo kwa kusahau, basi
itambidi akisie kile alichotoa au alichouza na akitolee Zaka yake.
Ama kile alichokula
mkulima kabla ya kuvuna, hakimo katika hesabu.
Alipoulizwa Imam Ahmad
juu ya wanachokula wenye ardhi kabla ya mavuno alisema:
"Hapana
neno ikiwa atakula katika mazao yake kiasi anachohitajia".
Anasema Sh. Sayed
Sabiq:
"Kauli
hii pia imetamkwa na Imam Shafi na Allayth na Ibni Hazm'.
Ama
Imam Malik na Imam Abu Hanifa wanasema:
"Anachokula
mtu katika mazao yake kabla ya mavuno atahesabiwa katika Niswaab"
Mwisho wa maneno ya
Sayed Sabiq.
Baadhi ya wenye kumiliki
mitende walikuwa wakitoa Zaka yao ya mazao katika tende au zabibu au mazao
yasiyokuwa mazuri. Walikuwa wakichagua mazao yasiyokuwa mazuri na kuyatolea Zaka,
na yale mazuri walikuwa wakichukua wenyewe.
Mwenyezi Mungu Akasema:
íóÇ
ÃóíøõåóÇ ÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇú ÃóäÝöÞõæÇú ãöä ØóíøöÈóÇÊö ãóÇ ßóÓóÈúÊõãú æóãöãøóÇ
ÃóÎúÑóÌúäóÇ áóßõã ãøöäó ÇáÃóÑúÖö æóáÇó ÊóíóãøóãõæÇú ÇáúÎóÈöíËó ãöäúåõ
ÊõäÝöÞõæäó æóáóÓúÊõã ÈöÂÎöÐöíåö ÅöáÇøó Ãóä ÊõÛúãöÖõæÇú Ýöíåö æóÇÚúáóãõæÇú Ãóäøó
Çááøåó Ûóäöíøñ ÍóãöíÏñ
"Enyi
mlioamini! Toeni katika vile vizuri mlivyovichuma na katika vile
tulivyokutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya hali nyinyi
wenyewe msingevipokea isipokuwa kwa kutoviangalia (Basi Mungu atapokea
vibaya?). Basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mkwasi na asifiwaye".
Al Baqarah - 267
Anasema Imam As
Shoukani:
"Hii
ni dalili kuwa, haijuzu mtu kuwapa watu Zaka katika yale mazao mabovu na
yasiyokuwa mazuri."
Wanyama wanaofugwa
wanalazimika kutolewa Zaka kwa masharti yafuatayo:
1.
Lazima watimie Niswabu
2.
Wakamilishe mwaka
3.
Wawe wanyama wa kufugwa.
Wanyama wasiokuwa wa
kufugwa kama vile wa kupandwa au wanaotumiwa kwa kubeba mizigo au kwa kilimo
n.k. Hawa hawatolewi Zaka.
Wanyama wanaotolewa Zaka
ni Ngamia, Ng'ombe, Mbuzi na Kondoo.
Ngamia hawatolewi Zaka
mpaka watimie watano. Wakitimia watano wa kufugwa hadi tisa na kutimiza mwaka
chini ya milki ya mtu, basi atawatolea mbuzi mmoja.
Wakitimia ngamia 10
mpaka 14 atawatolea mbuzi wawili.
Na hivyo hivyo kila
wakizidi ngamia watano ataongeza mbuzi mmoja.
Wakitimia ngamia 25
mpaka 35 atatoa mtoto wa ngamia jike aliyekamilisha mwaka na kuingia mwaka wa
pili au mtoto wa ngamia dume aliyekamilisha mwaka wa 2 na anaingia wa 3.
Kuanzia ngamia 36
mpaka 45 atatoa mtoto wa ngamia jike aliyekamilisha miaka 2 na keshaingia wa 3.
Kuanzia ngamia 46
mpaka 60 atatoa mtoto wa ngamia jike aliyekamilisha miaka 3 na kuingia wa 4.
Kuanzia ngamia 61
mpaka 75 atatoa mtoto wa ngamia jike aliyekamilisha miaka 4 na kuingia mwaka wa
5.
Kuanzia ngamia 76
mpaka 90 atatoa watoto wa ngamia wawili jike waliokamilisha miaka miwili na
kuingia wa tatu.
Kuanzia ngamia 91
mpaka 120 atatoa watoto wa ngamia wa kike wawili waliotimia miaka 3 na kuingia
mwaka wa 4.
Wakizidi kuliko hapo,
basi katika kila ngamia 40 atatoa mtoto wa ngamia wa kike aliyekamilisha miaka
2 na kuingia wa 3. Na katika kila ngamia 50 waliozidi kuliko hapo atatoa mtoto
wa ngami wa kike aliyekamilisha miaka 3 na kuingia wa nne.
Anasema Sayed Sabeq
katika Fiqhis Sunnah:
"Hawatolewi Zaka
ngamia dume ikiwa wapo wa kike, lakini anatolewa mtoto wa ngamia wa kiume
aliyetimia miaka miwili na kuingia wa tatu ikiwa hajapatikana wa kike
aliyekamilisha mwaka na kuingia wa pili.
Ng'ombe hawatolewi Zaka
mpaka watimie 30 wa kufugwa. Wanapotimia 30 mpaka 39 wa kufugwa na kukamilisha
mwaka, atatolewa ndama aliyekamilisha mwaka mmoja.
Wakitimia ng'ombe 40
mpaka 59 atatolewa ndama asiyepungua umri wa miaka miwili.
Wakitimia ng'ombe 60
mpaka 79 atatolewa ndama wawili wa mwaka mmoja.
Kutoka hapo, kila
wakizidi ng'ombe 30, ataongeza kutoa ndama wa mwaka mmoja.
Na kila wakizidi
ng'ombe 40 atawatolea ndama wa miaka miwili.
Mbuzi hawatolewi Zaka
mpaka watimie 40, na wakitimia arubaini mpaka 120 wa kufugwa na kukamilisha
mwaka kwa mwenye kuwamiliki, atawatolea mtoto wa mbuzi wa mwaka mmoja.
Hatowatolea tena
mpaka wafikie idadi yao mbuzi 121.
Wakiongezeka na
kutimia 121 mpaka 200, atawatolea mtoto wa miaka miwili.
Kuanzia mbuzi 201
mpaka 300 atawatolea kondoo watatu.
Wakizidi kuliko mbuzi
300, basi atawatolea kondoo mmoja katika kila mbuzi mia waliozidi.
Inaruhusiwa pia kutoa
mbuzi badala ya kondoo.
Wanyama wengine
wasiokuwa hawa kama vile farasi, nyumbu, punda na wengineo, hawatolewi Zaka
isipokuwa kama ni kwa ajili ya biashara.
Madini inayotolewa
ardhini kama vile petroli, gesi, shaba, chuma n.k, hivi vyote havitolewi Zaka,
isipokuwa dhahabu na fedha tu na tushaelezea hapo mwanzo namna ya kutoa Zaka
yake. Ama vilivyobaki vinatolewa Zaka ya biashara baada ya kuchimbuliwa au
kutolewa na kuuzwa.
Imefaridhishwa katika mwezi wa Shaabani
mwaka wa 2 baada ya Hijra (baada ya kuhamia Madina). Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) alifaridhisha Zakatul Fitr ili iitakase saumu kutokana
na dhambi ndogo ndogo zilizopatikana ndani ya mazungumzo na matendo. Na wakati
huo huo Zaka hiyo iwe msaada kwa mafakiri na wasiojiweza katika kuisherehekea
Sikukuu.
Imepokelewa kutoka kwa Ibni Abbas (Radhiya
Llahu anhu) kuwa amesema:
"Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alifaridhisha Zaka ya Fitri kwa ajili ya
kumtakasa aliyefunga kutokana na dhambi ndogo ndogo za mazungumzo na matendo,
na ili wafaidike masikini . Atakayeitoa kabla ya Swala (ya Idi) inakubaliwa
kama Zaka ya Fitri na atakayeitoa baada ya Swala inakubaliwa kama Sadaka ya
kawaida."
Abu Daud – Ibni Majah na Addaraqutni
Alikuwa (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
akitoa Zaka ya Fitri siku ya mwisho ya mwezi wa Ramadhan kabla ya Swala ya Idi
kuswaliwa.
Abu Daud na Ibni Majah na Al Hakim
Kila aliyefunga Mwezi
wa Ramadhani mwenye kumiliki chakula cha kumtosha kwa muda wa siku moja,
inamwajibikia kutoa Zakatul Fitri, nayo ni pishi ya tende au pishi ya ngano au
pishi ya shaiyri. Anatakiwa atowe kwa ajili yake na kwa ajili ya kila
anayemtegemea kama vile wanawe, wakeze nk. na kuwapa masikini ili nao wapate
kufurahi katika Siku ya Sikukuu.
Kwa vipimo vya
kisasa, pishi moja ya mbao iliyokuwa ikitumika wakati wa Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) ni kiasi cha kilo 2.
Zaka hii ni wajibu
kwa kila Muislam mdogo na mkubwa, mwanamume au mwanamke.
Ibni Umar (Radhiya
Llahu anhu) amesema:
"Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amefaridhisha kwa kila mtu
kutoa Zakatul Fitri katika mwezi wa Ramadhani, pishi ya tende (au) pishi ya
shaiyri, ikiwa yeye ni mtumwa au mtu aliye huru, mwanamume au mwanamke, mdogo
au mkubwa miongoni mwa Waislam".
Bukhari na Muslim
Zakatul Fitri
ilifaridhishwa katika mwezi wa Shaabani mwaka wa pili baada ya Hijra kwa ajili
ya kumtwahirisha aliyefunga kutokana na makosa yoyote yale aliyotenda katika
mwezi wa Ramadhani pale alipokuwa amefunga, kama vile mazungumzo ya upuuzi au
madhambi, na wakati huo huo Zaka hiyo itawafaa masikini na wahitaji ili nao
wapate kufurahi pamoja na Waislam wenzao siku ya Sikukuu.
Ibni Abbas (Radhiya
Llahu anhu) amesema:
"Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) amefaridhisha Zakatul Fitri kwa ajili ya
kumtahirisha aliyefunga kutokana na maneno ya upuuzi au madhambi madogo madogo
na ili masikini nao wapate chakula. Atakayeitoa (Zaka hiyo) kabla ya Swala (ya
Idi) inakubaliwa Zaka yake, ama atakayeitoa baada ya Swala (ya Idi),
itahesabiwa kama ni Sadaka ya kawaida tu".
Abu Daud na Ibni
Majah na Addaraqutniy
Anayeitoa Zaka hiyo
ni mtu aliyefunga. Anajitolea yeye mwenyewe, mkewe na watoto wake wanaomtegemea
na anawatolea pia wote wale wanaomtegemea wakiwemo watumishi wake.
Iliyowajibishwa
katika Zakatul Fitri ni pishi ya ngano au ya shaiyri au ya tende au zabibu au
mchele au mahindi na vinginevyo vilivyo na mfano huo katika vyakula.
Imam Abu Hanifa peke
yake amejuzisha kutoa pesa zenye thamani hiyo badala ya kutoa nafaka panapo
udhuru
Maulamaa wengi
wamekubalina kuwa Zakatul Fitri itolewe katika Ramadhani ya mwisho, lakini
wamekhitalifiana juu ya wakati maalum unaowajibika kuitoa.
Wapo waliosema kuwa
wakati unaowajibika kuitoa ni pale jua la Ramadhani ya mwisho linapozama, na
wengine wakasema kuwa wakati wake ni kuanzia baada ya kuingia alfajiri ya siku
ya Sikukuu.
Kutokana na hitilafu
hii tunapata faida ya kuwajibika kumtolea Zaka hiyo mtoto aliyezaliwa kabla ya
kuingia alfajiri ya siku ya Sikukuu na baada ya jua kuzama, je mtoto huyo
anatolewa Zaka?
Kwa wale wenye
kufuata rai kuwa wakati wa kuitoa Zaka hiyo ni pale jua la siku ya Ramadhani ya
mwisho kuzama, mtoto huyo hatolewi Zaka kwa sababu amezaliwa baada ya
kumalizika wakati wa kuwajibika, na kwa wenye kufuata rai ya pili, kwa sababu
amezaliwa kabla ya wakati unaomwajibika.
Maulamaa wengi
wanakubali kuwa Zakatul Fitri inaweza kutangulizwa na kutolewa kabla ya wakati
wake kwa siku moja au mbili.
Hadithi iliyopokelewa
kutoka kwa Ibni Umar (Radhiya Llahu anhu) inasema:
"Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) ametuamrisha kuitoa Zakatul Fitri kabla ya watu
kutoka msikitini (katika Sala ya Idi)".
Anasema Nafe-a (Radhiya
Llahu anhu):
"Ibni
Umar (Radhiya Llahu anhu) alikuwa akiitoa kwa siku moja au siku mbili kabla ya
Siku ya Sikukuu".
Ama zaidi ya hapo,
maulamaa wamekhitalifiana.
Imam Abu Hanifa
amesema:
"Inaweza
kutolewa wakati wowote ule katika mwezi wa Ramadhani".
Imam Shafi amesema:
"Inajuzu kuitoa
(hata) katika siku za mwanzo za mwezi wa Ramadhani".
Imam Malik amesema:
"Inajuzu
kutanguliza kwa siku moja au mbili kabla ya Sikukuu".
Lakini maulamaa wote
wamekubaliana kuwa haijuzu kuiahirisha na kuitowa baada ya Idi.
Muislam anaipa mali
yake mtazamo wa aina nyingine kabisa tofauti na asiyekuwa Muislam, kwani dini
ya Kiislam inampa kila mtu haki ya kutafuta mali na kufanya biashara ya halali
na kuwa tajiri anayeweza kumiliki mali nyingi. Isipokuwa baada ya kuimiliki
mali hiyo, analazimika kuwapa maskini Zaka, ambayo ni haki yao maalum waliyopangiwa
na Mola wao Subhanahu wa Taala.
Wakati huo huo
Muislam anatakiwa ajipatie thawabu nyingi zaidi na ajiepushe na shari nyingi
pamoja na kuwasaidia ndugu na jamaa zake, na masikini waislamu wenzake wenye
kuhitaji, kwa kutowa kiasi kingine katika mali zao kwa hiari yao wenyewe na kwa
kiasi anachokitaka mwenyewe, na hii inaitwa 'Sadaka'.
Kinyume na njia
inayotumika katika nchi za kikoministi za kuwanyang'anya matajiri mali zao kwa
nguvu na kuwapa masikini, kitendo cha dhulma na cha ufisadi, kwa sababu
binadamu kwa kawaida wanakhitalifiana katika ujuzi na katika jitihada zao, na
kwa ajili hiyo lazima wahitalifiane katika ujira na mapato yao, kwani katika
kuwafanya watu wote wawe sawa katika mapato, utakuwa unamweka katika daraja
moja mvivu na mwenye kujitahidi, hodari na asiyekuwa hodari, mtaalamu na
asiyekuwa mtaalamu.
Hii ikiwa mali hiyo
wanayonyang'anywa matajiri wanapewa kweli masikini na wale wanaostahiki, na
ikiwa watu wote watakuwa sawa kweli, lakini uhakika wa mambo umethithibitisha
kuwa yanayotendeka ni kinyume kabisa na maneno yao, kwani wao huwanyang'anya
mali matajiri na kuwapa viongozi wa vyama vyao pamoja na vibaraka wao.
Mwenyezi Mungu
Anasema:
ãøóÇ
ÃóÝóÇÁ Çááøóåõ Úóáóì ÑóÓõæáöåö ãöäú Ãóåúáö ÇáúÞõÑóì Ýóáöáøóåö æóáöáÑøóÓõæáö
æóáöÐöí ÇáúÞõÑúÈóì æóÇáúíóÊóÇãóì æóÇáúãóÓóÇßöíäö æóÇÈúäö ÇáÓøóÈöíáö ßóíú áóÇ
íóßõæäó ÏõæáóÉð Èóíúäó ÇáúÃóÛúäöíóÇÁ ãöäßõãú
"Mali
aliyoleta Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake kutoka kwa watu wa hivi vijiji ni kwa
ajili ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili ya Mtume na jamaa na mayatima na masikini
na msafiri aliyeharibikiwa, ili isiwe kinyang'anyiro baina ya matajiri wenu
tu."
Al Hashar - 7
Mwenyezi Mungu katika
aya hii anatujulisha kuwa jamaa na mayatima na masikini na wasafiri
walioharibikiwa wana haki zao katika mali zetu, na anawakataza matajiri
wasiifanye mali ikawa kinyang'anyiro baina yao tu na kusahau haki za wengine.
Muislam pia anatakiwa
aitumie mali yake katika kuijenga akhera yake na kujitayarishia Pepo yake.
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóÇÈúÊóÛö
ÝöíãóÇ ÂÊóÇßó Çááøóåõ ÇáÏøóÇÑó ÇáÇÎöÑóÉó æóáóÇ ÊóäÓó äóÕöíÈóßó ãöäó ÇáÏøõäúíóÇ
æóÃóÍúÓöä ßóãóÇ ÃóÍúÓóäó Çááøóåõ Åöáóíúßó æóáóÇ ÊóÈúÛö ÇáúÝóÓóÇÏó Ýöí ÇáÇóÑúÖö
Åöäøó Çááøóåó áóÇ íõÍöÈøõ ÇáúãõÝúÓöÏöíäó
"Na
utafute kwa yale aliyokupa Mwenyezi Mungu - makazi mazuri ya akhera, wala
usisahau sehemu yako ya dunia, na ufanye wema kama Mwenyezi Mungu
alivyokufanyia, wala usitafute kufanya ufisadi katika nchi, bila shaka Mwenyezi
Mungu hawapendi mafisadi".
Al Qasas - 77
Haya ndiyo mafundisho
ya Kiislam yaliyo kinyume kabisa na mafundisho ya mafisadi wanaojishughulisha
na kukusanya mali tu na kurimbika, na wakati huo huo yanatufundisha kuwa
Musilam hatakiwi abaki msikitini tu akifanya ibada bila kujishughulisha na
elimu pamoja na kufanya biashara, na kuwaachia makafiri peke yao katika uwanja
wa elimu na biashara na viwanda, na kwa ajili hiyo wanapata nguvu ya kututawala
kiuchumi na kielimu, bali Muislam anatakiwa asiisahau pia sehemu yake ya dunia.
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóáÇ
ÊóäÓó äóÕöíÈóßó ãöäó ÇáÏøõäúíóÇ æóÃóÍúÓöä ßóãóÇ ÃóÍúÓóäó Çááøóåõ Åöáóíúßó
"Wala
usisahau sehemu yako ya dunia, na ufanye wema kama Mwenyezi Mungu
alivyokufanyia".
Al Qasas - 77
Dini ya Kiislam
inatutaka tuwe msitari wa mbele katika kutoa, na Mwenyezi Mungu amewaahidi
kheri nyingi wale wanaotoa katika njia Yake.
Mwenyezi Mungu öAnasema:
ãøóËóáõ
ÇáøóÐöíäó íõäÝöÞõæäó ÃóãúæóÇáóåõãú Ýöí ÓóÈöíáö Çááøåö ßóãóËóáö ÍóÈøóÉò
ÃóäÈóÊóÊú ÓóÈúÚó ÓóäóÇÈöáó Ýöí ßõáøö ÓõäÈõáóÉò ãøöÆóÉõ ÍóÈøóÉò æóÇááøåõ íõÖóÇÚöÝõ
áöãóä íóÔóÇÁ æóÇááøåõ æóÇÓöÚñ Úóáöíãñ
"Mfano
wa wale wanaotoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa punje
moja iliyotoa mashuke saba; ikawa katika kila shuke pana punje mia. Na Mwenyezi
Mungu humzidishia amtakaye, (zaidi kuliko hivi), na Mwenyezi Mungu ni Mwenye
wasaa mkubwa (na) Mwenye Kujua".
Al Baqarah - 261
Na Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) akasema:
"Hakika
ya sadaka inazima ghadhabu ya Mola Mlezi na inamuondolea maiti adhabu"
Attirmidhiy
Na akasema:
"Haipiti
asubuhi wanayoiamkia watu, ila Malaika wawili wanateremka. Mmoja wao anasema: "Mwenyezi
Mungu muongezee mtoaji badala ya kile anachokitoa".Na mwengine anasema: "Mwenyezi
Mungu mharibie mali yake (usiite baraka) aliyeacha kutoa ".
Muslim
Sadaka haina maana ya
kutoa pesa tu au kumsaidia mtu, bali Sadaka ziko aina nyingi sana.
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Kila
Muislam anatakiwa atoe Sadaka".
Wakasema:
"Ewe
Mtume wa Mwenyezi Mungu, asiyekuwa na mali (je)?"
Akasema:
"Afanye
kazi kwa mikono yake, ajisaidie nafsi yake kisha atoe Sadaka".
Wakasema:
"Ikiwa
hajapata?"
Akasema:
"Amsaidie
mwenye shida".
Wakasema:
"Asipompata?"
Akasema:
"Afanye
mema na aache shari, kwani akifanya hivyo anaandikiwa (thawabu ya)
Sadaka".
Bukhari na wengineo
Na katika riwaya
nyingnem amesema:
"Kila
siku jua linapochomoza nafsi inaandikiwa juu ya kila inachotenda (katika thawabu
ya) Sadaka. Katika hayo ni kuwapatanisha wawili wanaogombana (anaandikiwa mtu
thawabu ya kutoa) Sadaka. Akimsaidia mtu kumnyanyua ili aweze kumpanda mnyama
wake, anaandikiwa Sadaka, akimnyanyulia mzigo wake, Sadaka, kuondoa udhia
barabarani, Sadaka, neno jema, Sadaka, na kila hatua anayokwenda msikitini
Sadaka".
Ahmad na wengineo
Na akasema:
"Kati
yenu kama yupo mwenye kuuogopa moto, basi atoe Sadaka walau kwa nusu ya tende,
na asiyepata, basi kwa neno jema”.
Ahmad na Muslim
Na akasema:
"Siku
ya Kiama Mwenyezi Mungu Atasema:
"Ewe
mwanadamu, niliumwa (kwa nini) hukunitembelea?"
Atasema
(mwanadamu):
"Ewe
Mola Mlezi, vipi nitakutembelea na wewe ni Mola wa Ulimwengu?"
Atasema:
"Hukujuwa
kuwa mja wangu fulani alikuwa akiumwa na hukumtembelea? Ama ungelimtembelea,
ungelinikuta kwake. Ewe mwanadamu nimekuomba chakula na wewe hukunilisha?"
Atasema:
"Ewe
Mola wangu, vipi nitakulisha na wewe ni Mola wa ulimwengu wote?"
Atasema:
"Hukujuwa
kuwa fulani alikuomba chakula na hukumpa. Huelewe kuwa ungelimpa chakula,
ungelikikuta kwangu?
Ewe
mwanadamu, nilikuomba maji hukunipa".
Atasema:
"Ewe
Mola wangu, vipi nitakunywesha nawe ni Mola wa Ulimwengu wote?'
Atasema:
"Mtu
fulani alikuomba maji, na wewe hukumpa. Ama ungelimpa ungeyakuta hayo
kwangu".
Muslim
Na Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) akasema pia:
"Mtu
hapandi kitu au halimi kitu kisha mwanadamu akala katika mazao hayo au mnyama
au chochote ila ataandikiwa kwa ajili yake Sadaka".
Ahmad na Attirmidhiy
Na akasema:
"Kila
wema ni Sadaka, na katika wema ni kumkabili mwenzio kwa uso wa bashasha…(uso
mkunjufu)."
Ahmad na Attirmidhiy
Watu wako, mkeo na
watoto wako pamoja na ndugu zako wa nasaba ndio wanaoistahiki zaidi sadaka
yako.
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Mmoja
wenu akiwa fakiri, basi ajitosheleze nafsi yake, kinachozidi awape watoto wake,
kinachozidi, awape ndugu zake wa nasaba, na kikizidi basi atoe huku na kule".
Ahmad na Muslim
Hukumu ya Sadaka
inahitilafiana na ya Zaka, kwani mali ya Zaka haijuzu kupewa asiyekuwa Muislam,
lakini Sadaka anaweza kupewa asiyekuwa Muislam.
Mwenyezi Mungu
Anasema:
æóíõØúÚöãõæäó
ÇáØøóÚóÇãó Úóáóì ÍõÈøöåö ãöÓúßöíäðÇ æóíóÊöíãðÇ æóÃóÓöíÑðÇ
"Na
huwalisha chakula maskini na mayatima na wafungwa na hali ya kuwa wenyewe
wanakipenda".
Ad Dahar - 8
Neno lililotumika kwa
'wafungwa', katika aya hii ni 'Asiyran', na maana yake ni mateka wa
kivita ambaye bila shaka ni kafiri aliyetekwa baada ya kupigana vita dhidi ya
Waislam, lakini juu ya hivyo Mwenyezi Mungu anawasifia Waislam wanaowalisha
chakula wafungwa hao.
Haijuzu kumsimbulia
au kumdharau anayepokea Sadaka kwa sababu kilichomfanya akubali kuipokea sadaka
hiyo ni umasikini wake, na mtu kumtakabaria masikini ni dhambi kubwa sana, na
anapofanya hivyo thawabu zake zinapotea bure.
Mwenyezi Mungu Anasema:
íóÇ
ÃóíøõåóÇ ÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇú áÇó ÊõÈúØöáõæÇú ÕóÏóÞóÇÊößõã ÈöÇáúãóäøö æóÇáÃÐóì
ßóÇáøóÐöí íõäÝöÞõ ãóÇáóåõ ÑöÆóÇÁ ÇáäøóÇÓö æóáÇó íõÄúãöäõ ÈöÇááøåö æóÇáúíóæúãö
ÇáÂÎöÑö
"Enyi
mlioamini! Msiharibu sadaka zenu kwa masimbulizi na udhia kama yule anayetoa
mali yake kwa kuwaonyesha watu, wala hamwamini Mwenyezi Mungu wala siku ya
mwisho".
Al Baqarah – 264
Mwenyezi Mungu
haikubali sadaka ikiwa inatokana na mali ya haramu. Mtume (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) amesema:
"Enyi
watu! Mwenyezi Mungu ni mzuri na hakubali isipokuwa kizuri tu".
Imesimuliwa kuwa siku
moja mtu mmoja aliiba tufaa kisha akaliuza, na pesa alizopata akawagawia
masikini.
Habari zilipomfikia
kadhi wa mji huo, akamwita na kumuuliza:
"Kwa
nini umeiba kisha ukazigawa sadaka pesa za mali ya wizi?"
Yule mtu akajibu:
"Kwa sababu
Mwenyezi Mungu Anasema:
ãóä
ÌóÇÁ ÈöÇáúÍóÓóäóÉö Ýóáóåõ ÚóÔúÑõ ÃóãúËóÇáöåóÇ æóãóä ÌóÇÁ ÈöÇáÓøóíøöÆóÉö ÝóáÇó
íõÌúÒóì ÅöáÇøó ãöËúáóåóÇ
"Afanyae
kitendo kizuri atalipwa mfano wake mara kumi. Na afanyae kitendo kibaya
hatalipwa ila sawa nacho tu".
Al An am - 160
Kwa
hivyo,
akaendekelea kusema mtu Yule aliyeiba tufaa: ‘Kutokana
na aya hii, mimi nilipoiba tufaa nilifanya kitendo kibaya nikalipwa dhambi moja
tu sawa na tufaa moja nililoiba, lakini nilipowagawia masikini nilifanya
kitendo chema nikalipwa mara kumi, na thawabu 10 nilizozipata kwa kuligawa
tufaa lile,ukitoa ile dhambi moja ya kuiba, nitabakiwa na thawabu tisa"
Kadhi akamwambia:
"Lakini
umesahau jambo moja ewe ndugu Muislam, (Mwenyezi Mungu ni mwema, na hakubali
isipokuwa chema tu).”
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) alisema kuwaambia Masahaba (Radhiya Llahu anhum):
"Mtu
mmoja aliyekuwa akitembea, alishikwa na kiu, akaona kisima mbele yake,
akateremka na kunywa maji ndani yake kisha akatoka. Alipokuwa akitoka alimuona
mbwa akihema kwa kiu. Yule mtu akasema; "Bila shaka mbwa huyu ameshikwa na
kiu kama nilivyoshikwa mimi. Akateremka (tena) kisimani, akajaza maji kiatu
chake, kisha akamshika kichwa chake mbwa yule na kumnywesha.
Akashukuriwa
na Mwenyezi Mungu na kughufuriwa".
Masahaba
(Radhiya Llahu anhu) wakasema:
"Hata
katika wanyama tunapata thawabu?"
Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:
"Katika
kila chenye uhai mna thawabu".
Bukhari
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Mwanadamu
anapokufa, amali zake zote zinakatika isipokuwa tatu. Sadakatun jaariah (Sadaka
inayoendela), au elimu yenye kunufaisha watu, au mtoto mwema
anayemuombea".
Ahmad na Muslim
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Atakayekufanyieni
wema mlipeni, na ikiwa hamna cha kumlipa, basi muombeeni dua mpaka muhisi kuwa
mumemlipa".
Abu Daud na Annasai
Imesimuliwa na Imam
Ahmad kutoka kwa Al Ash-ath bin Qays kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
amesema:
"Hamshukuru
Mwenyezi Mungu yule aisyewashukuru watu."
Ahmad
Na akasema:
"Alieyetendewa
jema, akasema kumwambia aliyemtendea: “Jazaaka Llahu khayran', (MwenyeziMungu
akujaze kheri), huyo amekwisha shukuru kama inavyotakikana".
Sadaka ya kawaida,
anapewa mtu yeyote hata akiwa si Muislam, ama Zakatul Fitri wanapewa watu wa
aina mbili tu, nao ni masikini na mafakiri Waislam.
Zakatul Maal (Zaka ya
mali), hii wanapewa aina 8 tu ya Waislamu waliowataja na Mwenyezi Mungu katika
kitabu chake kitukufu Aliposema:
ÅöäøóãóÇ
ÇáÕøóÏóÞóÇÊõ áöáúÝõÞóÑóÇÁ æóÇáúãóÓóÇßöíäö æóÇáúÚóÇãöáöíäó ÚóáóíúåóÇ
æóÇáúãõÄóáøóÝóÉö ÞõáõæÈõåõãú æóÝöí ÇáÑøöÞóÇÈö æóÇáúÛóÇÑöãöíäó æóÝöí ÓóÈöíáö
Çááøåö æóÇÈúäö ÇáÓøóÈöíáö ÝóÑöíÖóÉð ãøöäó Çááøåö æóÇááøåõ Úóáöíãñ Íóßöíãñ
"Sadaka
hupewa (watu hawa):-
·
Mafakiri na
·
Masikini na
·
Wanaozitumikia na
·
Wanaotiwa nguvu nyoyo zao
(juu ya Uislam) na
·
Katika kuwapa uungwana
watumwa na
·
Katika kuwasaidia Wenye
deni na
·
Katika (kutengeneza)
Mambo aliyoamrisha Mwenyezi Mungu na
·
Katika (kupewa) Wasafiri
(walioharibikiwa).
Ni
faradhi inayotoka kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi (na) Mwenye
hikima".
At Tawaba - 60.
Ayakayeichunguza aya
hii ataona kuwa Mwenyezi Mungu ametumia neno 'Lil' katika kuwataja watu aina
nne wa mwanzo wanaostahiki kupewa Zaka. Na hii inaitwa Laam ya tamliyk,
na maana yake ni kuwa lazima kuwamilikisha watu wa aina nne wa mwanzo (yaani
kuwapa mikononi mwao) Zaka yao.
Mwenyezi Mungu öAnasema:
ÅöäøóãóÇ
ÇáÕøóÏóÞóÇÊõ áöáúÝõÞóÑóÇÁ æóÇáúãóÓóÇßöíäö æóÇáúÚóÇãöáöíäó ÚóáóíúåóÇ
æóÇáúãõÄóáøóÝóÉö ÞõáõæÈõåõãú
Ama katika aina nne
waliobaki, Mwenyezi Mungu ametumia neno 'Fiy'. Na kwa kutumia neno hilo
Mwenyezi Mungu hatulazimishi, kuwamilikisha kwa kuwapa Zaka yao mikononi mwao.
Mwenyezi Mungu
anasema:
æóÝöí
ÇáÑøöÞóÇÈö æóÇáúÛóÇÑöãöíäó æóÝöí ÓóÈöíáö Çááøåö æóÇÈúäö ÇáÓøóÈöíáö
Kwa hivyo katika aina
nne za mwisho, kwa mfano kama unataka kumsaidia mwenye deni, hulazimiki kumpa
pesa hizo mkononi mwake, bali unaweza kwenda kumlipia deni hilo moja kwa moja
bila ya kumkabidhi mdaiwa huyo pesa hizo mkononi mwake. Hata hivyo, ukitaka
unaweza pia kumkabidhi mweyewe mkononi mwake.
Ukitaka kuzitumia
pesa za Zaka katika njia ya Mwenyezi Mungu, unaweza kununua kwa mfano silaha na
kuwakabidhi wapiganaji 'Mujahidiin' au unaweza kuzitumia katika njia ya
Mwenyezi Mungu bila ya kumkabidhi mtu pesa hizo mkononi mwake, wakati huo huo
unaweza ukitaka kuwakabidhi wanaohusika au wajuzi ili ipate kutumika kwa
usahihi zaidi.
Juu ya kuwa watu
wamehitalifiana juu ya nani masikini na nani fakiri, lakini kwa ujumla hawa ni
watu ambao wanachokipata hakiwatoshi katika matumizi yao ya kila siku.
Mtu anaweza kuwa
masikini hata kama anapata mshahara mkubwa lakini wakati huo huo ana watoto
wengi au wazee na ndugu wanaomtegemea anaowajibika kuwatizama, au ana madeni
kiasi ambapo juu ya kuwa anapata mshahara mkubwa, pesa hizo hazimtoshi
kuwalisha watu wake hao.
Kwa ajili hiyo juu ya
tofauti iliyopo baina ya masikini na fakiri katika sharhi yake, lakini katika
kuhitajia kwao msaada, wote wawili wapo katika hali moja.
Zipo hadithi zinazotujulisha
kuwa wapo baadhi ya masikini wenye kustahi kuombaomba juu ya shida kubwa
walokuwa nazo. Waislam wanatakiwa wawachunguze watu wa aina hii na kuwasaidia
na wasiwaache mpaka hali zao zikawa mbaya.
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) anasema:
"Masikini
si yule anayeomba akapewa tende moja au mbili akaondoka, au tonge moja au
mbili, lakini masikini wa kweli ni yule anayejizuwia. Someni mkitaka (kauli ya
Mwenyezi Mung isemayo):
ÇáÊøóÚóÝøõÝö
ÊóÚúÑöÝõåõã ÈöÓöíãóÇåõãú áÇó íóÓúÃóáõæäó ÇáäøóÇÓó ÅöáúÍóÇÝðÇ
"Utawafahamu kwa alama zao hawawaombi watu wakafanya
ung'ang'anizi".
Anayepewa Zaka ni
Masikini au Fakiri Muislam tu, ama Masikini au Fakiri asiyekuwa Muislam hapewi
katika mali ya Zaka, na kama Fakiri asiyekuwa Muislam atahitajia msaada, basi
atapewa katika mali ya Sadaka na si ya Zaka.
Wanaozitumikia Zaka
ni wale waliopewa jukumu la kuipokea, kuikusanya kutoka kwa matajiri na wenye
kazi ya kuihifadhi, waandishi, na wenye kuigawa, wakiwemo wachungaji wa wanyama
wa Zaka.
Ili waweze kupewa
katika Mali ya Zaka, watu hao lazima wawe Waislam, na wasiwe katika wale
walioharamishwa kupokea Zaka katika watu wa Ahlul Bayt ya Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) katika Banu Abdul Muttalib ambao tutawataja baadaye.
Katika wanaoitumikia Zaka,
hata akiwa mtu tajiri basi anastahiki kupewa katika mali hiyo, na ikiwa mtu wa
aina hiyo amepewa na wakubwa wanaohusika na akawa hana haja nayo mali hiyo,
basi aichukuwe na kuwagawia anaowataka au kumnunulia zawadi anayemtaka.
Imepokelewa
kuwa Umar bin Khattab (Radhiya Llahu anhu) alipokuwa akifanya kazi ya kukusanya
mali ya Zaka, Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alimpa katika mali hiyo.
Umar
(Radhiya Llahu anhu) akasema:
"Mimi
najitolea tu na sina haja ya kulipwa, mpe mwenye kuzihitajia zaidi kuliko
mimi".
Mtume
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:
"Alichokupa
Mwenyezi Mungu katika mali hii bila ya wewe mwenyewe kuiomba, uichukuwe na
uitumie au itolee Sadaka."
Bukhari na Annasai
Hawa ni watu
wanaopewa katika mali ya Zaka kwa ajili ya kulainishwa nyoyo zao na kutiwa
nguvu kutokana na udhaifu wa nyoyo hizo, na wengine hupewa kwa ajili ya
kuwaepusha Waislam na shari zao, au kuwavutia katika kuupenda Uislam na kuupa
nguvu.
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) alikuwa akiwapa wakubwa wa makabila ya kiarabu na hasa
makabila ya kibedui kwa ajili ya kuwapendekeza katika Uislam.
Imepokelewa kuwa
Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alimpa mtu mmoja aitwae Safwan bin Umayyah
ngamia wengi sana katika ngamia wa ngawira waliopatikana katika vita vya
Hunain, na Safwan huyu alikuwa mkubwa wa kabila lake.
Safwan alikuwa wakati
huo bado hajasilimu, na alipopewa mali hiyo, akarudi kwa watu wake na
kuwaambia:
"Enyi
watu wangu, ingieni katika dini ya Kiislam, kwani Muhammad anatoa utoaji wa mtu
asiyeogopa ufakiri".
(Mwenye kuchunguza,
ataona kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akiwatendea makabila
ya Kibedui tofauti na anavyowatendea watu wa mijini. Alikuwa akiwachukulia kwa
akili zao. Na hii ni kwa sababu Mabedui ni watu wagumu sana kufahamu. Hata
katika kuuliza masuali, Mabedui walikuwa wakimuuliza Mtume (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) masuali na kujibiwa, wakati masuali hayo hayo wangeuliza Masahaba
wanaokaa mjini (Radhiya Llahu anhum), basi Mtume (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) angekasirika nayo masuali hayo).
Wakati wa ukhalifa
wake Abubakar (Radhiya Llahu anhu) alikuwa akiendelea kuwapa watu wa aina hii,
lakini Umar bin Khattab (Radhiya Llahu anhu) siku moja alikataa kutoa, akawaambia:
"Hii Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akikupeni kwa ajili ya kuzizowesha nyoyo zenu
na kuzilainisha, lakini sasa Mwenyezi Mungu amekwishautukuza Uislam na hatuna
haja nanyi tena, mkitaka ingieni katika Uislam, na kama hamtaki basi baina yetu
na baina yenu ni panga. Mwenyezi Mungu amesema:
æóÞõáö
ÇáúÍóÞøõ ãöä ÑøóÈøößõãú Ýóãóä ÔóÇÁ ÝóáúíõÄúãöä æóãóä ÔóÇÁ ÝóáúíóßúÝõÑú
"Na
sema; 'Huu ni ukweli ulotoka kwa Mola wenu, basi anayetaka na aamini na
anayetaka na akufuru.”
Al Kahf - 29
Anasema Sayed Sabeq
katika Fiqhis Sunnah:
"Abubakar
(Radhiya Llahu anhu) alikubaliana na Umar (Radhiya Llahu anhu) katika uamuzi
wake huo, na hapana hata Sahaba mmoja (Radhiya Llahu anhum) aliyepinga. Na hii
ni katika Ijtihadi zake Umar (Radhiya Llahu anhu), na hata makhalifa waliokuja
baada yake, Uthmaan na Aliy (Radhiya llahu anhum) hawakuwapa tena watu wa aina
hii katika mali ya Zaka.
Hata
hivyo,"
anaendela kusema Sh. Sabeq, "hii haimaanishi
kuwa watu wa aina hii wasipewe, na Imam yeyote yule atakayetawala na akaona
kuwa ipo haja ya kuwapa watu wa aina hii, basi atawapa kwa sababu dalili ipo
katika Qurani na Sunnah.”
Uislam umeijaalia
ibada hii ya kuwagomboa mateka na watumwa kuwa ni kitendo kinachompatia mtu
thawabu nyingi sana na kumuingiza katika Pepo za Mwenyezi Mungu Subhanahu wa
Taala.
Kutoka kwa Al Barra-a
(Radhiya Llahu anhu) amesema:
"Mtu
mmoja alikuja kwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na kumwambia:
"Nijulishe
juu ya amali (njema) itakayonikurubisha na Pepo na kunibaidisha na Moto".
Akasema:
"Waachie
huru watu na wagomboe watumwa".
Akauliza
(tena):
"Ewe
Mtume wa Mwenyezi Mungu, si yote hayo yanabeba maana moja tu?"
Akasema:
"La,
(sivyo), 'kuwaachia huru' ni kujihusisha peke yako katika kuwaacha huru, na
'kuwagomboa' ni kusaidia katika kulipa thamani ya kuwagomboa".
Ahmed na
Addaraqutniy.
Wakati ule ilikuwa
mtumwa anaweza kuandikiana na kukubaliana kuwa atakapoweza kulipa malipo fulani
katika muda fulani, ataachwa huru. Kwa hivyo Waislam walitakiwa wawasaidie watu
wa aina hiyo kwa kuwalipia kiasi hicho ili waweze kujigomboa.
Hawa ni wale wenye
madeni makubwa wakashindwa kuyalipa kutokana na kula hasara katika biashara zao
nk. Sharti madeni hayo yawe katika mambo ya halali au yatokane na maasi
aliyotubu nayo mtu huyo.
Imepokelewa kutoka
kwa Maimam Ahmad na Abu Daud na Ibni Majah na Attirmidhiy, kutoka kwa Anas (Radhiya
Llahu anhu) kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alisema:
"Mas-ala
(ya kuwasaidia wenye madeni), hayawi halali isipokuwa katika mambo matatu; aliye
fakiri sana, au mwenye deni zito sana, au mwenye kudaiwa damu (ya diya - fidiya).”
(Huyu ni mtu
aliyejikuta amebebeshwa deni la diya kutokana na ndugu yake au jamaa yake
aliyeuwa kwa bahati mbaya. Ikiwa hajalipa diya hiyo, basi ndugu yake huyo au
jamaa yake atauliwa kwa ajili ya kulipa kisasi)
(Fiy sabiyli Llah),
ni njia yoyote ile inayomfikisha mtu katika kumpatia radhi za Mwenyezi Mungu
Subhanahu wa Taala, juu ya kuwa maulamaa wengi wanasema kuwa haya ni mambo
yanayohusiana na vita vya Jihadi tu pamoja na watu wanaopigana vita hivyo.
Hawa wana sehemu yao
katika mali ya Zaka wanayopewa hata kama askari mpiganaji Jihadi ni tajiri
anayejiweza.
Anasema Sayed Sabeq,
katika Fiqhis Sunnah:
"Maulamaa
wengine wamesema kuwa inajuzu kuzitumia pesa hizo katika kutengeneza njia
inayowapeleka watu Makka kwa ajili ya Hija na katika kuwanunulia maji ya kunywa
na chakula ikiwa hapana mali nyingine inayoweza kutumiwa katika kazi hiyo.
Inajuzu pia kuzitumia katika kuwasomesha na kuwatayarisha walinganiaji wa dini
kwa ajili ya kuwapeleka katika nchi zisizokuwa za Kiislam kwa ajili ya kufanya
da-awa nk."
Vitu vinavyonunuliwa
kutokana na pesa za Zaka kwa ajili ya vita, kama vile farasi, panga, nk. lazima
virudishwe katika nyumba ya hazina ya Waislam (Baytul maal) baada ya kumalizika
kwa vita.
Msafiri aliyeishiwa na
pesa akawa hana njia nyingine ya kupata pesa za matumizi, huyu anapewa katika
mali ya Zaka, sharti safari yake hiyo iwe katika mambo ya twa-a na si katika
kumuasi Mola wake, hata akiwa msafiri huyo huko kwao alikotoka ni mtu tajiri
mwenye mali nyingi.
1.
Kafiri
Katika hadithi
iliyotangulia, Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"Zichukuliwe
kutoka kwa matajiri Wao na kurejeshewa masikini Wao"
Na maana yake ni
kuwa:-
Zichukuliwe kutoka
kwa matajiri wa Kiislam na kupewa masikini wa Kiislam.
2.
Bani Hashim
Nao ni watoto wa Aliy
na Aqiyl na Jaafar na Al Abbas na Al Harith (Radhiyallahu anhum).
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Sadaka
haijuzu kupewa kwa watu wa Muhammad".
Muslim
Maulamaa
wamekhatalifiana juu ya ukoo wa Bani Al Muttalib, iwapo nao pia hawapewi katika
mali ya Zaka au wanapewa.
Imam Shafi amesema
kuwa hawa nao wasipewe katika mali ya Zaka, na hii inatokana na hadithi
iliyotolewa na Imam Shafi na Imam Ahmad na Imam Bukhari kutoka kwa Jubair bin
Mut-am aliposema:
"Siku
ya Khaibar (baada ya kumalizika vita hivyo), Mtume (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) aliikusanya upande mmoja sehemu ya ngawira ya watu wa ukoo wake katika
Bani Hashim na ya Bani Al Muttalib na akawaacha (watu wa kabila lake) katika
Bani Nofel na Bani Abdu Shams. Tukamwendea mimi na Uthman bin Affan na
kumuuliza:
"Ewe
Mtume wa Mwenyezi Mungu hawa ni Bani Hashim na sisi hatukanushi fadhila zao
kutokana daraja yako mbele ya Mwenyezi Mungu, lakini vipi hawa ndugu zetu
katika Bani Al Muttalib, umewaingiza wao ukatuacha sisi wakati nasaba yao na
yetu juu yako ni sawa sawa?"
Mtume (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) akasema:
"Sisi
na Bani Muttalib hatujafarikiana katika ujahilia wala katika Uislam, bali sisi
na wao ni kitu kimoja". Akaviingiza vidole vyake vya mkono wa kulia ndani
ya vidole vya mkono wa kushoto na kuvichanganya."
Kutokana na ushahidi
huu, baadhi ya maulamaa wakasema;
'Bani Muttalib nao
pia wanaingia katika kuharamishiwa kupewa katika Mali ya Zaka".
3.
Baba na watoto
Haijuzu mtu kumpa
katika mali ya Zaka baba yake, mama yake, watoto wake na babu zake, na hii ni
kwa sababu mtoaji Zaka anawajibika kuwatizama watu hao na kuwapa katika mali
yake, na kwa ajili hiyo, watu hao wanalazimika kuwa matajiri kutokana na
utajiri wake.
4.
Mke
Haijuzu mtu kumpa
mkewe katika mali ya Zaka, na jambo hili linakubaliwa na maulamaa wote na hii
ni kwa sababu mtu anawajibika kumtizama na kumpa mkewe katika mali yake kama
anavyowajibika kuwapa wazee wake wawili akiwa anao uwezo huo.
Anasema Ibnil
Mundhir:
"Isipokuwa
kama mke ana deni, basi hupewa Zaka katika ile sehemu ya kuwasaidia wenye
madeni kwa ajili ya kulipa deni hilo".
Ama ikiwa mke ni
tajiri mwenye uwezo wa kutoa Zaka, basi yeye anarushusiwa kumpa mumewe katika
mali ya Zaka kutokana na kauli ya Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
aliposema:
"Amesema
kweli Ibni Masaud, mumeo na mwanao wanastahiki zaidi kuwapa Sadaka".
Bukhari
5.
Haijuzu kuitumia mali ya Zaka kwa ajili
ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kama vile kujenga misikiti, kununua
misahafu, kununua vifaa vya kusaidia kuosha maiti nk. Na hii ni kwa sababu
Mwenyezi Mungu kwa hekima yake keshazitaja na kuzisherehesha njia za kutoka Zaka
katika aya iliyotangulia ya Surat At Tawba -60, na akaikamilisha aya hiyo kwa
kusema;
"Na
Mwenyezi Mungu ni Mjuzi (na) Mwenye hikima".
Zaka anapewa Muislam
anayeistahiki akiwa Muislam huyo ni mtu mwema au mtu asi, isipokuwa mtu asi
hapewi kaika mali ya Zaka ikiwa itajulikana kwa uhakika kuwa atakuja kuitumia
mali hiyo katika kuuendeleza uasi wake.
Ikijulikana kwa
uhakika kuwa ataitumia mali hiyo katika kumuasi Mwenyezi Mungu, basi mtu huyo
atanyimwa, ama ikiwa hayajulikani hayo, au ikijulikana kuwa ataitumia mali hiyo
katika shida zake, basi hapo atapewa.
Hata hivyo ni bora
kwa mtoaji Zaka aihusishe mali hiyo kwa kuwapa watu wema au maulamaa
wanaostahiki wanaoifayia kazi elimu yao, kwani Mtume (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) amesema:
"Walisheni
chakula chenu wachaMungu na mnaowajuwa katika walioamini (kweli)".
Ahmad
Anasema Ibni Taymiya:
"Asiyeswali
hapewi katika mali ya Zaka mpaka pale atakapotubu akawa anaswali."
Anasema Sayed Sabeq:
"Katika
kundi hilo wanaingia pia wale wanaomuasi Mwenyezi Mungu bila kujali wala kuona haya,
na kuendelea kuzama katika maasi huku nyoyo zao zikiwa zishafisidika na dhamiri
zao zimekwisha haribika".
Hawa hawapewi katika
mali ya Zaka isipokuwa kama Zaka hiyo itawasaidia katika kuwaongoza mwongozo
ulio sahihi au itawasaidia katika kutoka hali yao hiyo.
Mtume (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amekataza mtu kuinunua Zaka yake.
Kutoka kwa Abdillahi
bin Umar (Radhiya Llahu anhu), amesema:
"Umar
(Radhiya Llahu anhu) alimtoa farasi wake Sadaka fiy sabiyli Llah, kisha
akamkuta farasi huyo anauzwa na akataka kumnunua. Akamuuliza Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) juu ya jambo hilo, akamwambia:
"Usimnunue
na wala usirudie (kutaka kuimiliki tena) Sadaka yako"
Bukhari, Muslim na
wengineo
Baadhi ya maulamaa
wakasema kuwa kukataza huko ni kwa ajili ya kujiepusha tu, na si kwa ajili ya
kuharamisha, wakiegemea hadithi nyingine inayoruhusu mtu kuipokea sadaka yake
kama zawadi itokayo kwa masikini aliyempa.
Mulamaa wengi
wamekubali kuwa mali ya Zaka (Zakatul Maal - si Zakatul Fitr) inaweza
kusafirishwa na kutolewa katika nchi nyingine kwa wanaoistahiki zaidi ikiwa
watu wa mji anaoishi mtoaji hawaihitajii zaidi mali hiyo. Ama ikiwa katika nchi
hiyo wapo wanaoihitajia, basi zipo hadithi zinazotujulisha kuwa Zaka ya kila
nchi wanapewa masikini wake.
Katika madhehebu ya
Imam Abu Hanifa, wao wanasema:
"Ni
Makruh kuisafirisha mali ya Zaka isipokuwa ikiwa kwa ajili ya kumsaidia ndugu
wa nasaba mwenye kuihitajia, na hii inatokana na umuhimu wa kuunganisha undugu
huo, au pia kwa ajili ya watu wenye shida sana katika watu wa nchi yake, au kwa
ajili ya kuiondoa kutoka nchi ya kikafiri na kuipeleka katika nchi ya kiislam."
Madhehebu ya Imam
Shafi yanasema:
"Haijuzu
kuisafirisha mali ya Zaka na inawajibika kutolewa katika nchi iliyochumwa mali
hiyo isipokuwa pakikosekana wenye kuihitajia Zaka hiyo katika nchi hiyo".
Muadh bin Jabal (Radhiya
Llahu anhu) alipewa ugavana wa nchi ya Yemen na Mtume (Swalla Llahu alayhi wa
sallam), na alipotawala Umar bin Khattab (Radhiya Llahu anhu) alimuacha Muadh
aendelea kuwa gavana wa nchi hiyo. Lakini Muadh (Radhiya Llahu anhu)
alipompelekea Umar bin Khattab (Radhiya Llahu anhu) theluthi ya mali ya Zaka, Umar
(Radhiya Llahu anhu) alikataa kuzipokea akamwambia:
"Sikukupeleka
uwe mchotaji (wa mali) wala mpokeaji wa kodi, bali nimekupeleka kwa ajili ya
kuchukua mali (ya Zaka) kutoka kwa matajiri wao na kuzirudisha kwa masikini
wao".
Muadh (Radhiya Llahu
anhu) akasema:
"Nisingekuletea
ila kwa sababu sikumpata (masikini) anayezistahiki kuzichukua".
Inazuju kwa mtoaji
kuidhihirisha au kuitoa kwa siri Zaka yake, yote sawa ikiwa anachokitowa ni
Sadaka ya kawaida au Zaka ya mali, ingawaje kuitoa kwa siri ni bora zaidi.
Mwenyezi Mungu Anasema:
Åöä
ÊõÈúÏõæÇú ÇáÕøóÏóÞóÇÊö ÝóäöÚöãøóÇ åöíó æóÅöä ÊõÎúÝõæåóÇ æóÊõÄúÊõæåóÇ
ÇáúÝõÞóÑóÇÁ Ýóåõæó ÎóíúÑñ áøõßõãú
"Kama
mkitoa sadaka kwa dhahiri ni vizuri, na kama mkitoa kwa siri na kuwapa
mafakiri, basi huo ni ubora zaidi kwenu".
Al Baqarah - 271