KUTHIBITISHA MWEZI WA RAMADHAN NA
TAREHE NYENGINE ZA KIISLAMU
Qur'an wa Sunnah Society
Imefasiriwa Na Abufarida Muhammad A. Basawad
Al-hamdu
lillah. Sifa zote
njema na shukrani ni zenye kumthubutukia Mwenyezi
Mungu, Mola wa walimwengu. Tunamuhimidi na kumshukuru
Yeye na kumtaka msaada na msamaha. Kwake Yeye tunajilinda na
ushawishi wa nafsi zetu na makosa yetu. Yeyote ambae alieongozwa na Mwenyezi Mungu (kwa Rehma Zake hawezi kupotolewa na
yeyote. Na aliepotolewa na Mwenyezi Mungu (kwa Hikma
Zake) hawezi kuongozwa na yeyote.
Nashuhudia yakwamba hapana Mola apasae kuabudiwa kwa
haki illa Allah, peke yake, Asokuwa na mshirika na Muhammad (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) ni mtume Wake.
MWEZI
KONGO (CRESCENT) HUTHIBITISHA TAREHE ZA KIISLAMU:
Mwenyezi Mungu (s.w.t.)
ametubainishia ya kwamba kuandama kwa mwezi ndio njia
ya pekee ya kuthibiti kwa tarehe na matukio ya kiislamu
Wanakuuliza juu ya miezi. Sema: "Hiyo ni
vipimo vya nyakati kwa ajili (ya mambo) ya watu (mengine) na ya Hija
(zao)." [Al-Baqarah (2):189]
Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) ametilia mkazo
"Fungeni (waislamu) mukiuona mwezi kongo. Ukifichikana,
basi kamilisheni siku thalathini katika hisabu ya Sha'baan. Na mufungue
muuonapo mwezi kongo. Ukifichikana,
basi kamilisheni siku thalathini."[1]
Alikuwa mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akishughulika zaidi katika
kuhakikisha kuandama kwa mwezi wa Sha'baan, kwa sababu ifikapo siku ya ishirini
na tisa huutafuta mwezi wa Ramadhani au hukamilisha siku thalathini kabla ya
kuanza kufunga. Ikapokewa kutoka kwa 'Aisha (Radhiya
Llahu anhaa):
"Alikuwa mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akishughulika
MASHAHIDI
WANAOHITAJIKA:
Wanavyuoni wa
kiislamu wamekubaliana ya kuwa mashahidi wawili wa kiislamu wanatosheleza
ushahidi wao kuhusu kuandama kwa mwezi. Ushahidi wao umetokamana na riwaya kutoka kwa baadhi ya maswahaba (Radhiya Llahu
anhum) ya kwamba, amesema mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam):
"Waislamu wawili waadilifu wakiapa (wameuona mwezi) basi fungeni au
fungueni saumu zenu."[3]
Wakakubaliana wanavyuoni wengi zaidi kuwa ushuhuda wa Muislamu mmoja
utatosheleza kuhusu kuandama kwa mwezi. Dalili
"Watu walikuwa, wakiutafuta mwezi kongo (wa Ramadhani). Mimi nikampasha
habari mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam) yakuwa nimeuona mwezi. Kwa hivyo akafunga (siku
iliyofuata) na akawaamrisha watu wafunge."[4]
USHAHIDI
WA UTAALAMU WA NYOTA:
Hupatikana miongoni mwa watu
ambao wanapendekeza kuhisabu masiku kulingana na ilimu
ya nyota katika kuukadiria mwezi kongo.
"Sisi ni taifa lisilojuwa kusoma wala kuandika. Hatutumii maandishi wala
hesabu za ilimu ya utaalamu wa nyota (katika kufunga).
Mwezi ni kadha na kadha (akaashiria kwa mikono yake mara tatu, akakunja kidole
cha gumba mara ya tatu, kumaanisha siku ishirini na tisa) au ni kadha na kadha
na kadha (akaashiria kwa mikono yake mara tatu, kumaanisha siku
thalathini)."[5]
Riwaya ya Abu-Dawud, ikaendelea zaidi: "Kwa hivyo Ibn 'Umar alikuwa
akimaliza kufunga na watu pamoja bila ya kuzitegemea hisabu za wataalamu wa
nyota."
Hii inaonyesha vipi mtume (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) alitaka kuifanya ibada hii iwe rahisi na pia iwe katika daraja ya watu
wa kawaida. Ikaepushwa ibada
"Hali ya taifa hili ya kutojuwa kusoma na
kuandika ni sifa, kwani lajitosheleza na kila matatizo katika utekelezaji wa
misingi ya ibada."
Basi yoyote atakaepinga jambo
KUTOELEWEKA
I: UHAKIKA WA MWANZO WA MWEZI
Jambo la kawaida lisiloeleweka na lenye
umuhimu kwa watu wengi ni iwapo hatufanyi jitihada katika kukubali ushuhuda wa
wale waliodai kuuona mwezi (kwa ushahidi wa wataalamu wa nyota na njia
nyenginezo) basi huenda tukahatarisha kuzibatilisha baadhi ya ibada zetu kwa
kufunga katika siku zisizostahiki. Mwenendo kama huu umekataliwa katika uislamu
juu ya matukio mengi:
a. Jambo hili lahusiana na kutia shaka kuhusu ukweli (ushuhuda) wa
waislamu waadilifu (udul). Tumekatazwa kutokamana na
(Nas ya) Qur'an na Sunnah.
b. Jambo
c. Jambo
"Jihadharini na (kuvuka mipaka) kuongeza mambo kwenye dini; kwa hakika
waliokuwa kabla yenu waliangamizwa kwa kuongeza mambo katika dini."[6]
d. Jambo
"Watu wengi wanadhania ya kuwa mwezi mpya ukijitokeza mawinguni basi huo
ndio usiku wa kwanza wa mwezi, bila ya kujali iwapo watu wameuona mwezi au la.
Hayo ni makosa. Ni sharti mwezi huo ujitokeze kwa watu na watu wauone ili kuuanza mwezi. Ndio sababu ya
mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akasema:
'(Uhakika wa) Saumu huanza ile siku muanzapo kufunga.'[7] Ikamaanisha ya
kwamba: hii ndio siku ambayo munayoitambua
Rai hii imetiliwa mkazo na riwaya ifuatayo akasema Abu Al-Bakhturi,
"Tulikwenda kufanya umra na tukaushuhudia (kuuona) mwezi kongo wa Ramadhani,
tulipokuwa mahali paitwapo Dhatu 'Irq, ingawa mwezi wenyewe ulikuwa ni wa siku
mbili au tatu. Kisha baadae tulipomuona Ibn 'Abbas (Radhiya Llahu anhu)
tukamueleza kuhusu jambo
Jee, ikiwa wanaodai yakuwa wameuona mwezi walisema uwongo au walipitikiwa?
Maadam uislamu wao ni wenye kudhihirika na ni
waaminifu basi ni sharti kukubali ushuhuda wao na kuanza kufunga (au kufungua).
Hatuna haki yoyote kukataa bila ya kuwa na ushahidi
ulio wazi (unaoafikiana na sunnah
Kutokamana na
hadithi zilizopita, inampasa kila muislamu afuate amri kuhusu kuonekana kwa mwezi.
Kwa kulikariri jambo hilo, ikapokewa kutoka kwa Abu Huraira, 'Aisha na wengineo
(Radhiya Llahu anhum), mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"(Uhakika wa) Saum huanza ile siku muanzapo kufunga; (Uhakika wa) Fitr
('Idd) huwa ni ile siku mumalizapo kufunga; (Uhakika wa) Adh-ha ('Idd) huwa ni
ile siku munapochinja."[10]
Kwa hivyo uonekanapo mwezi popote ulimwenguni na angalau muislamu mmoja
muaminifu, hii yamaanisha ya kwamba umma mzima umeuona. Kutokamana na hayo,
KUTOELEWEKA II: MATLA' TAFAUTI
Idadi kubwa ya watu
wameipotoa riwaya ifuatayo ya Kurayb.
Akatuhadithia Kurayb yakwamba Umm ul-Fadhl Bint ul-Harith alimtuma kwenda kwa Mu'awiyah (Radhiya Llahu anhu) huko
Baada ya majadiliano kuhusu riwaya hii, Shaykh-ul-Islam Ibn Taymiyyah
(Rahimahullah) akamalizia:
"Kwa ufupi, yoyote itakaemfikia habari ya kuonekana kwa mwezi na akapata
wasaa wa kufunga au kumaliza kufunga au kuchinja basi hana budi atekeleze.
Ushahidi kamili na riwaya nyingi kutoka kwa Ma-Salaf
unaunga mkono kikamilifu mas-ala hayo. Kuweka vipimo vya masafa au miji ni kukhalifu malengo na shar' (sheria ya uislamu)."[12]
Imam Ash-Shawkani (rahimahullah) akaigusia hii riwaya kutoka kwa Kurayb na
akataja maoni mbali mbali ya wanavyuoni walivyozungumza. Kisha akaeleza
"Inakupasa kujua ya kwamba ushahidi unaokubalika ni
'Musifunge mpaka muuone mwezi na musimalize saumu zenu mpaka muuone...'
Hii haihusiani na sehemu maalum bali hayo ni maelezo
kwa waislamu wote kwa ujumla. Kwa hivyo huo ni
ushahidi wa wazi ya kuwa kuonekana kwa mwezi katika sehemu moja kunawahusu watu
wa sehemu yoyote nyingine. Sababu ni kwamba watu
(waislamu) katika sehemu fulani wakiuona, hiyo yamaanisha kuwa waislamu wote
wameuona; linalowahusu wao (waliouona) vile vile litawahusu wengine (katika
sehemu nyingine.) Licha ya hayo, mji wa Ash-Sham
haukuwa mbali mno kutoka Madina hata ipatikane matla' tafauti. Ibn 'Abbas alikataa kuwafuata waliouona. Hii
yamaanisha tabia yake imetokamana na ijtihadi yake na kwa hivyo hauwezekani huo
kuwa ni ushahidi (makhsusi)."[13]
Siddiq Hassan Khan (rahimaullah)[14] akasema:
"Mwezi kongo utakaposhuhudiwa na watu katika kitongoji chochote, basi
itawapasa watu wote wakubaliane kuhusu kuonekana kwa mwezi huo. Ushahidi
unatokamana na hadithi zinazoeleza kuhusu kuanza na
kumaliza kufunga kwa kuuona mwezi kongo. Hadithi hizi zawaeleza Umma mzima wa waislamu: Muislamu yoyote akiushuhudia mwezi popote,
ushuhuda wake utakuwa ni ushuhuda wa waislamu wote. Itakuwa ni
makosa kwenda kinyume na hivi kwa kuitumia hadithi ya Kurayb (sahih Muslim) kwa
sababu Ibn 'Abbas kwenye hadithi hiyo hakukatazwa na mtume (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) kufuata utazamaji wa sehemu nyingine za mji."[15]
Kuhusu mas-ala haya, akaeleza mwanachuoni wa karne hii, Muhammad Nasir Ud-Din
Al-Albaani, (Rahimahullah):
"Matla' zinahusiana wala hazina mipaka maalum ambayo watu waweza
kuyatafautisha ili wazitegemee... wanavyuoni wengi hawakuyapa uzito mas-ala
hayo ya tafauti za matla'. Ushahidi ukapatikana kutokamana na
hadithi iliyosahih, 'Fungeni kwa kuuona na fungueni kwa kuuona.'
Huu ndio ukweli uliothubutu, wala mtu asiupinge ukweli huu kwa
kuitumia hadithi ya Ibn 'Abbas, huwenda ikawa ni bora kusema yakwamba hadithi
ya Ibn 'Abbas inawahusu waliofunga kwa kuuona mwezi kwenye sehemu
Ufuatao ni mukhtasar wa
maelezo yaliopita:
a. Kuanza kwa mwezi wa ki-islamu hutegemea (kwa min-ajil ya kufunga,
Hija na matukio mengine ya ki-islamu). Kuuona mwezi kongo
kwa macho makavu.
b. Ushahidi wa utaalamu wa elimu ya nyota
haufai kutumiwa katika kuthibitisha, kuhakikisha na wala kumkanusha muislamu
muaminifu alieuona mwezi.
c. Pindi mwezi kongo uonekanapo popote
ulimwenguni itawapasa watu wengine wote kufunga, maadamu habari zitawafikia
ndani ya muda ambao watakuwa wepesi wa utekelezaji. Watu wasiowajibika
kutekeleza amri hiyo ni waislamu wanaoishi chini ya
mamlaka ya serikali inayokanusha (kwa masikitiko), kwa sababu mbalimbali,
kufuata kuonekana kwa mwezi kutoka nchi nyengine.
d. Mwanzo wa mwezi ni kuonekana kwa mwezi
kongo, bila ya kujali iwapo mwezi huo uliandama kabla, baada ama ndio
umejitokeza wakati huo. Kwa hayo tunamuomba Allah (s.w.t.) atuongoze na atuwezeshe kuifuata Sunnah wakati wowote na mwito wetu wa
mwisho uwe ni: AL-HAMDU LILLAHI RABBIL 'ALAMIN.
Nukta Ya Maelezo:
[1] Bukhari,Muslim na wengineo; imepokewa na Abu Hurayrah, 'Aisha, 'Adiyy Bin
Hatim, Hudhayfah, Ibn 'Abbas, Ibn 'Umar, Jabir Bin 'Abdillah na maswahaba
wengine.
[2] Abu Dawud, Ahmad na wengineo; imepewa hukmu ya
usahihi na al-Haakim, Adh-Dhahabi na Al-Albaani.
[3] Ahmad, an-Nasa'i na ad-Daaraqut'ni; imehukumiwa
usahihi wake na al-Albaani.
[4] Abu Dawud na wengineo; imehukumiwa kuwa sahih na
adh-Dhahabi, Ibn Hajar na al-Albaani.
[5] Bukhari, Muslim, Abu Dawud na an-Nasa'i.
[6] An-Nasa'i, Ahmad na wengineo, imesahihishwa na Ibn
Taymiyyah na wengineo.
[7] Abu Dawud, at-Tirmidhi na wengineo, imehukumiwa
kuwa sahih na al-Albaani na wengineo.
[8] Al-Fatawi 5:203.
[9] Muslim na wengineo.
[10] Abu Dawud, at-Tirmidhi na wengineo, imehukumiwa
kuwa sahih na al-Albaani na wengineo.
[11] Muslim.
[12] Al-Fatawi 5:111.
[13] Nayl ul-Awtar, 4:268.
[14] Akiwa ni miongoni mwa wanavyuoni wakubwa aliewhi
kuishi katika bara hindi.
[15] Ar-Rawdhat un-Nadiyyah, 1:224.
[16] Tamam ul-Minnah,