KUOSHA MAITI
HUKMU YAKE
Maulamaa wanasema kuwa hukmu ya kuosha maiti ni 'fardhi kifaya', na maana yake ni kuwa;
"ikiwa baadhi ya watu wataifanya kazi hiyo, basi waliobaki wale wanaolazimika watasameheka".
MAITI GANI WANAOWAJIBIKA KUOSHWA?
Ni wajibu kuosha maiti wote wa kiislam isipokuwa wale waliouliwa na makafiri katika vita vya Jihadi.
HUKMU YA KUOSHA SEHEMU YA MWILI WA MAITI
Maulamaa wamekhitalifiana juu ya hukmu ya kuosha sehemu za mwili wa maiti ikiwa haukupatikana mwili wote kamili.
Katika madhehebu ya Imam Shafi na Imam Ahmed bin Hanbal, wao wanaona kuwa sehemu hiyo ioshwe na kukafiniwa na kusaliwa.
Anasema Imam Shafi;
"Tumejulishwa kuwa ndege mmoja ulimwanguka mkono wa mtu mjini Maka wakati wa vita vya ngamia (Waqaat al jamal), wakaujuwa mkono wa nani kutokana na pete, wakauosha na kuusalia".
(Mkono huo ulikuwa wa Abdurahman bin Utaab bin Usayd(RA)).
Anasema Imam Ahmed;
"Abu Ayub (RA) aliwahi kuusalia mguu, na Omar bin Khatab (RA) aliwahi kuyasalia mafupa, na Ibni Hazam anasema kuwa; Ikipatikana sehemu yoyote ile ya maiti ya Muislam, basi inasaliwa na kukafiniwa isipokuwa kama sehemu hizo ni za maiti aliyekufa shahid katika vita vya Jihad. Na anayesali anatia nia sawa na nia ya kumsalia maiti aliyekamilika mwili wake.
Ama Maimam Abu Hanifa na Malik wao wanasema;
"Ukipatikana mwili zaidi ya nusu, hapo unakoshwa na kusaliwa, ama sivyo hapana haja ya kuoshwa wala kusaliwa".
ALIYEKUFA SHAHID HAOSHWI
Shahid aliyeuliwa vitani na makafiri, haoshwi hata kama alipokufa alikuwa na janaba, kama Mtume (SAW) alivyofanya juu ya Handhalah (RA) aliyeuliwa vitani akiwa na janaba, Mtume (SAW) alimzika bila kumuosha.
Anasema Sayed Sabeq, katika Fiqhi ssunah kuwa:
Shahidi anakafiniwa kwa ngou zake zile zile alozivaa ikiwa zitatosha kumkafinia, kama hazikumtosha, basi anakamilishiwa nguo nyengine, na zinapunguzwa zikizidi kupindukia, na anazikwa na damu yake bila kuoshwa.
Imepokelewa kuwa Mtume (SAW) amesema;
"Msiwakoshe, kwa sababu kila jeraha (au kila damu) litanukia harufu ya miski siku ya Kiama".
Ahmed
Anasema Imam Shafi;
"Huenda ikawa sababu ya kutooshwa maiti na kutosaliwa ni kwa ajili ya kukutana na Mola wao wakiwa na majeraha yao, kwani imepokelewa katika hadithi kuwa damu zao zitanukia harufu ya hal miski.
MASHAHIDI WANAOOSHWA NA KUKAFINIWA NA KUSALIWA
Ama wale waliouliwa nje ya uwanja wa vita, yote sawa ikiwa wameuliwa na kafiri au Muislam, hao kisheria pia wanaitwa mashahidi, isipokuwa wao wanaoshwa na kukafiniwa na kusaliwa.
Mtume (SAW) aliwaosha na kuwasalia watu wa aina hiyo waliouliwa wakati yeye Mtume (SAW) alipokuwa bado yu hai. Na Waislam waliwaosha Omar na Othman na Ali na wote hao waliuliwa, na kwa ajili hiyo walikufa mashahidi.
Kutoka kwa Abu Huraira alisema kuwa Mtume (SAW) aliuliza;
"Wepi mnaowahesabu kuwa ni mashahid?"
Masahaba (RA) wakasema;
"Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, aliyeuliwa katika vita vya Jihadi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu huyo ni shahid".
Akasema;
"(Ikiwa ni hao tu) Basi mashahid katika umma wangu watakuwa wachache".
Wakamuuliza;
"Wepi wengine ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?"
Akasema;
"Atakayeuliwa katika njia ya Mwenyezi Mungu huyo ni shahid, na atakayekufa akiwa katika njia ya Mwenyezi Mungu huyo ni shahid, na atakayekufa kwa (maradhi) ya tauni ni shahid, na atakayekufa kwa maradhi ya tumbo ni shahid na aliyezama (alyekufa kwa kuzama) ni shahid".
Muslim
Na kutoka kwa Said bin Zeid kuwa Mtume (SAW) amesema;
"Atakayeuliwa kwa kuilinda mali yake naye ni shahid, atakayeuliwa kwa kujihami nafsi yake naye ni shahid, na atakayeuliwa kwa kuilinda dini yake, naye ni shahid na atakayeuliwa akiwalinda ahli yake naye ni shahid".
Imam Ahmed na Attirmidhiy
KUMUOSHA MAITI
Si vizuri kuhudhuria watu wengi katika kuosha maiti isipokuwa wale wanaohitajika tu na walioruhusiwa na watu wa maiti, na muoshaji lazima awe mtu muaminifu ili awe anawaeleza watu yale ya kheri tu katika mambo atakayoona, na ayasitiri yale yenye shari.
Mtume (SAW) amesema;
"Waoshe maiti zenu wale wanaoaminika".
Ibni Majah
Maulamaa wamekhitalifiana juu ya maiti avuliwe nguo zake zote wakati wa kuoshwa au asivuliwe. Anasema Ibni Rushd al Qurtubiy katika 'Bidayatul mujitahid wa Nihayatul muqtasid';
"Imam Abu Hanifa anaona kuwa maiti avuliwe nguo zake na afunikwe tupu zake.
Ama Imam Shafi, yeye anaona kuwa maiti aoshwe akiwa amevalishwa sanda yake atakayobadilishwa baada ya kuoshwa.
Sababu ya kuhitalifiana kwao inatokana na kukoshwa kwa Mtume (SAW) akiwa na nguo zake. Wengine wakasema kuwa wamemuosha vile kwa sababu yule ni Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW). Wengine wakasema;'La, bali hivyo ndivyo inavyotakiwa". Wote wamekubaliana kuwa kilichoharamishwa kukitizama mtu anapokuwa hai, basi kwa maiti pia ni haramu kukitizama.
Anasema Sheikh Nasseriddin al Albani katika kitabu chake kitwacho; 'Ahkam al Janaiz wa Bidaiha';
"Katika kuosha maiti yazingatiwe yafuatayo;
Na dalili ya yote hayo inapatikana katika hadithi ya Mtume (SAW) ifuatayo;
Anasema Ummu Atiya (RA);
"Aliingia Mtume (SAW) wakati sisi tunamuosha binti yake (Zeinab) akasema;
"Muosheni mara tatu au tano (au saba), au zaidi kuliko hapo mkiona panahitajika kwa maji na majani ya mkunazi".
Anasema;
"Nikamuuliza; 'witran'?" (kwa tarakimu za witri?)
Akasema;
"Ndiyo, na mnapotia maji mara ya mwisho changanyeni na kafur na mkeshamaliza niiteni".
Tulipomaliza tukamuita, akatutupia saruni yake, kisha akasema;
"Mvalisheni kwanza (igusane na ngozi yake)".
Kisha tukamsuka mikia mitatu na kuitupa nyuma. Mtume (SAW) alituamiba (pia);
"Anzeni upande wa kulia".
Bukhari - Muslim - AbuDaud - Annasaiy - Attirmidhiy - Ibni Majah - Ibni l Jarudi - na Ahmed.
"Msimpake mafuta mazuri kwani anafufuliwa siku ya kiama akiwa anafanya talbiya (akiwa anasema 'Labbayka llahumma labbayka')".
"Nilipokuwa nikimuosha Mtume (SAW) nilikuwa nikimtizama sana nikidhani kuwa kutakuwa na hitilafu yoyote ile, lakini sikuona kitu, na alikuwa akipendeza (sana) pale alipokuwa yuhai na hata baada ya kufa kwake".
Ibni Majah - Al Hakim na wengineo na akasema hadithi ni sahihi kwa masharti yaliyowekwa na Bukhari na Muslim.
Anasema Sh.Al Albani (Mwenyezi Mungu amrehemu) kuwa;
"Na muoshaji ana ujira mkubwa sana kwa Mwenyezi Mungu, lakini kwa masharti mawili yafuatayo;
"Atakayemuosha Muislam na asizungumze juu yake, Mwenyezi Mungu anamghufiria mara arubaini…."
Al Hakim - Al Baihaqi na wengineo.
Na katika riwaya iliyotolewa na Attabarani;
"Anasamehewa madhambi makubwa arubaini (arbaina kabiyrah)".
Katika kuithibitisha hoja hii, Sheikh aliandika aya mbali mbali pamoja na hadithi ya Mtume (SAW) isemayo;
"Hakika ya amali (yoyote ile inakubaliwa) kwa nia zake, na kila mja anapata kutokana na nia yake…"
Bukhari na Muslim
NAMNA YA KUMUOSHA MAITI
Hapa nitanukuu moja kwa moja kutoka katika kitabu kidogo kiitwacho 'Huduma za kuosha Maiti', nilichopewa zawadi na Bwana Muhammed Humaid Al Khatry - mwandishi wa kitabu hicho, nilipokwenda kumtembelea nyumbani kwake.
Katika mlango wa 'Namna ya kumuosha maiti', Sheikh ameandika;
Ni vizuri huduma za Maiti zote zifanywe na jamaa zake au kwa ruhusa yao. Maiti huoshwa juu ya mnyanyuko kama kitanda au ubao au baraza ya saruji. Hulazwa chali. Na muoshaji huwa mmoja, wengine huwa watiliaji maji. Wote huitwa waoshaji. Ni uzuri wasiwe wengi. Na ni uzuri wale wasiohusika wasikaribie kama hawahitajiki. Wasijipeleke, wangoje wenyewe wawaombe kuosha na kuvika sanda. Ama kumsalia na kumchukua haihitaji ruhusa.
Muoshaji huvaa gloves. Hizi zinaweza kuwa za plastic au za kitambaa. Zinaweza kushonwa hapo hapo kutokana na sehemu ndogo ndogo za sanda.Hatua za kuosha ni hizi;
((Mtume (SAW) amesema;
"Waosheni 'witran', mara tatu au tano au saba au zaidi ya hapo mkiona inahitajika kwa majani ya mkunazi na mara ya mwisho kwa kafur".))
((Mtume (SAW) amesema;
"Anzeni kuliani pao na sehemu za kutia udhu".))
TAYAMUM PAKIKOSEKANA MAJI
Pakikosekana maji, maiti anafanyiwa tayamum kutokana na kauli ya Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala aliposema;
"Na kama hamkupata maji basi tayamamuni"
Na kutokana na hadithi ya Mtume (SAW) aliposema;
"Imejaaliwa kwa ajili yangu ardhi yote (kuwa) msikiti na tahiri", na pia anaweza kutayamamishwa maiti ikiwa mwili utaharibika kwa kuoshwa na maji.
YASIYOFAA KUFANYIWA MAITI
Katika mambo yasiyofaa kufanyiwa matiti ni;
"Hata wewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?".
Mtume (SAW) akawajibu;
"Hakika jicho linatoka machozi na moyo unahuzunika, lakini hatusemi ila yale yanayomridhi Mola wetu".
Na katika hadithi nyingine akasema;
"Mwenyezi Mungu haadhibu kwa sababu ya kutoka machozi wala kwa huzuni ya moyo, lakini huadhibu au hurehemu kwa huu (ulimi)".
MUHAMMAD FARAJ SALEM AL SAIY