Suali;
Aslam aleykum kuna swali
linanitaza ninaomba ufafanuzi.
Mimi ninaishi marekani ya
kaskazini. Ninapokwenda msikitini baada kumaliza kutia udhu kutokana na baridi
kali ya marekani inanibidi tujifute maji ya udhu.
Je kidini inakubalika kuufuta
udhu naomba jibu
Majibu;
Anasema Imam Annawawiy kuwa ipo khitilafu
baina ya maulamaa katika Masaala ya kupangusa maji baada ya kutia udhu. Wapo
wanaosema kuwa ni Makruh na wapo wanaosema kuwa Inajuzu na hapana ubaya wowote.,
lakini hapana anayesema kuwa kupangusa kunavunja udhu juu ya kuwa maulamaa wengi
wanaona kuwa hapana ubaya wowote katika kupangusa.
Wanaosema kuwa ni Makruh, dalili
Wanasema kuwa kwa vile Mtume (SAW)
hakujipangusa, hii ni dalili kuwa kuacha kujipangusa ni bora kuliko kujipangusa,
wakati huo huo ingekuwa haijuzu kujipangusa basi Mtume (SAW) lazima angewajulisha
juu ya
Na hii ndiyo hoja waliyonayo wengi miongoni
mwa maulamaa kuwa hapana ubaya kujipangusa maji baada ya kutawadha, hasa panapo
udhuru
Wallahu taala aalam
Wassalaam alaykum wa Rahmatullahi wa Barakatuh