Hii ndiyo itikadi sahihi ya Kiislamu

 

Imeandikwa na Shaykh Muhammad bin Uthaymiyn

Imetafsiriwa na Muhammad Faraj Salem

 

www.mawaidha.info                                      www.alhidaaya.com

Utangulizi 2

Itikadi yetu. 3

Sifa ya kusema. 6

Kuwepo Kwake Juu  

 Anayo Arshi 9

Sifa ya kushuka. 10

Sifa ya Irada) 11

Sifa ya Kupenda. 13

Wajihi Wake. 14

Mikono. 14 Yake

Macho. 16

Tanbih. 18

Malaika. 19

Vitabu. 22

Mitume. 25

Dini Yake. 28

Makhalifa waongofu. 29

Siku ya mwisho. 31

Shafa’a. 33

Hodhi na Swiraat 33

Pepo na Moto. 34

Masuali ya kaburini 35

Adhabu ya kaburini 35

Qadar 36

Kutaka kwa Mwenyezi Mungu. 37

Baadhi ya faida. 41

Matunda ya kuamini Malaika. 41

Matunda ya kuviamini vitabu. 41

Matunda ya kuamini Mitume. 42

Matunda ya kuiamini Qiyaamah. 42 na Qadar 42

Utangulizi

Shukrani zote ni zake Mola wa uliwengu wote, na mwisho mwema ni wa wamchao Mwenyezi Mungu, na hapana uadui isipokuwa kwa madhalimu.

Nashuhudia kuwa hapana anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Allah Peke yake Asiye na mshirika mwenye Ufalme na haki iliyo wazi. Na nashuhudia kuwa Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) ni mjumbe wake na Mtume wake na mwisho wa wajumbe wake na ni kiongozi wa wacha Mungu. Mola wetu mswalie na msalimie Mtume wako huyu pamoja na Masahaba wake na kila atakayemfuata kwa wema na uongofu mpaka Siku ya Qiyaamah.

 

Amma baad,

Hakika Mwenyezi Mungu amemtuma Mtume wake Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) awe dalili iliyo wazi  juu ya waja wake, na awabainishie yale aliyoteremshiwa katika Kitabu, na awe mfano mwema wa kuigwa na walimwengu wote, na ili watu wapate kuwa na muongozo mwema katika dini yao na dunia yao.

Ametumwa kutufundisha itikadi sahihi pamoja na hekima kwa ajili ya kutengenea hali ya umati wake, na pia kuwaweka juu ya njia safi na sahihi, ili watu wawe juu ya kitanga cheupe, mchana wake sawa na usiku wake, na asiende kinyume na njia hiyo isipokuwa mpotofu.

Wakaifuata njia hiyo Maswahaba wake (Radhiya Llaahu ‘anhum) na wale waliokuja baada yao na waliowafuatilia kwa wema. Wakaisimamisha shari’ah ya Mwenyezi Mungu na kuyakamata vizuri mafundisho hayo kwa magego yao kwa kuifuata itikadi hii iliyo sahihi, na ibada na mwenendo na tabia. Na sisi Alhamdulillah tunaendelea kuufuata mwenendo wao huo kwa kufuata dalili zilizomo ndani ya Qur-aan na zilizomo ndani ya mafundisho yake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam), na tunamuomba Mwenyezi Mungu Atuthibitishe juu ya njia hiyo sisi na ndugu zetu wote wa Kiislamu kwa kauli iliyo thabit katika maisha ya duniani na ya akhera na atumiminie rehma Zake kwani yeye ni Mwenye kutoa kwa wingi.

 

Kutokana na umuhimu wa maudhui haya, na kutokana na tofauti iliyokuja baadaye, baada ya kuingizwa matamanio ya watu ndani ya itikadi hii, nilipenda kuiandika iwe kama ndiyo itikadi yetu. Itikadi ya Ahlus Sunnah wal Jama’ah, nayo ni imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu na Malaika Wake na vitabu Vyake na Mitume Yake na Siku ya Qiyaamah na Qadar (qudra) kheri yake na shari yake.

Namuomba Mwenyezi Mungu Aijaalie kazi hii iwe halisi kwa ajili yake, Aridhike nayo na iwe funzo kwa waja Wake.

Rudi juu

 

Itikadi Yetu

Itikadi yetu ni kumuamini Mwenyezi Mungu na Malaika Wake na Mitume Yake na Vitabu Vyake na Siku ya Mwisho na kila kinachotokea au kutusibu (Qadar) kheri na shari, vyote vinatoka kwa Mwenyezi Mungu.

Kwa hivyo sisi tunaamini kuwa Yeye Subhaanahu wa Ta’ala ndiye Aliyeumba na ndiye Mfalme Mwenye kukiendesha kila kitu, na ni Yeye peke yake anayestahiki kuabudiwa, na kila kinachoabudiwa kisichokuwa Yeye ni batil.

 

Tunaamini pia kuwa Mwenyezi Mungu Anayo majina mazuri mazuri na sifa nzuri nzuri na njema, sifa za ukamilifu, na tunaamini kuwa Yeye ni mmoja Asiye na mshirika katika kuumba Kwake na katika kuabudiwa Kwake na katika majina Yake mazuri na katika sifa Zake njema.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÑóÈøõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖö æóãóÇ ÈóíúäóåõãóÇ ÝóÇÚúÈõÏúåõ æóÇÕúØóÈöÑú áöÚöÈóÇÏóÊöåö åóáú ÊóÚúáóãõ áóåõ ÓóãöíøðÇ

"Mola wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake. Basi muabudu Yeye tu, na udumu katika ibada yake. Je, mnamjua mwenye jina kama lake?"

Maryam – 65

 

 

Na tunaamini kuwa Yeye ndiye:

 

Çááøåõ áÇó ÅöáóÜåó ÅöáÇøó åõæó ÇáúÍóíøõ ÇáúÞóíøõæãõ áÇó ÊóÃúÎõÐõåõ ÓöäóÉñ æóáÇó äóæúãñ áøóåõ ãóÇ Ýöí ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóãóÇ Ýöí ÇáÃóÑúÖö ãóä ÐóÇ ÇáøóÐöí íóÔúÝóÚõ ÚöäúÏóåõ ÅöáÇøó ÈöÅöÐúäöåö íóÚúáóãõ ãóÇ Èóíúäó ÃóíúÏöíåöãú æóãóÇ ÎóáúÝóåõãú æóáÇó íõÍöíØõæäó ÈöÔóíúÁò ãøöäú Úöáúãöåö ÅöáÇøó ÈöãóÇ ÔóÇÁ æóÓöÚó ßõÑúÓöíøõåõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖó æóáÇó íóÄõæÏõåõ ÍöÝúÙõåõãóÇ æóåõæó ÇáúÚóáöíøõ ÇáúÚóÙöíãõ

"Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye, Aliye hai, Msimamiaji wa mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni Vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini Yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi Wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; na wala haemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye Aliye juu, na ndiye Mkuu."

Al-Baqarah – 255

 

 

Na tunaamini kuwa:

 

åõæó Çááøóåõ ÇáúÎóÇáöÞõ ÇáúÈóÇÑöÆõ ÇáúãõÕóæøöÑõ áóåõ ÇáúÃóÓúãóÇÁ ÇáúÍõÓúäóì íõÓóÈøöÍõ áóåõ ãóÇ Ýöí ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃÑúÖö æóåõæó ÇáúÚóÒöíÒõ ÇáúÍóßöíãõ

"Yeye ndiye Mwenyezi Mungu, Muumbaji, Mtengenezaji, Mtia sura, Mwenye majina mazuri kabisa. Kila kilioko katika mbingu na ardhi kinamtakasa, naye ni Mwenye kushinda, Mwenye hikima."

Al-Hashr - 24

 

 

Na tunaamini kuwa:

 

áöáøóåö ãõáúßõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáúÃóÑúÖö íóÎúáõÞõ ãóÇ íóÔóÇÁ íóåóÈõ áöãóäú íóÔóÇÁ ÅöäóÇËðÇ æóíóåóÈõ áöãóä íóÔóÇÁ ÇáÐøõßõæÑó. Ãóæú íõÒóæøöÌõåõãú ÐõßúÑóÇäðÇ æóÅöäóÇËðÇ æóíóÌúÚóáõ ãóä íóÔóÇÁ ÚóÞöíãðÇ Åöäøóåõ Úóáöíãñ ÞóÏöíÑñ

"Ufalme wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu; Anaumba Apendavyo, Anamtunukia amtakaye watoto wa kike, na Anamtunukia amtakaye watoto wa kiume.

Au huwachanganya wanaume na wanawake, na akamfanya amtakaye tasa. Hakika Yeye ni Mjuzi Mwenye uweza."

Ash-Shuuraa – 49-50

 

 

Na tunaamini kuwa:

 

ÝóÇØöÑõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃÑúÖö ÌóÚóáó áóßõã ãøöäú ÃóäÝõÓößõãú ÃóÒúæóÇÌðÇ æóãöäó ÇáúÃóäúÚóÇãö ÃóÒúæóÇÌðÇ íóÐúÑóÄõßõãú Ýöíåö áóíúÓó ßóãöËúáöåö ÔóíúÁñ æóåõæó ÇáÓøóãöíÚõ ÇáÈóÕöíÑõ. áóåõ ãóÞóÇáöíÏõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃÑúÖö íóÈúÓõØõ ÇáÑøöÒúÞó áöãóä íóÔóÇÁ æóíóÞúÏöÑõ Åöäøóåõ Èößõáøö ÔóíúÁò Úóáöíãñ

"Yeye ndiye Muumba mbingu na ardhi, Amekujaalieni mke na mume katika nafsi zenu, na katika wanyama nao (Akawaumba) dume na jike, Anakuzidishieni namna hii. Hapana kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona.

Yeye ndiye Mwenye funguo za mbingu na ardhi. Humkunjulia riziki Amtakaye, na humpimia Amtakaye. Hakika Yeye ni Mjuzi wa kila kitu."

Ash-Shuuraa – 11-12

 

 

Na tunaamini kuwa:

 

æóãóÇ ãöä ÏóÂÈøóÉò Ýöí ÇáÃóÑúÖö ÅöáÇøó Úóáóì Çááøåö ÑöÒúÞõåóÇ æóíóÚúáóãõ ãõÓúÊóÞóÑøóåóÇ æóãõÓúÊóæúÏóÚóåóÇ ßõáøñ Ýöí ßöÊóÇÈò ãøõÈöíäò

"NA HAKUNA mnyama yoyote katika ardhi ila riziki yake iko kwa Mwenyezi Mungu. Naye Anajua makao yake na mapitio yake. Yote yamo katika Kitabu chenye kubainisha."

Huud - 6

 

 

Na tunaamini kuwa:

 

æóÚöäÏóåõ ãóÝóÇÊöÍõ ÇáúÛóíúÈö áÇó íóÚúáóãõåóÇ ÅöáÇøó åõæó æóíóÚúáóãõ ãóÇ Ýöí ÇáúÈóÑøö æóÇáúÈóÍúÑö æóãóÇ ÊóÓúÞõØõ ãöä æóÑóÞóÉò ÅöáÇøó íóÚúáóãõåóÇ æóáÇó ÍóÈøóÉò Ýöí ÙõáõãóÇÊö ÇáÃóÑúÖö æóáÇó ÑóØúÈò æóáÇó íóÇÈöÓò ÅöáÇøó Ýöí ßöÊóÇÈò ãøõÈöíäò

"Na ziko kwake funguo za ghaibu; hakuna azijuaye ila Yeye tu. Na Yeye Anajua kilioko nchi kavu na baharini. Na halidondoki jani ila Analijua. Wala punje katika giza la ardhi, wala kinyevu, wala kikavu ila kimo katika Kitabu kinachobainisha."

Al-An’aam – 59

 

 

Na tunaamini kuwa:

 

Åöäøó Çááøóåó ÚöäÏóåõ Úöáúãõ ÇáÓøóÇÚóÉö æóíõäóÒøöáõ ÇáúÛóíúËó æóíóÚúáóãõ ãóÇ Ýöí ÇáÃóÑúÍóÇãö æóãóÇ ÊóÏúÑöí äóÝúÓñ ãøóÇÐóÇ ÊóßúÓöÈõ ÛóÏðÇ æóãóÇ ÊóÏúÑöí äóÝúÓñ ÈöÃóíøö ÃóÑúÖò ÊóãõæÊõ Åöäøó Çááøóåó Úóáöíãñ ÎóÈöíÑñ

"Hakika kuijua Saa (ya Qiyaamah) kuko kwa Mwenyezi Mungu. Na Yeye ndiye Anayeiteremsha mvua. Na Anavijua viliomo ndani ya matumbo ya uzazi. Na haijui nafsi yoyote itachuma nini kesho. Wala nafsi yoyote haijui itafia nchi gani. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujua, Mwenye khabari".

Luqmaan – 34

 

Rudi juu

Sifa Ya Kusema

Tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Anasema wakati wowote Anapotaka na kwa njia yoyote Anayotaka.

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóßóáøóãó Çááøåõ ãõæÓóì ÊóßúáöíãðÇ

"Na Mwenyezi Mungu Akamsemeza Muusa."

An-Nisaa – 164

 

 

Na Akasema:

 

æóáóãøóÇ ÌóÇÁ ãõæÓóì áöãöíÞóÇÊöäóÇ æóßóáøóãóåõ ÑóÈøõåõ

"Na alipokuja Muusa kwenye miadi yetu, na Mola wake Akamsemeza."

Al-A’araf – 143

 

 

Na Akasema:

æóäóÇÏóíúäóÇåõ ãöä ÌóÇäöÈö ÇáØøõæÑö ÇáÃíúãóäö æóÞóÑøóÈúäóÇåõ äóÌöíøðÇ

"Na Tulimwita upande wa kulia wa mlima na tukamsogeza kunong'ona naye."

Maryam – 52

 

 

Na tunaamini kuwa:

 

Þõá áøóæú ßóÇäó ÇáúÈóÍúÑõ ãöÏóÇÏðÇ áøößóáöãóÇÊö ÑóÈøöí áóäóÝöÏó ÇáúÈóÍúÑõ ÞóÈúáó Ãóä ÊóäÝóÏó ßóáöãóÇÊõ ÑóÈøöí æóáóæú ÌöÆúäóÇ ÈöãöËúáöåö ãóÏóÏðÇ

"Lau kama bahari ndio wino kwa maneno ya Mola wangu, basi bahari ingelimalizika kabla ya kumalizika maneno ya Mola wangu, hata tungeliileta mfano wa hiyo kuongezea."

Al-Kahf – 109

 

 

Na tunaamini kuwa:

 

æóáóæú ÃóäøóãóÇ Ýöí ÇáÃÑúÖö ãöä ÔóÌóÑóÉò ÃóÞúáóÇãñ æóÇáúÈóÍúÑõ íóãõÏøõåõ ãöä ÈóÚúÏöåö ÓóÈúÚóÉõ ÃóÈúÍõÑò ãøóÇ äóÝöÏóÊú ßóáöãóÇÊõ Çááøóåö Åöäøó Çááøóåó ÚóÒöíÒñ Íóßöíãñ

"Na lau kuwa miti yote iliyomo duniani ikawa ni kalamu, na bahari (ikawa wino), na ikaongezewa juu yake bahari nyengine saba, maneno ya Mwenyezi Mungu yasingelikwisha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima."

Luqmaan – 27

 

 

Na tunaamini kuwa maneno Yake ni ya ukamilifu uliokamilika na ya ukweli uliokamilika na yenye uadilifu uliokamilika.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóÊóãøóÊú ßóáöãóÊõ ÑóÈøößó ÕöÏúÞðÇ æóÚóÏúáÇð áÇøó ãõÈóÏøöáö áößóáöãóÇÊöåö æóåõæó ÇáÓøóãöíÚõ ÇáúÚóáöíãõ

"Yametimia maneno ya Mola wako kwa kweli na uadilifu. Hapana awezaye kuyabadilisha maneno Yake. Na Yeye ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua."

Al-An’aam - 115

 

Na Akasema:

æóãóäú ÃóÕúÏóÞõ ãöäó Çááøåö ÍóÏöíËðÇ

"Na ni nani msema kweli kuliko Mwenyezi Mungu?"

An-Nisaa – 87

 

 

Na tunaamini kuwa Qur-aan ni maneno ya Mwenyezi Mungu, aliyeyatamka kwa uhakika kabisa kwa kumfundisha Jibriyl aliyeiteremsha ndani ya kifua cha Mtume wa Mwenyezi Mungu Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam).

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

Þõáú äóÒøóáóåõ ÑõæÍõ ÇáúÞõÏõÓö ãöä ÑøóÈøößó ÈöÇáúÍóÞøö

"Sema: Ameiteremsha hii (Qur-aan) Roho takatifu kutokana na Mola wako kwa haki."

An-Nahl – 102

 

 

Na Akasema:

æóÅöäøóåõ áóÊóäÒöíáõ ÑóÈøö ÇáúÚóÇáóãöíäó. äóÒóáó Èöåö ÇáÑøõæÍõ ÇáÃãöíäõ. Úóáóì ÞóáúÈößó áöÊóßõæäó ãöäó ÇáúãõäÐöÑöíäó. ÈöáöÓóÇäò ÚóÑóÈöíøò ãøõÈöíäò.

"Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola wa walimwengu wote.

Ameuteremsha Roho muaminifu, Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji. Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi."

Ash-Shu’araa – 192 – 195

Rudi juu

 

Sifa Ya Kuwepo Kwake Juu ‘Al-Uluw

Tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu yupo juu kabisa mbali na viumbe vyake kwa dhati Yake na kwa sifa Zake, na hii inatokana na kauli Yake Subhaanahu wa Ta’ala Aliposema:

 

æóåõæó ÇáúÚóáöíøõ ÇáúÚóÙöíãõ

"Na Yeye ndiye Aliye juu, na ndiye Mkuu."

Al-Baqarah – 255

 

Na Akasema:

 

ÊóÚúÑõÌõ ÇáúãóáóÇÆößóÉõ æóÇáÑøõæÍõ Åöáóíúåö Ýöí íóæúãò ßóÇäó ãöÞúÏóÇÑõåõ ÎóãúÓöíäó ÃóáúÝó ÓóäóÉò

"Malaika na roho hupanda kwake katika siku ambayo muda wake ni miaka elfu hamsini."

Al-Ma’aarij – 4

 

Na Akasema:

 

ÃóÃóãöäÊõã ãøóä Ýöí ÇáÓøóãóÇÁ Ãóä íóÎúÓöÝó Èößõãõ ÇáÃóÑúÖó ÝóÅöÐóÇ åöíó ÊóãõæÑõ

"Je! Mnadhani muko salama kwa (Mwenyezi Mungu) Ambaye Yuko mbinguni ya kuwa Yeye hatokudidimizeni ardhini tahamaki hiyo inataharaki?"

Al-Mulk - 16

 

Na Akasema:

 

æóåõæó ÇáúÞóÇåöÑõ ÝóæúÞó ÚöÈóÇÏöåö æóåõæó ÇáúÍóßöíãõ ÇáúÎóÈöíÑõ

"Naye Ndiye Mwenye nguvu juu ya waja Wake."

Al-An’am -18

 

Na imekuja katika Sunnah (Mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam):

 

"Mrehemu aliye ardhini Atakurehemu aliye mbinguni."

Abu Ya’ala na Atw-Twabaraaniy na Al-Haakim

 

Na kuwepo mbinguni hakuna maana kuwa yupo katika mojawapo ya sayari zilizopo juu kama baadhi ya watu wanavyoweza kudhania, bali dunia yetu ukiilinganisha na mbingu ni mfano wa doa dogo sana, bali hata haionekani. Kwani huko juu kuna nyota na sayari zilizoenea hata kama mtu atasafiri kwa kasi ya sauti? (speed of light) basi atachukuwa mamilioni ya miaka na hatoweza kufika mwisho wake, na hata kama ataufikia mwisho wake, basi atakuta kuwa bado ipo anga isiyo na mwisho. Kwa hivyo ni Mwenyezi Mungu Peke Yake ndiye Mwenye kuelewa mfano ya kuwa juu Kwake Subhaanahu wa Ta’ala.

 

Rudi juu

Mwenyezi Mungu Anayo ‘Arshi

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

Åöäøó ÑóÈøóßõãõ Çááøåõ ÇáøóÐöí ÎóáóÞó ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖó Ýöí ÓöÊøóÉö ÃóíøóÇãò Ëõãøó ÇÓúÊóæóì Úóáóì ÇáúÚóÑúÔö

"Hakika Mola wenu ni Mwenyezi Mungu, Ambaye Ameziumba mbingu na ardhi kwa siku sita, kisha Akawa juu ya ‘Arshi Yake."

Yuunus – 3

Na kuwa juu ya ‘Arshi Yake ni kuwa kunakonasibiana na utukufu wake Subhaanahu wa Ta’ala, hapana anayejua mfano wake isipokuwa Yeye.

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Akiwa juu ya ‘Arshi Yake, Yupo pamoja na viumbe Vyake kwa elimu Yake.  Anasikia kauli zao na kuona vitendo vyao, huku Akiyaendesha mambo yao. Anamruzuku fakiri na Anampa ufalme Amtakaye na Anamuondolea ufalme amtakaye, Anamnyanyua amtakaye na Anamuangusha amtakaye, na tunaamini kwamba kheri yote imo mikononi Mwake Subhaanahu wa Ta’ala, na kwamba Yeye ni muweza wa kila jambo.

Na Yeyote mwenye uwezo huo, basi bila shaka yupo pamoja na viumbe vyake kikweli huku akiwa juu ya Arshi yake kikweli, na ni Yeye Peke yake ndiye mwenye kuujuwa uhakika wake.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áóíúÓó ßóãöËúáöåö ÔóíúÁñ æóåõæó ÇáÓøóãöíÚõ ÇáÈóÕöíÑõ

"Hapana kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona."

Ash-Shuuraa – 11

 

Na Anasema:

 

æóÇáúãóáóßõ Úóáóì ÃóÑúÌóÇÆöåóÇ æóíóÍúãöáõ ÚóÑúÔó ÑóÈøößó ÝóæúÞóåõãú íóæúãóÆöÐò ËóãóÇäöíóÉñ

"Na Malaika watakuwa kandoni mwake (hizo mbingu) na Malaika wa namna nane watachukua Kiti cha enzi cha Mola wako (‘Arshi) juu yao."

Al-Haaqqah – 17

 

 

Sisi hatusema kama wanavyosema wengine kuwa eti Mwenyezi Mungu yupo ardhini pamoja na viumbe Vyake, kwani tunaona kuwa kusema hivyo ni kukufuru au ni upotofu, kwa sababu kumpa Mwenyezi Mungu wasfu usiolingana naye ni kupunguza katika sifa Zake.

 

Rudi juu

Sifa Ya Kushuka

Tunaamini pia yale aliyotujulisha Mtume wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) kuwa Mwenyezi Mungu Anashuka katika mbingu za dunia kila usiku katika thuluthi ya mwisho na kusema: "Nani mwenye kuniomba nimkubalie, nani mwenye kuniomba nimpe, nani mwenye kuniomba maghfira nimghufirie."

Alipoulizwa Imaam Ash-Shaafi’iy:

'Vipi Mwenyezi Mungu Anashuka?'

Akajibu:

'Kwani vipi Alipanda?'

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Atakuja Siku ya Qiyaamah kuwahukumu viumbe vyake.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ßóáøóÇ ÅöÐóÇ ÏõßøóÊö ÇáÃóÑúÖõ ÏóßøðÇ ÏóßøðÇ. æóÌóÇÁ ÑóÈøõßó æóÇáúãóáóßõ ÕóÝøðÇ ÕóÝøðÇ

"Sivyo hivyo! Itakapovunjwa ardhi vipande vipande. Na Akaja Mola wako na Malaika safu safu. Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?".

Al-Fajr – 21 – 22

 

Rudi juu

Sifa Ya Irada (Atakavyo Mwenyezi Mungu)

Tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Anatenda Atakavyo.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÝóÚøóÇáñ áøöãóÇ íõÑöíÏõ

"Atendaye Ayatakayo."

Al-Buruuj – 16

 

 

Na tunaamini kuwa zipo Irada namna mbili. 

Ya kwanza Anatujulisha katika kauli Yake:

 

æóáóæú ÔóÇÁ Çááøåõ ãóÇ ÇÞúÊóÊóáõæÇú æóáóÜßöäøó Çááøåó íóÝúÚóáõ ãóÇ íõÑöíÏõ

"Na lau kuwa Mwenyezi Mungu Alipenda wasingelipigana (Lau shaa'a Alaahu). Lakini Mwenyezi Mungu Hutenda Atakavyo."

Al-Baqarah – 253

 

Na hapa maana yake ni ‘kutaka’, kama ilivyo katika kauli Yake:

 

æóáÇó íóäÝóÚõßõãú äõÕúÍöí Åöäú ÃóÑóÏÊøõ Ãóäú ÃóäÕóÍó áóßõãú Åöä ßóÇäó Çááøåõ íõÑöíÏõ Ãóä íõÛúæöíóßõãú åõæó ÑóÈøõßõãú æóÅöáóíúåö ÊõÑúÌóÚõæäó

"Wala nasaha yangu haikufaini kitu nikitaka kukunasihini, ikiwa Mwenyezi Mungu Anataka (Law Yuriydu Allaah) kukuachieni mpotee."

Huud – 34

 

 

Na uwezo mwingine ni wa kishari’ah, na Hamtakii isipokuwa Anayempenda, kama ilivyo katika kauli Yake Subhaanahu wa Ta’ala:

 

æóÇááøåõ íõÑöíÏõ Ãóä íóÊõæÈó Úóáóíúßõãú æóíõÑöíÏõ ÇáøóÐöíäó íóÊøóÈöÚõæäó ÇáÔøóåóæóÇÊö Ãóä ÊóãöíáõæÇú ãóíúáÇð ÚóÙöíãðÇ

"Na Mwenyezi Mungu Anataka (Yuriydu Allaah) kukurejezeni kwenye utiifu wake, na wanaotaka kufuata matamanio wanataka mkengeuke makengeuko makubwa."

(Na maana yake hapa ni kuwa 'Hivi Ndivyo Anavyotaka Mwenyezi Mungu' lakini kakupeni uhuru wa kuchagua wenyewe mnakotaka kwenda.)

An-Nisaa – 27

 

 

Na tunaamini kuwa Atakacho Mwenyezi Mungu katika mambo ya kilimwengu na ya kishari’ah yote ni katika hekima Yake, na hafanyi kitu bila ya kuwa na hekima kubwa ndani yake, na sisi huenda tukaijua hekima hiyo au tusiijuwe kutokana na upungufu wa akili zetu.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÃóáóíúÓó Çááøóåõ ÈöÃóÍúßóãö ÇáúÍóÇßöãöíäó

"Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?"

Atw-Twiyn - 8

 

Na Akasema:

 

æóãóäú ÃóÍúÓóäõ ãöäó Çááøåö ÍõßúãðÇ áøöÞóæúãò íõæÞöäõæäó

"Na nani aliye mwema zaidi katika kuhukumu kuliko Mwenyezi Mungu kwa watu wenye yakini?"

Al-Maaidah - 50

 

Rudi juu

Sifa Ya Kupenda

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta’ala Anawapenda wacha Mungu wake wanaompenda.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

Þõáú Åöä ßõäÊõãú ÊõÍöÈøõæäó Çááøåó ÝóÇÊøóÈöÚõæäöí íõÍúÈöÈúßõãõ Çááøåõ æóíóÛúÝöÑú áóßõãú ÐõäõæÈóßõãú

"Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu Atakupendeni na Atakufutieni madhambi yenu."

Al-‘Imraan – 31

 

 

Na Akasema:

 

ÝóÓóæúÝó íóÃúÊöí Çááøåõ ÈöÞóæúãò íõÍöÈøõåõãú æóíõÍöÈøõæäóåõ

"Basi Mwenyezi Mungu atakuja leta watu anao wapenda nao wanampenda."

Al-Maaidah – 54

 

 

Na Akasema:

 

æóÇááøåõ íõÍöÈøõ ÇáÕøóÇÈöÑöíäó

"Hakika Mwenyezi Mungu Anawapenda wanaosubiri."

Al-‘Imraan – 146

 

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Huridhika zinapofuatwa shari’ah Zake na huchukizwa zisipofuatwa.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

Åöä ÊóßúÝõÑõæÇ ÝóÅöäøó Çááøóåó Ûóäöíøñ Úóäßõãú æóáÇ íóÑúÖóì áöÚöÈóÇÏöåö ÇáúßõÝúÑ

"Mkikufuru basi Mwenyezi Mungu si mwenye haja nanyi, lakini hafurahii kufuru kwa waja wake."

Az-Zumar – 7

 

 

Na Akasema:

 

æóáóÜßöä ßóÑöåó Çááøåõ ÇäÈöÚóÇËóåõãú ÝóËóÈøóØóåõãú æóÞöíáó ÇÞúÚõÏõæÇú ãóÚó ÇáúÞóÇÚöÏöíäó

"Lakini Mwenyezi Mungu Kachukia kutoka kwao, na kwa hivyo Akawazuia na ikasemwa: Kaeni pamoja na wanao kaa!"

 

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Huridhika na wale wanaoamini na kufanya mema.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÑøóÖöíó Çááøóåõ Úóäúåõãú æóÑóÖõæÇ Úóäúåõ Ðóáößó áöãóäú ÎóÔöíó ÑóÈøóåõ

"Mwenyezi Mungu Yu radhi nao, na wao waradhi naye. Hayo ni kwa anayemwogopa Mola wake."

Al-Bayyinah-6

 

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Anamkasirikia kila mwenye kustahiki kukasirikiwa katika makafiri na wasiokuwa makafiri.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÇáÙøóÇäøöíäó ÈöÇááøóåö Ùóäøó ÇáÓøóæúÁö Úóáóíúåöãú ÏóÇÆöÑóÉõ ÇáÓøóæúÁö æóÛóÖöÈó Çááøóåõ Úóáóíúåöãú

"Wanaomdhania Mwenyezi Mungu dhana mbaya. Utawafikia mgeuko mbaya, na Mwenyezi Mungu Awakasirikie."

Al-Fat-h – 6

 

 

Na Akasema:

 

æóáóÜßöä ãøóä ÔóÑóÍó ÈöÇáúßõÝúÑö ÕóÏúÑðÇ ÝóÚóáóíúåöãú ÛóÖóÈñ ãøöäó Çááøåö æóáóåõãú ÚóÐóÇÈñ ÚóÙöíãñ

"Lakini aliyekifungulia kifua chake kukataa - basi hao ghadhabu ya Mwenyezi Mungu ipo juu yao, na wao watapata adhabu kubwa."

An-Nahl – 106

Rudi juu

 

Wajihi Wa Mwenyezi Mungu

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Anao wajihi wenye utukufu na ukarimu.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóíóÈúÞóì æóÌúåõ ÑóÈøößó Ðõæ ÇáúÌóáÃáö æóÇáÇßúÑóÇãö

"Unabaki Wajihi wa Mola wako wenye utukufu na ukarimu."

Ar-Rahmaan – 27

 

Rudi juu

Mikono

Tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Anayo mikono miwili mitukufu.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

Èóáú íóÏóÇåõ ãóÈúÓõæØóÊóÇäö íõäÝöÞõ ßóíúÝó íóÔóÇÁ

"Bali mikono yake (miwili - yadaahu) iwazi. Hutoa Apendavyo."

Al-Maaidah – 64

 

Na Akasema:

 

æóãóÇ ÞóÏóÑõæÇ Çááøóåó ÍóÞøó ÞóÏúÑöåö æóÇáÃÑúÖõ ÌóãöíÚðÇ ÞóÈúÖóÊõåõ íóæúãó ÇáúÞöíóÇãóÉö æóÇáÓøóãÇæóÇÊõ ãóØúæöíøóÇÊñ Èöíóãöíäöåö ÓõÈúÍóÇäóåõ æóÊóÚóÇáóì ÚóãøóÇ íõÔúÑößõæäó

"Na wala hawakumhishimu Mwenyezi Mungu kama Anavyostahiki kadiri Yake. Na Siku ya Qiyaamah ardhi yote itakuwa mkononi Mwake, na mbingu zitakunjwa katika mkono Wake wa kuume. Subhaanahu wa Ta’ala Ametakasika na Ametukuka na hayo wanayomshirikisha nayo."

Az-Zumar – 67

 

 

(Siku ya RidhwAan Waislamu walipofungamana na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) chini ya mti kwa kumpa måkono wote kwa pamoja, mmoja baada ya mwengine, na Mwenyezi Mungu akateremsha kauli Yake:

 

Åöäøó ÇáøóÐöíäó íõÈóÇíöÚõæäóßó ÅöäøóãóÇ íõÈóÇíöÚõæäó Çááøóåó íóÏõ Çááøóåö ÝóæúÞó ÃóíúÏöíåöãú

"Bila Shaka wale wanaofungamana nawe, kwa hakika wanafungamana na Mwenyezi Mungu. Mkono wa Mwenyezi Mungu uko juu ya mikono yao."

Al-Fat-h – 10

 

 

Ieleweke kuwa Mwenyezi Mungu Anaposema Anayo mikono au macho, haina maana kuwa mikono Yake ni sawa na mikono yetu, au macho Yake ni sawa na macho yetu - AstaghfiruLlaah. Meza inayo miguu na viti vina miguu, lakini miguu ya viti na ya meza ni tofauti na miguu ya mwanaadamu aloitengeneza meza ile, kwani sifa ya mtengenezaji lazima iwe tofauti na sifa ya kilichotengenezwa, ama sivyo mtengenezaji na kilichotengenezwa watakuwa kitu kimoja. Na Mwenyezi Mungu Ndiye mwenye kupigiwa mifano bora, sifa Zake Subhaanahu wa Ta’ala haziwezi kufananishwa na sifa zetu. Lakini wakati huo huo lazima tukikubali kila Alichojinasibisha nacho Subhaanahu wa Ta’ala.)

Rudi juu

Macho

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Anayo macho mawili kikweli, na hii inatokana na kauli Yake Subhaanahu wa Ta’ala Aliposema kumwambia Nuuh (‘Alayhis-Salaam):

 

æóÇÕúäóÚö ÇáúÝõáúßó ÈöÃóÚúíõäöäóÇ æóæóÍúíöäóÇ

"Na unda jahazi mbele ya macho yetu na kwa mujibu wa ufunuo wetu."

Huud – 37

 

Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) amesema:

"Pazia yake ni nuru, na lau kama ataiondoa basi nuru ya wajihi wake ingeunguza kila kilichokifikia."

Na alipokuwa akihadithia juu ya Ad-Dajjaal alisema:

"Dajjaal ana chongo na Mola wenu hana chongo."

 

 

Na tunaamini kuwa macho yetu hayamfikii kumuona Mwenyezi Mungu.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áÇøó ÊõÏúÑößõåõ ÇáÃóÈúÕóÇÑõ æóåõæó íõÏúÑößõ ÇáÃóÈúÕóÇÑó æóåõæó ÇááøóØöíÝõ ÇáúÎóÈöíÑõ

"Macho hayamfikilii, bali Yeye anayafikilia macho. Naye ni Mjuzi, Mwenye khabari."

Al-An’aam – 103

 

 

Na tunaamini kuwa Waislamu watamuona Mola wao Siku ya Qiyaamah.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æõÌõæåñ íóæúãóÆöÐò äøóÇÖöÑóÉñ. Åöáóì ÑóÈøöåóÇ äóÇÙöÑóÉñ

"Zipo nyuso siku hiyo zitang'ara.  Zinamwangallia Mola wao."

Al-Qiyaamah – 22-23

 

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta’ala hana mfano wake katika ukamilifu wa sifa Zake.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áóíúÓó ßóãöËúáöåö ÔóíúÁñ æóåõæó ÇáÓøóãöíÚõ ÇáÈóÕöíÑõ

"Hapana kitu kama mfano Wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona."

Ash-Shuuraa – 11

 

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Hashikwi na usingizi wala halali.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áÇó ÊóÃúÎõÐõåõ ÓöäóÉñ æóáÇó äóæúãñ

"Hashikwi na usingizi wala kulala."

Al-Baqarah – 255

 

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Hamdhulumu mtu, na hii inatokana na ukamilifu wa uadilifu Wake Subhaanahu wa Ta’ala, na kwamba hapana Asichokijua katika matendo ya waja Wake, na kwamba Hashindiwi na chochote, kwani Anapotaka chochote kiwe hukiambia tu; 'Kuwa' na kikawa.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÅöäøóãóÇ ÃóãúÑõåõ ÅöÐóÇ ÃóÑóÇÏó ÔóíúÆðÇ Ãóäú íóÞõæáó áóåõ ßõäú Ýóíóßõæäõ

"Hakika amri Yake Anapotaka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa."

Yaasiyn – 82

 

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Haguswi na machofu wala tabu ya aina yoyote ile.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóáóÞóÏú ÎóáóÞúäóÇ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖó æóãóÇ ÈóíúäóåõãóÇ Ýöí ÓöÊøóÉö ÃóíøóÇãò æóãóÇ ãóÓøóäóÇ ãöä áøõÛõæÈò

"Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu."

Qaaf – 38

 

 

Na tunakiamini kila Alichojithibitishia nafsi Yake, Akasema kuwa Anacho, basi sisi tunaamini kuwa Anacho kwa uhakika, na tunaamini pia kila alichotujulisha Mtume wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) juu ya Mola wake, katika Majina Yake mazuri mazuri na Sifa Zake njema.

 

Lakini tunakataa mambo mawili, nayo ni:

 

1.  Kufananisha (kushabihisha). Nako ni kutamka kwa ulimi au kwa moyo kuwa wasfu wa Mwenyezi Mungu unafanana na wasfu wa viumbe Vyake.

2.  Na pia tunakataa kukisia. Nako ni kujisemeza moyoni au kutamka kwa ulimi kuzikisia sifa za Mwenyezi Mungu kuwa labda ni hivi au vile.

 

Na tunakanusha kila Mwenyezi Mungu Alichojikanushia nafsi Yake, au kile alichokikanusha Mtume wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam), na tunakinyamazia kila Alichokinyamazia, na tunaamini kuwa hii ndiyo njia sahihi, kwani kila Alichojikanushia nafsi Yake ni habari kutoka Kwake, na Yeye Subhaanahu wa Ta’ala ndiye mwenye kuijua nafsi Yake na ndiye Msema kweli kupita wote, Mwenye mazungumzo bora kupita wote, waja Wake hawana uwezo wa kujua chochote juu Yake bila Yeye kuwajulisha.

Rudi juu

 

 

Tanbihi:

Kila tulichokitaja katika sifa za Mwenyezi Mungu, iwe kwa urefu au kwa ujumla, katika kuthibitisha au katika kukanusha, yote tumeyanukuu kutoka katika kitabu cha Mwenyezi Mungu (Qur-aan) au mafundisho ya Mtume Wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) (Sunnah) iliyo sahihi nayo pia ni itikadi waliyokuwa nayo Maimamu wetu wema waliotangulia.

 

Tunaona kuwa inawajibika kuzifasiri nassw (dalili) zilizomo ndani ya Qur-aan kwa uhakika wake kama Anavyozistahiki Mwenyezi Mungu, na tunajitenga mbali na njia ya wageuzaji wa maana wale waliozigeuza maana na kuzifasiri kwa njia Asiyoitaka Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta’ala, na tunajitenga mbali na njia ya wabadilishaji waliobadilisha, mbali na maana iliyokusudiwa, na pia tunajitenga mbali na wazidishaji waliozidisha na kuzifanya sifa zake kuwa ni za kumfananisha.

 

Tuna hakika kuwa yale yaliyomo ndani ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu na ndani ya mafundisho ya Mtume Wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) ni haki isiyopingana, na hii inatokana na kauli Yake Subhaanahu wa Ta’ala Aliposema:

 

ÃóÝóáÇó íóÊóÏóÈøóÑõæäó ÇáúÞõÑúÂäó æóáóæú ßóÇäó ãöäú ÚöäÏö ÛóíúÑö Çááøåö áóæóÌóÏõæÇú Ýöíåö ÇÎúÊöáÇóÝðÇ ßóËöíÑðÇ

"Hebu hawaizingatii hii Qur-aan? Na lau kuwa imetoka kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu bila ya shaka wangeli kuta ndani yake khitilafu nyingi."

An-Nisaa – 82

 

Na kwa vile kauli zinazopingana huwa zinasutana, na hili ni jambo lisiliowezekana katika habari Anazotupa Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta’ala na anazotupa Mtume wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam). Na yeyote anayedai kuwa ndani ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu au ndani ya mafundisho ya Mtume Wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) yamo maneno yanayopingana, akasema hayo kwa kukusudia au kwa vile moyo wake umekwenda upande, basi huyo anatakaiwa atubu kwa Mola wake na atoke ndani ya upotofu wake.

 

Na yeyote anayedhani kuwa mna upungufu wowote ndani ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu au ndani ya mafundisho ya Mtume wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) au baina yao, basi huyo ima ana upungufu wa elimu au uchache wa fahamu au ana upungufu katika kuzingatia kwake, kwa hivyo aitafute elimu na ajitahidi katika kuzingatia mpaka ukweli utakapombainikia. Na kama haukumbainikia, basi amtafute mwenye elimu kupita yeye na aachane na upotofu wake, na aseme kama wanavyosema wale waliobobea katika elimu:

 

ÂãóäøóÇ Èöåö ßõáøñ ãøöäú ÚöäÏö ÑóÈøöäóÇ

"Tumeamini, zote zimetoka kwa Mola wetu."

Aali-‘ImraAn – 7

 

Na ajue ya kuwa Qur-aan na Sunnah haviwezi kugongana wala kupingana wala hapana hitilafu baina yake.

Rudi juu

 

Malaika

Na tunaamini juu Malaika wa Mwenyezi Mungu kama ulivyokuja wasfu wao ndani ya Qur-aan kwamba wao ni:

 

Èóáú ÚöÈóÇÏñ ãøõßúÑóãõæäó. áÇ íóÓúÈöÞõæäóåõ ÈöÇáúÞóæúáö æóåõã ÈöÃóãúÑöåö íóÚúãóáõæäó

"Bali hao ni watumwa walio tukuzwa. Hawamtangulii kwa neno, nao wanafanya amri Zake."

 

Mwenyezi Mungu Amewaumba ili wamuabudu na kumtii.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

 áÇ íóÓúÊóßúÈöÑõæäó Úóäú ÚöÈóÇÏóÊöåö æáÇ íóÓúÊóÍúÓöÑõæäó. íõÓóÈøöÍõæäó Çááøóíúáó æóÇáäøóåóÇÑó áÇ íóÝúÊõÑõæäó

"Hawafanyi kiburi wakaacha kumuabudu, wala hawachoki.

Wanamtakasa usiku na mchana, wala hawanyong'onyei."

Al-AnbiyAa – 19 – 20

 

Mwenyezi Mungu Akatujaalia tusiweze kuwaona, na Aliwafanya wengine kati ya waja Wake kuweza kuwaona, kwani Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) alimuona Jibriyl (‘Alayhis-Salaam) akiwa katika umbile lake la kweli ana mbawa mia sita, akiwa ameizinga anga yote juu yake.

Jibriyl (‘Alayhis-Salaam) aliwahi pia kuonekana na Bibi Maryam akiwa katika umbile la binaadamu aliyekamilika, akazungumza naye, na aliwahi pia kumjia Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) akiwa pamoja na Maswahaba wake (Radhiya Llaahu anhum) akiwa katika umbile la mwanamume asiyejulikana wala hapakuwa na ishara yoyote usoni mwake kama ni mtu aliyetoka safari ndefu, akaliegemeza goti lake juu ya goti la Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) na kuuweka mkono wake juu ya paja la Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam), kisha akazungumza naye huku Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) akimjibu, na baada ya kuondoka ndipo Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) akawaambia Maswahaba wake (Radhiya Llaahu anhum) kuwa yule alikuwa Jibriyl (‘Alayhis-Salaam).

 

Na tunaamini kuwa Malaika wana kazi zao maalum walizopewa na Mola wao. Jibriyl (‘Alayhis-Salaam)ni mletaji wahyi kwa Mitume. Anawateremshia kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kuwafikishia anaotumwa kuwafikishia katika Mitume yake Subhaanahu wa Ta’ala. Na yupo Mikaaiyl aliyepewa kazi ya kuteremsha mvua na ya mazao anapopewa amri na Mwenyezi Mungu. Na yupo Israafiyl mwenye kazi ya kupuliza parapanda (baragumu) siku ya Qiyaamah. Na yupo Malaika wa kifo aliyepewa kazi ya kutoa roho wakati wa kufa, na yupo Malaika wa majabali, na yupo Malik mlinzi wa mlango wa Motoni, na wapo Malaika wanaowashughulikia watoto wachanga matumboni mwa mama zao, na wengine waliopewa kazi ya kuwahifadhi wanaadamu na wengine wenye kuandika ‘amali zao, na kila mtu ana Malaika wawili.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÅöÐú íóÊóáóÞøóì ÇáúãõÊóáóÞøöíóÇäö Úóäö Çáúíóãöíäö æóÚóäö ÇáÔøöãóÇáö ÞóÚöíÏñ. ãóÇ íóáúÝöÙõ ãöä Þóæúáò ÅöáøóÇ áóÏóíúåö ÑóÞöíÈñ ÚóÊöíÏñ

"Wanapopokea wapokeaji wawili, wanaokaa kuliani na kushotoni

Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari (kuandika)."

Qaaf – 17 – 18

 

Na wengine wana kazi za kuwauliza maiti baada ya kufikishwa kaburini, wanajiwa na Malaika wawili na kumuuliza Nani Mola wake, nini dini yake, nani mtume wake?

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

íõËóÈøöÊõ Çááøåõ ÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇú ÈöÇáúÞóæúáö ÇáËøóÇÈöÊö Ýöí ÇáúÍóíóÇÉö ÇáÏøõäúíóÇ æóÝöí ÇáÂÎöÑóÉö æóíõÖöáøõ Çááøåõ ÇáÙøóÇáöãöíäó æóíóÝúÚóáõ Çááøåõ ãóÇ íóÔóÇÁ

"Mwenyezi Mungu Huwatia imara wenye kuamini kwa kauli imara katika maisha ya dunia na katika Akhera. Na Mwenyezi Mungu huwaacha kupotea hao wenye kudhulumu. Na Mwenyezi Mungu Hufanya apendavyo."

Ibraahiym – 27

 

Na wapo Malaika waliopewa kazi ya kuwashughulikia watu wa Peponi.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóÇáãóáÇóÆößóÉõ íóÏúÎõáõæäó Úóáóíúåöã ãøöä ßõáøö ÈóÇÈò. ÓóáÇóãñ Úóáóíúßõã ÈöãóÇ ÕóÈóÑúÊõãú ÝóäöÚúãó ÚõÞúÈóì ÇáÏøóÇÑö

"Na Malaika wanawaingilia katika kila mlango. (Wakiwaambia) Assalaamu ‘Alaykum! Amani iwe juu yenu, kwa sababu ya mlivyosubiri! Basi ni mema mno malipo ya Nyumba ya Akhera."

Ar-Ra’ad – 23 – 34

 

Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) alitujulisha kuwa ndani ya 'Baytul Ma’amuur', iliyopo mbinguni wanaingia na kuswali ndani yake kila siku Malaika elfu sabini wakishamaliza hawaipati fursa ya kurudi humo tena.

 

Rudi juu

Vitabu

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Amewateremshia Mitume Vitabu ili viwe hoja na mwangaza kwa walimwengu kwa ajili ya kuwafundisha hekima na kwa ajili ya kuwatakasa.

 

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Amemteremshia kila Mtume Kitabu.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áóÞóÏú ÃóÑúÓóáúäóÇ ÑõÓõáóäóÇ ÈöÇáúÈóíøöäóÇÊö æóÃóäÒóáúäóÇ ãóÚóåõãõ ÇáúßöÊóÇÈó æóÇáúãöíÒóÇäó áöíóÞõæãó ÇáäøóÇÓõ ÈöÇáúÞöÓúØö

"Kwa hakika tuliwatuma Mitume Wetu kwa dalili waziwazi, na tukateremsha Kitabu pamoja nao na Mizani, ili watu wasimamie uadilifu."

Al-Hadiyd – 25

 

Na katika vitabu hivyo tunavyovijua ni:

 

1.  Taurati; Mwenyezi Mungu Alimteremsia Nabii Muusa (‘Alayhis-Salaam), na hiki ni Kitabu kitukufu kupita vyote vya Bani Israaiyl.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

ÅöäøóÇ ÃóäÒóáúäóÇ ÇáÊøóæúÑóÇÉó ÝöíåóÇ åõÏðì æóäõæÑñ íóÍúßõãõ ÈöåóÇ ÇáäøóÈöíøõæäó ÇáøóÐöíäó ÃóÓúáóãõæÇú áöáøóÐöíäó åóÇÏõæÇú æóÇáÑøóÈøóÇäöíøõæäó æóÇáÃóÍúÈóÇÑõ ÈöãóÇ ÇÓúÊõÍúÝöÙõæÇú ãöä ßöÊóÇÈö Çááøåö æóßóÇäõæÇú Úóáóíúåö ÔõåóÏóÇÁ

"Hakika Sisi Tuliteremsha Taurati yenye uongofu na nuru, ambayo kwayo Manabii walionyenyekea Kiislamu, na wacha Mungu, na wanazuoni, waliwahukumu Mayahudi; kwani walikabidhiwa kukihifadhi Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Nao wakawa ni mashahidi juu yake."

Al-Maaidah – 44

 

2.  Injili; Mwenyezi Mungu alimteremshia Nabii ‘Iysa (‘Alayhis-Salaam), na hiki kinakisadikisha Taurati na kukikamilisha.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóÂÊóíúäóÇåõ ÇáÅöäÌöíáó Ýöíåö åõÏðì æóäõæÑñ æóãõÕóÏøöÞðÇ áøöãóÇ Èóíúäó íóÏóíúåö ãöäó ÇáÊøóæúÑóÇÉö æóåõÏðì æóãóæúÚöÙóÉð áøöáúãõÊøóÞöíäó

"Na tukampa Injili iliyomo ndani yake uongofu, na nuru na inayosadikisha yaliyokuwa kabla yake katika Taurati, na uongofu na mawaidha kwa wacha Mungu."

Al-Maaidah – 46

 

3.  Zaburi; Aliyopewa Nabii Daawuud (‘Alayhis-Salaam).

 

4.  Sahifa (Suhuf); Walizoteremshiwa Nabii Ibraahiym na Muusa (‘Alayhimas-Salaam).

 

5.  Qur-aan tukufu; Aliyoteremshiwa Mtume wetu Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) mwisho wa ma Nabii.

 

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

åõÏðì áøöáäøóÇÓö æóÈóíøöäóÇÊò ãøöäó ÇáúåõÏóì æóÇáúÝõÑúÞóÇäö

"Ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi."

Al-Baqarah – 185

 

 

Na Akasema:

 

ãõÕóÏöøÞðÇ áöøãóÇ Èóíúäó íóÏóíúåö ãöäó ÇáúßöÊóÇÈö æóãõåóíúãöäðÇ Úóáóíúåö

"Kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Vitabu na kuyalinda."

Al-Maaidah – 48

 

Kwa Kitabu hiki Mwenyezi Mungu Akavifuta vilivyotangulia na Akachukua Yeye mwenyewe jukumu la kukilinda ili kibaki kuwa hoja kwa viumbe wote mpaka siku ya Qiyaamah.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÅöäøóÇ äóÍúäõ äóÒøóáúäóÇ ÇáÐøößúÑó æóÅöäøóÇ áóåõ áóÍóÇÝöÙõæäó

"Hakika Sisi ndio Tulioteremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio Tutaoulinda."

Al-Hijr – 9

 

Ama Vitabu vilivyotangulia, vilikuwa vikiletwa kwa ajili ya wakati maalum, na ukishamalizika wakati wake vinaletwa vingine kuchukua nafasi yake, na hii ndiyo maana havikuwa na uwezo wa kujilinda kutokana na ubadilishaji.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ãøöäó ÇáøóÐöíäó åóÇÏõæÇú íõÍóÑøöÝõæäó Çáúßóáöãó Úóä ãøóæóÇÖöÚöåö

"Miongoni mwa Mayahudi wamo ambao hubadilisha maneno na kuyatoa mahala pake."

An-Nisaa -46

 

Na Akasema:

 

Ýóæóíúáñ áøöáøóÐöíäó íóßúÊõÈõæäó ÇáúßöÊóÇÈó ÈöÃóíúÏöíåöãú Ëõãøó íóÞõæáõæäó åóÜÐóÇ ãöäú ÚöäÏö Çááøåö áöíóÔúÊóÑõæÇú Èöåö ËóãóäÇð ÞóáöíáÇð Ýóæóíúáñ áøóåõã ãøöãøóÇ ßóÊóÈóÊú ÃóíúÏöíåöãú æóæóíúáñ áøóåõãú ãøöãøóÇ íóßúÓöÈõæäó

"Basi ole wao wanaoandika kitabu kwa mikono yao, kisha wakasema: Hiki kimetoka kwa Mwenyezi Mungu, ili wachumie kwacho pato dogo. Basi ole wao kwa yale iliyoandika mikono yao, na ole wao kwa yale wanayoyachuma."

Al-Baqarah – 79

 

Na Akasema:

 

Þõáú ãóäú ÃóäÒóáó ÇáúßöÊóÇÈó ÇáøóÐöí ÌóÇÁ Èöåö ãõæÓóì äõæÑðÇ æóåõÏðì áøöáäøóÇÓö ÊóÌúÚóáõæäóåõ ÞóÑóÇØöíÓó ÊõÈúÏõæäóåóÇ æóÊõÎúÝõæäó ßóËöíÑðÇ

"Sema: Nani aliyeteremsha Kitabu alichokuja nacho Muusa, chenye nuru na uongofu kwa watu, mlichokifanya kurasa kurasa mkizionyesha, na mengi mkiyaficha."

Al-An’aam – 91

 

Na Akasema:

 

æóÅöäøó ãöäúåõãú áóÝóÑöíÞðÇ íóáúæõæäó ÃóáúÓöäóÊóåõã ÈöÇáúßöÊóÇÈö áöÊóÍúÓóÈõæåõ ãöäó ÇáúßöÊóÇÈö æóãóÇ åõæó ãöäó ÇáúßöÊóÇÈö æóíóÞõæáõæäó åõæó ãöäú ÚöäÏö Çááøåö æóãóÇ åõæó ãöäú ÚöäÏö Çááøåö æóíóÞõæáõæäó Úóáóì Çááøåö ÇáúßóÐöÈó æóåõãú íóÚúáóãõæäó. ãóÇ ßóÇäó áöÈóÔóÑò Ãóä íõÄúÊöíóåõ Çááøåõ ÇáúßöÊóÇÈó æóÇáúÍõßúãó æóÇáäøõÈõæøóÉó Ëõãøó íóÞõæáó áöáäøóÇÓö ßõæäõæÇú ÚöÈóÇÏðÇ áøöí ãöä Ïõæäö Çááøåö æóáóÜßöä ßõæäõæÇú ÑóÈøóÇäöíøöíäó ÈöãóÇ ßõäÊõãú ÊõÚóáøöãõæäó ÇáúßöÊóÇÈó æóÈöãóÇ ßõäÊõãú ÊóÏúÑõÓõæäó

"Na wapo baadhi yao wanaopindua ndimi zao katika kusoma Kitabu ili mdhanie kuwa hayo yanatoka Kitabuni, na wala hayatoki Kitabuni. Na husema: Haya yametoka kwa Mwenyezi Mungu. Na wala hayatoki kwa Mwenyezi Mungu. Na wanamsingizia Mwenyezi Mungu uongo na wao wanajua.

Haiwezi kuwa mtu aliyepewa na Mwenyezi Mungu Kitabu na hikima na Unabii kisha awaambie watu: Kuweni wa kuniabudu mimi badala ya Mwenyezi Mungu. Bali atawaambia: Kuweni wenye kumuabudu Mola wa viumbe vyote, kwa kuwa nyinyi mnafundisha Kitabu na kwa kuwa mnakisoma."

Aali-‘Imraan – 78 – 79

 

Na Akasema:

 

íóÇ Ãóåúáó ÇáúßöÊóÇÈö ÞóÏú ÌóÇÁßõãú ÑóÓõæáõäóÇ íõÈóíøöäõ áóßõãú ßóËöíÑðÇ ãøöãøóÇ ßõäÊõãú ÊõÎúÝõæäó ãöäó ÇáúßöÊóÇÈö æóíóÚúÝõæ Úóä ßóËöíÑò ÞóÏú ÌóÇÁßõã ãøöäó Çááøåö äõæÑñ æóßöÊóÇÈñ ãøõÈöíäñ

"Enyi Watu wa Kitabu! Amekwishakujieni Mtume wetu anayekufichulieni mengi mliyokuwa mkiyaficha katika Kitabu, na anayesamehe mengi. Bila shaka imekujieni kutoka kwa Mwenyezi Mungu nuru na Kitabu kinachobainisha."

Al-Maaidah – 15

 

Rudi juu

Mitume

Na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Amewatuma kwa waja Wake Mitume ili wawe wabashiri na waonyaji.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÑøõÓõáÇð ãøõÈóÔøöÑöíäó æóãõäÐöÑöíäó áöÆóáÇøó íóßõæäó áöáäøóÇÓö Úóáóì Çááøåö ÍõÌøóÉñ ÈóÚúÏó ÇáÑøõÓõáö æóßóÇäó Çááøåõ ÚóÒöíÒðÇ ÍóßöíãðÇ

"Mitume hao ni wabashiri na waonyaji, ili watu wasiwe na hoja juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kuletewa Mitume. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima."

An-Nisaa – 165

 

Na tunaamini kuwa Muhammad ni mbora wa Mitume yote, kisha Ibrahim kisha Musa kisha Nuh kisha Issa mwana wa Maryam, na hawa ndio waliohuswa katika aya ifuatayo.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóÅöÐú ÃóÎóÐúäóÇ ãöäó ÇáäøóÈöíøöíäó ãöíËóÇÞóåõãú æóãöäßó æóãöä äøõæÍò æóÅöÈúÑóÇåöíãó æóãõæÓóì æóÚöíÓóì ÇÈúäö ãóÑúíóãó æóÃóÎóÐúäóÇ ãöäúåõã ãøöíËóÇÞðÇ ÛóáöíÙðÇ

"Na tulipochukua ahadi kwa Manabii na kwako wewe (Muhammad), na Nuuh na Ibraahiym na ‘Iysa mwana wa Mariamu, na tulichukua kwao ahadi ngumu."

Al-Ahzaab – 7

 

 

Na tunaamini kuwa shari’ah ya Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) imekusanya fadhila zote walizokuja nazo Mitume iliyotangulia.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÔóÑóÚó áóßõã ãøöäó ÇáÏøöíäö ãóÇ æóÕøóì Èöåö äõæÍðÇ æóÇáøóÐöí ÃóæúÍóíúäóÇ Åöáóíúßó æóãóÇ æóÕøóíúäóÇ Èöåö ÅöÈúÑóÇåöíãó æóãõæÓóì æóÚöíÓóì Ãóäú ÃóÞöíãõæÇ ÇáÏøöíäó æóáóÇ ÊóÊóÝóÑøóÞõæÇ Ýöíåö

"Amekuamrisheni Dini ile ile aliyomuusia Nuuh na tuliyokufunulia wewe, na tuliyowausia Ibraahiym na Muusa na ‘Iysa, kwamba shikeni Dini wala msifarikiane kwayo."

Ash-Shuuraa – 13

 

 

Na tunaamini kuwa Mitume yote ni watu, viumbe na hawana uwezo wowote wa kuumba au kugawa rizki wala hawajui ghaibu nk.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóáÇó ÃóÞõæáõ áóßõãú ÚöäÏöí ÎóÒóÂÆöäõ Çááøåö æóáÇó ÃóÚúáóãõ ÇáúÛóíúÈó æóáÇó ÃóÞõæáõ Åöäøöí ãóáóßñ

"Wala sikwambiini kuwa nina khazina za Mwenyezi Mungu; wala kuwa mimi najua mambo ya ghaibu; wala sisemi: Mimi ni Malaika."

Huud – 31

 

Mwenyezi Mungu Alimuamrisha Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) atamke maneno yafuatayo:

 

Þõá áÇøó ÃóÞõæáõ áóßõãú ÚöäÏöí ÎóÒóÂÆöäõ Çááøåö æóáÇ ÃóÚúáóãõ ÇáúÛóíúÈó æóáÇ ÃóÞõæáõ áóßõãú Åöäøöí ãóáóßñ

“Sema: Mimi sikwambiini kuwa ninazo khazina za Mwenyezi Mungu. Wala sijui mambo yaliyofichikana. Wala sikwambiini kuwa mimi ni Malaika”

Al-An’aam – 50

 

Na akaamrishwa pia atamke:

 

Þõá áÇøó Ãóãúáößõ áöäóÝúÓöí äóÝúÚðÇ æóáÇó ÖóÑøðÇ ÅöáÇøó ãóÇ ÔóÇÁ Çááøåõ

"Sema: Siimilikii nafsi yangu manufaa wala madhara, ila apendavyo Mwenyezi Mungu."

Al-A’araaf – 188

 

Na atamke:

 

Þõáú Åöäøöí áÇ Ãóãúáößõ áóßõãú ÖóÑøðÇ æáÇ ÑóÔóÏðÇ. Þõáú Åöäøöí áóä íõÌöíÑóäöí ãöäó Çááøóåö ÃóÍóÏñ æóáóäú ÃóÌöÏó ãöä Ïõæäöåö ãõáúÊóÍóÏðÇ

"Sema: Mimi sina mamlaka ya kukudhuruni wala kukuongozeni."

Sema: Hakika hapana yeyote awezaye kunilinda na Mwenyezi Mungu, wala sitapata pa kukimbilia isipokuwa kwake Yeye tu."

Al-Jinn – 21-22

 

Na tunaamini kuwa wao ni waja wa Mwenyezi Mungu Aliowakirimu kwa kuwapa ujumbe.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÐõÑøöíøóÉó ãóäú ÍóãóáúäóÇ ãóÚó äõæÍò Åöäøóåõ ßóÇäó ÚóÈúÏðÇ ÔóßõæÑðÇ

"Enyi kizazi tuliyowachukua pamoja na Nuuh! Hakika yeye alikuwa mja mwenye shukrani."

Al-Israa – 3

 

Na Akasema:

 

ÊóÈóÇÑóßó ÇáøóÐöí äóÒøóáó ÇáúÝõÑúÞóÇäó Úóáóì ÚóÈúÏöåö áöíóßõæäó áöáúÚóÇáóãöíäó äóÐöíÑðÇ

"Ametukuka aliye teremsha Furqaan kwa mja Wake, ili awe mwonyaji kwa walimwengu wote."

Al-Furqaan – 1

 

Na juu ya Mitume mingine Akasema:

 

æóÇÐúßõÑú ÚöÈóÇÏóäóÇ ÅÈúÑóÇåöíãó æóÅöÓúÍóÞó æóíóÚúÞõæÈó Ãõæúáöí ÇáÃóíúÏöí æóÇáÃÈúÕóÇÑö

"Wakumbuke waja wetu, Ibraahiym na Is-haaq na Yaa'quub waliokuwa na nguvu na busara."

Swaad – 45

 

Na Akasema:

 

æóæóåóÈúäóÇ áöÏóÇæõæÏó ÓõáóíúãóÇäó äöÚúãó ÇáúÚóÈúÏõ Åöäøóåõ ÃóæøóÇÈñ

"Na Daawuud Tukamtunukia Sulaymaan. Alikuwa mja mwema. Na hakika alikuwa mwingi wa kutubia."

Swaad – 30

 

Na juu ya ‘Iysa mwana wa Maryam Mwenyezi Mungu Anasema:

 

"Hakuwa yeye (‘Iysa) ila ni Mtumwa Tuliyemneemesha na tukamfanya ni mfano kwa Wana wa Israili."

Az-Zukhruf – 59

 

 

Tunaamini pia kuwa Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta’ala Amekamilisha ujumbe wake kwa kumleta Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) kama ni Mtume kwa watu wote.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

Þõáú íóÇ ÃóíøõåóÇ ÇáäøóÇÓõ Åöäøöí ÑóÓõæáõ Çááøåö Åöáóíúßõãú ÌóãöíÚðÇ ÇáøóÐöí áóåõ ãõáúßõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖö áÇ ÅöáóÜåó ÅöáÇøó åõæó íõÍúíöÜí æóíõãöíÊõ ÝóÂãöäõæÇú ÈöÇááøåö æóÑóÓõæáöåö ÇáäøóÈöíøö ÇáÃõãøöíøö ÇáøóÐöí íõÄúãöäõ ÈöÇááøåö æóßóáöãóÇÊöåö æóÇÊøóÈöÚõæåõ áóÚóáøóßõãú ÊóåúÊóÏõæäó

"Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume kwenu nyinyi nyote, niliyetumwa na Mwenyezi Mungu Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Hapana mungu ila Yeye Anayehuisha na Anayefisha. Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake asiyejua kusoma na kuandika, ambaye anamuamini Mwenyezi Mungu na maneno Yake. Na mfuateni yeye ili mpate kuongoka."

Al-A’araf – 158

 

Rudi juu

Dini Ya Mwenyezi Mungu

Na tunaamini kuwa dini alokuja nayo ni Islam aliyoridhika nayo Mwenyezi Mungu kwa waja Wake. Na kwamba Mwenyezi Mungu Haikubali dini nyingine isipokuwa hii.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

Åöäøó ÇáÏøöíäó ÚöäÏó Çááøåö ÇáÅöÓúáÇóãõ

"Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu."

Aali-‘Imraan – 19

 

Na Akasema:

 

Çáúíóæúãó ÃóßúãóáúÊõ áóßõãú Ïöíäóßõãú æóÃóÊúãóãúÊõ Úóáóíúßõãú äöÚúãóÊöí æóÑóÖöíÊõ áóßõãõ ÇáÅöÓúáÇóãó ÏöíäðÇ

"Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na Nimekutimizieni neema Yangu, na Nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini."

Al-Maaidah – 3

 

Na Akasema:

 

æóãóä íóÈúÊóÛö ÛóíúÑó ÇáÅöÓúáÇóãö ÏöíäðÇ Ýóáóä íõÞúÈóáó ãöäúåõ æóåõæó Ýöí ÇáÂÎöÑóÉö ãöäó ÇáúÎóÇÓöÑöíäó

"Na anayetafuta dini isiyokuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye khasara."

Aali-‘Imraan – 85

 

 

Na tunaamini kuwa yeyote atakayedai kuwa ipo dini nyengine inayokubaliwa na Mwenyezi Mungu isiyokuwa Islamu, kama vile dini ya Kiyahudi au ya Kinasara au dini nyengine yoyote, huyo anakuwa amekufuru, na lazima atubu kwa kufru yake hiyo. Akitubu anasamehewa, ama asipotubu huyo anauliwa kama ni Murtaddi, kwa sababu anakuwa ameikadhibisha Qur-aan tukufu.

 

Na tunaamini kuwa hapana tena Mtume baada ya Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam), na yeyote atakayejidai utume baada yake au akamsadiki mwenye kujidai utume anakuwa kafir, kwa sababu anakuwa amemkadhibisha Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Waislamu wote.

Rudi juu

 

Makhalifa Waongofu

Na tunaamini kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) anao Makhalifa waongofu waliouongoza umma baada ya kufa kwake kwa kueneza elimu na da’awah na uongozi, na kwamba mbora wao ni Abu Bakr Asw-Swiddiyq (Radhiya Llaahu ‘anhu) akifuatiwa na ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhiya Llaahu ‘anhu) kisha ‘Uthmaan bin ‘Affaan (Radhiya Llaahu ‘anhu), kisha ‘Aliy bin Abi Twaalib (Radhiya Llaahu ‘anhu), na huu ndio mpangilio wao katika kufadhilishwa kwao.

 

Na tunaamini kuwa umma ule ndio umma bora kupita zote, na hii inatokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Alipowaambia:

 

ßõäÊõãú ÎóíúÑó ÃõãøóÉò ÃõÎúÑöÌóÊú áöáäøóÇÓö ÊóÃúãõÑõæäó ÈöÇáúãóÚúÑõæÝö æóÊóäúåóæúäó Úóäö ÇáúãõäßóÑö æóÊõÄúãöäõæäó ÈöÇááøåö

"Nyinyi ndio umma bora kuliko umma zote waliodhihirishiwa watu, kwa kuwa mnaamrisha mema na mnakataza maovu, na mnamuamini Mwenyezi Mungu."

Aali-‘Imran – 110

 

 

Na tunaamini kuwa walio bora kupita wote ni Maswahaba (Radhiya Llaahu ‘anhum), kisha waliokuja baada yao, kisha waliokuja baada yao, na kwamba wangali wapo watu wenye kuidhihirisha haki bila kujali lawama za wanaowalaumu, mpaka siku Mwenyezi Mungu atakapoleta amri Yake.

 

Na tunaitakidi kuwa yaliyotokea baina ya Maswahaba (Radhiya Llaahu anhum) katika fitna na mapambano, yanatokana na jitihada zao katika uamuzi. Wapo waliosibu na wapo waliokosea, na kama alivyosema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam):

 

"Mwenyezi kusibu anapata ujira mara mbili, na mwenye kukosea anapata ujira mara moja."

 

Na kwamba Mwenyezi Mungu Atawasamehe makosa yao, na tunaamini kuwa lazima tuache kuwasema vibaya, na badala yake tuwaseme kwa wema, na tusiwataje isipokuwa kwa kuzitaja sifa wanazozistahiki, na tuziondoe chuki zetu juu yao.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áÇ íóÓúÊóæöí ãöäßõã ãøóäú ÃóäÝóÞó ãöä ÞóÈúáö ÇáúÝóÊúÍö æóÞóÇÊóáó ÃõæúáóÆößó ÃóÚúÙóãõ ÏóÑóÌóÉð ãøöäó ÇáøóÐöíäó ÃóäÝóÞõæÇ ãöä ÈóÚúÏõ æóÞóÇÊóáõæÇ æóßõáÇ æóÚóÏó Çááøóåõ ÇáúÍõÓúäóì

"Hawawi sawa miongoni mwenu wenye kutoa kabla ya Ushindi na wakapigana vita. Hao wana daraja kubwa zaidi kuliko wale ambao waliotoa baadae na wakapigana. Na wote hao Mwenyezi Mungu Amewaahidia wema."

Al-Hadiyd – 10

 

Na Akasema:

 

æóÇáøóÐöíäó ÌóÇÄõæÇ ãöä ÈóÚúÏöåöãú íóÞõæáõæäó ÑóÈøóäóÇ ÇÛúÝöÑú áóäóÇ æóáÇÎúæóÇäöäóÇ ÇáøóÐöíäó ÓóÈóÞõæäóÇ ÈöÇáÇíãóÇäö æóáÇ ÊóÌúÚóáú Ýöí ÞõáõæÈöäóÇ ÛöáÇ áøöáøóÐöíäó ÂãóäõæÇ ÑóÈøóäóÇ Åöäøóßó ÑóÄõæÝñ ÑøóÍöíãñ

"Na waliokuja baada yao (wakawa wanawapenda Waislamu waliotangulia wanawaombea du’aa) wanasema: Mola wetu! Tughufirie sisi na ndugu zetu waliotutangulia (kufa) katika Uislamu, wala usijaalie ndani ya nyoyo zetu undani kuwafanyia Waislamu (wenzetu). Mola wetu! Hakika Wewe ni Mpole na Mwenye kurehemu."

Al-Hashr – 10

 

Rudi juu

Siku Ya Mwisho

Tunaamini kuwa Siku ya Mwisho ndiyo Siku ya Qiyaamah, ambapo hapana tena siku nyingine baada yake, na siku hiyo Mwenyezi Mungu Atawafufua waja wake kwa ajili ya kuwaingiza katika nyumba ya neema 'Peponi', au katika nyumba ya adhabu iumizayo 'Motoni'.

 

Tunaamini kuwa watu watafufuliwa baada ya baragumu kupigwa, kama Mwenyezi Mungu Alivyosema:

 

æóäõÝöÎó Ýöí ÇáÕøõæÑö ÝóÕóÚöÞó ãóä Ýöí ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóãóä Ýöí ÇáÃÑúÖö ÅöáÇ ãóä ÔóÇÁ Çááøóåõ Ëõãøó äõÝöÎó Ýöíåö ÃõÎúÑóì ÝóÅöÐóÇ åõã ÞöíóÇãñ íóäÙõÑõæäó

"Na litapulizwa barugumu, wazimie waliomo mbinguni na waliomo katika ardhi, isipokuwa Aliyemtaka Mwenyezi Mungu. Kisha litapulizwa mara nyengine. Hapo watainuka wawe wanangojea."

Az-Zumar – 68

 

 

Kisha watu watasimamishwa mbele ya Mwenyezi Mungu wakiwa kama siku waliyozaliwa bila viatu wala nguo (kama ilivyoelezwa katika Swahiyh Al-Bukhaariy na Muslim – Imepokelewa kuwa Bibi ‘Aaishah (Radhiya Llaahu ‘anha) alimuuliza Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam):

"Watu watafufuliwa wakiwa uchi kila mmoja anamtizama mwenzake?" Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) akamwambia: "Ewe Aisha! mambo siku hiyo yatakuwa magumu kuliko hivyo."

Watu hawatakuwa na wakati wa kutizamana - mambo yatakuwa magumu sana - Ya rabbi sallim.)

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

íóæúãó äóØúæöí ÇáÓøóãóÇÁ ßóØóíøö ÇáÓøöÌöáøö áöáúßõÊõÈö ßóãóÇ ÈóÏóÃúäóÇ Ãóæøóáó ÎóáúÞò äøõÚöíÏõåõ æóÚúÏðÇ ÚóáóíúäóÇ ÅöäøóÇ ßõäøóÇ ÝóÇÚöáöíäó

"Siku tutakapozikunja mbingu kama mkunjo wa karatasi za vitabu. Kama tulivyoanza umbo la mwanzo tutalirudisha tena. Ni ahadi iliyo juu yetu. Hakika Sisi ni watendao."

Al-Anbiyaa – 104

 

 

Na tunaamini kuwa watu watapewa madaftari yao kwa mkono wa kulia au nyuma ya migongo yao au kushotoni mwao.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÝóÃóãøóÇ ãóäú ÃõæÊöíó ßöÊóÇÈóåõ Èöíóãöíäöåö. ÝóÓóæúÝó íõÍóÇÓóÈõ ÍöÓóÇÈðÇ íóÓöíÑðÇ. æóíóäÞóáöÈõ Åöáóì Ãóåúáöåö ãóÓúÑõæÑðÇ. æóÃóãøóÇ ãóäú ÃõæÊöíó ßöÊóÇÈóåõ æóÑóÇÁ ÙóåúÑöåö. ÝóÓóæúÝó íóÏúÚõæ ËõÈõæÑðÇ. æóíóÕúáóì ÓóÚöíÑðÇ

"Ama atakayepewa daftari lake kwa mkono wa kulia. Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi. Na arudi kwa ahali zake na furaha.

Na ama atakayepewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake. Basi huyo ataomba kuteketea. Na ataingia Motoni."

Al-Inshiqaaq – 7 – 12

 

Na Akasema:

 

æóßõáøó ÅöäÓóÇäò ÃóáúÒóãúäóÇåõ ØóÂÆöÑóåõ Ýöí ÚõäõÞöåö æóäõÎúÑöÌõ áóåõ íóæúãó ÇáúÞöíóÇãóÉö ßöÊóÇÈðÇ íóáúÞóÇåõ ãóäÔõæÑðÇ . ÇÞúÑóÃú ßóÊóÇÈóßó ßóÝóì ÈöäóÝúÓößó Çáúíóæúãó Úóáóíúßó ÍóÓöíÈðÇ

"Na kila mtu tumemfungia ‘amali yake shingoni mwake. Na Siku ya Qiyaamah tutamtolea kitabu atakachokikuta kiwazi kimekunjuliwa.

Ataambiwa: Soma kitabu chako! Nafsi yako inakutosha leo kukuhisabu."

Al-Israa- 13 – 14

 

 

Na tunaamini kuwa mezani zitawekwa Siku ya Qiyaamah na kwamba hapana atakayedhulumiwa.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

Ýóãóä íóÚúãóáú ãöËúÞóÇáó ÐóÑøóÉò ÎóíúÑðÇ íóÑóåõ. æóãóä íóÚúãóáú ãöËúÞóÇáó ÐóÑøóÉò ÔóÑøðÇ íóÑóåõ

"Basi anayetenda chembe ya wema, atauona! Na anayetenda chembe ya uovu atauona!."

Zilzaal – 7 – 8

 

Na Akasema:

 

Ýóãóä ËóÞõáóÊú ãóæóÇÒöíäõåõ ÝóÃõæúáóÆößó åõãõ ÇáúãõÝúáöÍõæäó. æóãóäú ÎóÝøóÊú ãóæóÇÒöíäõåõ ÝóÃõæúáóÆößó ÇáøóÐöíäó ÎóÓöÑõæÇ ÃóäÝõÓóåõãú Ýöí Ìóåóäøóãó ÎóÇáöÏõæäó. ÊóáúÝóÍõ æõÌõæåóåõãõ ÇáäøóÇÑõ æóåõãú ÝöíåóÇ ßóÇáöÍõæäó

"Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa. Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu. Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizokunjana."

Al-Muuminuun – 102-104

Rudi juu

Shafa’ah

Na tunaamini kuwa ipo Shafa’ah (msamaha) kubwa ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) atakapowaombea umma wake baada ya kupewa idhini hiyo na Mola wake Subhaanahu wa Ta’ala, na baada ya watu kuona dhiki na kuanza kuwaendea Manabii Nuuh kisha Ibraahiym kisha Muusa kisha ‘Iysa (Alayhimus-Salaam) mpaka watakapoishia kwake Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam).

 

Na tunaamini pia kuwa wale watakaoingia Motoni katika Waislamu (tu) nao pia wataombewa Shafa’ah watolewe humo, na Shafa’ah hii ni kwa ajili ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) na Mitume mingine na watu wema na Malaika, na tunaamini kwamba Mwenyezi Mungu Atawatoa Motoni pia makundi kwa makundi ya Waislamu kwa fadhila Zake tu na rehma Yake, bila hata kuombewa Shafa’ah.

 

 

Hodhi na Swiraat

Na tunaamini kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) ana hodhi lake, na maji yake ni meupe kuliko maziwa na matamu kuliko asali, na yenye harufu nzuri kuliko hal miski. Urefu wake hodhi hilo ni mwendo wa mwezi mzima, na upana wake mwendo wa mwezi mzima.na vyombo vyake vinang'aa kama nyota za mbinguni.

 

Waislamu watakunywa humo, na atakayekunywa hatopata kiu tena.

 

Tuaamini kuwa ipo 'Swiraat' itakayowekwa juu ya Jahannam, na watu watapita juu yake, na kasi zao zitakuwa kiasi cha ‘amali zao. Wapo watakaopita kama umeme, na wengine kama upepo, na wengine kama ndege, na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) atakuwa juu yake huku akisema: "Ya rabbi Sallim sallim" (Mwenyezi Mungu Salimisha Salimisha)

 

 

Na tunaamini kila kilichokuja katika mafundisho ya Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) kuhusu Siku hiyo pamoja na vitisho vyake - Tunamuomba Mwenyezi Mungu Atusaidie.

 

Rudi juu

Pepo Na Moto

Na tunaamini juu ya Pepo na Moto, na kwamba Pepo ni nyumba ya neema Aliyowaandalia Mwenyezi Mungu waja wake wema wamchao. Ndani yake mna yale ambayo macho hayajapata kuyaona, wala masikio kuyasikia wala halijapata kumpitikia mtu yeyote nafsini mwake.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÝóáÇ ÊóÚúáóãõ äóÝúÓñ ãøóÇ ÃõÎúÝöíó áóåõã ãøöä ÞõÑøóÉö ÃóÚúíõäò ÌóÒóÇÁ ÈöãóÇ ßóÇäõæÇ íóÚúãóáõæäó

"Nafsi yoyote haijui waliyofichiwa katika hayo yanayofurahisha macho - ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda."

As-Sajdah – 17

 

 

Na Moto ni nyumba ya adhabu Aliyoitayarisha Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta’ala kwa ajili ya makafiri madhalimu. Ndani yake mna kila aina ya adhabu ambazo hazijapata kumpitikia mtu yeyote nafsini mwake.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóÅöä íóÓúÊóÛöíËõæÇ íõÛóÇËõæÇ ÈöãóÇÁ ßóÇáúãõåúáö íóÔúæöí ÇáúæõÌõæåó ÈöÆúÓó ÇáÔøóÑóÇÈõ æóÓóÇÁÊú ãõÑúÊóÝóÞðÇ

"Na wakiomba msaada watasaidiwa kwa kupewa maji kama mafuta yaliyotibuka. Yatayowababua nyuso zao. Kinywaji hicho ni kiovu mno!"

Al-Kahf – 29

 

Na Akasema:

 

Åöäøó Çááøóåó áóÚóäó ÇáúßóÇÝöÑöíäó æóÃóÚóÏøó áóåõãú ÓóÚöíÑðÇ. ÎóÇáöÏöíäó ÝöíåóÇ ÃóÈóÏðÇ áÇ íóÌöÏõæäó æóáöíøðÇ æóáÇ äóÕöíÑðÇ. íóæúãó ÊõÞóáøóÈõ æõÌõæåõåõãú Ýöí ÇáäøóÇÑö íóÞõæáõæäó íóÇ áóíúÊóäóÇ ÃóØóÚúäóÇ Çááøóåó æóÃóØóÚúäóÇ ÇáÑøóÓõæáÇ

"Hakika Mwenyezi Mungu Amewalaani makafiri na Amewaandalia Moto unaowaka kwa nguvu. Watadumu humo milele. Hawampati mlinzi wala wa kuwanusuru. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungelimtii Mwenyezi Mungu, na tungelimtii Mtume!"

Al-Ahzaab – 64 – 66

 

 

 

Maswali Ya Kaburini

Na tunaamini juu ya mtihani wa kaburini, wakati mtu atakapoulizwa nani Mola wake na ipi dini yake na yupi Mtume wake.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

íõËóÈøöÊõ Çááøåõ ÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇú ÈöÇáúÞóæúáö ÇáËøóÇÈöÊö Ýöí ÇáúÍóíóÇÉö ÇáÏøõäúíóÇ æóÝöí ÇáÂÎöÑóÉö

"Mwenyezi Mungu Huwatia imara wenye kuamini kwa kauli imara katika maisha ya dunia na katika Akhera."

Ibraahiym – 27

 

 

Na tunaamini juu ya neema za kaburini.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÇáøóÐöíäó ÊóÊóæóÝøóÇåõãõ ÇáúãóáÂÆößóÉõ ØóíøöÈöíäó íóÞõæáõæäó ÓóáÇãñ Úóáóíúßõãõ ÇÏúÎõáõæÇú ÇáúÌóäøóÉó ÈöãóÇ ßõäÊõãú ÊóÚúãóáõæäó

"Wale ambao Malaika huwafisha katika hali njema, wanawaambia: Amani iwe juu yenu! Ingieni Peponi kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyatenda."

An-Nahl – 32

 

 

 

Adhabu Ya Kaburini

Na tunaamini juu ya adhabu ya kaburini kwa madhalimu na makafiri.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

æóáóæú ÊóÑóì ÅöÐö ÇáÙøóÇáöãõæäó Ýöí ÛóãóÑóÇÊö ÇáúãóæúÊö æóÇáúãóáÂÆößóÉõ ÈóÇÓöØõæÇú ÃóíúÏöíåöãú ÃóÎúÑöÌõæÇú ÃóäÝõÓóßõãõ Çáúíóæúãó ÊõÌúÒóæúäó ÚóÐóÇÈó Çáúåõæäö ÈöãóÇ ßõäÊõãú ÊóÞõæáõæäó Úóáóì Çááøåö ÛóíúÑó ÇáúÍóÞøö æóßõäÊõãú Úóäú ÂíóÇÊöåö ÊóÓúÊóßúÈöÑõæäó

"Na lau ungeliwaona madhaalimu wanavyokuwa katika mahangaiko ya mauti, na Malaika wamewanyooshea mikono wakiwambia: Zitoeni roho zenu! Leo mtalipwa adhabu ya fedheha kwa sababu ya mliyokuwa mkiyasema juu ya Mwenyezi Mungu yasiyo ya haki, na mlivyokuwa mkizifanyia kiburi Ishara Zake."

Al-An’aam – 93

 

Katika mlango huu zipo Hadiyth nyingi zilizo sahihi, na kila Muislamu anatakiwa aamini yote yaliyomo ndani ya Qur-aan na ndani ya Sunnah (Mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) yanayohusu mambo ya ghaibu na wala asiyakatae kwa sababu hayalingani na mambo yanayotendeka duniani, kwani ya Akhera hayakisiwi na haya ya duniani kutokana na hitilafu kubwa sana iliyopo baina ya mawili hayo – WaLlaahu l Musta’aan.

 

Rudi juu

Qadar

Tunaamini juu ya Qadar (kudra – majaliwa - yale yaliyokwisha andikwa) kheri yake na shari yake kuwa yote yamekwisha andikwa na yote yanatokana na Mwenyezi Mungu na kwamba kisha waqadiria waja wake kwa elimu yake iliyokienea kila kitu.

Na Qadar imegawika sehemu nne.

 

1.  Ujuzi:   Tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu ni Ujuzi wa kila kitu, Anajua kilichotokea na kitakachotokea na namna inavyotokea, na hii inatokana na elimu yake isiyo na mwanzo wala mwisho ilichokienea kila kitu. Hakitokei kipya ikawa Mwenyezi Mungu Hakuwa na elimu nacho, na tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu hasahau.

 

2.  Maandishi:  Tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Ameandika katika ubao wa Lawh al-Mahfuudh yote yaliyotokea na yatakayotokea mpaka siku ya Qiyaamah.

 

    Mwenyezi Mungu Anasema:

 

Ãóáóãú ÊóÚúáóãú Ãóäøó Çááøóåó íóÚúáóãõ ãóÇ Ýöí ÇáÓøóãóÇÁ æóÇáÇóÑúÖö Åöäøó Ðóáößó Ýöí ßöÊóÇÈò Åöäøó Ðóáößó Úóáóì Çááøóåö íóÓöíÑñ

"Je! Hujui kwamba Mwenyezi Mungu Anayajua yaliyomo mbinguni na katika ardhi? Hakika hayo yamo Kitabuni. Hakika (kuyadhibiti) hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi."

Al-Hajj – 70

 

3.  Kutaka:       Tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Ametaka kiwepo kila kilicho mbinguni na ardhini, kwani hakiwezi kuwepo kitu chochote bila Yeye kutaka kiwepo. Anachokitaka kinakuwa na Asichokitaka hakiwi.

 

4.  Kuumba:  Tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Aliyeumba kila kitu.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áóåõ ãóÞóÇáöíÏõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃÑúÖö æóÇáøóÐöíäó ßóÝóÑõæÇ ÈöÂíóÇÊö Çááøóåö ÃõæúáóÆößó åõãõ ÇáúÎóÇÓöÑõæäó

"Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wa kila kitu, na Yeye ndiye Mlinzi juu ya kila kitu. Yeye Anazo funguo za mbingu na ardhi."

Az-Zumar – 63

 

Rudi juu

Kutaka kwa Mwenyezi Mungu

Na sehemu hii ya tatu imekusanya kutaka kwa Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta’ala na kutaka kwa viumbe Vyake, kwa sababu Mwenyezi Mungu Anakijuwa kila kinachotendwa na waja Wake, na kwamba Yeye mwenyewe Ametaka kiwepo, ama sivyo kisingewezekana kutendeka.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áöãóä ÔóÇÁ ãöäßõãú Ãóä íóÓúÊóÞöíãó. æóãóÇ ÊóÔóÇÄõæäó ÅöáÇ Ãóä íóÔóÇÁ Çááøóåõ ÑóÈøõ ÇáúÚóÇáóãöíäó

"Kwa yule miongoni mwenu anayetaka kwenda sawa. Wala nyinyi hamtataka isipokuwa Atake Mwenyezi Mungu Mola wa walimwengu wote."

At-Takwiyr – 28 – 29

 

Na Akasema:

 

æóáóæú ÔóÇÁ Çááøåõ ãóÇ ÇÞúÊóÊóáõæÇú æóáóÜßöäøó Çááøåó íóÝúÚóáõ ãóÇ íõÑöíÏõ

"Na lau kuwa Mwenyezi Mungu Alipenda wasingelipigana. Lakini Mwenyezi Mungu Hutenda atakavyo."

Al Baqarah – 253

 

Na Akasema:

 

æóáóæú ÔóÇÁ ÑóÈøõßó ãóÇ ÝóÚóáõæåõ ÝóÐóÑúåõãú æóãóÇ íóÝúÊóÑõæäó

"Na lau kuwa Mwenyezi Mungu Angelipenda wasingefanya hayo. Basi waache na hayo wanayoyazua."

Al-An’aam – 112

 

Lakini juu ya yote hayo, tunaamini pia kuwa Mwenyezi Mungu Amempa mwanaadamu uhuru wa kuamua na Akampa uwezo wa kutenda. Na ufuatao ni ushahidi kuwa mwanaadamu amepewa uwezo huo.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÝóÃúÊõæÇú ÍóÑúËóßõãú Ãóäøóì ÔöÆúÊõãú

"Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo.'

Al-Baqarah – 223

 

Na Akasema:

æóáóæú ÃóÑóÇÏõæÇú ÇáúÎõÑõæÌó áÃóÚóÏøõæÇú áóåõ ÚõÏøóÉð

"Na ingelikuwa kweli walitaka kutoka bila ya shaka wangelijiandalia maandalio."

At-Tawbah – 46

 

Kwa hivyo Mwenyezi Mungu Amempa mwanaadamu uwezo wa kutaka, kuamua na wa kwenda atakapo na kujiandalia atakavyo.

 

Pili, kule kuamrishwa kufanya mema na kukatazwa kufanya mabaya ni dalili kuwa mwanaadamu anao uwezo wa kufanya atakalo, maana kama asingekuwa na uwezo huo kule kukatazwa na kuamrishwa kusingekuwa na maana yoyote.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

áÇó íõßóáøöÝõ Çááøåõ äóÝúÓðÇ ÅöáÇøó æõÓúÚóåóÇ

"Mwenyezi Mungu Haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri iwezavyo."

Al-Baqarah - 286

 

Tatu, Mwenyezi Mungu Anamsifia Atendaye mema kwa wema wake, na Anamlaumu atendaye ovu kwa ovu lake. Mwanaadamu asingekuwa na uwezo wa kutenda atakalo basi pasingekuwa na haja ya kumsifia mwema wala kumlaumu muovu kwa sababu huko ni kumpa mtu sifa asiyoistahiki.

 

Nne, Mwenyezi Mungu Ameleta Mitume.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

 

ÑøõÓõáÇð ãøõÈóÔøöÑöíäó æóãõäÐöÑöíäó áöÆóáÇøó íóßõæäó áöáäøóÇÓö Úóáóì Çááøåö ÍõÌøóÉñ ÈóÚúÏó ÇáÑøõÓõáö

"Mitume hao ni wabashiri na waonyaji, ili watu wasiwe na hoja juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kuletewa Mitume."

An-Nisaa – 165

 

Yangelikuwa matendo ya watu hayafanyiki kwa uwezo wao na uchaguzi wao, hoja yao isingebatilika kwa kuletewa Mitume.

 

Tano, kila mtu anapotenda jambo huhisi kuwa ametenda au ameacha kutenda. Utamuona anaposimama, anapokaa, anapoingia, anapotoka, anaposafiri, anapolala. Anapotenda lolote katika haya hufanya kama anavyotaka na wala hahisi kama yupo yeyote anayemlazimisha kufanya hayo, bali anaiona tofauti iliyopo anapofanya jambo kwa hiari yake mwenywe na anapolazimishwa, na hata shari’ah inatofautisha pale mtu anapofanya jamb