Harun Al Rashid
Juu ya kuwa Harun al Rashid
alikuwa Khalifa wa dola ya Abbasiya aliyepigana jihadi mara nyingi zaidi
kupita makhalifa wote wa utawala wa bani Abbas, akateka miji mingi zaidi
kuliko makhalifa wote wa kabila lake, akajishughulisha zaidi na elimu pamoja
na kuwaheshimu maulamaa kupita makhalifa wote wa dola hiyo, hata hivyo huyu ni
Khalifa aliyezuliwa uongo mwingi kupita makhalifa wote wa Kiislamu.
Wamemzulia kuwa eti alikuwa
akijishughulisha na wanawake na ulevi, wakamtungia
visa vingi visivyosadikika isipokuwa tu kwa wale wenye maradhi ya kusadiki
kila wanachokisoma.
Katika waandishi waliompa sifa
zinazomsitahikia Khalifa huyu ni Ahmed bin Khalkan
aliyeandika yafuatayo ndani ya kitabu chake 'Wafiyat al Aayan'. Aliandika:
"Harun al
Rashid alikuwa miongoni mwa makhalifa wenye sifa njema, wanaoheshimika, mwingi
wa kusali na kuhiji na kupigana jihadi na kuteka.
Alikuwa shujaa na mwenye rai yenye kusibu."
Sifa zake njema nyingi juu ya
kupenda kwake kuinusuru haki na kuwaheshimu
maulamaa na kusikiliza na kufuata nasaha zao zimeandikwa ndani ya vitabu mbali
mbali vya historia, na hayakanushi haya isipokuwa tu mwenye kupenda kusoma
maneno yaliyobadilishwa na kugeuzwa kwa ajili ya matamanio ya nafsi.
Jina lake ni Abu Jaafar – Harun
al Rashid bin al Mahdi Muhammad al Mansur Abu Jaafar Abdullah bin Muhammad bin
Ali bin Abdullah bin Abbas Al Hashimy Al Abbasiy.
Alizaliwa katika mji wa al Riy
katika mwaka wa 148 Hijri na wakati huo baba yake ndiye aliyekuwa gavana wa
mji huo pamoja na mji wa Khurasan, na mama yake alikuwa akiitwa Um Khaizaran
ambaye pia ni mama wa Al Hadiy, kaka yake Harun al Rashid.
Harun al Rashid alikuwa bado
mtoto mdogo alipochukuliwa na baba yake ambaye
wakati huo alikuwa mkuu wa jeshi lililofanikiwa kulishinda
jeshi
la Roma.
Harun al Rashid alipewa ukhalifa
baada ya kufariki ndugu yake Al Hadiy usiku wa
Jumamosi tarehe 16 Rabiul Awwal mwaka wa 170 Hijri kama alivyousia baba
Ndani ya usiku huo huo Mwenyezi
Mungu alimruzuku Harun al Rashid mtoto wa kiume
aliyepewa jina la Abdullah al Maamun, na haijapata kutokea siku katika
historia ya Kiislamu ambayo ndani yake siku hiyo hiyo alifariki Khalifa
akatawazwa Khalifa na akazaliwa Khalifa.
Harun al Rashid alikuwa mfasihi
wa lugha, mwenye elimu na hekima nyingi katika
mambo yanayohusu uendeshaji wa nchi, na alikuwa mwingi wa kusali na mwingi wa
kutoa sadaka.
Alikuwa akipenda watungaji
mashairi na alikuwa akiwalipa vizuri, na alikuwa akipenda kucheza mpira,
kurusha mikuki na kupanda farasi na kucheza mchezo wa sataranji 'chess', na
inajulikana kuwa yeye ni khalifa wa mwanzo wa Bani Abbas kuucheza mchezo huo.
Harun al Rashid alikuwa
akiwapenda
Anasema al Qadhi al Fadhl;
"Sijapata kusikia juu ya Khalifa
aliyesafiri kwa ajili ya kutafuta elimu isipokuwa Harun al Rashid aliyesafiri
pamoja na wanawe wawili al Amin na Al Maamun mpaka Madina kwa Imam Malik (Mwenyezi
Mungu amrehemu) kwa ajili ya kusikiliza sharhi yake ya kitabu cha Al Muwatta"..
Alihuzunika
"Kila ninapomtaja Mtume
wa Mwenyezi Mungu (SAW) mbele ya Harun al Rashid
humsikia akimsalia akisema 'Allahumma salliy alaa sayidiy', na siku ile
nilipomsomea hadithi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) inayosema; 'Natamani
nipigane vita katika njia ya Mwenyezi Mungu, kisha niuliwe kisha nihuishwe
tena ili nipigane tena na niuliwe tena', Harun al Rashid alilia kwa huzuni
"Siku moja baada ya kumaliza
kula", anaendelea kusema Abu Muawiya (Kipofu), "mtu mmoja alikimbilia
kunimiminia maji kwa ajili ya kuosha mikono yangu
huku akiniuliza; "Unajuwa nani anakumiminia maji? Ni Mimi Harun al Rashid,
kwa kwa ajili ya kuiheshimu elimu yako."
Anasema Mansur bin Ammar; "Sijapa
kuona mtu anayelia
Na siku ile
Al Fudhali bin Iyadh alipomwambia Harun al Rashid; 'Wewe ndiye mbebaji jukumu
la umma huu." Harun
alilia
Imenukuliwa kutoka kwa Imam al
Qurtuby katika tafsiri yake kuwa mwanamke wa kiyahudi aliyekuwa na shida
alijaribu mara nyingi sana kutaka ruhusa ya kuingia
katika kasri ya Khalifa Harun al Rashid apate kumuelezea shida
zake, lakini walinzi hawakumruhusu kuingia, na siku moja akabahatika kumuona
Haruna al Rashid akitoka akiwa juu ya farasi, akamsogelea na kumwambia; "Muogope
Mwenyezi Mungu ewe Harun al Rashid!"
Kusikia maneno hayo Harun al
Rashid akateremka moja kwa moja kutoka juu ya
farasi wake na kusujudu, kisha akaamrisha mwanamke huyo akidhiwe haja zake
zote.
Watu wakamuuliza;
"Ewe Amiri
wa Waislamu, umeteremka kutoka juu ya farasi wako kwa ajili ya maneno
ya mwanamke wa kiyahudi?"
Harun akasema;
"Sivyo, bali
nimeteremka nilipoikumbuka kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo; 'Na wanapoambiwa.
"Mcheni Mwenyezi Mungu," mori wao huwapeleka zaidi kwenda kufanya madhambi
hayo. Basi Jahannam inawatosha (kuwatia adabu).
Al Baqarah – 206
Imepokelewa kuwa siku moja Ibni
Sammak alipokuwa akimimina maji katika gilasi ya Harun al Rashid akamuuliza;
"Ewe Khalifa
wa Waislamu!
Iwapo duniani hapana maji mengine isipokuwa haya utakuwa
tayari kuyanunua kwa kiasi gani?"
Harun al Rashid akasema;
"Nusu ya
Akamwambia;
"Kunywa
Mwenyezi Mungu akubariki nayo."
Na alipomaliza kunywa akamuuliza:
"Ikiwa maji
haya uliyokunywa yatazuilikia tumboni mwako yasiweze kutoka utakuwa tayari
kutoa kiasi gani ili yatolewe?"
Akasema;
"Ufalme
wangu wote."
Akamwambia;
"Ufalme
thamani yake maji na mkojo sina haja nao."
Harun al Rashid akalia
Anasema Ibni l Jawzi;
"Siku moja
Harun al Rashid alimwambia Sheiban; 'Niwaidhi.'
Sheiban akamwambia;
'Upae sahibu
mwenye kukutisha ukasalimika ni bora kuliko kuwa na sahibu mwenye kukusifia
akakutia mashakani.'
Haruna al Rashid akamwambia;
"Nishereheshee."
Akamwambia;
"Mwenye kukuambia; Wewe ndiye
mbebaji jukumu la raia hawa kwa hivyo muogope
Mwenyezi Mungu ni bora kwako kuliko mwenye kukuambia; Nyinyi watu wa Ahlul
Bayt mumekwisha samehewa madhambi yenu na kwamba nyinyi ndiyo wenye haki ya
kutawala."
Harun akalia
kwa furaha.
Katika mwaka wa mia na themanini
na saba ilimfikia Harun al Rashid barua kutoka kwa mfalme wa Waroma Naghfur
ikivunja mkataba na ahadi waliyokubaliana baina ya Harun al Rashid na mfalme
wa Roma mwanamke aitwae Rene aliyetawala kabla yake.
Barua hiyo iliandikwa ifuatavyo;
"Kutoka kwa
Naghfur mfalme wa Roma kumfikia Harun al Rashid mfalme wa Waarabu.
Amma baad, kwa hakika mfalme aliyetawala kabla yangu
alikuwa akikupa wewe
Uso
wa Harun al Rashid ulibadilika kwa ghadhabu baada ya kuisoma barua hiyo hata
waliokuwa pamoja naye katika majlis ile walianza kutawanyika kwa hofu, baada
ya kumuona Harun al Rashid akiinuka, na kumwita waziri wake huku akimuambia:
"Lete kidawati cha uwino na
kalamu kisha andika yafuatayo;
"Bismillahi Rahmani Rahiym,
kutoka kwa Harun al Rashid Khalifa wa Waislamu,
imfikie Naghfur Mbwa wa Roma! Nimeisoma barua yako
ewe mwana wa kikafiri na jawabu utaiona na wala hutoisikia."
Harun al Rashid akatayarisha
jeshi kubwa na kuondoka nalo mpaka alipoufikia mji wa Heracles na
kuuteka , kisha akamlazimisha Naghfur atie sahihi
ya kulipa fidia kila mwaka.
Imepokelewa kutoka
kwa Al Sauly kutoka kwa Yakub bin Jaafar kuwa
katika mwaka alotawazwa Harun al Rashid alimuota Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW)
akimwambia;
"Mambo yatakuendea vizuri, kwa
hivyo teka miji, nenda kahiji na uwagawie
Harun al Rashid akafanya kama
alivyoambiwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW), akaifunga safari katika mwezi
wa Shaabani mwaka wa mwanzo wa ukhalifa wake, akateka miji mingi ya Roma kisha
akaelekea moja kwa moja mpaka Makka kwa ajili ya kuhiji, kisha akenda Madina,
na kote huko aligawa mali nyingi sana kwa wote wanaostahiki
Amehiji mara nyingi
na ameteka miji mingi ya makafiri.
Anasema Al Masuudiy katika
kitabu chake 'Muruuj al Dhahab':
"Harun al Rashid alikuwa
na nia ya kuendelea kuteka na kuifanya dola ya
Kiislamu kuwa kubwa kuanzia bahari ya Roma hadi bahari ya Qalzam."
Katika mwaka
wa 175Hijri alimchaguwa Al Ghatrif bin Ataa kuwa gavana wa Khurasan na
akamchaguwa Jaafar Barmaki kuwa gavana wa Misri, na katika mwaka huo
vilishtadi vita baina ya makabila ya Al Qisiya na Al Yamaniya katika nchi ya
Sham na chuki baina
Majeshi ya Harun al Rashid
yakiongozwa na Yahya al Barmaki yalifanikiwa
kuiteka miji ya Qazwin na miji iliyo karibu na nchi ya Urusi.
Katika Ramadhani ya mwaka 179 H.
Harun al Rashid alifanya Umra na akabaki Makka
mpaka musimu wa Hijja, akahiji akitembea kwa miguu kutoka Makka mpaka Arafat
na Muzdalifa na Mina nk.
Kutoka hapo akaingia vitani tena
na kufanikiwa kuiteka miji mingine ya Roma, akauteka mji wa Safsaf na Ankara,
kisha mwaka uliofuata akahiji tena akifuatana na wanawe wawili Al Amin na Al
Maaamun, na baada ya hapo Jaafar al Barmaki pamoja baba yake wakafanya khiana
juu ya kuwa Haruna al Rashid aliwaokowa walipotaka kuuliwa kisha akawapa vyeo
vikubwa katika ukhalifa wake, akahukumu Jaafar auliwe na baba yake atiwe jela.
Na katika mwaka huo huo majeshi
ya Harun al Rashid chini ya uongozi wa Abdul Rahman
bin Abdul Malik bin Saleh al Abbasi yaliuteka mji wa Dibsah.
Na katika Ramadhani ya mwaka 179
Harun al Rashid alifanya tena Umra na akabaki na
nguo zake za Ihram mpaka ulipoingia musimu wa Hija, akahiji tena kwa miguu
yake kutoka Makka hadi Arafat na kurudi tena Makka.
Harun al Rashid alifariki dunia
akiwa vitani katika mji wa Al Tuss uliopo Khurasan siku ya tarehe tatu mwezi
wa Jamadil Akhira mwaka wa 193H akiwa na umri wa miaka 45 na zipo riwaya
zinazosema kuwa alikuwa na umri wa miaka 48, akazikwa huko na kusaliwa na
mwanawe Al Saleh.