FUNGA YA SITA
Muhammad Faraj
Shukrani zote
ni zake Mwenyezi Mungu. Tunashuhudia ya kwamba
hapana mola anaepaswa kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu,
na kwamba Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam) ni Mtume wake. Ameufikisha ujumbe
na kuituwa amana, kwa hivyo tunakuomba Mola wetu
umsalie na kumsalimu Mtume wako huyu mtukufu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) pamoja na Ali yake na
Masahaba Wake Watukufu - Aamin.
Amma baad,
Saumu
ni
Ibada ambayo nguzo
zake ni mbili;
Ya
Ya Pili
ni ‘Kujizuwia na kila kinachofungulisha kuanzia
inapoingia Alfajiri mpaka linapozama jua.’
Baadhi
Ya
Hadithi Zinazozungumzia Juu Ya
1.
Katika
hadithi Al Qudsy, Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) anasema;
"Mwenyezi Mungu anasema, 'Ibada za mwanadamu zote
ni zake isipokuwa Saumu, hiyo ni Yangu, na Mimi ndiye ninaetoa jazaa yake…(Malipo
yake)'
Imam Ahmed na
Muslim na Annasai
2.
Anasema Abi
Amama (Radhiya Llahu anhu)
“Nilimwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) nikamwambia, 'Niamrishe juu ya Ibada itakayoniingiza Peponi'.
Akanambia; 'Pendelea kufunga, kwa sababu (Ibada)
hiyo haina mfano. Nilipomwendea mara ya pili, akanambia;
‘Endelea kufunga".
Ahmad ,
Annasai na Al Hakim .
3.
Kutoka kwa
Abi Saeed Al Khodary (Radhiya Llahu anhu)
anasema kwamba Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
"Mja anapofunga siku moja katika njia ya Mwenyezi Mungu (kwa ajili ya
kutaka radhi za Mwenyezi Mungu), basi Mwenyezi Mungu
anamuepusha na Moto wa
Jahannam umbali wa Miaka Sabini"
Maimam wote wa
Hadithi isipokuwa Abu Daood.
4.
Imepokelewa
kutoka kwa Sahal bin Saeed (Radhiya Llahu anhu) kwamba Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) amesema;
,"Hakika Pepo ina
mlango uitwao Ar Rayaan. Siku ya Kiama patasemwa; "Wako wapi wafungaji?"
Wakeshaingia wafungaji wote (kupitia mlango huo), mlango
utafungwa".
Bukhari na Muslim.
Sheikh Shaarawi
(Mwenyezi Mungu amrehemu) alitoa mfano wa mtu
anayependa kujikurubisha kwa Mola wake kwa kupiga mfano wa baba mwenye watoto
wawili. Mmoja kati
Anasema Sheikh
Shaarawi;
"Bila shaka baba atampenda yule mtoto anayependa kujikurubisha
kwake.
Mfano huu ni mfano wa mtu mzito wa kutimiza Ibada
zake za Fardhi. Bila shaka huyu ni bora kuliko yule
asiyetimiza Ibada zake kabisa. Lakini yupo mwingine anayetimiza Ibada
alizofaridhishiwa kisha huongeza kwa kufanya Ibada
nyingine za Sunna.
Bila shaka huyu
wa pili
atapendwa
zaidi
na Mola
wake.”
(Mwisho
wa maneno ya Sheikh Shaarawi)
Na hii
ni tafsiri ya hadithi ya Al Qudsy ambayo ndani yake
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) anasema;
"Mwenyezi Mungu
anasema;
“Atakayemfanyia uadui kipenzi changu nitamtangazia vita.
Na mja wangu hajisogezi kwangu kwa jambo
ninalolipenda kuliko lile nililomfaridhishia. Na mja wangu huwa anaendelea
kujisogeza kwangu kwa Ibada za Sunna, mpaka Nimpende, na Nitakapompenda, basi
Mimi Nitakuwa ndiyo masikio yake anayosikilizia (Hatopenda kusikiliza
isipokuwa Ninayoyapenda) na macho yake anyoyaonea (Hatopenda kutizama
isipokuwa Ninayoyapenda) na mkono wake anaoutumia (Hatopenda kuutumilia
isipokuwa katika yale Ninayoyapenda) na miguu yake anayoiendea, (Hatopenda
kwenda isipokuwa katika yale Ninayoyapenda) na anaponiomba, Nitampa, na
anapotaka ulinzi wangu, Nitamlinda."
Bukhari.
Saumu
Ya
Siku Sita Katika Mwezi Wa Shawaal
Tukirudi katika
maudhui yetu ya Saumu ya Siku sita katika mwezi wa
Shawaal, anasema Sheikh Sayed Sabiq katika kitabu chake kiitwacho ‘Fiq -hi
Sunnah’ kwamba wamesimulia Maimam wote wa Hadithi isipokuwa Bukhari kuwa;
Ameelezea Abu Ayoub Al Ansari (Radhiya Llahu anhu) kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
"Atakeyefunga
Mwezi wa Ramadhani kisha akafuatilia (kufunga) siku
sita katika mwezi wa Shawaal, (anakuwa)
Na hii ni kwa
sababu mtu anapofunga mwezi mmoja wa Ramadhani, anapata thawabu ya kufunga
miezi kumi, kwa sababu mtu anapotenda jema moja hulipwa kumi badala yake. Na
anapofunga siku sita katika Shawwal, anakuwa mfano wa
aliyefunga siku sitini. Ukijumlisha funga ya Ramadhani na
funga ya sita, unapata miezi kumi na miwili, na kwa ajili hiyo anakuwa mfano
wa aliyefunga mwaka mzima. Na mtu anapoendelea hivyo
maisha yake yote anakuwa mfano wa
anayefunga maisha yake yote”.
NAMNA YA KUFUNGA
Imam Annawawi
ambae ni katika Maulamaa wakubwa wa madhehebu ya
Imam Shafi anasema;
"Ni vizuri
kufunga siku sita mfululizo mara tu baada ya kumalizika sikukuu ya mwanzo, na
atakayefunga siku sita mbali mbali katika mwezi wa Shawaal
, pia inakubaliwa”.
Amma
Imam Ahmed bin Hanbal anasema;
“Ukifunga mfululizo au ukizifunga siku sita tofauti katika mwezi
wa Shawaal yote ni sawa tu.”
Maulamaa wanasema kuwa;
‘Lazima mtu atimize Ramadhani yake
kwanza, ndiyo aweze kufunga sita. Yaani ikiwa mtu anadaiwa
katika Ramadhani, basi lazima alipe kwanza deni
Na hii
ni tafsiri ya kauli ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) aliposema;
“ATAKAYEFUNGA Mwezi wa Ramadhani KISHA akafuatilia (kufunga) siku sita…”
Wakasema kuwa kutokana na
kauli hii, Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) hapa anasisitiza kuwa mtu lazima kwanza afunge Mwezi wa
Ramadhani, KISHA afunge sita. Na ikiwa mtu ana deni la kufunga, basi huyo
anakuwa hakufunga mwezi wa Ramadhani, na kwa ajili
hiyo ikiwa anazitaka thawabu zilizotajwa katika hadithi hiyo, basi inampasa
kulipa deni lake kwanza, kisha ndiyo afunge sita.
Wallahu taala aalam
Wassalaam alaykum wa
Rahmatullahi wa Barakatuh