FUNGA/ SAUMU
Na Hamzah Z. Rijaal
Wengi
wetu wanajiuliza kawanini tunafunga? Wengine hufika hadi ya kusema kuwa
Baada
ya Ramadhani kuna funga nyenginezo amabazo mtu akifunga hupata jazaa kubwa kwa
Mola wake.
“Enyi
mloamini! Mmelazimishwa kufunga (saumu)
(Al-
Baqarah 2:183).
Kuna
hadithi vile vile ya Bwana Mtume isemayo “Fungeni mtapata siha”
“Yule
ambaye hatakuwa tayari kuwacha kusema uwongo, Allah hatompa kitu, na kukaa
kwake na njaa na kiu huwa ni bure.’
Vile
vile Bwana Mtume ameeleza kuwa:
“Kuna
wengi hukaa na njaa na kutokunywa vinywaji huwa hawana funga sawa na wale ambao
husali usiku kucha bila ya kupata chochote kile ila kukaa bila ya usingizi”
Funga
ina mambo mengi na katika makala haya nitazungumzia mambo hayo kwa mukhtasar.
Wataalamu
wa sayansi hutuelezea kuwa mtu anapotia chakula kinywani na kufikia hatua ya
mwisho (mouth to the end of large intestine /clon) huchukua masaa 14, na nchi
nyingi saumu huwa baina ya masaa 14, hiyo ni kusema mashine ya tumbo husita na
kupumzishwa sawa na wenye vyombo vya moto pale wanaposema kuwa wanapeleka
chombo chake ‘service’.
Masaa
14 bila ya kula katika mwezi nisawa na masaa 420 mashine yako ya kufanya kazi
ya kusagia chakula huwa imesita, hizo ni sawa na siku 17.5 yaani siku 18 umekaa
mashine yako haifanyi kazi ni faida kubwa sana ambayo hivi sasa watalamu
wamaekuja kutambua na kutibu baadhi ya maradhi kuwataka wawele wawe hawali
sana.
Wapingao
saumu husema kuwa waislamu wanajiumiza na kupoteza nguvu nyingi wakati
wanapofunga na kupoteza sukari kiwiliwilini mwao ‘hypoglycemia’ na kuhatarisha
maisha
Katika
Ramadhani au katika funga hutakiwa tujitahidi na viungo vyetu kwa mfano:
Ulimi:
Tujiepushe
kusema uwongo, kusengenya, kuchongea, kutukana, kutongoza na yale yote
yatakupelekea wewe kusema na kuiharibu saumu yako. Ulimi ndio nguvu kuu ya
ushetani wa kila aina.
Mkono:
Mkono
nao unachangia mengi, kudhulumu
Miguu:
Miguu
ndio tunayoiringia kwenda kila tunakokutaka, ndani ya funga mtu ajilinde zaidi
na miguu yake. Mtu awe anakwenda msikitini kwa darsa, kwa kusali na kwenda
kusoma Quran.
Macho:
Macho
ndio yenye kutizama na kutoa maamuzi ya kila kitu, kwenda kuiba, kumfwata
mwanamke kwa njia za shari, n.k.
Funga
inatupa fursa na kuwa ni chuo kinachomtengeneza mtu kuweza kuwa mtu mwema na
kuweza kubaki na taratibu za uwema kwa mwaka mzima. Kinyume chetu ni kuwa mwezi
ukiandama huwa ndio mfungwa kafunguliwa na kuanza uafriti wa kila aina, Disco,
ulevi, vimwana, na kila aina ya ufirauni na upashkuki.
Faida za kufunga katika nyanja za kiafya na sayansi
Sayansi
ilivyokuwa ni elimu ya mwanadamu, kwa hivyo siku zote haiko thabiti na
inabadilika pale uvumbuzi mwipya unapotolewa. Wengi husema kuwa Saumu humuumiza
mwenye kufunga na huumia
Nini
watalamu wa Tiba walichokiona?
v
Kile kinachofanya damu ‘haematology or
serum’ haibadiliki wala haiathiriki kwa funga
v
“Metabolic rate” haibadiliki, yaani
harakati mbali mbali za kutengeneza mwili nazo haziathiriki
v
Uzito nao wa mtu haubadiliki na kuna
wengi katika Ramadhani huongezeka uzito kutokana na maanjumati na jazba za kula
v
Nnitrogin ipatikanayo kwenye mkojo huwa
ni ya kawaida ‘blood urea nitrogen is normal’
v
Sukari ndani ya kiwiliwili hubakia 80
mgms %
Funga na madini ya Magnesium
Madini
ya magnesium husaidia katika kuulinda moyo.
Kwenye
saumu magnesium hutoka kidogo, na mtu akipatwa na mshtuko wa moyo husaidiwa kwa
magnesium.
Magnesium
hutumika katika ‘mitochondria’ nyezo moja ya “cell” ambayo ndio ipayo nguvu chembe za uhai, na
mtu akifunga, magnesium hufanya kazi vizuri, mishipa ya damu huchakaa lakini
magnesium husaidia pakubwa kuweka sawa mambo.
Funga na malaji madogo au machache
Imeonekana
kuwa wanyama walishwao kidogo bila kuvimbiana huishi
Watu
wauguwao maradhi
Bwana
Mtume Muhammad S.A.W hajawahi kula akashiba na kuvimbiwa.
Bwana
Mtume amesisitiza kuwa tule kwa kiasi. Amefika kusema;
"Sahani
moja ailayo mtu mmoja inatosha kushibisha watu wawili’, na aliwahi kuulizwa
Bwana Mtume kuwa kwanini kabila fulani inaishi umri mrefu? Alijibu;
"Watu
wa kabila lile huwa hawali ila wanapokuwa na njaa na wanapokula wanapoanza
kukaribia kushiba humaliza kula.”
Bwana
Mtume alikuwa akila futari nyepesi na akila daku jepesi kinyume na wengi wa
watu ambao hula useme kesho ndio
watakufa.
Funga
inasaidia mengi mfano wa akili kuwa madhubuti ingawa wengi wakifunga huwa
dhaifu kwa kujiregeza wenyewe.
Funga nyenginezo zisokuwa Ramadhani na Sunnah Kufunga
1.
Funga ya siku 6 baada ya Ramadhani, yaani sitatul shawal.
Funga
hii ina faida kubwa, Bwana Mtume anatuambia;
“Mwenye
kufunga Ramadhani kisha akaifuatilia kwa kufunga siku 6 za mfungo mosi sawa na
mtu aliyofuga mwaka mzima."
Wewe
mwenzangu umezungukwa na mambo ya uchafu wa kila aina, hiyo ni fursa kubwa
kwako kujiweka katika njia ya kuipata Pepo.
2.Funga ya Ashura ya mfungo 4
Funga
hii Bwana Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) ametusisitiza tuifunge na iwe siku mbili badala ya siku tarehe
9, iwe 9 na 10, au 10 na 11, ili isiwe
3.Funga
ya Arafa katika mfungo tatu, mwezi tisa
4.Funga
ya Ijumatatu na Alkhamisi, Siku aliyozaliwa Mtume
5.”Ayam
Bidh” Masiku Meupe tarehe 13, 14, 15
6.”Ayam
Sud” Masiku Meusi 27, 28, 29
7.Shaaban
8.Rajab
9.Ashhurul
Hurum - Dhulkaad, Dhul Hijja, Muharam na Rajab
10.Sunatil
Daud (kufunga siku moja na kula siku moja)
11.Siku
tatu zozote zile katika kila mwezi.
Tujitahidi
baada ya mafunzo haya ya mwezi wa Ramadhani kuweza kustahmili na kufunga, na
pia tujitahidi miezi ifwatayo nayo tuwe tunafunga.
Tusiwache
kufunga kutokana na fadhila zake, pamoja na kuwa na afya nzuri.