Zakat ul-Fitr
Na: Qur'an wa Sunnah Society
Imefasiriwa Na Abufarida Muhammad A.
Basawad
UFAFANUZI:
Maana ya Zakat-ul-Fitr au Sadaqat-ul-Fitr
ni "Sadaqa ya utakaso wa kufungua Saumu. Nacho ni kiwango fulani cha chakula kinachotolewa na waislamu
katika siku chache za mwisho wa Ramadhan au siku ya 'Idd asubuhi, kabla ya
kuswaliwa Swala ya 'Idd.
HEKIMA:
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) ametuamrisha
kutoa zakat-ul-fitr kwa sababu mbili:
a. Kuwatakasa wale waliofunga, kuzisafisha saumu zao kutokamana na mambo
ya upuzi,
b. Kuwalisha waislamu masikini ili nao wawe na
chakula cha kuwatosha siku ya 'Idd.
Ibn 'Abbas (Radhiya Llahu anhu) akasema: "Mtume
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) ametuamrisha kutoa Zakat-ul-Fitr ili mwenye kufunga ajitakase kutokamana na maneno
machafu au vitendo vibaya na pia kuwalisha wanaohitaji. Hukubaliwa kama Zaka
kwa yule atoae kabla ya swala ya 'Idd, lakini huwa ni sadaqa
HUKUMU YAKE:
Zakat-ul-fitr ni
Faradhi (wajib) kwa wale wenye uwezo wa kutoa. Imeelezwa hii waziwazi kwenye
Hadith ya Ibn 'Umar (Radhiya Llahu anhu): "Mtume
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) ameamrisha zakat-ul-fitr itolewe kwa kiwango cha Sa'[2] moja ya tende au Sa'
moja ya shayiri (Barley), kwa Waislamu (Mtumwa au alie huru mume au mke, mdogo
au mkubwa). Na akaamrisha itolewe kabla ya watu kwenda kuswali swala ya
'Idd".[3]
Hadithi hii inazidi kudhihirisha ya kwamba ni wajib juu ya kila muislamu
(mwenye uwezo) bila ya kujali umri wala hali ya kijamii.
Jukumu la kutoa zakat ul-fitr ni juu ya kiongozi wa
nyumba; inampasa kutoa kwa niaba yake mwenyewe na wale walio chini ya usimamizi
wake: wadogo kwa wakubwa, waume na wake, watumwa na waungwana. Ibn Umar (Radhiya Llahu anhu) akasema:
"Ameamrisha Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) sadaqat ul-fitr itolewe kwa walio chini ya
usimamizi wako: wadogo na wakubwa, waungwana na watumwa."[4]
Ama kwa yule asokuwa na uwezo wa kifedha, huyo amesamehewa kwa sababu ya Nas'
kutoka kwenye Qur'ani na Sunna,
Na Hadithi iliyopokewa na Abu Huraira: "Ninapowaamrisha kitu chochote,
fanyeni kadiri ya uwezo wenu."[6]
Baadhi ya wanavyuoni waonelea kuwa hata kijusu (mtoto kabla ya kuzaliwa) nae
alipiwe kwa niaba yake. Hata hivyo, hapana ushahidi wa
hayo; na huyo kijusu hachukuliwi kuwa ni kijana - si katika lugha wala kawaida
za watu.
AINA ZA
ZAKAT-UL-FITR
Alivyokuwa akifanya Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na Maswahaba zake ni kutoa zakat-ul-fitr kwa njia ya
chakula. Akapokea Abu Sa'id al-Khudri (r.a): "(Katika wakati wa Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) tulikuwa tukitoa zakat-ul-fitr
Imepatikana ikhtilafu baina ya wanavyuoni kuhusu neno "twa'am"
(chakula) lililotajwa kwenye riwaya iliyotangulia hapo juu. Vile vile ni rahisi kutambua yakuwa neno
"Sadaqa ya Ramadhan ni Sa' moja ya chakula, kwa hivyo yule atakaeleta
ngano, atakubaliwa nayo; kwa yule atakaeleta shayiri, atakubaliwa nayo; kwa
yule atakaeleta tende, atakubaliwa nayo; kwa yule atakaeleta nafaka (kama
ngano) atakubaliwa nayo; kwa yule atakaeleta zabibu kavu, atakubaliwa
nayo..."[8]
Hadithi hizo zilizopita zimezidi kudhihirisha yakuwa haifai mtu kutoa kwa njia
ya pesa; wala kutoa kwa kutumia aina nyengine ya chakula kama vile nyama au
mafuta, maadamu hilo ni jambo la ibada, ni lazima litekelezwe kulingana na
Sunna.
Hata hivyo, mtu anaweza kukadiria kiwango cha fedha cha gharama ya
KIWANGO:
Hadithi zilizotangulia zina ashiria
yakwamba kiwango cha zakat ul-fitr ni Sa' moja ya aina
mbali mbali ya chakula kinachoweza kupimika. Isipokuwa tu kwa jambo moja:
kuhusu ngano, Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) aliwaamrisha watu watoe 'madd' mbili, zilizo sawa
na nusu Sa'.[9] Na hivyo ndivyo alivyokuwa akifanya
Mu'awiyah (r.a) huko
Sa' ilikuwa ni kipimo kisichobadilika au sehemu ya
ndani ya chombo kilichowazi. Ilikuwa ikibadilika kulingana na
pahali, lakini Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akaisawazisha kwa kusema: "Uzani ni
kulingana an uzani wa Makkah; na vipimo ni kulingana na vipimo vya
Madinah."[10]
Kwa hivyo, kipimo nakikadiriwe kulingana na kipimo cha Sa' ya Madinah, ambacho
mpaka leo chapatikana. Walaakin kipimo hicho hakiwezi kufikiwa na watu
wengi.Kwa sababu hiyo, wanavyuoni wengi wamekadiria karibu kuwa sawa sawa na
miteko mine iliyojaa (kwa kushikanisha mikono miwili pamoja) ya mtu
wastani.[11]
Hii inathibitisha ya kwamba ni makosa kupima zakat ul-fitr kwa uzani, kwa
sababu uzani wa Sa' moja hubadilika kulingana na vitu tafauti. Hata hivyo,
iwapo uhusiano baina ya uzani wa kitu chochote na
kipimo kwenye chombo utathibitika, basi uzani wa Sa' moja wa kitu hicho unaweza
kutumika.
WAKATI WA KUTOA:
Ikazidi kupokewa yakuwa Ibn 'Umar (Radhiya Llahu anhu) alikuwa akitoa siku moja au mbili
kabla ya siku ya 'Idd.[12] Kutokamana na hayo
imepatikana misingi ya ushahidi wa kutoa kwa siku chache kabla ya 'Idd. Lakini ni makosa kutoa mapema mno katika mwezi wa Ramadhan. Na
kufanya hivyo itakuwa ni kwenda kinyume na hikima yake ya kuwa kafara ya
madhambi wakati wa mwezi (wa Ramadhan), na kuwalisha wanaohitaji siku ya 'Idd,
na zaidi itakuwa ni kwenda kinyume na walivyokuwa wakifanya Maswahaba na
Ma-Salaf (Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote).
Hata hivyo. Inaruhusiwa kuwapa mapema wale
wanaokusanya, ukiamini yakwamba hawatozifikisha kwa
wanaohitaji kabla ya mwisho wa mwezi (wa Ramadhan). Hivyo ndivyo ilivyokuwa ikifanywa
wakati wa maswahaba, ilipokuwa wakusanyaji wakimaliza kukusanya siku moja au
mbili kabla ya 'Idd.[13]
UKUSANYAJI:
Inaruhusiwa kuchagua watu kukusanya zakat-ul-fitr
miongoni mwao. Vile vile
inaruhusiwa kuwapa (hiyo zaka) hao wakusanyaji iwapo wanahitaji na wanastahiki. Ibn 'Umar (Radhiya Llahu anhu) alikuwa akifanya hivyo.[14]
Ikazidi kusisitizwa kumchagua mtu kulinda zakat-ul-fitr iliyokusanywa. Mtume
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) alimchagua Abu Hurairah (r.a) kwa kazi hii;
WANAOSTAHIKI
KUPEWA:
Zakat-ul-fitr inapasa kugawanyiwa masikini (wanaohitaji)
Nukta Ya Maelezo:
[1] Abu Dawud, an-Nasa'i na wengineo, imepewa hukmu ya hasan (al-Hilaali).
[2] Miteko mine, na kila mteko mmoja, ni kwa mikono
miwili kwa pamoja. Mikono ya mtu wa umri wastani.
Tazama chini kwa maelezo.
[3] Al-Bukhari na Muslim.
[4] Ad-Daraqutni na wengineo. Imepewa hukmu ya hasan kwa mkusanyiko wa riwaya.
[5] Al-Baqarah 2:286.
[6] Al-Bukhari na Muslim.
[7] Al-Bukhari.
[8] Ibn Khuzaymah kwa upokezi sahih (al-Hilaali).
[9] Amenukuu maneno hayo at-Tahawi; akapokea Sa'id Bin al-Musayyib na wengineo miongoni mwa ma-Taabi'in. Ikapewa hukmu kuwa ni riwaya nzuri ('Abdullah Bin Yusuf).
[10] Abu Dawud na wengineo kutoka kwa Ibn 'Umar, Sahih
(al-Hilaali).
[11] An-Nawawi katika al-Majmu' 6:69.
[12] Ibn Khuzaymah (al-Hilaali).
[13] Ibn Khuzaymah (al-Hilaali).
[14] Ibn Khuzaymah (al-Hilaali).
[15] Al-Bukhari.