FADHILA
ZA KUFUTARISHA
Sameer
Zulfikar
FADHILA ZA KUFUTARISHA.
Sahaba Zayd bin Khalid Al-Juhany
(Radhiya Llahu anhu) kuwa amemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) akisema;
“Mwenye kumfutarisha aliyefunga
atapata ujira
(Tirmidhy).
Pia imepokewa hadithi na Ibni Khuzayma
kutoka kwa sahaba Salman (Radhiya Llahu anhu), kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Mwenye kumfutarisha aliyefunga katika
mwezi wa ramadhani atasamehewa madhambi yake na ataepushwa na moto na atapata
ujira
Hizi hi hadithi maarufu zilizopokelewa
kuelezea fadhila za kufutarisha ingawa zipo nyengine lakini madhumuni yake huwa
ni moja hivyo tutosheke na hizi mbili.
Maana ya hadithi ni kwamba yoyote
atakayemfutarisha mtu aliyefunga sio kwa kujionyesha kuwa anatoa sadaka bali
anafanya hayo kwa kutaraji kupata thawabu kutoka kwa Aallah (Subhaanahu wa
Ta’ala), basi
atalipwa ujira ulio sawa na ujira wa yule aliyefunga, na jambo linalojulikana
kuwa aliyefunga ujira wake haujulikani na yeyote isipokuwa Aallah (Subhaanahu wa
Ta’ala), hayo
ni kutokanao na wingi wa fadhila zake, hapo hapo yule aliyefunga ana fungu lake
pale.
Tusije tukafanya mchezo katika ibada
kwa kusema kuwa nikimpa aliyefunga kokwa
ya tende afutarie nitakuwa ni sawa na aliyefunga basi hakutokuwa na haja ya
kufunga. Afahamu mtu huyo kuwa hajafahamu makusudio yake na atapata dhambi
nyingi kwa kuifanyia mchezo sheria ya Allah (Subhaanahu wa Ta’ala).
Ama wakati wa kufutari ni ule wakati
jua linapozama, au tuseme pale utapomsikia mwadhini wa magharibi, na wale ambao
vyote hivyo vinashindikana, juu
Kutoka kwa Abu Hurayra, amesema Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema;
“Hakika mja ampendaye Allah ni yule anayefutari mapema.”
Na maana ya kufutari mapema sio
kufutari kabla ya wakati, bali iwe mwanzo wa wakati baada ya kuingia kwake tu.
Lakini kuna watu wengi hukosa fadhila hizi za kufutari mapema na si kwa jengine
illa kutokujuwa umuhimu wa jambo lenyewe na utawaona wakisha maliza kusali
magharibi ndio hutafuta tende. Haya ni
makosa, nayo ni katika mambo yanayochukizwa katika funga na yule anayetaka
kumfuata Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) basi na afahamu kuwa alikuwa akifutari kwa tende kabla
ya kusali sala ya magharibi.
Kwa hivyo
Hali kadhalika katika mambo muhimu
yanayopaswa kufanyiwa kazi ni kuomba dua
wakati wakufutari na hii inatokana na maneno ya Mtume (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) ya kuwa dua
hupokelewa haraka wakati wakufutari, hivyo watu wasiwe wanazungumza mambo ya
kipuuzi wakati huu kwani wanajikosesha fadhila za bure ambazo hawawezi
kuzidiriki illa mwaka mara moja na unatakiwa useme;
“Ewe Mola hakika mimi nimefunga kwa
ajili yako na kutokana na riziki hii uliyonipa nafutari.” Kisha uombe maghfira.
Chakula gani aliyefunga anatakiwa
afutarie?
Ama chakula cha kufutaria na kiwe
chakula cha aina yeyote ile, la muhimu kiwe cha halali yaani kimechumwa kwa
njia za halali kuliwa, iwe kwa maji au vyakula vikavu, muhimu kiwe ni kitu chenye
kuliwa. Chakula hasa kinachopendezewa kwa kufungua kinywa ni tende na ukipata
zinazoitwa Rutab (nusu mbichi nusu mbivu) ni bora zaidi maana Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam)
ndizo alizozitumia, na kama huzipati basi ni tende za kawaida inatosha, na
ukizikosa hizo basi ufutarie kwa chakula cha sukari au maji lakini mwenye
kujitahidi kufungua kinywa kwa tende hupata daraja ya kwanza katika fadhila na
iwe kwa njia za witri (odd number) moja, tatu, tano, saba tisa, n.k yaani kwa
idadi isiyogawika kwa mbili.
Hivyo watu wasikimbilie kula
vyenginevyo wakaacha tende, kwani kuna hikma maalumu Mtume (Swallah Llahu alayhi
wa sallam) kuhimiza
kufungua kwa tende na itoshe kumfuata Mtume wako ambaye tumetakiwa matendo yetu
yaambatane na yale aliyoyatenda yeye.
Pia la muhimu kuzingatiwa ni kuwa mtu