AQIQAH
Shukrani zote ni zake Mwenyezi Mungu, na sala na salam
zimfikie Mtume wake Muhammad (SAW) pamoja na Aali zake na Sahaba zake wakarimu
(Radhiyallahu anhum).
Wa baad,
Aqiqah ni mbuzi anayechinjwa pale mtu anapopata mtoto, na
maulamaa wengi wanasema kuwa kitendo hicho ni Sunnah muakkadah (Sunnah
iliyotiliwa nguvu).
Imeelezwa na Imam Malik katika Muwatta'a kuwa Mtume wa
Mwenyezi Mungu (SAW) alisema;
"Aliyepata mtoto akataka kuchinja na achinje."
Na imepokelewa na maulamaa wa Ahlu ssunah kutoka kwa
Samarah (RA) kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amesema;
"Kila mtoto aliyezaliwa yupo rahani kwa mbuzi wake,
anachinjiwa siku ya saba kisha anakatwa nywele kisha inatolewa sadaka uzito wa
nywele zake kwa fedha au kilicho mfano wake."
Mtoto wa kiume anachinjiwa mbuzi wawili na wa kike mbuzi
mmoja, kama ilivyopokelewa na Attirmidhiy kutoka kwa mama wa Waislamu Bibi
Aisha (RA) kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) aliwaamrisha wachinje kwa ajili
ya mtoto wa kiume mbuzi wawili wasio na kilema na kwa ajili ya mtoto wa kike
mbuzi mmoja."
Ni Sunnah kuchinja siku ya saba tokea kuzaliwa mtoto.
Kutoka kwa Al Baihaqiy kutoka kwa Buraidah (RA) kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu
(SAW) alisema;
"Aqiqah huchinjwa siku ya saba."
Na
Aina ya Mbuzi;
Mbuzi wa aina yoyote anaweza kuchinjwa, sharti asiwe na
kilema, yaani asiwe kiguru wala kipofu wala aliyekatika pembe au sikio au
aliyevunjika sehemu yoyote ya mwili wake nk.
Isiuzwe nyama yake wala sufi yake wala ngozi yake wala
chochote katika mwili wake.
Nyama inaliwa na watu wa nyumba na kutolewa sadaka na
kugawiwa ndugu na jamaa na marafiki.
Imam Malik anaona kuwa si vizuri kupikwa nyama na kualikwa
watu kuja kuila, na pia anaona kuwa inajuzu kuvunjwa mafupa yake na kupikwa na
kuliwa
Ama ile
hadithi inayosema kuwa si vizuri kuvunja mifupa kwa ajili ya usalama wa mtoto
mchanga Imam watu wa madhehebu ya Imam Malik wanasema kuwa hadithi yake si
sahihi, na hadithi yenyewe inasema hivi;
"Amesema
Bibi Aisha (RA) kuwa Sunnah ni kuchinja mbuzi wawili wasio na kilema kwa ajili
ya mtoto wa kiume na mmoja kwa ajili ya mtoto wa kike, kisha ipikwe bila
kuvunjwa mafupa yake."
Na hadithi
hii imetolewa na Al Baihaqiy na Al Hakim na kusimuliwa na Ataa (RA).
Anasema Imam
Al Dhahabiy kuwa hadithi hii ni sahihi, lakini Imam Annawawiy katika Majmua
juzuu ya 8 hadithi nambari 407 anasema;
"Hadithi
hii haina nguvu na haiwezi kuwa dalili."
Al Albani
yeye anasema;
"Inavyoelekea
isnadi ya hadithi hii ni sahihi, isipokuwa kwangu mimi ina ila mbili;
Ya kwanza
kukatika kwa isnadi, na ya pili kuongezeka kwa maneno, kwani ile kauli isemayo;
"Ipikwe bila kuvunjwa mafupa", ni maneno ya Ataa (na si maneno ya
Mtume (SAW)."
Irwaa
lghaliyl takhrij ya hadithi za Subuli ssalaam (4\392-395).
Ama Imam Shafi
na Imam Ahmed, wao wanaona kuwa hapana ubaya kuvunja mafupa yake, kwani hapana
hadithi sahihi inayokataza, isipokuwa wao wanaona kuwa ni bora kutovunja