![]() |
Mapenzi ya Ahli Sunnah juu ya Ahlil Bayt
(Watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam) |
Mmoja katika wana falsafa wa zamani
alisema:
“Haki yote haiwezi kumilikiwa na upande
mmoja, wala makosa yote hayawezi kuwepo upande mwingine, bali kila upande
husibu sehemu yake. Mfano wa kundi la vipofu waliopelekwa mbele ya tembo wakatakiwa
wamguse mwili wake, kisha kila mmoja aelezee umbile lake.
Katika muda mfupi waliopewa, hapana
aliyewahi kukamilisha kuushika mwili wote. Kila mmoja alifanikiwa kugusa sehemu
tu.
Aliyeushika mkonga akidhani kuwa amemshika
tembo wote akasema: “Mwili wa tembo ni mrefu mfano wa gogo la mti”,
Aliyeshika mgongo akasema:
“Hapana, bali mwili wa tembo ni mfano wa
jabali dogo”,
Aliyeshika sikio akasema:
“Nilivyouona mimi mwili wa tembo ni mpana,
duara na laini”.
Kila mmoja anahadithia juu ya ile sehemu
aliyodiriki kuishika katika muda mfupi ule akidhani anatoa maelezo kamili. Wote
wamesema kweli, lakini kila mmoja amehadithia sehemu tu ya ukweli anoujua yeye akidhani kuwa ndio
ukweli wote.”
Hitilafu husababishwa na mambo mengi,
yakiwemo upeo wa kufahamu, kupenda, matamanio ya nafsi, mielekeo ya elimu, ya
kifikra, kuiga waliotangulia, kupenda umaarufu, kupenda ukubwa, hitilafu za
ustaarabu. Wengine huiga waliyowakuta nayo wazee wao, na wengine wanafuata
mafundisho ya walimu wao wanaowaamini n.k. Na wengine
huiendeleza hitilafu kwa sababu ya ubishi au kiburi tu, hata kama wataiona haki
mbele yao.
Si vibaya kuhitilafiana, kwa sababu Mwenyezi Mungu Ametuumba
kila mmoja na akili yake pamoja uwezo wake wa kufahamu.
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóáóæú
ÔóÇÁ ÑóÈøõßó áóÌóÚóáó ÇáäøóÇÓó ÃõãøóÉð æóÇÍöÏóÉð æóáÇó íóÒóÇáõæäó ãõÎúÊóáöÝöíäó .ÅöáÇøó
ãóä ÑøóÍöãó ÑóÈøõßó æóáöÐóáößó ÎóáóÞóåõãú.
«Na Mola wako Mlezi Angelipenda Angewafanya
watu wote wakawa umma mmoja. Lakini hawaachi kukhitalifiana, Isipokuwa
wale ambao Mola wako Mlezi Amewarehemu; na kwa hiyo ndio Mwenyezi Mungu
Amewaumba.»
Huud-118-119
Anasema
Al Hasan Al Basry: æóáöÐóáößó
ÎóáóÞóåõãú maana
yake ni kuwa; Amewaumba ili wakhitalifiane.
Wenye
kukhitilifiana wanaweza kusikilizana na kufahamiana ikiwa hapana chuki baina
yao, lakini chuki inapoingia, hayapatikani tena masikilizano wala kufahamiana.
Chuki inaondoa mapenzi na inavunja uhusiano mwema na inaendeleza bughudha na
kuondoa uwezekano wowote wa masikilizano.
Imepokelewa
kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) usiku mmoja
aliamka uso wake ukiwa mwekundu huku akisema:
áÇ Åöáåó ÅöáÇø Çááå¡ æóíúáñ ááÚóÑóÈö¡ ãöäú ÔóÑó
ÞóÏö ÇÞúÊóÑóÈ
Laa
ilaaha illa Llah, Ole wao Waarabu kwa shari iliyo karibu
Alirudia maneno
haya mara tatu.
Maulamaa
wanasema kuwa;‘Hii
ilikuwa ishara kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa
sallam) juu ya hitilafu itakayotokea baada yake’.
Hitilafu
iliyopo hivi sasa baina ya Shia na Sunni inakula kibichi na kikavu.
Mamia
ya Waislamu wanauliwa kila siku huko Iraq, na wanaendelea kuuliwa, na mamilioni
wengine wamejeruhiwa. Mamilioni
wamekwishaihama nchi yao, na mamilioni hawana kazi wala bazi.
Lebanon, nchi iliyojaa neema, nchi ya elimu
na ziraa. Nchi ya historia na sanaa, leo kila kitu kimesimama katika
nchi hii kwa sababu ya fitna ya umadhehebu. Nchi haina serikali, ina majeshi
mawili, kila moja linadai kuwa wao ndio wenye kuipenda nchi. Ina makundi
mawili, kila moja linalituhumu jingine kuwa ni vibaraka. Watu hawaelewi
wanapelekwa wapi, kila siku mapambano ya risasi na mabomu.
Huko Yemen, maelfu ya watu wamekwishapoteza
maisha yao katika mapambano baina ya majeshi ya serikali na makundi ya watu wa
kabila la Houthi wenye kufuata madhehebu ya
Shia Ishnaashariyah.
Hii ni fitna iliyopenyezwa katika mwili wa Waislamu kwa
ajili ya kuwagawa. Inatumiliwa na kuchochewa na wale wasiopenda kuuona umma wao
umetulia huku ukipiga hatua katika kuziendeleza nchi zao na kuwaelimisha watu
wao.
Na katika kila pembe ya ulimwengu chuki hizi zinaanza
kupasua njia kidogo kidogo na ni Mwenyezi Mungu peke Yake Anaelewa wapi
yataishia.
Mambo yaliyotokea miaka elfu moja mia nne iliyopita yanaendelea
kuwagawa na kuwafarikisha Waislamu hadi hivi sasa katika karne hii ya satellite
na computer.
Umma huu ni Umma mmoja, Mungu wetu ni Mungu Mmoja, na
Dini yetu ni moja na Mtume wetu ni mmoja, Lengo letu ni moja na adui yetu ni
mmoja, kwa nini basi hatuungani tukawa kitu kimoja?
Ikiwa kuwapenda
watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) ni
Ushia, basi sisi sote ni Mashia, na ikiwa kuwapenda Masahaba (Radhiya Llaahu
‘‘anhum) ni Usunni, basi sote tuwe Masunni. Waislamu hawatakuwa na kheri yoyote
ikiwa watawachukia watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu
‘alayhi wa sallam) ambao Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi
wa sallam) ametuamrisha tuwaswalie kila tunapomswalia.
Na Waislamu
hawatakuwa na kheri yoyote ikiwa watawachukia Sahibu zake Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) (Radhiya Llaahu ‘anhum), ambao baada ya
kufariki dunia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam), wao
ndio walioibeba bendera na kuueneza Uislamu kila pembe ya ulimwengu.
Waislamu
wanatakiwa waone fahari kubwa kila wanapotajwa Masahaba hawa watukufu (Radhiya
Llaahu ‘‘anhum), kwa sababu wao ndio waliotuletea Uislamu. Wao ndio
waliotufikishia Qur-aan tukufu ambayo ni Nuru itokayo kwa Mola wetu.
Mwenyezi Mungu Amewajaalia wao kuwa ndiyo sababu ya
kutufikia dini hii kote huku tuliko. Kwa juhudi yao kubwa na kujitolea kwao
mhanga kwa hali na mali waliuwezesha Uislamu kuingia na kuenea na kufuatwa na
kupendwa Arabuni kote, Iran, Asia, Afrika hadi Ulaya na Marekani.
Wangelikuwa
watu hawa ni makafiri basi wangelituletea ukafiri badala ya Uislamu.
Wangelituletea misalaba na masanamu badala ya Qur-aan na Swalah na salamu
(amani ?).
Tunamshukuru
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) kuwa hitilafu baina ya madhehebu ya
Kiislamu si katika kiini cha dini na asili ya mafundisho yake, kama vile
kuabudiwa Mwenyezi Mungu Mmoja na kwamba Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa
sallam) ni Mtume Wake. Hitilafu haikuwa juu ya Qur-aan tukufu, kwani
AlhamduliLlaah Waislamu wote kwa pamoja wanaamini kuwa Qur-aan hii tuliyonayo
hivi sasa ndiyo ile ile aliyoteremshiwa Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa
sallam) miaka elfu moja mia nne iliyopita bila ya kubadilika.
Tunaelewa kuwa
walikuwepo baadhi ya Maulamaa wachache wa madhehebu ya Kishia mfano wa Nuwriy
At-Tubrusiy aliyeandika kitabu ‘Faslu l Khitwaab fiy ithbaat tahriyf kitaab
Rabbil Arbaab’, akidai ndani ya kitabu hicho kuwa Qur-aan hii tuliyonayo
ilibadilishwa na kupunguzwa na kuzidishwa, lakini AlhamduliLlaah katika wakati
wetu huu hapana tena anayeziamini kauli hizo hata miongoni mwa wengi kati ya
Mashia, ikiwa si wote, na kama watakuwepo basi watakuwa wachache sana.
Tunamshukuru
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) pia kuwa hitilafu hii haikuwa katika
kuharamisha au kuhalalisha mambo yanayojulikana katika dini kuwa ni ya dharura
kama vile uharamu wa Pombe, kula nyama ya nguruwe n.k.
Hapana shaka
yoyote kuwa ipo hitilafu juu ya baadhi ya mambo yanayohusiana na Itikadi ‘Aqiydah’,
kama vile kumuomba mwengine asiyekuwa Mwenyezi Mungu na kuyatukuzu makaburi ya
watu wema.
Naelewa pia
kuwa wapo wanaojinasibisha na Ahlus Sunnah wenye kuwaomba wengine wasiokuwa
Mwenyezi Mungu na kuyatukuza makaburi ya watu wema, lakini tofauti iliyopo
baina ya Sunnah na Shia ni kuwa Maulamaa wa Ahlus Sunnah wanayakemea na
kuyakataza mambo haya, wakati maulamaa wa Shia wanayanyamazia na kuyapa
kipaumbele.
Anasema
Dr. Ahmed Al Kaatib mwanachuoni wa Kishia kutoka Iraq ambaye ni mwalimu katika
vyuo vikuu mbali mbali vya dini huko Iraq, Kuwait na Iran na ambaye ni
Mwenyekiti wa Jumuia ya Majadilianao ya Ustaarabu, 'Al Hiwaar al Hadhwaariy',
ambayo makao yake makuu yapo London, alisema: