![]() |
Mapenzi ya Ahli Sunnah juu ya Ahlil Bayt
(Watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam) |
Mmoja katika wana falsafa wa zamani
alisema:
“Haki yote haiwezi kumilikiwa na upande
mmoja, wala makosa yote hayawezi kuwepo upande mwingine, bali kila upande
husibu sehemu yake. Mfano wa kundi la vipofu waliopelekwa mbele ya tembo wakatakiwa
wamguse mwili wake, kisha kila mmoja aelezee umbile lake.
Katika muda mfupi waliopewa, hapana
aliyewahi kukamilisha kuushika mwili wote. Kila mmoja alifanikiwa kugusa sehemu
tu.
Aliyeushika mkonga akidhani kuwa amemshika
tembo wote akasema: “Mwili wa tembo ni mrefu mfano wa gogo la mti”,
Aliyeshika mgongo akasema:
“Hapana, bali mwili wa tembo ni mfano wa
jabali dogo”,
Aliyeshika sikio akasema:
“Nilivyouona mimi mwili wa tembo ni mpana,
duara na laini”.
Kila mmoja anahadithia juu ya ile sehemu
aliyodiriki kuishika katika muda mfupi ule akidhani anatoa maelezo kamili. Wote
wamesema kweli, lakini kila mmoja amehadithia sehemu tu ya ukweli anoujua yeye akidhani kuwa ndio
ukweli wote.”
Hitilafu husababishwa na mambo mengi,
yakiwemo upeo wa kufahamu, kupenda, matamanio ya nafsi, mielekeo ya elimu, ya
kifikra, kuiga waliotangulia, kupenda umaarufu, kupenda ukubwa, hitilafu za
ustaarabu. Wengine huiga waliyowakuta nayo wazee wao, na wengine wanafuata
mafundisho ya walimu wao wanaowaamini n.k. Na wengine
huiendeleza hitilafu kwa sababu ya ubishi au kiburi tu, hata kama wataiona haki
mbele yao.
Si vibaya kuhitilafiana, kwa sababu Mwenyezi Mungu Ametuumba
kila mmoja na akili yake pamoja uwezo wake wa kufahamu.
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóáóæú
ÔóÇÁ ÑóÈøõßó áóÌóÚóáó ÇáäøóÇÓó ÃõãøóÉð æóÇÍöÏóÉð æóáÇó íóÒóÇáõæäó ãõÎúÊóáöÝöíäó .ÅöáÇøó
ãóä ÑøóÍöãó ÑóÈøõßó æóáöÐóáößó ÎóáóÞóåõãú.
«Na Mola wako Mlezi Angelipenda Angewafanya
watu wote wakawa umma mmoja. Lakini hawaachi kukhitalifiana, Isipokuwa
wale ambao Mola wako Mlezi Amewarehemu; na kwa hiyo ndio Mwenyezi Mungu
Amewaumba.»
Huud-118-119
Anasema
Al Hasan Al Basry: æóáöÐóáößó
ÎóáóÞóåõãú maana
yake ni kuwa; Amewaumba ili wakhitalifiane.
Wenye
kukhitilifiana wanaweza kusikilizana na kufahamiana ikiwa hapana chuki baina
yao, lakini chuki inapoingia, hayapatikani tena masikilizano wala kufahamiana.
Chuki inaondoa mapenzi na inavunja uhusiano mwema na inaendeleza bughudha na
kuondoa uwezekano wowote wa masikilizano.
Imepokelewa
kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) usiku mmoja
aliamka uso wake ukiwa mwekundu huku akisema:
áÇ Åöáåó ÅöáÇø Çááå¡ æóíúáñ ááÚóÑóÈö¡ ãöäú ÔóÑó
ÞóÏö ÇÞúÊóÑóÈ
Laa
ilaaha illa Llah, Ole wao Waarabu kwa shari iliyo karibu
Alirudia maneno
haya mara tatu.
Maulamaa
wanasema kuwa;‘Hii
ilikuwa ishara kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa
sallam) juu ya hitilafu itakayotokea baada yake’.
Hitilafu
iliyopo hivi sasa baina ya Shia na Sunni inakula kibichi na kikavu.
Mamia
ya Waislamu wanauliwa kila siku huko Iraq, na wanaendelea kuuliwa, na mamilioni
wengine wamejeruhiwa. Mamilioni
wamekwishaihama nchi yao, na mamilioni hawana kazi wala bazi.
Lebanon, nchi iliyojaa neema, nchi ya elimu
na ziraa. Nchi ya historia na sanaa, leo kila kitu kimesimama katika
nchi hii kwa sababu ya fitna ya umadhehebu. Nchi haina serikali, ina majeshi
mawili, kila moja linadai kuwa wao ndio wenye kuipenda nchi. Ina makundi
mawili, kila moja linalituhumu jingine kuwa ni vibaraka. Watu hawaelewi
wanapelekwa wapi, kila siku mapambano ya risasi na mabomu.
Huko Yemen, maelfu ya watu wamekwishapoteza
maisha yao katika mapambano baina ya majeshi ya serikali na makundi ya watu wa
kabila la Houthi wenye kufuata madhehebu ya
Shia Ishnaashariyah.
Hii ni fitna iliyopenyezwa katika mwili wa Waislamu kwa
ajili ya kuwagawa. Inatumiliwa na kuchochewa na wale wasiopenda kuuona umma wao
umetulia huku ukipiga hatua katika kuziendeleza nchi zao na kuwaelimisha watu
wao.
Na katika kila pembe ya ulimwengu chuki hizi zinaanza
kupasua njia kidogo kidogo na ni Mwenyezi Mungu peke Yake Anaelewa wapi
yataishia.
Mambo yaliyotokea miaka elfu moja mia nne iliyopita yanaendelea
kuwagawa na kuwafarikisha Waislamu hadi hivi sasa katika karne hii ya satellite
na computer.
Umma huu ni Umma mmoja, Mungu wetu ni Mungu Mmoja, na
Dini yetu ni moja na Mtume wetu ni mmoja, Lengo letu ni moja na adui yetu ni
mmoja, kwa nini basi hatuungani tukawa kitu kimoja?
Ikiwa kuwapenda
watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) ni
Ushia, basi sisi sote ni Mashia, na ikiwa kuwapenda Masahaba (Radhiya Llaahu
‘‘anhum) ni Usunni, basi sote tuwe Masunni. Waislamu hawatakuwa na kheri yoyote
ikiwa watawachukia watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu
‘alayhi wa sallam) ambao Mtume (Swalla Llaahu ‘alayhi
wa sallam) ametuamrisha tuwaswalie kila tunapomswalia.
Na Waislamu
hawatakuwa na kheri yoyote ikiwa watawachukia Sahibu zake Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) (Radhiya Llaahu ‘anhum), ambao baada ya
kufariki dunia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam), wao
ndio walioibeba bendera na kuueneza Uislamu kila pembe ya ulimwengu.
Waislamu
wanatakiwa waone fahari kubwa kila wanapotajwa Masahaba hawa watukufu (Radhiya
Llaahu ‘‘anhum), kwa sababu wao ndio waliotuletea Uislamu. Wao ndio
waliotufikishia Qur-aan tukufu ambayo ni Nuru itokayo kwa Mola wetu.
Mwenyezi Mungu Amewajaalia wao kuwa ndiyo sababu ya
kutufikia dini hii kote huku tuliko. Kwa juhudi yao kubwa na kujitolea kwao
mhanga kwa hali na mali waliuwezesha Uislamu kuingia na kuenea na kufuatwa na
kupendwa Arabuni kote, Iran, Asia, Afrika hadi Ulaya na Marekani.
Wangelikuwa
watu hawa ni makafiri basi wangelituletea ukafiri badala ya Uislamu.
Wangelituletea misalaba na masanamu badala ya Qur-aan na Swalah na salamu
(amani ?).
Tunamshukuru
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) kuwa hitilafu baina ya madhehebu ya
Kiislamu si katika kiini cha dini na asili ya mafundisho yake, kama vile
kuabudiwa Mwenyezi Mungu Mmoja na kwamba Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa
sallam) ni Mtume Wake. Hitilafu haikuwa juu ya Qur-aan tukufu, kwani
AlhamduliLlaah Waislamu wote kwa pamoja wanaamini kuwa Qur-aan hii tuliyonayo
hivi sasa ndiyo ile ile aliyoteremshiwa Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa
sallam) miaka elfu moja mia nne iliyopita bila ya kubadilika.
Tunaelewa kuwa
walikuwepo baadhi ya Maulamaa wachache wa madhehebu ya Kishia mfano wa Nuwriy
At-Tubrusiy aliyeandika kitabu ‘Faslu l Khitwaab fiy ithbaat tahriyf kitaab
Rabbil Arbaab’, akidai ndani ya kitabu hicho kuwa Qur-aan hii tuliyonayo
ilibadilishwa na kupunguzwa na kuzidishwa, lakini AlhamduliLlaah katika wakati
wetu huu hapana tena anayeziamini kauli hizo hata miongoni mwa wengi kati ya
Mashia, ikiwa si wote, na kama watakuwepo basi watakuwa wachache sana.
Tunamshukuru
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) pia kuwa hitilafu hii haikuwa katika
kuharamisha au kuhalalisha mambo yanayojulikana katika dini kuwa ni ya dharura
kama vile uharamu wa Pombe, kula nyama ya nguruwe n.k.
Hapana shaka
yoyote kuwa ipo hitilafu juu ya baadhi ya mambo yanayohusiana na Itikadi ‘Aqiydah’,
kama vile kumuomba mwengine asiyekuwa Mwenyezi Mungu na kuyatukuzu makaburi ya
watu wema.
Naelewa pia
kuwa wapo wanaojinasibisha na Ahlus Sunnah wenye kuwaomba wengine wasiokuwa
Mwenyezi Mungu na kuyatukuza makaburi ya watu wema, lakini tofauti iliyopo
baina ya Sunnah na Shia ni kuwa Maulamaa wa Ahlus Sunnah wanayakemea na
kuyakataza mambo haya, wakati maulamaa wa Shia wanayanyamazia na kuyapa
kipaumbele.
Anasema
Dr. Ahmed Al Kaatib mwanachuoni wa Kishia kutoka Iraq ambaye ni mwalimu katika
vyuo vikuu mbali mbali vya dini huko Iraq, Kuwait na Iran na ambaye ni
Mwenyekiti wa Jumuia ya Majadilianao ya Ustaarabu, 'Al Hiwaar al Hadhwaariy',
ambayo makao yake makuu yapo London, alisema:
"Nimefanya
utafiti ulionipa uhakika kuwa hitilafu iliyopo baina ya Sunnah na Shia hauna
msingi wowote na imenithibitikia baada ya kuidurusu kadhia hii kuwa hitilafu
zilizokuwepo ni za kisiasa tu na wala si za itikadi.
Baada
ya kufanya utafiti wangu ulionichukua muda mrefu sana imenithibitikia kuwa
hitilafu iliyokuwepo baina yetu (Shia na Sunnah) ni juu ya Imam Al Mahdi na pia
yale madai kuwa ‘‘Umar (Radhiya Llaahu ‘‘anhu) alimpiga Bibi Faatwimah Az
Zahraa (‘Alayhas Salaam) siku ile watu walipofungamana na Abu Bakr (Radhiya
Llaahu ‘anhu).
Baada
ya kumaliza utafiti wangu," anaendelea kusema Ahmed Al Kaatib ambaye hadi
hivi sasa ni mwalimu mkubwa wa madhehebu ya Shia Ithnaashariyah;
"imenidhihirikia kuwa madai hayo kuwa ‘Umar (Radhiya Llaahu ‘anhu) alimpiga
Bibi Faatwimah (Alayhas Salaam) hayana msingi wowote na kwamba ni uzushi
ulioenezwa na kuandikwa katika vitabu mbali mbali vya historia kwa ajili ya
kuipa nguvu nadharia ya Uimamu, nadharia ambayo inafutika ikithibiti kuwa ‘Aliy
(Radhiya Llaahu ‘anhu) alikubali kwa hiari yake kufungamana na Abu Bakr na ‘Umar
na ‘Uthmaan (Radhiya Llaahu ‘anhum) walipochaguliwa kuwa Makhalifa, kwa sababu
angelikuwa Imam ‘Aliy (‘Alayhis Salaam) amechaguliwa na Mwenyezi Mungu, basi
asingekubali kufungamana nao kwa hiari yake.
Wazushi
wa kisa hicho walidai kuwa Aliy (Alayhis Salaam) alikubali kufungamana na Abu
Bakr baada ya Umar kuingia kwa nguvu nyumbani kwake na kumpiga mkewe ambaye
ni Bibi Faatwimah (‘Alayhas Salaam)
binti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) mpaka mimba
ikamtoka."
Anasema
Ahmed Al Kaatib:
"Nilikifanyia
uchunguzi kisa hiki lakini sijakikuta katika kitabu chochote chenye kutambulika
na kuaminika miongoni mwa vitabu vya Kishia kama vile Al Kafi na vyenginevyo.
Kinachokikanusha
zaidi kisa hicho ni ule uhusiano mzuri uliokuwepo baina yao hadi kufikia kuwa ‘Aliy
na Faatwimah (‘Alayhimas Salaam) walimuozesha binti yao Ummu Kulthum kwa ‘Umar.
Itawezekanaje
basi, kwa mama akubali kumuozesha binti yake mtu aliyempiga mpaka mimba
ikamtoka?"
"Ama
kisa cha Uimamu," anaendelea kusema Ahmed Al Kaatib: "Hata Ayatollah
Sistani ametamka kuwa jambo hili si katika mambo ya msingi wa dini kwa Shia, na
kwamba linaweza kujadiliwa.
Nilifuatilia
vitabu vilivyoandikwa na waandishi wa Kishia katika karne ya tatu na ya nne na
ya tano Hijri nikaona kuwa hapana ushahidi wowote unaothibitisha kuwa Imam huyu
alizaliwa, na kwamba Sayed Murtadha na Al Umani na wengine wanasema: "Sisi
tunaona kuwa haya ni mambo ya kukisia tu kwa dalili za kiakili na hatuna dalili
za kielimu zisizopingika.
Kwa
hivyo nadharia ya kuwepo kwa Imam wa kumi na mbili mwenye kusimamia,
anayetokana na Imam Husayn (Radhiya Llaahu ‘anhu) aliyepewa jina na Muhammad
bin Hasan Al Askary na nadharia ya kutoweka kwake, si katika itikadi za Ahlul
Bayt, bali wamenasibishwa nazo na baadhi ya waandishi.
Na
hivi sasa kwa vile serikali ya Iran imeamua kuipa nguvu nadharia ya Utawala
wa mwanachuoni 'Wilayat al Faqiyh' na imeamua kufuata nidhamu ya
kuchagua viongozi wa dini kwa njia ya kushauriana, 'Shuura' na kuchagua
viongozi wa nchi kwa njia ya demokrasia (democracy), kwa hivyo haya
yanafuta ile kauli ya kuwa kiongozi lazima awe aliyechaguliwa na Mwenyezi
Mungu, na badala yake mtu yeyote anaweza kuwa kiongozi ikiwa watu wataridhka
naye na kumchagua, (pia siyo lazima awe katika ‘Ahlul Bayt’)
Kwa
ajili hiyo ile khitilafu iliyokuwepo baina ya Shia na Sunnah juu ya Uimamu sasa
itakuwa ishaondoka pia kwa sababu Shia hawaamini tena juu ya ulazima wa kuwepo
Imam aliyetoweka akaingia ndani ya pango na wala hawasubiri tena kutoka pangoni
alipoingia miaka elfu moja iliyopita ili wapate kuisimamisha dola ya Kiislamu.
Na
lile sharti ya kuwa Imam mwenye kuwaongoza Waislamu lazima awe Aliyechaguliwa
na Mwenyezi Mungu na awe aliyekingwa asiyefanya makosa anayetokana na ukoo
maalum, nayo pia imeondoka kwa sababu kiongozi hivi sasa anachaguliwa kwa njia
ya uchaguzi au kwa kushauriana ‘Shuura’."
Mwisho wa maneno ya Al Kaatib
(Website ya Al
Arabiyah.net. Tarehe 27 May 2008)
Anasema mwanachuoni mwengine maarufu Dr. Musa al Musawiy
katika kitabu chake ‘Ash Shi’ah wat Tas’hiyh’’:
«Baada
ya utafiti mkubwa nilioufanya katika kulichambua tatizo hili la hitilafu kubwa
iliyopo baina ya Shia Ithanaashariyah na Ahlus Sunnah, nimegundua kuwa yale
yaliyotokea baada ya kufariki kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu
‘alayhi wa sallam) siyo sababu ya hitilafu hii kubwa, wala si kwa sababu ya
kuwa ‘Aliy (Alayhis Salaam) ndiye anayestahiki ukhalifa baada ya Mtume (Swalla
Llaahu ‘alayhi wa sallam), kwa sababu nawaona wenye kufuata madhehebu ya Shia Zaydiyah
wapo kwa mamilioni katika ulimwengu na wanaishi kwa wema na mapenzi na
masikilizano baina yao na Masunni.
Kwa
hivyo sababu ya hitilafu baina ya Shia Ithnaashariyah na Madhehebu mengine ya
Kiislamu ni ule msimamo wao dhidi ya Makhalifa walioongoka na kuwatukana kwao
na kuwalaani, jambo ambalo halipo upande wa Shia Zaydiyah na makundi mengine.
Lau kama Shia Ithnaashariyah walingelifuata mwenendo wa Shia Zaydiyah basi
hitilafu ingelipungua sana na tatizo lingekuwa dogo. Lakini Shia Ithnaashariyah
wameingia katika shimo la kuwatukana Makhalifa walioongoka na kuwalani na
kuwashambulia, jambo linalosababisha
hitilafu hii izidi na kuongezeka.»
Ash Shi’ah wat Tashiyh’. Uk.4
Kutokana na maelezo haya ya Maulamaa wa Kishia,
inatubainikia kuwa laiti kama wafuasi wa Shia wangeliacha mwenendo wa
kuwatukana na kuwalaani Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu
‘alayhi wa sallam) pamoja na wake zake Mama wa Waislamu, na lau kama wataacha
mwenendo wa kuwatukana na kuwalaani Waislamu wenzao katika siku za Muharram na
kuwaapiza kwa kula viapo kuwa lazima watalipa visasi vya kuuliwa kwa Al Husayn,
basi sehemu kubwa ya chuki baina ya makundi mawili haya yangeondoka.
Masunni wanawaheshimu sana na kuwatukuza watu wote wa
nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam), na
wanawaheshimu pia Masahaba wake (Radhiya Llaahu ‘anhum), na wanaamini kuwa wote
hao ni watu bora ambao Mwenyezi Mungu Ameridhika nao, kama ilivyoandikwa katika
Qur-aan tukufu.
Masunni wanajitenga na kila aliyeshiriki katika vile vita
vilivyosababisha kuuliwa kwa Al Husayn (Radhiya Llaahu ‘anhu), na wanajitenga
na wote waliomuua na waliosababisha kuuliwa kwa Al Husayn (Radhiya Llaahu
‘anhu) na aila yake, na wanaamini kuwa wameuliwa kwa dhulma na kwa uadui, na
kwamba wote wamekufa Shahiyd.
Wakati huo huo Masunni wanashangazwa wanaposikia vilio na
maneno ya kulipwa visasi katika vikao vya Al Husayniyah. Maneno kama vile:
íÇ áÊÇÑÇÊ ÇáÍÓíä
Maneno yanayohimiza kulipwa visasi kwa ajili ya kuuliwa
Al Hussayn (Radhiya Llahu anhu).
Wanajiuliza; visasi hivyo watalipiwa nani wakati wote
waliomuua Al Husayn (Radhiya Llaahu ‘anhu) wamekwishafariki dunia.
Al Hurr bin Yazid At-Tamimiy keshakufa, ‘Umar bin Dhil
Jawshan keshakufa, Zara'a bin Shariyk keshakufa, ‘Umar bin Sa’ad keshakufa, Ubaydullah bin Ziyad naye pia
keshakufa, na wote walioshiriki katika vita vile wamekwisharudi kwa Mola wao
tokea miaka elfu moja mia nne iliyopita.
Maneno haya ya kuhimiza kulipa visasi yanatafsiriwa na
Ahlus Sunnah kuwa wao ndio wanaokusudiwa, na haya ni katika chuki
zilizopandikizwa na wasiopenda kuwaona Waislamu wa kila Madhehebu wakiishi pamoja kwa kupendana na
kushirikiana katika kuziendeleza mbele dola zao.
Mojawapo ya hitilafu
kubwa baina ya Sunnah na Shia ni juu ya tafsiri ya neno 'Ahlul Bayt'. (Watu
wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Wakati Shia
wanasema kuwa Ahlul Bayt ni Aly bin Abu Talib na Fatima binti Muhammad
na wanawe (Radhiya Llahu anhum) peke yao, Ahlus Sunnah wanaitakidi kuwa Ahlul
Bayt ni wote hao waliotangulia kutajwa pamoja na wake wa Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) na binti zake waliobakia wasiotambuliwa na Shia, na pia
wajukuu zake na baadhi ya waliohusiana naye katika ukoo wake.
Imeandikwa
katika kamusi maarufu "Lisanul Arab" kuwa; mke na jamaa za mtu
ni Ahli Bayti yake.
Na katika
Qurani tukufu, Mwenyezi Mungu anawataja wake wa mtu kuwa ni Ahli yake.
Mwenyezi Mungu anasema:
ÞóÇáõæÇú ÃóÊóÚúÌóÈöíäó ãöäú ÃóãúÑö Çááøåö
ÑóÍúãóÊõ Çááøåö æóÈóÑóßóÇÊõåõ Úóáóíúßõãú Ãóåúáó ÇáúÈóíúÊö
Åöäøóåõ ÍóãöíÏñ ãøóÌöíÏñ
"Wakasema:
Je, unastaajabia amri ya Mwenyezi Mungu? Rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka
zake ziko juu yenu, enyi watu wa nyumba hii! Hakika Yeye ndiye Msifiwa wa
kutukuzwa."
Hud-73
Maulamaa wote
wanasema kuwa neno (Watu wa nyumba), katika
aya hii anakusudiwa Sarah mke wa Nabii Ibrahim (Alayhi ssalaam).
Na Akasema:
ÅöÐú
ÑóÃóì äóÇÑðÇ ÝóÞóÇáó áöÃóåúáöåö ÇãúßõËõæÇ Åöäøöí ÂäóÓúÊõ äóÇÑðÇ
"Alipo uona moto,
akawaambia watu wake (Ahli yake): Ngojeni! Mimi nimeuona moto."
Taha-10
Inajulikana
hapa pia kuwa neno (Ahli yake) anakusudiwa mke
wa Nabi Musa (Alayhi ssalaam) aliyekuwa amefuatana naye katika safari hiyo.
Na Mwenyezi Mungu akasema pia:
ÞóÇáóÊú
ãóÇ ÌóÒóÇÁ ãóäú ÃóÑóÇÏó ÈöÃóåúáößó ÓõæóÁðÇ ÅöáÇøó Ãóä íõÓúÌóäó Ãóæú ÚóÐóÇÈñ
Ãóáöíãñ
"Hapana malipo ya mwenye kutaka kumfanyia maovu mkeo isipo
kuwa kufungwa au kupewa adhabu chungu."
Yusuf-25
Neno (Ahlika katika aya hii) na maana yake ni 'mkeo' aliyekusudiwa ni mke wa Al Aziz.
Kwa hivyo
dalili zote zinaonyesha kuwa neno Ahlul Bayt au Ahl linatumika
zaidi kwa maana ya mke.
Na katika Surat Al Ahzab kuanzia aya ya 28 hadi ya 33
Mwenyezi Mungu anasema:
íóÇ
ÃóíøõåóÇ ÇáäøóÈöíøõ Þõá áøöÃóÒúæóÇÌößó Åöä ßõäÊõäøó ÊõÑöÏúäó ÇáúÍóíóÇÉó
ÇáÏøõäúíóÇ æóÒöíäóÊóåóÇ ÝóÊóÚóÇáóíúäó ÃõãóÊøöÚúßõäøó æóÃõÓóÑøöÍúßõäøó ÓóÑóÇÍðÇ
ÌóãöíáðÇ¡ æóÅöä ßõäÊõäøó ÊõÑöÏúäó Çááøóåó æóÑóÓõæáóåõ æóÇáÏøóÇÑó ÇáúÂÎöÑóÉó
ÝóÅöäøó Çááøóåó ÃóÚóÏøó áöáúãõÍúÓöäóÇÊö ãöäßõäøó ÃóÌúÑðÇ ÚóÙöíãðÇ
"Ewe Nabii!
Waambie wake zako: Ikiwa mnataka maisha ya dunia na pambo lake, basi njooni,
nitakupeni kitoka nyumba, na kukuacheni mwachano mzuri.
Na
ikiwa mnamtaka Mwenyezi Mungu na Mtume wake na nyumba ya Akhera, basi Mwenyezi
Mungu amewaandalia wafanyao mema, miongoni mwenu, malipo makubwa."
íóÇ äöÓóÇÁ ÇáäøóÈöíøö ãóä íóÃúÊö ãöäßõäøó ÈöÝóÇÍöÔóÉò
ãøõÈóíøöäóÉò íõÖóÇÚóÝú áóåóÇ ÇáúÚóÐóÇÈõ ÖöÚúÝóíúäö æóßóÇäó Ðóáößó Úóáóì Çááøóåö
íóÓöíÑðÇ¡ æóãóä íóÞúäõÊú ãöäßõäøó áöáøóåö æóÑóÓõæáöåö æóÊóÚúãóáú ÕóÇáöÍðÇ
äøõÄúÊöåóÇ ÃóÌúÑóåóÇ ãóÑøóÊóíúäö æóÃóÚúÊóÏúäóÇ áóåóÇ ÑöÒúÞðÇ ßóÑöíãðÇ
"Enyi wake wa Nabii! Atakaye fanya uchafu dhaahiri miongoni
mwenu, atazidishiwa adhabu mara mbili. Na hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi.
Na
miongoni mwenu atakeye mt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na akatenda mema,
tutampa malipo yake mara mbili, na tutamwandalia riziki ya ukarimu."
íóÇ äöÓóÇÁ ÇáäøóÈöíøö áóÓúÊõäøó ßóÃóÍóÏò ãøöäó ÇáäøöÓóÇÁ Åöäö
ÇÊøóÞóíúÊõäøó ÝóáóÇ ÊóÎúÖóÚúäó ÈöÇáúÞóæúáö ÝóíóØúãóÚó ÇáøóÐöí Ýöí ÞóáúÈöåö
ãóÑóÖñ æóÞõáúäó ÞóæúáðÇ ãøóÚúÑõæÝðÇ
"Enyi
wake wa Nabii! Nyinyi si kama yeyote katika wanawake wengine. Kama mnamcha
Mungu basi msiregeze sauti zenu, akaingia tamaa mwenye maradhi katika moyo
wake. Na semeni maneno mema."
æóÞóÑúäó Ýöí ÈõíõæÊößõäøó
æóáóÇ ÊóÈóÑøóÌúäó ÊóÈóÑøõÌó ÇáúÌóÇåöáöíøóÉö ÇáúÃõæáóì æóÃóÞöãúäó ÇáÕøóáóÇÉó
æóÂÊöíäó ÇáÒøóßóÇÉó æóÃóØöÚúäó Çááøóåó æóÑóÓõæáóåõ ÅöäøóãóÇ íõÑöíÏõ Çááøóåõ
áöíõÐúåöÈó Úóäßõãõ ÇáÑøöÌúÓó Ãóåúáó ÇáúÈóíúÊö æóíõØóåøöÑóßõãú
ÊóØúåöíÑÇð
"
Na kaeni majumbani kwenu, wala msijishauwe kwa majishauwo ya kijahilia ya
kizamani. Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume
wake. Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu, enyi Watu wa Nyumba (ya
Mtume), na kukusafisheni baarabara."
Ahlu Sunnah
wanasema kuwa; kama vile katika aya zote zilizotangulia, kila anapotajwa Ahli
ya mtu hukusudiwa mke, na katika aya hizi pia Mwenyezi Mungu anapotaja Ahli
anawakusudia wake zake Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Ukizisoma kwa
utulivu aya hizi utaona kuwa kuanzia aya ya 28 Mwenyezi Mungu anazungumza na
wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam):
Mwenyezi Mungu
anasema : "Ewe Nabii! Waambie wake zako….”, Akaendelea: "Enyi wake wa
Nabii! Nyinyi si kama yeyote katika wanawake wengine.” Akaendelea
kuwahutubia: «Kaeni majumbani mwenu» «Toeni Zaka». «Mt'iini Mwenyezi
Mungu». Mpaka Aliposema: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu, enyi Watu wa
Nyumba (ya Mtume), na kukusafisheni baarabara." Yote haya
wanaambiwa wake zake Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kuanzia aya ya 28 hadi
33.
Hivi ndivyo
ulivyo mfumo wote wa aya hizi zilizokamatana na haziwezi kutenganishwa
isipokuwa kama mtu anataka kuvuka mipaka na kwenda kinyume na nassi.
Mtu anaweza
kuuliza: ‘Kwa nini basi Mwenyezi Mungu Ametumia ‘sigha’ (mfumo wa
maneno) ya wingi wa wanaume na wanawake kwa pamoja aliposema:
ÅöäøóãóÇ íõÑöíÏõ Çááøóåõ áöíõÐúåöÈó Úóäßõãõ ‘Ankum’
Ikiwa
Amewakusudia wake za Mtume (Swallah Llahu alyhi wa sallam) kwa nini asitumie sigha ya wanawake
peke yao akasema:
ÅöäøóãóÇ íõÑöíÏõ Çááøóåõ áöíõÐúåöÈó Úóäßõä ‘Ankunnaõ
Kwa nini
asitumie sigha ya wanawake kama alivyotumia katika aya nyingine zilizomo ndani
ya mfumo huu?
Majibu ni kuwa;
Aya za mwanzo Mwenyezi Mungu Alipozungumza juu ya hukmu za kisheria na makatazo
na maamrisho yanayowahusu wake za Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam) alitumia ‘Nuun’ ya wanawake Úäßä lakini alipozungumza juu ya wema
anaotaka kuuingiza ndani ya nyumba ile pamoja na kuwasafisha watu wa nyumba ile
barabara, alimuingiza pia na mwenye nyumba ambaye ni mwanamume naye ni Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) ili kheri hiyo iwaenee wote. Na
kawaida katika lugha ya kiarabu wanapotajwa wanawake na wanaume kwa pamoja
hutumiwa wingi wa wanaume Úäßã
‘Ankum’
Nani wanaostahiki
zaidi kusafishwa na kutakaswa kuliko wake zake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah
Llahu alayhi wa sallam), watu wa nyumba yake, mama wa Waislamu, na wanaostahiki
pia ni jamaa zake, watu wa aila yake. Kwa sababu Mtume wetu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) anastahiki kuwa pamoja na kila kheri na kila jema na kila
kilicho bora, na anastahiki zaidi kuwa pamoja na watu wema, naye haridhiki
isipokuwa awe pamoja na watu wema, kwani wema lazima siku zote uwe katika
mtiririko mmoja.
Na Mwenyezi
Mungu Subhanahu wa Taala alitaka kuwatakasa wake zake na jamaa zake,
akamtunukia haya Mtume wake (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Ikiwa tumemkubali
mke wa Nabi Musa (Alayhissalaam) katika aya tuliyotangulia kuitaja kuwa ni Ahli
yake na tukamkubali mke wa Al Aziz kama ilivyokuja katika aya kuwa ni Ahli
yake na tukamuingiza Sarah mke wa Nabi Ibrahim (Alayhissalaam) kuwa ni Ahli
yake, juu ya kuwa katika aya ile Mwenyezi Mungu alitumia mfumo ule ule wa wingi
wa wanaume na wanawake kwa pamoja Aliposema:
ÑÍãÉ Çááå æÈÑßÇÊå Úáíßã
Ãåá ÇáÈíÊ
Alitumia neno (ÚáíßãAlaykum)
Kama alivyotumia
(Úäßã Ankum) katika Suratul Ahzab
aliposema:
ÅöäøóãóÇ íõÑöíÏõ Çááøóåõ
áöíõÐúåöÈó Úóäßõãõ ÇáÑøöÌúÓó Ãóåúáó ÇáúÈóíúÊö
Ikiwa
tumewakubali wake wa Mitume wote hao kuwa ni watu wa nyumba, tunalazimika pia
kuwakubali wake wa Mtume wetu Muhammad (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kuwa ni
watu wa nyumba yake.
Kutokana na
haya inafahamika zaidi tafsiri ya ile hadithi maarufu inayoitwa Hadiyth al
Kisaa na maana yake ni hadithi ya nguo au hadithi ya shuka, wakati Mtume
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) alipowaingiza ndani ya shuka ile Aly na Bibi
Fatima na Al Hassan na Al Hussayn (Radhiya Llahu anhum), kwa ajili ya
kuwaingiza na wao katika zile baraka zilizoteremshwa ndani ya aya ile ya Surat
al Ahzab.
Hadithi
inasimulia kuwa baada ya kuwaingiza wote hao ndani ya shuka, akasema:
"Ãááåãøó åÄáÇÁ Ãåá ÈíÊí ÝÇÐåÈ Úäåã
ÇáÑÌÓ æØåÑåã ÊØåíÑÇð
"Mola
wangu hawa ni watu wa nyumba yangu, waondolee uchafu na uwasafishe
baarabara."
Na
Ummu Salama (Radhiya Llahu anha) mke wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) alipoingiza kichwa chake ndani ya shuka hiyo akasema:
"Ewe
Mtume wa Mwenyezi Mungu na mimi ni katika watu wa nyumba yako.»
Mtume
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) akamuambia:
ÊäÍí ÝÅäß Úáì ÎíÑ
"Wewe
umo katika kheri wewe umo katika kheri."
Na maana yake
ni kuwa Ummu Salama na wake wenzake wote wamekwisha tajwa na Mwenyezi Mungu
katika aya hiyo na kwamba wao wamo katika kheri hiyo ya kusafishwa na kutakaswa.
Ndiyo maana akaambiwa:
"Wewe
umo katika kheri wewe umo katika kheri."
Dalili nyingine
inayothibitisha kuwa wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) ni katika watu wa nyumba yake imo katika Bukhari na Muslim na
Attirmidhy na Annasaiy na wengine kama ilivyopokelewa kuwa Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) alipoulizwa na Masahaba:
"Vipi
tukuswalie?
Akasema:
"Semeni:
Çááåã Õá Úáì ãÍãÏ æÃÒæÇÌå æÐÑíÊå¡ ßãÇ ÕáíÊ Úáì ÅÈÑÇåíã¡ æÈÇÑß
Úáì ãÍãÏ æÃÒæÇÌå æÐÑíÊå¡ ßãÇ ÈÇÑßÊ Úáì Âá ÅÈÑÇåíã Åäß ÍãíÏ ãÌíÏ
"Mola
wangu mswalie Muhammad na wake zake na vizazi vyake, kama ulivyomswalie Ibrahim,
na umbariki Muhammad na wake zake na vizazi vyake kama ulivyowabariki watu wa
nyumba ya Ibrahim hakika Wewe ni Mwenye kuhimidiwa uliye Mtukufu."
Ikajulisha kuwa mke wa mtu na vizazi vyake ni watu wa nyumba
yake.
Ikiwa mtu hajatoshelezwa na dalili zote tulizozinukuu kutoka
katika kitabu cha Mwenyezi Mungu na mafundisho ya Mtume wake (Swallah Llahu
alayhi wa sallam), basi ipo dalili nyingine katika Sahih al Bukhari
itakayoondoa shaka yoyote iliyobaki kwa mwenye kuutafuta ukweli bila ya chuki
moyoni mwake.
Inajulikana kuwa Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha) mke wa
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) alisingiziwa uwongo
katika kisa mashuhuri kinachojulikana kwa jina la Haadithatul If’k ,
uwongo ambao Mwenyezi Mungu aliteremsha aya katika Qurani tukufu kuukanusha, na
wakati huo huo aya hizo ziliwaonya Waislamu kutorudia tena kueneza uvumi huo,
na zikawatahadharisha juu ya adhabu kali itakayomfikia mwenye kurudia tena.
Wakati ule Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) alipanda juu ya membari yake kuhutubia, akasema:
"íÇ ãÚÔÑ ÇáãÓáãíä ãä íÚÐÑäí ãä ÑÌá ÞÏ
ÈáÛäí ÃÐÇå Ýí Ãåáí¡ ÝæÇááøå ãÇ ÚáãÊ Úáì Ãåáí ÅáÇ ÎíÑÇð¡ æáÞÏ ÐßÑæÇ ÑÌáÇð ãÇ
ÚáãÊ Úáíå ÅáÇ ÎíÑÇð¡ æãÇ ßÇä íÏÎá Úáì Ãåáí ÅáÇ ãÚí"
“Enyi Waislamu! Nani
atakayenipumzisha na mtu aliyeniudhi katika Ahli yangu, kwani Wallahi sijaona
kwa Ahli yangu isipokuwa kheri tupu, na hakuwa akiingia kwa Ahli yangu
isipokuwa akiwa pamoja nami.”
Bukhari
Atakayechunguza, ataona kuwa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amelitaja neno Ahly (watu wa nyumba yangu) katika hotuba hii
fupi mara tatu, zote zikimaanisha mkewe Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha),
ikituthibitishia kuwa neno Ahly lina
maana ya mke.
Sisi tunawakubali na tunawapenda na tunawapa heshima kubwa na
tunawatambua watu wote wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah LLahu
alayhi wa sallam), wale wanaokubaliwa na Shia na pia wasiokubaliwa na Shia kuwa
ni katika Ahlul Bayt kama vile ami zake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah
LLahu alayhi wa sallam), watoto wa ami zake pamoja na watoto wao (Radhiya Llahu
anhum), hawa ambao Shia hawawatambui kuwa ni watu wa nyumba yake (Swallah LLahu
alayhi wa sallam), kama walivyotajwa katika hadithi iliyotangulia, nao ni kama
ifuatavyo:-
1.
Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
2.
Wake zake
3.
Binti zake wote
4.
Watu wa nyumba ya Al Abbas bin Abdulmuttalib
5.
Watu wa nyumba ya Aqiyl bin Abu Talib
6.
Watu wa nyumba ya Aly bin Abu Talib
7.
Watu wa nyumba ya Jaafar bin Abu Talib
Hawa wote wametajwa katika hadithi iliyotolewa na Muslim wakati Zeid bin
Al Arqam (Radhiya Llahuanhu) alipoulizwa:
‘Wake zake si katika watu wa nyumba yake?’
Akasema:
‘Wake zake ni watu wa nyumba yake. Lakini watu wa
nyumba yake (waliokusudiwa hapa) ni wale walioharimishwa kupokea sadaka.’
Akaulizwa:
‘Nani hao.
Akasema:
‘Hao ni watu wa nyumba ya Aly na watu wa nyumba ya
Aqiyl na watu wa nyumba ya Jaafar na watu wa nyumba ya Abbas (Radhiya Llahu
anhum).’
Kwa hiyvo watu wa nyumba hizo juu ya kuwa wengine hawakuwemo ndani ya
ile shuka lakini wametajwa kuwa ni watu wa nyumba yake (Swallah LLahu alayhi wa
sallam).
Wake zake bila shaka wanaingia katika watu wa nyumba yake kwa sababu ya
kutajwa katika Suratul Ahzab kama ilivyotangulia, na ndiyo maana katika
kuikamilisha aya hiyo Mwenyezi Mungu akasema :
{ æóÇÐúßõÑúäó ãóÇ íõÊúáóì Ýöí ÈõíõæÊößõäøó ãöäú
ÂíóÇÊö Çááøóåö æóÇáúÍößúãóÉö Åöäøó
Çááøóåó ßóÇäó áóØöíÝÇð ÎóÈöíÑ}
‘Na
watajieni (watu) yasomwayo majumbani mwenu katka Aya za Mwenyezi Mungu na
hikima (ya Mtume), kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo ya siri na Mjuzi
wa mambo ya dhahiri.’
Al Ahzab-34
Na maana yake ni kuwa zifanyieni kazi zile aya zilizoteremshwa ndani ya
nyumba zenu, kwa sababu Mwenyezi Mungu amezihusisha nyumba zenu kwa kuteremsha
aya Zake, tofauti na nyumba nyingine. Na Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha) ndiye
anayehusika zaidi kwa sababu hazikupata kuteremshwa aya juu ya kitanda cha
yeyote miongoni mwa wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) isipokuwa kwake.
Na watoto na wajukuu wa Al Hassan bin Aly na Al Hussayn bin Aly na Abdillahi
bin Abbas na Muhammad bin Al Hanafiyah (mtoto wa Sayiduna Aly kwa mke
mwengine), na Al Abbas bin Aly na wajukuu zao na wajukuu wa wajukuu zao, wote
hao pia ni miongoni watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam), na hii ni kwa wale waliokuwa Waislamu.
Abu Lahab juu ya kuwa ni ami yake Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam),
lakini yeye hayumo katika Ahli yake kwa sababu hakuwa Muislamu.
Nabi Nuh (Alayhissalaam) allipomuona mwanawe amekimbilia jabalini na
maji yanaanza kumfikia alimuomba Mwenyezi Mungu amuokowe.
Mwenyezi Mungu anasema :
æóäóÇÏóì äõæÍñ ÑøóÈøóåõ ÝóÞóÇáó ÑóÈøö Åöäøó ÇÈõäöí ãöäú Ãóåúáöí æóÅöäøó æóÚúÏóßó
ÇáúÍóÞøõ æóÃóäÊó ÃóÍúßóãõ ÇáúÍóÇßöãöíäó {45}þ ÞóÇáó íóÇ äõæÍõ Åöäøóåõ áóíúÓó
ãöäú Ãóåúáößó Åöäøóåõ Úóãóáñ ÛóíúÑõ ÕóÇáöÍò ÝóáÇó ÊóÓúÃóáúäö
ãóÇ áóíúÓó áóßó Èöåö Úöáúãñ Åöäøöí ÃóÚöÙõßó Ãóä Êóßõæäó
ãöäó ÇáúÌóÇåöáöíäó {46)
“Na Nuhu alimuomba Mola wake akasema: ‘Ewe Mola wangu! Mwanangu
ni katika watu wa nyumbani kwangu. Na hakika ahadi yako ni haki. Nawe ni Mwenye
haki kuliko mahakimu (wote).
Akasema (Mwenyezi
Mungu), “Ewe Nuhu! Huyu si miongoni mwa watu wako. Yeye ni (mwenye) mwendo
usiokuwa mzuri. Basi usiniombe ambayo huyajui . mimi nakunasihi usiwe miongoni
mwa wajinga.”
Hud-45-46
Mwenyezi Mungu alimkatalia na
kumuambia kuwa huyo si mwanawe, wala si katika watu wa nyumba yake kwa sababu
ya kuukanusha ujumbe aliokuja nao Nabi Nuh (Alayhissalaam).
Shia hawakubali kuwaingiza wengine isipokuwa wale tu waliotajwa katika
hadithi ya shuka pamoja na maimamu kumi na mbili waliofuata wa madhehebu ya
Ithnaasheri kwa sababu wanaamini kuwa hao ndio viongozi wa Waislamu
waliotakaswa wasiotenda makosa watakaowaongoza Waislamu baada ya kufa kwa Mtume
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) mpaka Siku ya Kiama.
Ahlus Sunnah wanawapenda na kuwaheshimu watu wa ukoo
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na wamewaweka katika
daraja ya juu wanayoistahiki.
Hawa ni binti zake wote, pamoja na Bibi Fatima Al Zahraa na
wanawe Al Hassan na Al Hussayn na watu wa ukoo wake tuliotangulia kuwataja kuwa
ni katika Ahlul Bayt wakiwemo Aly bin Abi Talib na watu wa nyumba yake, na Al Abbas bin Abdulmuttalib na
watu wa nyumba yake, na Aqiyl bin Abi
Talib na watu wa nyumba yake
na Jaafar bin Abi Talib na watu wa nyumba yake (Radhiya Llahu anhum).
Mwenyezi Mungu amewaondolea uchafu na kuwasafisha barabara watu hawa na
akatuamrisha katika kitabu chake kitukufu kuwapenda, na pia Mtume wake (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) ametuamrisha tuwapende.
Katika Sahih Muslim imeelezwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) alipowahutubia watu mahali panapoitwa Ghadiyr aliwaambia:
{ æÃåá ÈíÊí¡ ÃÐßÑßã Çááå Ýí Ãåá ÈíÊí¡ ÃÐßÑßã Çááå Ýí Ãåá ÈíÊí
}.
«Na watu wa nyumba yangu. Nakukumbusheni Mwenyezi
Mungu juu ya watu wa nyumba yangu, Nakukumbusheni Mwenyezi Mungu juu ya watu wa
nyumba yangu.»
Muslim
Mwenyezi Mungu anasema:
((Åöäøó Çááøóåó æóãóáÇÆößóÊóåõ íõÕóáøõæäó Úóáóì ÇáäøóÈöíøö íóÇ ÃóíøõåóÇ
ÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇ ÕóáøõæÇ Úóáóíúåö æóÓóáøöãõæÇ ÊóÓúáöíãðÇ))
«Hakika
Mwenyezi Mungu na Malaika wake wanamsalia Nabii. Enyi mlio amini! Msalieni na
mumsalimu kwa salamu»
Al Ah’zaab -56
Ilipoteremshwa aya hii Masahaba (Radhya Llahu anhum) walimuuliza Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam):
«Vipi tukuswalie?»
Akawaambia:
«Semeni:
{Çááåã Õá Úáì ãÍãÏ æÚáì Âá ãÍãÏ¡ ßãÇ ÕáíÊ Úáì
ÅÈÑÇåíã æÚáì Âá ÅÈÑÇåíã Åäß ÍãíÏ ãÌíÏ¡ æÈÇÑß Úáì ãÍãÏ æÚáì ãÍãÏ¡ ßãÇ ÈÇÑßÊ Úáì ÅÈÑÇåíã
æÚáì Âá ÅÈÑÇåíã Åäß ÍãíÏ ãÌíÏ}.
“Mola wangu Mswalie Muhammad na Aali ya Muhammad, kama
ulivyomswalia Ibrahim na aali ya Ibrahim hakika Wewe ni Msifiwa
na Mwenye kutukuzwa. Na umbariki Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali ya
Ibrahim hakika Wewe ni Msifiwa na Mwenyeye kutukuzwa.”
Anasema Ibnul Qayyim katika kuisherehesha hadithi hii:
Kuwaswalia Aali zake ni katika kukamilisha kumswalia Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) kwa sababu kufanya hivyo ni katika kumfurahisha Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), na Mwenyezi Mungu
anamuongezea daraja na heshima (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Imepokelewa kuwa Abubakar Al Siddiq (Radhiya Llahu anhu) alisema:
[[ÇÑÞ龂 ãÍãÏÇð Ýí Âá ÈíÊå]].
“Mpeni heshima
Muhammad kwa (kuwaheshimu) watu wa nyumba yake.”
Na alisema pia:
[[æÇááå áÃä ÃóÕöáó ÞÑÇÈÉ ÑÓæá Çááå Õáì Çááå
Úáíå æÓáã ÃÍÈ Åáí ãä ÃÕá ÞÑÇÈÊí]]
“Wallahi, kuwasiliana na jamaa zake Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) ni bora kwangu kuliko kuwasiliana na
jamaa zangu.”
Bukhari
Na ile hadithi isemayo: « Fatima ni
Bibi wa wanawake wa Peponi.»
Imepokelewa kutoka kwa Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha).
Imepokelewa pia kuwa siku ile Abu Sufyan alipokuja kusilimu mbele ya
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), Umar bin Khataab
(Radhiya Llahu anhu) alimuambia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam):
«Huyu hapa Abu Sufyan amekuja mwenyewe kwa miguu yake,
niruhusu nimkate kichwa chake».
Al Abbas (Radhiya Llahu anhu) ami yake Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akasema:
«Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu mimi namuingiza Abu
Sufiyan katika himaya yangu.»
Al Abbas akakaa karibu na Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam), na alipomuona Umar (Radhiya Llahu anhu)
anashikilia kutaka kumkata kichwa Abu Sufyan, Al Abbas akamuambia:
«Taratibu ewe Umar angelikuwa huyu ni katika watu wa
kabila lako la Bani Uday bin Kaab usingelishikilia namna hii, lakini kwa vile
huyu ni mtu (wa kabila langu) anayetokana na ukoo wa Abdu Manaf.»
Umar akasema kumuambia Al Abbas (Radhiya Llahu anhum):
«Taratibu ewe Abbas, kwani Wallahi naapa kuwa siku uliyosilimu
wewe ilikuwa bora kwangu kuliko angelisimu baba yangu Al Khattab,
kwa sababu naelewa kuwa kusilimu kwako kulimfurahisha sana Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam).»
Attabarani, Al Bidaya wal Nihayah- Ibni Kathiyr na Siyrat Ibn Hisham
Hadithi hizi na nyingi nyingine zinatufundisha namna gani watu wa nyumba
ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) walivyokuwa
wakiwapenda Masahaba, na pia Masahaba walivyokuwa wakiwapenda watu wa nyumba ya
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), na zinatufundisha pia
namna gani Ahlu Sunnah walivyojishughulisha kuzitafuta na kuziandika hadithi
zinazowahusu watu wa \nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam).
Masahaba na pia ‘Tabi’iyna’ (waliokuja baada yao)
walijishughulisha sana kutafuta na kuziandika fadhila za watu wa nyumba ya
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) ili watakaokuja baada
yao wazijuwe na kuzichunga na kuzifuata. Na hii ndiyo sababu utakaposoma kitabu
chochote katika vitabu vya Ahli Ssunnah hukosi kuona ndani yake mlango maalum
uliohusishwa kwa ajili ya sifa za Ahlul Bayt. Utayakuta haya katika
vitabu vya Hadiyth na vitabu vya Aqida na hata katika vitabu vya Tariykh
‘historia’.
Imam Bukhari kwa mfano, amehusisha mlango maalum juu ya fadhila za Imam
Aly (Radhiya Llahu anhu), na amehusisha mlango wa fadhila za Bibi Fatima
(Radhiya Llahu anha) nk.
Imam Muslim katika mlango wa Fadhila za Masahaba ameandika juu ya
fadhila za Maimam Al Hassan na Al Hussayn (Radhiya Llahu anhum).
Imam Attirmidhy na Ibni Maajah na Imam Ahmad bin Hanbal na Ibni Kathiyr
na Attabariy na Ibni Taymiyah na Adh’dhahabiy na wengine, wote hawa katika
vitabu vyao wameandika kwa mapana na marefu juu ya fadhila za Maimam hawa
wawili ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amewaita ‘Mabwana wa vijana wa Peponi.’
Hizi zote ni dalili wazi juu ya heshima tunayowapa watu wa nyumba hii
tukufu (Radhiya Llahu anhum).
Anasema Ayidh Al Qar’niy katika kitabu ‘Mawaddat Ahlil Bayt inda
Ahlis Sunnah:
«Sisi tunawaheshimu na tunawaenzi watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), lakini hatuamini kama wanavyoamini Shia
kuwa wao wanajua elimu ya Ghaibu na wamekingwa hawafanyi makosa nk. Tunaamini
kuwa mwenye kujuwa ghaibu ni Mwenyezi Mungu peke yake.
Mwenyezi Mungu anasema:
Þá áÇ íÚáã ãä Ýí ÇáÓãæÇÊ
æÇáÃÑÖ ÇáÛíÈ ÅáÇ Çááå" [Çáäãá: 65]
Sema: “Hakuna aliyeko katika mbingu na ardhi ajuaye
Ghayb (yasiyotokea) ila Mwenyezi Mungu."
An Naml-65
Na akasema:
Þá áÇ
Ããáß áäÝÓí äÝÚÇ æáÇ ÖÑÇ ÅáÇ ãÇ ÔÇÁ Çááå æáæ ßäÊ ÃÚáã ÇáÛíÈ áÇÓÊßËÑÊ ãä ÇáÎíÑ
æãÇ ãÓäí ÇáÓæÁ Åä ÃäÇ ÅáÇ äÐíÑ æÈÔíÑ áÞæã íÄãäæä
Sema: “Sina mamlaka ya kujipa nafuu wala ya kujindolea
madhara ila apendavyo Mwenyezi Mungu; na lau kama ningelijua ghaibu
ningejizidishia mema mengi; wala isingalinigusa dhara. Mimi si chochote ila ni
muonyaji na mtoaji wa habari njema kwa watu wanaoamini.”
Al Aaraf-188
«Na tunaamini kuwa aliyekingwa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) peke yake.
Mwenyezi Mungu anasema:
æóÇááøåõ íóÚúÕöãõßó ãöäó ÇáäøóÇÓö
“Na Mwenyezi Mungu amekukinga“
Al
Maidah-67
Sisi tunaamini kuwa hapana yeyote aliyekingwa (Maaswum
ãÚÕæã), si katika watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) wala katika Masahaba wake, kwa sababu zifuatazo:-
1.
Hapana nassi iliyo
wazi isiyopingika inayoeleza juu ya kukingwa kwao. Lau kama ingekuwepo basi
tungelifuata bila matatizo wala kipingamizi.
2.
Hapana hata mmoja katika watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) aliyedai kuwa
yeye amekingwa, akawataka watu waamini hivyo, isipokuwa katika vitabu ambavyo
maulamaa wote kama vile Ibni Kathiyr na Ibni Hajar na Adhahaby na wengineo
wamesema kuwa hadithi hizo si dhaifu tu, bali maudhui. (zimepachikwa).
3.
Hapana hata mwanachuoni mmoja katika maulamaa wetu aliyesema hivyo, juu
ya kukhitalifiana kwao katika mambo mengi, lakini juu ya jambo hili hapana
hitilafu baina yao.
4.
Lau kama wangelikuwa wamekingwa, basi wasingelikubali kukosolewa na mtu
yeyote katika Ijtihadi zao. Kwa mfano kama Aly (Radhiya Llahu anhu) angelikuwa
amekingwa, basi asingelikubali kukosolewa na Abubakar au Umar au Uthman
(Radhiya Llahu anhum), na anapokosolewa angelisema kwa mfano; ‘Vipi
mnanikosoa wakati mimi nimekingwa?’
Lakini Aly alikuwa akiwakosoa na wao walikuwa wakimkosoa, akiwaheshimu
na wao wakimuheshimu, akiwapenda na wao wakimpenda.
5.
Maulamaa wanasema kuwa ÇáÊØåíÑ ‘kusafishwa’ kama ilivyokuja katika aya, maana
yake si kukingwa, bali ni kusafishwa na kutakaswa. Na si kila aliyetakaswa amekingwa akawa hafanyi
makosa, ama sivyo basi kila aliyesifiwa kuwa ametakaswa au amesafishwa atakuwa
amekingwa. Kama ilivyokuja katika hadithi:
æÇÌÚáäí ãä ÇáÊæÇÈíä æÇÌÚáäí ãä ÇáãÊØåÑíä
Na unijaalie niwe miongoni mwa waliotubu na unijaalie
niwe miongoni mwa wenye kujitakasa.
Na Mwenyezi Mungu anawapenda
wenye kutubu na anawapenda wenye kujitakasa, lakini haimaanishi kuwa hao
wamekingwa hawafanyi makosa.
6.
Kama Muislamu atachukua elimu yake kutoka katika Qurani na Mafundisho ya
Mtume wake (Swallah Llahu alayhi wa sallam) peke yake bila ya kuchukua kutoka
kwa watu wa Ahlul Bayt, huyo Uislamu wake unakuwa sahihi na hauna dosari
yoyote. Wangelikuwa Ahlul Bayt wamekingwa ‘Maasumiyn’, basi ingelimuwajikia
kila Muislamu kuchukua elimu kutoka kwao.
7.
Kwetu Ahlus Sunnah, Abubakar na Umar ni viumbe bora kupita wote baada ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah
Llahu alayhi wa sallam). Na Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) mara zote
alikuwa akiwatanguliza mbele ya Aly. Alikuwa akimuacha Abubakar aswalishe na
Aly akiswali nyuma yake, na hapana hata mmoja katika Ahlis Sunnah aliyewahi
kusema kuwa Abubakar amekingwa (Maaswum
ãÚÕæã). Itakuwaje basi awe mwengine
asiyekuwa yeye?
8.
Imepokelewa kuwa Aly (Radhiya Llahu anhu) aliwasifia waliojitenga katika
vita vya wenyewe kwa wenyewe, na alijuta kwa yaliyotokea katika vita vya ngamia
na vita vya Swiffiyn. Angelikuwa amekingwa asingetenda matendo kisha akajuta.
9.
Imepokelewa kuwa Aly (Radhiya Llahu anhu) alipanda juu ya membari katika
mji wa Al Kufa akasema:
«Namshitakia Allah dhiki zangu na matatizo yangu.» Kisha akasema:
«Wana daraja zao kwa Mwenyezi Mungu Muhammad bin
Maslamah na Usama bin Zeyd na Saada bin Abi Waqaas. Kama ni shari basi ndogo,
na kama ni kheri basi ni nyingi (kwa kujitenga kwao na fitna).»
Naye ni mkweli (Radhiya Llahu anhu), lakini angelikuwa Maasuwm
basi asingetamka haya. Asingewasifia waliojitenga na fitna ile wakati yeye mwenyewe alikuwemo
ndani yake.
10.
Siku ya Saqiyfah, siku ile baada
ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kufariki dunia,
wakati Waislamu walipojumuika na kumchagua Abubakar kuwa Khalifa wao, hapana
hata mmoja aliyejitokeza akasema : «Jamani tunaye aliyekingwa hapa, kwa
hivyo yeye ndiye anayestahiki kuchaguliwa.» Hilo halijatokea, na siku ile
walikuwepo waliopigana vita vya Badar na pia walikuwepo wale ambao Mwenyezi
Mungu alitangaza kuridhika nao chini ya mti. Inaingia akilini kweli kuwa watu
wote hao waliosifiwa na Mwenyezi Mungu ndani ya Qurani tukufu, na wakasifiwa na
Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) wafanye njama dhidi ya Mwenyezi Mungu na
Mtume wake (Swallah Llahu alayhi wasallam)?
(Mwisho wa maneno ya Ayidh Al
Qar’niy)
Mawaddat Ahlil Bayt inda Ahlis
Sunnah Uk.317-322
Tunaweza kugawa fadhila za Ahlul Bayt katika mafungu
mawili:-
1.
Fadhila
za ujumla
2.
Fadhila
makhsusi
Fadhila za
ujumla mfano wa hadithi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) aliposema:
{ æÃåá ÈíÊí¡ ÃÐßÑßã Çááå Ýí Ãåá ÈíÊí¡ ÃÐßÑßã Çááå Ýí Ãåá ÈíÊí
}.
«Na watu wa nyumba yangu. Nakukumbusheni Mwenyezi
Mungu juu ya watu wa nyumba yangu, Nakukumbusheni Mwenyezi Mungu juu ya watu wa
nyumba yangu.»
Muslim
Na fadhila
zilizotajwa katika Surat al Ahzab:
ÅöäøóãóÇ íõÑöíÏõ Çááøóåõ áöíõÐúåöÈó Úóäßõãõ ÇáÑøöÌúÓó Ãóåúáó
ÇáúÈóíúÊö æóíõØóåøöÑóßõãú ÊóØúåöíÑÇð
"Hakika
Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu, enyi Watu wa Nyumba (ya Mtume), na
kukusafisheni baarabara."
Ndani yake fadhila hizi wanaingia wake wa Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kwa sababu wao ndio
waliokusudiwa, na pia wanaingia Sayiduna Aly na Bibi Fatima na Al Hassan na Al
Hussayn (Radhiya Llahu anhum) kupitia hadithi ya Al Kisaa.
Fadhila za ujumla zinapatikana pia katika kutoa shahada
ndani ya Swala wakati wa kusoma Tahiyatu, tunaposema:
Çááåã Õá Úáì ãÍãÏ æÚáì Âá ãÍãÏ
"Mola wangu mswalie
Muhammad na Aali yake Muhammad”
Na yote haya yanatokana na fadhila zao na daraja yao
mbele ya Mwenyezi Mungu.
Wafuatao ni baadhi ya watu wa nyumba ya
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na hawa ni maimamu
kumi na mbili wa Shia:-
1.
Aly bin Abu Talib
2.
Al Hassan
3.
Al Hussayn
4.
Aly bin Al Hussayn (Zeinul Abedeen)
5.
Muhammad bin Aly bin Al Hussayn (Al Baqer)
6.
Jaafar Al Sadeq
7.
Musa Al Kadhim
8.
Aly Ridha
9.
Muhammad Al Jawaad
10.
Aly Al Haadi
11.
Al Hassan Al Askary
12.
Muhammad (Imam wa kumi na mbili wanayemsubiri)
Hawa tunaweza kuwagawa makundi manne.
1-
Kundi la mwanzo ni Masahaba (waliomuona Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam)), nao ni Aly na Al Hassan na Al Hussayn
(Radhiya Llahu anhum).
2-
Kundi la pili ni maulamaa wacha Mungu miongoni mwa
maulamaa wa Ahlis Sunnah wal Jama’a nao ni:
|
1-Aly bin al Hussayn |
2-Muhammad Al
Baqer |
|
3-Jaafar al
Sadeq |
4-Musa Al
Kadhem |
|
5-Ali Ridha |
6-Muhammad Al Jawaad |
3-
Kundi la tatu; hawa ni wacha Mungu lakini si katika
maulamaa na inawatosha fahari ya kuwa wanatoka katika nyumba ya Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), na wanayo haki ya kwenda penye
kaburi la Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na kusema:
‘Assalaam alayka ewe baba yangu.’
Na hawa ni: Aly Al Haadi na Al Hassan Al
Askary.
4-
Sehemu ya nne ni mtu asiyezaliwa wanayemsubiri, naye ni
Muhammad bin Al Hassan.
Wa mwanzo wao ni Aly bin Abu Talib (Radhiya Llahu anhu) ambaye ni mtoto
wa ami yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na mume wa
Bibi wa mabibi wa Peponi Fatima (Radhiya Llahu anha) binti wa Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam). Na Aly (Radhiya Llahu anhu) ni Khalifa
wa nne muongofu, na ni katika wale kumi waliobashiriwa kuingia Peponi.
Ndani ya Bukhari na Muslim ipo hadithi kutoka kwa Abul Abbas Sahal bin
Saad Al Saidiy (Radhiya Llahu anhu), aliyesema kuwa siku ya vita vya Khaibar,
Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) alisema:
(áÃÚØíä åÐå ÇáÑÇíÉ ÛÏÇ ÑÌáÇ íÝÊÍ Çááå Úáì
íÏíå¡ íÍÈ Çááå æÑÓæáå æíÍÈå Çááå æÑÓæáå)
"Nitampa bendera hii kesho, mtu ambaye atatupa
ushindi Mwenyezi Mungu kwa mikono yake. (Mtu huyo) Anampenda Mwenyezi Mungu na
Mtume wake na anapendwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake".
Anaendelea kusema Sahal (Radhiya Llahu anhu):
"Usiku kucha watu walikuwa wakiwaza wakitaka
kujua ni nani huyo mwenye kupendwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake atakayepewa
bendera hiyo. Asubuhi yake watu wote wakaamkia kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam), kila mmoja akitamani apewe yeye bendera siku
hiyo".
Baada ya watu kujikusanya mbele yake, Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akauliza:
"Yuwapi Aly bin Abi Talib?...."
Bukhari na Muslim
Na akasema pia (Swallah Llahu alayhi wa sallam) juu ya Aly (Radhiya
Llahu anhu):
áÇ íÍÈß ÅáÇ ãÄãä¡ æáÇ íÈÛÖß ÅáÇ ãäÇÝÞ
«Hakupendi isipokuwa muumini na hakuchukii isipokuwa
mnafiki »
Na sisi Wallahi tunampenda na kumuenzi na kumheshimu yeye na mkewe na
watoto wake wote (Radhiya Llahu anhum). Hadithi zake zimejaa ndani ya vitabu
vyetu. Hekima yake tunaitumia na tunawafunza watoto wetu. Mashairi yake
yaliyojaa mafunzo ya kheri na busara tunayasoma na kuyarudia na tunamfunza kila
mmoja wetu.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema pia:
{ÃãÇ ÊÑÖì Ãä Êßæä ãäí ÈãäÒáÉ åÇÑæä ãä ãæÓì}
æÒÇÏ ãÓáã: { ÅáÇ Ãäå áÇ äÈí ÈÚÏí}
Bukhari
«Hutoridhika
ukiwa wewe kwangu upo katika daraja ya Harun kwa Musa» na Muslim akaongeza: «Isipokuwa
hapana Mtume baada yangu».
Hadithi zote hizi na nyingi nyingine zimo ndani ya vitabu vya Ahlis
Sunnah zikituhakikishia kuwa hatuna uzito wowote kwetu katika kuzitaja au
kuziandika ndani ya vitabu vyetu na hata kuzisema hadharani, bali ni fahari
kwetu kufanya hivyo, kwa sababu hawa ni watu wa nyumba ya Mtume wetu Muhammad
(Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Bibi Fatima (Radhiya Llahu anha) binti yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah
Llahu alayhi wa sallam). Kipenzi chake (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Manukato yake mazuri aliyesema juu yake :
{Åä ÝÇØãÉ ÈÖÚÉ ãäí íÄÐíäí ãÇ ÂÐÇåÇ}
«Hakika Fatima ni sehemu inayotokana na mimi
kinaniudhi kinachomuudhi»
Muslim
Na akasema kumuambia Fatima:
{ÃãÇ ÊÑÖí Ãä Êßæäí ÓíÏÉ äÓÇÁ ÇáãÄãäíä¡ Ãæ ÓíÏÉ
äÓÇÁ åÐå ÇáÃãÉ}
«Huridhiki ukiwa wewe ni Bibi wa wanawake waumini, au
Bibi wa wanawake wa umma huu»
Na katika Bukhari :
ÝÇØãÉ ÓíÏÉ äÓÇÁ Ãåá ÇáÌäÉ
« Fatima ni Bibi wa wanawake wa Peponi»
Tunawaheshimu na kuwapenda pia Al Hassan na Al Hussayn (Radhiya Llahu
anhum), na ndani ya vitabu vya Ahlus Sunnah utakuta maelezo mengi juu ya
wajukuu hawa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) aliyokuwa
akitamka mbele ya Masahaba (Radhiya Llahu anhum). Alikuwa akisema:
Çááåã Åäí ÃÍÈåãÇ ÝÃÍÈåãÇ
‘Mola wangu kwa hakika mimi ninawapenda na Wewe
wapende’
Attirmidhiy
Na akasema:
ÇáÍÓä æÇáÍÓíä ÓíÏÇ ÔÈÇÈ Ãåá ÇáÌäÉ
‘Al Hassan na Al Hussayn ni mabwana wa vijana wa
Peponi’
Attirmidhy na Ahmad na Al Hakim na wengine
Huyu ni ami yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah llahu alayhi wa
sallam) aliyesema juu yake:
Úã ÇáÑÌá Õäæ ÃÈíå
‘Ami yake mtu ni sawa na baba yake
Attirmidhy
Huyu ni mtoto wa ami yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam) aliyemuombea dua nzuri aliposema:
{Çááåã Úáãå ÇáÊÃæíá æÝÞåå Ýí ÇáÏíä}
“Mola wangu mpe elimu ya kujuwa uhakika wa mambo na mjaalie
awe na fiq-hi katika dini."
Ahmad
Huyu ni Aly bin Al Hussayn bin Aly bin Abi Talib (Radhiya Llahu anhum)
ambaye amesema Imam Al Zuhry juu yake:
‘Sijapata kumuona mtu kutoka kabila la Quraysh aliye
bora kupita yeye.’
Na alisema Said bin Musayib:
‘Sijapata kumuona mcha Mungu kupita huyu.’
Amesema juu yake Abu Naeem:
‘Alikuwa mtu wa kuaminika, mwingi wa elimu na
hadithi.’
Huyu ndiye Jaafar As Sadeq bin Muhammad Al Baqer ambaye Imam Abu Hanifa
alisema juu yake :
‘Sijapata kuona mtu mwenye elimu ya fiq’hi kupita
Jaafar bin Muhammad.’
Amesema pia juu yake Ibni Hibban :
‘Mwenye kuaminika asiye na mfano.’
Amesema Imam Adhahaby :
« Imam As Sadeq ni Shekhe katika Mashekhe wa
Kikureshi anayetokana na ukoo wa Bani Hashim na ni miongoni mwa maulamaa wao.»
Huyu ni mtoto wa Jaafar As Sadeq (Radhiya Llahu anhu)
Amesema juu yake Ibni Tayimiyah:
« Mashuhuri kwa kufanya ibada na kuhiji.»
Akasema Abu Hatim Al Razi:
« Ni mwenye kutegemewa msemakweli, Imam katika
maimamu wa Kiislamu.»
Amesema juu yake Ibni Kathiyr:
« Alikuwa mwingi wa kufanya ibada na mwenye
kuheshimika.»
Anasema Adhahaby katika ‘Siyar’ kuwa
siku moja Harun Al Rashiyd alipokuwa katika Hija alikwenda mbele ya kaburi la
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na alikuwa pamoja naye
katika safari hiyo Musa bin Jaafar Al Kadhim (Radhiya Llahu anhu). Harun Al
Rashiyd alipofika penye kaburi la Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi
wa sallam) akasema kwa ufahari mbele ya watu: “Assalaam alayka ewe mtoto wa ami yangu.” Harun Al Rashiyd
anatokana na ukoo wa Al Abbas bin Abdul Muttalib (Radhiya Llahu anhu). Musa bin
Jaafar naye akasogea mbele ya kaburi hilo kisha akasema: “Assalaam
alayka ewe baba yangu.”
Uso
wa Harun Al Rashiyd ulibadilika. Akamtizama kisha akamuambia: “Hili
Wallahi ni la kujionea fahari.”
Amesema juu yake Ibni Hibban:
« Huyu ni miongoni mwa mabwana wa Ahlul Bayt
na katika wenye hekima.»
Na Adhahaby amesema juu yake :
« Alikuwa mwenye shani kubwa mwenye kustahiki
ukhalifa.»
Amesema juu yake Ibni Taymiyah:
«Alikuwa miongoni mwa watu wema na mkarimu sana, na
kwa ajili hii alipewa jina la Al Jawaad. Na alikuwa mwenye kuheshimika sana.»
Yote haya yanabatilisha zile kauli kuwa Masunni hawawapendi watu wa
nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Alipotuhumiwa Abdullah mwana wa Imam Muhammad bin Abdul Wahaab kwamba alisema
kuwa watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
hawana haki yoyote” akajibu:
“Subhana Llah huu ni uongo mkubwa. Waliotuzulia
haya au kutunasibisha nayo wamesema uongo mtupu juu yetu.”
Na hivi ndivyo ilivyo kwa wote wanaotokana na ukoo wa Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na pia wajukuu wote wa Sayiduna Aly
(Radhiya Llahu anhu), wote tunawapenda bila kuwafarikisha na wote wamepewa sifa
wanazozistahiki ndani ya vitabu vya Sunni ikiwa ni dalili wazi kuwa watu hawa
tunawaenzi na kuwaheshimu.
Shia juu ya kudai kwao kuwa wanawapenda na kufuata mwenenendo wa watu wa
nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), lakini ukweli
ni kuwa wao wanawafarikisha na kuwatenga wengine. Kwa sababu watu wa nyumba ya
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kwao ni Aly na Fatima
na Al Hassan na Al Hussayn na watoto wao na wajukuu zao peke yao, na wengine
wasiokuwa hao wamewatoa katika sifa hii.
Aly (Radhiya Llahu anhu) alioa wake wengine akazaa nao watoto wengi,
lakini Mashia hawahesabu watoto hao kuwa
ni Ahlul Bayt.
Watoto wengine wa Aly (Radhiya Llahu anhu) kama vile Muhammad bin Al
Hanafiyah, Abubakar bin Aly, Umar bin Aly na Uthman bin Aly na Abbas, wote hawa
ni watoto wa Sayiduna Aly (Radhiya Llahu anhu).
Wamewatoa pia mabinti wengine wa Aly kama walivyowatoa mabinti wengine
wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), nao ni Zeinab na
Ruqayah na Ummu Kulthum, kama walivyowatoa wake wa Mtume (Swallah Llahu alayhi
wa sallam) hapo mwanzo.
Sisi
tunaamini kuwa wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
ni katika watu wa nyumba yake, na kwamba wao ni mama zetu.
Mwenyezi
Mungu anasema:
(( ÇáäøóÈöíøõ Ãóæúáóì ÈöÇáúãõÄúãöäöíäó ãöäú
ÃóäúÝõÓöåöãú æóÃóÒúæóÇÌõåõ ÃõãøóåóÇÊõåõãú ))[ÇáÃÍÒÇÈ:6]
«Nabii
ana haki zaidi kwa Waislamu kuliko nafsi zao.na wakeze ni mama zao.»
Al
Ahzab -6
Na
akaharamisha kuwaoa baada ya kufariki Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam).
Mwenyezi
Mungu anasema:
(( æóãóÇ ßóÇäó áóßõãú Ãóäú ÊõÄúÐõæÇ ÑóÓõæáó
Çááøóåö æóáÇ Ãóäú ÊóäúßöÍõæÇ ÃóÒúæóÇÌóåõ ãöäú ÈóÚúÏöåö ÃóÈóÏðÇ))
«Wala
haikupasieni kumuudhi Mtume wa Mwenyezi Mungu. Wala kuwaoa wake zake baada yake
kabisa. Hakika jambo hilo ni dhambi kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.»
Al
Ahzab-53
Tunawapa
heshima kubwa mama zetu hawa, na wa mwanzo wao ni Bibi Khadija (Radhiya Llahu
anha. Wa mwanzo kuamini, aliyemsaidia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) kwa hali na mali huku akimpa moyo na kumliwaza kila
anapopatwa na masaibu au shida. Bibi Khadija ndiye aliyeambiwa na Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam):
"Åä Çááøå
ÃãÑäí Ãä ÃÈÔÑ ÎÏíÌÉ ÈÈíÊ Ýí ÇáÌäÉ áÇ ÕÎÈ Ýíå æáÇ äÕÈ"
“Mwenyezi
Mungu ameniamrisha nimpe bishara njema Khadija juu ya nyumba yake Peponi ya
Lulu, hamna zogo ndani yake wala tabu (yoyote).”
Bukhari
na Muslim
Na
kutoka kwa Aly bin Abi Talib (Radhiya Llahu anhu) kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema:
ÎíÑ äÓÇÆåÇ ãÑíã ÈäÊ ÚãÑÇä¡ æÎíÑ äÓÇÆåÇ ÎÏíÌÉ ÈäÊ ÎæíáÏ
«Mwanamke
bora (katika zama zake) ni Maryam binti Imran, na mwanamke bora (katika zama zake)
ni Khadija binti Khuwaylid»
Bukhari
na Muslim
Kisha
anafuatia Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha), binti wa Abubakar Al Siddique
(Radhiya Llahu anhu), Bibi aliyetakaswa kutoka mbingu ya saba baada ya mnafiki
yule aliyejitwika sehemu yake kubwa katika uzushi wake ambaye ni Abdullahi bin
Ubay bin Saluul kueneza uvumi mbaya juu ya mama huyu wa Waislamu kipenzi cha
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Maulamaa wote wamekubaliana
kuwa kumsingizia uwongo bibi Aisha (Radhiya Llahu anha) katika kile kisa cha
uwongo alichozuliwa (hadithi ya "Al-Ifki") wakati
MwenyeziMungu kishamtakasa, basi anakuwa si Muislamu tena.
MwenyeziMungu anasema:-
Åöäøó ÇáøóÐöíäó ÌóÇÄõæÇ ÈöÇáúÅöÝúßö
ÚõÕúÈóÉñ ãøöäßõãú áóÇ ÊóÍúÓóÈõæåõ ÔóÑøÇð áøóßõã Èóáú åõæó ÎóíúÑñ
áøóßõãú áößõáøö ÇãúÑöÆò ãøöäúåõã ãøóÇ ÇßúÊóÓóÈó ãöäó ÇáúÅöËúãö æóÇáøóÐöí
Êóæóáøóì ßöÈúÑóåõ
ãöäúåõãú áóåõ ÚóÐóÇÈñ ÚóÙöíãñ {11} áóæúáóÇ ÅöÐú ÓóãöÚúÊõãõæåõ Ùóäøó
ÇáúãõÄúãöäõæäó
æóÇáúãõÄúãöäóÇÊõ ÈöÃóäÝõÓöåöãú ÎóíúÑÇð æóÞóÇáõæÇ åóÐóÇ
ÅöÝúßñ ãøõÈöíäñ {12} áóæúáóÇ
ÌóÇÄõæÇ Úóáóíúåö ÈöÃóÑúÈóÚóÉö ÔõåóÏóÇÁ
ÝóÅöÐú áóãú íóÃúÊõæÇ ÈöÇáÔøõåóÏóÇÁ ÝóÃõæúáóÆößó ÚöäÏó
Çááøóåö åõãõ ÇáúßóÇÐöÈõæäó {13} æóáóæúáóÇ ÝóÖúáõ Çááøóåö Úóáóíúßõãú
æóÑóÍúãóÊõåõ
Ýöí ÇáÏøõäúíóÇ æóÇáúÂÎöÑóÉö áóãóÓøóßõãú Ýöí ãóÇ
ÃóÝóÖúÊõãú Ýöíåö ÚóÐóÇÈñ ÚóÙöíãñ {14} ÅöÐú ÊóáóÞøóæúäóåõ ÈöÃóáúÓöäóÊößõãú æóÊóÞõæáõæäó
ÈöÃóÝúæóÇåößõã ãøóÇ áóíúÓó áóßõã Èöåö Úöáúãñ æóÊóÍúÓóÈõæäóåõ
åóíøöäÇð æóåõæó ÚöäÏó Çááøóåö ÚóÙöíãñ {15} æóáóæúáóÇ ÅöÐú ÓóãöÚúÊõãõæåõ ÞõáúÊõã
ãøóÇ íóßõæäõ áóäóÇ Ãóä äøóÊóßóáøóãó ÈöåóÐóÇ ÓõÈúÍóÇäóßó åóÐóÇ ÈõåúÊóÇäñ ÚóÙöíãñ {16} íóÚöÙõßõãõ
Çááøóåõ Ãóä ÊóÚõæÏõæÇ áöãöËúáöåö ÃóÈóÏÇð Åöä ßõäÊõã ãøõÄúãöäöíäó {17}
æóíõÈóíøöäõ Çááøóåõ áóßõãõ ÇáúÂíóÇÊö æóÇááøóåõ Úóáöíãñ
Íóßöíãñ {18} Åöäøó ÇáøóÐöíäó
íõÍöÈøõæäó Ãóä ÊóÔöíÚó ÇáúÝóÇÍöÔóÉõ Ýöí ÇáøóÐöíäó
ÂãóäõæÇ áóåõãú ÚóÐóÇÈñ Ãóáöíãñ
Ýöí ÇáÏøõäúíóÇ æóÇáúÂÎöÑóÉö æóÇááøóåõ íóÚúáóãõ
æóÃóäÊõãú áóÇ ÊóÚúáóãõæäó {19} æóáóæúáóÇ ÝóÖúáõ Çááøóåö Úóáóíúßõãú æóÑóÍúãóÊõåõ æóÃóäøó Çááøóå
ÑóÄõæÝñ ÑóÍöíãñ {20}þ
"Hakika
wale walioleta uwongo huo (wa kumsingizia bibi AishaRadhiya Llahu anha) mkewe
Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kuwa amezini)) Ni kundi miongoni mwenu
(ni jamaa zenu) msifikiri ni shari kwenu bali hiyo ni kheri kwenu. Kila mtu
katika wao atapata aloyachuma katika madhambi yao na yule aliyejitwika sehemu
yake kubwa miongoni mwao atapata adhabu kubwa (zaidi).
Kwa nini mlipo
sikia khabari hii, wanaume Waumini na wanawake Waumini hawakuwadhania wenzao
mema, na kusema: Huu ni uzushi dhaahiri?
Kwa nini
hawakuleta mashahidi wane? Na ilivyo kuwa hawakuleta mashahidi wane basi hao
mbele ya Mwenyezi Mungu ni waongo.
Na lau kuwa
si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenu na rehema yake katika dunia na
Akhera, bila
ya shaka ingeli kupateni adhabu kubwa kwa sababu ya yale mliyo jiingiza.
Mlipoupokea (uwongo huo mkawa mnautangaza) kwa ndimi zenu na mkasema kwa vinywa
vyenu msiyo yajua, na mlifikiri ni jambo dogo, kumbe mbele ya Mwenyezi Mungu ni
kubwa.
Na kwa nini
mlipo yasikia msiseme: Haitufalii kuzungumza haya. Subhaanaka (Mola wetu)
Umetakasika! Huu ni uzushi mkubwa!?
Mwenyezi
Mungu anakuonyeni msirudi kabisa (msirejee tena) kufanya kama haya, ikiwa
nyinyi ni Waumini! (Waislamu) kweli.”
An Nur– 11-17
Mwenyezi Mungu Subhanahu wa
Taala katika aya hizi ametumia neno; ‘Subhaanaka’ katika kumtakasa Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha)
kutokana na uwongo aliozuliwa, na neno hili ‘Subhanaka’
Mwenyezi Mungu analitumia katika kukanusha uongo mkubwa tu, Anaponasibishwa na
mwana au mshirika.
Mwenyezi Mungu amesema:
ÓõÈúÍóÇäóßó åóÐóÇ ÈõåúÊóÇäñ ÚóÙöíãñ
(Mola wetu)
Umetakasika! Huu ni uzushi mkubwa!?’
Anasema Az Zamakhshary:
“Alipokanusha kuwa hana
mwana wala mshirka alisema:
æóÞóÇáõæÇú ÇÊøóÎóÐó Çááøåõ
æóáóÏÇð ÓõÈúÍóÇäóåõ Èóá áøóåõ ãóÇ Ýöí ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖö
ßõáøñ áøóåõ ÞóÇäöÊõæäó
“Na
wanasema:”Mwenyezi Mungu amejifanyia mtoto” ‘Subhaanahu’ Ameepukana na hilo bali ni vyake hivyo vilivyomo
mbinguni na ardhini . Vyote vinamtii Yeye.”
Al Baqarah-116
Na akasema:
ãóÇ ßóÇäó áöáøóåö Ãóä íóÊøóÎöÐó
ãöä æóáóÏò ÓõÈúÍóÇäóåõ
“Haiwi kwa Mwenyezi Mungu
kufanya mtoto; ‘Subhanahu’
Ametakasika.”
Maryam-35
Amelitumia
neno ‘Subhanahu’ kwa ajili ya kujitakasa na kukanusha
kuwa anaye mwana, na amelitumia neno hilo hilo ‘Subhanahu’
katika kuukanusha uwongo aliozuliwa Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha).
Miongoni mwa wake wa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) pia ni Ummu Salamah (Radhiya
Llahu anha), mama yetu mtulivu wa tabia, mwenye akili yenye uwezo wa kupima
mambo, mwingi wa hekima ambaye Mtume (Swallah Llahu alayhi wa sallam) mara
nyingi alikuwa akichukuwa ushauri wake katika baadhi ya mambo. Alimshauri siku
ile ya Sulhu ya Hudaibiya na akapata ushauri mwema kutoka kwake.
Hawa na wake zake wengine
wote ni mama zetu. Ni watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) kama ilivyokuja katika aya za Surat al Ahzab, na kama
tulivyoona katika dalili mbali mbali kutoka katika Qurani tukufu na katika
Mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Inatuwajibikia kuwapenda na
kuwaenzi na kuwaheshimu mama zetu hawa.
Baada ya kumalizika vita vya
Ngamia (Waqaat al Jamal), Aly (Radhiya Llahu anhu) aliamua kumuacha huru
Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha). Wafuasi wake wakamuuliza:
«Inakuwaje
halali kumwaga damu zao na haiwi halali kwetu mali zao na mateka wao?»
Aly (Radhiya
Llahu anhu) akasema:
«Yupi kati yenu
atakayefurahi Mama wa Waislamu awe mateka wake?»
Wote wakanyamaza.
Ikiwa ni haramu kumsema vibaya
Muislamu yeyote, basi inakuwa vibaya zaidi kuwasema vibaya watu wa nyumba ya
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) wakiwemo wake zake na
watu wa ukoo wake pamoja na wajukuu wake na wajukuu wa wajukuu wakiwemo Al
Hassan na Al Hussayn na Abdullah bin Al Hassan na Aly bin Al Hassan na Muhammad
bin Alyn a Jaafar bin Muhammad na Musa bin Jaafar na Aly bin Musa Al Ridha na
waliobaki, na pia Sahaba zake (Radhiya Llahu anhum) wote kwa pamoja wa Makkah
na wa Madina, na wale ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa
sallam) amewabashiria Pepo, na pia viongozi wetu wa dini.
Haiwezekani ukapatikana umoja wa
Waislamu ikiwa kundi lolote litakuwa shughuli yao kubwa ni kuweka vikao vya
kila mwaka kuwalani na kuwatukana Watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swallah Llahu alayhi wa sallam) wakiwemo wake zake, au Sahaba zake (Radhiya
Llahu anhum), kwa sababu hawa ni viongozi wetu waliokuwa naye tokea siku ile ya
mwanzo. Hawa ni mifano mema kwetu, walioisimamia dini hii na kuieneza
ulimwenguni kote, na hawa ndio waliotufikishia dini hii baada ya kujitolea mhanga
roho zao na mali zao.
Wakati huo huo sisi tunaamini
kuwa watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
wanatoka katika nyumba bora kupita zote, lakini pia tunaamini kuwa hapana
ajuaye Ghaybu isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake.
Mwenyezi Mungu anasema:
(( Þõáú áÇ íóÚúáóãõ ãóäú Ýöí ÇáÓøóãóæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖö
ÇáúÛóíúÈó ÅöáøóÇ Çááøóåõ ))[Çáäãá:65].
“Sema:
‘Hakuna aliyoko katika mbingu na ardhi ajuaye Ghayb ila Mwenyezi Mungu.”
An Naml-65
Na anasema:
(( æóÚöäúÏóåõ ãóÝóÇÊöÍõ ÇáúÛóíúÈö áÇ íóÚúáóãõåóÇ
ÅöáøóÇ åõæó ))[ÇáÃäÚÇã:59]
“Na ziko
Kwake (Mwenyezi Mungu tu) funguo za siri (Ghayb) hakuna azijuaye ila Yeye tu.”
Al An-Am-59
Katika kamusi la lugha ya Kiarabu, neno ‘Sahaba’, maana
yake ni Rafiki, Mwenzi wake, Sahibu nk.
Katika dini, neno ‘Sahaba’ maana yake ni Mwislamu
aliyemuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), akamfuata
na kumuamini na akafariki katika imani hiyo.
Na hii ina maana kuwa, yeyote aliyewahi kumouna Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na asimuamini, basi hawezi
kuingia katika maana ya neno ‘Sahaba’.
Katika kamusi la lugha ya kiarabu, neno ‘Mnafiki’ maana
yake ni mtu mwenye kigeugeu au mwenye kuwa na sura mbali mbali: Leo hivi kesho
vile.
Katika dini, neno ‘Mnafiki’ maana yake ni yule
anayejidhihirisha kuwa ni Muislam na kumfuata Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam), wakati undani wake ni kafiri na adui wa Mwenyezi Mungu
na adui wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
Baada ya tafsiri hii fupi ya nani Sahaba na nani Mnafiki,
tutakubaliana kuwa maneno hayo mawili hayawezi kuwa na maana moja, (hayawezi
kwenda sambamba) Kilugha wala Kidini.
Kwa sababu Sahaba ni yule aliyemuamini Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akafariki dunia akiwa Muislam, wakati
Mnafiki ni mwenye kujidhihirisha kama ni Mwislam wakati ndani ya nafsi yake ni
kafiri.
Kwa hivyo haiwezekani Sahaba akawa Mnafiki na wala
Mnafiki hawezi akawa Sahaba.
Sasa Mtu anaweza kuuliza:
'Vipi tutaweza kutofautisha baina ya Sahaba na Mnafiki?'
Majibu:
Mnafiki ana sifa na alama maalum tulizojulishwa katika
Qurani na katika Mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam), na kwa ajili hiyo tunaweza kutofautisha baina yake na Sahaba.
Wanafiki ni watu;
‘Wanaoeneza ufisadi ardhini, kuifanyia istihzai dini,
kuwafanyia istihzai wacha Mungu, ni wavukaji mipaka katika kufanya maasi wenye kuununua
upotofu (upotevu) kwa uongofu, wavivu katika kufanya ibada, hugeuka geuka, mara
Waislamu mara makafiri, kama alivyosema Mwenyezi Mungu:
ãøõÐóÈúÐóÈöíäó Èóíúäó
Ðóáößó áÇó Åöáóì åóÜÄõáÇÁ æóáÇó Åöáóì åóÜÄõáÇÁ
“Wanayumba yumba baina ya huku (kwa
Waislam) na huko (kwa makafiri). Huku hawako wala huko hawako)”.
Annisaa-143
Na katika sifa
za wanafiki pia ni;
‘Kuwa
hawamwamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Akhera na kwamba Waislam wanapopata
kheri yoyote au mafanikio, wao wanahuzunika, na hufurahi pale Waislamu
wanapopata tabu au wanapokumbwa na masaibu au mitihani.
Huchukizwa na kutoa
mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu na hufurahi wanaporudi nyuma na kumuacha
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) peke yake vitani.
Wameingia katika
dini kwa ajili ya kujikinga wasiambiwe kuwa wao ni makafiri, na wanapenda kuwadhuru
Waislam na kuwafarikisha. Na katika sifa za unafiki ni kuwa; wanaiahirisha swala
mpaka nyakati zake za mwisho na hawahudhurii Swala za jamaa na kwamba wanaionea
uzito kabisa Swala ya Alfajiri na ya Ishaa’.
Hizi ni baadhi
tu ya sifa za Wanafiki alizozitaja Mwenyezi Mungu katika Qurani tukufu, na
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) katika mafundisho yake.
Bila shaka
Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ni watu
walio mbali kabisa na sifa hizi. Hawa ambao Mwenyezi Mungu Amewaambia:
ßõäÊõãú
ÎóíúÑó ÃõãøóÉò ÃõÎúÑöÌóÊú áöáäøóÇÓö ÊóÃúãõÑõæäó ÈöÇáúãóÚúÑõæÝö æóÊóäúåóæúäó
Úóäö ÇáúãõäßóÑö æóÊõÄúãöäõæäó ÈöÇááøåö
“Nyinyi ndio umma bora kuliko umma zote
zilizodhihirishiwa watu (ulimwenguni) mnaamrisha yaliyo mema na mnakataza
yaliyo maovu, na mnamwamini Mwenyezi Mungu”.
Aali Imran- 110
Na Akasema juu
yao:
íÇ ÃíåÇ ÇáäÈí ÍÓÈß Çááå
æãä ÇÊÈÚß ãä ÇáãÄãäíä
“Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mwenyezi
Mungu anakutoshelezea wewe na wale walokufuata katika hao walioamini”.
Al Anfal-64
Na Akasema juu
yao:
ãøõÍóãøóÏñ
ÑøóÓõæáõ Çááøóåö æóÇáøóÐöíäó ãóÚóåõ ÃóÔöÏøóÇÁ Úóáóì ÇáúßõÝøóÇÑö ÑõÍóãóÇÁ
Èóíúäóåõãú ÊóÑóÇåõãú ÑõßøóÚÇð ÓõÌøóÏÇð íóÈúÊóÛõæäó ÝóÖúáÇð ãøöäó Çááøóåö
æóÑöÖúæóÇäÇð
“Muhammad
ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na walio pamoja naye ni wenye nyoyo thabiti mbele
ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao. Utawaona wakiinama kwa kurukuu na
kusujudu (pamoja), wakitafuta fadhila za Mwenyezi Mungu na radhi (yake).”
Al Fat-h- 29
Na Akasema:
æóÇáøóÐöíäó
ÂãóäõæÇú æóåóÇÌóÑõæÇú æóÌóÇåóÏõæÇú Ýöí ÓóÈöíáö Çááøåö æóÇáøóÐöíäó ÂæóæÇú
æøóäóÕóÑõæÇú ÃõæáóÜÆößó åõãõ ÇáúãõÄúãöäõæäó ÍóÞøÇð áøóåõã ãøóÛúÝöÑóÉñ æóÑöÒúÞñ
ßóÑöíãñ
“Na
wale walioamini wakahama (kuja Madina) na wakaipigania dini ya Mwenyezi Mungu
(Nao ni Muhajir); na wale waliowapa (Muhajir) mahala pa kukaa na wakainusuru
dini (ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake).(nao ni Ansar) Hao ndio Waislam wa
kweli. Watapata msamaha (wa Mwenyezi Mungu) na kuruzukiwa kuzuri (kabisa huko
Akhera)”.
Al Anfal – 74.
Masahaba wa
Makka (Radhiya Llahu anhum) ndio walioamini, wakahama, na wakapigana jihadi. Na
Masahaba wa Madina (Radhiya Llahu anhum) ndio waliowapa mahala pa kukaa na
wakainusuru dini.
Baada ya maelezo
haya kutoka kwa Muumba wa mbingu na ardhi, asije mtu akatuambia kuwa Masahaba
na wanafiki ni kitu kimoja. Hakika haya ni matusi makubwa kabisa!
Hawawezi kuwa wanafiki
watu ambao Mwenyezi Mungu Amesema juu yao; “Nyinyi
ndio umma bora kuliko umma zote zilizodhihirishiwa watu (ulimwenguni).”
Hawawezi kuwa
wanafiki watu ambao Mwenyezi Mungu Ameshuhudia kuwa ni “Wenye
nyoyo thabiti mbele ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao. Utawaona
wakiinama kwa kurukuu na kusujudu (pamoja), wakitafuta fadhila za Mwenyezi
Mungu na radhi (yake).”
Hawawezi kuwa
wanafiki watu ambao Mwenyezi Mungu Mwenyewe Anashuhudia kuwa “Hao ndio
Waislam wa kweli.”
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alisema:
"áÇ ÊóÓõÈøæÇ ÃóÕúÍóÇÈöí¡ ÝóæóÇáøÐöí
äóÝúÓöí ÈöíóÏöåö áóæú Ãóäø ÃóÍóÏóßõãú ÃóäúÝóÞó ãöËúáó ÃõÍöÏò ÐóåóÈÇð ãóÇ
ÃóÏúÑóßó ãõÏø ÃóÍóÏöåöãú æóáÇó äóÕöíÝóåõ".
"Msiwatukane
Sahaba wangu. Ninaapa kwa Yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, hata
mmoja wenu atajitolea katika njia ya MwenyeziMungu kugawa dhahabu ukubwa wake
mfano wa jabali Uhud, basi hatofikia gao lao wala hata nusu ya gao lao".
Bukhari na
Muslim
Na akasema:
ãä ÓÈ ÃÕÍÇÈí ÝÚáíå áÚäÉ
Çááå æÇáãáÇÆßÉ æÇáäÇÓ ÃÌãÚíä
“Atakayewatukana
Masahaba wangu, basi itampata laana ya Mwenyezi Mungu na (laana ya) Malaika na
(laana ya) watu wote”.
((Attabariy,
katika ‘Al Kabeer’, Abi Naeem katika ‘Al Hiliya’ na Abi Asim, na hadithi hii
pia inapatikana katika ‘Silsila za hadithi sahihi kilichoandikwa na Sheikh Al
Albani)).
Na akasema
(Swallah Llahu alayhi wa sallam):
“Nihifadhieni
Masahaba wangu, kisha wale waliowafuatilia kisha wale waliofuatilia”.
Imam Ahmad, Ibni
Majah, na Al Haakim.
Ikiwa Masahaba
waliokuwa wengi wanatuhumiwa kuwa ni watu wenye kigeugeu na unafiki, hii
italeta maana kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
hakuweza kuwalea na kuwafundishsa vizuri Masahaba wake (Radhiya Llahu anhum)
wakaijuwa haki, na kwamba yeye ni mlezi asiyefanikiwa, aliyeshindwa kuifanya kazi
yake ya kuwalea Masahaba (Radhiya Llahu anhum).
Haikubaliki
akilini abadan kuwa baada ya kuishi nao muda mrefu wote huo alifanikiwa kuwalea
na kuwafundisha Masahaba watatu tu au wasiozidi saba?
Kila anayesoma
na kuidurusu sira (historia) ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam), anaelewa kwamba wakati Waislam walipokuwa Makka hapakuwa na unafiki,
na hii ni kwa ajili ya adhabu kali walizokuwa wakipata waliosilimu wakati ule.
Na inajulikana pia kwamba unafiki ulianza kujitokeza baada ya Waislam kuhamia
Madina, na baada ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
kupata nguvu, na dini ya Mwenyezi Mungu kuanza kutambulika kila mahala.
Na inaeleweka
pia kwa kila mwenye kuidurusu sira ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) kuwa Abubakar, Umar na Uthman na wengineo ni miongoni mwa Masahaba
walioingia katika dini ya Mwenyezi Mungu tokea siku za mwanzo, wakapata tabu na
shida kama walivyopata wenzao, na hii ni dalili wazi kuwa walikuwa mbali na sifa
ya unafiki.
Mwenyezi Mungu
amewafedhehesha wanafiki kwa kuwateremshia Suratul Munafiqun na At Tawba;
akaelezea ndani ya sura hizo juu ya hali zao na vitimbi vyao; na akatuelezea
yale yaliyofichika nyoyoni mwao katika kuwachukia Waislam, na ndiyo maana Surat
at Tawba ikaitwa 'Sura ya Kufedhehesha'. Katika sura hiyo Mwenyezi Mungu
alitaja pia sifa za Masahaba (Radhiya Llahu anhum) na akatujulisha kuridhika
kwake nao. Na huu ni ushahidi utokao Kwake Subhanahu wa Taala.
Ama Suratul
Munafiqun, hii imeteremshwa kwa ajili ya kutujulisha juu ya mkubwa wa wanafiki
na kiongozi wao aitwae Abdillahi bin Ubay bin Salool na wenzake.
Anasema Zayd bin Al Arqam (Radhiya Llahu anhu):
"Nilikuwa
vitani, nikamsikia Abdillahi bin Ubay akisema:
“Msitoe
mali kuwasaidia waliokuwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu mpaka watakapomwondokea
pale alipo, na tutakaporudi Madina yule mtukufu (akimaanisha yeye Abdillahi bin
Ubay ‘mkuu wa wanafiki’kuwa ni mtukufu) atamtoa (katika mji wa Madina) yule
aliyedhalilika (akimaanisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam kuwa eti ndiye aliyedhalilika)”.
Nikamhadithia
ami yangu hayo niliyoyasikia (au Umar) naye akamhadithia Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam): Akaniita na mimi nikamhadithia. Kisha
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamtuma mtu amuite
Abdillahi bin Ubay pamoja na wenzake, wakaapa na kukanusha yale waliyosema, na
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) hakunisadiki na
akamsadiki yeye. Nikaona dhiki sijapata kuona mfano wake. Nikakaa nyumbani
kwangu, lakini haujapita muda Mwenyezi Mungu akateremsha Suratul Munafiqun,
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamtuma mtu aniite,
akanisomea (Sura hiyo) kisha akaniambia:
“Mwenyezi
Mungu amesadikisha maneno yako ewe Zeyd”.
Bukhari.
Tafsiri hii pia
inapatikana katika kitabu cha tafsiri cha Mashia kiitwacho ‘Maj maa l bayan
fiy tafsiyri l Quran’, kilichoandikwa na Imam Al Tubrusy ambaye ni miongoni
mwa maulamaa wakubwa wa Kishia. Na katika kitabu hicho, ameelezea sababu ya
kuteremshwa Suratul Munafiqun kuwa ni juu ya Abdillahi bin Ubay ‘mnafiki’ na
wenzake …..
(Maj maa l bayan
fiy tafsiyr l Qur an ukurasa 85)
Kisha
Mwanachuoni huyu wa Kishia akazitaja riwaya zile zile alizozielezea Imam
Bukhari zinazothibitisha hoja hiyo.
Inajulikana wazi
kuwa Abdillahi bin Ubay pamoja na wafuasi wake walikuwa wakijulikana na
Masahaba wote (Radhiya Llahu anhum) kuwa ni wanafiki, na mtu yeyote anaposoma Surat
at Tawba ataona kuwa sura hiyo imeelezea juu ya vituko mbali mbali
walivyokuwa wakivifanya wanafiki hao kiasi ambapo ilikuwa ikijulikana wazi
mbele ya kila mtu kuwa wao ndio waliokusudiwa.
Kwa mfano
kuanzia aya ya 44 hadi 49 ya sura hiyo Mwenyezi Mungu anasema:
áÇó
íóÓúÊóÃúÐöäõßó ÇáøóÐöíäó íõÄúãöäõæäó ÈöÇááøåö æóÇáúíóæúãö ÇáÂÎöÑö
Ãóä íõÌóÇåöÏõæÇú ÈöÃóãúæóÇáöåöãú æóÃóäÝõÓöåöãú æóÇááøåõ Úóáöíãñ
ÈöÇáúãõÊøóÞöíäó {44} ÅöäøóãóÇ íóÓúÊóÃúÐöäõßó ÇáøóÐöíäó áÇó íõÄúãöäõæäó ÈöÇááøåö
æóÇáúíóæúãö ÇáÂÎöÑö æóÇÑúÊóÇÈóÊú ÞõáõæÈõåõãú Ýóåõãú Ýöí ÑóíúÈöåöãú
íóÊóÑóÏøóÏõæäó {45} æóáóæú ÃóÑóÇÏõæÇú ÇáúÎõÑõæÌó áÃóÚóÏøõæÇú áóåõ ÚõÏøóÉð
æóáóÜßöä ßóÑöåó Çááøåõ ÇäÈöÚóÇËóåõãú ÝóËóÈøóØóåõãú æóÞöíáó ÇÞúÚõÏõæÇú ãóÚó
ÇáúÞóÇÚöÏöíäó {46} áóæú ÎóÑóÌõæÇú Ýöíßõã ãøóÇ ÒóÇÏõæßõãú ÅöáÇøó
ÎóÈóÇáÇð æáÃóæúÖóÚõæÇú ÎöáÇóáóßõãú íóÈúÛõæäóßõãõ ÇáúÝöÊúäóÉó æóÝöíßõãú
ÓóãøóÇÚõæäó áóåõãú æóÇááøåõ Úóáöíãñ ÈöÇáÙøóÇáöãöíäó {47}þ áóÞóÏö ÇÈúÊóÛóæõÇú
ÇáúÝöÊúäóÉó ãöä ÞóÈúáõ æóÞóáøóÈõæÇú áóßó ÇáÃõãõæÑó ÍóÊøóì ÌóÇÁ ÇáúÍóÞøõ æóÙóåóÑó
ÃóãúÑõ Çááøåö æóåõãú ßóÇÑöåõæäó {48} æóãöäúåõã ãøóä íóÞõæáõ ÇÆúÐóä áøöí æóáÇó
ÊóÝúÊöäøöí ÃóáÇó Ýöí ÇáúÝöÊúäóÉö
ÓóÞóØõæÇú
æóÅöäøó Ìóåóäøóãó áóãõÍöíØóÉñ ÈöÇáúßóÇÝöÑöíäó {49}
“Hawatakuomba
ruhusa wale wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, wasende kupigana
Jihadi kwa mali yao na nafsi zao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwajua
wachaMungu.
Wasio
muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na nyoyo zao zikatia shaka, hao tu
ndio wanao kutaka ruhusa. Basi hao wanataradadi katika shaka zao.
Na
ingeli kuwa kweli walitaka kutoka bila ya shaka wangeli jiandalia maandalio,
lakini Mwenyezi Mungu kachukia kutoka kwao, na kwa hivyo akawazuia na ikasemwa:
Kaeni pamoja na wanao kaa!
Lau
wangeli toka nanyi wasingeli kuzidishieni ila mchafuko, na wange tanga tanga
kati yenu kukutilieni fitna. Na miongoni mwenu wapo wanao wasikiliza. Na
Mwenyezi Mungu anawajua madhaalimu.
Tangu
zamani walitaka kukutilieni fitna, na wakakupindulia mambo juu chini, mpaka
ikaja Haki na ikadhihirika amri ya Mwenyezi Mungu, na wao wamechukia”.
Na
miongoni mwao wapo wanao sema: ‘Niruhusu wala usinitie katika fitina’. Kwa
yakini wao hivyo wamekwisha tumbukia katika fitina. Na hakika Jahannamu
imewazunguka.”
At Tawba – 44-49
Inaeleweka na
kila mtu kuwa Masahaba wote walitoka kwenda vitani siku hiyo ya vita vya Tabuk
(vita ambavyo aya hizo zinazungumzia juu yake), na waliobaki nyuma ni Aba Dhar
na Aba Khaythamah (Radhiya Llahu anhum), kisha nao pia wakenda kujiunga na
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pamoja na wenzao, na walikutana
nao njiani kabla ya kuwasili uwanja wa vita.
Na ineleweka pia
kuwa miongoni mwa waliobaki nyuma ni Kaab bin Malik, Hilal bin Umayyah na
Mirara bin Rabia (Radhiya Llahu anhum), nao ni katika watu wa Madina na
inajulikana na kila mtu kuwa Mwenyezi Mungu aliwasamehe Masahaba hao kama
ilivyoelezwa katika kisa cha ‘Wale watatu waliongojeshwa’.
Ama wengine waliobaki
Madina wasiende vitani walikuwa wakijulikana kuwa ni katika wale wanafiki
waliomuendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kuomba
udhuru wa uongo, au wale waliokuwa na udhuru wa kutopigana Jihad kwa ajili ya
ugonjwa au udhuru mwingine unaokubalika.
Na haya
tulieleza hapo mwanzo katika kisa cha Kaab (Radhiya Llahu anhu) kuwa
katika waliobaki pale Madina wasende vitani hakuwa akimuona aliye kufu yake
isipokuwa wenye udhuru au wale waliokuwa wakijulikana kuwa ni Wanafiki.
Na hii ni dalili
kuwa wanafiki walikuwa wakijulikana na Masahaba.
Na katika sura
hiyo hiyo ya At Tawba, Mwenyezi Mungu Anatujulisha kuridhika kwake na Masahaba
waliotangulia kuingia katika Uislamu miongoni mwa Wahajir (watu wa Makka
waliohamia Madina) na Ansaar (Watu wa Madina waliowapokea Wahajir wa Makka) na
akawatayarishia Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo milele.
Mwenyezi Mungu
anasema:
æóÇáÓøóÇÈöÞõæäó
ÇáÃóæøóáõæäó ãöäó ÇáúãõåóÇÌöÑöíäó æóÇáÃóäÕóÇÑö æóÇáøóÐöíäó ÇÊøóÈóÚõæåõã ÈöÅöÍúÓóÇäò
ÑøóÖöíó Çááøåõ Úóäúåõãú æóÑóÖõæÇú Úóäúåõ æóÃóÚóÏøó áóåõãú ÌóäøóÇÊò ÊóÌúÑöí
ÊóÍúÊóåóÇ ÇáÃóäúåóÇÑõ ÎóÇáöÏöíäó ÝöíåóÇ ÃóÈóÏÇð Ðóáößó ÇáúÝóæúÒõ
ÇáúÚóÙöíãõ
“Na
wale walio tangulia, wa kwanza, katika Wahajiri na Ansari, na walio wafuata kwa
wema, Mwenyezi Mungu ameridhika nao, na wao wameridhika naye; na amewaandalia
Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo milele. Huko ndiko kufuzu
kukubwa.”
At Tawba 100
Sasa tizameni
ndugu zangu, vipi Mwenyezi Mungu anatuelezea juu ya
kuridhika kwake na Masahaba katika Muhajir na Ansar kinyume na wanavyotuhumiwa
unafiki, na kwamba walirudi nyuma na kukufuru, akiwemo mbora wa Masahaba wote
Abubakar Al Siddique (Radhiya Llahu anhu).
Sisi tunaridhika
na wote alioridhika nao Mwenyezi Mungu, na tunawafanyia uadui maadui wote wa
Mwenyezi Mungu, na tunafuata yale tuliyofundishwa na Mwenyezi Mungu pamoja na
mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu wake (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
Mwenyezi Mungu anasema:
áóÞóÏ
ÊøóÇÈó Çááå Úóáóì ÇáäøóÈöíøö æóÇáúãõåóÇÌöÑöíäó æóÇáÃóäÕóÇÑö
ÇáøóÐöíäó ÇÊøóÈóÚõæåõ Ýöí ÓóÇÚóÉö ÇáúÚõÓúÑóÉö ãöä ÈóÚúÏö ãóÇ ßóÇÏó
íóÒöíÛõ ÞõáõæÈõ ÝóÑöíÞò ãøöäúåõãú Ëõãøó ÊóÇÈó Úóáóíúåöãú Åöäøóåõ
Èöåöãú ÑóÄõæÝñ ÑøóÍöíãñ {117}þ
“Mwenyezi
Mungu amekwisha pokea toba ya Nabii na Wahajiri na Ansari walio mfuata katika
saa ya dhiki, pale baada ya kukaribia nyoyo za baadhi yao kugeuka. Basi
akapokea toba yao, kwani hakika Yeye kwao wao ni Mpole na ni Mwenye
kuwarehemu.”
Attawba 117
Mwenyezi Mungu ni
mpole kwao na anawarehemu na ameridhika nao na anawasifia namna walivyosimama pamoja
na Mtume wake (Swallah Llahu alayhi wa sallam) katika saa ile ya dhiki (vita
vya Tabuk), na huu ni ushahidi utokao kwa Mwenyezi Mungu Asiye mshirika.
Utayakuta haya
pia katika vitabu vya wanavyuoni wakubwa wa Kishia (Ithnaasheri) waliotamka
ukweli ndani ya baadhi ya vitabu vyao vinavyotambulika.
Anasema Abu Nasr Muhammad bin Masaud, anayejulikana kwa jina la ‘Al
Iyashi’ katika tafsiri yake juu ya kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:
Åöäøó Çááøåó íõÍöÈøõ ÇáÊøóæøóÇÈöíäó æóíõÍöÈøõ ÇáúãõÊóØóåøöÑöíä
“Hakika
Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubu na huwapenda wanaojitakasa.’
Al Baqarah –
222
Alisema:
"Kutoka
kwa Salaam anasema: ‘Nilikuwa kwa Abu Jaafar (Muhammad Al Baqer Alayhi ssalaam- Imam
wa tano kwa Shia) akaingia Hamran bin Ayun na kumuuliza
baadhi ya mambo, na alipotaka kuondoka, Ayun akamuuliza Abu Jaafar:
'Tuelezee
Mwenyezi Mungu akupe umri mrefu, sisi tunapokuwa nawe nyoyo zetu hulainika na
nafsi zetu zinakuwa mbali na dunia, tunadharau kila kilichomo mikononi mwa watu
katika mali, lakini tunapotoka na kuchanganyika na watu na kufanya biashara,
tunaanza kuipenda tena dunia.’
Abu
Jaafar akasema:
"Nyoyo
zinashindwa na mambo baadhi ya wakati, na wakati mwengine mambo yanakuwa
mepesi.’ Kisha Abu Jaafar (Alayhi ssalaam) akaendelea kusema: ‘Kwa hakika
Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu walisema:
‘Ewe
Mtume wa Mwenyezi Mungu, tunajiogopea unafiki’ akasema: “Kwa nini mnaogopa?”
Wakasema:
“Sisi
tunapokuwa nawe ukatukumbusha, huwa na uoga, na nyoyo zetu zinalainika
tukaisahau dunia, hatuitamani, hata hufikia kuwa tunaiona akhera Pepo na Moto
mbele yetu. Lakini mara tunapotoka kwako na kuingia majumbani mwetu na kuanza
kuwabusu watoto wetu na kuonana na wake zetu na mali zetu, tunaanza kubadilika
hali zetu kinyume na pale tunapokuwa nawe, kama kwamba hatukuwa na kitu. Je!
Hutuogopei unafiki?"
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akawaambia:
“Kabisa
sikuogopeeni hilo, kwani hizi ni katika hatua za shetani akijaribu
kukupendezesheni dunia, Wallahi lau kama mungebaki katika hali ile mliyokuwa
nayo pale mlipokuwa nami, basi Malaika wangekusalimieni majiani na mungekuwa
mnatembea juu ya maji, na kama mungelikuwa hamtendi madhambi na kumuomba
Maghfira Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu angeliumba viumbe vingine ili
wafanye madhambi kisha wamuombe maghfira ili apate kuwaghufiria, kwani Muislam
siku zote yupo katika mtihani, hukuisikia kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:
Åöäøó Çááøåó íõÍöÈøõ ÇáÊøóæøóÇÈöíäó
‘Hakika
Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubu?’
na isemayo:
æóÃóäö ÇÓúÊóÛúÝöÑõæÇú ÑóÈøóßõãú Ëõãøó ÊõæÈõæÇú Åöáóíúåö
“Na
ili muombe msamaha kwa Mola wenu kisha mtubie (mrejee)?"
Hud 3
(Tafsir Al
Iyashi Juz1 uk.128)
Katika riwaya
hii, anatubainishia Al Iyashi katika tafsiri yake kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) ameshuhudia kuwa hawaogopei Sahaba zake
unafiki. Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) hasemi kwa
matamanio ya nafsi yake.
Kwa hivyo mwenye
kumuita Sahaba yeyote kuwa ni mnafiki, mtu huyo atakuwa ana moja katika
mawili:-
1-
Ama anakwenda
kinyume na mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa
sallam).
2-
Au anajua zaidi
kupita Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam).
Ikiwa tunautaka
umoja wa Waislamu kikweli na kuiondoa chuki iliyopo, basi nawaomba ndugu zetu
Mashia waache kuwakufurisha Masahaba au kuwaita wanafiki na kuwaapiza, na
badala yake tumfanye Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
kuwa ni ruwaza njema kwetu, kuwa ni mfano mwema kwetu wa kuigwa, na tuwapende
kama alivyokuwa akiwapenda Swallah Llahu alayhi wa sallam.
Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akiwapenda Swahaba zake
(Radhiya Llahu anhum). Na watu wa nyumba yake 'Ahlul Bayt' (Radhiya
Llahu anhum) nao pia walikuwa wakiwapenda Maswahaba (Radhiya Llahu anhum), na
Maswahaba nao walikuwa wakiwapenda Ahlul Bayt.
Huyu hapa Imam Al Hassan Al Askari, ambaye ni Imam wa
kumi na moja wa Shia alipokuwa akiwafahamisha watu daraja ya Masahaba (Radhiya
Llahu anhum) mbele ya Mwenyezi Mungu alisema:
‘Miongoni wa masuala aliyouliza Musa
(Alayhi Ssalaam) kumuuliza Mwenyezi Mungu alisema:
‘Wapo
Masahaba wa Mtume yeyote wa Mwenyezi Mungu walio bora kuliko Masahaba wangu?'
Mwenyezi
Mungu akamjibu:
“Ewe
Musa kwani hujui kuwa ubora wa Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu Muhammad juu
ya Masahaba wa Mitume yote ni sawa na ubora wa watu wa nyumba ya Muhammad juu
ya watu wa nyumba za Mitume yote, na mfano wa ubora wa Muhammad juu ya Mitume
yote?”
Tafsiri ya
Al Hassan Al Askary uk.11(Tafsiri ya Surat Al Baqarah
Ndani ya kitabu
kitukufu kwa Shia kiitwacho ‘Nahaj al Balaghah’, Sharhi ya Muhammad Abdo
Uk. 225, imeandikwa kua Imam Aly alisema:
“Nimewaona
Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu alayhi wa sallam), na sioni
yeyote kati yenu aliyeshabihiana nao. Walikuwa wakati wa asubuhi utawaona
nywele zimetimka kwa sababu ya kusimama kwao usiku kucha wakisujudu na kusimama
(kwa kuswali), wanaomba huku wakisujudu, na wanapolala, na wanapokumbuka akhera
yao utawaona wanasimama kama kwamba wamesimamia makaa ya moto. Na anapotajwa
Allah basi macho yao yanatoa machozi mpaka nyuso zao zinaroa, na wanainamisha
vichwa vyao chini mfano wa miti iliyopinda kwa upepo mkali wa kimbunga kwa
kuhofia adhabu na kutarajia thawabu”.
Ama Ibarahim Al
Thaqafi ambaye ni katika maulamaa wakubwa wa Shia, katika kitabu chake
kiitwacho ‘Al Ghaaraat’ Juzuu ya 1 Uk.177 akimnukuu Aly (Radhiya Llahu
anhu):
“Aliulizwa
Aly: ‘Ewe Amiri wa Waislam, tuelezee juu ya Sahibu zako.’
Akauliza:
“Juu
ya sahibu zangu wepi?”
Wakamwambia:
“Juu
ya Sahaba wa Muhammad (Swalla Llahu alayhi wa sallam).”
Akasema:
“Masahaba
wa Muhammad wote ni sahibu zangu”.
Tunamuomba
msomaji arudie marejeo yote tuliyonukuu kutoka katika Qurani tukufu na kutoka
kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na kutoka kwa
maulamaa wa pande zote mbili ili imbainikie heshima ya Masahaba hawa wakiwemo
Makhalifa watatu wa mwanzo wa Waislam mbele ya Mwenyezi Mungu na mbele ya Mtume
wake (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na mbele ya maulamaa waliotangulia wa
pande zote mble, kisha ajiulize; ni kwa maslahi ya nani mtu anaweza kuthubutu
kuwatukana au kuwazulia uongo na kuwawekea vikao vya kila mwaka kuwalani na
kuapa juu ya kulipa visasi.
Bali hata
Sayiduna Al-Husayn (Radhiya Llahu anhu) alikuwa katika nchi ya Constantinople
akipigana jihadi, na wakati huo Mu’awiyah (Radhiya Llahu anhu) ndiye aliyekuwa
Khalifa wa Waislamu. Kwa hivyo Masahaba na Watu wa Nyumba ya Mtume (Radhiya
Llahu anhum) walikuwa wakishirikiana na kupendana na kunasibiana na walikuwa
pamoja katika jihadi yao dhidi ya maadui wa Uislamu.
Siku moja kundi
la watu lilikwenda kwa Imam Aly Zeinul Abideen (Radhiya Llahu anhu) na walikuwa
wakiwasema vibaya Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu alayhi wa
sallam); Abubakar, Umar na Uthman (Radhiya Llahu anhum).
Aly Zeinul
Abideen (Radhiya Llahu anhu) akawauliza:
“Kwanza
nielezeni ni nani nyinyi? Nyinyi ni katika wale Wahajir (Watu wa Makka)
waliohama mwanzo waliotolewa majumbani mwao na katika mali zao wakitaka fadhila
za Mwenyezi Mungu na radhi zake na wakamnusuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake?”
ÇáøóÐöíäó ÃõÎúÑöÌõæÇ ãöä ÏöíÇÑöåöãú æóÃóãúæóÇáöåöãú íóÈúÊóÛõæäó ÝóÖúáÇð ãøöäó Çááøóåö
æóÑöÖúæóÇäÇð æóíóäÕõÑõæäó Çááøóåó æóÑóÓõæáóåõ
Al Hashr -8
Wote
kwa pamoja wakasema: “La, sisi si katika hao”
Akawauliza
tena:
“Basi
nyinyi ni katika watu waliofanya maskani yao hapa (Madina) na wakautakasa
Uislamu (wao barabara) kabla ya (kuja ) hao (Muhajirin) na wakawapenda hao
waliohamia kwao”.
æóÇáøóÐöíäó ÊóÈóæøóÄõæÇ ÇáÏøóÇÑó æóÇáúÅöíãóÇäó ãöä ÞóÈúáöåöãú
íõÍöÈøõæäó ãóäú åóÇÌóÑó Åöáóíúåöãú
Al Hashr -9
Wakajibu:
“La!
Sisi si katika hao”
Kisha
Imam Aly Zeinul Abideen (Radhiya Llahu anhu)
akawaambia:
“Nyinyi
wenyewe mumeshuhudia kuwa si katika hawa wala si katika wale. Basi na mimi
ninashuhudia pia kuwa nyinyi si katika kundi lile la tatu ambalo Mwenyezi Mungu
Amesema juu yao:
æóÇáøóÐöíäó ÌóÇÄõæÇ ãöä ÈóÚúÏöåöãú íóÞõæáõæäó ÑóÈøóäóÇ ÇÛúÝöÑú
áóäóÇ æóáöÅöÎúæóÇäöäóÇ ÇáøóÐöíäó ÓóÈóÞõæäóÇ ÈöÇáúÅöíãóÇäö æóáóÇ ÊóÌúÚóáú Ýöí
ÞõáõæÈöäóÇ ÛöáøÇð áøöáøóÐöíäó ÂãóäõæÇ ÑóÈøóäóÇ Åöäøóßó ÑóÄõæÝñ ÑøóÍöíãñ
“Na Waliokuja baada yao (wakawa wanapendana na Waislamu
waliotangulia wanawaombea dua) wanasema; ‘”Mola wetu! Tusamehe sisi na ndugu
zetu waliotutangulia (kufa) katika Uislamu. Wala usijaaliye katika nyoyo zetu
undani kuwafanyia Waislamu (wenzetu). Mola wetu! Hakika Wewe ni Mpole sana,
Mwenye Rehema mno”.
Al Hashr – 10
Katika aya hizi
Mwenyezi Mungu anashuhudia kuwa watu wa Makka waliacha majumba yao na mali zao
na watu wao kwa ajili ya kutaka fadhila za Mwenyezi Mungu na radhi zake, na kwa
ajili ya kumnusuru Mwenyezi Mungu na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam), na akashuhudia kuwa ni wakweli.
Na Mwenyezi
Mungu anashuhudia pia watu wa Madina waliutakasa Uislamu baraabara, juu ya kuwa
walifikiwa na wageni wazito na hawakuwa na mali ya kutosha, waliwapokea wageni
hao kwa moyo mkunjufu, wakahiari kujinyima wao kwa ajili ya kuwakirimu wageni.
Kisha Mwenyezi
Mungu Akatuamrisha tuliokuja baada yao kuwaombea maghfira na akatutaka tusijaaliye
ndani ya nyoyo zet undani wowote juu yao.
Imepokelewa
kutoka kwa Yahya bin Kathiyr kutoka kwa Jaafar bin Muhammad bin Aly bin Al
Hussayn kutoka kwa baba yake ((Radhiya Llahu anhum) kuwa amesema:
« Alikuja
mtu kwa baba yangu akamuambia : ‘Nihadithie juu ya Abubakar.’ Akasema:
‘Unauliza juu ya Al Siddique.’ Akasema yule mtu : ‘Mwenyezi Mungu
akurehemu, na wewe pia unamuita Al Siddique ?’ Akamuambia : ‘Akukose
mama yako wewe. Ameitwa As Siddique na aliye bora kupita mimi na wewe, Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) na Watu wa Makkah na watu wa
Madina. Asiyemuita kwa jina la Al Siddique basi Mwenyezi Mungu hatosadiki kauli
yake duniani wala akhera. Nenda, tena umpende Abubakar na Umar.»
Imeandikwa
katika Nahj Al Balaghah pia kuwa Aly (Radhiya Llahu anhu) alimuandikia Muawiyah
bin Abi Sufiyan (Radhiya Llahu anhu) akimuambia:
Kwa
Muawiyah:
"Bisimillahi
Rahmaani Rahiym,
Amma
baad, kwa vile watu wote wamefungamana nami katika mji wa Madina, basi nawe pia
uliyeko huko Sham (Syria) unalazimika kufungamana nami. Na hii ni kwa sababu
watu waliofungamana nami ni wale wale waliofungamana na Abubakar na Umar na
Uthmaan. Kwa hivyo aliyehudhuria hana haki ya kulikataa na asiyehudhuria hana
haki ya kulipinga. Kwa hakika ushauri ni wa Muhaajirin na Answaar (Watu wa
Makkah na wa Madina). Wanapokubaliana wote juu ya mtu na kumchagua kuwa Imam
wao, na Mwenyezi Mungu Anaridhika na uchaguzi wao.
Nimemtuma
kwako Jariyr, naye ni katika watu wa Imani na watu waliohajir, kwa hivyo
fungamana nami - Walaa quwwata illa billaah!!".
Nahjul-Balaaghah-
uk. 427 mlango wa 6
Subhanallah!
Huyu hapa Aly (Radhiya Llahu anhu) anakiri mwenyewe kuwa hapana mwenye haki ya
kupinga uchaguzi wa watu wa Makka na wa Madina na kwamba Mwenyezi Mungu
ameridhika na kuchaguliwa kwa Abubakar na Umar na Aly (Radhiya Llahu anhum) kwa
sababu wote wamechaguliwa kwa njia hiyo.
Mtume (Swallah
Llahu alayhi wa sallam) ameoa mabinti wa Abubakar na Umar. Na Uthman alioa mabinti
wawili wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), Mabibi
Ruqayya na Ummu Kulthum, na alijulikana kwa jina la 'Dhiy Nnurayn', na
maana yake ni Mwenye Nuru mbili kwa sababu ya mabinti hao wawili (Radhiya Llahu
anhum).
Alihuzunika
sana alipofariki mkewe wa pili Bibi Ummu Kulthum (Radhiya Llahu anha) na Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) alipomuona katika hali ile
akamuuliza:
"Kipi
kinachokuliza ewe Uthman?"
Uthman
akajibu:
"Ninalia
ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa sababu kumekatika kunasibiana kwangu na
wewe."
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:
"Usilie
ewe Uthman, naapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, lau kama nina
mabinti mia wanakufa mmoja baada ya mwengine, basi ningekuozesha mpaka wasibaki
katika mia hao hata mmoja."
Attabarani na
wengine
Hii ni katika dalili za mapenzi makubwa yaliyokuwepo
baina ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) pamoja na watu
wa nyumba yake juu ya Masahaba (Radhiya Llahu anhum).
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
alimuoa Bibi Aisha binti wa Abubakar Al Siddiquqe na alimuoa Hafsa binti wa
Umar bin Khatab na alimuoa pia Ummu Habiybah Ramlah binti Abu Sufyan (Radhiya
Llahu anhum).
Aly (Radhiya Llahu anhu) alimuozesha binti yake Ummu
Kulthum kwa Umar bin Khatab.
(Al Kafi/346/5)
Alipouliwa
Jaafar bin Abi Talib (Radhiya Llahu anhu), mkewe Asmaa binti Umays (Radhiya
Llahu anha) aliolewa na Abubakar Al Siddique na alipofariki Abubakar (Radhiya
Llahu anhu), Bibi Asmaa aliolewa na Aly bin Abu Talib (Radhiya Llahu anhu).
Jaafar Assadiq
ni mjukuu wa Abubakar As Siddique, kwa sababu Muhammad Al Baqer mjukuu wa Al
Hussain alimuoa Um Farwah mjukuu wa Muhammad bin Abubakar, na kutokana na ndoa
hiyo akapatikana Jaafar As Sadiq. Kwa hivyo Jaafar ni mjukuu wa Abubakar na
mwanawe Musa Al Kadhim anakuwa pia mtoto wa mjukuu
wa Abubakar na kwa njia hii Maimam wote waliofuata wa Shia ni wajukuu wa
Abubakar Al Siddique (Radhiya Llahu anhum jamiy’an)
Imepokelewa kuwa Jaafar
Al Sadeq alikuwa akisema:
“Amenizaa Abubakar mara
mbili.”
Siyar aalam al
Nubalaa
Abaad bin Uthman bin
Affan alimuoa Ummu Kulthum binti yake Abdullah bin Jaafar bin Abi Talib.
Shia wa Ahlul
Bayt/141
Sakina binti Al Hussayn
bin Aly bin Abi Talib aliolewa na Masaab bin Al Zubair bin Al Awaam.
Tabaqaat ibn
Saad183/5
(Mwenyezi Mungu awe
radhi nao wote)
Majina ya watoto
Aly bin Abi Talib
aliwapa wanawe majina ya Abubakar na Umar na Uthman.
Kashf al Ghumah
2/67
Al Hassan bin Aly
alimpa mmoja wa watoto wake jina la Abubakar.
Kashf al Ghumah
2/198
Musa bin Jaafar alikuwa
na watoto aliowapa majina ya Aisha na Umar.
Kashf al Ghumah 3/29
Itakuwa siku ya
furaha kubwa tutakapowaona wafuasi wa Sunni wakipeana mikono na wafuasi wa Shia
kwa furaha bila kinyongo wala undani. Lakini hatuwezi kulifikia lengo hilo ikiwa
Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam)
wataendelea kutukanwa na kukashifiwa na kulaaniwa.
Hatuwezi
kulifikia ikiwa watu wataendelea kulizuru kaburi la Majusi Abu Lulua aliyemuua
Khalifa wa Waislamu na Sahibu yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu
alayhi wa sallam) Umar bin Khataab (Radhiya Llahu anhu) na kuliita kaburi la Majusi
huyo ‘Babu Shujaa ddiyn’ ‘Mlango wa shujaa wa
dini.’
Dini gani
wakati mtu huyu hakuwa Muislamu? Kwa nini wanakubali kuisherehekea siku ambayo
Mmajusi aliyekuwa akiabudu moto alimuuwa Khalifa wa Wasilamu?
Narudia mwito
wa Sheikh Al Qaradhawi aliposema : «Enyi
viongozi wa Shia wenye akili na hekima, upigeni vita mnasaba huu kwa ajili ya
umoja wa Waislamu. Inatosha jamani kueneza chuki kwa mambo yaliyotokea miama
1500 iliyopita.»
Msisahau kuwa
Umar huyu ni ami yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam),
kwa sababu Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amemuowa
bini yake Hafsa (Radhiya Llahu anha), na Umar huyu huyu ni mume wa Ummu Kulthum
binti Aly bin Abi Talib (Radhiya Llahu anhu).