Makusudio sahihi ya Aliyekunja uso
Muhammad Faraj Salem Al Saiy
Imepokelewa kuwa siku moja Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa amekaa na wakubwa wa Ma-Quraysh akiwalingania Diyn kwa hima kubwa akitaraji kuwa wakisilimu wakubwa hao, na wanyonge wao watafuata kwa sababu wengi kati ya wanyonge walitaka kusilimu lakini walijizuia kwa kuwaogopa wakubwa wao hao
Wakati huo akatokea kipofu
mmoja aliyesilimu tokea zamani aitwaye Ibn Ummi Maktuum (Radhiya Allaahu ‘Anhu),
na bila kujua kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameshughulika akawa anampigia kelele
kumwambia: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, nifunze na
mimi katika aliyokufunza Mwenyezi Mungu.”
Akawa anayarudia maneno
hayo, na kwa vile Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam) alikuwa ameshughulika kutaka kuwasilimisha viongozi wale wakubwa,
akamfinyia uso yule kipofu wala asimsikilize, ndipo Mwenyezi Mungu
Alipomteremshia aayah za mwanzo za Suuratu-‘Abasa. Mwenyezi Mungu Anasema:
|
ÈÓã Çááå ÇáÑÍãä ÇáÑÍíã |
|
|
ÚóÈóÓó
æóÊóæóáøóìٰ ﴿١﴾ |
Alikunja (Mtume) uso akageuka |
|
Ãóä ÌóÇÁóåõ ÇáÃÚúãóìٰ
﴿٢﴾ |
Kwa sababu alimjia kipofu |
|
æóãóÇ
íõÏúÑöíßó áóÚóáøóåõ íóÒøóßøóìٰ﴿٣﴾ |
Na nini kilichokujulisha (ya kuwa huyo Swahaabah
kipofu hahitaji mawaidhah mapya), huenda yeye atatakasika (kwa kusikia
mawaidha yako). |
|
Ãóæú
íóÐøóßøóÑõ ÝóÊóäÝóÚóåõ ÇáÐöøßúÑóìٰ ﴿٤﴾ |
Au atakumbuka ukumbusho huo upate kumfaa |
|
ÃóãøóÇ ãóäö
ÇÓúÊóÛúäóìٰ ﴿٥﴾ |
Ama ajionaye hana haja |
|
ÝóÃóäÊó áóåõ
ÊóÕóÏøóìٰ ﴿٦﴾ |
Wewe ndiye unayemshughulikia. |
|
æóãóÇ
Úóáóíúßó ÃóáøóÇ íóÒøóßøóìٰ ﴿٧﴾ |
Na si juu yako kama hakutakasika. |
|
æóÃóãøóÇ ãóä
ÌóÇÁóßó íóÓúÚóìٰ ﴿٨﴾ |
Lakini anayekukimbilia |
|
æóåõæó
íóÎúÔóìٰ ﴿٩﴾ |
Naye anaogopa |
|
ÝóÃóäÊó
Úóäúåõ Êóáóåøóìٰ ﴿١٠﴾ |
Wewe unapuuza (Usifanye hivyo) |
|
ßóáÇ ÅöäøóåóÇ
ÊóÐúßöÑóÉñ ﴿١١﴾ |
Sivyo! Hakika hii (Qur-aan) ni nasaha |
|
Ýóãóä ÔóÇÁó
ÐóßóÑóåõ ﴿١٢﴾ |
Basi kila apendaye atawaidhika |
Shi’ah wanasema kuwa
makatazo ndani ya aayah hizi si kwa ajili ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa sababu si yeye (Swalla Llaahu ‘alayhi
wasallam) aliyekunja uso na kugeuka na kwamba yeye (Swalla Allaahu ‘alayhi wa
aalihi wa sallam) hawezi kukunja uso wala kukosolewa, bali aliyekosea na
kukosolewa ndani ya aayah hizo ni ‘‘Uthmaan (Radhiya Allaahu ‘Anhu).
Tatizo ni
kuwa baadhi yao hawana uoga hata kidogo, na wako tayari kubadilisha maneno ya
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu Wa Ta’ala), kwa ajili ya kutaka kuiuza bidhaa yao
mbovu.
Sisi Tunasema: Lau kama aliyeteremshiwa aayah hizi ni ‘Uthmaan (Radhiya Allaahu ‘Anhu),
basi hii ni sifa kubwa kwake, kwa sababu mtiririko wa aayah unatujuulisha kuwa
aliyekatazwa ni mtu aliyekuwa akiwalingania watu katika Diyn, na hii ni sifa
nzuri hata kama atakatazwa au kukaripiwa kidogo na Mola wake (Subhaanahu wa
Ta’ala).
Mwenyezi Mungu Anasema:
{{Alikunja uso na akageuka. Kwa sababu alimjia kipofu.
Na nini kilichokujuulisha (ya kuwa huyo Swahaabah
kipofu hahitaji mawaidhah mapya), huenda yeye atatakasika (kwa
kusikia mawaidha yako).}} [‘Abasa: 1-3]
Kutokana na aayah hizi,
(kwa rai ya Shi’ah) inaleta maana kuwa kipofu (‘Abdullaah mwana wa Ummi
Maktuum), hakumuendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi
wa sallam), wala hakumuendea ‘Aliy bin Abi Twaalib wala Maswahaabah (Radhiya
Llaahu ‘anhum) waliokuwepo mahali hapo, bali alimuendea ‘‘Uthmaan (Radhiya
Allaahu ‘Anhu) kwa ajili ya kutaka kupata mawaidhah na uongofu kutoka kwake. Kwa
sababu aliyekunja uso ni ‘‘Uthmaan (Radhiya Allaahu
‘Anhu) na si Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam).
Huu ni
ubabaishaji wa maneno, kwa sababu aayah zinatufahamisha kuwa aliyejiwa ndiye
aliyekunja uso, na haiwezekani kwa mwana wa Ummi Maktuum kumuacha Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuendea ‘‘Uthmaan
(Radhiya Allaahu ‘Anhu).
Kama wangelitafakari kidogo
tu kabla ya kuandika maandishi yao haya yenye sumu,
wangeligundua kuwa maneno yao ni utovu wa adabu dhidi ya Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
Hadiyth sahihi zinasema
kuwa kipofu yule alimuendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) huku akimuambia: “Nifundishe
katika yale Aliyokufundisha Mwenyezi Mungu.” Akawa anaendelea kuyakariri
maneno hayo, na kwa vile yeye ni kipofu, hakuelewa
kuwa wakati ule Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam) alikuwa ameshughulika kutaka kuwasilimisha wakubwa wa Ma-Quraysh
waliokuwa naye akiwa na tumaini kuwa huenda mmoja wao atasilimu. Ndipo
alipokunja uso na hakumjibu, na hapo ndipo
zilipoteremshwa aayah za kumkosoa (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
Na hili ni
jambo la kawaida kwa mtu yeyote anayekatwa maneno wakati akizungumza, na hili
ni funzo kwetu kutoka kwa Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) kuwa tusiwakate
watu maneno wanapozungumza kwa sababu hili ni jambo linalokera.
Na Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakumdharau kipofu
yule wala hakumkaripia kwa kumuambia kwa mfano: “Nyamaza!” au “Ondoka hapa!”
bali alikunja uso wake tu bila kumjibu. Lakini Mwenyezi Mungu (Subhaanahu Wa Ta’ala) alimkaripia Mtume wake na kipenzi chake (Swalla
Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya kuwa kipofu yule hawezi kuuona uso
wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wala
kujua kuwa amekasirikiwa.
Ikiwa aayah hizi
ameshushiwa ‘‘Uthmaan (Radhiya Allaahu ‘Anhu), kwa
nini basi asikaripiwe kwa unafiki na ukafiri wake kama Mashi’ah wanavyoamini
kuwa yeye ni mnafiki. Wakati kitendo cha unafiki ni
kikubwa zaidi na kinachostahiki zaidi kukaripiwa kuliko kukunja uso.
Wengine wakasema kuwa eti
mwana wa Ummi Maktum hakuwa akiuliza mambo ya Diyn,
bali ni mambo ya kidunia tu ndiyo maana akamuendea ‘Uthmaan!
Enyi Shi’ah! Hebu
zingatieni vizuri mtiririko wa hizi aayah:
Mwenyezi Mungu Anasema:
“Lakini anayekukimbilia. (Ewe ‘Uthmaan?) Naye anaogopa
(Anaogopa nini?). Wewe
unapuuza (Usifanya hivyo, sivyo! Hakika hii
(Qur-aan) ni nasaha huenda yeye atatakasika (Akatakasika
na nini?).”
Kama aayah hizi
ametereshiwa ‘Uthmaan (Radhiya Allaahu ‘Anhu), basi ni
sifa kubwa kwake kwa kukimbiliwa na kutakiwa amsikilizishe kipofu yule mawaidhah
apate kuongoka.
Kwa kila mwenye kupenda
haki, musikubali kudanganywa na tafsiri kama hizi
zenye kubadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu na kupotosha.
Hii si mara ya mwanzo kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa
aalihi wa sallam) kukosolewa ndani ya Qur-aan tukufu. Na sisi tunaamini kuwa
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakosolewi
kwa kuwa amefanya kitendo cha dhambi, bali hukosolewa kutokana na kujitahidi
kwake sana au kwa ajili ya huruma nyingi aliyonayo au kwa ajili ya kuwataka
watu waingie haraka ndani ya Diyn ili waepukane na Moto kama ilivyoelezwa
katika Suuratul-Kahf.
Mwenyezi Mungu Anasema:
ÝóáóÚóáøóßó ÈóÇÎöÚñ äøóÝúÓóßó Úóáóìٰ ÂËóÇÑöåöãú Åöä áøóãú
íõÄúãöäõæÇ ÈöåóÜٰÐóÇ ÇáúÍóÏöíËö ÃóÓóÝðÇ
{{Labda
unajiangamiza nafsi yako kwa kusikitikia hali yao kuwa
hawaziamini Hadiyth hizi. Usijihuzunishe hivyo, kama
hawataki kuamini basi.}} [Al-Kahf:
6]
Ifuatayo ni
mifano mingine michache:
Mwenyezi Mungu Anasema:
íóÇ ÃóíøõåóÇ ÇáäøóÈöíøõ áöãó ÊõÍóÑöøãõ ãóÇ ÃóÍóáøó
ÇááøóÜåõ áóßó ۖ ÊóÈúÊóÛöí ãóÑúÖóÇÊó ÃóÒúæóÇÌößó ۚ æóÇááøóÜåõ ÛóÝõæÑñ ÑøóÍöíãñ
{{Ewe Nabii! Kwa nini unaharimisha Alichokuhalilishia Mwenyezi Mungu?
Unatafuta kuwaridhi wake zako. Na Mwenyezi Mungu ni
Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.}} [At-Tahriym:
1]
Na Akasema:
ãóÇ ßóÇäó áöáäøóÈöíöø æóÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇ Ãóä íóÓúÊóÛúÝöÑõæÇ
áöáúãõÔúÑößöíäó æóáóæú ßóÇäõæÇ Ãõæáöí ÞõÑúÈóìٰ ãöä ÈóÚúÏö ãóÇ ÊóÈóíøóäó
áóåõãú Ãóäøóåõã ÃóÕúÍóÇÈõ ÇáúÌóÍöíãö ú
{{Haimpasii Nabii
na wale walioamini kuwatakia msamaha washirikina,
ijapo kuwa ni jamaa zao, baada ya kwisha bainika kuwa hao ni watu wa Motoni.”
At-Tawbah -113
Na Akasema:
ãóÇ ßóÇäó
áöäóÈöíøò Ãóä íóßõæäó áóåõ ÃóÓúÑóì ÍóÊøóì íõËúÎöäó Ýöí ÇáÃóÑúÖö ÊõÑöíÏõæäó
ÚóÑóÖó ÇáÏøõäúíóÇ æóÇááøåõ íõÑöíÏõ ÇáÂÎöÑóÉó æóÇááøåõ ÚóÒöíÒñ Íóßöíãñ.
áøóæúáÇó ßöÊóÇÈñ ãøöäó Çááøåö ÓóÈóÞó áóãóÓøóßõãú ÝöíãóÇ ÃóÎóÐúÊõãú ÚóÐóÇÈñ
ÚóÙöíãñ
“Haimfalii Nabii
yeyote kuwa na mateka mpaka awe ameshinda baraabara katika nchi. Munataka vitu
vya dunia, na Mwenyezi Mungu anataka Akhera. Na
Mwenyezi Mungu ni Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye hikima.}}
[Al-Anfaal: 67]
Sisi tunaamini kuwa hizi ni
sifa njema na fahari kubwa kwa kiumbe kusemeshwa na kufundishwa na Mola wake
(Subhaanahu wa Ta’ala), na kukosolewa kwa ajili ya huruma zake na wala si sifa
mbaya. Lakini wanayoyatambua haya ni wenye akili peke
yao.
Mwenyezi Mungu Anasema:
áóÞóÏú ÌóÇÁóßõãú ÑóÓõæáñ ãöøäú ÃóäÝõÓößõãú ÚóÒöíÒñ Úóáóíúåö ãóÇ
ÚóäöÊøõãú ÍóÑöíÕñ Úóáóíúßõã ÈöÇáúãõÄúãöäöíäó ÑóÁõæÝñ ÑøóÍöíãñ
﴿١٢٨﴾ ÝóÅöä ÊóæóáøóæúÇ ÝóÞõáú ÍóÓúÈöíó ÇááøóÜåõ
áóÇ ÅöáóÜٰåó ÅöáøóÇ åõæó ۖ Úóáóíúåö
ÊóæóßøóáúÊõ ۖ æóåõæó ÑóÈøõ ÇáúÚóÑúÔö ÇáúÚóÙöíãö
{{Amekufikieni
Mtume aliye jinsi moja na nyinyi; yanamhuzunisha
yanayo kutaabisheni; anakuhangaikieni sana, kwa Walioamini ni mpole na mwenye
huruma. Basi wakidumu kukengeuka (hao makafiri), sema: ‘Mwenyezi Mungu
Ananitosheleza. Hapana wa kuabudiwa ila Yeye tu.
Namtegemea Yeye, na Yeye ndiye Mola wa (hiyo) Arshi
iliyo kubwa kabisa.’}} [At-Tawbah:
128-129]
Ndani Ya Vitabu Vya Kishi’ah
Tafsiri sahihi kuwa
aliyekusudiwa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam) zimo hata ndani ya vitabu vyao na tafsiri za Ma’ulamaa wao wakubwa na
maarufu, na zinakubaliwa na wanavyuoni mbali mbali wa Shi’ah kuwa aliyekusudiwa
ni Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) .
Anasema At-Tubrusiy ambaye ni mmoja katika Ma’ulamaa wakubwa wa Shi’ah
Ithna-‘Ashariyah: “Kule kuambiwa Mtume ‘alayhis salaam kuwa aliukunja uso
wake siyo tuhuma, kwake.” [Tafsiyr
Majma’al Bayaan, ukurasa 266 Juzuu ya 10]
Tembelea tafsiri ya
At-Tubrusiy katika anuani hii: http://www.holyquran.net/cgi-bin/majma.pl
Anaendelea kusema
At-Tubrusiy:
“Aayah
hii imeteremshwa kwa ajili ya ‘Abdullaah mwana wa Ummi
Maktuum na jina lake ni Shurayh bin Maalik bin Rabiy’ah Al-Fahary, anayetokana
na kabila la Bani ‘Aamir bin Luay. Aliyemjia Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na wakati huo
alikuwa akiwalingania ‘Utbah bin Rabiy’ah na Abu Jahal bin Hishaam na
Al-‘Abbaas bin ‘Abdil Muttwalib na Umayah bin Khalaf akiwalingania wamuamini
Allaah, akitarajia kusilimu kwao. Akasema (Mwana wa
Ummi Maktuum): “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, nifunze na mimi katika
Aliyokufunza Mwenyezi Mungu.” Akawa anamuita huku akiyakariri maneno yale bila kujua kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu
‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa ameshughulika na watu wengine. Mpaka
kuchukizwa na kukabainika usoni mwa Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kutokana na kukatwa maneno
yake kila anapotaka kusema. Ikampitikia nafisini mwake kuwa wakubwa wa makafiri hawa watasema kuwa wafuasi wake ni vipofu na watumwa,
akageuka asimjibu na kuwaelekea wale aliokuwa akiwalingania, ndipo
zilipoteremka aayah.
Akawa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam) baada ya siku ile akimkirimu na kila anapomuona, husema: “Karibu ewe
ambaye kwa ajili yake Amenikosoa Mola wangu.” Kisha humuuliza: “Una haja yoyote?:” Na alimpa ugavana wa mji wa Madiynah mara mbili.”
Anaendelea kusema At-Tubrusiy
ambaye ni mmoja wa Ma’ulamaa wakubwa wa Shi’ah akijibu
hoja za wenye madai hayo:
“Kutajwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa
amekunja uso siyo tuhuma kwake. Kama mtu atasema: ‘Ikiwa
kweli amekosolewa, hii ina maana kuwa kumkunjia mtu
uso ni dhambi?
Jawabu: ‘Kukunja uso au kutabasamu mbele ya uso wa kipofu si kitendo cha
dhambi kwa sababu kitendo hicho hakimdhuru, na kwa ajili hiyo si kitendo cha
dhambi.’
Huenda ikawa Mwenyezi Mungu
Amemkosoa Mtume wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ili awe na tabia bora kupita zote na kumtanabahisha juu ya
utukufu wa Muislamu anayetafuta uongofu na kumjuulisha kuwa kumuongoza Muislamu
apate kuthibiti katika imani yake ni bora kuliko kutegemea kusilimu kwa
mshirikina.”
(Mwisho wa
kunukuu maneno ya At-Tubrusiy)
Mwanachuoni mwengine wa Kishi’ah aitwae Al-Jibaiy anasema: “Ndani yake mna
fundisho kuwa hapo mwanzo kitendo cha kukunja uso hakikuwa cha dhambi, mpaka
amri ya kukataza ilipoteremka.”
Anaendelea kusema:
“Imepokelewa kuwa Mtume (Swalla
Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa kila anapomuona ‘Abdullaah mwana wa Ummi Maktuum humuambia: “Karibu karibu, hapana Wallah! Mwenyezi Mungu Hatonikataza tena juu yako.” Na alikuwa mpole sana kwake.”
Maneno kama
haya pia yamenukuliwa kutoka mmoja katika Ma’ulamaa wakubwa wa Shi’ah Muhammad
Haadi Al-Yuusufiy kutoka kwa At-Tubrusiy katika kitabu chake ‘Encyclopedia ya Taariykh’ Juzuu ya 1, ukurasa
494.
Na maneno hayo pia
yameandikwa na mwanachuoni wa Kishi’ah Al-Majlisiy
katika Bihaar al Anwaar, juzuu ya 17,
ukurasa wa 78.
Yamenukuliwa maneno kama haya pia kutoka kwa mwanachuoni mkubwa wa Kishi’ah
katika wakati wetu huu Muhammad Husayn Fadhlullah katika tafsiri yake ‘Wahyul Qur-aan’.
Atakaye anaweza kuutembelea
ukurasa huo katika mtandao wake unaopatikana penye anuani ifuatayo: http://arabic.bayynat.org.lb/books/quran/abas1.htm
Hebu tumsikilize Ayatullah
Muhammad Husayn Fadhlullah akiwajibu Mashi’ah wenzake wanaosema kuwa
waliokusudiwa katika aayah zile ni ‘Uthmaan au mtu
katika watu wa kabila la Bani Umayyah. Anasema mwanachuoni huyu wa Kishi’ah:
“Riwaya inayonasibishwa na Imaam Asw-Swadiq (Radhiya Allaahu ‘Anhu) kuwa aayah imeteremshwa kwa ajli ya mtu wa kabila la Bani Umayyah
haikubaliani na mtiririko wa aayah. Kwa sababu ni wazi kuwa kusudi la aayah
hizo ni kuwa aliyekusudiwa ni mtu mwenye kumiliki sehemu muhimu katika
kuifikisha risala na kwamba mtu huyo anabeba jukumu la kuwatakasa na
kuwafundisha wale waliokwisha hidika na kuikubali risala hiyo kwanza, ili wawe
na msingi mzuri na uwezo wa kuifikisha Dini kwa watu, kinyume na wale
wasiohidika ambao hawastahiki kupewa juhudi kubwa.”
(Mwisho wa
maneno ya Muhammad Husayn Fadhlullah)
Kutokana na
haya, tunaona kuwa waliosema kuwa aliyekusudiwa katika aayah zile ni Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) si Masunni peke yao.
Bali pia yamesemwa na Ma’ulamaa wakubwa wa Kishi’ah
ambao ni At-Tubrusiy, Al-Majilisy, Al-Yuusufiy na Muhammad Husayn Fadhlullah
kama tulivyoona.
Na hii chini ni anuani ya mtandao unaoitwa Az-Zahraa wa mwanachuoni wao aliyesema uongo juu ya aayah
hizi, na ndani ya mtandao huu zimo hotuba mbili za Muhammad Fadhlullah akitamka
kuwa aayah hizo ziliteremshwa kwa ajili ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).