SAYID AL ISTIGHFAR
Tembelea: http://mawaidha.info/
Mwezi wa
Ramadhani huo unaingia. Mwezi wa Rehma,
mwezi wa Barka, mwezi wa
Maghfira, mwezi wa kuepushwa na
moto wa Jahannam.
Mwenyezi Mungu ametutunukia
mwezi huu
Kwa ajili hii
inatupasa kuukabili ukarimu huu utokao
kwa Mola wetu Mkarimu Subhanahu
wa Taala kwa kujitakasa na kutubu kutokana
na madhambi tuliyoyachuma miezi kumi na moja
iliyopita huku tukimuomba atughufurie na huku tukimuahidi
kutoyarudia tena madhambi hayo.
Mwenyezi Mungu anasema:
"Na ambao pindi
wafanyapo uchafu au wakajidhulumu nafsi zao humkumbuka Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha
kwa dhambi zao - na nani
anaye futa dhambi isipo kuwa
Mwenyezi Mungu? - na wala hawaendelei
na waliyo yafanya na hali
wanajua."
Aali Imran – 135
Imepokelewa kuwa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu
alayhi wa sallam) amesema:
"Mwenyezi Mungu huifurahia toba ya mja
wake kuliko mmoja wenu anapokuwa juu ya mnyama
wake jangwani akamuangusha na kumkimbia."
Bukhari
Na katika riwaya ya Muslim na wengine:
"Mwenyezi Mungu huifurahia toba ya mja
wake kuliko mmoja wenu anapokuwa juu ya mnyama
wake jangwani akamuangusha na kumkimbia. Mnyama
huyo akiwa amebeba chakula chake na maji
yake, kisha mtu huyo akakata
tamaa, akauendea mti na kuegemea
chini ya kivuli chake akiwa
keshakata tamaa ya kumuona mnyama
wake tena. Na anapokuwa katika hali hiyo,
ghafla anamuona mnyama wake mbele yake. Akazishika hatamu zake, kisha
akasema kwa furaha: "Mola wangu Wewe ni
mja wangu na mimi ni
mola wako". Alikosea kwa wingi
wa furaha."
Muslim na wengine
Na maana ya
Mwenyezi Mungu kuifurahia toba hiyo ni kuwa
anaridhika na nia ya mja
wake huyo juu ya kuwa alikosea
kutamka.
Miongoni mwa dua
za kuomba maghfira ni hii
dua inayoitwa 'Sayyid al Istighfaar' (Dua bora ya kuomba
Maghfira kupita zote) aliyotuusia Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Laahu alayhi wa
sallam). Dua ambayo ndani yake
imekusanya maana zote za Toba
na kukiri na kwamba hapana
mwenye kusamehe makosa isipokuwa Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala.
Imepokelewa kutoka Shaddad
bin Aus (Radhiya Llahu anhu) kuwa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu alayhi
wa sallam) amesema:
"Bwana wa
kuomba maghfira ni kusema:
Çááøóåõãøó
ÃóäúÊó ÑóÈøöí áÇ Åöáóåó ÅáÇ ÃóäúÊó ÎóáóÞúÊóäöí æóÃóäóÇ ÚóÈúÏõßó æóÃóäóÇ Úóáóì
ÚóåúÏößó æóæóÚúÏößó ãóÇ ÇÓúÊóØóÚúÊõ ÃóÚõæÐõ Èößó ãöäú ÔóÑøö ãóÇ ÕóäóÚúÊõ ÃóÈõæÁõ áóßó ÈöäöÚúãóÊößó Úóáóíøó
æóÃóÈõæÁõ áóßó ÈöÐóäúÈöí
ÝóÇÛúÝöÑú áöí ÝóÅöäøóåõ áÇ íóÛúÝöÑõ ÇáÐøõäõæÈó ÅöáÇ ÃóäúÊó.
(Allahumma anta Rabbiy laa ilaaha
illa Anta. Khalaqtaniy wa ana abduka.
Wa ana alaa
ahadika wa waadika ma statwaatu. Audhu bika min sharri ma sanaatu. Abu'u laka biniimatika alayya wa
abu'u laka bidhanbiy, faghfirliy, fainnahu laa yaghfiru
dhunuuba illa anta.)
Akasema: "Atakayesema
hayo wakati wa mchana
akiwa na yakini juu yake
akafa siku hiyo kabla ya
usiku kuingia, huyo ni katika
watu wa Peponi.
Na atakayesema hayo wakati wa usiku akiwa na yakini juu yake akafa
kabla ya asubuhi kuingia, huyo ni katika
watu wa Peponi."
Bukhari na
Attirmidhy na Annasai na wengine
Maana ya yake
|
Ewe Allah. Wewe ni Mola wangu
mlezi hapana anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Wewe |
Çááøóåõãøó ÃóäúÊó ÑóÈøöí áÇ Åöáóåó ÅáÇ ÃóäúÊó |
|
Umeniumba na mimi ni
mja Wako |
ÎóáóÞúÊóäöí
æóÃóäóÇ ÚóÈúÏõßó |
|
Na mimi nimo katika kutekeleza
maamrisho Yako na waadi Wako niwezavyo |
æóÃóäóÇ
Úóáóì ÚóåúÏößó æóæóÚúÏößó ãóÇ ÇÓúÊóØóÚúÊõ |
|
Ninajikinga Kwako na
kila shari niliyoitenda |
ÃóÚõæÐõ
Èößó ãöäú ÔóÑøö ãóÇ ÕóäóÚúÊõ |
|
Ninakiri Kwako kwa
neema Zako juu yangu |
ÃóÈõæÁõ áóßó
ÈöäöÚúãóÊößó Úóáóíøó |
|
Na ninakiri Kwako juu ya
dhambi zangu |
æóÃóÈõæÁõ áóßó ÈöÐóäúÈöí |
|
Kwa hivyo unisamehe
kwa sababu hapana mwenye kusamehe madhambi isipokuwa Wewe |
ÝóÇÛúÝöÑú
áöí ÝóÅöäøóåõ áÇ íóÛúÝöÑõ ÇáÐøõäõæÈó ÅöáÇ ÃóäúÊó. |
Nakutakieni nyote
na kila
Muislamu Ramadhani njema ya mwaka
huu na kila
mwaka, huku nikimuomba Mwenyezi Mungu atujaalie tufaidike na Ramadhani
hii na nyingi
zijazo. miaka
baada ya miaka -Amin