KATIKA

KUTHIBITISHA KUONEKANA ALLAH

(SUB’HAANAHU WATA’ALAA) KWA MACHO HUKO AKHERA

MAJIBU NA MAELEZO

Muandishi: Abul Fadhl Kassim Mafuta Kassim

Yaliyomo

Utangulizi 5

Pongezi Na Shukrani (1) 11

Pongezi Na Shukrani (2) 13

Shukrani 20

Mpangilio Wa Kitabu Hiki 22

Sura Ya Kwanza. 25

Vipi Tutamfahamu Mola Wetu Na Wapi Tuichukue Imani Ya Dini Yetu?. 25

Sura Ya Pili 34

Uchambuzi Yakinifu Juu Ya Elimu Ya Hadithi. 34

Mashar’ti Ya Usahihi Wa Hadithi 37

Tuhuma Za Uwongo Dhidi Ya Ahli Sunna. 42

Majibu Yetu. 45

Tuhuma Ya Kwanza. 46

Majibu Yetu. 47

Tuhuma Ya Pili 51

Majibu Yetu. 52

Majibu Yetu. 59

Historia Ya Abul-Hasan Kwa Ufupi 60

Yaliyomo Katika Kitabu “Al-Ibana”. 63

Tuhuma Ya Tatu. 68

Majibu Yetu. 69

Majibu Yetu. 71

Tuhuma Ya Nne. 76

Majibu Yetu. 77

Sura Ya Tatu. 87

Chanzo Na Chimbuko La Upotevu. 87

Uchambuzi Yakinifu Juu Ya Suala La Majazi 93

“Chanzo Cha Kutumbukia Katika Itikadi Batili 95

Majibu Yetu. 96

Je Wenye Kupinga Majazi Wana Hoja Za Kielimu?. 102

Hoja Yao Ya Kwanza. 102

Hoja Yao Ya Pili 104

Hoja Za Wenye Kuthibitisha Majazi 107

Majibu Ya Wenye Kupinga. 108

Hoja Yao Ya Tatu. 111

Sura Ya Nne. 116

Hoja Za Wenye Kuitakidi Kuonekana Allah Huko Akhera. 116

Hoja Ya Kwanza. 117

Jaribio La Kwanza La Kuipotosha Hoja Hii 123

Majibu Yetu. 125

Majibu Yetu. 128

Jaribio La Pili La Kupotosha Hoja Hii 135

Majibu Yetu. 137

Majibu Yetu. 141

Hoja Ya Pili 145

Jaribio La Kwanza La Kuipotosha Hoja Ya Pili 154

Juma Na Sheikh Wake Al-Qannubi Wamzulia Uwongo Sheikh Al-Bani. 167

Majibu Yetu. 168

Hata Mufti Wao Pia Asema Uwongo! 179

“Kasoro Ya Pili Ya Hadithi Hii: 181

Nakala Kutoka Kwa Al-Qannubi. 181

Majibu Yetu. 181

Maana Sahihi Ya Neno “Al-Ziyadah”. 184

Majibu Yetu. 185

Majibu Yetu. 190

Mukhtasari 197

Hoja Ya Tatu. 198

Hadithi Ya Kwanza. 201

Sanadi Ya Hadithi Hii 206

Kuhusu Mat’ni Ya Hadithi Hii: 206

Jaribio La Kwanza La Kupotosha Hadithi Hii 208

Majibu Yetu. 208

Tuhuma Yake Ya Pili Dhidi Ya Qais: 211

Majibu Yetu: 212

Majibu Yetu. 215

Jaribio Lake Jingine. 216

Majibu Yetu. 218

Ufahamu Wake Mbaya Juu Ya Hadithi Hii 225

Majibu Yetu. 227

Hadithi Ya Pili 236

Jaribio La Kwanza La Upotoshaji 245

Majibu Yetu. 245

Jaribio Lake La Pili 252

Majibu Yetu. 253

Jaribio Lake La Tatu. 255

Majibu Yetu. 256

Jaribio Lake La Nne. 259

Majibu Yetu. 260

Majibu Yetu. 262

Sura Ya Tano. 270

Hoja Za Wenye Kupinga Kuonekana Allah Kwa Macho Huko Akhera. 270

Majibu Yetu. 274

Hoja Yao Ya Kwanza. 276

Majibu Yetu. 278

Hoja Yao Ya Pili 297

Majibu Yetu. 298

Majibu Yetu. 304

Jaribio Lake Jingine La Upotoshaji 311

Majibu Yetu. 312

Hoja Yao Ya Tatu. 314

Majibu Yetu. 315

Hoja Yao Ya Nne. 317

Majibu Yetu. 318

Hadithi Wanayoitegemea. 324

Majibu Yetu. 325

Sura Ya Sita. 327

Kauli Za Baadhi Ya Maimamu Juu Ya Suala Hili. 328

Jaribio La Kuipotosha Kauli Hii 329

Majibu Yetu. 329

Hatima. 337

 

 

© 2008-02-25 Haki ya uchapishaji inamilikiwa na muandishi.

 

Ni ruhusa kwa mtu yoyote kukitoa copy na kukisambaza kitabu hiki kwa dhumuni la kufikisha ujumbe kwa waislamu kokote walipo.

Lakini hairuhusiwi kubadilisha chochote bila ruhusa ya muandishi wa kitabu hiki.

 

Abul-Fadhli Kassim Mafuta Kassim

 

 

KITABU HOJA ZENYE NGUVU KATIKA KUTHIBITISHA KUONEKANA ALLAH KWA MACHO HUKO AKHERA, MAJIBU NA MAELEZO.

 

MARKAZ SHEIKHIL-ISLAMI IBN TAYMIYYAH AL-SALAFIY,

P.O.BOX 398 TANGA,

MOBILE: 0715 615645 / 0784 615645.

BARUA PEPE: kassimmafuta@yahoo.com

PONGWE-TANGA.

TANZANIA.

                                              

UTANGULIZI

بسم الله الرحمن الرحيم

إنَّ الحمْدَ للهِ نَحْمَدُهُ ونستعينُ بهِ ونَستَغْفِرُهُ، ونعوذُ باللهِ من شرورِ أنفُسِنا وسيِّئاتِ أعمالِنا من يهْدِهِ اللهُ فلا مضل له ، ومن يُضْلِلْ فلا  هاديَ له. وأشهد أن لا إلهَ إلاّ اللهُ وحدَهُ لا شريكَ له. وأشهَدُ أنَّ مُحمَّداً عبْدُهُ ورَسولُهُ، ارسله بالهدى ودين الحق ليظهره على الدين كله ولو كره الكافرون.

(يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنْتُمْ مُسْلِمُونَ)([1]) [سورة آل عمران: الآية: 102]. (يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُمْ مِنْ نَفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالاً كَثِيراً وَنِسَاءً وَاتَّقُوا اللَّهَ الَّذِي تَسَـاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ إِنَّ اللَّهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيباً)([2]) [سورة النساء، الآية: 1].

(يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَقُولُوا قَوْلاً سَدِيداً يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَنْ يُطِعِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزاً عَظِيماً)([3]) [سورة الأحزاب، الآيتان: 70، 71].

أما بعد فإنَّ أصدَقَ الحَديثِ كِتَابُ اللهِ تعالى، وخَيرَ الهَدْيِ هَدْيُ مُحَمدٍ صلى الله عليه وسلَّمَ، وشَّرَّ الأمورِ محدثاتُها، وكُلَّ مُحْدَثَةٍ  بِدْعَه وكُلَّ بدعةٍ ضلالةٌ، وكُلَّ ضلالَةٍ في النار.

 

Ama baada ya kumsifia mola wetu kwa sifa njema, sina budi kumswalia Mtukufu Mtume wetu Muhammad –swalla llaahu alayhi wasallam-, na swala na salamu hizo pia ziwafikie Aali zake, wake zake, maswahaba zake na wale wote walioiandama njia yao kwa wema mpaka siku ya malipo.

 

Kwanza, napenda kusema machache kuhusu kitabu hiki, sababu za kuandikwa kwake na madhumuni yake.

Sababu kuu na asili ya kitabu hiki ni majibu na maelezo dhidi ya kitabu kiitwacho; “HOJA ZENYE NGUVU JUU YA KUTOONEKANA MWENYEZI MUNGU KWA MACHO” cha Ndugu JUMA M. Al-Mazrui.

Maudhui ya kitabu hicho ni kama kinavyojieleza chenyewe katika anwani yake, nayo ni kupinga kuonekana kwa Allah kwa macho huko akhera, na hiyo ndiyo itikadi ya makundi mengi ya batili kama vile: Mu’tazila, Khawariji (Ibadhi), Shia, na wengineo.

 

Ndugu Juma M. Al-Mazrui muandishi wa kitabu hicho hakuleta jambo jipya, bali amejikakamua kwa kiasi kikubwa mno kuitetea itikadi hiyo batili inayopingana na mafundisho sahihi ya Qur’an na Sunna za Mtume wetu Muhammad-swalla llaahu alayhi wasallam-.

Baada ya kukisoma kwa utulivu na umakini kitabu hicho chenye kurasa 339 kutoka mwanzo hadi mwisho, sikuweza kuuvumilia upotoshaji alioufanya, ndipo nilipoamua kukirudia tena na tena kwa lengo la kuyadhibiti yale ambayo nimeyaona kuwa ndio mambo ya msingi aliyoyategemea muandishi huyo kwenye kitabu chake hicho kwa lengo la kutaka kuhakiki zaidi.

Baada ya kufanya utafiti wa kielimu ambao lengo lake lilikuwa ni kupata faida, nikaona kuwa ninaowajibu wa kuzitawanya faida hizi ili ziwafikie wengineo katika waislamu ambao wengi wao hawana uwezo wa kufanya utafiti wa kielimu kwa kutumia misingi sahihi mpaka kuufikia ukweli.

Kutokana na majukumu niliyonayo pamoja na ufinyu wa wakati, kazi hii niliiona kuwa ni ngumu mno hivyo nilikata tamaa, kwa sababu shughuli hii si ndogo na inahitaji muda wa kutosha, lakini mambo makuu manne ndiyo yaliyonipa moyo wa kukiandika kitabu hiki:

i) Amri zilizokuja kuhimiza kuibainisha haki, na makatazo yaliyokuja kuharamisha kuinyamazia batili.

 

ii) Hali ya hatari ambayo inayowakabili waislamu wengi hasa wale wasio na uwezo wa kufanya utafiti wa kielimu; ima kwa sababu ya udhaifu wa kielimu au kwa sababu ya uvivu wa kutafiti au kukosa nyenzo za kufanyia utafiti huo au kwa sababu nyinginezo, hivyo hawataweza kukabiliana kielimu dhidi ya ubabaishaji alioufanya ndugu Juma, na hatima yake wataingia kwenye dimbwi la batili kwa kudhania kuwa upotoshaji alioufanya ndugu Juma Mazrui kuwa ni haki.

 

iii) Kupambana kwa kalamu dhidi ya watu wa bid’a na wapotoshaji wote ni moja katika amali njema za kumweka mtu karibu na Mola wake kwa sababu ni katika sampuli za Jihadi.

 

iv) Na kwa kuwa suala hili linafungamana na kuhusiana na mambo ya itikadi, ambayo ndiyo msingi wa dini, bado tuna wajibu wa kuielimisha jamii hata kama hakujitokeza mpotoshaji.

Kwa kuyazingatia yote hayo, nilipata ari na hima ya kulikabili jambo hili kwa  umakini, na kwa Tawfeeq ya Allah nikafanikiwa kukikamilisha kitabu hiki kwa salama.

Na zote hizo ni miongoni mwa fadhila nyingi za Mola wangu juu yangu, ninamuomba anijaalie niwe miongoni mwa wenye kumshukuru.

 

 

Muandishi.

 

 

Abul-Fadhli Kassim Mafuta Kassim.

 

 

كلمة شكر وتقدير

 

بسم الله الرحمن الرحيم

الحمد لله رب العالمين والصلاة والسلام على اشرف الانبياء والمرسلين وعلى آله واصحابه والتابعين لهم باحسان الى يوم الدين.

فقد اطلعت على كتاب الأخ الفاضل ابى الفاضل قاسم مفوتا فاسم فوجدته كتابا مفيدا فياثبات رؤية الله تعالى في الآخرة وكشف فيه عن كذب الأخ جمعة المزروعي وشوخه وتلبيسهم في تلك الحجج الظاهرة كالشمس في رابعة النهار. فجزى الله المؤلف عنا وعن المسلمين خير، وبارك الله له في علمه وفي جهوده الجبارة في نشر عقيدة السلف الصالح والذب عنها.

وصلى الله وسلم على نبينا محمد وعلى آله وصحبه أجمعين.

كتبه الفقير الى رحمة الله:

ابوهاشم عبدالقادر بن هاشم بن عبدالقادر المساوي

13/جمادي الأولى/1430 هـ

8/مايو/2009

Rudi juu

PONGEZI NA SHUKRANI (1)

 

Sifa njema zote ni za Allah Bwana wa viumbe wote, na swala na salamu zimshukie mtukufu wa Manabii na Mitume, na Jamaa zake na Swahaba zake na waliowafuatia hao kwa wema mpaka siku ya malipo.

 

Ama baada ya yaliyotangulia.

 

Nimekitalii kitabu cha ndugu mbora Abul-Fadhli Kassim Mafuta Kassim, nikakikuta kuwa ni kitabu kilicho na faida kwa sampuli yake, katika kuwajibu Makhawariji wa Kiibadhi, pale mtunzi alipozileta HOJA ZENYE NGUVU katika kuthibitisha kuonekana Allah huko Akhera kwa macho, na akaufichua uwongo wa ndugu Juma Al-Mazrui na masheikh zake pamoja na ubabaishaji wao kwa hoja za wazi wazi kama vile jua lililokuwa katikati ya mchana.

 

Allah amlipe mtunzi kheri kwa sababu ya kuwatumikia waislamu, na ambariki katika elimu yake na juhudi zake kubwa katika kuitangaza itikadi ya Salaf na kuitetea.

 

Na swala na salamu zimshukie Mtume wetu Muhammad na Jamaa zake na Maswahaba zake wote.

 

 

 

Al-Akhi Sheikh Abu Hashim Abdul-Qadir Ibn Hashim Ibn Abdul-Qadir Al-Musawaa

13 /Jumadal-Ulaa /1430 H.

8 /Mei / 2009 M.

Rudi juu

Pongezi na Shukrani (2)

 

Ama baada ya kukipitia kitabu cha ndugu yetu Abul fadhli Kassim Mafuta, kitabu chenye anuani ya kitabu HOJA ZENYE NGUVU katika kuthibitisha kuonekena Allah kwa macho huko akhera, majibu na maelezo, kitabu hiki nimekipitia chote kwa uwangalifu na insaafu, ni kitabu madhubuti kinacholingana na jina lake kwani makusudio yake makubwa ni kutetea itikadi sahihi ya Manabii na Mitume wote, itikadi ya AHLI SUNNATI WAL-JAMAA dhidi ya waandishi wa uwongo, walio dhidi ya itikadi hii safi, kwani kitabu hiki kimebainisha waziwazi kwa hoja sahihi juu ya upotovu  wa mtunzi wa kitabu kiitwacho HOJA ZENYE NGUVU JUU YA KUTOONEKANA MWENYEZI MUNGU KWA MACHO cha ndugu JUMA AL-MAZRUI ambae ni miongoni mwa wafuasi wa mapote ya matamanio kwani ndugu Juma ndani ya kitabu chake hicho amemsingizia uwongo Mwenyezi Mungu na Mtume wake kama kawaida ya watu wa matamanio kumsifu Allah sub’haanahu wata’alaa kwa sifa ambazo ametakasika nazo za kutoonekana, ilhali  Mwenyezi Mungu Sub’haanahu wata’alaa amejisifu yeye mwenyewe nafsi yake kwa sifa ya kuonekana huko akhera na pia akasifiwa na Mtume wake Muhammad swalla llaahu alaihi wasallam kwa sifa hiyo hiyo ya kuonekana na hii ndio itikadi ya Maswahaba wa Mtume Muhammad  swalla llaahu alaihi wasallam na ndio itikadi ya Taabiina na wema waliofuata baada yao itikadi ya Ahli-Sunnat Wal-Jamaa.

Ndugu Juma Al-Mazrui ameandika kitabu hicho ili atetee itikadi yake ya kikhawarij kama ilivyo kawaida ya watu wa matamanio kabla ya kusoma na kufahamu jambo, wao kwanza ni kutetea itikadi zao vyovyote iwavyo kama vile walivyoipokea toka kwa mababu zao, lakini kwa rehema za Mwenyezi Mungu sub’haanahu wata’alaa amejaalia katika umma huu kama anavyosema Mtume katika hadithi sahihi kwamba: HALITAACHA KUWEPO KUNDI KATIKA UMMA WANGU LENYE KUPIGANIA HAKI HAWATADHURIWA NA WASIOWASAIDIA NA WALA HATADHURIWA NA WANAOWAPINGA  MPAKA KITAKAPO SIMAMA KIYAMA na watu hawa ni AHLI-SUNNAT WAL-JAMAA.

Ama ndugu Juma Mazrui mimi namlaumu sana kwa kufanya haraka kuandika kitabu hicho bila ujuzi wa dini, lakini baada ya lawama namuomba Mwenyezi Mungu amuongoze ndugu Juma na ampe maarifa na amtoe katika hali ya itikadi potofu, kwani kubwa la Juma ni kumuamini sana Said Mabruk Al-Qanuubi bila kumuelewa elimu yake na uwadilifu wake kwani inaonyesha bwana Juma hamfahamu bwana huyu Qannubi na ndio maana akampachika majina makubwa ya kielimu ambayo hastahiki jinsi alivyo, kwani Said Qannubi si mwengine zaidi ya kuwa ni mwanakasumba wa kikhawariji si mkweli, angelikuwa ni mkweli asingelifikia hali ya kunukuu hoja hai za ndani ya vitabu vya wanakasumba na watu wa matamanio na yeye kuzifanya hoja za kuwarudi Ahli-Sunnat wal-Jamaa.

 

Ama marudio anayorudiwa ndugu Juma ndani ya kitabu hiki ni malipo yatokanayo na chumo la mikono yake iliyoandika maandiko ya Qannubi ambaye ni  mwanakasumba wa kikhawariji aliyeiajiri mikono yake juu ya kunukuu maneno ya watu wa matamanio wenye chuki dhidi ya wanasunnah, na maimamu wa Ahli-Sunnat.

Miongoni mwa watu anaowaiga Qannubi maandiko yao ni kama Al-kauthari, na Abuu Ghudah na Jamal-din Af’ghani ambaye si Muaf’ghani bali ni Muirani, na Butwi na Al-Maliki katika watu wa hivi karibu na pia miongoni mwao hao ni pote la Muutazilah kwani wao ndio wanaopinga sana kuonekana kwa Mwenyezi Mungu sub’haanahu wata’alaa kwani pote hili elimu yao yote imejengeka juu ya misingi ya mijadala ambayo asili yake ni vipimo vilivyo juu ya kufananisha kisichopo kwa kilicho kuwepo na miongoni mwa maigizo ya Qannubi ni pote la Jahmiyyah, Baatiniyya, Mashia Imamiyyah ndio maana utayakuta maandishi yao yote juu ya kutoonekana  Mwenyezi Mungu sub’haanahu wata’alaa wanayanukuu kwa mwana matamanio mkubwa adui wa Mwenyezi Mungu sub’haanahu wata’alaa Abdul Jabbar al-Muutazili kwenye kitabu chake almughni, hasa katika zile hoja za kiakili alizozitaja Alkhalili kama alivyomnukuu Juma Mazrui katika kitabu chake Al-Haqu Addamigh ukurasa 67, kwamba kuona kwa macho ni kuingia sura …., na kadhalika amefananisha kuonekana Mwenyezi Mungu sub’haanahu wata’alaa na kuonekana viumbe, ametakasika Mwenyezi Mungu na dhana zao.

 

Na vilevile Qannubi si mwenye elimu ya vitendea kazi (Qawaid)  vya elimu za waislamu kama somo la hadithi na ala zake na usuli na misingi ya fiqhi na lugha ya waarabu, lakini ni shujaa asiye na uwoga wala aibu na ndio maana utakuta mara nyingi hutoa hukumu juu ya hadithi kutokana na ushujaa wake mfano;- anasema kwamba hadithi ambazo zimepokewa zenye kuifasiri aya ya 22 na ya 23 za surat Al-Qiyamah ni dhaifu na za uwongo, na Juma Al-Mazrui akamfuata kiongozi wake Qannubi na ilhali hadithi hizo zote zilizokuja kutafsiri aya hizo ni Mutawatir kwa mujibu wa majio yake na kwa mujibu wa ushuhuda wa wanazuoni wa somo la hadithi, pia Qannubi kutokana na kutoelewa somo hili utakuta anamtia ila (dosari) mpokezi wa hadithi pasi na kuielewa ila ile kwamba haiwi hadithi ya mpokezi yule ni dhaifu, mfano amemwita imamu Zuhri kwamba ni Mudalis ili aidhoofishe hadithi zake bila kubainisha ni tadlis ipi ili muradi atetee matamanio yake.

 

Haya nimeyataja machache, lakini makosa ya namna hii ni mengi juu ya Qannubi na mfano wa hayo, na yote haya yanatokana na kasumba za kimadhehebu zinazompelekea Qannubi na mfano wake kuandika mambo wasioyajua ili watetee madhehebu yao kwa hali na mali, mfano Juma Mazrui, nikisema kwamba hana ujuzi katika somo la hadithi sitakosea, lakini hebu tumsikilize yeye mwenyewe anavyojieleza katika kitabu chake “Hoja zenye nguvu”  katika ukurasa wa 194 anamwita mpokezi wa hadithi kwa jina ambalo sio lake, mpokezi huyu jina lake ni Ibn Halbas yeye akamwita Abu Halbas, mfano mwingine katika kitabu chake hicho katika ukurasa wa 69 amemwita Al-Duuriy, Al-Dauri na haya ni mengi mno kwenye maandiko ya Juma na haya ni kwa kuwa haja wahi kukaa na watu wa elimu hizi, labda aliwahi kukaa na Qannubi kisha akamuiga porojo zake na ndio maana akasema Ibnu-Halbas ni majhulil-ayn bila ya kubainisha ni majhul wa vipi, lakini yeye katika uibadhi wake Imamu wake aitwae Abuu Ubaidah Muslim Ibni Abi Karimah yeye ndiye Majhuli tena ni Majhulil-Ayn, mtu huyu ni kigano, lakini kwa kutojua kwao wanadhania yupo, sitaeleza mengi bali mengi yameshaelezwa ndani ya kitabu hiki na mwenye kutaka haya arudi kuangalia vitabu vya watu wa Sunnah kama kitabu Assunnah, Arrisalatu alhamawiyyatu alkubraa, Al-Aqidatu Atwahawiyah, na Minhaju Assunnah na vinginevyo.

 

Ama kitabu hiki cha ndugu yetu Abul-Fadhli ni kitabu kilichokusanya faida nyingi sana haswa katika somo azizi la hadithi na pia katika somo la lugha ya waarabu, faida ambazo hazipatikani katika vitabu vingi vilivyokwisha andikwa kwa lugha ya waswahili. Mwenyezi Mungu sub’haanahu wata’alaa amlipe ndugu yetu huyu kheri na amzidishie elimu na uongofu na kulingania dini ya Mwenyezi Mungu sub’hanahu wata’alaa kwa hekima na elimu, kwani Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kutakabali dua za watu wake na rehema na amani zimfikie Mtume wetu Muhammad swalla llaahu alaihi wasallam na Aali zake na Maswahaba zake.

 

Al-Akhi Sheikh Abuu Saam Seif .S. Al-Ghafriy.

Rudi juu

SHUKRANI

 

Ni Allaah peke yake ndiye wa kuhimidiwa na kushukuriwa, kwa hiyo sina budi kusema:

الحمد لله  (Al-Hamdu lillaahi) kwa kuniwezesha kukiandika kitabu hiki na ninamuomba Allaah akijaalie kitabu hiki kiwe ni chenye kheri, faida na manufaa kwa waislamu wote hasa wasomi wa mambo ya dini na wale wenye kuitafuta elimu ya dini na kuyafuatilia mambo ya dini kwa ukaribu na wakawa wako tayari kutoa wakati wao na hali na mali zao kwa ajili ya elimu ya kuutafuta ukweli kupitia elimu ya dini.

Pamoja na hayo, pia ninawashukuru wale wote ambao wametoa juhudi zao kwa njia mbali mbali kwa ajili ya kufanikisha kutoka kwa kitabu hiki, ima kwa kutoa nasaha na ushauri wao, au kwa kuutumia wakati na mali zao.

 

Pia ninawashukuru ndugu zangu wapenzi:

Sheikh Abu Hashim Abdul-Qadir Hashim Al-Musawaa Al-Hashimiy.

Na Sheikh Abu Saam Seif .S. Said Al-Ghafriy.

Kwa kazi yao kubwa waliyoifanya ya kukipitia kitabu hiki na kwa nasaha zao na ushauri wao walioutoa. Pia ninamshukuru ndugu yangu mpenzi Sheikh Abu Ar’qam Abdallah Muhsin kwa kunishajiisha na kunipa moyo wa kukichapisha kitabu hiki wakati nilipomuonyesha nuskha ya kitabu hiki kabla ya kukichapa.

Mwisho ninamshukuru Ahli yangu Ummul-Fadhli kwa ustahamilivu wake na uzito alioubeba mpaka nikaweza kukimaliza kitabu hiki.

 

Abul-Fadhli Kassim Mafuta Kassim

Markaz Sheikhil-Islami Ibn Taymiyyah, Pongwe-Tanga Tanzania

25/SHAABAN/1428 H = 26/08/08 M.

Rudi juu

MPANGILIO WA KITABU HIKI

Nimekianza kitabu hiki kwa kumsifia Allah sub’haanahu wata’alaa Mola wetu mkarimu na kumswalia Mtume wetu Muhammad swalla llaahu alaihi wasallam pamoja na Aali zake na Maswahaba zake wote.

Kisha nikalazimika kuzijibu baadhi ya tuhuma za uwongo ambazo amezileta ndugu Juma dhidi ya maulamaa wa kiislamu kama vile Ibnu Taymiyyah, na Ibnul-Qayyim Allah awarehemu kwa lengo la kutaka kuwachafua.

Kisha nikaweka mlango maalumu kwa ajili ya kuelezea kwa muhtasari uchambuzi wa elimu ya hadithi, na kanuni za upokezi wa habari.

Pia tukabainisha sababu za msingi za upotevu wa watu, na kuyabatilisha madai ya uwongo ya ndugu Juma pale alipodai kuwa chanzo na sababu ya upotevu ni kukataa kuwepo kwa majazi ndani ya Qur’ani.

     

Pia tumelazimika kujadili kielimu tena kwa muhtasari suala la Majazi kuwepo kwake na kutokuwepo na tofauti za maulamaa wa kiislamu juu ya suala hilo.

Kisha ndio tukaanza kuubainisha msimamo sahihi wa AHLI-SUNNA WALJAMAA,  juu ya mas’ala ya kuonekena Allah kwa macho huko akhera, na suala hili ndiyo maudhui mama ya kitabu hiki.

 

Na tumelizungumzia suala hili kwa namna tatu:

 

i) Kuithibitisha itikadi hii kupitia maandiko matakatifu ya dini yetu kama vile; Qur’an na Hadithi sahihi za Mtume Muhammad -swalla llaahu alayhi wasallam- pamoja na kutoa maelezo kwa muhtasari juu ya maandiko hayo. 

ii) Pia nimetumia kauli za Maswahaba na wanafunzi wa Maswahaba (Taabiina) na Maimamu wakubwa wa kiislamu kama vile Imamu Malik, Imamu Shaafiy, Imamu Ah’mad bin Hanbal na wengineo kwa lengo la kuutilia nguvu msimamo wetu, na kuibatilisha dhana ya kwamba itikadi ya kuonekana Allah akhera kwa macho ni itikadi ya wale ambao ndugu Juma na kaumu yake anawaita kuwa ni Mawahabi.

 

iii) Kuzivunja baadhi ya hoja batili zilizotolewa na muandishi huyo hasa zile ambazo ndiyo msingi aliojengea juu yake itikadi yake hiyo potofu.

 

iv) Mwisho tukamalizia kwa kuweka Khatima.

Hayo yote nimeyafanya kwa ufupi mno, na sikutaka kumjibu hoja baada ya hoja au neno kwa neno kwa kuhofia kurefusha, hasa ukizingatia kuwa ndugu Juma Mazrui amekijaza kitabu chake maneno mengi ambayo si ya kweli na yasiyo na uzito katika misingi ya kielimu.

 

Rudi juu

SURA YA KWANZA

 

VIPI TUTAMFAHAMU MOLA WETU NA WAPI TUICHUKUE IMANI YA DINI YETU?

 

Hili ni swali muhimu mno na jawabu sahihi la swali hili ndiyo ufumbuzi wa matatizo mengi yaliyojitokeza katika umma wa kiislamu, kwa sababu waislamu wengi hawajui vipi watamfahamu mola wao muumba, na wapi wanatakiwa kuichukua dini yao !

 

Ama Ahlu Sunna wal Jama’a wao wanaitakidi kwamba:

Tutamjua mola wetu kwa vile alivyojielezea yeye mwenyewe katika kitabu chake (Qur’an tukufu) na vile alivyotuelezea mjumbe wake mtukufu katika mafundisho yake yaliyo sahihi.

Kwa kuyathibitisha yale yote ambayo Allah amejithibitishia mwenyewe au ambayo ameyathibitisha Mtume wake -swalla llaahu alayhi wasallam-, na kuzikanusha sifa ambazo Allah na Mtume wake swalla llaahu alaihi wasallam wamezikanusha, bila ya kupotosha, wala kupinga, wala kumfananisha yeye na chochote katika viumbe vyake, pamoja na kufuta dhana ya kwamba kuyathibitisha yale ambayo Allah amejisifia nayo kuwa ni kumfananisha yeye –Jalla Jalaaluh- na viumbe vyake.

 

Na tunaichukua imani ya dini yetu kutoka kwenye Qur’an na Sunna (mafundisho) sahihi ya Mtume wetu Muhammad -swalla llaahu alayhi wasallam- pamoja na kuuzingatia ufahamu wa Salaf Swaalih (wema waliotangulia) kama vile; Maswahaba na Taabi’ina (wanafunzi wa Maswahaba) na maulamaa waliokuja baada yao.

Na hivi ndivyo tulivyoamrishwa na Qur’an kadhalika Sunna sahihi za Mtume swalla llaahu alayhi wasallam.

 

 

Amesema Allah -azza wajalla-:

وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ آمِنُواْ كَمَا آمَنَ النَّاسُ قَالُواْ أَنُؤْمِنُ كَمَا آمَنَ السُّفَهَاء أَلا إِنَّهُمْ هُمُ السُّفَهَاء وَلَـكِن لاَّ يَعْلَمُونَ

البقرة13

 

“Na wanapoambiwa:aminini KAMA WALIVYOAMINI WATU wanasema;

Tuamini kama walivyoamini wapumbavu?...”.

Suratul-Baqarah aya ya 13.

 

Imepokewa kutoka kwa Ibnu Mas’oud na Ibn Abbaas kwamba wamesema: “Watu waliokusudiwa hapa ni maswahaba”.

Tazama tafsiri al-Durrul-Manthuur juzuu ya 1 ukurasa 70-71.

 

Na maana ya aya hii ni kwamba makafiri na wanafiki walikuwa wakiambiwa kwamba wamuamini Allah kama walivyoamini Maswahaba wa Mtume Muhammad -swalla llaahu alayhi wasallam- wao kwa sababu ya kiburi, na jeuri zao walikuwa wakiwatukana Maswahaba kwa kuwaita wapumbavu, na hali ya kuwa wapumbavu ni wao !

 

Na amesema tena Allah:

فَإِنْ آمَنُواْ بِمِثْلِ مَا آمَنتُم بِهِ فَقَدِ اهْتَدَواْ وَّإِن تَوَلَّوْاْ فَإِنَّمَا هُمْ فِي شِقَاقٍ فَسَيَكْفِيكَهُمُ اللّهُ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ

“Basi wakiamini KAMA MLIVYOAMINI NYINYI (maswahaba) basi watakuwa wameongoka.Na wakikengeuka basi wao wamo katika upinzani”.

Suratul Baqarah aya ya 137.

 

Katika aya hii Allah anawataka Ahlul-kitabi (Mayahudi na Wakristo) wamuamini Allah kama walivyoamini Maswahaba na waislamu wote kwa ujumla walio na imani kama ya Maswahaba, na kama wataasi wakenda kinyume na Amri hiyo, basi wao watakuwa ni waasi na ni wapinzani wa Allah.

Na amesema tena Allah: 

 

وَمَن يُشَاقِقِ الرَّسُولَ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُ الْهُدَى وَيَتَّبِعْ غَيْرَ سَبِيلِ الْمُؤْمِنِينَ نُوَلِّهِ مَا تَوَلَّى وَنُصْلِهِ جَهَنَّمَ وَسَاءتْ مَصِيرًا

 

“Na anaye mpinga Mtume baada ya kumdhihirikia uwongofu na AKAFUATA NJIA ISIYOKUWA YA WAUMINI,tutamuelekeza alikoelekea mwenyewe,na tutamuingiza katika Jahannamu....”.

Surat An Nisaa aya ya 115.

Amesema Allah:

 

وَالسَّابِقُونَ الأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالأَنصَارِ وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ رَّضِيَ اللّهُ عَنْهُمْ وَرَضُواْ عَنْهُ

“Na wale waliotangulia, wakwanza katika Muhajirina na Answaari,na wale  waliowafuata kwa wema, Allah ameridhika nao, na wao wameridhika naye....”.

Suratut Tawba aya ya 100.

 

Kwa mujibu wa aya hizo zote tulizozitaja, tunatakiwa waislamu wote kuamini kama walivyoamini maswahaba wa Mtume Muhammad -swalla llaahu alayhi wasallam- pamoja na kuifuata njia waliyoipita.

 

Na kama imani zetu zitatofautiana na imani zao na njia yetu ikitofautiana na njia yao, basi tutakuwa ndani ya mashaka makubwa mno na upotevu uliowazi kama zilivyoeleza aya tulizozitaja.

 

Hivyo basi, tunapolizungumzia suala zima la kumuamini Allah –Sub’haanahu Wata’alaa- ni lazima tujiulize maswali yafuatayo:

 

Je imani zetu zinaendana na mafundisho ya Qur’an na Sunna kama walivyofahamu wema waliotangulia (Salaf Swalih)?

Je hivi tunavyoitakidi ndivyo walivyoitakidi hao Salafu Swalihi (wema waliotangulia) au la?

 

Na kama jawabu likiwa la, basi tujue kwamba tumo ndani ya upotevu kwa kuifuata njia isiyokuwa ya hao waumini wa mwanzo.

 

Na bila shaka, wao wameifahamu vizuri Qur’an na walimfahamu vizuri Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- kuliko walivyomfahamu na wanavyomfahamu na watakavyofahamu watakaokuja baada yao, ndiyo maana Allah akawasifia wao na wale walioifuata njia yao kwa wema, na akawaahidi mambo mazuri.

Na wakati huo huo akawasema vibaya wale waliyoihalifu njia hiyo, na kuwaandalia makazi  mabaya motoni -Allah atuepushe na adhabu zake-.

 

Hivyo basi, katika suala hili la kuonekana au kutokuonekana Allah kwa macho huko akhera pia tunatakiwa pale tunapozitazama aya na hadithi zinazo lizungumzia suala hili tuutangulize mbele ufahamu wa hao wema waliotutangulia (Salafu Swalihi) katika imani, vipi wao walizifahamu aya na hadithi hizo?

 

Na ilikuwaje imani yao juu ya suala hilo?

Je waliamini kwamba Allah ataonekena kwa macho huko akhera kama wanavyo amini Ahli Sunna?

Au Allah hataonekana kwa macho huko akhera kama ilivyokuwa itikadi ya makundi mengine kama vile: Jah’miyyah, Mu’tazila na wajukuu zao kama vile Shia, Ibadhi na wengineo miongoni mwa watu wa bid’a?

 

Inshaallah swali hili litajibiwa na kitabu chetu hiki, tafadhali fuatilia kwa makini na insafu utagundua ukweli juu ya suala hili.

 

Huenda mtu akatatizika au akatatizwa kwa kuambiwa: vipi tufuate njia ya hao waliotangulia (Maswahaba,Taabi’ina, na Maimamu waliokuja baada yao) na hali yakuwa wao wenyewe wametofautiana katika mambo mbalimbali?

 

Jawabu ni kwamba; tutashikamana na ufahamu wao katika mambo ambayo wameafikiana, na yale waliyotofautiana sisi tutaichukua kauli iliyoungwa mkono na maandiko sahihi, na wala haifai kuzusha kauli ya tatu zaidi ya kauli zao mbili zilizo tofauti.

 

Ama mambo ambayo hayakuwepo katika wakati wao katika yale ambayo yanafaa kutumia akili na rai, basi huo ndiyo uwanja wa kuogelea maulamaa katika kufanya ijtihadi na kutumia rai zao kwa mujibu wa kanuni na misingi ya kielimu. 

 

Swali la kujiuliza ni; Je hao wema waliotangulia wametofautiana juu ya suala la kumuona Allah kwa macho huko akhera?

 

Jawabu ni kwamba:

Maswahaba Hawakutofautiana katika suala hili, bali wote waliafikiana kwamba watu wema watamuona mola wao kwa macho huko akhera kama lilivyo thibitishwa suala hilo na Qur’an na Sunna sahihi za Mtume –swalla llaahu alayhi wasallam-.

 

Na hakuna mtu yeyote aliyemuona, wala atakayemuona Allah kwa macho yake hapa duniani, na hivyo ndivyo wanavyoamini na kuitakidi Ah’lu Sunna Wal-jamaa.

 

Lakini tofauti imekuja katika jambo ambalo ni nje ya maudhui yetu hii, jambo lenyewe ni: Je bwana Mtume –swalla llaahu alayhi wasallam- alimuona Mola wake katika usiku aliokwenda mbinguni (Miraji) ?

Jawabu ni kwamba, kuna kauli iliyopokewa kutoka kwa Ibn Abbas -Allah amridhie- kwamba; bwana Mtume –swalla llaahu alayhi wasallam- alimuona Mola wake katika usiku huo.

 

Wengi katika wanavyuoni wakayachukulia maneno yake hayo kwamba, makusudio yake ni kuwa bwana Mtume alimuona Mola wake kwa moyo wake, na wakategemea riwaya nyingine zilizopokewa kutoka kwa huyo huyo Ibn Abbas.

 

Ama kuhusu suala la kumuona Allah usingizini hili pia si katika maudhui ya kitabu hiki.

Rudi juu

 

SURA YA PILI

 

UCHAMBUZI YAKINIFU JUU YA ELIMU YA HADITHI.

 

Kabla ya kuanza kuzitaja hoja na dalili wanazozitegemea Ahli sunna wal- Jamaa juu ya kuonekana Allah kwa macho huko akhera, kwanza napenda kuzungumzia suala linalofungamana na elimu ya istilahi ya upokezi wa riwaya za hadithi za bwana Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- na suala hili litakuwa  katika nukta zifuatazo:

 

i) Kwanza, tufahamu kuwa mafundisho yote ya bwana Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- ni wah’yi (ufunuo) utokao kwa Allah, na Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- hazungumzi kwa matashi wala matamanio ya nafsi yake.

 

ii) Pili, mafundisho yote ya Mtume wetu Muhammad -swalla llaahu alayhi wasallam- yamehifadhiwa katika vitabu vya maulamaa wa Ahlu Sunna wal-Jamaa kwa ufanisi mkubwa mno kiasi ambacho hakuna jambo lolote linalohitajika kubainisha itikadi au hukumu ya mambo ya dini ya kiislamu isipokuwa jambo hilo  limedhibitiwa kwa ufanisi wa hali ya juu.

 

iii) Tatu, katika kuhakikisha kuwa mafundisho hayo sahihi ya dini ya kiislamu yanahifadhiwa na hayachanganyiki na upotofu wowote, maulamaa wa Ahli Sunna wal Jamaa wameweka misingi madhubuti  juu ya usahihi wa mapokezi hayo ya riwaya za hadithi za bwana Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- na ukweli wa wapokezi hao kama tulivyofundishwa na Qur’an tukufu pale aliposema Allah:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن جَاءكُمْ فَاسِقٌ بِنَبَأٍ فَتَبَيَّنُوا

 “Enyi mlioamini ! akikujilieni mwovu (fasiki) na habari yoyote ichunguzeni basi.”

al Hujraat (49) aya 6.

 

Kwa mujibu wa aya hii ni kwamba, si kila asemaye; amesema Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- atakuwa msemaji huyo ni mkweli, na atakayo yanukuu yatakuwa ni kweli maneno ya Mtume, bali ni lazima uchunguzi wa kina ufanyike ili kujua usahihi wa habari hiyo aliyoileta na udhaifu wake.

 

Kwa sababu hiyo, maulamaa wa hadithi baada ya kufanya utafiti wa kina pamoja na kutumia uzoefu wao wa muda mrefu, wakaweka misingi madhubuti inayowahusu wapokezi wa hadithi.

Pia wakaweka kanuni maalumu kwa ajili ya udhibiti wa njia sahihi za kukubaliwa hadithi na kurudishwa.

Na pia yakatumika maneno ya kiistalahi ambayo yanaleta maana maalumu na hayo yamejaa kwa wingi katika vitabu vyao.

 

Kwa mantiki hiyo, yeyote  anayetaka kuzungumzia masuala yanayofungamana na elimu ya hadithi; usahihi wake na udhaifu wake, hana budi kuzijua kanuni hizo na maneno hayo ya kiistilahi.

Na kama hatafanya hivyo, basi lililobora kwake ni kunyamaza kuliko kusema, kwa sababu hatima yake ni kupotosha watu kwa kuzisahihisha hadithi zisizo sahihi au kuzidhoofisha hadithi zilizo sahihi na yote mawili ni balaa, hasa ukizingatia kwamba maneno ya Mtume Muhammad -swalla llaahu alayhi wasallam- ni sheria.

 

 

Rudi juu

MASHAR’TI YA USAHIHI WA HADITHI

 

 1)  العدالة Uadilifu, ni lazima kila mpokezi wa hadithi za Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- awe ni mtu mwenye akili timamu,mwenye uwezo wa kupambanua mambo hata kama ni mtoto mdogo, awe mkweli, mcha mungu na wala asiwe mwongo, wala asiwe mwenye kufanya maasia kwa dhahiri wala asiwe na tabia mbaya zenye kuvunja heshima.

2)  لضبطا تمام Hifdhi nzuri, mpokezi awe na uwezo wa kudhibiti maneno aliyo yapokea, bila ya kubadilisha chochote katika maana yake,au kukosea sana,au kubabaika kulikopetuka mipaka wakati wa kusimulia mapokezi hayo.

3) السند اتصال Kuungana kwa sanadi (msururu wa wapokezi) kwa kuwa kila mpokezi awe amepokea kutoka kwa aliye juu yake mpaka mwisho wake (kwa huyo ambaye habari hiyo imenasibishwa kwake, ima bwana -Mtume swalla llaahu alayhi wasallam-, au swahaba, n.k.

4)  الشذوذ عدم Isiwe habari aliyoileta mpokezi huyo ni “SHAADHUN” (ni yenye kupingana na habari ya mpokezi mwingine aliye madhubuti au wengi zaidi kuliko yeye).

5) القادحة الخفية العلة عدم Wala isiwe na ila (kasoro iliyojificha) kama vile Idh’tiraabu (mgongano baina ya wapokezi n.k) au kuwa ni habari Maq’luub (yenye kugeuzwa)

 

Katika masharti haya tuliyoyataja, yako ambayo likikosekana moja tu basi hadithi haitakubaliwa,kama vile:

1-Kuwa mpokezi si muadilifu,kwa kuwa ni mwongo au asherati n.k.

 

2-Kupatikana kasoro kama vile mgongano katika sanadi (njia) au mgongano wa maneno katika habari hiyo, kisha ikawa imeshindikana kuziunganisha au kuipa nguvu njia moja juu ya nyingine.

 

Tanbihi:

Habari inaweza kuwa na njia nyingi, na katika njia hizo wakawepo  wapokezi wasio madhubuti kwa kuwa wanakosea kiasi, au silsila (mtiririko) wa wapokezi haukuungana, kutokana na wingi wa njia hizo habari hiyo itapata uzito na kuhesabiwa kuwa ni sahihi, na kwa lugha ya kitaalamu huwa wanaiita “HASANUN-LIGHAIRIHI”.

 

Amesema Imamu An-Nawawiy:

بل ما كان ضعفه لضعف حفظ رواية الصدوق الأمين من وجه آخر وصار حسنا وكذا اذا كان ضعفها لارسال زال بمجيئة من وجه آخر

 

 “Bali ile hadithi ambayo imekuwa ni dhaifu kwa sababu ya udhaifu wa mpokezi wake ambaye ni mkweli mwaminifu utaondoka (udhaifu huo) kwa kuja kwake kupitia njia nyingine na itakuwa ni HASAN (sahihi)

Na vile vile ukiwa udhaifu wake ni kwa sababu ya Ir’saal (atakaposema Taabi’I amesema Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam-) pia udhaifu huo utaondoka kwa kuja (kupokewa) kwa njia nyingine…”.

 

Hivyo basi, inawezekana ukaifuatilia hadithi kisha ukazikuta takriban njia zake zote zina udhaifu, hapo hutakiwi kuwa na pupa na kuanza kuihukumu hadithi yote kuwa ni dhaifu, bali unatakiwa kuihukumu sanad husika tu, na useme kwamba sanad ya hadithi hii ni dhaifu.

 

Kwa sababu udhaifu wa sanad moja tu, si ushahidi wa udhaifu wa hadithi yote yenye njia nyingi.

Na kama ukitaka kuihukumu hadithi yote kwa njia zake zote unatakiwa ufanye kazi ya kuzikusanya sanad (njia) zote kisha ndiyo uichambue sanad moja baada ya nyingine kwa kufuata kanuni na taratibu za elimu ya hadithi (mustalahul-hadithi).

Na kama itakubainikia kuwa njia zote zina udhaifu, basi pia unatakiwa kuangalia sababu za udhaifu wake.

Je  udhaifu wake ni mwepesi au mzito?

Kama ni mwepesi basi hadithi hiyo kwa kuzijumuisha njia zote hizo itakuwa ni “Hasanun-Lighayrihi” (sahihi) na itafaa kuifanya kuwa ni hoja ya kisheria, na wala haitohesabiwa kuwa ni dhaifu.

Hili ni jambo muhimu sana katika elimu ya hadithi kulifahamu na kulizingatia, lakini ndugu Juma kwa makusudi hakuuzingatia utaratibu huu kwenye kitabu chake “Hoja zenye Nguvu” kwa sababu anazozijua mwenyewe, kwani yeye ndiye aliyesema hivi:

“kitaalamu ikiwa hadithi imepokewa na wapokezi wengine kabisa, lakini hadithi ni ile ile, basi huambiwa kuwa hadithi hiyo ina shahidi.”

Mwisho wa kunukuu.

Tazama “Hoja zenye Nguvu” ukurasa 70.

 

Lakini  huko mbele -Inshaallah- utazigumdua sababu zilizomfanya ndugu Juma aupuuze utaratibu huu.

Rudi juu

 

TUHUMA ZA UWONGO DHIDI YA AHLI SUNNA

 

Kama ilivyokuwa kawaida ya watu wanaofuata matamanio ya nafsi zao katika mambo ya dini kama vile: Mayahudi, Manasara, Washirikina na kadhalika watu wa bid’a, huwa hawaachi kuwasema vibaya wale walioshikamana na njia sahihi na kuwataja kwa kebehi na uovu, tena mpaka kufikia kuwazulia uwongo.

 

Huu ndiyo mwenendo wao na sera yao tangu zamani, jambo la kusikitisha zaidi ni kuwa hata ndugu Juma naye ameifuata njia hiyo ovu dhidi ya Ahli Sunna wal-Jama’a.

 

Amekianza kitabu chake kwa mashambulizi yasiyo na ukweli dhidi ya Ah’li Sunna na maulamaa wao, tena bila ya kuwa na insafu wala uadilifu, bali chuki binafsi na uadui ndivyo  vilivyomuongoza na kumsababishia kuacha kuyahakiki mambo kwa njia za kielimu, kwa mfano:

 

1-Hakuna kitu kingine zaidi ya chuki kilichomfanya awaite Ah’lu Sunna kwa jina la Mawahabi, au Hashawiya, au Mujasima.

 

2- Hakuna kitu kingine zaidi ya chuki dhidi ya Ah’li Sunna kilichomfanya awatie kasoro kwa mambo ambayo hayakuthibiti kuwa ndiyo itikadi yao, kama  suala la kuwa Allah ana sura ya kijana, au ana viatu vya dhahabu na mengineyo.

 

3-Hakuna jambo jingine zaidi ya chuki na uadui lililompelekea kuwatuhumu baadhi ya wanavyuoni wa Ah’li Sunna kama vile Ibn Taymiyyah na Ibn Al-Qayyim kwa sababu ya misimamo  yao na kuwaita kuwa ni wanavyuoni wa kiwahabi! Maimamu wa Hashawiya! Mujasima! Na hali yakuwa hakuna tofauti yoyote baina ya misimamo yao hiyo na misimamo ya Maimamu wakubwa wa Ahli Sunna kama vile: Abu Hanifa, Imamu Malik, Imamu Shaafiy, Imamu Ah’mad Ibn Hanbal, Imamu Bukhari, Imamu Muslimu, Imamu Abu Daud, Imamu Tirmidhiy, Imamu Abul-Hasan Al-Ash’ariy, Imamu Abdul-Qadir Jaylaaniy !!!                                                                                                                 

                                                                                                                                                                                                            

Kwamfano katika suala la sifa za Allah: kuwa Allah ana mikono miwili, ana macho mawili, ana uso, anacheka, ana mguu na nyinginezo katika sifa za Allah za ukamilifu ambazo amejisifia nazo au amesifiwa na Mtume wake –swalla llaahu alayhi wasallam- utawakuta maimamu hawa wakubwa wanazithibitisha sifa hizo kama zilivyopokewa, na hivyo ndivyo anavyofanya Ibn Taymiyya na Ibn al-Qayyim.

 

Lakini Juma kwa sababu ya chuki zake dhidi ya Ibn Taymiyya na Ibn al-Qayyim  akalizungumzia suala hilo kwa sura ambayo msomaji anaweza kudhania kuwa Ibn Taymiyya na Ibn al-Qayyim wana itikadi ambayo si ya kiislamu na wala hakuna muislamu yeyote mwenye itikadi hiyo ila Ibn Taymiyya na mwanafunzi wake Ibnul-Qayyim.

 

Kwa mfano amesema Juma:

“Na itikadi hizi ambazo nitakutajia sasa hivi (Inshala) zimo hasa katika                                    madhehebu ya kiwahabi na wao wamezirithi kutoka kwa maimamu wa madhehebu za Al-hashawiya Al-mujasima kama Ibn Taymiyya Ibn Qayyim Al-jawziya na wengineo”.Mwisho wa kunukuu. Tazama kitabu chake “Hoja zenye Nguvu” ukurasa wa 23.

 Rudi juu

 

MAJIBU YETU

 

Sisi tunasema kwamba msimamo wa Sheikhul-Islami Ibn Taymiyya na mwanafunzi wake Ibn al-Qayyim katika mas’ala ya sifa za Allah hauna tofauti na msimamo wa Qur’an na Sunna, bali ndiyo msimamo wa maswahaba na wanafunzi wao, na ndiyo msimamo wa maulamaa wakubwa waliokuja baada ya wanafunzi wa maswahaba, kama vile: Abu Hanifa, Malik, Shaafiy, Ah’mad bin Hanbal, Abul-Hasan al-Ash’ariy na wengineo katika maimamu wakubwa, kwa hiyo kumuita Ibn Taymiyya na mwanafunzi wake Ibn al-Qayyim kuwa ni maimamu wa Hashawiya Mujasima ni matusi dhidi maimamu hao wote waliotangulia kama tutakavyoona hapo mbeleni Inshaallah.

 

Rudi juu

TUHUMA YA KWANZA

 

Kisha akasema ndugu Juma katika ukurasa wa 23:

“Falsafa ya Ibn Taymiyya kuhusu maumbile ni kuwa ulimwengu una sifa ya kutangulia kama alivyosema haya katika kitabu chake NAQDU MARATIBIL AL-IJMAA.

Nini maana ya sifa ya kutangulia? Sisi waislamu tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu tu ndiye mwenye sifa ya kutangulia, yaani kabla yake hapakuwa na kitu chochote: kila kilichopo tunapopajua na tusipopajua, tunapopaona na tusipopaona basi ni kiumbe cha Mwenyezi Mungu.

Lakini itikadi ya Ibn Taymiyya wanaemwita Sheikh wa waislamu ni kuwa Mwenyezi Mungu alikuwa navyo vitu ambavyo kutokana na hivyo ndio kaanzia kuumba maumbile yote.

Sasa suala ni kuwa hivi vitu vya nani? Je haoni yeye huyu Ibn Taymiyya kuwa falsafa hii inapelekea kurudi kwenye itikadi ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu zaidi ya mmoja?

Huyu ndiye ambaye Mawahabi wanamwita Sheikh Al-islam……”.

Mwisho wa kunukuu.

Rudi juu

 

MAJIBU YETU

 

Maneno yote haya ya ndugu Juma ni maneno ya uwongo yaliyojaa chuki dhidi ya mwanachuoni huyu mkubwa wa kiislamu, si kweli kwamba itikadi ya Ibn Taymiyya ni kuwa ulimwengu una sifa ya kutangulia.

Na wala maneno ya Ibn Taymiyya katika suala hili hayapelekei kwenye dhana ya kuwepo Mungu zaidi ya mmoja, lakini huo ni ufahamu mbaya wa ndugu yetu Juma uliosababishwa na chuki binafsi dhidi ya maulamaa wa Ah’li Sunna hasa Ibn Taymiyya.

 

Katika kubatilisha madai haya ya uwongo ya Juma, hebu tukunukulie kidogo ndugu msomaji  maneno ya Ibn taymiyya yanayohusu masuala haya ya maumbile, amesema Ibn Taymiyya:

كل ما سوى الرب حادث كائن بعد أن لم يكن وهو - سبحانه - المختص بالقدم والأزلية، فليس في مغعولاته قديم وإن قدر أنه لم يزل فاعلا وليس معه شيء قديم بقدمه، بل ليس في المفعولات قديم ألبته، بل لا قديم إلا هو - سبحانه - وهو وحده الخالق لكل ما سواه وكل ما سواه مخلوق كما قال – سبحانه ((الله خالق كل شيء)) الزمر26

درء تعارض العقل والنقل8/272

 

“KILA KISICHOKUWA MOLA NI CHENYE KUZUKA KIMEPATIKANA BAADA YA KUTOKUWEPO, ay eye (Allah) –Sub’hanah- ndiye mwenye kuhusishwa na kutangulia na azal, hakuna kitu katika viumbe vyake kilichokuwa ni chenye kutangulia, hata kama ikikadiriwa kuwa yeye (Allah) hakuacha kuwa ni mwenye kutenda, (lakini) hakuna kitu kilichotangulia kwa kutangulia kwake, bali hakuna kabisa katika viumbe (vyake ambavyo ) ni vyenye kutangulia, BALI HAKUNA KILICHOTANGULIA ILA YEYE (ALLAH) – Sub’haanah-.

Na yeye pekeyake  ndiye mwenye kukiumba kila kisichokuwa yeye, kila kisichokuwa yeye ni chenye kuumbwa kama alivyosema –Sub’ahaanah-:

((Allah ni muumba wa kila kitu))”. Surat Zumar aya ya 26.

Tazama kitabu Dar’u Ta’arudh juzuu ya 8 ukurasa wa 272 cha Ibn Taymiyya.

 

Ndugu msomaji, je kwa maneno haya umefahamu kwamba Ibn Taymiyya ana itikadi ya kuwa ulimwengu una sifa ya kutangulia kama anavyodai Juma?

 

Au umefahamu kwamba Ibn Taymiyya anasema kuwa kila kisichokuwa Allah ni chenye kuzuka na kimepatikana baada ya kutokuwepo?

 

Je kwa  maneno haya ya Ibn Taymiyya umefahamu kwamba ana itikadi ya kuwepo Mungu zaidi ya mmoja kama anavyodai ndugu Juma kuwa sheikhul islam Ibn Taymiyya ana itikadi hiyo?

Au umefahamu kwamba ndugu Juma si mkweli?

Hebu yatupie jicho maneno mengine ya Sheikul-Islam Ibn Taymiyya tuone anavyosema:

"كل واحد من أفعاله لا بد أن يكون مسبوقا بالفاعل وأن يكون مسبوقا بالعدم، ويمنتع كون الفعل المعين مع الفاعل أزلا وأبدا .. فافاعل يتقدم على كل فعل من أفعاله وذلك يوجب أن كل ما سواه محدث مخلوق"

مجموع الفتاوي 18/227-228

“Kila kitu katika vitendo vyake hakuna budi kuwa ni chenye kutanguliwa na mwenye kutenda na ni chenye KUTANGULIWA NA KUTOKUWEPO. NA HAIWEZEKANI KUWA KITENDO FULANI KILIKUWEPO PAMOJA NA MTENDAJI TANGU MWANZO NA AZAL…..

Mwenye kutenda (ambaye ni Allah) anakitangulia kila kitendo katika vitendo vyake na hilo linawajibisha kuwa KILA KISICHOKUWA YEYE (ALLAH) NI CHENYE KUZUKA NA NI CHENYE KUUMBWA”.

Tazama Maj’muul-Fatawa juzuu ya 18 ukurasa wa 227-228.

Bila shaka maneno haya yako wazi katika kuufichua uwongo wa ndugu Juma na wala hayahitajii maelezo.

Rudi juu

 

TUHUMA YA PILI

 

Kisha ndugu Juma akaleta tuhuma nyingine dhidi ya Ibn Taymiyya na mwanafunzi wake (Ibn al-qayyim) kuhusiana na suala la sifa za Allah akasema:

“Anasema Ibn Al-qayyim katika kitabu chake “HADI AL-ARWAAH” ukurasa wa 13 akitaja sifa za Mwenyezi Mungu anasema:

“na kwamba yeye (Mwenyezi Mungu) ana mikono miwili bila ya mfano na ana macho mawili na ana uso”. Naye Ibn Al-qayyim anasema kuwa kayanukuu maneno haya kutoka kwa Abul-hasan Al-ash’ari….

Lakini kudai kwamba maneno haya ni maneno ya Al-imamu Al-ash’ari ni kitu cha kutazama zaidi kwani wafuasi wa Al-imamu Al-ash’ari nao ni masuni kama mashafi hawakubaliani na haya”.

Mwisho wa kunukuu.

Tazama ukurasa wa 24-25 katika kitabu chake “Hoja zenye Nguvu”.

           

Rudi juu

MAJIBU YETU

 

Majibu yetu dhidi ya maneno haya ya ndugu Juma yatakuwa katika nukta kuu tatu:

Nukta ya kwanza:

Suala kuwa Allah ana Mikono miwili bila ya mfano.

Ana Macho mawili bila ya mfano.

Ana Uso bila ya kuwa na mfano.

Hii si itikadi ya Ibn Taymiyya na mwanafunzi wake peke yao, hiyo ndiyo itikadi iliyo elezewa na Qur’an na Sunna na ndiyo itikadi ya maswahaba na wanafunzi wao na ndiyo itikadi ya maimamu wakubwa wa kiislamu.

Amesema Imamu Shaafiy –Allah amrehemu-:

 

"لله تبارك وتعالى أسماء وصفات جاء بها كتابه وأخبر بها نبيه صلى الله عليه وسلم أمته.......أتانا أنه سميع وأن له يدين  بقوله ((بل يداه مبسوطتان)).

وقال رحمه الله :

"........وأن له وجهاً بقوله ((كل شيئ هالك إلاّ وجهه)).

 

“Allah –Tabaaraka Wata’alaah- ana majina na sifa ambazo zimetajwa na kitabu chake na amezielezea Mtume wake –swalla llaahu alayhi wasallam- kwa uma wake…… zimetufikia (habari) kuwa yeye ni mwenye kusikia na ana mikono miwili kwa kauli yake (Allah) : “Bali mikono yake (Mwenyezi Mungu) iwazi”.

Na akasema tena (Imamu Shaafiy) –Allah amrehemu-:

 

“…..Na yeye (Allah) ana Uso kwa sababu ya kauli yake (Allah):

((Kila kitu ni chenye kuangamia isipokuwa Uso wake))”.

Tazama kitabu “Twabaaqatul-Hanabila” juzuu ya 1 ukurasa wa 283-284 cha Imamu Ibn Abi Ya’ala.

Pia tazama kitabu “Man’haju Imami Shaafiy fi Ith’batil-Aqidah” ukurasa wa 370-378. cha Dkt. Muhammad al-Aqil.

 

قَالَ أَبُو عِيسَى رحمه الله:

 وَقَدْ قَالَ غَيْرُ وَاحِدٍ مِنْ أَهْلِ الْعِلْمِ فِي هَذَا الْحَدِيثِ وَمَا يُشْبِهُ هَذَا مِنْ الرِّوَايَاتِ مِنْ الصِّفَاتِ وَنُزُولِ الرَّبِّ تَبَارَكَ وَتَعَالَى كُلَّ لَيْلَةٍ إِلَى السَّمَاءِ الدُّنْيَا قَالُوا قَدْ تَثْبُتُ الرِّوَايَاتُ فِي هَذَا وَيُؤْمَنُ بِهَا وَلَا يُتَوَهَّمُ وَلَا يُقَالُ كَيْفَ هَكَذَا رُوِيَ عَنْ مَالِكٍ وَسُفْيَانَ بْنِ عُيَيْنَةَ وَعَبْدِ اللَّهِ بْنِ الْمُبَارَكِ أَنَّهُمْ قَالُوا فِي هَذِهِ الْأَحَادِيثِ أَمِرُّوهَا بِلَا كَيْفٍ وَهَكَذَا قَوْلُ أَهْلِ الْعِلْمِ مِنْ أَهْلِ السُّنَّةِ وَالْجَمَاعَةِ.

 وَأَمَّا الْجَهْمِيَّةُ فَأَنْكَرَتْ هَذِهِ الرِّوَايَاتِ وَقَالُوا هَذَا تَشْبِيهٌ وَقَدْ ذَكَرَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ فِي غَيْرِ مَوْضِعٍ مِنْ كِتَابهِ : الْيَدَ وَالسَّمْعَ وَالْبَصَرَ فَتَأَوَّلَتْ الْجَهْمِيَّةُ هَذِهِ الْآيَاتِ فَفَسَّرُوهَا عَلَى غَيْرِ مَا فَسَّرَ أَهْلُ الْعِلْمِ وَقَالُوا إِنَّ اللَّهَ لَمْ يَخْلُقْ آدَمَ بِيَدِهِ وَقَالُوا إِنَّ مَعْنَى الْيَدِ هَاهُنَا الْقُوَّةُ.

 و قَالَ إِسْحَقُ بْنُ إِبْرَاهِيمَ إِنَّمَا يَكُونُ التَّشْبِيهُ إِذَا قَالَ يَدٌ كَيَدٍ أَوْ مِثْلُ يَدٍ ......".

انظر جامع الترمذي 1/ 166 رقم الحديث 772.

 

Amesema Imamu Abu Issa Al-Tirmidhiy  –Allah amrehemu- alipoitaja hadithi namba 772:

“Na wamesema wengi katika wanavyuoni kuhusu hadithi hii na inayofanana na hii katika mambo ya sifa (za Allah) na kushuka Mola katika mbingu (iliyokaribu na) dunia, wamesema: zimethibiti riwaya nyingi kuhusu suala hili, na sisi tunaliamini na wala hatusemi kwa dhana na wala hatusemi vipi? Na hivi ndivyo ilivyopokelewa kutoka kwa Malik,Ibn Uyaina, na Abdullahi bin Mubarak kuwa wamesema kuhusu hadithi hizi: zipitisheni bila ya kuzipa namna.

Na hii ndiyo kauli ya wanavyuoni wa Ah’li Sunna wal-Jamaa. Ama Jah’miya wao wamezipinga riwaya hizi na wakasema: huko ni kumfananisha Allah (na viumbe).

Na hali yakuwa ametaja Allah katika kitabu chake katika sehemu nyingi: (ametaja kuwa ana) Mkono, Usikivu, Uoni.

Lakini Jah’miya wakazitafsiri aya hizi tofauti na wanavyuoni, wakasema: Allah hakumuumba Adam kwa mkono wake, na (wakasema kuwa) maana ya mkono hapa ni nguvu.

Na amesema Is’haq bin Ibrahim: inakuwa ni kumfananisha Allah (na viumbe) atakaposema: Mkono (wa Allah) ni kama mkono au mfano wa mkono (wa kiumbe).

Tazama kitabu chake Jamiul-Tir’midhiy/Sunan Tir’midhiy hadithi namba 772.

قال الإمام أبو جعفر محمد بن جرير الطبري [224-310]:

"القول فيما أدرك علمه من الصفات خبراً, وذلك نحو إخباره عز وجل أنه سميع بصير , وأن له يدين بقوله: ((بل يداه مبسوطتان))

وأن له وجهاً بقوله: ((ويبقى وجه ربك)) وأن له قدماً بقول النبي صلى الله عليه وسلم: ((حتى يضع الرب فيها قدمه)) وأنه يضحك بقوله: ((لقي الله وهو يضحك إليه))......".

مختصر العلو للعلي الغفار ص 224.

 

Amesema Imamu Abu Ja’far Muhammad bin Jarir al-Tabariy aliyefariki mwaka [310 H]:

“Kauli katika yale yaliyofahamika ujuzi wake katika sifa (za Allah) kwa habari, ni mfano wa kuelezea kwake (Allah) -Azza wajalla- kuwa yeye (Allah) ni mwenye kusikia mwenye kuona, na kwamba yeye (Allah) ana mikono miwili aliposema:

“Bali mikono yake (Mwenyezi Mungu) iwazi”.

 

Na kwamba yeye (Allah) ana Uso pale aliposema:

“Na utabakia Uso wa Mola wako”

 

Na kwamba yeye Allah ana Mguu, kwa kauli ya Mtume –swalla llaahu alayhi wasallam-: “Mpaka atakapo weka Mola ndani yake Mguu wake”

 

Na kwamba yeye (Allah) anacheka kwa kauli yake Mtume:

“Na atakutana na Allah na hali ya kuwa anamchekea”.

 

Tazama kitabu Mukh’tasarul-Uluwi ukurasa wa 224.

قال الإمام أبو بكر الخطيب  البغدادي [392-463]:

"فإذا قلنا : يد , وسمع, وبصر ,فإنما هو إثبات صفات أثبتها الله لنفسه , ولا نقول : إن معنى اليد القدرة....".

انظر كتاب " الصفات" للخطيب 16/ 43-44. بواسطة مختصر العلو ص 272.   

 

Amesema Imamu Abu Bakar al-Khatib al-Bagh’dadiy aliyefariki mwaka [463 H]:

“Sisi tunaposema: (kuwa Allah ana) Mkono, Usikivu,na Uoni ni kuthibitisha sifa za Allah kama alivyo jithibitishia mwenyewe, na wala hatusemi maana ya mkono ni uwezo…..”.  

Tazama Mukh’tasarul-Uluwi ukurasa 272.

 

Hizi ni baadhi ya kauli za maulamaa wa Ah’li Sunna ambao wamemtangulia Ibn Taymiyya kwa kar’ne nyingi.

Wao wanasema kuwa Allah ana Macho, Mikono miwili, Mguu, n.k. na hiyo ndiyo itikadi ya maimamu wote wanne: Abu Hanifa, Malik, Shaafiy, na Ah’mad bin Habal, sasa kwanini ndugu Juma ainasibishe itikadi hii sahihi na Ibn Taymiyya na mwanafunzi wake Ibn al-Qayyim peke yao?

 

Kwani kuna kioja gani kwa mtu kumsifia Allah kwa sifa ambazo amejisifia nazo mwenyewe katika Qur’an na amesifiwa na Mtume wake –swalla llaahu alayhi wasallam-?

Je wakumshangaa ni yule aliyehalifu hilo au yule aliyetii? Ama kweli walimwengu wana mambo !

 

Amesema tena Juma:

“Lakini kudai kwamba haya ni maneno ya Al-imamu Al-ash’ari ni kitu cha kutazamwa zaidi kwani wafuasi wa Al-imamu Al-ash’ari nao ni masuni kama mashafi hawakubaliani na haya”.

Rudi juu

 

MAJIBU YETU

 

Kwa maneno haya ya ndugu Juma anatuwekea wazi zaidi namna asivyokuwa mtafiti mzuri wa mambo na huwa hukumu zake ni za kubuni.

 

Tangu lini mtu akahukumiwa kwa matendo ya watu wengine?

Kuwa wafuasi wa Abul-Hasan al-Ash’ari wako kinyume na itikadi yake, basi hiyo ndiyo hoja yakwamba hakusema maneno hayo?

Kwanini usiwashangae watu  wanaodai kuwa ni wafuasi wa Imamu Shaafiy katika mambo ya twahara na swala lakini katika mambo la itikadi wamemfuata Abul-Hasan na wako kinyume na Imamu wao?

Kwanini wamemkwepa Imamu Shaafiy aliyefariki mwaka 205 H na kumfuata Abul-Hasan al-Ash’ariy aliyezaliwa mwaka 260 H na kufariki mwaka 324 H?

Abul-Hasan yeye amezaliwa  nusu karne baada ya Imamu Shaafiy kufariki, je Imamu Shaafiy hakuwa na itikadi yoyote? Na je yeye alikuwa akimfuata nani?

Rudi juu

 

HISTORIA YA ABUL-HASAN KWA UFUPI

 

Abul-Hasan al-Ash’ariy jina lake kamili ni: Aliy bin Ismail bin Is’haq bin Salim bin Ismail bin Abdillahi bin Musa bin Abi Bur’da bin Abi Musa al-Ash’ariy, amezaliwa mwaka 260 H.

 

Mwanzoni mwa uhai wake alikuwa na itikadi ya Mu’tazila kwa muda wa miaka 40 na sababu yakuwa na itikadi hiyo ni sheikh wake aliyesoma kwake ambaye ni baba yake wa kufikia (mume wa mamake) jina lake ni Abu Aliy al-Jubbai, yeye alikuwa na itikadi potofu za Mu’tazila (itikadi za kupinga sifa za Allah)  na hiyo ni itikadi iliyo anzishwa na Waasil bin Atwaa.

 

Kisha Imamu Abul-Hasan akaiwacha itikadi hiyo ya Mu’tazila na kuifuata itikadi ya Ibn Kullaabi kwa muda, na miongoni mwa itikadi za Ibn Kullaabi ni kumthibitishia Allah sifa saba tu, sifa ya: Uhai, Elimu, Uwezo, Utashi, Usikivu, Uoni, na kusema.

Na ama sifa nyingine zote kama vile Uso, Mikono miwili, Mguu na mfano wa hizo alizipa tafsiri potofu.

 

Alijifungia ndani kwake kwa muda wa siku kumi na tano kisha akatoka akaelekea msikiti mkuu wa Bas’ra akapanda juu ya mimbari baada ya swala ya Ijumaa kisha akawaambia watu, nilijificha kwenu kwa muda kwa sababu nimezitazama dalili lakini zikawa sawa kwangu na haikunipambanukia haki na batili, nikamwomba Allah aniongoze ndipo akaniongoza kwenye haya niliyo yaweka humu kwenye vitabu hivi, na nimejivua na yale yote niliyokuwa nikiyaitakidi kama ninavyoivua kanzu yangu hii, kisha akaivua kanzu yake na akaitupa kwa watu, kisha akavitoa vitabu vyake akawapa watu.

 

Na miongoni mwa vitabu vyake ni “al-Ibana an Usuli-Diyana” na ndani ya kitabu hicho amesema wazi wazi kwamba msimamo wake huo ndiyo msimamo wa Salaf Swalih msimamo wa maimamu wakubwa kama vile: Malik, Shaafiy, Ah’mad bin Hanbal na wengineo na kuwalingania watu washikamane nao.

 

Na wanavyuoni walio lithibitisha suala hili la kutubia kwake, kuacha misimamo hiyo potofu na kushikamana na msimamo wa Salaf Swalih na kuandika kitabu “al-Ibana”, ni hawa wafuatao:

1-  Abul-Qasim Aliy bin al-Hasan bin Hibatu-llaahi Ibn Asaakir aliyefariki mwaka 571 H, katika kitabu chake “al-Tabyiin” ukurasa wa 28.

2-  Imamu al-Baihaqiy al-Shaafiy aliyefariki mwaka 458 katika kitabu chake al-I’tikad ukurasa wa 31na 32.

3-   Imamu al-Dhah’biy aliyefariki mwaka 748 H katika kitabu chake “al-Uluwu” ukurasa wa 160.

4-  Imamu Ibn al-Imadi aliyefariki mwaka 1098 H katika kitabu chake “Shadharaatul-Dha’hbi” ukurasa wa 303.

5-  Imamu Abul-Hasan al-Sayyid Murtaza al-Zabidiy katika kitabu chake “It’hafu Saadatil- Mutaqina” juzuu ya 2 ukurasa 2.

6-  Imamu Ibn Kathir al-Qurashiy al-Shaafiy aliyefariki mwaka 774H, katika kitabu chake “al-Bidayatu wal-Nihayah” juzuu ya 11 ukurasa wa 187.

7-  Imamu Taaju-Din Abu Nasri Abdul-wahab bin Taqiyu-Din al-Subkiy al-Shaafiy aliyefariki mwaka 771 H, katika kitabu chake “Twabaqaatu al-Shaafi’iya al-Kubraa” juzuu ya 2 ukurasa 246.

 

Na wengi katika maulama ambao hatukuwataja, wote hao wamekiri na kuthibitisha katika vitabu vyao tulivyo vitaja kuwa Abul-Hasan aliziwacha itikadi zote hizo potofu na kushikamana na itikadi sahihi ya Salaf Swalih na akatunga kitabu “al-Ibana”.

Rudi juu

 

YALIYOMO KATIKA KITABU “AL-IBANA”

 

Hebu tunukuu baadhi ya maneno yake kutoka kwenye kitabu hicho ili tuone je anayoyasema yeye yanatofauti yoyote na yale anayoyasema Ibn Taymiyya na mwanafuzi wake?Au chuki binafsi inafanya kazi yake?

 

Anasema Abul-Hasan baada ya kuzitaja itikadi potofu za watu wa bid’a na kuzipinga:

 

"الباب الثاني

فى إبانة قول أهل الحق والسنة

فإن قال لنا قائل : قد أنكرتم قولَ المعتزلة والقدرية والجهمية والحرورية والرافضة والمرجئة , فعرِّفونا قولكم الذي به تقولون وديانتكم التي بها تدينون.

قيل له: قولنا الذي نقول به , وديانتنا التي ندين بها: التمسك بكتاب ربنا عزّ وجل , وبسنَّة نبيِّنا صلى الله عليه وسلم وما روي عن السادة الصحابة والتابعين وأئمة الحديث , ونحن بذلك معتصمون, وبما كان يقول به أبوعبدالله أحمد بن محمد بن حنبل –نضَّر الله وجهه وفع درحته وأجزل مثوبته- قائلون.....

 وجملة قولنا.....وأن الله استوى على عرشه كما قال: ((الرحمن على العرش استوى)) طه 5.

وأن له سبحانه وجهاً بلا كيف كما قال: ((ويبقى وجه ربك ذوالجلال والإكرام)) الرحمن 27.

وأن له سبحانه يدين بلا كيف كما قال سبحانه: ((خلقتُ بِيَدَيَّ)) ص75.وكماقال: ((بل يداه مبسوطتان)) المائدة:64.

وأن له عيناً بلا كيف كما قال سبحانه : ((تجري بأعيننا)) القمر 14...".

 

“MLANGO WA PILI

Katika kuibainisha kauli ya watu wa haki na sunna Ikiwa atasema mwenye kusema : mmeipinga kauli ya Mu’tazila, na kauli ya Qadariya (wenye kupinga Qadari) na kauli ya Jah’miya na kauli ya Haruuriya (miongoni mwao ni maibadhi) na kauli ya Raafidha (Shia) na kauli ya Mur’jia (wenye kuitakidi kuwa watu wote ni sawa katika imani) basi hebu tuelezeeni kauli yenu na msimamo wenu ambao mnaufuata.

 

Ataambiwa: Kauli yetu tunayoisema na msimamo wetu tunaoufuata ni kushikamana na kitabu cha Mola wetu na Sunna za Mtume wetu –swalla llaahu alayhi wasallam- na yale yaliyopokelewa kutoka kwa mabwana wakubwa katika maswahaba na Taabi’ina (wanafunzi wa maswahaba) na maimamu wa hadithi, sisi ni wenye kushikamana na hilo na yale anayoyasema Abu Abdillahi Ah’mad bin Muhammad bin Hanbal –Allah autie nuru Uso wake na ainyanyue daraja yake na ampe thawabu kwa wingi- sisi ni wenye kuyasema…..

 

Na jumla ya kauli ni kuwa sisi tunakiri kwamba ….Allah yuko juu ya Arshi yake kama alivyosema: ((Allah mwingi wa reh’ma yuko juu ya Ar’shi)) Twaha aya ya 5.

 

Na kwamba yeye Allah ana uso bila kuwa na namna kama alivyosema: ((Na utabakia Uso wa Mola wako wenye utukufu)).  Al-Rah’man aya ya 27.

 

Na kwamba yeye ana mikono miwili bila ya kuwa na namna kama alivyosema Allah: ((…Niliye muumba kwa mikono yangu miwili?)) surat Saad (38) aya ya 75.

Na akasema ((Bali mikono yake (Allah) iwazi)) al-Maida aya ya 64.

 

Na kwamba yeye ana jicho bila kuwa na namna kama alivyosema: ((Linakwenda(jahazi la Nuh) kwa uwangalizi wa macho yetu)) al-Qamar aya ya 14.”

 

Tazama katika kitabu chake “al-Ibana” kuanzia ukurasa wa 38-44, chapa ya Daarul-Bayaan Damascus - Syria ya mwaka 2004.

 

Bila shaka ndugu msomaji kwa mujibu wa nukuu hizi utakuwa umefahamu kwamba itikadi anayoielezea Ibn Taymiyya ndiyo itikadi halisi ya Ahli Sunna, itikadi ya maimamu wakubwa waliotangulia ambayo ndiyo itikadi iliyoelezwa na kitabu kitukufu Qur’an na Sunna sahihi za Mtume Muhammad –swalla llaahu alayhi wasallam-.

 

Na hiyo ndiyo itikadi ya Imamu Abul-Hasan al-Ash’ariy, kama alivyojielezea mwenyewe katika kitabu chake, kwa hiyo maneno ya ndugu Juma yanayotilia shaka maneno ya Ibn al-Qayyim na kudai kuwa ni maneno ya kutazamwa, madai hayo hayana uzito wowote wa kielimu.

Rudi juu

 

TUHUMA YA TATU

 

Ndugu Juma hakuchoka kusema uwongo na kuwatuhumu maulamaa wa Ah’li Sunna, bali akaamua kumzushia Imamu Ibn al-Qayyim tuhuma nyingine nzito, amesema ndugu Juma:

“katika kuifasiri aya ya Mwenyezi Mungu inayosema kwamba:

 

"نسوا الله فنسيهم"

“Wamemsahau Mwenyezi Mungu na yeye akawasahau.”

Sura ya 9 aya 67.

Kaifasiri aya hii kuwa ni kusahau kweli kweli akasema: “Zingatia kauli yake Mwenyezi Mungu (katika aya hio na ilio mfano wa hio) namna alivyofanya uadilifu kamili kwao akawasahau kama walivyo msahau !!!”.

Mwisho wa kunukuu.

Tazama ukurasa wa 25 wa kitabu chake.

 

Rudi juu

 

MAJIBU YETU

Miongoni mwa mambo mabaya kabisa katika uislamu ni kumzulia mtu jambo asilolifanya au asilosema, na kama mtu mwenyewe ni mwanachuoni basi ubaya unakuwa maradufu.

Vitendo vya ndugu Juma anavyovifanya dhidi ya maulamaa ni hiyana na ni dhulma ambayo inamporomoshea mtu uadilifu wake na kumfanya asikubaliwe maneno yake.

Je ni kweli Ibn al-Qayyim anasema kuwa Allah anasahau kweli kweli?

Au Juma amekusudia kusema uwongo ili kupotosha?

 

Jawabu ni kwamba, si kweli kuwa Ibn al-Qayyim anaitikadi kwamba Allah anasahau, bali itikadi yake ni itikadi ya Qur’an na Sunna kuwa Allah hasahau, lakini ndugu yetu Juma alikusudia kupotosha kama ilivyo kawaida ya watu wa batili.

 

Na ushahidi wa kuwa Ibn al-Qayyim hana itikadi hiyo chafu ni pale alipokuwa akiitafsiri kauli ya Allah isemayo:

" ((علمها عند الله)) طه 52 :

أي أعمال تلك القرون وكفرهم وشركهم معلوم لربي قد أحصاه وحفظه وأودعه فى كتاب فيجازيهم عليه يوم القيامة, ولم يودعه فى كتاب خشية النسيان والضلال فإنه سبحانه لا يضل ولا ينسى "!!!!! 

انظر كتابه شفاء العليل ص 141 مطبعة دار الكتاب العربي بيروت – لبنان الطبعة الأولى لعام 1424هـ

 

“[Ujuzi wake (karne hizo) uko kwa Allah] surat Twaha aya ya 52:

Makusudio ni kwamba matendo ya karne hizo (zilizopita) kufru zao na shirki zao zote zinajulika kwa Mola wangu amezidhibiti, amezihifadhi na ameziweka katika kitabu na atawalipa siku ya Qiyama, na hakuziweka katika kitabu kwa sababu ya kuogopea kusahau na kupotea

KWA SABABU YEYE –SUB’HANAH- HAPOTEI WALA HASAHAU!!!!!

Tazama kitabu chake “Shifaul-Alili” ukurasa wa 141 chapa ya Darul-kitabil- Arabi Beirut – Lebanon,chapa ya kwanza mwaka 2004.

 

Swali, kwa mujibu wa maneno haya, je ndugu msomaji umefahamu kwamba Ibn al-Qayyim itikadi yake ni kuwa Allah anasahau au hasahau?

Je umegundua kwamba Juma al-Mazrui anaendelea kusema uwongo?

 

Pengine Juma mwenyewe au mtu mwengine katika wapenzi wake anaweza kusema: lakini maneno hayo siyo aliyo yanukuu kutoka kwa Ibn al-qayyim bali yeye amenukuu maneno mengine kwenye kitabu kingine ambayo Ibn al-Qayyim anaelezea kwa uwazi kuwa Allah anasahau kweli kweli!

Rudi juu

MAJIBU YETU

 

Sababu ya kunukuu kauli hiyo ya Imamu Ibn al-Qayyim ni kutaka kukuthibitishia ndugu msomaji kwamba Ibn al-Qayyim hana itikadi hiyo ya kikafiri ambayo ndugu Juma amembabatiza nayo.

 

Kisha ndiyo tutupie macho hayo maneno ya Ibn al-Qayyim aliyo yanukuu Juma, na tutakapoyatazama tunakuta kwamba Ibn al-Qayyim hakutoka nje ya ibara ya Qur’an na Sunna, na wala maneno yake hayamaanishi kuwa Allah anasahau kweli kweli. Na kama maneno hayo yanaleta maana hiyo, basi hata Qur’an yenyewe na Sunna zitakuwa zina maanisha hivyo.

 

Ibn al-Qayyim katika maneno yake ametumia ibara isemayo:

"بأن نسيهم كما نسوه"

“Bi an-nasiyahum kamaa nasuuhu”

Maana yake Kiswahili ni “kwa kuwa amewaacha (amewapuuza) wao kama walivyo msahau (walivyompuuza)”

Na ibara hiyo hiyo ndiyo iliyotumika katika Qur’an amesema Allah:

"نسوا الله فنسيهم"

 

“Wamemsahau Allah naye akawaacha (akawapuuza) ”.

 

Na haya hapa ni maneno ya Ibn al-Qayyim kwa ukamilifu :

 

"وتأمل قوله الحق ((نسوا الله فنسيهم )) وقوله : ((ولا تكونوا كالذين نسوا الله فأنساهم أنفسهم))  كيف عدل فيهم كل العدل بأن نسيهم كما نسوه".

مختصر الصواعق المرسلة 1/210

 

“Izingatie kauli yake al-Haq (Allah) “Wamemsahau Allah na yeye akawaacha wao (katika adhabu), na kauli yake “Wala msiwe kama wale ambao wamemsahau Allah na yeye akawasahaulisha nafsi zao” (zingatia) namna alivyo wafanyia wao uadilifu kwa kuwa walimsahau na yeye akawaacha (katika adhabu).”

Tazama kitabu “Mukh’tasaru Sawaaiqil-Mur’slah” juzuu ya 1 ukurasa wa 210.

Hapa nataka kuelezea kitu kimoja muhimu kwa faida ya wasomaji:

 

Tulipo litafsiri neno “Nasiya hum” kwa maana ya kuacha, lengo si kutaka  kuleta taawili na kupotosha.

Bali neno hili la kiarabu “Nasiya” ambalo limetasuliwa (limenyambuliwa) kutoka kwenye asili ya neno “Al-Nis’yaanu”  lina maana mbili na zote ni za asili.

 

Amesema Imamu Abul-Husain Ah’mad bin Faaris aliyefariki mwaka 395 H, katika kamusi yake “Mu’jamu Maqaaisil-Lugha” ukurasa wa 987:

 

"نسي : النون والسين والياء أصلان صحيحان : يدل أحدهما على إغفال الشيئ , والثاني على ترك شيئ".

معجم مقاييس اللغة ص987.

 

“Nasiya: Nuni, Siin, na Yaau ni asili mbili zilizo sahihi: moja yao inafahamisha

“Kughafilika” na ya pili ni “Kuacha kitu”.

 

Kwa hiyo tumefahamu kuwa neno “Nasiya” lina maana mbili:

i)            Kughafilika.

ii)           Kuacha.

 

Na kwa mujibu wa kanuni na misingi ya elimu ya itikadi linapotumika neno lolote lenye zaidi ya maana moja: Maana moja inalingana na utukufu wa Allah, na maana ya nyingine hailingani na utukufu wake Allah, basi neno hili litachukuliwa kwa maana ambayo inalingana na utukufu wake Allah.

 

Kwamfano hapa limetumika neno “Nasiyahum” ambalo maana yake ima itakuwa :

“(Allah) Amewasahau wao” au “(Allah) Amewaacha wao”.

Tukitazama baina ya maana mbili hizi, ni ipi  inayonasibiana na utukufu wake Allah –Jalla Jalaaluh-?

Bila shaka kulitumia neno hili kwa maana ya “kuacha” ndiyo sahihi bali ni wajibu kufanya hivyo kwa sababu Allah hasahau kama ilivyotuelezea Qur’an na Sunna na alivyotuelezea Ibn al-Qayyim hapo nyuma.

Na hakuna shaka kwamba naye Ibn al-Qayyim amelitumia neno hili hapa kwa maana inayolingana na utukufu wake Allah, nayo ni kwa maana ya “kuacha”.

Na mtu akilitumia neno hili na jingine kama hili kwa utaratibu ule ule uliotumika katika Qur’an au katika Sunna hatakuwa na hatia wala hastahiki lawama, na hivyo ndivyo alivyofanya Ibn al-Qayyim, lakini kwa masikitiko makubwa jambo hili halikumfurahisha ndugu Juma na kaumu yake na wakalifanya hilo ni kosa kubwa lisilo na mfano !

Na -wali llaahil-hamdu- ukirejea sehemu mbali mbali katika vitabu vya Ibn al-Qayyim utaona anavyosema kwa uwazi kabisa kwamba:

فإنه سبحانه لا يضل ولا ينسى "! 

“KWA SABABU YEYE (ALLAH)  –SUB’HANAH- HAPOTEI WALA HASAHAU” !

Tazama kitabu chake “Shifaul-Alili” ukurasa wa 141 chapa ya Darul-kitabil- Arabi Beirut – Lebanon,chapa ya kwanza mwaka 2004.

 

Lakini ah ! tutazifanya nini sisi nyoyo  zilizonyweshwa chuki, husda na uadui mpaka zikawa hazioni kwa waislamu wenzao ila shari tupu !

Lakini hii ndiyo sera ya watu wote wa bid’a tangu azal.

Ewe Mola wetu usijaalie ndani ya nyoyo zetu chuki na undani dhidi ya ndugu zetu walio amini, Allaahumma Aamin!

Rudi juu

TUHUMA YA NNE

 

Amesema Juma kuhusu Ibn al-Qayyim:

“Na Ibn Al-qayyim akafikia kusema kuwa moto wa akhera kuna siku adhabu yake itakwisha kwa waislamu na wasio kuwa waislamu na utabaki mtupu bila ya mtu yeyote.

Na akainasibisha kauli hii kwa Sheikh wake Ibn Taymiyya na akaisifu kuwa kauli hii ndio inayokubaliana na Qur’an na suna.”

Mwisho wa kunukuu. Tazama katika kitabu chake “Hoja zenye Nguvu” ukurasa wa 25.

Rudi juu

 

MAJIBU YETU

 

Ibn al-Qayyim kwenye kitabu chake “Haadil-Ar’waahi” chapa ya Daarul-Kitabil-Arabi  amenukuu mjadala ulio kuwa kati ya pande mbili: upande wa wasemao kuwa moto utakwisha na upande wa wasemao kuwa moto hautakwisha, kwa hiyo yeye kazi yake ilikuwa kunukuu hoja za pande mbili na ndiyo maana utaona anasema:

"والذين قطعوا بدوام النار لهم ست طرق"

“Na wale (wanaosema kwa) kukata kudumu kwa moto wana njia sita”.

Tazama “Haadil-Ar’waahi” ukurasa wa 232.

 

Kisha akasema tena:

"قال أصحاب الفناء....".

“Wamesema wenye kusema kwisha (kwa moto)….” Tazama kitabu “Haadil-Ar’waahi” ukurasa 233.

 

Na mwisho alipofikia kuufunga mjadala huo akasema:

 

“Kama ukiulizwa ni wapi umefikia unyayo wenu katika mas’ala haya makubwa, ambayo ni makubwa kuliko dunia kwa mara nyingi?

Ataambiwa : tumefikia kwenye kauli yake –Tabaaraka wata’alaa-:

 

((إنَّ ربَّك فعَّالٌ لمايريد)) هود:107.

Kwa hakika Mola wako ni mwenye kufanya analo litaka….”.

 Surat Huud aya ya 107.

Tazama “Haadil-Ar’waahi” ukurasa wa 248.

 

Mpaka hapo inaonyesha kwamba Ibn al-Qayyim hakuunga mkono hoja ya upande wowote ule.

Lakini ukweli ni kwamba Ibn al-Qayyim amebabaika sana katika mas’ala haya, na hakuwa na kauli ya wazi katika suala hili kwenye kitabu hiki.

Lakini tulipo yafuatilia maneno yake yaliyomo kwenye vitabu vyake vingine tukakuta kuwa ameuweka wazi msimamo wake juu ya mas’ala haya kwa mfano kwenye kitabu chake “Al-Waabilu al-Sayibu” ukurasa wa 49 chapa ya “al-Na