Itikadi ya Ahlus Sunnah

 

 

Muhammad Faraj Salem Al Saiy

 

Aqida ya Ahlus Sunnah ni sahili na nyepesi, haina tabu kufahamika wala haina mikanganyo. Haina tabu kuisherehesha. Bali inafahamika na mtu wa kawaida kama inavyofahamika na mtaalamu. Mtu yeyote anaweza kuifahamu kwa wepesi kabisa.

 

Vitabu vyao vya Hadithi kama vile Bukhari na Muslim na vingine, pamoja na mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) yaliyonukuliwa ndani ya vitabu hivyo na kuenezwa kila mahali ulimwenguni kwa njia ya isnadi yenye kufuata mfumo na elimu ya hali ya juu, vitabu hivyo vinakubaliwa na sehemu kubwa sana ya umma huu na vinatumiwa katika kuitimiza na kuisherehesha sheria ya Mwenyezi Mungu.

 

Maulamaa wake kama vile Imam Abu Hanifa na Imam Malik na Imam Shafi na Imam Ahmad bin Hanbal na Ibnil Mubaraka na Ibni Taymiyah na wenzao wengi wengine wanapendwa na kufuatwa na asilimia zaidi ya 95 ya Waislamu ulimwenguni, kutokana na elimu yao kubwa na masharti yao mepesi. Walikuwa daima wakisema: “Ukikuta katika mafundisho yetu yanayokubaliana na Qur’ani au Sunnah sahihi, basi yafuateni. Na kama hayakubaliani na hayo basi yapigeni na ukuta.”

 

Watu wamedurusu sira zao na mwenendo wao na elimu yao heshima yao, wakawakubali kama ni Maimamu wao walioisherehesha Qurani tukufu na mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kwa njia ya kitaalamu na kwa uhodari mkubwa.

 

Viongozi wao walipambana na maadui wa Waislamu, wakaweza kuzifungua nchi nyingi sana na nyoyo nyingi. Walitayarisha majeshi na wapiganaji walioweza kuziteka nchi kubwa kubwa kuanzia Uturuki, sehemu kubwa ya Uchina na Urusi. Afghanistan na Africa na Asia na sehemu kubwa ya Ulaya, na kwa njia hiyo mamilioni kwa mamilioni ya watu waliingia katika dini hii tukufu.

Walifanikiwa kote huko kuwatoa watu katika giza la kumkufuru Mwenyezi Mungu na kuwaingiza katika nuru ya Uislamu, kuwatoa katika jeuri ya watawala wao, na kuwaingiza katika uadilifu wa Uislamu, kuwatoa katika kuipenda dunia, na kuwaingiza katika kuipenda akhera yao, na juu ya kuwa wao ndio walioziteka nchi hizo, lakini wananchi wake wanandelea mpaka leo kuwapa watoto wao majina ya wafunguzi wale wa Kiislamu.

Utamkuta mtoto wa Kirusi au wa Kituruki au wa Ki Africa au Asia au Ulaya au hata Marekani akipewa jina la Abubakar au Umar au Aly au Uthman au Muawiyah au Khalid (Khalid bin Waliyd) au Harun au Salahuddin, nk.

 

Kutokana na mafundisho ya maulamaa wao yaliyo mepesi yanayokubalika na akili ya mwanadamu yeyote wa kawaida, madhehebu haya yalipendwa na kufuatwa na asilimia kubwa sana ya Waislamu duniani.

 

Kuthibitisha

Kwa mfano katika kuzithibitisha sifa za Mwenyezi Mungu, Ahlus Sunnah wanakubali na kukithibitisha kila Alichokubali na Kukithibitisha Mwenyezi Mungu bila ya kuchelewesha wala kubadilisha.

Mwenyezi Mungu Anaposema kuwa Anao Uwezo, na sisi tunaamini kuwa Anao Uwezo. Anaposema kuwa Anaona, na sisi tunaamini kuwa Anaona Subhanahu wa Taala.

Anaposema kuwa Anasikia, na sisi tunaamini kuwa Anasikia. Na anaposema kuwa Anayo macho, na sisi tunaamini kuwa Anayo Macho, Subhanahu wa Taala, na Anaposema kuwa Anayo Mikono na sisi tunaamini kuwa Anayo Mikono, na Anaposema kuwa Anao Wajihi, na sisi tunaamini kuwa Anao Wajihi Subhanahu wa Taala. Lakini macho Yake na mikono Yake na Wajihi wake na Kuona Kwake na kusikia Kwake hauna mfano wowote na kitu chochote.

áóíúÓó ßóãöËúáöåö ÔóíúÁñ æóåõæó ÇáÓøóãöíÚõ ÇáÈóÕöíÑõ

Hapana kitu kama mfano Wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona

Ashuuraa-10

 

Maulamaa wetu wametufundisha kuzikubali sifa zote za Mwenyezi Mungu bila ya kukisia kwa akili zetu namna yake au mfano wake. Kwa sababu kuzikataa sifa ambazo  Mwenyewe Amejipa Subhanahu wa Taala, ni makosa, na kuzifananisha sifa hizo pia ni makosa.

Hapana kitu kama mfano Wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona

 

Mwenyezi Mungu anaposema:

íóÏõ Çááøóåö ÝóæúÞó ÃóíúÏöíåöãú

Mkono wa Mwenyezi Mungu Uko juu ya mikono yao

Al Fat’h-10

Sisi tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Anao Mkono. Kwa sababu Yeye Mwenyewe Subhanahu wa Taala Amesema hivyo. Lakini hatuufananishi Mkono Wake na vijikono vyetu.

 

Anasema mwanachuoni wa Kishia Al Sayed Muhammad Al Huseyniy Al Shiraziy katika tafisri yake inayoitwa; Taqriyb al Qur’an fil Adh’haan katika kuifasiri aya hii: “Mkono wa Mwenyezi Mungu Uko juu ya mikono yao.”  “Aya hii inazungumza juu ya Mashaba (Radhiya Llahu anhum) waliofungamana na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) (chini ya mti), na katika kufungamana, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akiutandaza mkono wake huku matumbo ya vidole yakielekea juu, na wanapokuja wenye kufungamana naye walikuwa wakiweka mikono yao juu ya mkono wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam.)”

Aya hii ilitemshwa baada ya Masahaba kufungamana na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) walipokuja chini ya ule mti na kuiweka mikono yao juu ya mkono wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam), ndipo Mwenyezi Mungu Aliposema;

Mkono wa Mwenyezi Mungu Uko juu ya mikono yao

 

Al Fat’h-10

 

Maulamaa wanasema: ‘Mguu wa meza hauwezi kufanana na mguu wa Seremala aliyeichonga meza hiyo na kutengeneza miguu yake, kama vile mkono wa fundi aliyetengeneza simu hauwezi kuwa sawa na mkono wa simu. Siku zote sifa za mtengenezaji haziwezi kufanana na sifa za bidhaa yake.

Na Mwenyezi Mungu Ndiye Mwenye mifano mikubwa. Kwa hivyo Anaposema Subhanahu wa Taala kuwa anao Mkono, na sisi tunakubali kuwa Anao Mkono lakini hatuufananishi na mikono wetu, kwa sababu sifa za Muumba haziwezi kufanana na sifa za viumbe

 

Na katika aya nyingine Mwenyezi Mungu anamuuliza Ibilisi:

ÞóÇáó íóÇ ÅöÈúáöíÓõ ãóÇ ãóäóÚóßó Ãóä ÊóÓúÌõÏó áöãóÇ ÎóáóÞúÊõ ÈöíóÏóíøó ÃóÓúÊóßúÈóÑúÊó Ãóãú ßõäÊó ãöäó ÇáúÚóÇáöíäó

Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumt'ii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?

Saad- 75

 

Sisi tunaamini kuwa; kwa vile Mwenyezi Mungu amesema kuwa Amemuumba Adam kwa mikono yake basi haiwezekani kuwa amekusudia kuwa amemuumba kwa njia nyingine.

Ndani ya Qur’ani tukufu Mwenyezi Mungu Anazungumza na watu wa kila aina, wenye elimu na wasiokuwa na elimu. Na kusudi Lake Subhanahu wa Taala ni kuwafundisha watu hao waijuwe dini yao, juu ya hitilafu ya ufahamu wao. Kwa hivyo haiwezekani Azungumze nao kwa njia ya mafumbo au majazi akawa anasema neno huku akikusudia jambo au neno lingiine.

Mwenyezi Mungu angelitaka kusema kuwa amemuumba mwanadamu kwa Kudra Yake, kwa mfano; basi Angelisema tu, pasingekuwa na haja ya kuutaja mkono.

 

Na katika aya nyingine pia Mwenyezi Mungu Anasema:

Ãóæóáóãú íóÑóæúÇ ÃóäøóÇ ÎóáóÞúäóÇ áóåõãú ãöãøóÇ ÚóãöáóÊú ÃóíúÏöíäóÇ ÃóäúÚóÇãðÇ Ýóåõãú áóåóÇ ãóÇáößõæäó

Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.

Yasin - 71

 

Na hivi ndivyo ilivyo katika sifa Zake zote Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala, kila Anapozitaja, ni juu yetu kusema: ‘Sam’an wa ta’an’, tuzikubali bila kubabaisha maana yake wala kubadilisha wala kufananaisha sifa hizo na sifa za viumbe.

Kwa mfano Mwenyezi Mungu Anaposema:

ÅöäøóãóÇ ÃóãúÑõåõ ÅöÐóÇ ÃóÑóÇÏó ÔóíúÆðÇ Ãóäú íóÞõæáó áóåõ ßõäú Ýóíóßõæäõ

Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa 

Yasin -71

 

Tunapoisikia kauli hiyo ya Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala, hatuna budi kuikubali na kuiamini. Kwa nini? Kwa sababu Mwenyezi Mungu Mwenyewe Amesema hivyo. Ikiwa Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala Hasemi, kwa nini basi alisema kuwa; hukiambia tu: Kuwa! Na kikawa?

 

Na katika aya nyingine Mwenyezi Mungu Anasema:

æóßóáøóãó Çááøåõ ãõæÓóì ÊóßúáöíãðÇ

Na Mwenyezi Mungu alinena na Musa kwa maneno.

Annisaa - 164

 

Bali hata Qurani tukufu ni maneno ya Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala. Mwenyezi Mungu Anasema:

 æóÅöäú ÃóÍóÏñ ãøöäó ÇáúãõÔúÑößöíäó ÇÓúÊóÌóÇÑóßó ÝóÃóÌöÑúåõ ÍóÊøóì íóÓúãóÚó ßóáÇóãó Çááøåö Ëõãøó ÃóÈúáöÛúåõ ãóÃúãóäóåõ Ðóáößó ÈöÃóäøóåõãú Þóæúãñ áÇøó íóÚúáóãõæäó

Na ikiwa mmoja wapo katika washirikina akikuomba ulinzi, basi mpe ulinzi apate kusikia maneno ya Mwenyezi Mungu. Kisha mfikishe pahala pake pa amani. Haya ni kwa kuwa hao ni watu wasiojua kitu.

At Tawba - 6

 

Wengine wanasema kuwa Mwenyezi Mungu hakusudii hivyo, bali hayo ni majazi tu. Na maana yake ni kuwa Anaposema kuwa Anasikia, hakusudii kuwa Anasikia kweli bali hayo ni majazi tu, na Anaposema kuwa Anaona hakusudii kuwa Anaona kweli bali hayo ni majazi tu, na Anaposema kuwa Anayo macho, hakusudii kuwa Anayo macho, bali hayo ni majazi tu, na Anaposema kuwa Anayo mikono hakusudii kuwa Anayo mikono bali hayo ni majazi tu, na anaposema kuwa Anao wajihi hakusudii kuwa Anao wajihi kikweli bali hayo ni majazi tu…… SubhanaLlah!!!

Sisi tunasema; Majazi yapo, lakini majazi ni kwa mfano mtu shujaa akaitwa Simba, au mtu muovu akaitwa nyoka nk. Haya ni majazi. Lakini maneno ya Mwenyezi Mungu Aliyotuletea waja wake kwa ajili ya kutufundisha dini yetu na kutujulisha sifa Zake Subhanahu wa Taala , hayawezi kuingia katika mfumo huu. Ni maneno ya kiarabu yasiyokwenda upande. Lugha ya kiarabu safi kabisa.

Mwenyezi Mungu Anasema:

ÞõÑÂäðÇ ÚóÑóÈöíøðÇ ÛóíúÑó Ðöí ÚöæóÌò áøóÚóáøóåõãú íóÊøóÞõæäó

Qur'ani ya Kiarabu isiyo na upogo (isiyokwenda upande), ili wamche Mungu

Azzumar-28