ni rahisi sana, nayo ni kushindana naye katika kufanya ibada na katika mambo mema, na kwa njia hii ataipata sifa kama ya mwenzake na atakuwa ameshindana naye kwa njia zilizoruhusiwa na sheria kama alivyosema MwenyeziMungu Subhaanahu wa Taala:

æóÝöí Ðóáößó ÝóáúíóÊóäóÇÝóÓö ÇáúãõÊóäóÇÝöÓõæäó

"Na katika haya washindane wenye kushindana".

Al Mutafifiyn aya ya 26:

 

 

6) Kujitetea

Wengine wanapotuhumiwa juu ya makosa au ila fulani, utawasikia wakijibu kwa haraka:

“Hata fulani pia anafanya hivyo”

Mtu huyu ilimpasa ajitetee nafsi yake bila kuwafedhehesha wengine.

7) Mitihani

Mwengine utamsikia akizungumza juu ya masaibu yaliyomfikia  mwenzake kwa kusema kwa mfano:

“Maskini fulani mambo yamezidi kuwa magumu kwake, namuonea huruma”, kisha utamsikia akilitaja jina la mtu huyo aliyefikiwa na masaibu.

Huenda akawa mkweli katika kumuonea huruma mwenzake, lakini nia yake nzuri haimpi uhuru wa kuzungumza juu ya mtihani wa mwenzake mbele ya watu, hasa ikiwa hapana udhuru wowote wa kuyazungumza.

Siku zo4"/>

Kusengenya (Ghiyba)

 

Muhammad Faraj Al Saiy

Utangulizi 1

Dhana mbaya. 2

Dawa ya Dhana. 4

Nukhsi 4

Husda. 5

Kupeleleza. 6

Yaliyodhihirika. 7

Ghiyba 7

Maana ya Ghiyba. 9

 

Hukmu yake. 9

Heshima ya Muislamu. 10

Mifano ya Ghiyba. 11

1-Kuashiria Kwa Mkono  11

 

2-Waambie Mumekwishakula. 12

3-Mwenye Kusengenya Na Msikilizaji Wote Sawa. 14

Heshima ya ndugu yako. 15

Sababu zake. 17

Ghadhabu. 17

Kuridhishana  19

 

Kujipendekeza  19

Kuchekesha watu. 20

Husda. 20

Kujitetea  20

Mitihani 20

Kutokuwa na la kufanya. 21

Kujikurubisha  21

Kujiona  21

Baadhi ya hadithi

Mwenye kusengenya ni muoga. 23

Yayoruhusiwa

Yanayofaa kuchungwa

Kutubia Ghiyba. 26

Yasiyodhaniwa

Kumsaidia mzito wa kufahamu  28

Hitimisho. 28

Utangulizi

Shukrani zote ni zake Allah. tunamshukuru, tunamtegemea, tunafuata uongofu Wake na tunajilinda kwake kutokana na shari za nafsi zetu na amali zetu zilizo ovu. Atakayeongozwa na MwenyeziMungu hapana wa kumpotosha (kumpoteza), na atakayeachwa kupotea kwa sababu ya kukataa kwake kufuata uongofu, hatopata wa kumuongoza.

Ninashuhudia ya kwamba Hapana Mola anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Allah na kwamba Muhammad (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ni mja wake na Mtume wake na kipenzi chake mbora wa viumbe vyote. Ameutimiza Ujumbe, ameifikisha Amana, amewanasihi Umma na amepigana Jihadi kwa ajili ya dini ya MwenyeziMungu kama inavyopaswa.

Mola wetu zifikishe swala na salaam zetu kwa kipenzi chako huyu Al Habiyb Muhammad (Swalla Llahu alayhi wa sallam) uliyemsifia katika kitabu chako kitukufu Ulipomwambia:

æóÅöäøóßó áóÚóáì ÎõáõÞò ÚóÙöíãò

"Na bila shaka una tabia njema kabisa."

Al Qalam-4

 

Kusudi la kuandika makala haya lilikuwa ni kuandika maudhui ya Ghiyba (kusengenya), kwani hayo ni maradhi yaliyoukumba umma, na wengi hawafahamu hatari yake na namna yanavyoweza kumpotezea mtu thawabu zake zote alizochuma kwa tabu ya kukesha huku akiswali na kufunga na kutoa sadaka na kusoma Qurani nk.

ÇÍÝÙ áÓÇäß ÇíåÇ ÇáÇäÓÇä – áÇ íáÏÛäß Çäå ËÚÈÇä

Chunga mwanangu chunga

Lisije kukuponyoka

Usije ukakudunga

Kwani ulimi ni nyoka

 

Kusudi langu ni kubainisha hatari inayotokana na ulimi pamoja na shari zake na kufahamisha namna ya kuyatibu maradhi haya pamoja na kusherehesha yale ambayo kwa ajili ya ulimi yatampeleka mtu ima katika faida kubwa na radhi za Mwenyezi Mungu hapa duniani na huko akhera, au katika hasara kubwa na ghadhabu za Mwenyezi Mungu katika nyumba mbili hizo za Dunia na Akhera.

 

Kusengenya ni maradhi yanayoondoa mapenzi na kuleta chuki baina ya ndugu, rafiki, jamaa, na hatimaye yanakula thawabu za mtu na kuzimaliza kama moto unavyokula kuni.

Mtume(Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Yamekufikieni maradhi ya waliokuja kabla yenu, Husda na chuki. Maradhi hayo ndiyo yanayonyoa, yananyoa dini hayanyowi nywele. Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, hamuingii Peponi mpaka muamini, na hamuamini mpaka mpendane. Nikuambieni ni jambo gani mkilifanya mtapendana? Enezeni (salam) amani baina yenu".

Ahmed - Attirmidhy na Al Bazzar

 

Kama nilivyosema kuwa nilitaka kuandika juu ya maudhui ya Ghiyba peke yake, lakini kwa vile aya ya Ghiyba ndani ya Qurani inashamili mambo matatu mengine, na yote ni muhimu sana katika jamii ya Kiislam, nikaona itakuwa vyema kama nitazungumzia juu ya kila jambo angalau kwa uhaba, kisha nikamilishe kwa kuyasherehesha vizuri maudhui haya ya Ghiyba - (kusengenya).

 

Mwisho, namuomba Mwenyezi Mungu aninufaishe mimi na atunufaishe sote katika somo hili na aijaalie iwe hoja kwa ajili yangu siku ya Kiama na isiwe hoja dhidi yangu, kwani Yeye ni Muweza wa kila kitu.

 

Dhana mbaya

Maana ya neno 'Dhana' ni mtu kufasiri vibaya matendo au maneno ya mwenzake kama anavyodhania yeye, kisha akaiendekeza nafsi yake na kuyakubali yale aliyoyadhania akaamini kuwa ndio ukweli wenyewe na kuyasadiki.

Wanaopenda kuwadhania wenzao vibaya mara nyingi huwa ni dalili kuwa wao ni watu wenye tabia mbaya, na kwa kawaida mwenye mwenendo mbaya siku zote hudhania kuwa wenzake wote ni sawa naye.

 

Mwenyezi Mungu Anasema:

íóÇ ÃóíøõåóÇ ÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇ ÇÌúÊóäöÈõæÇ ßóËöíÑðÇ ãøöäó ÇáÙøóäøö Åöäøó ÈóÚúÖó ÇáÙøóäøö ÅöËúãñ æáÇ ÊóÌóÓøóÓõæÇ æóáÇ íóÛúÊóÈ ÈøóÚúÖõßõã ÈóÚúÖðÇ ÃóíõÍöÈøõ ÃóÍóÏõßõãú Ãóä íóÃúßõáó áóÍúãó ÃóÎöíåö ãóíúÊðÇ ÝóßóÑöåúÊõãõæåõ æóÇÊøóÞõæÇ Çááøóåó Åöäøó Çááøóåó ÊóæøóÇÈñ ÑøóÍöíãñ

"Enyi mlioamini! Jiepusheni sana na (kuwadhania watu) dhana (mbaya) kwani (kuwadhania watu) dhana (mbaya) ni dhambi. Wala msipeleleze (habari za watu) Wala baadhi yenu wasiwasengenye wengine. Je! Mmoja wenu anapenda kula nyama ya nduguye aliyekufa? La, Hampendi; (Basi na haya msiyapende). Na Mcheni MwenyeziMungu. Bila shaka MwenyeziMungu ni Mwenye kupokea toba (na) Mwingi wa kurehemu".

Hujuraat - 12

 

Katika aya hizi MwenyeziMungu anatuamrisha tuepukane na maradhi matatu yafuatayo:-

1.           Kudhania waislamu wenzetu Dhana mbaya.

2.           Kupeleleza habari za watu.

3.           Kusengenyana wenyewe kwa wenyewe.

 

Kisha MwenyeziMungu Subahanahu wa Taala akaikamilisha aya kwa kutufahamisha kuchukizwa kwake na wafanyao maasi hayo yanayoondoa heshima na mapenzi baina ya Waislamu kwa kumfananisha anayefanya maovu hayo na mtu mbaya, mchafu, muovu, anayekula mzoga wa nyama ya ndugu yake aliyekwisha kufa.

 

Anasema Imam Al Zamakhshariy:

"Kumdhania vibaya mtu wa kawaida au mtu anayejulikana kwa wema wake ni haram, lakini si haramu kumdhania vibaya mtu anayejulikana kuwa ni asi mwenye kufanya uasi wake dhahir shahir bila kumuogopa Mwenyezi Mungu wala kuwastahi wanadamu wenzake, tena bila kujificha wala kuona haya, na hii ni kwa sababu mtu wa aina hii yeye mwenyewe anakuwa keshajidhihirisha ubaya wake. Ama yule anayejisitiri, haijuzu kumdhania vibaya".

 

Anasema Umar bin Khattab (Radhiya Llahu anhu):

"Usilidhanie neno lililotoka kinywani mwa ndugu yako Muislam kuwa amelikusudia vibaya, bali ulidhanie kuwa alikusudia kheri tu huku ukilitafutia (neno hilo) udhuru wowote wa kheri unaoweza kulibeba ".

 

Kutoka kwa Abu Huraira (Radhiya Llahu anhu) amesema kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Jiepusheni na dhana mbaya, kwani hakuna uongo mkubwa kuliko dhana mbaya, na wala msipelelezane wala msibishane wala msihusudiane wala msichukiane wala msiendeane kinyume, na kuweni enyi waja wa Mwenyezi Mungu mfano wa ndugu".

Bukhari na Imam Malik

 

Na katika riwaya nyingine iliyopokelewa na Muslim na Attirmidhy imekuja hadithi hii hii ikiwa na ziada ifuatayo:

"Na wala si halali kwa Muislam kumpiga pande (asimsemeshe) ndugu yake (Muislam) kwa muda wa siku tatu".

 

Na katika riwaya nyingine kutoka kwa Bukhari inasema:

"Jiepusheni na dhana mbaya, kwani hakuna uongo mkubwa kuliko dhana mbaya, na wala msipelelezane wala msibishane wala msihusudiane wala msichukiane wala msiendeane kinyume, na kuweni enyi waja wa Mwenyezi Mungu mfano wa ndugu kama alivyokuamrisheni (Mola wenu). Muislam ni ndugu wa Muislam, asimdhulumu, asimuache bila kumsaidia, asimdharau, taqwa ipo hapa taqwa ipo hapa (akawa anaashiria kifuani pake). Inatosha peke yake kuwa shari kubwa mtu kumdharau Muislam mwenzake. Kila kitu baina ya Muislam na Muislam ni haramu, damu yake, heshima yake na mali yake. Hakika Mwenyezi Mungu haiangalii miili yenu wala sura zenu, bali anaangalia ndani ya nyoyo zenu na matendo yenu".

Bukhari

 

Dawa ya Dhana

Kutoka kwa Haritha bin Noaman (Radhiya Llahu anhu) amesema kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Mambo matatu si rahisi kuepukana nayo Umati wangu, Kuamini nukhsi, (kuwa na) husda na (kudhania) dhana mbaya".

Mtu mmoja akamuuliza:

"Tufanye nini ili tuepukane nayo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?"

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

"Ukihusudu, sema; 'Astaghfirullah', ukimdhania mtu dhana mbaya, usitake kumchunguza, na ukiamini kuwa jambo lina nukhsi, basi lifanye tu (na umtegemee Mwenyezi Mungu)".

Attabarani

 

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) katika hadithi hii anatutahadharisha na mambo matatu pamoja na kutufundisha namna ya kuepukana nayo.

Mambo yenyewe ni;

1.   Kuamini Nukhsi

2.   Husda

3.   Dhanna mbaya

Nukhsi

Kuamini 'Nukhsi' ni tatizo kubwa lililoenea sehemu zote ulimwenguni. Wapo wanaoamini kuwa baadhi ya nambari kama vile nambari 13 zina nukhsi na hawakubali kuitumia nambari hiyo katika shughuli zao zote. Hawakubali hata kuiandika nambari hiyo juu ya milango ya nyumba zao au katika viti vya ndege, bali wengine hawakubali kuvaa jezi za mpira zinazobeba nambari hiyo, nk.

Wapo wasiokubali kufunga safari yoyote ile siku ya terehe 13, na ikisadifu tarehe hiyo kuwa siku ya Ijumaa, basi wanaitakidi kuwa nukhsi yake itakuwa kubwa zaidi, na kwa ajili hiyo hawatoki hata majumbani mwao.

Wengine wanaamini kuwa baadhi ya siku kama vile Jumaane nk. zina nukhsi kusafiri ndani yake, na wengine wakikumbana na paka mweusi njiani, huivunja safari na kurudi makwao.

Hofu za namna hii zilizoingia ndani ya nyoyo katika kuviogopa viumbe alivyoviumba Mwenyezi Mungu au kuziogopa siku alizoziumba Mwenyezi Mungu, ni dalili ya udhaifu wa imani na upungufu wa Itikadi sahihi, nayo ni kuamini kuwa hapana anayeweza kudhuru wala kunufaisha isipokuwa Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala.

Þõá áøóä íõÕöíÈóäóÇ ÅöáÇøó ãóÇ ßóÊóÈó Çááøåõ áóäóÇ åõæó ãóæúáÇóäóÇ æóÚóáóì Çááøåö ÝóáúíóÊóæóßøóáö ÇáúãõÄúãöäõæäó

"Sema: Halitusibu ila alilo tuandikia Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye Mola wetu Mlinzi. Na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu!"

At Tawbah - 51

 

Husda

'Husda', maana yake ni kutamani neema aliyoipata mwenzio imuondoke.

Mfano mzuri ni pale mtu anapopandishwa cheo kazini kisha mwenzake anayefanya kazi naye akaona kuwa cheo kile alistahiki kukipata yeye.

Kibinadamu hili ni jambo la kawaida. Lakini mtu huyo anapoanza kutamani mwenzake anyanganywe cheo alichokipata au afukuzwe kazi au apatwe na masaibu yoyote, muhimu cheo kile kimuondokee na akipate yeye. Hiyo ndiyo 'Husda'.

 

Huo ni mfano mmoja tu, na mara nyingine mtu humhusudu mwenzake bila sababu yoyote.

 

Kutokana na 'Husda' yake, hasidi anaweza kudhurika yeye mwenyewe kwa kupata maradhi mbali mbali kama vile maradhi ya moyo na shinikizo la damu, 'blood pressure' au maradhi ya kisukari na mengineyo yanayosababishwa na kuathirika kwa moyo na nafsi kutokana na kusugulika mtu roho yake huku akijiunguza kwa uchungu wa husda.

Ndiyo maana Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akatufundisha kuomba Maghfira kwa Mwenyezi Mungu mara inapompitikia mtu husda moyoni mwake ili asiiendekeze nafsi yake na kuendelea na husda yake itakayomdhuru mwenyewe na kumpatia madhambi pamoja na maradhi mabaya kama hayo.

Katika hadithi iliyotangulia, Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliposema: "Ukihusudu, sema; 'Astaghfirullah', alikusudia kuwa zinapoanza kumpitikia mtu fikra kama hizo za kutaka neema aliyoipata mwenzake imuondokee, basi haraka aombe maghfira kutoka kwa Mola wake, kwani Mwenyezi Mungu anayajuwa yote yanayotupitikia nyoyoni mwetu.

Mwenyezi Mungu anasema:

æóÑóÈøõßó íóÚúáóãõ ãóÇ Êõßöäøõ ÕõÏõæÑõåõãú æóãóÇ íõÚúáöäõæäó

"Na Mola wako anayajua yanayoficha vifua vyao na wanayoyadhihirisha".

Al Qasas - 69

 

Mtu anapoomba maghfira kwa Mola wake maana yake ni kuwa amelitambua kosa lake na kwamba hatorejea tena kulifanya kosa hilo. Na kutokana na hayo, mtu huyo ataacha kumuonea husda mwenzake, atarudi kwa Mola wake Mwenye kusababisha yote hayo, na kumuomba Yeye tu Subhanahu wa Taala ampatie cheo kama kile au daraja kama ile ikiwa vitu hivyo vina kheri naye, au akinai na kile alichokuwa nacho.

Kupeleleza

Maana yake ni kufuatilia habari za watu kwa nia ya kutaka kujua habari zao, au aibu zao au makosa yao. Tabia hii ni kinyume kabisa na mafundisho ya Kiislam yanayotutaka tujishughulishe na kufuatilia na kuyachunguza makosa yetu wenyewe na kujirekebisha ili tusiyarudie tena, kwani hapana mtu asiyefanya makosa au asiyekuwa na aibu.

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Enyi mlioamini kwa ndimi zenu na ambao imani haijaingia ndani ya nyoyo zenu! Msiwasengenye Waislam wala msifuatilie kutaka kujua makosa yao, kwa hakika yule anayefuatilia makosa ya Waislam, na Mwenyezi Mungu atafuatilia makosa yake, na yule ambaye Mwenyezi Mungu atafuatilia makosa yake, basi atamfedhehesha hata ndani ya nyumba yake".

Abu Daud - Attirmidhy na Abu Yaala - imesahihishwa na Sh. Al Albani

 

Kupeleleza habari za watu ni katika dhambi kubwa sana iliyoharamishwa na Mwenyezi Mungu Aliposema:

æáÇ ÊóÌóÓøóÓõæÇ

"Wala msipeleleze (habari za watu)".

 

Imepokelewa kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Mtu anayesikiliza maneno ya watu huku wenyewe wakichukizwa (bila idhini yao), atamiminiwa sikioni mwake shaba (imoto iliyoyeyushwa) Siku ya Kiama".

Bukhari

 

Imepokelewa pia kuwa usiku mmoja Umar bin Khattab (Radhiya Llahu anhu) alipokuwa katika zamu akilinda mji yeye na Abdulrahman bin Auf (Radhiya Llahu anhu) alipita nje ya nyumba inayowaka taa na kusikia watu wakizungumza kwa sauti za juu.

Umar akamuuliza Abdulrahman:

"Unaijua nyumba ya nani hii?

Abdulrahman (Radhiya Llahu anhu) akajibu:

"Sijuwi".

Umar (Radhiya Llahu anhu) akamwambia:

"Hii ni nyumba ya Rabia bin Umayya na waliomo ndani hivi sasa wanakunywa pombe. Unasemaje?"

Abdulrahaman (Radhiya Llahu anhu) akasema:

"Mimi naona kuwa sasa tumefikia pale alipokataza Mwenyezi Mungu áÇ ÊóÌóÓøóÓõæÇ(Wala msipelelezane).

Wakaondoka wote wawili na kuelekea kwengine

 

Kutoka kwa Muawiya bin Abu Sufyan (Radhiya Llahu anhu) amesema:

"Nilimsikia Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akisema:

"Ukianza kufuatafuata kupeleleza juu ya mambo ya Waislam basi utawafisidi".

Abu Daud

Yaliyodhihirika

Kutoka kwa Yaziyd amesema:

"Mtu mmoja alikamatwa na kupelekwa mbele ya Abdillahi bin Masaud (Radhiya Llahu anhu) akishtakiwa kuwa ndevu zake mtu huyo zilikuwa zimerowa na kuchururika ulevi na kwamba zinanuka harufu ya ulevi. Abdillahi bin Masaud (Radhiya Llahu anhu) akasema:

"Hakika sisi tumekatazwa kupeleleza, lakini jambo lolote likitudhihirikia lazima tulichukulie hatua".

Abu Daud

 

Ghiyba (Kusengenya)

Kusengenya ni tatizo kubwa lililowakumba Waislamu wakiwemo hata baadhi ya wanavyuoni.

Kutokana na chuki inayosababishwa na kusengenyana baina ya waislamu pamoja na mfarakano mkubwa unaopatikana baina yao, ukijumlisha na hasara inayopatikana kutokana na mfarakano huo, nimeona bora niyachambue zaidi maudhui haya ya Ghiyba huku tukimuomba Mwenyezi Mungu atusaidie katika kupunguza ukali wa Moto huu, na atujaalie tuifahamu vizuri darsi hii na atupe uwezo wa kuyatekeleza maamrisho yake - Amin.

 

Moto, ni jina linalofaa kuliita tatizo hili, kwa sababu kusengenya, kunaziunguza thawabu za mtu aliyehangaika kuzichuma kwa Kuswali na Kufunga na kutoa Zaka na kusoma Qurani na mengineyo kama moto unavyokula kuni.

                                                                                                    

           

Ulimi ulionolewa kwa ajili ya kusengenya watu ni sababu kubwa ya mtu kupoteza thawabu zake alohangaika kuzichuma kwa tabu na pia ni sababu kubwa ya watu kutumbukizwa kwa wingi katika Moto wa Jahannam kama alivyotufahamisha Mtume wa MwenyeziMungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) katika hadithi ya Muadh bin Jabal (Radhiya Llahu anhu) iliyoshamili mambo yote muhimu katika dini na namna gani mtu anavyoweza kuzipoteza thawabu zake zote hizo baada ya kuhangaika kufanya yote anayotakiwa kuyafanya.

Hebu tumsikilize Muadh mwenyewe (Radhiya Llahu anhu) akituhadithia juu ya mazungumzo yaliyopita baina yake na sahibu yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).

Muadh bin Jabal (Radhiya Llahu anhu) amesema:

 

"Nilisema ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu; nitajie amali itakayoniingiza Peponi na itakayoniweka mbali na moto. Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

((Hakika umeuliza juu ya jambo kubwa mno, nalo ni jepesi kwa mwenye kuwepesishiwa kwalo na MwenyeziMungu aliyetukuka. Umuabudu MwenyeziMungu na usimshirikishe na chochote na usimamishe Swala na utoe Zaka na ufunge Ramadhani na uikusudie kwa Hijja nyumba (ya MwenyeziMungu) ukiweza kuifikia)). Kisha akasema:

((Je nikujulishe pia na milango ya kheri? Saumu humkinga mtu na moto, na Sadaka huzima madhambi kama maji yanavyozima moto, na Swala ya mtu katikati ya usiku)).

Kisha Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akaisoma aya za 16 na 17 Suratul Sajdah;

(("Huinua mbavu zao kutoka vitandani wakati wa usiku ili kumuabudu Mola wao kwa kuogopa Moto na kutaraji Pepo; na hutoa (Zaka na sadaka) katika yale Tuliyowapa. Nafsi yoyote haijui waliyofichiwa katika hayo yanayofurahisha macho (huko Peponi));

Kisha akasema:

((Je nikujulishe nini kichwa cha jambo na nguzo yake na kilele chake?))

Nikasema:

"Ndiyo ewe Mtume wa MwenyeziMungu".

Akasema:

((Kichwa cha jambo ni Uislamu na nguzo yake ni Swala na kilele chake ni Jihadi)).

Kisha akasema:

((Je nikujulishe kisimamio cha yote hayo?))

Nikasema:

"Ndiyo ewe Mtume wa MwenyeziMungu".

Akaushika ulimi wake, kisha akaniambia:

((Ufunge huu juu yako)).

Nikasema:

"Ewe Mtume wa MwenyeziMungu kwani sisi ni wenye kuhesabiwa kwa tunayoyasema?"

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

((Amekukosa mama yako ewe Muadh, unadhani kwa sababu gani watu watatupwa kwa nyuso zao katika Moto (Jahanam) isipokuwa kwa yale yaliyochuma ndimi zao?))."

Imesimuliwa na Attirmidhy na akasema ni hadithi njema na sahihi

 

Katika hadithi hii Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) anamfahamisha sahibu yake na kipenzi chake Muadh bin Jabal (Radhiya Llahu anhu) juu ya mambo yaliyo muhimu katika Uislam moja baada ya jingine kufuatana na daraja zake.

Ameanzia juu ya ubaya wa shirki, kisha juu ya nguzo za dini, kama vile Swala na Zaka, Kufunga na Kuhiji, kisha akamjulisha juu ya kheri inayotakiwa kupigiwa hodi mara kwa mara, nayo ni funga za Sunnah zinazomkinga mtu na moto, pamoja na kutoa sadaka kuwasaidia masikini, na kwamba sadaka hizo hufuta madhambi kama maji yanavyozima moto, na kwamba Swala nyakati za usiku zinamnyanyua mtu daraja za juu.

Baada ya kumjulisha juu ya yote hayo, akamfahamisha kuwa 'Kichwa cha jambo ni Uislamu', akimaanisha kwamba Muislamu anatakiwa kuuweka Uislamu mbele kuliko jambo lake lolote lile na kwamba asikubali kutenda jambo au kutii amri yoyote ile inayokwenda kinyume au kupingana na dini ya Kiislamu.

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alimwambia Muadh (Radhiya Llahu anhu) kuwa haya yote ni mfano wa nyumba na kama ilivyokuwa nyumba haisimami bila ya nguzo, basi Muislamu bila ya kutimiza nguzo za Uislam kwa kuswali na kutoka zaka na kufunga na kuhiji kwa mwenye uwezo, basi hawi Muislamu wa kweli.

Kisha akaendelea kumfahamisha Sahaba wake huyo (Radhiya Llahu anhu) kwamba kilele cha Uislamu ni Jihadi. Na maana yake ni kuwa heshima ya mpiganaji Jihadi iko juu, 'Kileleni', na hii ni kwa sababu Umma wa Kiislamu ni Umma wa Jihadi ambayo kwayo tu ndiyo umma utaheshimiwa, na kwamba umma utakapoiacha Jihadi na kuyakimbilia maisha ya dunia, basi utadhalilika.

Mwisho akamtahadharisha kuwa baada ya kutenda yote hayo na kuzikusanya thawabu zake, itambidi aufunge ulimi wake, ama sivyo utakuja kumpotezea thawabu zake zote na kusababisha kutumbukizwa ndani ya Moto wa Jahannam juu mema yake aliyotenda katika Kufunga na Kuswali na kutoa Zaka na Kuhiji na kupigana Jihadi.

 

Maana ya Ghiyba

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliwauliza Masahaba (Radhiya Llahu anhum):

"Mnajua nini maana ya kusengenya (Ghiyba)? "

Wakasema:

"MwenyeziMungu na Mtume wake wanajua zaidi."

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

"Kusengenya, ni kuzungumza juu ya nduguyo (Muislam) yale asiyoyapenda".

Akaulizwa:

"Unaonaje ikiwa ninayoyasema anayo kweli?"

Akasema:

"Ikiwa anayo kweli basi huko ndiko kusengenya, na ikiwa hanayo basi hayo ni madhambi makubwa zaidi (kwa kumsingizia uongo)".

Muslim

 

Hukmu yake

Maulamaa wote wamekubaliana kuwa Kusengenya ni Haramu na ni katika madhambi makubwa (Kabair).

Amesema Ibni Kathiyr katika tafsiri yake:

"Ghiyba (Kusengenya), ni haramu pasipo na hitilafu baina ya maulamaa na hasameheki yeyote anayesengenya isipokuwa ikiwa nia ya kusengenya huko iwe kwa ajili ya kupinga ushahidi wa dhulma au kusahihisha makosa au katika kutoa nasaha".

 

Anasema Imam Al Qurtubiy:

"Hapana hitilafu yoyote baina ya maulamaa kwamba kusengenya ni katika madhambi makubwa, na atakayefanya kosa hilo lazima atubu kwa Mola wake".

Na hii ndiyo maana Mwenyezi Mungu Subhanahau wa Taala akasema:

"Je! Mmoja wenu anapenda kula nyama ya nduguye aliyekufa? La, Hampendi; (Basi na haya msiyapende)".

 

Kama ilivyokuwa hapana kitendo kibaya kuliko mtu kula nyama ya ndugu yake aliyekufa asiyeweza kujitetea, basi hivyo hivyo hapana kitendo kibaya kuliko mtu kumsengenya ndugu yake asiyekuwepo na kwa ajili hiyo hana uwezo wa kujitetea".

Na Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

"Lililo baya zaidi kuliko mtu kula riba ni kule kuendelea kwa mtu kuzungumza juu ya makosa ya nduguye".

Attabarani

 

Heshima ya Muislamu

MwenyeziMungu ameitukuza heshima ya mwanadamu pale alipowaamrisha Malaika wake watukufu wasiomuasi wamsujudie baba yao Adam (alayhi ssalaam), kisha akamtukuza kwa kumruzuku vitu vizuri vizuri na kumwezesha kupanda vipandio vya barani na baharini.

Mwenyezi Mungu anasema:

æóáóÞóÏú ßóÑøóãúäóÇ Èóäöí ÂÏóãó æóÍóãóáúäóÇåõãú Ýöí ÇáúÈóÑøö æóÇáúÈóÍúÑö æóÑóÒóÞúäóÇåõã ãøöäó ÇáØøóíøöÈóÇÊö æóÝóÖøóáúäóÇåõãú Úóáóì ßóËöíÑò ãøöãøóäú ÎóáóÞúäóÇ ÊóÝúÖöíáÇð

"Na hakika tumewatukuza wanaadamu na tumewapa vya kupanda barani na baharini na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri na tumewatukuza kuliko wengi katika wale tuliowaumba kwa utukufu ulio mkubwa (kabisa)".

Bani Israil - 70

 

Kutoka kwa Abdillahi bin Umar bin Khattab (Radhiya Llahu anhu) alisema kwamba siku moja alimuona Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akitufu huku akisema kuiambia Al Kaaba:

"Uzuri ulioje ulio nao, uzuri ulioje wa harufu yako. Utukufu ulioje wako na wa Heshima yako. Ninaapa kwa yule ambaye nafsi ya Muhammad imo mikononi mwake kwamba Heshima ya Muislamu ni tukufu zaidi mbele ya MwenyeziMungu kuliko heshima yako".

Ibni Majah

 

Huu ndio utukufu wa heshima ya Muislamu mbele ya MwenyeziMungu, na hii ndiyo sababu Mwenyezi Mungu akaharamisha kuvunjiwa heshima hiyo kwa kudhulumiwa, kudhaniwa vibaya, kupelelezwa na kusengenywa.

Kabla mtu hajaufungua mdomo wake kuanza kuzungumza juu ya makosa ya ndugu yake, inampasa akumbuke kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:

ãóÇ íóáúÝöÙõ ãöä Þóæúáò ÅáÇ áóÏóíúåö ÑóÞöíÈñ ÚóÊöíÏñ

"Hatoi kauli yoyote isipokuwa karibu naye yuko mngojeaji tayari (kuandika)".

Qaf - 18

 

Na kauli Yake Subhanahu wa Taala Aliposema:

Åöäøó ÇáÓøóãúÚó æóÇáúÈóÕóÑó æóÇáúÝõÄóÇÏó ßõáøõ ÃõæáÜÆößó ßóÇäó Úóäúåõ ãóÓúÄõæáÇð

"Hakika masikio na macho na moyo hivyo vyote vitaulizwa".

Al Israa - 36

 

Na hii ni kwa sababu Muislam anaamini kuwa macho aliyopewa na Mola wake pamoja na ulimi na masikio, vyote hivyo ni amana na kwamba siku moja ataulizwa juu yake. Bali Muislam anatakiwa avitumie viungo hivyo katika mambo yanayomridhisha Mola wake, na kwa ajili hiyo pale anapoona mazungumzo yanageuka kuwa kusengenya watu (kuzungumza habari za watu), akataze na ikiwa hawamsikii basi ajitenge nao, kwa sababu dhambi anapata msemaji na msikilizaji pia kama tutakavyoona kila tukiendelea mbele.

Mwenyezi Mungu anasema:

æóÅöÐóÇ ÓóãöÚõæÇ ÇááøóÛúæó ÃóÚúÑóÖõæÇ Úóäúåõ æóÞóÇáõæÇ áóäóÇ ÃóÚúãóÇáõäóÇ æóáóßõãú ÃóÚúãóÇáõßõãú ÓóáÇãñ Úóáóíúßõãú áÇ äóÈúÊóÛöí ÇáúÌóÇåöáöíäó

"Na wanaposikia upuzi hujitenga nao na husema (kuwaambia wapuuzi hao),; 'Sisi tuna vitendo vyetu (amali zetu) na nyinyi mna vitendo vyenu, amani juu yenu (inayotokana na sisi - hamtasikia kwetu baya). Sisi hatutaki (kujibizana na) watu wajinga".

Al Qasas 55

Na Akasema:

ó æóÅöÐóÇ ãóÑøõæÇ ÈöÇááøóÛúæö ãóÑøõæÇ ßöÑóÇãðÇ

"Na wanapopita penye upuzi hupita kwa hishima (yao)".

Al Furqan - 72

 

Mifano ya Ghiyba

1-   Kuashiria Kwa Mkono

Anasema Bi bi Aisha (Radhiya Llahu anha):

"Siku moja nilimwambia Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam):

"Muangalie Swafia yuko hivi".

(Akaashiria kwa mkono wake kuonyesha kuwa ni mfupi).

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:

"Umetamka neno, lingechanganywa na maji ya bahari basi maji yangebadilika".

 

Huyu ni Mke wa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam), mama wa Waislam (Radhiya Llahu anha), alipoashiria tu kwa mkono bila ya kutamka kwa ulimi wake, akikusudia kuwa mke mwenzake Bibi Swafiya binti Huyay (Radhiya Llahu anhu) ni mfupi, - juu ya kuwa bibi Swafiya (Radhiya Llahu anha) alikuwa ni mfupi kweli, lakini Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alimkataza Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha) na kumfahamisha kuwa kufanya hivyo ni katika kusengenya na kwamba uzito wa dhambi ya kuashiria ni sawa na kutamka kwa ulimi, na kama ishara yake ile ingechanganywa na maji ya bahari basi maji yangebadilika.

 

2-    Waambie Mumekwishakula

Imesimuliwa na Anas bin Malik (Radhiya Llahu anhu) kuwa Waarabu walikuwa wakitumikiana katika safari na kwamba katika mojawapo ya safari zao pamoja na Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam), Abubakar na Umar (Radhiya Llahu anhum) walikuwa na mtumishi wao akiwatumikia.

Wakiwa safarini, asubuhi moja waliamka na kumuona mtumishi bado amelala.

Mmoja wao akasema:

“Muamshe, huyu analala kama yuko nyumbani“.

Wakamwamsha na kumwambia:

“Nenda kwa Mtume wa MwenyeziMungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na umwambie kuwa Abubakar na Umar wanakusalimia na wanataka chakula (chao)“

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:

“Waambie mumekwishakula“.

Walipoambiwa hivyo wakashangaa na kumuuliza Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam):

“Kitu gani tulichokula?”

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

“Nyama ya ndugu yenu - Ninaapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, naiona nyama yake baina ya meno yenu“.

Wakasema;

"Tuombee maghfira".

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema;

"Muombeni yeye akusameheni".

 

Hawa ni Masahaba watukufu (Radhiya Llahu anhum) wakiwa safarini kwa ajili ya jukumu tukufu nalo ni Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, lakini kwa vile wamemsema mwenzao kuwa; "Analala kama yuko nyumbani“, bila mwenyewe kuwasikia, Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akawaambia kwamba wamekwisha kula nyama ya ndugu yao huyo.

Tutahadhari ndugu zangu Waislam kwani mara ngapi tunasema maneno huku tukiyaona mepesi ulimini mwetu bila kujuwa uzito wake mbele ya Mwenyezi Mungu;

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Hakika mja anaweza kutamka neno litakalomridhisha Mwenyezi Mungu bila yeye mwenyewe kuhisi na (kwa neno hilo) Mwenyezi Mungu atamnyanyua daraja nyingi. Na hakika mja anaweza kutamka neno litakalomghadhibisha Mwenyezi Mungu bila yeye mwenyewe kuhisi, akaporomoka nalo neno hilo ndani ya moto wa Jahannam."

Bukhari

 

Utawasikia watu wakisema kwa mfano:

“Fulani anakula sana ”

“Fulani bakhili”.

 

Bali wengine wanavuka mipaka zaidi na utawasikia wakisema:

"Ah! Nasikia utajiri ule kaupata kwa sababu ya maunga".

Au wanasema;

"Fulani mnafiki"

Na ukiwakataza watakujibu:

“Kwani sisi hatumsemi vibaya eti, yote hayo anayo kweli.”

 

Wengine utawasikia wakisema:

"Sisi hatuzungumzi kwa nia mbaya, bali nia yetu ni kujaribu kuwasaidia, kwani katika kuzungumza huku huenda tukapata ufumbuzi wa tatizo ".

Wanaosema hivi inawapasa wajuwe yafuatayo:

Kwanza kabisa lazima wakumbuke maana ya neno 'Kusengenya' kama lilivyofasiriwa na Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pale alipowauliza Masahaba wake (Radhiya Llahu anhu) iwapo wanajuwa maana ya neno 'Ghyba',

Masahaba (Radhiya Llahu anhu) wakamjibu:

"MwenyeziMungu na Mtume wake wanajua zaidi"

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

"Kusengenya, ni kuzungumza juu ya nduguyo (Muislam) yale asiyoyapenda".

Akaulizwa:

"Unaonaje ikiwa ninayoyasema anayo kweli?"

Akasema:

"Ikiwa anayo kweli basi huko ndiko kusengenya, na ikiwa hanayo basi hayo ni madhambi makubwa zaidi (kwa kumsingizia uongo)".

 

Wakumbuke kuwa kitendo chochote lazima kikubaliane na sheria. Nia nzuri peke yake haitoshi kumsalimisha mtu na adhabu ya MwenyeziMungu. Na kumsema mtu vibaya kwa nia mbaya au nzuri akiwa hayupo huko ni Kusengenya.

Tatu, mwenye kutaka maslahi ya mwenzake anaweza kumnasihi aache mabaya na afanye mema, hata kama itambidi azungumze naye tena na tena au kumtumia mtu mwenye hekima zaidi ikiwa atashindwa. Na kama baada ya kufanya yote hayo na kujaribu njia mbali mbali za kisheria bado mtu huyo haachi maovu yake, basi amuache kama alivyo bila ya kumfedhehesha wala kumsengenya.

 

3-   Mwenye Kusengenya Na Msikilizaji Wote Sawa

Katika hadithi iliyotangulia ya mtumishi wa Abubakar na Umar (Radhiya Llahu anhum) aliyeambiwa kuwa analala usingizi wa nyumbani, tumeona kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliwaambia wote wawili kuwa wamemsengenya mwenzao ingawaje aliyetamka maneno yale ni mmoja wao na mwingine alisikiliza tu.

Hii ni dalili kuwa msemaji na msikilizaji wote wana makosa na wote wanapata dhambi.

Hadithi ifuatayo iliyosimuliwa na Abu Huraira (Radhiya Llahu anhu) inatupa fundisho hilo hilo kuwa msemaji na msikilizaji wote ni sawa:-

 

Anasema Abu Huraiarah (Radhiya Llahu anhu):

"Alikuja Al Aslamiy (Radhiya Llahu anhu) kwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akatoa ushahidi dhidi ya nafsi yake mara nne kuwa alizini, na alikuwa kila anapojishtaki, Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akimkatalia (huku akimtafutia udhuru). Lakini ilipofika mara ya nne, Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:

"Ulimwingila?"

Akasema:

"Ndiyo".

Akamuuliza:

"Mpaka ikapotea yako ndani ya yake?"

Akasema:

"Ndiyo".

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuuliza:

"Kama inavyopotea 'mili' (kifuniko cha chupa ya wanja) ndani ya chupa ya wanja na kamba ndani ya kisima?"

Akasema:

"Ndiyo"

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuuliza:

"Unajuwa nini maana ya zina wewe?"

Akasema:

"Ndiyo, najuwa, nimefanya kitendo cha haramu kile ambacho mtu anatenda na mkewe kwa halali".

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuuliza:

"Unakusudia nini kwa kauli yako hii?"

Akasema:

"Nataka unitahirishe ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu".

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akaamrisha apigwe mawe mpaka afe.

 

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliwasikia watu wawili katika Masahaba (Radhiya Llahu anhum) wakisema:

"Mtizameni huyu ambaye Mwenyezi Mungu amemsitiri na hakuridhika mpaka alipopigwa mawe kama mbwa".

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akanyamaza kimya bila kuwaambia kitu, na baada ya kwenda masafa marefu kidogo akaona mzoga wa punda, akasema:

"Wako wapi fulani na fulani?"

Wakasema:

"Sisi hapa ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu".

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:

"Shukeni mule mzoga huu wa punda".

Wakasema:

"Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, vipi mtu anaweza kula mzoga?".

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akawaambia:

"Basi kile mlichokula katika heshima ya ndugu yenu muda mchache uliopita (pale mlipomsengenya) ni kibaya zaidi kuliko kuula mzoga huu. Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, yeye hivi sasa yumo ndani ya mito ya Peponi anajichovya ndani yake".

Bukhari - Imam Ahmed - Al Bayhaqiy na wengineo

 

Katika hadithi hii, tunapata fundisho jingine kuwa msemaji na msikilizaji wa ghiyba wote ni sawa, kwani juu ya kuwa aliyetamka maneno yale ni mtu mmoja, na mwenzake alikuwa akimsikiliza tu, lakini Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliwaambia wote wawili:

"Shukeni mule mzoga huu wa punda".

Kisha akawaambia:

"Kile mlichokula katika heshima ya ndugu yenu muda mchache uliopita ni kibaya zaidi kuliko kuula mzoga huu".

 

Heshima ya ndugu yako

Kutoka kwa Kaab bin Malik (Radhiya Llahu anhu) akisimulia kile kisa cha 'Wale watatu waliongojeshwa' - ambapo yeye ni mmojawapo - kwa sababu ya kutokwenda vitani pamoja na wenzake siku ya vita vya Tabuk, alisema:

"Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alisema akiwa amekaa baina ya watu wake alipowasili mji wa Tabuk:

"Amefanya nini Kaab bin Malik?'

Mtu mmoja kutoka katika kabila la Bani Salamah akasema:

"Kilichomzuwia ni shuka yake na kuipenda nafsi yake".

Muadh bin Jabal (Radhiya Llahu anhu) akasema:

"Maneno gani mabaya haya uliyosema? Wallahi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu hatujapata kuona kutoka kwake (Kaab) isipokuwa kheri tupu".

 

Hivi ndivyo Muislam anavyotakiwa. Afanye kama alivyofanya Muadh bin Jabal (Radhiya Llahu anhu), mara anapomsikia mtu akimsengenya mwenzake amtetee, kwani katika kumtetea nduguyo Muislam utapata radhi za Mola wako na kuepushwa na Moto siku ya Kiama.

Kwa hivyo unapomsikia mtu anamsengenya mwenzake wewe usijiingize katika bahari hiyo na kupiga mbizi naye, bali umkataze na kujaribu kumtetea kama uwezavyo yule anayesengenywa, kwa sababu ukinyamaza na kusikiliza, ujuwe kuwa wewe na msengenyaji mko katika daraja moja ya maasi.

Mwenyezi Mungu anasema:

Åöäøó ÇáÓøóãúÚó æóÇáúÈóÕóÑó æóÇáúÝõÄóÇÏó ßõáøõ ÃõæáÜÆößó ßóÇäó Úóäúåõ ãóÓúÄõæáÇð

"Hakika masikio na macho na moyo hivyo vyote vitaulizwa".

Al Israa - 36

Na Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Atakayeitetea heshima ya ndugu yake, Mwenyezi Mungu atamuondolea moto mbele ya uso wake Siku ya Kiama".

Ahmed na Attirmidhy na wengine

 

Na akasema:

"Atakayemnusuru mwenzake asiyekuwepo, Mwenyezi Mungu atamnusuru duniani na akhera".

Al Baihaqiy

 

Yote haya ni mafundisho mema na makatazo makali kutoka kwa Mtume wetu mtukufu Muhammad (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kwa ajili ya kuujenga umma huu uwe umma unaopendana, umma unaosikilizana, umma unaositiriana ili upate kuwa umma wenye nguvu na kujishughulisha na mambo yatakayoweza kuupa nguvu na kuunyanyua badala ya kujishughulisha na yale yatakayoudhoofisha na kuuangusha.

Katika kusengenyana yanapatikana maovu mengi sana yakiwemo yafuatayo:-

a) Kwenda kinyume na sheria inayomuamrisha kila Muislamu kumsitiri Muislamu mwenzake.

b) Kueneza na kuitia mizizi shaka katika mwili wa Waislamu na kusababisha Waislamu wasiwe na Imani hata juu ya watu wema miongoni mwao.

c) Waislamu kushughulika na kusengenyana wao kwa wao na kueneza chuki baina yao na kuacha kushughulika na yaliyo muhimu yatakayowaondolea shida zao na shida za Umma.

d) Kumpa nguvu mwenye kitendo  hiki na dhambi hii (ya kusengenya) na kumfanya asitake kuiacha na aendelee nayo bila kujali.

e) Kila mwenye akili timamu anatambua kwamba jamii ya kiislamu haiwezi kunufaika na lolote kwa njia hii ya kumsengenya mtu aliyejisitiri na aibu yake. Na ni faida gani inayoweza kupatikana katika kumsengenya mtu aliyefanya madhambi yake kwa kujificha au aliyeificha siri au aibu yake, au yule aliyesitiriwa na Mola wake?

 

Sababu zake

Yafuatayo ni baadhi tu ya mambo yanayosababisha au kumpatia mtu kisingizio cha kumsengenya mwenzake;

1-   Ghadhabu

Mara nyingi ghadhabu hupowa pale mtu anapomuona yule anayemchukia akipatwa na masaibu, na huburudika roho yake kwa kumsengenya kila anapopata fursa.

Mtu wa aina hii dawa yake ni kuikumbuka kauli ya MwenyeziMungu isemayo:

óæÓóÇÑöÚõæÇú Åöáóì ãóÛúÝöÑóÉò ãøöä ÑøóÈøößõãú æóÌóäøóÉò ÚóÑúÖõåóÇ ÇáÓøóãóÇæóÇÊõ æóÇáÃóÑúÖõ ÃõÚöÏøóÊú áöáúãõÊøóÞöíäó. ÇáøóÐöíäó íõäÝöÞõæäó Ýöí ÇáÓøóÑøóÇÁ æóÇáÖøóÑøóÇÁ æóÇáúßóÇÙöãöíäó ÇáúÛóíúÙó æóÇáúÚóÇÝöíäó Úóäö ÇáäøóÇÓö æóÇááøåõ íõÍöÈøõ ÇáúãõÍúÓöäöíäó

"Na yaendeeni upesi maghufira ya Mola wenu na Pepo (Yake) ambayo upana wake (tu) ni (sawa na ) mbingu na ardhi (Pepo) iliyowekewa wamchao Mungu.

Ambao hutoa katika wasaa na katika (hali ya) dhiki, na wazuiyao ghadhabu na wanaosamehe watu (na wafanyao ihsani); na MwenyeziMungu hupenda wafanyao ihsani".

Aali Imran 133-134

 

Na pia akumbuke maneno ya Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliposema:

"Atakeyeizuwia ghadhabu na hali ya kuwa anaweza kuitowa, MwenyeziMungu atamuita (Siku ya Kiama) akiwa katikati ya watu na kumtaka achague miongoni mwa Huurul ayni ili amuozeshe anayemtaka".

 

Imepokelewa kuwa Imam Aliy Zeinul Abideen (Radhiya Llahu anhu) alikuwa mwingi wa kusamehe. Siku moja kijakazi wake alipokuwa akimmiminia maji kwa ajili ya kutawadha kikamponyoka chombo cha maji na kumuangukia Imam usoni pake na kumchana juu ya kipaji cha uso wake.

Imam akainua uso wake juu na kumtizama mtazamo wa kumlaumu. Kijakazi akasema:

“Mwenyezi Mungu anasema; ‘æóÇáúßóÇÙöãöíäó ÇáúÛóíúÙó’ “Na wazuiyao ghadhabu”

Akamjibu: “Na mimi nimeizuwiya ghadhabu yangu.”

Akasema; “Na amesema; ‘æóÇáúÚóÇÝöíäó Úóäö ÇáäøóÇÓö“Na wanaosamehe watu”

Akamjibu; “Na mimi nimekusamehe.”

Akasema: æóÇááøåõ íõÍöÈøõ ÇáúãõÍúÓöäöíäó “Na Mwenyezi Mungu anawapenda wafanyao ihsani”.

Akamwambia: “Nimekuachia huru kwa ajili ya Mwenyezi Mungu”.

 

Na kutoka kwa Anas (Radhiya Llahu anhu) amesema:

"Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alinambia: "Ukiweza kuwa mtu asiyekuwa na chuki wala kuwaghadhibikia wenzake wakati wote asubuhi na jioni, basi kuwa hivyo".

Tulikuwa tumekaa siku moja pamoja na Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam), akasema:

"Sasa hivi ataingia ndani humu mtu katika watu wa Peponi".

Akaingia mtu katika watu wa Madina.

Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akayarudia tena maneno yale siku ya pili na ya tatu yake na ya nne na zote hizo alikuwa akiingia mtu yule yule katika watu wa Madian.

Abdillahi bin Umar (Radhiya Llahu anhu) akamfuata yule mtu hadi nyumbani kwake kutaka kujuwa jambo gani analolifanya hata akastahiki kuwa mtu katika watu wa Peponi. Na katika riwaya nyingine aliyemfuata alikuwa ni Abdillahi bin Amru bin al Aas (Radhiya Llahu anhu), akakaa naye nyumbani kwake muda wa siku tatu.

Anasema Abdillahi bin Umar (Radhiya Llahu anhu):

"Siku zote hizo nilizokaa naye sikumuona akifanya ibada zozote zile za zaidi isipokuwa anapokuwa usingizini alikuwa kila anapogeuka akimtaja Mwenyezi Mungu".

Siku ya mwisho akamuelezea juu ya yale Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliyosema juu yake. Yule mtu akasema:

"Mimi kama ulivyoniona sifanyi ibada zozote za zaidi isipokuwa kabla sijajitupa juu ya godoro langu ninamsamehe kila Muislam aliyenikosea na silali mpaka nihakikishe kuwa moyoni mwangu hamna husda yoyote ile juu ya mwenzangu kwa kheri aliyopewa na Mwenyezi Mungu".

Abdillahi (Radhiya Llahu anhu) akamwambia:

"Hili ndilo lililokufikisha (Peponi)".

Attirmidhiy na Annasaiy

 

Imepokelewa na Ibni Majah na Al Baihaqiy pia kwa isnadi zilizo sahihi kuwa Abdillahi bin Umar (Radhiya Llahu anhu) amesema:

"Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliulizwa 'Watu gani walio bora?"

Akajibu:

"Wenye nyoyo safi, wanaopenda kusema kweli".

 

Na kutoka kwa Ibni Abi Dunya amesema kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Wengi kati ya umati wangu wataingia Peponi si kwa ajili ya wingi wa kuswali wala wingi wa kufunga wala wingi wa kutoa zaka, bali wataingia kwa rehma ya Mwenyezi Mungu na kwa usafi wa nyoyo zao na usalama wa vifua vyao".

 

Na kutoka kwa Imam Ahmed na Al Baihaqih wamesema kuwa Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:

"Wamefuzu wale wenye kuzishughulisha nyoyo zao kwa ajili ya imani tu pamoja na kuzisalimisha nyoyo hizo".

 

2) Kuridhishana

Miongoni mwa yanayomuingiza mtu katika ghiyba ni pale mtu anaponyamaza kwa ajili kuwaridhisha marafiki ili wasiudhike naye kwa kuwavunjia raha zao katika mazungumzo pale anapowasikia wakizungumza juu ya watu na ili wasichukizwe naye wakamuona kuwa ni mzigo kwao ikiwa atawakataza kila mara kwa kuwaambia:

“Haramu, msifanye hivi, haijuzu, msisengenye watu”.

 

Anayefanya hivyo atajikuta anaishia kusaidia katika kuwasengenya waislamu wenzake na kudhani kuwa huko ndiko kuishi na watu vizuri.

Hii, dawa yake ni kuikumbuka Hadithi ya Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliposema:

"Anayetafuta kumridhisha Mwenyezi Mungu bila kujali kama atawaghadhibisha watu, basi Mwenyezi Mungu atamtosheleza, na kuwafanya watu wampende. Na anayetafuta kuwaridhisha watu bila kujali kama atamghadhibisha Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu atamsukumiza huko huko kwa watu."

3) Kujipendekeza

          Mwengine hupenda kujinyanyua daraja yake aonekane kuwa ni bora kuliko mwenzake kwa njia ya kumtia kasoro mwenzake kwa kusema kwa mfano:

“Fahamu yake Fulani huyu ni ndogo masikini” nk.

 

Maneno ya aina hii anayasema akiwa na nia ya kutaka kujipendekeza na kujionyesha kuwa yeye ni bora kuliko mwenzake.

Dawa ya maradhi haya ni kuamini kwamba yaliyoko kwa MwenyeziMungu ni bora zaidi na ndiyo yatakayobaki na kwamba dunia hii kwa MwenyeziMungu thamani yake ni ndogo kuliko hata ubawa wa mbu, na kwamba huenda mtu huyo anayemdharau akawa ni bora kuliko yeye mbele ya MwenyeziMungu kama alivyosema Mtume (Swalla Llahu alayhi wa sallam):

"Huenda mwenye nywele zilizotimka (masikini) anayefukuzwa milangoni, akimuomba MwenyeziMungu akamkubalia dua yake".

 

4) Kuchekesha watu

Nako ni kuwapaka matope wenzao kwa kuzungumza juu ya makosa yao kwa ajili ya kuwachekesha watu katika mabaraza. Watu wa aina hiyo kila siku utawasikia wakileta habari mpya:-

“Umesikia mpya sheikh! Nasikia fulani hivi, au fulani vile", na watu wanacheka na kuyafurahia.

Wengine kazi zao za kujipatia rizki katika radio na television na juu ya majukwaa ni kuchekesha watu kwa kuwafedhehesha wengine.

Hawa waikumbuke kauli ya Mtume wa MwenyeziMungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliposema:

"Adhabu kali itamthubutukia mwenye kuzungumza maneno ya uongo ili achekeshe watu, adhabu kali itamthubutukia adhabu kali itamthubutukia."

 

5) Husda

Huenda mtu anayependwa na watu alisifiwa katika kikao, na hasidi akayasikia hayo akaungulika moyoni mwake, akataka kumpaka matope mwenzake ili sifa ile pamoja na heshima aloipata imuondokee.

Hasidi huyo ajuwe ya kuwa anapotumia njia hiyo anamfanya mtu huyo awe juu yake kwa daraja duniani na akhera pia.

 

Ikiwa na yeye anaitaka sifa aloipata mwenzake, basi njia yake