1. Utangulizi
2. Mashia
wanavyowagawa Masahaba
3. Nani Sahaba –
kilugha na kidini
4. Nani Mnafiki –
kilugha na kidini
5. Pili
- Ugawaji wa kweli wa Masahaba Kishia (Ithnaasheri)
6. Majibu juu ya
itikadi ya ugawaji wa Masahaba Kishia
Kitabu
kinachofichua uongo wa Attiygany uliomo ndani ya kitabu chake alichokiita (ثم اهتديت) 'Kisha Nikaongoka'
Kimeandikwa
na Khaled al Asqalaani
Kimetafsiriwa
na Muhammad Faraj
Abdullahi
bin Saba-a aliyekuwa Myahudi kutoka mji wa Sana-a - Yemen, aliingia katika dini
ya Kiislamu akiwa na nia ya kuwatenganisha na kuwafitinisha Waislamu kwa
kisingizio cha kuwapenda sana Ahlul Bayt (Watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi
Mungu wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
Mtu
huyu alifanikiwa kiasi kikubwa kulifanya kundi kubwa la Waislam liamini kuwa
Qurani Tukufu ina makosa, haikukamilika, na kwamba imebadilishwa na kupunguzwa.
Alifanikiwa pia kulifaya kundi hilo liwatuhumu Masahaba wakubwa wa Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kuwa ni Wanafiki pamoja na kuwatuhumu
Maimam wakubwa wa Kiislam kuwa ni watu wajinga, pamoja na kuvituhumu vitabu vya
hadithi Sahihi kama vile Bukhari na Muslim na venginevyo kuwa ni vya uongo.
Abdillahi
bin Saba- a huyu, ni mtu wa mwanzo kuueneza uongo wa kufaridhisha Uimamu wa
Sayiduna Aly (Radhiya Llahu anhu), na
kwamba anayeukataa Uimamu huo anakuwa kafiri na hatoingia Peponi, pamoja na
kuwatukana na kuwakufurisha Makhalifa watatu wa mwanzo, Abubakar, Omar na
Othman (Radhiya Llahu anhum).
Aliweza
kupata wafuasi wengi kiasi walioyameza na kuyakubali maneno hayo, na kuueneza
ufisadi huo kwa kusudi la kuwagawa Waislam kwa bidhaa yake hiyo ovu.
Bidhaa
yenyewe ni madai kuwa Makhalifa wa mwanzo hawakuwa na haki ya kutawala na
kwamba wamemdhulumu Aly (Radhiya Llahu anhu) , na kwamba Aly (Radhiya Llahu
anhu) aliteuliwa na Mwenyezi Mungu kuwa Khalifa wa Waislam kwa ushahidi wa
Qurani na Sunnah, na kwamba kwenda kiyume na hayo ni kufru.
Wafuasi
hawa wa Abdullahi bin
Kwa
ajili ya kuziendeleza fikra hizo, kisa cha kuuliwa kwa Al Husayn (Radhiya Llahu
anhu) kikageuzwa kuwa ni matanga yanayofanywa kila mwaka. Haya ni mambo ya
ajabu kabisa, kwani tatizo hili limekwisha malizika tokea karne nyingi
zilizopita lakini kwa makusudi wanaihuisha kila mwaka siku hii wa ajili ya
kuiendeleza fikra hii ya Uimam.
Wanaendelea
kujiadhibisha kwa kujipiga vifua, kujitoa damu tena kwa visu na minyororo huku
wakilizana, wakati kulia na kujitesa kwa ajili ya kifo kilichotokea miaka elfu
moja mia nne iliyopita, bali hata kwa kifo kilichotokea leo, ni haramu kubwa na
haijuzu kwa kila Muislam mwenye akili timam na mwenye kufuata maamrisho ya dini
na mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu alayhi wa sallam).
Mtume
wa Mwenyezi Mungu(Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Hayuko pamoja nasi anayepiga mashavu na kuchana nguo na kuomboleza
Bukhari
na Muslim
Na
akasema;
“Atakayelia kwa kuomboleza kisha asitubu, basi atavishwa nguo za
moto Siku ya Kiama.”
Bukhari
na Muslim
Na
hadithi za namna hii ziko nyingi
Mitume
wangapi (Alayhimus Salaam) wameuliwa. Masahaba walio bora kuliko Al Husayn
(Radhiya Llahu anhu) wameuliwa, akiwemo baba yake - Aly, pamoja na Othman bin
Affan (Radhiya Llah anhum), bila shaka Aly na Othman ni bora kuliko Al Husayn
(Radhiya Llahu anhum). Wote hawa waliuliwa kwa dhulma na kuonewa lakini
hatujawaona wakifanya misiba na maombolezi.
Isitoshe,
ikiwa sisi tunaamini kuwa Al Husayn (Radhiya Llahu anhu) yuko Peponi
akineemeka,
Wanayahuisha
matendo
Chuki za kuwachukia nani? Mayahudi au Manasara? La,
bali chuki za kuwachukia watukufu wa Umma huu na Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi
Mungu Muhammad bin Abdillah (Swalla Llahu alayhi wa sallam) walioinyanyua
bendera ya Mwenyezi Mungu na kuieneza kila pembe ya dunia, mara tu baada ya
kufariki kwa kipenzi chao, Mtume wa Mwenyezi Mungu wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam).
Mashia wanawagawa Masahaba
(Radhiya Llahu anhu) katika makundi matatu:
La kwanza ni wale wanaowaita
kuwa ni wema waliomjua Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala na kumjua Mtume wa
Mwenyezi Mungu wake (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kama inavyopaswa,
wakafungamana naye na kuwa Masahaba wa kweli katika kauli zao na kuwa wakweli
katika matendo yao na baada ya kufa kwake hawakugeuka, bali walithibiti; hata
Mwenyezi Mungu aliwasifia katika kitabu chake kitukufu katika aya nyingi, na Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pia aliwasifia katika hadithi
nyingi.
Mashia wanapowataja Masahaba
hawa, huwataja kwa heshima na kuwapa utukufu mkubwa
La pili ni Mashaba
(Radhiya Llahu anhum) walioingia katika dini na kumfuata Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ama kwa hiari zao au kwa uoga, lakini
walikuwa wakijivunia kusilimu kwao mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam), na baadhi ya wakati walikuwa wakimuudhi Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), na hawakuwa wakifuata maamrisho
na makatazo yake sawasawa, bali walikuwa wakizitanguliza rai zao mbele ya
maamrisho yaliyo wazi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) mpaka pale zinapoteremshwa aya za Qurani zikiwakemea au kuwatisha,
ndipo wanapokubali kufuata maamrisho.
Na wanaamini kuwa Mwenyezi
Mungu amekwisha wafedhehesha Masahaba hao katika aya nyingi za Qurani, na Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pia alikiwisha waonya katika
hadithi nyingi, na Masahaba hawa hawatajwi na Mashia isipokuwa kwa matendo
La tatu, ni wale wanaowaita Wanafiki
waliomfuata Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kwa ajili
ya kumfanyia inda tu, na kwamba waliufanyia inda Uislam na Waislam na kwamba
Mwenyezi Mungu ameteremsha Sura kamili na kuwataja katika mwahali mwingi na
kuwapa ahadi ya kuwaingiza katika tabaka za chini za Motoni. Wanasema kuwa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) keshawataja na kuwaonya watu
juu
Fungu hili la tatu
ni wale ambao Masunni na Mashia wanakubaliana juu ya unafiki wao.
Huu ndio ugawaji wa Mashia kwa
Masahaba, ukilitenga fungu la Masahaba ambao ni watu wa nyumba ya Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ambao wana fadhila zaidi za
kinafsi na za kimaumbile kuliko Masahaba waliobaki.
Kuhusu
Masunni, wao wanasema yafuatayo:
“Juu
ya Masunni kuwaheshimu kwao Ahli l Bayt na kukubali fadhila zao, lakini
hawaukubali ugawaji huu na wala hawakubali kuwa baadhi ya Masahaba ni wanafiki,
bali kwao wao Masahaba wote ni watu walio bora baada ya Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swalla Llahu alayhi wa sallam). Na ikiwa wanawagawa basi ni kwa ajili ya
kutangulia kwao katika Uislam na kwa ajili ya mitihani waliyokumbana nayo, na
wanawafadhilisha Makhalifa waongofu na kuwaweka katika daraja la mbele, kisha
Masahaba sita waliobaki katika wale waliokwisha bashiriwa Pepo
Hii ni kauli ya Mashia ju ya
Masunni.
Majibu:
Kwanza kabisa kabla sijaanza kujibu na kuuchambua
ugawaji huu wa Masahaba katika Itikadi ya Mashia (Ithnaasheri) na kuonesha
ubatilifu wake, sina budi kueleza; Nani Sahaba na nani mnafiki, Kilugha
na kidini, kisha itatubidi tujulishe kusudi la Mashia (Ithnaasheri) katika
ugawaji huu kama walivyoandika katika vitabu vyao wanavyovikubali, ili
iwepesike kwa msomaji kuijua haki iko wapi na batili iko wapi, ikiwa msomaji
huyo ni Sunni au Shia.
Kisha nitajibu juu ya ugawaji wao huo ili aelewe
kila mtu kuwa ugawaji huo uko mbali na haki.
Katika kamusi la lugha ya kiarabu, neno ‘Sahaba’,
maana yake Rafiki, Mwenzi wake, Sahibu nk.
Katika kamusi la dini neno ‘Sahaba’ maana yake ni
Mwislam aliyemuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam),
akawa pamoja naye na kumfuata na kumuamini mpaka kufa kwake.
Na hii ina maana kuwa, yeyote aliyewahi kumouna Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na asimuamini, basi hawezi
kuingia katika maana ya neno ‘Sahaba’.
(Maelezo haya utayapata katika kitabu cha Ibni
Qudama kiitwacho ‘Lam-atul Itiqad’.
Katika
kamusi la lugha ya kiarabu, neno ‘Mnafiki’ maana yake ni mtu
mwenye kigeugeu au mwenye kuwa na sura mbali mbali: Leo hivi kesho vile.
Katika
kamusi ya dini, Mnafiki ni yule anayejidhihirisha kuwa ni Muislam
na kumfuata Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) wakati
undani wake ni kafiri na adui wa Mwenyezi Mungu na adui wa Mtume wa Mwenyezi
Mungu wake (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
(Tafsiri
hii utaipata katika kitabu kiitwacho;
Tariyqul hijratayn wa baabul
saadatayn’ kilichoandikwa na
Ibnul Qayim).
Baada ya tafsiri hii fupi ya nani Sahaba na nani
Mnafiki, tutakubaliana kuwa maneno hayo mawili hayawezi kukubaliana (hayawezi
kwenda sambamba) hata siku moja Kilugha wala Kidini.
Kwa sababu Sahaba ni yule aliyemuamini Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na akafa akiwa Muislam, wakati
Mnafiki ni yule mwenye kujidhihirisha kama ni Mwislam wakati ndani ya nafsi yake
ni kafiri.
Kwa hivyo maneno haya mawili hayakubaliani, na
haiwezekani Sahaba akawa Mnafiki na wala Mnafiki hawezi akawa Sahaba.
Sasa Mtu anaweza kuuliza:
'Vipi tutaweza kutofautisha baina
ya Sahaba na Mnafiki'
Majibu:
Mnafiki ana sifa na alama maalum tulizojulishwa
katika Qurani na katika Mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam), na kwa ajili hiyo tunaweza kutofautisha baina yake na
Sahaba. Tutayaelezea yote kila tukiendelea mbele huku tukizijibu hoja za Mashia
(Ithnasheri).
Ingawaje
kama tulivyoona hapo mwanzo kuwa baadhi ya Mashia wanadai kuwa wao wanawagawa
Masahaba mafungu (makundi) matatu, lakini ukweli ni kuwa wanawagawa mafungu
Mawili tu na wala hakuna la tatu, na haya ni kutokana na kauli mbali mbali za
maulamaa wao na katika vitabu vyao
Kundi
la kwanza la Masahaba (Radhiya Llahu anhu,) katika itikadi ya Kishia, ni lile
waliloridhika nalo wenyewe ambao idadi
Al
Koshy, ambaye ni Mwanachuoni wa Kishia katika elimu ya wapokezi wa hadithi
(Ilmu rijaal), ameelezea kuwa; “ Imam Al Baaqer amesema:
‘Watu
wote walirtadi (baada ya kufariki Mtume wa Mwenyezi Mungu - Swalla Llahu alayhi
wa sallam), isipokuwa Salman na Abu Dhar na Al Miqdad (Radhiya Llahu anhum)’.
Anayesimulia
hadithi hii anaendelea kusema:
‘Nilimuuliza; 'Na Ammar je?’
AkanijibuM
‘Alikuwa akitia na kutoa kisha akarudi’.
(Maelezo haya utayapata katika kitabu kiitwacho ‘Haqul
yaqiin fiy maarifat usuul uddin’ kilichoandikwa na Abdulla Shiyr – aalim wa
Kishia - juzuu ya kwanza ukurasa 370 hadi 371, na katika kitabu ‘Rijalul
Koshy’ ukurasa 17 na ‘Tafsiyr al Abbasy’ juzuu 1 ukurasa 223).
Na
katika mapokezi mengine anasema:
‘Kisha
wakarudi (baadhi ya) watu, na wa mwanzo katika waliorudi ni Abu Sasan Al Ansari
na Ammar na Abu Umeira na Shateera. Walikuwa watu saba, na Amiril Muuminin
hakuwa akiwajuwa isipokuwa hawa saba”.
(Utayakuta
haya katika vitabu hivyo tulivyovitaja).
Ama
Al Kulayni ambaye ni katika wakuu wa Maulamaa wa Kiithnaasheri, katika kitabu
chake kiitwacho ‘Usool mina l Kafi’ (na kitabu hiki ni katika vitabu
kumi na nne ambavyo ni marejeo makubwa ya Madhehebu ya Kishia) anasema:
“Humran
bin Ayun anasema: "Nilimuambia Aba Jaafar alayhi salaam:
"Tuko
wachache
Akaniambia:
’Nitakuhadithia
ya ajabu kupita hayo; Muhajirina (Watu wa Makka) na Answaar (Watu
wa Madina) wote wameangamia isipokuwa ---‘akaniashiria kwa vidole vyake
vitatu…..”
(Usul
minal Kafi – juzu ya 2 ukurasa 191)
Kitabu
cha Al Iman wal Kufr – mlango wa Upungufu wa idadi ya Waislam.
Rijal
l Koshy uk.13
Tafsir
al Safi – juzu 1
Na
katika kitabu kiitwacho Al Rawdha anasema:
“Kutoka
kwa Abdul Rahim al Qasiyr, kasema:
‘Nilimuambia
Aba Jaafar alayhi salaam ‘Watu huwa wanaogopa pale tunapowaambia kuwa watu wote
wamertadi’, akaniambia:
"Ewe
Aba Abdurahim, watu walirudi ‘kuwa makafiri’
“Ewe
Saad wewe ndiye tunayekutegemea ….”
(Al
Raudha ya Al Kafi juzuu ya 8 uk.246)
Hii
ni sehemu ya kwanza ya Masahaba wanaokubalika na Mashia wa Ithnaasheri.
Ama
kundi la pili la Masahaba katika Itikadi ya Kishia, ni Masahaba wote waliobaki
wasiotajwa katika kundi la mwanzo, na wote hao kwao ni Wanafiki na wamertadi na
wenye kigeugeu. Wote wakiongozwa na Makhalifa walioongoka (Al Al Khulafaa Arrashidun),
kisha wale kumi waliobashiriwa Pepo, kisha Masahaba waliobaki.
Hii
ni itikadi ya Mashia Ithnaasheri juu ya Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kutoka katika vitabu vyao
wanavyovitegemea.
Lakini
nini hasa sababu ya ugawaji wao ule wa makundi matatu (uliotajwa hapo mwanzoni)
wa Masahaba?
Sababu
yake ni kujaribu kuwopotosha watu, hasa katika Masunni ili pale unapoanza
kusoma katika vitabu vyao kuwa Masahaba hawakurtadi isipokuwa tu walikuwa
wakiipenda dunia na kwa ajili hiyo walimfuata Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) ama kwa ajili ya kuitaka dunia au kwa ajili ya
kumuogopa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), (yaani
walikuwa wanafiq) na msomaji kila anapoendelea kusoma inakuwa rahisi kwake
kukubali kila wanachoandika juu ya Masahaba hao, na mwisho inakuwa rahisi
kukubali kuwa Masahaba walirtadi. Na kila msomaji anapoendelea kusoma juu ya
kundi la pili, kisha la tatu ambao ni wanafiki na kumfanya msomaji ayameze yote
anayoyasoma kisha anajikuta anawachanganya wale walio katika kundi la pili pamoja
na wa kundi la tatu na kuwaunganisha kuwa ni kundi moja na hatimaye Masahaba
wanageuka kuwa makundi mawili; Kundi moja lenye kuridhisha na lingine
lililogeuka na kurtadi, na mwisho inakuwa rahisi kwa msomaji kuukubali ugawaji
halisi wa Kishia wa kuwagawa Masahaba makundi mawili tu.
Mtu
anapoanza kusoma atadhani kuwa wanafiki waliokusudiwa ni Abdillahi bin Ubay bin
Salool, ambaye ni mkuu wa wanafiki pamoja na kundi lake, lakini jambo la
kushangaza ni kuwa utawaona huyo wanamtetea, na hasa pale Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipomsalia, wakati Umar (Radhiya Llahu
anhu) alipomtaka Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
asimsalie. Kisha wanapinga msimamo wa Masahaba juu ya wanafiki hao.
Ikiwa
wanafiki pia watawaita Masahaba, hii itakuwa na maana kuwa yeyote aliyemuona Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aitwe Sahaba hata
Lakini
Mashia hawaongezi sharti hii; ya kuwa ‘Sahaba lazima awe yule aliyemuamini Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)’.
Iwapo
tutafuata mantiki hiyo, kwa hivyo Mayahudi, Manasara na Washirikina wa Makka
waliomuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) nao pia
wataitwa masahaba kwa sababu ili mtu aitwe Sahaba halazimiki kuwa amemuamini Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
Maneno haya hasema isipokuwa mtu aliyeshiba ujinga.
Wao
wanasema hivyo bila ya kuweka sharti hiyo, kwa sababu ikiwa watasema kuwa;
Sahaba ni yule aliyemuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) na sharti awe amemuamini na afe katika imani hiyo, basi madai yao kuwa wanafiki
nao pia ni Masahaba yatabatilika kwa sababu wanafiki si katika watu
waliomuamini Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam). Na jambo
hili limekubaliwa na Maulamaa wote wa Kishia na Kisunni. (Kuwa Wanafiki si
katika watu Walioamini).
Aly
(Radhiya Llahu anhu) pamoja na wale Masahaba walioridhika nao Mashia, nao pia
wataweza kuingizwa katika kundi la wanafiki (Astaghfirullah), kwa sababu
wao wenyewe watakuwa wameufungua mlango wa kukufurishana bila ya kuweka vipimo
vya kumjua nani Sahaba na nani Mnafiki, na kwa ajili hiyo kila mtu atakuwa na
haki ya kuamini atakavyo juu ya Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam). Wote wataweza kuitwa wanafiki kwa sababu wanafiki ni
miongoni mwa Masahaba (Radhiya Llahu anhum).
Na
kwa mlango huu wamepita wale wasioamini Mungu, wazandiki na wale wazungu wenye
elimu za mambo ya Mashariki (Orientalists), ili kuushambulia Uislamu na watu
wake.
Msomaji
wa vitabu vya Kishia (Ithnaasheri) ataona kuwa wanafiki ndio waliokuwa wengi
miongoni mwa Masahaba (Radhiya Llahu anhum), bali wao ndio walioukamata uongozi
wa Waislamu mara baada ya kufa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam), (na hii ni itikadi ya Kishia), na wao (Mashia) ndio wanaosema kuwa wanafiki
ndio walioshika hatamu mara baada ya kufa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) na wakauendea kinyume Uislam pamoja na Waislam.
Sasa
ikiwa kweli hao wanaowaita kuwa ni wanafiki walio wengi walioshika hatamu za
Uislamu lengo lao lilikuwa kuwaendea kinyume Waislam, basi kwa nini
wasingemzunguka Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pamoja
na Masahaba wake wazuri (hao Masahaba watatu au sita tu) na kuwaua na
kuiangamiza Dola ya Kiislamu tokea mwanzo? Kwa nini wakangoja mpaka Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) afariki?
Lakini
anayechunguza hali ya mambo, ataona kinyume na madai hayo. Ataona kuwa;
Masahaba (Radhiya Llahu anhum) wanowaita kuwa ni wanafiki, waliposhika hatamu,
Uislam ulishinda na kusonga mbele na kuenea katika kila pembe ya dunia. Na
bendera yake ilinyanyuka juu na kuziangusha bendera za kikafiri Mashariki ya
ardhi na Magharibi yake.
Tizameni
ndugu zangu vipi hoja zao zinavyogongana na uhakika wa mambo na uhakika wa
kiakili pamoja na uhakika wa historia.
Hapo
Madina, wale wanafiki wa kweli walikuwa ni watu wachache waliokuwa wakijulikana
na kila mtu kutokana na wasfu wao, maana Qurani mara nyingi ilikuwa ikizungumza
juu yao, na ushahidi wa kauli hii unapatikana katika hadithi ya Kaab bin Malik
(Radhiya Llahu anhu), ambaye ni mmoja katika wale Masahaba watatu (Radhiya
Llahu anhum) waliotakiwa wasubiri baada ya kutohudhuria kwao vita vya Tabuk,
pale Kaab bin Malik aliposema
“Nikawa kila ninapotoka nje ya nyumba yangu na kuonana na watu,
ninahuzunika
(Bukhari
juzuu ya 4 uk.1604 nayo ni sehemu ya hadithi ndefu ya Kaab bin Malik (Radhiya
Llahu anhu)).
Zifuatazo
ni baadhi tu ya sifa za wanafiki
Wanafiki
ni watu;
‘Wanaoeneza
ufisadi ardhini, kuifanyia istihzai dini, kuwafanyia istihzai wacha Mungu,
wavukaji mipaka katika maasia na kuwa wao wanaununua upotofu (upotevu) kwa
uongofu, viziwi, mabubu na vipofu (sumun bukmun umyun), waliotahayari, wavivu
katika kufanya ibada, hugeuka geuka, mara Waislamu mara makafiri, kama
alivyosema Mwenyezi Mungu:
“Wanayumba yumba baina ya huku (kwa Waislam) na huko (kwa makafiri).
Huku hawako wala huko hawako)”.
Annisaa-143
Wanafiki
wanapenda kuapa uongo kwa jina la Mwenyezi Mungu, hawaijui dini na kwamba wao
ni waoga.
Na
katika sifa za wanafiki pia ni;
‘Kuwa
hawamwamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Akhera na kwamba Waislam wanapopata
kheri yoyote au mafanikio wao wanahuzunika, na huwa wanafurahi pale Waislamu
wanapopata tabu na mitihani na kwamba kazi yao ni kuwavizia Waislam, na pia
huchukizwa katika kutoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu na hufurahi
wanaporudi nyuma na kumuacha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) peke yake aende vitani na kwamba wao ni watu waovu kabisa mbele ya
Mwenyezi Mungu na wameingia katika dini yake ili wajikinge wasiambiwe kuwa wao
ni makafiri na wanapenda kuwadhuru Waislam na kuwafarikisha na hupindukia
mipaka pale wanapohasimiana na kwamba wanaiahirisha sala mpaka nyakati zake za
mwisho na hawahudhurii Sala za jamaa na kwamba wanaionea uzito kabisa Sala ya
Alfajiri na ya Ishaa’.
Hizi
ni baadhi tu ya sifa za Wanafiki alizozitaja Mwenyezi Mungu katika Qurani tukufu,
na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) katika mafundisho
yake.
Ndugu
zangu Waislam, hivyo kweli hizi ni sifa wanazostahiki kupewa Masahaba wa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)?
Bila
shaka Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ni
watu walio mbali kabisa na sifa
“Nyinyi ndio umma bora kuliko umma zote zilizodhihirishiwa watu
(ulimwenguni) mnaamrisha yaliyo mema na mnakataza yaliyo maovu, na mnamwamini
Mwenyezi Mungu”.
Aali
Imran- 110
Na
akasema juu
“Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mwenyezi Mungu anakutoshelezea wewe na
wale walokufuata katika hao walioamini”.
Al
Anfal-64
Na
akasema juu
“Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu . Na walio pamoja naye ni wenye
nyoyo thabiti mbele ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao. Utawaona
wakiinama kwa kurukuu na kusujudu (pamoja), wakitafuta fadhila za Mwenyezi
Mungu na radhi (yake).”
Al
Fat-h- 29
Na
akasema:
“Na wale walioamini wakahama (kuja Madina) na wakaipigania dini ya
Mwenyezi Mungu (Nao ni Muhajir); na wale waliowapa (Muhajir) mahala pa kukaa na
wakainusuru dini (ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake).(nao ni Ansar) Hao ndio
Waislam wa kweli. Watapata msamaha (wa Mwenyezi Mungu) na kuruzukiwa kuzuri
(kabisa huko Akhera)”.
Al
Anfal – 74.
Kwa
hivyo wale Walioamini, Wakahama, Wakapigana jihadi ni Wahajir (Masahaba wa
Makka). Na wale Waliowapa mahala pa kukaa na Kuwanusuru nao ni Maanswar (Masahaba
wa Madina), Mwenyezi Mungu amewapa wote hao sifa kuwa ni Waislam wa kweli. Kisha aje mtu atuambie kuwa Masahaba na wanafik ni kitu
kimoja!!!?
Katika
mambo yanayokubaliwa na Maulamaa wote ni kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) aliwajulisha baadhi ya Masahaba (Radhiya Llahu anhum) majina ya baadhi ya wanafiki, na haya
yanakubaliwa na maulamaa wa Kishia pia kama yanavyokubaliwa na Masunni.
Na
katika mambo wanayokubaliana pia ni kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) amezungumza juu ya kuridhika kwake na Masahaba wake (Radhiya
Llahu anhum) na akasema:
"Msiwatukane masahaba wangu. Ninaapa kwa jina la Yule ambaye
nafsi yangu imo mikononi mwake, hata mmoja wenu akijitolea katika njia ya
MwenyeziMungu kugawa dhahabu ukubwa wake mfano wa jabali Uhud, basi hatofikia
gao lao wala hata nusu ya gao lao".
Bukhari
na Muslim
Kuwatia
Masahaba na wanafiki katika kundi moja ni katika matusi makubwa kabisa.
Na
Mtume wa Mwenyezi Mungu(Swalla Llahu alayhi wa sallam) pia akasema:
“Atakayewatukana Masahaba wangu, basi itampata laana ya Mwenyezi
Mungu na (laana ya) Malaika na (laana ya) watu wote”.
((Attabariy,
katika kitabu chake kiitwacho ‘Al Kabeer’, Abi Naeem katika ‘Al Hiliya’ na Abi
Asim, na hadithi hii pia inapatikana katika ‘Silsila za hadithi sahihi
kilichoandikwa na Sheikh Al Albani)).
Na
akasema:
“Nihifadhieni Masahaba wangu, kisha wale waliowafuatilia kisha wale
waliofuatilia”.
Imam
Ahmad, Ibni Majah, na Al Haakim.
Sifa
hizi lazima wapewe Masahaba wote kwa uadilifu na haiwezekani kuwaingiza
wanafiki katika sifa hizi, wanafiki ambao Mwenyezi Mungu anasema juu
“Bila shaka wanafiki watakuwa katika tabaka za chini kabisa katika
moto”.
An
Nisaa- 145
Kisha
tunauliza:
Ikiwa
tutafuata ugawaji wao (Mashia) wa Masahaba wa makundi matatu na kuyahesabu yale
makundi mawili, la pili na la tatu kuwa ni hao waliomfuata Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kwa maslahi yao au kwa kuogopa na kwamba
walikuwa na kigeu geu wakarudi nyuma baada ya kufa kwake (Swalla Llahu alayhi
wa sallam), pamoja na kuwa wanafiki.
Kwa
vile wao ndio waliokuwa wengi
Ikiwa
wengi wa Masahaba walikuwa ni watu waliokuwa na kigeugeu na unafiki, hii
italeta maana kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
hakuweza kuwalea na kuwafundishsa vizuri Masahaba wake (Radhiya Llahu anhum) wakaijuwa haki, na kwamba yeye ni mlezi
asiyefanikiwa, aliyefeli katika kazi yake ya kuwalea Masahaba (Radhiya Llahu
anhum).
Baada
ya kuishi nao muda mrefu wote huo amefanikiwa kuwalea na kuwafundisha Mashaba
watatu tu au wasiozidi saba?
Sisi
tunakanusha kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alifikia
daraja hii ya kuangushwa na kuwa alishindwa kuwalea Masahaba wake (Radhiya
Llahu anhum).
Nawauliza
ndugu zangu Waislam:
‘Je!
Huku si kumshutumu hata Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa Sallam)?’
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akifanya nini miaka
yote aliyoishi na Masahaba wake (Radhiya Llahu anhum)?
Subhanallah! Hivyo kweli Mtume wa Mwenyezi Mungu
huyu mtukufu ambaye ni kipenzi cha Mola wake na mbora wa viumbe vyote (Swalla
Llahu alayhi wa sallam), aliyelea vizazi vitukufu, na Mwenyezi Mungu
akamfungulia dunia yote akaweza kuwaokoa watu kutoka katika kuwaabudu viumbe na
kuwafanya wamuabudu Mungu wa viumbe; akawatoa katika dini za dhulma na kuwatia katika
Uadilifu wa Uislam, na akaweza kuwatoa katika viza vya dini za kijahilia na
kuwaingia katika nuru ya Uislam, na watu wakaingia makundi kwa makundi katika
dini hii kutoka katika kila pembe ya dunia mpaka wanavyuoni wa Kiyahudi na
Manasara waliukubali ukweli huu.
Leo na baada ya kupita karne kumi
na tano, waje wajukuu wa Abdillahi bin Saba-a - Myahudi, na kutustua kuwa eti
Masahaba walikuwa wanafiki na kwamba walirudi nyuma?
Kila anayesoma na kuidurusu sira (historia) ya Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), anaelewa kwamba wakati
Waislam walipokuwa Makka hapakuwa na unafiki, na hii ni kwa ajili ya adhabu
kali walizokuwa wakipata wale waliosilimu, na kwamba unafiki ulianza kujitokeza
baada ya Waislam kuhamia Madina na baada ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) kupata nguvu, na dini ya Mwenyezi Mungu kuanza kutambulika
kila mahala.
Na inaeleweka pia kwa kila mwenye kudurusu sira
(historia) ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kuwa
Abubakar, Umar na Uthman na wengineo ni miongoni mwa Masahaba (Radhiya Llahu
anhum) walioingia katika dini ya
Mwenyezi Mungu tokea siku za mwanzo, wakapata tabu na shida kama walivyopata
wenzao, na hii ni dalili wazi kabisa kuwa walikuwa mbali kabisa na unafiki.
Mwenyezi Mungu amewafedhehesha wanafiki kwa
kuwateremshia Suratul Munafiqun na At Tawba; akaelezea ndani sura hizo juu ya hali zao na vitimbi
vyao; na akatuelezea yale yaliyofichika nyoyoni mwao katika kuwachukia Waislam,
na hii ndiyo maana Surat at Tawba ikaitwa 'Sura ya Kufedhehesha'. Katika
sura hiyo Mwenyezi Mungu alitaja sifa za Masahaba (Radhiya Llahu anhum) na akatujulisha kuridhika kwake nao. Na huu ni
ushahidi utokao Kwake Subhanahu wa Taala.
Ama Suratul Munafiqun, hii imeteremshwa kwa
ajili ya kutujulisha juu ya mkubwa wa wanafiki na kiongozi wao aitwae Abdillahi
bin Ubay bin Salool na wenzake.
Anasema Zayd bin Al Arqam (Radhiya Llahu anhu):
"Nilikuwa vitani, nikamsikia
Abdillahi bin Ubay akisema:
“Msitoe mali kuwasaidia waliokuwa na Mtume
wa Mwenyezi Mungu mpaka watakapomwondokea pale alipo, na tutakaporudi Madina
yule mtukufu (akimaanisha yeye Abdillahi bin Ubay ‘mkuu wa wanafiki’) atamtoa
(katika mji wa Madina) yule aliyedhalilika (akimaanisha Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swalla Llahu alayhi wa sallam)”.
Nikamhadithia hayo niliyoyasikia Ami
yangu (au Umar) naye akamhadithia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam): Akaniita na mimi nikamhadithia. Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamtuma mtu amuite Abdillahi bin Ubay pamoja
na wenzake, wakaapa na kukanusha yale waliyosema, na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) hakunisadiki na akamsadiki yeye. Nikaona dhiki sijapata
kuona mfano wake. Nikakaa nyumbani kwangu, lakini haujapita muda Mwenyezi Mungu
akateremsha Suratul Munafiqun (Idhaa jaaa-aka l Munafiqun), Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamtuma mtu aniite,
akanisomea (Sura hiyo) kisha akaniambia:
“Mwenyezi Mungu amesadikisha maneno yako ewe Zeyd”.
Bukhari.
Tafsiri hii pia inapatikana katika kitabu cha
tafsiri cha Mashia kiitwacho ‘Maj maa l bayan fiy tafsiyri l Quran’,
kilichoandikwa na Imam Al Tubrusy ambaye ni miongoni mwa maulamaa wakubwa wa
Kishia. Na katika kitabu hicho, ameelezea sababu ya kuteremshwa Suratul
Munafiqun kuwa ni juu ya Abdillahi bin Ubay ‘mnafiki’ na wenzake …..
(Maj
maa l bayan fiy tafsiyr l Qur an ukurasa 85)
Kisha
Mwanachuoni huyu wa Kishia akazitaja riwaya zile zile alizozielezea Imam
Bukhari zinazothibitisha hoja hiyo.
Inajulikana
wazi kuwa Abdillahi bin Ubay pamoja na wafuasi wake walikuwa wakijulikana wazi
wazi na Masahaba wote (Radhiya Llahu anhum) kuwa ni wanafiki, na mtu yeyote anaposoma Surat
at Tawba ataona kuwa sura hiyo imeelezea juu ya vituko mbali mbali
walivyokuwa wakivifanya wanafiki hao kiasi ambacho ilikuwa wazi kabisa mbele ya
kila mtu kuwa wao ndio waliokusudiwa.
Kwa
mfano katika kuanzia aya ya 44 hadi 49 ya sura hiyo Mwenyezi Mungu anasema:
“Hawatakuomba ruhusa wale wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya
Mwisho, wasende kupigana Jihadi kwa
Wasio muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na nyoyo zao zikatia
shaka, hao tu ndio wanao kutaka ruhusa. Basi hao wanataradadi katika shaka zao.
Na ingeli kuwa kweli walitaka kutoka bila ya shaka wangeli jiandalia
maandalio, lakini Mwenyezi Mungu kachukia kutoka kwao, na kwa hivyo akawazuia
na ikasemwa: Kaeni pamoja na wanao kaa!
Lau wangeli toka nanyi wasingeli kuzidishieni ila mchafuko, na wange
tanga tanga kati yenu kukutilieni fitna. Na miongoni mwenu wapo wanao
wasikiliza. Na Mwenyezi Mungu anawajua madhaalimu.
Tangu zamani walitaka kukutilieni fitna, na wakakupindulia mambo juu
chini, mpaka ikaja Haki na ikadhihirika amri ya Mwenyezi Mungu, na wao
wamechukia”.
Na miongoni mwao wapo wanao sema: ‘Niruhusu wala usinitie katika
fitina’. Kwa yakini wao hivyo wamekwisha tumbukia katika fitina. Na hakika
Jahannamu imewazunguka.”
Inaeleweka
na kila mtu kuwa Masahaba wote walitoka na kwenda vitani siku hiyo ya vita vya
Tabuk (vita ambavyo aya hizo zinazungumzia juu yake), na waliobaki nyuma ni Abi
Dhar na Abu Khaythamah (Radhiya Llahu anhum), kisha nao pia wakenda kujiunga na
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pamoja na wenzao, na
waliwawahi njiani kabla vita kuanza.
Na
ineleweka pia kuwa miongoni mwa waliobaki nyuma ni Kaab bin Malik, Hilal bin
Umayya na Mirara bin Rabia (Radhiya Llahu anhum), nao ni katika watu wa Madina
na inajulikana na kila mtu kuwa Mwenyezi Mungu aliwasamehe Masahaba hao
Ama
wengine waliobaki Madina na wasende vitani walikuwa wakijulikana kuwa ni katika
wale wanafiki waliomuendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) na kuomba udhuru wa uongo, au wale waliokuwa na udhuru wa kutopigana
Jihad kwa ajili ya ugonjwa au udhuru mwingine unaokubalika.
Na
haya tulieleza hapo mwanzo katika kisa cha Kaab (Radhiya Llahu anhu) kuwa katika waliobaki pale Madina wasende
vitani hakuwa akimuona aliye kufu yake isipokuwa wenye udhuru au wale waliokuwa
wakijulikana kuwa ni Wanafiki.
Na
hii ni dalili kuwa wanafiki walikuwa wakijulikana na Masahaba.
Ama
katika kauli yake Subahanahu wa Taala katika Sura hiyo hiyo ya At Tawba aya ya
64, Mwenyezi Mungu anasema:
“Wanafiki wanaogopa isije teremshwa Sura itakayo watajia yaliyomo
katika nyoyo zao. Sema: ‘Fanyeni mzaha! Hakika Mwenyezi Mungu atayatoa nje hayo
mnayo yaogopa.”
Anasema
Ibni Kathiyr katika kuifasiri aya hii:
“Kasema Mujahid: ‘Walikuwa wakizungumza baina
Na
hii inasadikisha kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:
“Na wafikapo kwako wanakuamkia kwa (maamkio) ambayo siyo maamkio
aliyoamrisha Mwenyezi Mungu uamkiwe kwa maamkio hayo, na husema katika nyoyo
zao; ‘Mbona Mwenyezi Mungu hatuadhibu kwa haya tunayoyasema?’ Basi Moto wa
jahannam utawatosha kuwatia adhabu, watauingia, napo ni mahali pabaya
Al
Mujadalah - 8
Na
maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu atamteremshia Mtume wake (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) yale yatakayowafedhehesha na kubainisha juu yenu.
Na
mfano wake ni mfano wa kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:
“Je! Wale wenye maradhi nyoyoni mwao wanadhani kwamba Mwenyezi Mungu
hataidhihirisha bughudha
Na
Muhammad
– 29 – 30
Na kwa sababu hii Qatada amesema:
“Sura hii ilikuwa ikiitwa kashfa iliyowafedhehesha Wanafiki.”
(Tafsiri
ya Ibni Kathiry)
Na
hii ni kwa sababu Mwenyezi Mungu amewafedhehesha ili watu wawajue, wakati kabla
ya hapo hapana aliyekuwa akiwajua, na walikuwa wakifanya vitimbi vyao kwa siri.
Kisha
baada ya yote hayo aje mtu awatie moja wao katika fungu la Masahaba watukufu
(Radhiya Llahu anhum).
Ama
katika kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:
“Watakuapieni kwa Mwenyezi Mungu mtakapo rudi kwao ili muwaachilie
mbali. Basi waachilieni mbali. Hakika hao ni najsi, na makaazi
Wanakuapieni ili muwe radhi nao. Basi
hata mkiwa radhi nao nyiye, Mwenyezi Mungu hawi radhi na watu wapotofu”.
Al Tawba – 95-96
Aya hizi ziliteremshwa juu ya wale wanafiki
waliobaki nyuma wasiende kupigana katika vita vya Tabuk kisha wakaja kutoa
udhuru wa uongo kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na
idadi yao ilikuwa wanaume wapatao themanini na kidogo hivi, na hakuwa miongoni
mwao hata mmoja katika Sahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam).
Anayetaka maelezo zaidi na asome kisa CHA WALE
WATATU WALIONGOJESHWA, kilichomo katika Sahihul Bukhari, kisa kinachoelezea
sababu za kuteremshwa aya hizi.
Ama kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu katika sura
hiyo hiyo ya Al Tawba kuanzia aya ya 107 hadi 108 isemayo:
“Na wapo walio jenga msikiti kwa ajili
ya madhara na ukafiri na kuwafarikisha Waumini, na pa kuvizia kwa walio mpiga
vita Mwenyezi Mungu na Mtume wake hapo kabla. Na bila ya shaka wataapa kwamba:
Hatukukusudia ila wema tu. Na Mwenyezi Mungu anashuhudia kuwa wao ni waongo.
Usisimame kwenye msikiti huo kabisa. Msikiti ulio jengwa juu
ya msingi wa uchaMungu tangu siku ya mwanzo unastahiki zaidi wewe usimame ndani
yake. Humo wamo watu wanao penda kujitakasa. Na Mwenyezi Mungu anawapenda wanao
jitakasa”.
At Tawba -107-108
Aya hizi pia ni miongoni mwa aya
zilizowafedhehesha wanafiki walipojenga msikiti kwa kusudi la kuwatakia Waislam
madhara, na msikiti huo ulikuwa wa Abu Amer aliyekuwa mtu asi. Alijenga msikiti
huo kwa kusudi la kuwapiga vita Waislam, kisha akamtaka Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) aswali katika msikiti huo, lakini Jibril (Alayhi
Ssalaam) akamteremshia Wahyi Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) kutoka kwa Mola wake kuwa asende kusali mahali hapo, na Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akawaamrisha baadhi ya Masahaba
(Radhiya Llahu anhu) kuubomoa msikiti huo na wasali katika msikiti uliojengwa
juu ya msingi wa uchaMungu (Masjid Qubaa).
Bila shaka wanafiki hao waliotaka kuudhuru Uislam
walikuwa wakijulikana na Masahaba (Radhiya Llahu anhu), lakini Mashia wanasema
kuwa eti Masahaba wengi walikuwa wanafiki.
Mtu yeyote akitumia akili yake kidogo tu, ataona
kuwa ule msikiti aliosali ndani yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) ‘Masjid Qubaa’, ndio uliojengwa na Masahaba (Radhiya
Llahu anhum), na ule ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) aliamrisha ubomolewe ni msikiti wa wanafiki.
Sasa ikiwa Masahaba walio wengi ni wanafiki
(waliomo katika kundi la kwanza na la pili – kutokana na ugawaji wao Mashia),
na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alisali katika
msikiti wa Masahaba wanafiki (kama wasemavyo wao). Je! Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) aliamrisha ubomolewe ule wa Masahaba ambao ni wachache,
kisha akasali katika msikiti wa wanafiki walio wengi?
Wakati katika sura hiyo hiyo Mwenyezi Mungu
anatuelezea juu ya kuridhika kwake juu ya Sahaba waliotangulia wa kwanza katika
Wahajir (watu wa Makka waliohamia Madina) na Ansar (Watu wa Madina waliowapokea
Wahajir wa Makka) na akawatayarishia Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu
humo milele.
Mwenyezi Mungu anasema:
“Na wale walio tangulia, wa kwanza,
katika Wahajiri na Ansari, na walio wafuata kwa wema, Mwenyezi Mungu ameridhika
nao, na wao wameridhika naye; na amewaandalia Bustani zipitazo mito kati yake,
wadumu humo milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa.”
At Tawba 100
Sasa tizameni ndugu zangu vipi Mwenyezi Mungu
anatuelezea juu ya kuridhika kwake na Masahaba katika Muhajir na Ansar na vipi
wenzetu wanatuambia kuwa wao ni wanafiki na kwamba walirudi nyuma na kukufuru,
akiwemo mbora wa Masahaba wote Abubakar Al Siddique (Radhiya Llahu anhu).
Ama Masunni wanaridhika na wote Mwenyezi Mungu
aloridhika nao, na wanawafanyia uadui wale maadui wa Mwenyezi Mungu tu, na
wanafuata yale waliyofundishwa na Mwenyezi Mungu pamoja na mafundisho ya Mtume
wa Mwenyezi Mungu wake (Swalla Llahu alayhi wa sallam), na wala hawavumbui
mambo katika vichwa vyao.
Na katika kauli yake Mwenyezi Mungu pale aliposema:
“Mwenyezi Mungu amekwisha pokea toba ya Nabii na Wahajiri na Ansari
walio mfuata katika saa ya dhiki, pale baada ya kukaribia nyoyo za baadhi
Attawba 117
Katika aya hii na aya iliyotangulia nambari 100
inaonyesha wazi namna gani Mwenyezi Mungu alivyoridhika nao na anavyowasifia
Muhajir na Ansar waliomfuata katika ile saa ya dhiki (vita vya Tabuk), na pia Mwenyezi
Mungu anatujulisha juu ya usafi wa yale yaliyofichika nyoyoni mwao.
Huu ni ushahidi utokao kwa Mwenyezi Mungu asiye
mshirika.
Ksha Mwenyezi Mungu anatujulisha juu ya kuridhika
kwake na wale watatu walioambiwa wangoje ambao ni miongoni mwa Masahaba
(Radhiya Llahu anhum) kinyume na wale
wanafiki ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
alikubali udhuru wao bila kujua undani wao, lakini hatimae Mwenyezi Mungu
akawafedhehesha. Na hii ni dalili kubwa kabisa kuwa ipo tofauti baina ya
Masahaba JUU YA KUKOSEA KWAO BAADHI YA WAKATI na WANAFIKI aliowafedhehesha
Mwenyezi Mungu katika kitabu chake kitukufu.
Hapa tutaleta dalili kutoka kwa Wanavyuoni wakubwa
wa Kishia (Ithnaasheri) ambao Mwenyezi Mungu atakayekifanya kila kitu kiseme siku
ya Kiama, aliwafanya wanavyuoni hao kuutamka ukweli wakitaka wasitake. Na
wameyasema haya katika vitabu vyao vinavyoaminika na kutambulika.
Anasema Abu Nasr Muhammad bin Masaud,
anayejulikana kwa jina la ‘Al Iyashi’ katika tafsiri yake juu ya kauli
ya Mwenyezi Mungu isemayo:
“Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda
wanaotubu na huwapenda wanaojitakasa’
Al Baqarah – 222
Mwanachuoni huyu wa Kishia ametamka kauli
inayokanusha wazi wazi kuwa Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) walikuwa wanafiki.
Na kauli hii imetamkwa na Muhammad al Baqer
(Radhiya Llahu anhu) ambae ni Imam wa
tano katika Maimam waliokingwa kwa Mashia.
Anasema Al Iyashi:
‘Kutoka kwa Salam anasema: ‘Nilikuwa
kwa Abu Jaafar (AS) akaingia Hamran bin Ayun akamuuliza baadhi ya mambo na
alipotaka kuondoka, Ayun akamuuliza Abu Jaafar:
'Tuelezee Mwenyezi Mungu akupe umri
mrefu, sisi tunapokuwa nawe nyoyo zetu hulainika na nafsi zenu zinakuwa mbali
na dunia, tunadharau kila kilichomo mikononi mwa watu katika hizi mali, lakini tunapotoka
na kuchanganyika na watu na kufanya biashara tunaanza kuipenda tena dunia.’
Anasema, Abu Jaafar akasema:
"Nyoyo zinashindwa na mambo baadhi
ya wakati, na wakati mwengine mambo yanakuwa mepesi’, kisha Abu Jaafar (AS)
akaendela kusema: ‘Kwa hakika Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu walisema:
‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu,
tunajiogopea unafiki’ akasema: “Kwa nini mnaogopa?”
Wakasema:
“Sisi tunapokuwa nawe ukatukumbusha,
huwa na uoga na nyoyo zetu zinalainika tukaisahau dunia, hatuitamani, hata
hufikia kuwa tunaiona akhera, Pepo na Moto mbele yetu. Lakini mara tunapotoka
kwako na kuingia majumbani mwetu na kuanza kuwabusu watoto wetu na kuonana na
wake zetu na mali zetu, tunaanza kubadilika hali zetu kinyume na pale
tunapokuwa nawe, kama kwamba hatukuwa na kitu. Je! Hutuogopei unafiki?"
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) akawaambia:
“Kabisa sikuogopeeni hilo, kwani hizi
ni katika hatua za shetani akijaribu kukupendezesheni dunia, Wallahi lau kama
mungebaki katika hali ile mliyokuwa nayo pale mlipokuwa kwangu, basi Malaika
wangekusalimieni barabarani na mungekuwa mnatembea juu ya maji, na kama
mungelikuwa hamtendi madhambi na kumuomba Maghfira Mwenyezi Mungu, basi
Mwenyezi Mungu angeliumba viumbe ili wafanye madhambi kisha wamuombe maghfira
ili apate kuwaghufiria, kwani Muislam siku zote yupo katika mtihani, kwani
hukuisikia kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo;
‘Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda
wanaotubu?’ na isemayo;
“Na ili muombe msamaha kwa Mola wenu
kisha mtubie (mrejee)?"
Hud
3
(Tafsir
Al Iyashi Juz1 uk.128)
Ama
Imam Al Hassan Al Askari, ambaye ni Imam wao wa kumi na moja alipokuwa
akiwafahamisha watu daraja ya Masahaba (Radhiya Llahu anhum) mbele ya Mwenyezi Mungu alisema:
‘Miongoni wa masuala aliyouliza Musa (Alayhi Ssalaam) kumuuliza
Mwenyezi Mungu alisema:
‘Je! Wapo Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu yeyote walio bora
kuliko Masahaba wangu?'
Mwenyezi Mungu akamjibu:
“Ewe Musa kwani hujui kuwa ubora wa Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi
Mungu Muhammad juu ya Masahaba wa Mitume yote ni sawa na ubora wa Aali ya
Muhammad juu ya Aali za Mitume yote, na mfano wa ubora wa Muhammad juu Mitume
yote?”
Kwa
kumalizia tutizame nini anasema Imam Aly bin Abu Talib (Radhiya Llahu anhu) juu
ya Masahaba hawa watukufu.
Imam
Aly ni Imam wao wa mwanzo na kwetu sisi ni Khalifa wa nne aliyeongoka.
Tutanukuu kauli yake kutoka katika kitabu kitukufu
“Nimewaona Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu alayhi
wa sallam), na sioni yeyote kati yenu aliyeshabihiana nao. Walikuwa wakati wa
asubuhi utawaona nywele zimetimka kwa sababu ya kusimama kwao usiku kucha
wakisujudu na kusimama (kwa kusali), wanaomba huku wakisujudu, na wanapolala na
wanapokumbuka akhera
Ama
Ibarahim Al Thaqafi ambaye ni katika maulamaa wakubwa wa Kishia, katika kitabu
chake kiitwacho ‘Al Ghaaraat’ Juzuu ya 1 Uk.177 akimnukuu Aly (Radhiya
Llahu anhu) anasema:
“Aliulizwa Aly: ‘Ewe Amiri wa Waislam, tuelezee juu ya Sahibu zako.’
Akauliza:
“Juu ya sahibu zangu wepi?”
Wakamwambia:
“Juu ya Sahaba wa Muhammad (Swalla Llahu alayhi wa sallam).”
Akasema:
“Masahaba wa Muhammad wote
ni sahibu zangu”.
Hizi ni kauli za Imam Ali (Radhiya Llahu anhu) juu
ya Masahaba ambao wao wanadai kuwa wengi wao au karibu wote ni Wanafiki.
Tunamuomba msomaji arudie marejeo yote tuliyonukuu
ushahidi wetu huu ili imbainikie wapi ukweli upo, na ili aelewe uovu wa msimamo
wa ndugu zetu hawa juu ya Masahaba wakiwemo Makhalifa watatu wa mwanzo wa Waislam.
Mlango wa pili
Atakayesoma kitabu hiki au makala haya ataona kuwa
ushahidi wote unaegemezwa kutoka katika yale yaliyokubaliwa na pande zote mbili
kutoka katika Qurani na Sunnah na ushahidi mwengine ni wa kutumia akili na
mantiki.
Kwanza
Kisa
cha Hudaybiya kilikuwa
Katika
mwaka wa sita baada ya Hijra, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) alitoka pamoja na Masahaba wapatao elfu moja na mia nne kuelekea Makka,
wakiwa na nia ya kufanya Umra, na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) aliwataka Masahaba (Radhiya Llahu an'hum) waziache panga zao ndani
ya ala zake. (yaani wasitoe panga zao nje)
Wakavaa
nguo zao za Ihram katika Miyqaat, hapo Dhul Hulayfa (Abyaar Aly), kisha
wakaondoka pamoja na mbuzi wao, ili Maqureshi wajue kuwa wamekuja kwa nia ya
kufanya Umra na si kivita. Lakini Maqureshi wakafanya kiburi kwa kuogopa watu
wakisikia kuwa Muhammad ameingia Makka bila bila ya kufanyiwa tabu yoyote, na
akafanya Umra, watu watawadharau na kuona kwamba labda wameshindwa kumzuwia.
Wakatuma
ujumbe ulioongozwa na Suhail bin Amru bin Wud Al Amry aliyemtaka Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pamoja na alokuja nao warudi
Madina mwaka huu bila ya kufanya Umra na kamba mwaka ujao watamruhusu aje
kufanya Umra kwa muda wa siku tatu.
Wakamwekea
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) masharti mazito
aliyoyakubali.
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliyakubali masharti yao kwa
ajili ya kutaka sulhu - kama alivyofunuliwa na Mola wake, lakini baadhi ya
Masahaba (Radhiya Llah anhum) waliyakataa masharti hayo, na Umar (Radhiya Llahu
anhu) alimwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swalla Llahu alayhi wa sallam) na kumuuliza:
“Kwani
wewe si Mtume wa Mwenyezi Mungu wa kweli?”
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuambia:
“Ndiyo.”
Umar
(Radhiya Llahu anhu) akamuuliza:
“Sisi
si tuko katika haki na adui zetu wako katika batil?”
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuambia:
“Ndiyo.”
Umar (Radhiya Llahu anhu) akasema:
“Kwa
nini basi tunakubali dini yetu idhalilike?”
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuambia:
“Mimi
ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na sitomuasi, na Yeye ndiye mwenye kuninusuru”.
Umar (Radhiya Llahu anhu) akamuuliza tena:
“Si ulituambia kuwa tutakwenda (Makka) na tutatufu
penye nyumba?”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) akamuambia:
“Ndiyo, lakini nilikuambia kuwa tutakwenda mwaka
huu?”
Umar (Radhiya Llahu anhu) akasema:
“La, sivyo.”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) akasema:
“Hakika
utakwenda na utatufu penye nyumba.”.
Kisha
Umar (Radhiya Llahu anhu) akamuendea
Abubakar (Radhiya Llahu anhu) na kumuambia:
“Abubakar,
kwani yeye si Mtume wa Mwenyezi Mungu kweli?”
Abubakar
(Radhiya Llahu an'hu) akamuambia:
“Ndiyo.”
Kisha
akamuuliza msuali yale yale aliyomuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) na Abubakar (Radhiya Llahu anhu) akamjibu majibu yale yale
aliyojibiwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), kisha
akamuambia:
“Ewe
mwanamume, huyu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na hatomuasi, kwa hivyo shikamana
naye vizuri."
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipomaliza kuandikiana
mkataba wa Mapatano, akawaambia Masahaba wake:
“Inukeni
mchinje kisha nyoweni nywele.”
Alisema
hivyo mara tatu na hapana hata Sahaba mmoja aliyeinuka na kufanya
Masahaba
nao (Radhiya Llahu anhum) walipoona vile, wote wakainuka na kuanza kuchinja
wanyama wao na kunyoana nywele.
Hiki
ni kisa cha Sulhu ya Hudaybiya ambacho Mashia na Masunni wote wanakubaliana
kuwa hivi ndivyo ilivyokuwa na haya ndiyo yaliyotokea.
Na
hivi ndivyo kilivyoelezwa na maulamaa wa historia kama vile Attabary na Ibni l
Athiyr na Ibni Saad na Maulamaa wa hadithi wengineo kama vile Bukhari na
Muslim.
Katika
kisa hiki ndugu zetu Mashia wanawatuhumu Mashaba kuwa walipinga amri ya Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) wakakataa kufuata amri pale alipowaambia
wachinje na wanyoe na kwamba kuchelewa kufuata amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) ni dhambi kubwa
“Naapa kwa (haki ya) Mola wako. Wao hawawi wenye kuamini (kweli
kweli) mpaka wakufanye (wewe ndiye) hakim (mwamuzi) kati ya yale
wanayokhitilafiana, kisha wasione uzito nyoyoni mwao juu ya hukumu uliyoitoa,
na wanyenyekee kabisa”.
Annisaa
65
Inaelekea
ndugu zetu wanasahau kuwa katika kisa hiki pana sehemu muhimu
Na
sehemu hiyo ni pale Urwa bin Masaood (aliyekuwa miongoni mwa washirikina),
alipotamka kuwaambia Maqureshi:
"Huyu Muhammad, (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amekupeni
fikra nzuri, bora muikubali na muniache mimi nimuendee."
Wakamuambia;
‘Muendee’. Akamuendea na akawa anamsemesha Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) akamuambia maneno yale yale aliyomuambia hapo mwanzo.
Urwa,
baada ya kuyasikia hayo akasema:
‘Ewe Muhammad unaonaje ikiwa nitawamaliza watu wako wote,
(niwauwe), Kwa sababu mimi sioni nyuso, bali naona makundi ya watu waliokuwa
tayari kukukimbia na kukuacha peke yako.”
(huku akijaribu kutaka kuzichezea ndevu za Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam).
Abubakar
(Radhiya Llahu anhu) akasema:
“Nenda kabusu utupu wa (Mungu wako) Lata. Sisi tumkimbie na
kumuacha?”
Urwa akauliza:
“Nani huyu?”
Wakamjibu; “ Huyu ni Abubakar”
Akasema:
"Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi mwake,
Kisha
akaendelea kumsemesha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam),
na kila anapomsemesha hujaribu kuzishika ndevu za Mtume wa Mwenyezi Mungu na Al
Mughiyra bin Shuuba (Radhiya Llahu anhu) aliyekuwa amesimama mbele ya Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akiwa ameshika upanga wake na
ngao, humpiga mikono yake kwa mkono wa upanga na kumwambia:
“Ondoa mkono wako na uweke mbali na ndevu za Mtume wa Mwenyezi
Mungu wa Mwenyezi Mungu”.
Urwa akaunyanyua uso wake na kuuliza:
“Ni nani huyu?”
Akamjibu: “Mughiyra bin Shuuba.”
Akasema:
“Ah! Haini, mimi bado nakutafuta kwa ajili ya uhaini wako.”
Mughiyra
huyu, wakati alipokuwa kafiri alifuatana na kundi la watu akawaua na
kuwanyang’anya
Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:
“Ama Kusilimu kwake nimekukubali, lakini hiyo
Kisha
Urwa akawa anawatizama Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) machoni pao mmoja mmoja.
Kisa
akaondoka na kurudi kwa wenzake, akawaambia:
“Wallahi Muhammad huyu hata anapotema mate, basi Sahaba zake
wanayapokea kwa mikono
‘Watu wa aina gani hawa, Wallahi nishawahi kuwatembelea wafalme na
nishamtembelea Qaysar (mfalme wa Warumi) na Kisraa (mfalme wa Wafursi) na
Annajashi (mfalme wa Wahabeshi), Wallahi sikumuona hata mfalme mmoja
anayeheshimiwa kama anavyoheshimiwa Muhammad na Sahibu zake."
Hivyo
ndivyo Masahaba wanavyomuheshimu Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) akishuhudia mmoja katika washirikina.
Sehemu
hii wao hawaitaji, na hii ni kwa sababu wakiitaja basi ushahidi wao kuwa
Mashaba walikuwa waasi ungetoweka.
Masahaba
hawakumbishia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kwa nia
ya kumuasi pale walipochelewa kufuata amri ya kuchinja na kukata nywele, na
wala hapana dalili yoyote ile katika hadithi kuwa walikuwa na nia ya kwenda
kinyume na maamrisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam),
bali walifanya waliyofanya na kutamka waliyotamka kwa sababu ya kuionea wivu
dini yao na kuona uchungu kuwa makafiri wamekubaliwa masharti yao yote, na
wakaona kama vile mtu yeyote wa kawaida angeliona, kuwa masharti yaliyokuwemo
ndani ya mkataba huo kama kwamba Waislamu wamejidhalilisha. Na hivi ndivyo
ilivyokuwa katika dhahiri ya mkataba huo, na wao ni wanadamu wa kawaida, hawapokei
wahyi
Masahaba
wangelikuwa wamekwenda kinyume na maamrisho ya Mtume wao (Swalla Llahu alayhi
wa sallam), vipi basi baada ya tukio
"Kwa hakika Mwenyezi Mungu amewapa radhi Waislamu
walipofungamana nawe chini ya mti na alijua yaliyomo nyoyoni mwao. Basi
akateremsha utulivu juu
Al
Fath – 18
Vipi
Mwenyezi Mungu anayejua ya ghaibu na ya dhahiri angeridhika nao na kuwapa ushindi
wa katika zama za karibu,
Ili
ieleweke vizuri nitanukuu kisa hiki cha Sulhuya Hudaybiya
Katika
Sahih Muslim inaelezwa vizuri zaidi ni nani katika Masahaba waliokataa kufuata
amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam):-
Kutoka
kwa Al Bara -a bin Aazib (Radhiya Llahu anhu) anasema:
“Ilipombidi Mtume wa Mwenyezi Mungu(Swalla Llahu alayhi wa sallam)
kuandikiana mkataba wa Sulhu na watu wa Makka kwamba wataruhusiwa kuingia Makka
(mwaka ujao) na kubaki hapo siku tatu, na kwamba wasichukue silaha isipokuwa
panga na ala zao tu, na asiruhusiwe Muislam yeyote katika watu wa Makka kuondoka
nao na kwamba yeyote katika Waislam anayetaka kubaki Makka asizuiliwe. Akamuambia
Aly bin Abi Talib:
‘Andika masharti yaliyokubaliwa baina yetu; Bismillahi Rahmani Rahiym,
haya yaliyokubaliwa na Muhammad Mtume wa Mwenyezi Mungu ….”
Makafiri wakasema:
“Tungekuwa tunaamini kuwa wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu basi
tungelikufuata. (usiandike hivyo)
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
akamuamrisha Aly afute, lakini Aly akamjibu:
“La wallahi sitofuta”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamuambia:
“Nionyeshe mimi wapi ilipoandikwa.”
Akamuonyesha, akafuta na akaandika badala yake ‘Ibnu Abdullah’
badala ya ‘Rasulu Llah’, na akabaki hapo siku tatu.
Muslim
Ikiwa
tutatumia mantiki yao ya kulifanya kila tukio baina ya Sahaba (Radhiya Llahu
anhu) na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kuwa ni
kutotii amri yake na kwamba hii haijuzu na kwamba huu ni unafiki na uhaini,
basi hapa tungemlaumu Aly (Radhiya Llahu anhu) kwa sababu Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipomtaka afute akajibu:
“Wallahi sitofuta”.
Na
kwa njia hii tungefungua mlango kwa kila mtu kuanza kuwashambulia Masahaba
(Radhiya Llahu anhu) kuwa ni watu waliokuwa wakimuasi Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam).
Tuwaulize
ndugu zetu hapa;
‘Je
mtakubali kukifasiri kitendo hiki cha Aly (Radhiya Llahu anhu) kuwa ni kutotii
amri za Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)? Ikiwa
wataikubali hukmu hii basi itakuwa wamemhukumia Aly (Radhiya Llahu anhu) pia
kuwa ameshindwa kutii amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam), na kwa ajili hiyo itabidi wamtie katika kundi la Masahaba wenzake
wanaodai kuwa huwa hawatii amri za Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam).
Kisha
wanasema kuwa Umar (Radhiya Llahu anhu) hakusalimu amri na kutii pale
alipotakiwa kufanya hivyo na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam), bali alimwendea Abubakar (Radhiya Llahu anhu) na kumuuliza maswali
yale yale aliyokuwa akimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam):
“Kwani wewe si Mtume wa Mwenyezi Mungu kweli?”.
“Si ulituambia kuwa ………”. Kisha akaendelea kusema:
“Nikafanya mambo siku hiyo”.
Mashia
wanasema kuwa hawajui mambo gani hayo, kisha wanaendelea kuwatuhumu Masahaba
(Radhiya Llahu anhum) kuwa hawakufuata amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) pale walipoambiwa wachinje na kunyoa juu ya kuwakariria
mara tatu; wakati wanaelewa kwamba Mwenyezi Mungu ametuamrisha kufuata amri ya Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
Majibu:
Hapana
shaka yo yote kuwa Umar (Radhiya Llahu anhu) alisalimu amri na kuyakubali
maneno ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) isipokuwa tu
alionyesha kutoridhika kwake kwa yale yaliyokuwemo ndani ya mkataba ule kwa
sababu hakuelewa undani wake wakati ule, hasa tukikumbuka kuwa alimuuliza
maswali yale yale Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kisha
Abubakar (Radhiya Llahu anhu) baada ya kuwekewa masharti mazito sana yakiwemo
(Mtu ye yote wa Makka atakayesilimu asiruhusiwe kukimbia na kuwafuata
watakaporudi Madina).
Kwa sababu hadithi inasema hivi:
“Waislamu walisema Subhanallah, vipi
arudishwe kwa washirikina yule aliyesilimu na kukimbilia kwetu?”
Hapo ndipo alipotokea Aba Jundul bin
Suheil bin Amr akiwa amefungwa minyororo kwa sababu amekimbia kutoka Makka, akajitupa
mbele ya Waislamu na kuwaomba wamchukuwe Madina, mbali na mateso ya Makafiri.
Suheil aliyekuwa kiongozi wa washirikina
na pia ni baba yake huyo Aba Jundul akasema:
"Huyu ewe Muhammad ni mtu wa
mwanzo ambaye huna budi kumrudisha kwetu."
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) akasema:
‘Lakini bado hatukumaliza kutia saini (kutia
sahihi) mkataba.’
Suheil akasema:
‘Kwa hivyo hakutokuwa na mapatano yoyote baina yetu’.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema:
‘Nakuomba umruhusu huyu tu’.
Suheil akasema:
‘Sitofanya hivyo’.
Ikambidi Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akubali
kuwaache makafiri wale wamchukue, ndipo Abu Jundul aliponyanyua sauti na
kusema:
‘Enyi Waislam, mnaniacha nirudishwe kwa Makafiri na mimi ni Muislam
mwenzenu nakimbilia kwenu. Hamuoni jinsi gani wameniadhibisha?’
Aba Jundul alikua ameadhibishwa adhabu kali
Sasa
ukiichunguza kauli ya Umar (Radhiya Llahu anhu) pale alipomuuliza Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam):
“Si ulituambia kuwa tutakwenda (Makka) na tutatufu penye
nyumba…….nk.?”
Utaona
kuwa alimuuliza kwa sababu Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) aliwaambia hapo mwanzo kuwa aliota kuwa wanafanya Umra yeye na Masahaba
zake na kutufu Al Kaaba, na Masahaba walipoona mambo yanachelewa wakaona uzito
kidogo.
(Fathi
l
Kwa
ajili hiyo Umar (Radhiya Llahu anhu) alimuendea na kumuuliza Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam). Na hii ni kwa sababu ya Umar (Radhiya
Llahu anhu) alitaka kuwaona washrikina wakidhalilika na kuinusuru dini ya
Mwenyezi Mungu.
Hata
ukiyachunguza masuali yake utaona kuwa hayabebi isipokuwa maana hiyo.
Hapana
shaka yoyote kuwa Umar (Radhiya Llahu anhu) alikuwa akiamini kuwa Muhammad (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) ni Mtume wa Mwenyezi Mungu wa kweli.
Ukiisoma
riwaya iliyonukuliwa kutoka kwa Is-haq (Radhiya Llahu anhu) na kutolewa na Imam
Bukhari (Fathi l Bari Juz.5 uk.409) inayosema:
“Pale Abubakar (Radhiya Llahu anhu) alipomuambia Umar (Radhiya Llahu anhu):
“Shikamana naye kwani huyu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu wa Mwenyezi
Mungu”.
Umar akajibu:
“Mimi nashuhudia kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu”.
Na
kwa ajili hii Imam Ibni Hajar Al Asqalani anasema:
‘Ni wazi kuwa Umar alipokuwa akiuliza masuali yale, alikuwa na nia
ya kutaka kujua hekima ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) kuyakubali masharti yale ili umdhihirikie ukweli na asibabaike. Na
mfano wake ni mfano wa kisa chake pale aliposimama mbele ya Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), wakati Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) alipotaka kumsalia mnafiki maarufu aitwae Abdillahi bin
Ubay, isipokuwa siku hiyo hakufanya mambo
(Al
Fat h- ju. 5
Ni
kweli kabisa kuwa Umar (Radhiya Llahu anhu), siku hiyo alikuwa na msimamo wa
kutaka kuijua hekima ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
ya kukubali masharti yale ya makafiri, na haya yanadhihirika katika hadithi
iliyopokelewa kutoka kwa Imam Muslim akielezea kisa cha Hudaybiya baada ya Umar
(Radhiya Llahu anhu) kuuliza masuali.
Hadithi
hiyo inasema hivi:
“Kisha ikateremshwa Suratul Fat-h, (Sura ya Ufunguzi), na Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwita Umar (Radhiya Llahu
anhu) na kumsomea sura hiyo. Umar (Radhiya Llahu anhu) akamuuliza Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam):
“Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, huu ndio ufunguzi?”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akajibu:
“Naam (Ndiyo).”
Umar akafurahi na kuridhika.”
(Muslim
na Sharhi yake Juz. 12 Uk.194 (Kitabu cha Jihad na Sira No.1784)
Na
ni katika sura hii ya Al Fathi (Ufunguzi), iliteremka kauli Yake Subahanahu
wa Taala isemayo:
"Kwa hakika Mwenyezi Mungu amewapa radhi Waislamu
walipofungamana nawe chini ya mti na alijua yaliyomo nyoyoni mwao. Basi
akateremsha utulivu juu
Al
Fathi - 18
Na
katika Musnad ya Imam Ahmed kutoka kwa Jabir bin Abdillah amesema:
“Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Hatoingia Motoni kamwe yeyote aliyepigana vita vya Badar na
(yeyote) aliyefungamana (na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam)) siku ya Hudaybiya”.
(Musnad
Imam Ahmed Juz. 5 No.15262 na hadithi hii imesahihishwa na Sheikh Al Albani
katika Silsila Sahiha No.2160).
Mwenyezi
Mungu katika aya iliyotangulia anatujulisha juu ya kuridhika kwake na Waislam
waliofungamana na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) chini
ya mti siku hiyo na anashuhudia kuwa atawaingiza Peponi.
Kwa
ajili gani Mwenyezi Mungu atawaingiza Peponi?
Kwa
ajili ya usafi wa yaliyomo nyoyoni mwao, na hii ni kauli ya Mwenyezi Mungu na
ushahidi Wake Subuhanahu wa Taala katika Sura hiyo.
Sasa
vipi tena aje mtu atuambie kuwa hawa ni wanafiki, makafiri na ni watu wa
Motoni?
Tufuate
maneno ya Mwenye Kujua siri za moyoni na yaliyodhihiri au tufuate kauli za
binadamu?
Wengine
wanaichukulia ile kauli ya Umar (Radhiya Llahu anhu), aliposema:
“Nilifanya mambo siku hiyo”
Na
kauli yake katika hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Bukhari na kusimuliwa na
Is-haq (Radhiya Llahu anhu) kuwa:
“Umar
alikuwa akisema:
‘Niliendelea kutoa Sadaka, Kufunga, Kuswali na kununua watumwa na
kuwaacha huru ili Mwenyezi Mungu anisamehe kwa yale niliyotenda siku hiyo,
nikiogopa juu ya maneno niliyotamka siku hiyo”.
Na
katika hadithi nyingine:
“Kwa ajili yake nilinunua na kuwaacha huru watumwa wengi
(Bukhari – Fathi l Bari – Juz.5
Uk. 408).
Wanazichukulia kauli hizi kama ni dalili kuwa Umar
(Radhiya Llahu anhu) alitamka maneno
mabaya sana siku hiyo na wengine wakabuni kauli mbali mbali na kuzinasibisha na
Umar (Radhiya Llahu anhu) kuwa alizitamka siku hiyo.
Anayechunguza ataona kuwa kule Kufunga kwake,
Kusali, Kutoa Sadaka na Kuwaacha huru watumwa kwa ajili ya kutaka kusamehewa na
Mola wake, ni dalili ya UchaMungu wake kwa kuogopa kwake kwa yale masuali
aliyokuwa akimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam),
na dalili nyingine ya ucha Mungu wake ni kule kuielekea kwake haki mara
anapoitambua ilipo, na kwamba hakutaka isipokuwa Uislam uwe na utukufu mbele ya
makafiri na kuwadhalilisha makafiri hao, na haya yote yako wazi kabisa katika
hadithi zilizotangulia.
Wengine wanasema:
“Hata hao Waislam wengine pia
hawakutii amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu siku hiyo.”
Jawabu:
Tulieleza hapo mwanzo kuwa na Aly (Radhiya Llahu
anhu) alikuwepo siku hiyo, na pale Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) alipowaambia:
“Inukeni chinjeni na nyoeni
nywele”, hapana hata Sahaba mmoja aliyeinuka, basi kwa vile hata Aly (Radhiya
Llahu anhu) hakuinuka, hii inaleta maana kuwa hata Aly (Radhiya Llahu anhu) hakuridhika
na masharti hayo kama vile alivyokuwa Umar bin Khatab (Radhiya Llahu anhu).
Zipo sababu nyingi zilizowafanya Masahaba (Radhiya
Llahu anhum) wachelewe kutii amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) siku hiyo. Ibni Hajar katika Fat h Juz. 5 Uk. 409 na 410
anasema:
“Inaelekea kwamba Masahaba (Radhiya
Llahu anhum) walisubiri kwa kutegemea wasifaridhishiwe amri hiyo, huku
wakitamani iteremke aya kutoka kwa Mwenyezi Mungu itakayoubatilisha mkataba huo
wa Sulhu, au Aya itakayowahusisha kuingia Makka na kufanya Umra waliyoikusudia.
Na hii ni kwa sababu wakati huo zilikuwa zikiteremka aya za kufuta ‘Nas'kh’.
Huenda pia pale walipotakiwa wachinje
na kunyoa walikuwa wamezama katika kutafakari juu ya hali zao kwa mshangao
waliopigwa nao wakihisi kuwa wamedhalilishwa na makafiri hasa kwa vile wao
walikuwa na nguvu za kutosha kuweza kuingia Makka na kufanya Umra.
Au huenda ikawa walichelewa kutii amri
hiyo wakidhani kuwa amri waliyopewa haikubeba maana ya kulazimika kuitimiza hapo
hapo, na hivi ndivyo ilivyo, kuwa zipo dalili nyingi zinazowapa Masahaba
(Radhiya Llahu anhum) kila aina ya udhuru wa kuchelewa kufuata amri hiyo”.
Mfano wake ni mfano wa vita vya kuuteka mji wa
Makka vilivyokuwa katika Mwezi wa Ramadhani, pale walipotakiwa kufungulia Saumu
zao, na walipochelewa kufungulia kwa kufikiria kuwa huenda amri hiyo ikawa ni hiari
na sio lazima kwao. Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
akaamrisha aletewe birika na kunywa mbele yao. Masahaba (Radhiya Llahu anhum) walipomuona akinywa, nao pia wakanywa.
(Bukhari).
Hizi ni sababu mbali mbali walizoziweka Maulamaa
katika kutoa udhuru wa kuchelewa kwa Masahaba (Radhiya Llahu anhum) kunyoa na
kuchinja, pale walipotakiwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) kufanya hayo. Lakini mara Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) alipotoka na kuanza kunyoa na kuchinja mnyama wake, Masahaba wote
(Radhiya Llahu anhum) wakafanya kama alivyofanya Mtume wao (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) bila kuchelewa.
Mashia wanasema kuwa hiyo ndiyo siku ambayo Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alitaka kumchagua Aly
(Radhiya Llahu anhu) awe ndiye Imam wa
Waislam baada ya kufa kwake. Wakazua mengi kutokana na yaliyotokea siku hiyo
wakijaribu kuuthibitisha uongo wao huo.
Wanasema hivi:
“Masahaba wote walikuwepo nyumbani kwa Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) siku ya Alkhamis, siku tatu
kabla ya kufariki kwake, na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) akasema:
“Leteni kidawati na kalamu
nikuandikieni maneno yatakayokukingeni na upotovu baada yangu”.
Umar akasema: “Mtume wa Mwenyezi
Mungu anasema bila fahamu (hii ni kauli ya Mashia). Munayo Qurani, kinatutosha
kitabu cha Mwenyezi Mungu”.
Masahaba wakaasi amri, na Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), akuwafukuza nyumbani kwake bila
ya kuwaandikia chochote”.
Katika vitabu vyao, wanakielezea kisa hiki kwa
ufupi na kwa kubadilisha badilisha maneno.
Katika vitabu vingine wanasema:
Ibni Abbas (Radhiya Llahu anhum) alisema:
“Siku ya Alkhamisi, na kipi
kitakachokujulisha hiyo siku ya Al Khamis, siku hiyo maumivu yalimzidi Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), akasema:
“Ngojeni nikuandikieni maandishi,
hamtopotoka baada yake”.
Umar akasema:
“Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) anasema bila fahamu, na tunayo Qurani, kinatutosha
kitabu cha Mwenyezi Mungu.”
Wakakhtilafiana na watu wa nyumba ya Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu alayhi wa sallam) na kukasirikiana, na kwamba wapo
waliokuwa wakisema:
“Jisogezeni ili aandike yale ambayo
baada yake hamtapotea tena”
Na wapo waliokuwa wakisema yale
aliyosema Umar. Na mazungumzo na khitilafu zilipozidi, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) akawaambia:
“Ondokeni karibu yangu”.
Ibni Abbas akawa anasema:
“Msiba wa kweli hasa ni kule Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kutoweza kuwaandikia
maandishi yale kutokana na kukhitilafiana kwao”.
Tukio
hili lilitokea kweli na limenukuliwa na Maulamaa wa Kishia pamoja na Maulamaa
wa Kisunni, kwa hivyo halina shaka yoyote kuwa lilitokea.
Mashia
wanajaribu kulifasiri tukio hili kama kwamba jambo jipya litakalokata mzizi wa
fitna baina ya Waislam ambalo Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) siku hiyo alitaka kuwaandikia Masahaba (Radhiya Llahu anhum), ni usia
wa kumchagua Ali (Radhiya Llahu anhu) kuwa Khalifa wa Waislam baada ya kufa
kwake na kwamba Umar (Radhiya Llahu anhu) aliyajua hayo, ndio maana akawaambia
watu kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) hajui nini
anasema na kwamba tunayo Qurani inatutosha.
Atakayeichunguza
hadithi hii kwa njia zake zote zilizopokelewa ataona kuwa ndugu zetu wanajaribu
kuchanganya maneno na kuacha maneno.
Kwa
mfano, katika hadithi iliyotolewa na Bukhari katika Kitabu cha Al Maghazi
hadithi Nambari 4168 inasema hivi:-
“Wakasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) hana
fahamu juu ya anayoyasema, jamani hebu msikilizeni vizuri." wakamuendea
huku wakimuuliza.
Akawaambia:
“Niacheni, maana haya niliyonayo ni bora kuliko mnayoniitia”, kisha
akawausia mambo matatu; akasema:
“Watoeni washirikina nje ya Bara ya Arabu na wapokeeni vizuri
wageni
Sahih Bukhari (Kitabul Maghazi)
Anasema Imam Annawawiy:
“Itikadi ya kila Muislam kuwa Mtume wa
Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) hawezi kusema neno la uongo wala
hawezi kubadilisha yale aliyotakiwa kutufikishia ikiwa yu mgonjwa au mzima na
afya yake. Na iwapo tushayajua hayo, basi inatubainikia kuwa Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) angekuwa ametumwa na Mola wake kutufikishia
jambo, basi lazima atatufikishia akiwa anaumwa au akiwa na afya yake.
Na kwa ajili hiyo angekuwa ametumwa
kutufikishia jambo la lazima ambalo baada yake hatutopotoka, basi hata Waislam
wangekhitilafiana namna gani, lazima angelifikisha neno hilo., na hii inatokana
na kauli Yake Subhanahu wa Taala pale aliposema:
“Wafikishie yale uliyofunuliwa” (Balligh
maa unzila ilayka)."
Kama vile alivyokuwa hakuacha kuyafikisha
aliyoteremshiwa kabla ya hapo juu ya inadi, mateso, inda na zogo alokuwa
akifanyiwa na makafiri.
Kutokana na sababu hizi inatubainikia kuwa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa anataka kuwaandikia
juu ya mwenendo mzuri wa kuufuata na siyo amri iliyowajibika.
Kwa sababu Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) baada ya tukio hilo aliishi siku nne nyingine, na katka siku
zote hizo hakuwaamrisha tena wamletee kitabu na kalamu.
Kisha
katika riwaya, pana kauli isemayo:
“Akawausia
mambo matatu”.
Na
hii ni dalili kuwa aliyotaka yaandikwe ni usia na si amri, kwa sababu angetaka
kuandika maamrisho basi asingeacha kwa sababu ya kukhitilafiana kwa Masahaba
(Radhiya Llahu anhum). Na Mwenyezi Mungu angemtia adabu yule aliyekuwa kizuizi
katika kuifikisha amri hiyo. Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam) angeliifikisha hata kwa matamshi
Katika
riwaya zao wanasema kuwa eti siku hiyo Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) alikasirka
Atakayechunguza
maneno aliyotamka Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
wakati ule, ataona kuwa hapakuwa na dalili yoyote kuwa alikasirika nao,
isipokuwa tu pale alipoona maradhi yanamzidi akawataka waondoke. Na yanabainika
haya zaidi pale Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
alipowausia juu ya mambo yale matatu.
Hata
tukichukulia kwa ajili ya mjadala kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) alikasirika nao, hii haina maana kuwa daraja
“Mola wangu! Muislam yeyote niliyemtukana, basi mjaalie tusi
Bukhari
Mlango wa Daawat – hadithi nambari 6000
Na
kutoka kwa Attabarani katika Al Kabeer na Imam Ahmed katika Musnad
yake imepokelewa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
amesema:
“…….Yeyote katika umati wangu niliyemtukana au kumlani wakati
nimeghadhibika, kwani mimi ni katika wana wa Adam, ninaghadhibika
Attabarani,
Ahmed na Abu Daud
Iwapo
wao wanaona kuwa pale Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam)
anapomkasirikia mtu, basi mtu huyo anageuka kuwa mnafiki au kafiri,
Imepokelewa kutoka kwa Bukhari katika hadithi iliyosimuliwa na Imam
Aly (Radhiya Llahu anhu) kuwa usiku mmoja Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu
alayhi wa sallam) alipita nje ya nyumba
“Mbona hamsali?”
Anasema Aly (Radhiya Llahu anhu), nikasema:
“Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, nafsi zetu zimo mikononi mwa Mwenyezi
Mungu, angetaka tuamke tungeamka”.
Aly (Radhiya Llahu anhu) anasema:
“Nilipomuambia vile, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) akaondoka bila kunijibu huku akilipigapiga paja
“Wa kaan l insaanu ak' thara shay in jadala”.
“Binadamu kwa ubishi hawezekani”
Bukhari
mlango wa Tahajjud – Hadithi nambari 1075
Sasa
hapa watasema nini juu ya Imam Aly (Radhiya Llahu anhu) ambaye ni Imam wao wa
mwanzo aliyekingwa (asiyekosea) na Khalifa wa nne wa Waislam?
Wanapoambiwa
kuwa sababu iliyomfanya Umar (Radhiya Llahu anhu) kutaka Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) asiandike wakati ule ni baada ya kumuona
kuwa alikuwa taabani
Tunawauliza;
“Umar
(Radhiya Llahu anhu) ambaye ni Al
Farook wa Umma huu (Mwenye kutenganisha haki na batil), na hii ni sifa
aliyopewa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), na ni
mbora wa Masahaba baada ya Abubakar (Radhiya Llah anhu), hivyo mnataka kusema
kuwa alikusudia kumuudhi Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa
sallam)?"
Wallahi
hayasemi haya isipokuwa yule aliyechagua ujinga kuwa ni muongozo wake na
ujahili kuwa ni Mantiki yake.
Hasa
pale tunaposoma katika hadithi kuwa:
"Alizidiwa na maradhi".
Si
hivyo tu, bali ilimbainikia Umar (Radhiya Llahu anhu) kuwa Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) hakukusudia kufaridhisha kitu, bali
alikusudia kupendekeza tu.
Mfano
wake ni mfano wa usiku ule wakati Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi
wa sallam) alipomwamsha Aly (Radhiya Llahu anhu) na kumtaka aswali.
Ilimbainikia Ali (Radhiya Llahu anhu) kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla
Llahu alayhi wa sallam) hakutaka kumfaradhishia jambo, bali alikusudia
kupendekeza tu tendo lile, ndiyo maana akajitetea kwa kusema kuwa hakujaaliwa
kuamka.
ITAENDELEA
INSHAALLAH
ثانياً: الرد على التيجاني في موقفه من الصحابة في رزيَّة يوم الخميس:
يقول التيجاني (( ومجمل القصة أن الصحابة
كانوا مجتمعين في بيت رسول الله قبل وفاته بثلاثة أيام فأمرهم أن يحضروا له الكتف
والدواة ليكتب لهم كتابا يعصمهم من الضلالة، ولكن الصحابة اختلفوا ومنهم من عصى
أمره واتهمه بالهجر، فغضب رسول الله وأخرجهم من بيته دون أن يكتب لهم شيئا، وإليك
شيئا من التفصيل، قال ابن عباس: يوم الخميس وما يوم الخميس اشتد برسول الله وجعه،
فقال: هلم أكتب لكم كتابا لا تضلوا بعده، فقال عمر إن النبي قد غلبه الوجع، وعندكم
القرآن حسبنا كتاب الله، فاختلف أهل البيت واختصموا، منهم من يقول قربوا يكتب لكم
النبي كتابا لا تضلوا بعده، ومنهم من يقول ما قال عمر، فلمّا أكثروا اللغو
والإختلاف عند النبي، قال لهم رسول الله (ص) قوموا عني، فكان ابن عباس يقول: إن
الرزيّة كل الرزيّة ما حال بين رسول الله وبين أن يكتب لهم ذلك الكتاب من اختلافهم
ولغطهم، هذه الحادثة صحيحة لا شك فيها، فقد نقلها علماء الشيعة ومحدثوهم في كتبهم،
كما نقلها علماء السنة ومحدثوهم ومؤرخوهم، وهي ملزمة لي على ما ألزمت به نفسي، ومن
هنا أقف حائراً في تفسير الموقف الذي وقفه عمر بن الخطاب من أمر رسول الله، وأي
أمر هو؟ أمر عاصم من الضلالة لهذه الأمة، ولا شك أن هذا الكتاب فيه شيء جديد
بالنسبة للمسلمين سوف يقطع عليهم كل شيء ... ثم يتابع فيقول ... ولنترك قول الشيعة
بأن الرسول أراد أن يكتب إسم علي خليفة له، وتفطن عمر لذلك فمنعه فلعلهم لا
يقنعوننا بهذا الزعم الذي لا يرضينا مبدئياً ولكن هل تجد تفسيراً لهذه الحادثة
المؤلمة التي أغضبت الرسول حتى طردهم وجعلت ابن عباس يبكي حتى يبلَّ دمعه الحصى
ويسميها رزية، أهل السنة يقولون بأن عمر أحس بشدة مرض النبي فأشفق عليه وأراد أن
يريحه، وهذا التعليل لا يقبله بسطاء العقول فضلاً عن العلماء، وقد حاولت مراراً
وتكراراً التماس بعض الأعذار لعمر ولكن وقع الحادثة يأبى علـي ذلك، وحتى لو أبدلت
كلمة يهجـر ( والعياذ بالله ) بلفظة ( غلبه الوجع ) فسوف لن نجد مبرراً لقول عمر (
عندكم القرآن ) حسبنا كتاب الله، أوكان هو أعلم بالقرآن من رسول اللـه الذي أنزل
عليه، أم أن رسول اللـه لا يعي ما يقول (حـاشـاه) أم أنـه أراد بأمـره ذلك أن يبعث
فيهـم الاختـلاف والفـرقة أستغفـر الله ))(1).
وللرد على ما سبق أقول:
1ـ خلط التيجاني في هذا الحديث يبن أكثر من
رواية مختلفة فقد ذكر أن الصحابة اتهموا النبي صلى الله عليه وآله وسلم
( بالهجر ) وفي الحديث الذي ذكره في كتابه لا وجود لهذه الكلمة وفي الحديث أيضاً
نقل قول ابن عباس ( يوم الخميس وما يوم الخميس اشتد برسول الله وجعه ) فهذه الجملة
ليست من الحديث المذكور والذي يعزوه للبخاري في بـاب المـرض ( بـاب قول المـريض
قـوموا عني ) بهـامش كتـابه ولكنـها
وكلمـة ( يهجر ) جزء من رواية أخرى تجاهلها هذا التيجاني لأنها توضح أموراً هامة
في هذه الحادثة وهي رواية سعيد ابن جبير قال (( قال ابن عباس: يوم الخميس وما يوم
الخميس، اشتد برسول الله صلى الله عليه وآله وسلم وجعه فقال: ائتوني
أكتب لكم كتاباً لن تضلوا بعده أبداً، فتنازعوا، ولا ينبغي عند نبي نزاع، فقالوا
ماشأنه؟ أهجر، استفهموه، فذهبوا يَرُدُّون عليه، فقال: دعوني، فالذي أنا فيه خيرٌ
مما تدعونني أليه، وأوصاهم بثلاث قال: أخـرجوا المشركين من جزيرة العرب، وأجيزوا
الوفد بنحو ما كنت أجيزهم، وسكت عن الثالثة أو قال فَنَسِيتُها ))(2).
2ـ إذا أراد هـذا التيجـاني أن يفسر
أحاديث المصطفى صلى الله عليه وآله وسلم لقلب الموازين، فالكاتب
الفاضل يدعي أن الرسول صلى الله عليه وآله وسلم أراد أن يكتب لهم كتاباً يعصمهم من ( الضلالة )!
هكذا بإطلاق، ومعلوم أن للضلالة معاني مختلفة، والصحيح أن النبي صلى الله
عليه وآله وسلم بقوله ( لن تضلوا بعده
) فإنه يخصه بأمر محدد كأن ينص على تعيين خليفة أو كتابة كتاب في الأحكام
ليرتفع النزاع في الأمة وإلا فبالله كيف يترك النبي صلى الله عليه وآله وسلم
أن يكتب أمراً يعصم الأمة به من الضلالة؟! فإن دل هذا على شيء فإنه يدل على أن
الأمر ليس للوجوب فتركه.
3ـ يجب أن يعتقد كل مسلم (( أن النبي صلى
الله عليه وآله وسلم معصوم من الكذب ومن تغيير شيء من الأحكام الشرعية في
حال صحته وحال مرضه ومعصوم من ترك بيان ما أمر ببيانه وتبليغ ما أوجب الله عليه
تبليغه ))(3) فإذا عرفنا ذلك تبين لدينا أنه
لو أمر بتبليغ شىء حال مرضه وصحته فإنه يبلغه لامحالة فــ(( لو كان مراده صلى الله عليه وآله
وسلم أن يكتب مـالا يستغنون عنه لم يتركـه لاختلافهم ولا لغيره، لقوله تعالى
{ بلغ ما أنزل إليك } كما لم يترك تبليغ غير ذلك لمخالفة من خـالفه ومعاداة من
عاداه ))(4) فدل ذلك على أن ما أراد النبي صلى
الله عليه وآله وسلم كتابته يحمل على الندب لا على الوجـوب وقد عـاش صلوات
الله وسلامه عليه أربعة أيام بعـد ذلك ولم يأمـرهم بإعـادة الكتابة، وقوله في
الرواية التى أخفاها الكاتب ( وأوصاهم بثلاث ) يدل على أن الذى أراد أن يكتبه لم
يكن أمراً محتّماً لأنه لو كان مما أمر بتبليغه لم يكن يتركه لوقوع الاختلاف،
ولعاقب الله من حـال بينه وبين تبليغه، ولبلغه لهـم لفظاً كما أوصاهم بإخـراج
المشركين وغير ذلك(5).
4- أمّا ادعاؤه بقوله ( ولكن هل تجد تفسيراً
معقولاً لهذه الحادثة المؤلمة التي أغضبت الرسول حتى طردهم )، قلت:
لم يظهر على النبي صلى الله عليه وآله
وسلم أي غضب على صحابته أو أمر بطردهم (هكذا ) ولم يرد هذا المعنى في أيٍ من
روايات الحديث السبع التي ذكرها البخاري في صحيحه، ولكنه لشدة إحساسه بالمرض طلب
منهم الكف عن الجدال فيما بينهم، ويظهر هذا واضحاً في الرواية التي أوصاهم فيها
بثلاثة أمور وذلك بعد جدالهم فلا دليل على أنه غضب منهم أو طردهم ولو فرضنا جدلاً
أنه غضب منهم فليس في هذا قدح بهم لأنهم ليسوا معصومين من الوقوع بذلك والرسول
صلى الله عليه وآله وسلم يغضب ويرضى بل لعل غضبه على أصحابه يكون خيراً لهم
فقد أخرج البخاري في صحيحه عن أبي هـريرة رضي اللـه عنه أنه سمع النبي صلى
الله عليه وآله وسلم يقول (( اللهم فأيما مؤمن سببته فاجعل ذلك له قربة إليك
يوم القيامة ))(6) وروى الطبراني في الكبير وأحمد
في المسند قوله صلى الله عليه وآله وسلم في جزء من الحديث (( أيما رجل
من أمتي سببته سُبة أو لعنته لعنة في غضبي فإنما أنا من ولد آدم، أغضب كما يغضبون،
وإنما بعثني رحمة للعالمين فاجعلها عليهم صلاة يوم القيامة ))(7) ثم أقول لهذا التيجاني ( المهتدي ) إذا لم تستطع أن تجد
تفسيراً معقولاً ( لغضب ) النبي صلى الله عليه وآله وسلم على الصحابة
كما تدعي فأقول لك أخرج البخاري عن علي بن أبي طالب قوله (( أن رسول الله صلى
الله عليه وآله وسلم طرقه وفاطمة بنت النبي عليه السلام ليلة فقال: ألا
تصليان؟ فقلت: يارسول الله أنفسنا بيد الله، فإذا شاء أن يبعثنا بعثنا، فانصرف حين
قلت ذلك ولم يرجع إليّ شيئاً، ثم سمعته وهومول يضرب فخذه وهـو يقول { وكـان
الإنسان أكثر شيء جدلا }))(8)! فهل يجد التيجاني تفسيراً
معقـولاً لمخـالفة (علي) أمر الرسول صلى
الله عليه وآله وسلم واحتجـاجه بالقـدر حتـى جـعل النبي صلى الله عليه
وآله وسلم يضرب علـى فخـذه ويقول معترضاً ( وكان الإنسان أكثر شيء جدلا )
فإن وجد تفسيراً معقولاً لجدال علي ففعل الرسول صلى الله عليه وآله وسلم
لجدال الصحابة معقول جداً؟!
5ـ أما عن بكاء ابن عباس حتى بل دمعه الحصى
وتسميته ذلك رزيّة فلست أدري والله ما الحجة التي فيه على أهل السنة فابن عباس كان
يقول ذلك عندما يروي الحديث وليس عندما حدثت الحادثة، والروايات كلها تدل على ذلك
ويحتمل أنه تذكر وفاة النبي صلى الله عليه وآله وسلم فزاد في حزنه
بالإضافة إلى أن عدم كتابة الكتاب كان هذا رزية في حق من شك في خلافة أبي بكر فلو
كتب الكتاب لزال الشك وكذلك سمـى تلك الحادثة رزية لأن ابن عباس كان ممن وافق على
ترشيح أبـي بكر، وعلـى كل حـال إذا اعتقد أحـد أن قول ابن عباس حـق في خـلافه مع
عمـر فأقـول لا شك عندنا أن عمر كان أفقه من ابن عبـاس والحمد اللـه.
6ـ وقوله ( أهل السنة يقولون بأن عمر أحس
بشدة مرض النبي فأشفق عليه وأراد أن يريحـه، وهـذا التعليل لا يقبله بسطاء العقـول
فضلاً عن العلماء )
فأقـول:
سبحان الله على هذا العقلاني فإذا كان قول
العلماء أن عمر أراد إراحة النبي صلى الله عليه وآله وسلم تعليل لا
يقبله بسطاء العقول؟! فهل القول بأن عمر وهو فاروق الأمة ومن خيرة الصحابة بعد أبي
بكر تعمد إيذاء الرسول صلى الله عليه وآله وسلم واتهامه بالهجر تعليل
يقبله عظماء العقول يا تيجاني؟! فوالله لا يقول هذا إلامن جعل الجهل منهجه وطريقه،
ولا شك لدينا أن هذا التعليل مقبول منطقياً خصوصاً إذا عرفنا أنه في الحديث اشتد
برسول الله صلى الله عليه وآله وسلم وجعه، ولكن ليس هذا هو السبب وحده
الذي جعل عمر يقول ما قال بل لأنه ظهرت لديه قرينة تدل على أن الرسول صلى
الله عليه وآله وسلملم يجزم بالكتابة فقال ما قال وهذا من اجتهاده،..كما
تبين لعلي عندما دعاه النبي صلى الله عليه وآله وسلم للصلاة فاحتج بالقدر لأنه تبين أن النبي عليه
السلام لم يقل هذا على سبيل الجزم أى بالوحي، والكاتب يدعي أن أهل السنة يتعللون
عن عمر بأنه أراد أن يريح النبي صلى الله عليه وآله وسلم شفقة عليه
وبما أنه نقل جزءاً من كلام أهل السنة مبتوراً فسأضطر لنقل بعض من أقوال علماء أهل
السنة ليظهر للقارئ مدى قوة حجج أهل السنة في تعليل موقف عمر ومدى الفرق بين تعليل
جاهل مفرط في جهله وبين عالم راسخ في علمه، يقول المازري عن هذه الحادثة (( إنما
جاز للصحابة الاختلاف في هذا الكتاب مع صريح أمره لهم بذلك لأن الأوامر قد يقارنها
ما ينقلها من الوجوب، فكأنه ظهرت منه قرينة دلت على أن الأمر ليس على التحتم بل
على الاختيار فاختلف اجتهادهم، وصمم عمر على الامتناع لما قام عنده من القرائن
بأنه صلى الله عليه وآله وسلم قال ذلك عن غير قصد جازم، وعزمه صلى
الله عليه وآله وسلم كان إما بالوحي
وإما بالاجتهاد وكذلك تركه إن كان بالوحي فبالوحي وإلا فبالاجتهاد أيضاً....))(9)
وقال الإمام البيهقي في أواخر
كتابه دلائل النبوة (( إنما قصد عمر
التخفيف على رسول الله صلى الله عليه وآله وسلم حين غلبه الوجع ولو كان
مراده صلى الله عليه وآله وسلم
أن يكتب ما لايستغنون عنه لم يتركه لاختلافهم ولا لغيره لقوله تعالى { بلغ
ما أنزل إليك } كما لم يترك تبليغ غير ذلك لمخالفة من خالفه ومعاداة من عاداه وكما
أمر في ذلك الحال بإخراج اليهود من جزيرة العرب وغير ذلك مما ذكره في الحديث ))(10) ويقول الإمام القرطبي (( ائتوني أمر، وكان حق المأمور أن
يبادر للإمتثال لكن ظهر لعمر رضي الله عنه مع طائفة أنه ليس على الوجوب، وأنه من
باب الإرشاد للأصلح فكرهوا أن يكلفوه من ذلك مايشق عليه في تلك الحالة مع استحضارهم
قوله تعالى { ما فرطنا في الكتاب من شيء } وقوله تعالى { تبياناً لكل شيء } ولهذا
قال عمر: حسبنا كتاب الله، وظهر لطائفة أخرى أن الأولى أن يكتب لما فيه من زيادة
الإيضاح، ودلّ أمره لهم بالقيام على أن أمره الأول كان على الاختيار، ولهذا عاش صلى
الله عليه وآله وسلم بعد ذلك أياماً ولم يعاود أمرهم بذلك ولو كان واجباً لم
يتركه لاختلافهم لأنه لم يترك التبليغ لمخالفة من خالف، وقد كان الصحابة يراجعونه
في بعض الأمور مالم يجزم بالأمر فإذا عزم امتثلوا ))(11)
وقـال الخطابي (( لم يتوهم عمر الغلط
فيما كان النبي صلى الله عليه وآله وسلم يريد كتابته، بل امتناعه محمول
على أنه لما رأى ما هو فيه من الكرب وحضور الموت خشي أن يجد المنافقون سبيلاً إلى
الطعن فيما يكتبه وإلى حمله على تلك الحـالة التي جرت العـادة فيها بوقوع بعض
مايـخالف الاتفاق فكان ذلك سبب توقف عمر، لا أنه تعمد مخالفة النبي صلى الله
عليه وآله وسلم ولا جواز الغلط عليه حاشا وكلا ))(12)
ويقول النووي في شرحه لمسلم (( أما
كلام عمر رضي الله عنه فقد اتفق العلماء المتكلمون في شرح الحديث على أنه من دلائل
فقه عمر وفضائله ودقيق نظره، لأنه خشي أن يكتب صلى الله عليه وآله وسلم
أموراً ربما عجزوا عنها واستحقوا العقوبة عليها لأنها منصوصة لامحالة للاجتهاد
فيها فقال عمر: حسبنا كتاب اللـه لقوله تعالى { مافرطنا في الكتاب من شيء } وقوله
تعالى { اليوم أكملت لكم دينكم } فعلم أن اللـه تعالى أكمل دينه فأمن الضلالة على
الأمـة وأراد الترفيه على رسول الله صلى الله عليه وآله وسلم فكان عمر
أفقه من ابن عباس وموافقيه ))(13) ومما يدلل على فقه وعلم عمر ما
رواه مسلم في صحيحه عن عائشة أن النبي صلى الله عليه وآله وسلم قال ((
قـد كان في الأمم قبلكم محدثـون، فـإن يكن في أمتي أحد فعمر ))(14)
وعن أبي سعيد الخدري قال: قال رسول
الله صلى الله عليه وآله وسلم (( بينما أنا نائم رأيت الناس يعرضون علي
وعليهم قمص، منها مايبلغ الثدي، ومنها ما يبلغ دون ذلك، ومر عمر بن الخطاب وعليه
قميص يجره. قالوا: ماأولت ذلك يارسول الله؟ قال الدين ))(15)
وأخرج البخاري في صحيحه عن ابن عمر
أن النبي صلى الله عليه وآله وسلم قال ((بينما أنا نائم إذ رأيت قدحاً
أتيت به فيه لبن فشربت منه حتى أني لأرى الرَّيَّ يخرج من أظافري، ثم أعطيت فضلي
عمر بن الخطاب فقالوا: فما أولته يارسول الله؟ قال العلـم ))(16)
وهذا علي بن أبي طالب يمدح عمر بن
الخطاب ويشهد بعدالته واستقـامته وذلك من كتاب الإمامية الحجة ( نهج البلاغة )
الذي جمعـه إمامهم (الشريف الرَّضى ) حيث يقول في جزء من خطبته (( ووليهم والٍ
فأقام واستقام حتى ضرب الدين بجرانه ))(17) ويقول ابن أبي الحديد الشيعي
شارح نهج البلاغة ((...هذا الوالي هو عمر بن الخطاب ))(18)
فأقول للتيجاني المهتدي كما يقول
الشاعر:
وكم من عائبٍ قولاً
صحيحاً..........وآفته من الفهم السقيم.
7ـ وقـوله ( وحتـى لـو أبدلت كلمة يهجـر ـ
والعياذ باللـه ـ بلفظة غلبـه الوجـع فسوف لـن نجـد مبرراً لقـول عمر ـ عندكم
القرآن ـ حسبنا كتاب الله ) فأقول:
لا يوجد في أي من روايات الحديث بأن قائل
هذه الكلمة هو عمر فقوله أنه لو أبدل كلمة ( يهجر ، بغلبه الوجع ) إيهام من هذا
التيجاني بأن عمر القائل غلبه الوجع قد قال أيضا بأنه يهجر وهذا من الكذب البين
على عمر لفروق المعنى بين الكلمتين ومن يجـد الكاتب وهو يقول وحتى لو أبدلت كلمة
يهجر( والعيـاذ بالله ) يظن أنه أكثر ورعـاً وتورّعا من صحابة رسول الله صلى
الله عليه وآله وسلم فيالسخافاته الجاهلية !! .
وأما بالنسبة لكمة ( أهَجَرَ ) فإنها جاءت
بصيغة الجمع وسبب قولهم ذلك إنكاراً لمن قال لاتكتبوا فقالوا كيف نتوقف هل تظن أنه
كغيره يقول الهذيان في مرضه ثم قالوا: إستفهموا للإنكار، وإن فرض صدور هذا الكلام
عن بعضهم فلعل أحدهم اشتبه عليه الأمر فشك في ذلك لأنه ليس معصوماً والشك جائز
عليه ولكن يستبعد ذلك لأنه لا بد أن ينكره الباقون، أو لعل قائل هذا القول هو من
قرب دخوله في الإسلام أو أن أحدهم أصيب
بالحيرة لدى مشاهدته النبي في حالته هذه
فقال ما قال و (( الهجر في اللغة هو اختلاط الكلام بوجه غير مفهِم وهو على قسمين:
قسم لا نزاع لأحد في عروضه للأنبياء عليهم السلام وهو عدم تبيين الكلام لبحَّة
الصوت وغلبة اليبس بالحرارة على اللسان كما في الحميات الحارة، وقد ثبت بإجماع أهل
السير أن نبينا صلى الله عليه وآله وسلم كانت بحة الصوت عارضة له في
مرض موته صلى الله عليه وآله وسلم، والقسم الآخر جريان الكلام غير
المنتظم أو المخالف للمقصود على اللسان بسبب الغشي العارض بسبب الحميات المحرقة في
الأكثر، وهذا القسم وإن كان ناشئاً من العوارض البدنية ولكن قد اختلف العلماء في
جواز عروضه للأنبياء، فجوزه بعضهم قياسا على النوم، ومنعه آخرون، فلعل القائل بذلك
القول أراد القسم الأول، يعني أنَّا نرى هذا الكلام خلاف عادته صلى الله عليه
وآله وسلم فلعلنا لم نفهم كلامه بسبب وجود الضعف في ناطقته فلا إشكال ))(19) فعلى العموم كل ما صدر عن الصحابة من أقوال لا تفيد الطعن
بالنبي صلى الله عليه وآله وسلم بيقين وليس فيها ما يقدح بعدالتهم.
8ـ وقوله (( أوكان هو أعلم بالقرآن من رسول
الله.....الخ )) فقوله هذا لا يدل إلا على جهله المركب لأن قول عمر حسبنا كتاب
الله هو رد على من نازعه لا رداً على رسول الله صلى الله عليه وآله وسلم
بالإضافـة إلى أنـه تبين لديه أن الرسـول صلى الله عليه وآله وسلم لم
يجـزم على الكتـابة فقال عمر قولته اعتماداً على قوله { اليوم أكملت لكم دينكم }
وقوله { ما فرطنا في الكتاب من شيء } وهذا كما بينت سابقاً يدل على عميق فقهه
وعلمه، والرسول صلى الله عليه وآله وسلم يعي ما يقوله هو وما يقوله
عمر، لذلك لم ينكر عليه قالته تلك تدليلاً على استصوابه ويعلم النبي صلى الله
عليه وآله وسلم أن هذا لن يبعث فيهم الاختلاف والفرقة وهو ما حدث بالفعل فقد
رشح المسلمون ( أبا بكر الصديق ) فقطع الخلاف وكتب الله لصحابته في عهد أبي بكر حب
الإئتلاف وبغض الاختلاف.
ثم يقول التيجاني ( ثم لو كان تعليل أهل
السنة صحيحاً، فلم يكن ليخفى على رسول الله حسن نية عمر، ولشكره رسول الله على ذلك
وقربه بدلاً من أن يغضب عليه ويقول أخرجوا عني ) أقول: يأبى هذا التيجاني إلا أن
يبرهن على سوء فهمه وقلة حيلته فيعيد كلامه تكراراً ولله در القائل:
إذا لم يكن لك حسن
فهم............أسأت إجابةً وأسأت فهماً!؟
فلو كانت حججك العقلانية صحيحة أن تقول
سكوت النبي صلى الله عليه وآله وسلم
على قول عمر ثم توقفه عن الكتابة يدل على موافقته له، ثم يجازف نحوياً
فيقول ( بدلاً من أن يغضب عليه ويقول أخرجوا عني ) عجباً فالهاء في ( عليه ) عائدة
على عمر والواو في (أخرجوا ) واو الجمع فكيف تستقيم الجملة هكذا؟ فالأصل أن يقال (
أن يغضب عليه ويقول أخرج عني ) ولو قال ذلك فلعلها كانت شبهة له وقول التيجاني هذا
أعظم دليل على أن النبي صلى الله عليه وآله وسلم سكت عن قول عمر ولم
يعترض عليه ولكن لما كثر اللغط والاختلاف قال ( دعوني ) وليس فيها ما يفيد الطرد
والإخراج خاصةً إذا ما عرفنا أنه أوصاهم بعدها بثلاثة وصايا.
ثم يهذي التيجاني فيقول (( وهل لي أن
أتساءل لماذا امتثلوا أمره عندما طردهم من الحجرة النبوية، ولم يقولوا بأنه يهجر؟
ألأنهم نجحوا بمخططهم في منع الرسول من الكتابة، فلا داعـي بعد ذلك لبقائهم،
والدليل على أنهم أكثروا اللغـط والاختـلاف بحضرته (ص)، وانقسموا إلى حـزبين منهم
من يقول: قربـوا إلى رسـول اللـه يكتب لكـم ذلك الكتاب ومنهم من يقول ما قال عمر
أي أنه يهجر ))(20).
الله أكبر!؟ آلصحابة يخططون ضد محمد بن عبد
الله صلى الله عليه وآله وسلم
ليمنعوه من الكتابة!!! فهذا والله اعتقاد من لم يدخل في قلبه حب وتوقير
لصحابة النبي صلى الله عليه وآله وسلم الذين آزروه ونصروه واتبعوا
النور الذي أنزل عليه، وأفدَوهُ بأرواحهم وأهليهم بل وبكل ما يملكون ففتح الله لهم
الدنيا وأذل لهم جبابرة الأرض من الفرس والروم بسبب نصرتهم للنبي صلى الله
عليه وآله وسلم ثم يأتي هذا الأنوك ليدعي أن الصحابة يخططون ضد من؟! رسول
الله صلى الله عليه وآله وسلم !!؟ فإنها والله لإحدى الكبر فهل هذا هو
المنطق السليم والعقلاني الذي أوصله إلى ما يخالف المعقول والمنقول؟!... سبحان
الله أكلّ هذا التحريف ليحاول أن يجعل النص يخدم أهداف الرافضة الشنيعة للحط من
الصحابة ولكن أَنّى لهم، ثم يعيد ويكرر حجته الخاوية على عروشها بأن عمر يقول بأنه
يهجر ودون إطالة أقول الحقيقة ظاهرة والحمد لله.
ثم يدلل هذا المهتدي على أسباب هدايته
فيقول (( والأمر لم يعد بتلك البساطة يتعلق بشخص عمر وحده ولو كان كذلك لأسكته
رسول الله وأقنعه (!) بأنه لا ينطق عن الهوى ولا يمكن أن يغلب عليه الوجع في هداية
الأمة وعدم ضلالتها ولكن الأمـر استفحل واستشرى ووجد له أنصاراً كأنهم متفقون
مسبقاً (!)، ولذلك أكثروا اللغط والاختلاف ونسوا أو تناسوا (!) قول اللـه تعالى {
ياأيها الذين آمنوا لا ترفعوا أصواتكم فوق صوت النبي ولا تجهروا له بالقول كجهر
بعضكم لبعض أن تحبط أعمالكم وأنتم لا تشعرون }
فإن تعجب فعجب قولهم! فإذا كان النبي صلى
الله عليه وآله وسلم يغضب على عمر ويقول له وللباقين اخرجوا عني ألا يستطيع
أن يسكت عمر؟ وفي الحديث أنه أوصاهم بثلاث وصايا، وعدم إسكاته دليل على الموافقة له
والرضا بما قال، أما أنهم أكثروا اللغط ونسوا أو تناسوا ( هكذا ) قول اللـه سبحانه
( الآية ) فأقول لهـذا التيجـاني: الصحـابة لم يرفعـوا أصواتهم فوق صوت النبي صلى
الله عليه وآله وسلم بل رفعوا أصواتهم على بعضهم البعض وهـذا جـائز بدلالة
الآية وعلى هذا فاحتجاجك السقيم ردٌ عليك.
ثم يخرج التيجاني أوضاره فيقول (( وفي هذه
الحادثة تعدوا حدود رفع الأصوات والجهر بالقول إلى رميه (ص) بالهجر والهذيان والعياذ بالله (!!) ثم أكثروا اللغط والاختلاف
وصارت معركة كلامية بحضرته وأكاد أعتقد بأن الأكثرية الساحقة كانت على قول عمر
ولذلك رأى رسول الله (ص) عدم الجدوى من كتابة الكتاب لأنه علم بأنهم لم يحترموه
(!!) ولم يمتثلوا لأمر الله فيه في عدم رفع أصواتهم بحضرته، وإذا كانوا لأمر الله
عاصين فلن يكونوا لأمر رسوله طائعين (!)، واقتضت حكمة الرسول بأن لا يكتب لهم ذلك
الكتاب لأنه طعن فيه في حياته فكيف يعمل بما فيه بعد وفاته، وسيقول الطاعنون: بأنه
هجر من القول ولربما سيشككون في بعض الأحكام التي عقدها رسول الله في مرض وفاته
(!)، إذا اعتقادهم بهجره ثابت، أستغفر الله (!) وأتوب إليه من هذا القول في حضرة
الرسول الأكرم (!!)، كيف لي أن أقنع نفسي وضميري الحر(!) بأن عمر بن الخطاب كان
عفوياً في حين أن أصحابه ومن حضروا محضره بكوا لما حصل حتى بل دمعهم الحصى وسموها
رزية المسلمين، ولهذا فقد خلصت إلى أن أرفض كل التعليلات التي قدمت لتوجيه ذلك،
ولقد حاولت أن أنكر هذه الحادثة وأكذبها لأستريح من مأساتها (!) ولكن كتب الصحاح
نقلتها وأثبتتها وصححتها ولم تحسن تبريرها ))(21)!
هاهو التيجاني يدلي بوعائه ليخرج لنا قيحه
الذي سود به صفحات كتابه، ولم يدر أنه بكلامه هذا قد خلع ربقة الإسلام من عنقه!
فكيف يدعي أن رسول الله صلى الله عليه وآله وسلم رأى عدم الجدوى من
كتابة الكتاب واقتضت حكمته ذلك (( هكذا!! )) بحجة أن الصحابة ( لن ) يحترموه و( لن
) يمتثلوا أمره بالإضافة إلى طعنهم به!! ولو فرضنا ( اعتباطاً ) أن هذا حق فكيف
يتوقف النبي صلى الله عليه وآله وسلم عن كتابة ما أمر ببلاغه وهو
الرسول المبلغ عن رب العالمين؟ وليس هو مخيرٌ في ذلك والله يقول { يأيها الرسول
بلغ ما أنزل إليك من ربك، وإن لم تفعل فما بلغت رسالته، والله يعصمك من الناس ...}
( المائدة 67) ويقول سبحانه { وما ينطق عن الهوى إن هو إلا وحي يوحى } ( النجم 3ـ
4) فلا بد للنبي صلى الله عليه وآله وسلم من التبليغ سواءٌ بالكتابة أو
بالقول كما أمرهم بإخراج المشركين من جزيرة العرب وغيره، وادعاء التيجاني هذا هو
طعن بالنبي صلى الله عليه وآله وسلم إذ كيف يتوقف عن التبليغ لمجرد
الطعن به؟! ومن قرأ كتاب الله يعلم مدى جهل هذا التيجاني بحقيقة الرسالة لأن الرسل
جميعاً تعرضوا من أقوامهم لشتى أنواع التعذيب الجسدية والنفسية فلم تثنيهم هذه
العذابات عن المضي قدماً بتبليغ رسالة الله، ونبينا محمد صلى الله عليه وآله
وسلم خاتم الأنبياء قد تعرض لأنواع من الاغراءات ثم التهديدات والتعذيب
ليثنيه المشركون عن تبليغ رسالة السماء، فقاموا بالاعتداء عليه وعلى أصحابه
وتعذيبهم وحاصروه وقومه بشعاب مكة ورموه بألقاب السخرية والاستهزاء كالساحر
والمجنون فلم تقف هذه الضغوط في طريقه ليبلغ دين الله كاملاً غير منقوص وجاهد في
سبيل الله مع أصحابه حتى مكن الله له في الأرض وجعل دينه يعلوا على كل الأديان
وبذلك استحق أن يكون خير رسل الله أجمعين، ثم يأتي هذا الرويبض ليدعي على نبي
المرحمة صلوات الله وسلامه عليه أنه توقف عن تبليغ أمر الله عاصماً للأمة من
الضلالة! لماذا؟ لمجرد عدم احترامه وإطاعة أمره أو الطعن به يتراجع عن تبليغ ما
أمر ببيانه! فحاشا نبينا صلى الله عليه وآله وسلم ذلك، فلا بد من أن
يبلغ الرسالة وأن يظهر الحق وإن حاربه أهل الأرض جميعاً وليظهر أهل الحق من أهل
الباطل ويعرف أولياءه من أعدائه، فمن اتبع أمر الله ورسوله نجا ومن خالف فقد هلك
ولذلك أنزل الله الرسل مبشرين للناس ومنذرين، ومن هنا نعلم أن الذي أراد النبي صلى
الله عليه وآله وسلم كتابته ليس وحياً بل على سبيل الاختيار ذلك لمن كان له
قلب أو ألقى السمع وهوشهيد، ثم يدعي هذا التيجاني على الصحابة بأنهم لم يحترموا
النبي صلى الله عليه وآله وسلم ولم يمتثلوا لأمره وطعنوا به!!؟ فيبدوا
أن الكلام عند هذا التيجاني لا يشترى بالمال فلا غضاضة إذاً من تسويد الصفحات
بالمجـازفات والافتراءات، فمرة يقول أن ابن عباس بكى وبل دمعه الحصى ومـرة يقول أن
الصحابة بكوا حتى بل دمعهم الحصى وفي نفس الوقت يخططـون لمنـع النبي صلى الله
عليه وآله وسلم من الكتابـة وأكثرهم كانوا على رأي عمر إلى آخر هذه التجنيات
التيجانية!!