‘Ayaat Madhluumah’ (Aya zilizodhulumiwa).
|
Maneno aliyofundishwa Aadam |
Shukrani zote ni zake Mola wa uliwengu wote, na mwisho mwema ni wa wamchao Mwenyezi Mungu, na hapana uadui isipokuwa kwa madhalimu.
Nashuhudia kuwa hapana anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Allaah Peke yake Asiye na mshirika mwenye Ufalme na haki iliyo wazi, na nashuhudia kuwa Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) ni mjumbe wake na Mtume wake na mwisho wa wajumbe wake, na ni kiongozi wa wacha Mungu. Mola wetu mswalie na msalimie Mtume wako huyu pamoja na Masahaba wake na kila atakayemfuata kwa wema na uongofu mpaka Siku ya Qiyaama.
Amma baad,
Hakika Mwenyezi Mungu Amemtuma Mtume Wake Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) awe dalili iliyo wazi juu ya waja Wake wote, na awabainishie yale aliyoteremshiwa katika Kitabu, na awe mfano mwema wa kuigwa na walimwengu wote, na ili watu wapate kuwa na muongozo mwema katika dini yao na dunia yao.
Ametumwa kutufundisha itikadi sahihi pamoja na hekima kwa ajili ya kutengenea hali za umma wake na kuwaweka juu ya njia safi na sahihi, ili watu wawe juu ya kitanga cheupe, mchana wake sawa na usiku wake, na asende kinyume na njia hiyo isipokuwa mpotofu.
Wakaifuata njia hiyo Masahaba wake (Radhiya Llaahu ‘anhum) na wale waliokuja baada yao na waliowafuatilia kwa wema. Wakaisimamisha sheria ya Mwenyezi Mungu na kuyakamata mafundisho hayo kwa magego yao kwa kuifuata itikadi hii sahihi, na ibada na mwenendo na tabia. Na sisi Alhamdulillah tunaendelea kuufuata mwenendo wao huo kwa kufuata dalili zilizomo ndani ya Qur-aan na zilizomo ndani ya mafundisho yake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam), na tunamuomba Mwenyezi Mungu Atuthibitishe juu ya njia hiyo sisi na ndugu zetu wote wa Kiislamu kwa kauli iliyo thabit katika maisha ya duniani na ya akhera na Atumiminie rehma Zake kwani yeye ni Mwenye kutoa kwa wingi.
Namshukuru Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala kwa kuniwezesha kutafsiri baadhi ya maudhui ndani ya kitabu hiki adhimu chenye faida nyingi sana, ‘Ayaat Madhluumah’ (Aya zilizodhulumiwa). Kimepewa jina hilo kwa sababu ndani ya Qurani tukufu zimo aya nyingi ambazo Waislamu wengi hawakuzifahamu maana yake vizuri na kwa sababu wasiokuwa Waislamu wale wenye kuudurusu Uislamu kwa ajili ya kuupiga vita, wanatumilia kutofahamika vizuri kwa aya hizi katika kuwagawa na kuingiza shaka ndani ya nafsi dhaifu.
Kitabu hiki kimeandikwa na Dr. ‘Umar bin ‘Abdil-‘Aziyz Qurayshi na kimepitiwa na Sheikh Dr. ‘Aidh Al-Qarniy mwanachuoni maarufu kutoka Saudia na ni mwandishi wa kitabu maarufu ‘Don’t be sad’ (Usihuzunike) na vitabu vinginevyo
Nimeamua kutafsiri baadhi ya maudhui muhimu yaliyomo ndani ya kitabu hiki (juu ya kuwa yote yaliyomo ni muhimu) kwa sababu ya kukithiri kufahamika vibaya maana ya nyingi kati ya aya za Qur-aan tukufu kutokana na ujinga uliokithiri kati ya Waislamu hasa katika wakati wetu huu, na muhimu zaidi ni kuwa nyingi kati ya aya zilizofahamika vibaya ni zile za misingi katika dini, na kwa ajili hiyo wale wanaopenda kufuata matamanio ya nafsi zao wakaichukua fursa hii na kuanza kujipoteza na kutaka kuwapoteza wenzao.
Kama tunavyoelewa kuwa maadui wa Uislamu wana msemo wao ‘Wagawe uweze kuwatawala’, kwa njia hiyo Waislamu wakagawanyika makundi mbali mbali, na maadui wa Uislamu wakaichukuwa fursa hii kuzidi kuwatenganisha.
Namuomba Mwenyezi Mungu Aniwezeshe kuyafikisha maana ya aya hizi kwa usahihi na Aijaalie kazi hii iwe halisi kwa ajili Yake na iwe katika mezani ya amali zangu njema na za kila msomaji siku ya Qiyaama – Aamin.
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóÅöÐú
ÞóÇáó ÑóÈøõßó áöáúãóáÇÆößóÉö Åöäøöí ÌóÇÚöáñ Ýöí ÇáÃóÑúÖö ÎóáöíÝóÉð ÞóÇáõæÇ
ÃóÊóÌúÚóáõ ÝöíåóÇ ãóäú íõÝúÓöÏõ ÝöíåóÇ æóíóÓúÝößõ ÇáÏøöãóÇÁó æóäóÍúäõ äõÓóÈøöÍõ
ÈöÍóãúÏößó æóäõÞóÏøöÓõ áóßó ÞóÇáó Åöäøöí ÃóÚúáóãõ ãóÇ áÇ ÊóÚúáóãõæäó ![]()
“Na pale Mola wako Mlezi Alipowaambia Malaika: Mimi nitamweka katika ardhi Khalifa (mfwatizi), wakasema: Utaweka humo atakayefanya uharibifu humo na kumwaga damu, hali sisi tunakutakasa kwa sifa Zako na tunakutaja kwa utakatifu wako? Akasema: Hakika Mimi nayajua msiyoyajua” Al Baqarah : 30
Maadui wa Kiislamu wakasema kuwa eti hapa Malaika wanambishia Mwenyezi Mungu, wakasahau kuwa kumbishia Mwenyezi Mungu si kitendo cha kuasi tu, bali ni kitendo cha kufru kubwa mfano wa kitendo cha Iblisi aliyelaaniwa.
Sisi tunasema kuwa msijaribu kuwakanganya watu, kwa sababu Malaika hawawezi kufanya kitendo cha kumbishia Mwenyezi Mungu, kwani wao wameumbwa kwa ajili ya kutii tu, na wamekingwa na kufanya uasi wa aina yoyote ile.
Mwenyezi Mungu Amesema juu yao:
áÇ
íóÚúÕõæäó Çááøóåó ãóÇ ÃóãóÑóåõãú æóíóÝúÚóáõæäó ãóÇ íõÄúãóÑõæäó![]()
“Hawamuasi Mwenyezi Mungu kwa Anayowaamrisha, na wanatenda wanayoamrishwa”. At-Tahriym. 6
Na Akasema:
æóãóäú ÚöäÏóåõ áóÇ íóÓúÊóßúÈöÑõæäó Úóäú ÚöÈóÇÏóÊöåö æóáóÇ íóÓúÊóÍúÓöÑõæäó íõÓóÈøöÍõæäó Çááøóíúáó æóÇáäøóåóÇÑóáóÇ íóÝúÊõÑõæäó
“Na walioko Kwake hawafanyi kiburi wakaacha kumuabudu, wala hawachoki. Wanamtakasa usiku na mchana, wala hawanyong'onyei” Al-Anbiyaa: 19 -20
Na Akasema:
Èóáú ÚöÈóÇÏñ ãøõßúÑóãõæäó áóÇ íóÓúÈöÞõæäóåõ ÈöÇáúÞóæúáö æóåõã ÈöÃóãúÑöåö íóÚúãóáõæäó íóÚúáóãõ ãóÇ Èóíúäó ÃóíúÏöíåöãú æóãóÇ ÎóáúÝóåõãú æóáóÇ íóÔúÝóÚõæäó ÅöáøóÇ áöãóäö ÇÑúÊóÖóì æóåõã ãøöäú ÎóÔúíóÊöåö ãõÔúÝöÞõæäó
“Bali hao (wanaowaita wana) ni watumwa waliotukuzwa. Hawamtangulii kwa neno, nao wanafanya amri Zake.Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao. Wala hawamwombei yeyote ila yule Anayemridhia Yeye, nao kwa ajili ya kumwogopa wananyenyekea.” Al-Anbiyaa: 26-28
Na Akasema juu yao:
íóÎóÇÝõæäó ÑóÈøóåõã ãøöä ÝóæúÞöåöãú æóíóÝúÚóáõæäó ãóÇ íõÄúãóÑõæäó
“Vinamkhofu Mola wao Mlezi Aliye juu yao, na vinafanya vinavyoamrishwa.” An-Nahl: 50
Ikiwa hii ndiyo hali yao, na zile ndiyo sifa zao, na kwamba hawamuasi Mola wao, itakuwaje basi waibishie amri ya Mola wao aliyewaumba na kuikanusha hekima ya Mola wao? Kisha wajifanye wanajua zaidi kupita Mola wao? Haiwezekani kabisa kwao kutenda hayo.
Huenda ikawa hekima ya Malaika wale kumuuliza Mola wao juu ya kiumbe kile na vizazi vyake ni kutaka kujua uhusiano utakaokuwa baina yao na viumbe vile, hasa kwa vile mara baada ya kuumbwa kiumbe kile, Malaika waliamrishwa kumsujudia.
Na Mwenyezi Mungu Alijaalia pia wakati ule kuwepo Malaika wote wakubwa kama vile Wenye kuhifadhi na Wenye kuandika na Malaika wa wahyi na wa mvua na wa adhabu na wa mauti…. Wote hawa watakuwa na uhusiano wa daima na kiumbe huyu mpya katika maisha yake yote kwa ujumla.
Suali lao halikuwa na maana ya kupinga au kubisha au kukataa, hasa tukitambua kuwa kumbishia Mwenyezi Mungu ni kufru aliyoifanya Ibilisi aliyelaaniwa.
Waliuliza kwa sababu hawakuilewa hekima ya kuumbwa kiumbe hiki kipya, kwa hivyo wakataka kujuwa; kwa nini Allaah Anaumba kiumbe kingine? Je wao walipunguza haki yoyote katika amri za Mwenyezi Mungu ndiyo sababu iliyomfanya Mwenyezi Mungu Akataka kuumba kiumbe kingine?
Hapo ndipo walipouliza kwa kutaka kujua.
Kwa vile hata kabla ya kuumbwa binaadamu huyo, Malaika waliitaja sifa yake kuwa atafanya uharibifu, huenda ikawa ni kwa sababu Mola wao keshawajulisha hayo.
Pengine walielewa kuwa; kwa vile kiumbe huyu ameumbwa kwa udongo na ataishi juu ya ardhi, bila shaka watakuwa na tabia ya kheri na shari, na kwa ajili hiyo bila shaka yatatokea mapambano baina yao, na uharibifu na ufisadi.
Lakini pale Malaika walipojulishwa sababu ya kuumbwa kiumbe huyo na walipotambua namna Mwenyezi Mungu Alivyompa uwezo wa kupata maarifa na elimu, walimsujudia sajdah ya heshima na kufuata maamrisho ya Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala).
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóÅöÐú ÞõáúäóÇ áöáúãóáÇóÆößóÉö ÇÓúÌõÏõæÇú áÂÏóãó ÝóÓóÌóÏõæÇú ÅöáÇøó ÅöÈúáöíÓó ÃóÈóì æóÇÓúÊóßúÈóÑó æóßóÇäó ãöäó ÇáúßóÇÝöÑöíäó
“Na tulipowaambia Malaika: Msujudieni Adam, wakamsujudia wote isipo kuwa Iblis, alikataa na akajivuna na akawa katika makafiri." Al Baqarah: 34
Hata aya hii wakaifanya kama ni dalili nyingine ya kuwababaisha watu kuwa eti Malaika wanafanya maasi.
Wakasema kuwa eti Ibilisi ambaye ni Malaika! Hakufuata amri ya Mwenyezi Mungu. Ibilisi aliyepinga alipokisia baina yake na baina ya Adam kwa akili yake iliyofisidika akasema:
ÃóäóÇú ÎóíúÑñ ãøöäúåõ ÎóáóÞúÊóäöí ãöä äøóÇÑò æóÎóáóÞúÊóåõ ãöä Øöíäò
“Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, naye umemuumba kwa udongo” Al-’Aaraaf : 12
Kwa ajili hiyo akastahiki kutolewa katika rehma ya Mwenyezi Mungu na Pepo Yake. Kama ilivyokuja katika aya nyingi ndani ya Qur-aan Tukufu.
Kwa hivyo tunasema; na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuleta tawfiyq kuwa; Mwenye kudai kuwa Ibilisi alikuwa Malaika, huyo amepotea, na hakuifahamu Qur-aan vizuri, na hii ni kwa sababu Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) keshatoa uamuzi Wake katika kadhia hii, na haijuzu kutanguliza kauli ya mwanadamu mbele ya kauli ya Mwenyezi Mungu au Mtume Wake (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam). Na haya yanapatikana katika Suratul-Kahf aliposema:
æóÅöÐú ÞõáúäóÇ áöáúãóáóÇÆößóÉö ÇÓúÌõÏõæÇ áöÂÏóãó ÝóÓóÌóÏõæÇ ÅöáøóÇ ÅöÈúáöíÓó ßóÇäó ãöäó ÇáúÌöäøö ÝóÝóÓóÞó Úóäú ÃóãúÑö ÑóÈøöåö ÃóÝóÊóÊøóÎöÐõæäóåõ æóÐõÑøöíøóÊóåõ ÃóæúáöíóÇÁ ãöä Ïõæäöí æóåõãú áóßõãú ÚóÏõæøñ ÈöÆúÓó áöáÙøóÇáöãöíäó ÈóÏóáÇð
“Na Tulipowaambia Malaika: Msujudieni Aadam! Walimsjudia isipokuwa Iblisi. Yeye alikuwa miongoni mwa majini, na akavunja amri ya Mola wake Mlezi. Je! Mnamshika yeye na dhuriya zake kuwa marafiki badala yangu, hali wao ni adui zenu? Ni ovu mno badala hii kwa wenye kudhulumu.” Al Kahf: 50.
Baada ya ukweli huu ulio wazi usiopingika, mtu anaweza tena kusema kuwa eti Ibilisi ni katika Malaika? Au anaweza kuzirudia zile kauli za Israiliyaat kuwa Ibilisi alikuwa Tausi wa Malaika na mwenye elimu kupita Malaika wote na mcha Mungu kupita Malaika wote na maneno mengine ya mfano huo?
Itakuwaje, wakati Ibilisi amekhitilafiana na Malaika kwa maumbile na tabia na mwanzo na mwisho na katika uhai na katika mwelekeo!
Kuna kushabihiana gani baina ya Ibilisi na Malaika? Wakati wao wameumbwa kwa nuru na yeye ameumbwa kwa moto? Wao hawamuasi Mola wao na wanafanya wanavyoamrishwa, wakati yeye amepinga amri ya Mola Wake na kuibishia hukumu ya Mola Wake. Wao hawaoi wala hawazai, wakati yeye anaoa na anao watoto, wakiwa upande wa maadui wa Mwenyezi Mungu.
Wao ni viumbe wasiofanya kiburi wakaacha kumuabudu Mola wao na wala hawachoki, wakati yeye alikataa na akajivuna na akawa miongoni mwa makafiri. Wao ni wenye kumtakasa Mola wao usiku na mchana, wala hawanyong'onyei, wakati yeye hima yake yote ni kwapoteza waja wa Mwenyezi Mungu, baada ya kuapa kwa utukufu wa Mwenyezi Mungu kuwa atawapoteza watu wote isipokuwa wale asioweza kuwafikia katika watu wema. Na yeye ni yule asiyeiacha njia yoyote wala mlango wowote wa kuwapoteza viumbe isipokuwa ataufuata na kuingia kwa ajili ya kuwafikia.
Mwenyezi Mungu Anasema:
ÞóÇáó ÝóÈöãóÇ ÃóÛúæóíúÊóäöí áÃóÞúÚõÏóäøó áóåõãú ÕöÑóÇØóßó ÇáúãõÓúÊóÞöíãó Ëõãøó áÂÊöíóäøóåõã ãøöä Èóíúäö ÃóíúÏöíåöãú æóãöäú ÎóáúÝöåöãú
æóÚóäú ÃóíúãóÇäöåöãú æóÚóä ÔóãóÂÆöáöåöãú æóáÇó ÊóÌöÏõ ÃóßúËóÑóåõãú ÔóÇßöÑöíäó
“Akasema: Kwa kuwa umenihukumia upotofu, basi nitawavizia katika Njia yako Iliyonyooka. Kisha nitawazukia mbele yao na nyuma yao na kuliani kwao na kushotoni kwao. Wala hutawakuta wengi wao wenye shukrani” Al-A’araf: 16-17.
Tofauti zote hizi zilizotajwa baina ya Malaika na Ibilisi zinamfanya Ibilisi asiweze kuwa Malaika hata kidogo, tukiongezea ile hukmu Aliyoitoa Mwenyezi Mungu juu yake Aliposema:
ÞóÇáó ÇÎúÑõÌú ãöäúåóÇ ãóÐúÄõæãÇð ãøóÏúÍõæÑÇð áøóãóä ÊóÈöÚóßó ãöäúåõãú áÃóãúáÃäøó Ìóåóäøóãó ãöäßõãú ÃóÌúãóÚöíäó
“Akasema: Toka humo, nawe umekwisha fedheheka, umekwisha fukuzwa. Hapana shaka atakaye kufuata miongoni mwao, basi nitaijaza Jahannam kwa nyinyi nyote.”
Al-A’araf: 18.
linabakia suala moja, nalo ni kuwa; Ikiwa Ibilisi si Malaika pana hekima gani iliyojificha hata Mwenyezi Mungu Akasema , “wakamsujudia wote isipokuwa Ibilisi?”
Tunasema; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuleta tawfiyq; hii katika Lugha ya Kiarabu inaitwa ‘istithnaa munqati’a’, (kielezi kilichokatika), na mfano wake kama wanavyosema wataalamu wa Lugha kuwa mfano mtu anaposema: ‘Walikuja wote isipokuwa punda,’ au; ‘Akayala matufaha yote isipokuwa chungwa.’ Na pakasemwa; ‘wakamsujudia wote isipo kuwa Ibilisi’.
Kwa hivyo tunasema; Malaika walipewa amri ya kumsujudia Aadam, na Ibilisi alikuwa pamoja nao (lakini hakuwa mmoja wao – hakuwa mwenzi wao – hakuwa Malaika kama wao), kama tulivyoona katika dalili mbali mbali, na kwa vile wakati ule alikuwa pamoja na Malaika, na alikuwa peke yake miongoni mwa Malaika wengi, ikambidi na yeye asujudu pia, lakini alikataa kwa sababu asili yake kwa kuwa yeye ameumbwa kwa moto na hakuumbwa kwa nuru kama walivyoumbwa Malaika, asili yake ikamzidi nguvu, akaanza kukisia na kupima akajifadhilisha, na matokeo yake akaangamia. Ndiyo maana akapata laana ya Mwenyezi Mungu na ya watu wote.
Mwenyezi Mungu Anasema:
æóÞõáúäóÇ íóÇ ÂÏóãõ ÇÓúßõäú ÃóäÊó æóÒóæúÌõßó ÇáúÌóäøóÉó æóßõáÇó ãöäúåóÇ ÑóÛóÏÇð ÍóíúËõ ÔöÆúÊõãóÇ æóáÇó ÊóÞúÑóÈóÇ åóÜÐöåö ÇáÔøóÌóÑóÉó ÝóÊóßõæäóÇ ãöäó ÇáúÙøóÇáöãöíä ÝóÃóÒóáøóåõãóÇ ÇáÔøóíúØóÇäõ ÚóäúåóÇ ÝóÃóÎúÑóÌóåõãóÇ ãöãøóÇ ßóÇäóÇ Ýöíåö æóÞõáúäóÇ ÇåúÈöØõæÇú ÈóÚúÖõßõãú áöÈóÚúÖò ÚóÏõæøñ æóáóßõãú Ýöí ÇáÃóÑúÖö ãõÓúÊóÞóÑøñ æóãóÊóÇÚñ Åöáóì Íöíäò
“Na tulisema: Ewe Aadam! Kaa wewe na mkeo katika Bustani, na kuleni humo maridhawa popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu tu; mkawa katika wale waliodhulumu. Lakini Shaytwaan aliwatelezesha hao wawili na akawatoa katika waliyokuwamo, na tukasema: Shukeni, nanyi ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Katika ardhi yatakuwa makaazi yenu na starehe kwa muda.” Al-Baqarah: 35-36.
Aya hii ilifahamika vibaya kutokana na hadithi za Israiliyaat (zilizosimuliwa na watu wa bani Israil kama walivyonukuu ndani ya Taurat). Imepokelewa katika riwaya za Israiliyaat maelezo ya mti aliokula tunda lake Aadam (‘Alayhis Salaam) kuwa ni mti wa ngano au mzabibu au tini nk.
Na imepokelewa pia katika Israiliyaat juu ya maelezo ya wasiwasi wa Ibilisi kwa Aadam kuwa hakuweza kumtia wasiwasi mpaka alipofanikiwa kuingia ndani ya mdomo wa nyoka, na nyoka wakati huo alikuwa na miguu mine mfano wa ngamia.
Imepokelewa katika Israiliyaat pia kuwa;
Na Ibilisi alipoingia Peponi pamoja na nyoka huyo alifanikiwa kumbabaisha Hawwaa na Hawwaa akaweza kumbabaisha Aadam!! Wote wawili wakala tunda, wakajikuta wako uchi, Aadam akajificha ndani ya mti, na Mwenyezi Mungu Akawa Anaita:”Uko wapi ewe Aadam.!!!”
Aadam akasema: “Nakuonea haya ewe Mola wangu kwani mimi niko uchi.” Akamuambia: “Isije kuwa umekula lile tunda nilokukataza?”
Mwenyezi Mungu Akamkasirkia nyoka yule aliyeingia Ibilisi ndani ya mdomo wake akamuambia: “Umelaaniwa wewe. Kuanzia leo miguu yako ni tumbo lako. Utasota juu ya ardhi na chakula chako kitakuwa ndani ya udongo, na uadui baina yako na wanadamu utakuwa wa milele.”
Kisha akamuangalia Hawwaa akamuambia: “Umelaaniwa wewe, umembabaisha mja wangu Aadam akala tunda la mti nilomkataza asile, kuanzia leo utabeba mimba kwa dhiki, na hutozaa mpaka utakapoyaona mauti mbele yako.”
Ukweli ni kuwa kilichotangulia ni mojawapo ya visa vya Israiliyaat vilivyonukuliwa katika Taurat iliyobadilishwa na kugeuzwa.. Hapana ndani ya Qur-aan dalili yoyote kuwa Hawwaa ndiye aliyembabaisha Aadam, na wala hapana mahali popote alipotuhumiwa Hawwaa, bali Mwenyezi Mungu Amesema:
ÝóÃóßóáóÇ ãöäúåóÇ
“Basi wakaula wote wawili.” Twahaa: 120.
Wote wawili kwa pamoja walikula.
Na ili Ibilisi aweze kuwababaisha Aadam na Hawwaa haikuwa lazima kwake aingie Peponi kupitia ndani ya mdomo wa nyoka au wa mnyama yeyote, kwa sababu ili kuingiza wasiwasi hapana lazima ya kukaribiana wala kugusana, bali wasiwasi unaweza kufanyika kwa mbali na kwa karibu pia.
Na nyoka huyu yuko vile vile tokea Alipoumbwa na Mwenyezi Mungu, hakuwa na miguu wala kitu cha kusimamia, bali yupo kama Alivyosema Mwenyezi Mungu:
æóÇááøóåõ ÎóáóÞó ßõáøó ÏóÇÈøóÉò ãöä ãøóÇÁ Ýóãöäúåõã ãøóä íóãúÔöí Úóáóì ÈóØúäöåö æóãöäúåõã ãøóä íóãúÔöí Úóáóì ÑöÌúáóíúäö æóãöäúåõã ãøóä íóãúÔöí Úóáóì ÃóÑúÈóÚò íóÎúáõÞõ Çááøóåõ ãóÇ íóÔóÇÁ Åöäøó Çááøóåó Úóáóì ßõáøö ÔóíúÁò ÞóÏöíÑñ
“Na Mwenyezi Mungu Ameumba kila kinyama kutokana na maji. Wengine katika wao huenda kwa matumbo yao, na wengine huenda kwa miguu miwili, na wengine huenda kwa miguu mine. Mwenyezi Mungu Huumba Ayatakayo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.” An-Nuur: 45.
Kwa hivyo haya yote yanatokana na hadithi za Israiliyaat zilizojaa ndani ya vitabu vya tafsiri ambazo Waislamu lazima watahadharishwe nazo.
Mwenyezi Mungu Anasema:
ÝóÊóáóÞøóì ÂÏóãõ ãöä ÑøóÈøöåö ßóáöãóÇÊò ÝóÊóÇÈó Úóáóíúåö Åöäøóåõ åõæó ÇáÊøóæøóÇÈõ ÇáÑøóÍöíãõ
“Kisha Aadam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na Mola wake Mlezi Alimkubalia toba yake; hakika Yeye ndiye Mwingi wa kukubali toba na Mwenye kurehemu.” Al-Baqarah: 37.
Sababu ya kufahamika vibaya aya hii ni baadhi ya hadithi za Israiliyaat na hadithi ‘maudhu’u’ hadithi za uongo zilizopachikwa tu, katika tafsiri ya aya hii, zilizosababisha kufahamika vibaya, na kwa ajili hiyo zikapatikana hukmu mbaya zinazowaingiza watu katika mambo ya shirk na katika aina za shirk.
Miongoni mwa visa hivyo vya uongo ni kile kisa kinachosema kuwa; Aadam alipoasi na kula katika mti ule, akatizama katika nguzo za ‘Arshi akaliona jina la Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) liko karibu na jina la Mwenyezi Mungu, au akaona imeandkwa:
áÇ Åáå ÅáÇ Çááå ãÍãÏ ÑÓæá Çááå
Laa ilaaha illa Llaah Muhammadan RasuluLlaah
Aadam akasema: “Ewe Mola wangu kwa haki ya Muhammad nisamehe.”
Allaah Akamuambia: Umemjuaje Muhammad wakati bado sijamuumba?”
öAadam akasema: “Ewe Mola wangu uliponiumba kwa mikono yako kisha ukanipulizia roho inayotokana na wewe, nilipoinua kichwa changu nikaona katika nguzo za ‘Arshi imeandikwa ‘Laa ilaaha illa Llaah Muhammadan RasuluLlaah’ nikaelewa kuwa huongezi pamoja na jina lako isipokuwa jina la kiumbe unayempenda kupita viumbe vyote.”
Mwenyezi Mungu Akasema: “Umesema kweli ewe Aadam. Huyu ni kiumbe ninayempenda kupita viumbe vyote. Niombe kwa haki yake na nishakusamehe, na lau kama si Muhammad basi nisingekuumba.”
Zimepokelewa zaidi ya riwaya moja juu ya kisa hiki, Maulamaa wote ‘Ij’mai’ wanasema kuwa hadithi hii ni ‘maaudhu’u’ hadithi ya uongo iliyopachikwa tu, na wala hapana ibra yoyote kwa anayejaribu kuisahihisha, kwa sababu Qur-aan inaikanusha hadithi.
Mwenyezi Mungu Anasema:
ÝóÊóáóÞøóì ÂÏóãõ ãöä ÑøóÈøöåö ßóáöãóÇÊò ÝóÊóÇÈó Úóáóíúåö
“Kisha Aadam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na Mola wake Mlezi Alimkubalia toba yake.”
Al Baqarah – 37
Kwa hivyo, Aadam alipokea maneno kutoka kwa Mola wake na Mola wake ndiye aliyemfundisha kutamka maneno hayo. Aadam hakujitahidi mwenyewe kuyatafuta maneno hayo wala hakuyavumbua yeye. Na maneno haya hayakuwa: “kwa haki ya Muhammad nisamehe.” Wala si kwa haki ya yeyote kati ya wanaozuwa, bali ni maneno aliyosema Mwenyezi Mungu Aliposema:
ÞóÇáÇó ÑóÈøóäóÇ ÙóáóãúäóÇ ÃóäÝõÓóäóÇ æóÅöä áøóãú ÊóÛúÝöÑú áóäóÇ æóÊóÑúÍóãúäóÇ áóäóßõæäóäøó ãöäó ÇáúÎóÇÓöÑöíäó
“Wakasema: Mola wetu Mlezi! tumejidhulumu nafsi zetu, na kama hutusamehe na kuturehemu, hakika tutakuwa katika wenye kukhasirika.” Al-A’araaf: 23.
Na haya ndiyo walioyasema Maulamaa waliofanya tahakiki miongoni mwa wanaotafsiri Qur-aan na wakakubaliana. Na kama inavyosemwa; ‘njia bora ya kufasiri Qur-aan ni kwa Qur-aan.
Kwa hivyo Aadam alipokea maneno kutoka kwa Mola wake kama yalivyowekwa wazi na Mola wetu. Hapana haja ya kufanya ijtihadi wala kujidai katika jambo hili.
Na ubaya mkubwa zaidi katika jambo hili ni kuwa njia yao hii inaweza kuwapeleka katika shirk.
Mwenyezi Mungu Anasema:
áóÞóÏú ÌöÆúÊõãú ÔóíúÆÇð ÅöÏøÇð ÊóßóÇÏõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊõ íóÊóÝóØøóÑúäó ãöäúåõ æóÊóäÔóÞøõ ÇáúÃóÑúÖõ æóÊóÎöÑøõ ÇáúÌöÈóÇáõ åóÏøÇð
“Hakika mmeleta jambo la kuchusha mno! Zinakaribia mbingu kutatuka kwa hilo, na ardhi kupasuka, na milima kuanguka vipande vipande.” Maryam: 89-90.
Kutokana na hadithi kama hizo watu wakaanza kuomba kwa Haki ya Muhammad na kwa jina la Muhammad na kwa Jaha ya Muhammad na hata kwa majina ya Mitume wengine na Mawalii, wakaisahau Haki ya Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) na Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Tawhiyd Yake.
Mwenyezi Mungu Anasema:
Åöäøó ÇáÕøóÝóÇ æóÇáúãóÑúæóÉó ãöä ÔóÚóÂÆöÑö Çááøåö Ýóãóäú ÍóÌøó ÇáúÈóíúÊó Ãóæö ÇÚúÊóãóÑó ÝóáÇó ÌõäóÇÍó Úóáóíúåö Ãóä íóØøóæøóÝó ÈöåöãóÇ æóãóä ÊóØóæøóÚó ÎóíúÑÇð ÝóÅöäøó Çááøåó ÔóÇßöÑñ Úóáöíãñ
“Hakika vilima vya Swafaa na Marwa ni katika alama za Mwenyezi Mungu. Basi anayehiji kwenye Nyumba hiyo au akafanya ‘Umrah, si kosa kwake kuvizunguka. Na anayejitendea mwenyewe kheri basi bila ya shaka Mwenyezi Mungu ni Mwenye shukrani na Mjuzi.” Al-Baqarah: 158.
Aya hii ni miongoni mwa Aya zinazoweza kufahamika vibaya, kwa sababu dhahiri yake inaonyesha kama kwamba ‘Sa’ayi’ (kutufu baina ya Swafaa na Marwa) si kitendo cha lazima katika Hija wala katika ‘Umrah, na kwamba si kosa kutufu baina yake, lakini ni kitendo kinachopendeza tu, kama aya ilivyosema: “si kosa kwake kuvizunguka.”
Ukweli ni kuwa tasfiri hiyo ya kuwa ‘Saa’yi’ baina ya Swafaa na Marwa si kitendo kilichowajibika siyo sahihi na aya haijakusudiwa hivyo.
Inaifasiri vizuri aya hiyo Hadithi iliyosimuliwa na Imaam Ahmad kutoka kwa ‘Urwah (Radhiya Llaahu ‘anhu) kutoka kwa mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Llaahu ‘anha) kuwa amesema:
“Umeisikia kauli ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka isemayo: “Hakika vilima vya Swafaa na Marwa ni katika alama za Mwenyezi Mungu. Basi anayehiji kwenye Nyumba hiyo au akafanya ‘Umrah, si kosa kwake kuvizunguka.” Nikasema; WaLlaahi hapana ubaya kwa mtu yeyote ikiwa hajatufu baina yake (vilima hivyo).
Akasema mama wa Waumini ‘Aaishah: “Umesema vibaya kabisa ewe mwana wa dada yangu. Ikiwa maana yake kama ulivyoidhania, basi pangesemwa: ‘si kosa kwake ku(to)vizunguka vilima hivyo,’ lakini imeteremshwa kwa sababu watu wa Madiynah mahali pale walikuwa kabla ya kusilimu wakimuabudu Manata, na (baada ya kusilimu) ikawa wanapofika pale wanaona uzito kutufu (Sa’ayi) baina ya Swafaa na Marwa, ndipo Mwenyezi Mungu Mtukufu Alipoteremsha aya: “Hakika vilima vya Swafaa na Marwa….”
Akasema mama wa Waumini ‘Aaishah: “Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) akasunisha (akafundisha) kutufu mahali hapo. Na haijuzu kwa mtu kuacha kutufu mahali hapo.” Al-Bukhaariy na Muslim katika kitabu cha A- Hajj.
Na amesimulia Al-Bukhaariy kutoka kwa ‘Aaswim bin Sulaymaan, kasema: “Nilimuuliza Anas juu ya Swafaa na Marwa” akasema; “Tulikuwa tukiona kuwa ni matendo ya wakati wa ujahilia (kabla ya kuja kwa Uislamu), na ulipokuja Uislamu tukajizuia kutufu mahali hapo, ndipo Mwenyezi Mungu Mtukufu Alipoteremsha: “Hakika vilima vya Swafaa na Marwa ni katika alama za Mwenyezi Mungu.” Al-Bukhaariy katika mlango wa Al-Hajj.
Na katika Sahih Muslim hadithi ndefu iliyosimuliwa na Jaabir (Radhiya Llaahu ‘anhu) alipokuwa akihadithia juu ya Hija ya mwisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) alisema: “… Na baada ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) kumaliza kutufu katika nyumba, alirudi katika nguzo akaigusa kisha akatoka kupitia mlango wa Swafaa huku akisema:
Åöäøó ÇáÕøóÝóÇ æóÇáúãóÑúæóÉó ãöä ÔóÚóÂÆöÑö Çááøåö
“Hakika vilima vya Swafaa na Marwa ni katika alama za Mwenyezi Mungu.”
Kisha akasema: “Naanzia pale alipoanzia Mwenyezi Mungu.” (Na maana yake ni kuwa kwa vile katika aya, Mwenyezi Mungu Ameanza kuitaja Swafaa kabla ya Marwa kwa hivyo na yeye Saaiy yake ataianzia Swafaa kabla ya Marwa.).
Na katika riwaya iliyosimuliwa na Imaam Ahmad, imepokelewa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) huku akifanya ‘Saa’ayi’ alikuwa akisema: “Fanyeni ‘Sa’ayi’ kwa sababu Mwenyezi Mungu Amekufaridhishieni ‘Sa’ayi’.” Ahmad na Ad-Daaraqutniy
Kutokana na hadithi hii, baadhi ya Maulamaa wakasema kuwa kitendo cha ‘Sa’ayi’ baina ya Swafaa na Marwa ni nguzo katika nguzo za Hija. Na haya ni katika Madhehebu ya Imaam Ash-Shafi’y na waliokubaliana naye.
Na imesemwa pia kuwa ni wajibu na si nguzo. Kwa hivyo mtu akiiacha kusudi au akiisahau anatakiwa achinje.
Na wengine wakasema kuwa ni vizuri mtu kutufu lakini si nguzo wala si wajibu, lakini kauli ya mwanzo (ya Imaam Ash-Shafi’y) ndiyo inayokubalika zaidi. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujua zaidi.
Mwenyezi Mungu anasema:
æóÅöäú ÎöÝúÊõãú ÃóáÇøó ÊõÞúÓöØõæÇú Ýöí ÇáúíóÊóÇãóì ÝóÇäßöÍõæÇ ãóÇ ØóÇÈó áóßõã ãøöäó ÇáäøöÓóÇÁ ãóËúäóì æóËõáÇóËó æóÑõÈóÇÚó ÝóÅöäú ÎöÝúÊõãú ÃóáÇøó ÊóÚúÏöáõæÇú ÝóæóÇÍöÏóÉð
“Na ikiwa mnaogopa kuwa hamtowafanyia mayatima uadilifu, basi oeni mnao wapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane. na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu.”
Annisaa -3
Mambo mawili yanawatatanisha watu katika aya hii, nayo ni:-
1. Uko wapo uhusiano baina ya kutowafanyia uadilifu mayatima na kuoa mke zaidi ya mmoja?
2. Si dhulma hii katika Uislamu kwa mwanamume aruhusiwe kuoa mke zaidi ya mmoja na mwanamke asiruhusiwe kuolewa na mume zaidi ya mmoja?
3. Kisha kuoa huku mke zaidi ya mmoja kumewekewa sharti la uadilifu. Mwenyezi Mungu Amesema: “Na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu.”
Na hili ni jambo lisilowezekana, kama ilivyoelezwa ndani ya Qurani katika sura hiyo hiyo.
Mwenyezi Mungu Amesema:
æóáóä ÊóÓúÊóØöíÚõæÇú Ãóä ÊóÚúÏöáõæÇú Èóíúäó ÇáäøöÓóÇÁ æóáóæú ÍóÑóÕúÊõãú ÝóáÇó ÊóãöíáõæÇú ßõáøó Çáúãóíúáö ÝóÊóÐóÑõæåóÇ ßóÇáúãõÚóáøóÞóÉö æóÅöä ÊõÕúáöÍõæÇú æóÊóÊøóÞõæÇú ÝóÅöäøó Çááøåó ßóÇäó ÛóÝõæÑÇð ÑøóÍöíãÇð
Wala hamtaweza kufanya uadilifu baina ya wake, hata mkikakamia. Kwa hivyo msimili moja kwa moja mkamwacha (mmojapo) kama aliye tundikwa. Na mkisikizana na mkamchamngu basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghfira na Mwenye kurehemu
Annisaa – 129
4. Na ikiwa kuoa huko zaidi ya mke mmoja kama ilivyoruhusiwa katika aya, kwa nini basi Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) alioa zaidi ya hao? Alioa wake tisa wakati mmoja.
Mambo haya yaliyowababaisha watu yaliyomo ndani ya aya hii ni dalili ya kufahamika vibaya kwa aya, na kutokana na haya kukatendeka aina nyingi za ufisadi na kufru. Na jambo hili wamelifanya Waislamu na wasiokuwa Waislamu, na pia makundi mbali mbali ya mafisadi, na kila anayetaka kuitia ila dini hii akatoka katika njia ya Mwenyezi Mungu.
Tunaanza kusahihisha kufahamika vibaya kwa aya hii kwa kujibu hoja moja baada ya nyingine, kwa haraka na kwa muhtasari.
Tunasema; huku tukimuomba Mwenyezi Mungu atusahilishie na atupe tawfiyq;
Kuhusu uhusiano baina ya kutowafanyia uadilifu mayatima na kuoa wake zaidi ya mmoja, kwa mwenye kuzizingatia vizuri aya kumi za mwanzo za Surat Annisaa, ataona kuwa karibu aya zote zinaelezea juu ya mayatima, na baada ya aya ya mwanzo ambayo ndani yake imejumuisha baina ya usia wa kumcha Mungu, aya ya pili ikaanza moja kwa moja kuzungumza juu ya mayatima, iliposema:
æóÂÊõæÇú ÇáúíóÊóÇãóì ÃóãúæóÇáóåõãú
“Na wapeni mayatima mali yao.”
Annisaa – 2
Na hizi ni aya zenye kuamrisha kuhifadhiwa kwa mali ya mayatima na kuzichunga vizuri zisipotee, na zinakataza kuikaribia isipokuwa kwa njia bora kwa ajili ya kuhifadhi mali hiyo au kuifanyia biashara tena kwa uadilifu. Uadilifu huo unatakiwa ufikie kiwango cha hali ya juu kilichowekewa na Uislamu katika utukufu wa sheria zake na namna ya kulea mayatima na madhaifu.
Na katika hadithi, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) amesema:
Åöäøöí ÃõÍóÑøöÌõ ÍóÞøó ÇáÖøóÚöíÝóíúäö: ÇáúíóÊöíãö æóÇáúãóÑúÃóÉö.
Mimi ninaharimisha (kupotea kwa) haki ya madhaifu wawili; Yatima na Mwanamke.
Ibni Majah na Ibni Hibban na Ahmad na Al Hakim na imesahihishwa na Adhahaby
Na mwanamke anapokuwa yatima, hapo anakuwa amejumuisha udhaifu mara mbili. Kwa ajili hiyo Uislamu ukaupa umuhimu mkubwa sana ‘haki za mayatima’ na ukasisitiza juu ya uadilifu mkubwa unaotakiwa katika kuhifadhi mali zao katika mandhari bora kupita zote zinazonasibiana na umuhimu wa sheria hii.
Ndipo Mwenyezi Mungu Aliposema:
æóÅöäú ÎöÝúÊõãú ÃóáÇøó ÊõÞúÓöØõæÇú Ýöí ÇáúíóÊóÇãóì ÝóÇäßöÍõæÇ ãóÇ ØóÇÈó áóßõã ãøöäó ÇáäøöÓóÇÁ ãóËúäóì æóËõáÇóËó æóÑõÈóÇÚó ÝóÅöäú ÎöÝúÊõãú ÃóáÇøó ÊóÚúÏöáõæÇú ÝóæóÇÍöÏóÉð
“Na ikiwa mnaogopa kuwa hamtowafanyia mayatima uadilifu, basi oeni mnao wapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane. na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu.”
Na hii ni kwa sababu wakati wa ujahilia, mwanamume alikuwa akilea mwanamke yatima nyumbani kwake, kisha binti huyo akishakuwa akapendezwa na uzuri wake na mali yake, mlezi wake hutaka kumuoa kwa sababu ya kujiepusha na gharama za kumlisha na kumvisha, na kwa vile yeye ndiye mlezi na msimamizi wa mambo yake, alikuwa akiruhusiwa kufanya hivyo. Kwa hivyo anamuoa kwa ajili ya mali yake na uzuri wake bila ya kulipa mahari wala kulipa haki yoyote katika haki zake. Ndipo Mwenyezi Mungu Alipokataza kitendo hicho Akaamrisha kuwafanyia uadilifu na kuwalipa mahari kwa ukamilifu kama wanavyolipwa wanawake wengine. Na kama hawataki basi wakaoe wanawake wengine wasiokuwa wao.
ÝóÇäßöÍõæÇ ãóÇ ØóÇÈó áóßõã ãøöäó ÇáäøöÓóÇÁ ãóËúäóì æóËõáÇóËó æóÑõÈóÇÚó
‘basi oeni mnao wapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane’
Kama vile Uislamu ulivyokataza mwenendo huu usiokuwa na uadilifu ndani yake kwa mayatima wanawake, mkabala wake ulikataza pia njia nyingine ambayo mtu alikuwa akilea yatima ambaye hana uzuri wa hivyo wala hana mali, au anakuwa mzuri kidogo na ana mali kidogo, kisha mlezi huyo akataka kumuowa. Mwenyezi Mungu Akateremsha aya isemayo:
æóíóÓúÊóÝúÊõæäóßó Ýöí ÇáäøöÓóÇÁ Þõáö Çááøåõ íõÝúÊöíßõãú Ýöíåöäøó æóãóÇ íõÊúáóì Úóáóíúßõãú Ýöí ÇáúßöÊóÇÈö Ýöí íóÊóÇãóì ÇáäøöÓóÇÁ ÇáøóáÇÊöí áÇó ÊõÄúÊõæäóåõäøó ãóÇ ßõÊöÈó áóåõäøó æóÊóÑúÛóÈõæäó Ãóä ÊóäßöÍõæåõäøó æóÇáúãõÓúÊóÖúÚóÝöíäó ãöäó ÇáúæöáúÏóÇäö æóÃóä ÊóÞõæãõæÇú áöáúíóÊóÇãóì ÈöÇáúÞöÓúØö æóãóÇ ÊóÝúÚóáõæÇú ãöäú ÎóíúÑò ÝóÅöäøó Çááøåó ßóÇäó Èöåö ÚóáöíãÇð
Wanakuuliza nini sharia ya wanawake. Sema: Mwenyezi Mungu ana kutoleeni fatwa juu yao, na mnayo somewa humu Kitabuni kukhusu mayatima wanawake ambao hamwapi walicho andikiwa, na mnapenda kuwaoa, na kukhusu wanyonge katika watoto, na kwamba mwasimamie mayatima kwa uadilifu. Na kheri yoyote mnayo fanya Mwenyezi Mungu anaijua
Annisaa -127
Na katika tafsiri nyingne, wafasiri wa Qurani tukufu wamesema pia kuwa pale Mwenyezi Mungu Alipokataza dhulma na kutowafanyia uadilifu mayatima, Alikataza pia dhulma na kutowafanyia uadilifu wanawake kwa wenye kuoa zaidi ya mke mmoja.
Kwa hivyo kama ilivyoamrishwa kuwafanyia uadilifu mayatima, ikaamrishwa pia kuwafanyia uadilifu wanawake kwa wenye kuoa zaidi ya mke mmoja. Uadilifu unalazimika katika yote mawili, na huu ndio uhusiano uliopo katika aya baina ya kutowafanyia uadilifu mayatima na kuoa mke zaidi ya mmoja.
Imesimuliwa na Imam Bukhari kutoka kwa Urwa bin Al Zubeir kuwa alimuuliza Bibi Aisha juu ya kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:
æóÅöäú ÎöÝúÊõãú ÃóáÇøó ÊõÞúÓöØõæÇú Ýöí ÇáúíóÊóÇãóì Na ikiwa mnaogopa kuwa hamtowafanyia mayatima uadilifu .
Akasema (Bibi Aisha): “Ewe mwana wa dada yangu, yatima huyu anakuwa ndani ya nyumba ya mlezi wake akishirikiana naye katika mali yake, akapendezwa na mali yake na uzuri wake, na mlezi wake akataka kumuoa bila ya kufanya uadilifu katika kumpa mahari yake akampa kama anavyowapa wengine. Wakakatazwa kuwaoa isipokuwa kama watawafanyia uadilifu, na kuwapa kile wanachostahiki katika mahari, na wakaamrishwa kuwaoa wanaowapenda katika wanawake wasiokuwa wao.” Amesema Urwa: kuwa Bibi Aisha alisema: “Hakika watu walimuendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swallah Llahu alayhi wa sallam) kutaka fatwa juu ya aya hii, ndipo Mwenyezi Mungu Alipoteremsha: íóÓúÊóÝúÊõæäóßó Ýöí ÇáäøöÓóÇÁ Wanakuuliza nini sharia ya wanawake. Akasema Bibi Aisha: “Kauli ya Mwenyezi Mungu katika aya hii pale Aliposema “na mnapenda kuwaoa,” kwa ajili ya uyatima wao ikiwa ni mpungufu wa mali au uzuri. (Lakini) Walikatazwa kuwaoa wale waliopendezwa na mali yao au uzuri wao katika wanawake isipokuwa kama watawafayia uadilifu kwa ajili ya kupenda kwao kuwaoa ikiwa wana upungufu wa mali au uzuri.”
Bukhari na Muslim
2- Wakasema: ‘Uislamu umemdhulumu mwanamke pale uliporuhusu kuoa mke zaidi ya mmoja na kuziumiza nyoyo zao, kisha haukufanya uadilifu wa kuwaruhusu na wao kuolewa na mume zaidi ya mmoja!!!’
Tunasema kwanza: Nani aliyemdhulumu mwanamke? Watasema: Uislamu.
Tunasema: Na huu Uislamu ni dini ya nani? Watajibu: Dini ya Mwenyezi Mungu.
Tunasema: Kwa hivo aliyemdhulumu mwanamke ni Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala :
ßóÈõÑóÊú ßóáöãóÉð ÊóÎúÑõÌõ ãöäú ÃóÝúæóÇåöåöãú Åöä íóÞõæáõæäó ÅöáÇ ßóÐöÈðÇ [ÇáßåÝ: 5
öNi neno kuu hilo litokalo vinywani mwao. Hawasemi ila uwongo tu
Al Kah’f -5
Tunasema pia: Je Mwenyezi Mungu Anaweza kudhulumu? Mwenyezi Mungu anasema:
æóáÇ íóÙúáöãõ ÑóÈøõßó ÃóÍóÏðÇ
Na Mola wako Mlezi hamdhulumu yeyote
Al Kah’f-49
Na Akasema katika aya nyingine:
æóãóÇ ÑóÈøõßó ÈöÙóáøóÇãò áøöáúÚóÈöíÏö
Wala Mola wako Mlezi si mwenye kuwadhulumu waja
Fussilat – 46
Na katika hadith Al Qud’sy Amesema:
(íÇ ÚÈÇÏí Åäí ÍÑãÊ ÇáÙáã Úáì äÝÓí æÌÚáÊå Èíäßã ãÍÑãÇ ÝáÇ ÊÙÇáãæÇ(
Enyi waja wangu, Hakika Mimi nimejiharamishia dhulma na Nikaijaalia iwe haramu baina yenu, kwa hivyo msidhulumiane.
Muslim
Kisha tunasema: Na kwa nini Mwenyezi Mungu Aliyetukuka amdhulumu mwanamke? Kisha kwa maslahi ya nani? Amdhulumu kwa maslahi ya mwanamume? Au kwa ajili ya uzuri wake mwanamume huyu kama wanavyosema, au kwa sababu gani?
Kwani mwanamke si kiumbe cha Mwenyezi Mungu, na mwanamume pia ni kiumbe cha Mwenyezi Mungu? Kwa nini basi Mwenyezi Mungu amdhulume kiumbe kwa ajili ya kumpendelea kiumbe mwingine? Na kwani Uislamu umehalalisha kuoa mke zaidi ya mmoja kwa ajili ya maslahi ya mwanamume, au kwa ajili ya maslahi ya mwanamke katika daraja ya mwanzo?
Tuelimisheni enyi watu. Munayatizama vipi mambo haya, au ni wapungufu wa akili?!!
Ifuatayo ni kauli ya Mwenyezi Mungu Aliposema: “Basi oeni mnao wapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane.”
Hapa Mwenyezi Mungu alifaridhisha au aliwajibisha? Hii ni rukhsa. Kwa hivyo kuoa mke zaidi ya mmoja si wajibu wala si fardhi, bali ni rukhsa iliyotolewa na Mwenyezi Mungu.
Kisha tunauliza: Kwani ni dini ya Kiislamu peke yake iliyoamrisha kuoa mke zaidi ya mmoja au ndiyo iliyoanzisha mwenendo huu?
Waislamu na watu wote kwa ujumla, wale wenye kufuata dini mbali mbali na wasiokuwa na dini wanaoa wake zaidi ya mmoja, tena wao wanaoa bila ya kiwango wala hesabu, bila kutimiza wajibu na bila ya kufanya uadilifu. Wanaoa bila kufuata kanuni wala kulinda uhusiano wa mke na mume, na bila ya kuulinda ubinadamu.