Funga Ya ‘Ashuraa
Baina Ya Wenye Kupinga
Na Wenye Kuunga Mkono
Muhammad Faraj Salem Al Saiy
Tukio
la ‘Ashuraa ni
tukio muhimu sana kwa walimwengu
wote kutoka wakati wa Mtume
wa Mwenyezi Mungu Muusa (‘Alayhi swalaatu was-salaam) hadi wakati wa
Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi
wa sallam).
Ndani ya siku hii
aliuliwa kwa
dhulma Al-Hussayn (Radhiya Allaahu ‘Anhu) kipenzi cha Mtume wa Mwenyezi
Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam) na bwana wa vijana wa
peponi. Aliyekuwa mfano mwema wa kuigwa na Ummah wote
kutokana na hikmah yake na
wema wake aliourithi kutoka kwa babu
yake Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi
wa sallam), na sisi tunajitenga
mbali kabisa na kila aliyeshiriki
katika mauaji hayo mpaka siku
ya Qiyaamah.
Masuala sasa yanakuja:
Yafuatayo ni majibu
ya masuala yaliyotangulia:
1 - Kutoka kwa Abul-Hassan
(‘Alayhi swalaatu
was-salaam) kuwa amesema:
"Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam) ameifunga siku ya ‘Ashuraa."
[Tahdhiybul-Ahkaam 29/4,
Al-Istibsaar 134/2, Al-Wafi
13/7, Wasailush-Shia 337/7, Jami’ah
Ahaadiythush-Shia 475/9, Al-Hadaaiqun-Naadhirah
370-371/13, Funga ya ‘Ashuraa ukurasa 112].
2 - Kutoka kwa Abu Ja’afar
(‘Alayhi swalaatu
was-salaam) kuwa amesema:
"Funga ya Ashura inafuta madhambi ya mwaka
mzima."
[Tahdhiybul-Ahkaam 300/4,
Al-Istibsaar 134/2, Jami’ah
Ahaadiythush-Shia 475/9, Al-Hadaaiqun-Naadhirah
371/13, Swiyaamul-‘Ashuraa ukurasa
112, Al-Wafi 13/7, Wasailush-Shia
337/7].
3 - Kutoka kwa As-Swaadiq
(Rahimahu Allaahu) kuwa amesema: "Mwenye kufunga Muharram anajikinga na kila
ovu."
[Wasailush-Shia 347/7, Al-Hadaaiqun-Naadhirah
377/13, Jami’ah Ahaadiythush-Shia
474/9].
4 - Na Kutoka kwa Mtume
wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi
wa sallam) kuwa amesema: ((Swalah bora
baada ya zilizofaridhishwa ni ya usiku wa
manane, na funga bora baada
ya mwezi wa Ramadhaan ni
Funga ya mwezi wanaouita Muharram.))
[Masdari zilizotangulia kutajwa]
Baada ya kuzisoma kauli
hizi za maulamaa
mbali mbali wenye kusifika wa Madhehebu
ya Kishia walizoziandika ndani ya vitabu mbali
mbali vinavyoheshimika, inatuwia wazi kuwa
haijuzu kuikanusha swaumu hii ya
‘Ashuraa na kudai kuwa eti
imeanzishwa na watawala wa kabila
la Bani Umayyah.
Funga hii ni Sunnah yenye uhakika
iliyothibiti ndani ya vitabu vya
madhehebu mbali mbali ya Kiislamu,
na Mtume wa Mwenyezi Mungu
(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam) ambaye ni mfano mwema
wetu sisi wa kumfuata, ameifunga
siku hii na akatutaka na
sisi pia tuifunge.
Anaweza mtu kwa kuuendekeza moyo wake na kwa kufuata
matamanio ya nafsi yake akasema
kuwa: “Hizi ni hadithi za
uongo zilizozushwa tu.” n.k, lakini
mwenye kuutafuta ukweli mara baada
ya kuiona haki hatoweza kusema
maneno haya, bali atasalimu amri na kuifuata
Sunnah hii tukufu. Kwani moyo
wa aliyeamini
kikweli haukubali kufuata matamanio ya nafsi. Haukubali
kufuata isipokuwa haki tu itokayo
kwa Mola
wake kupitia kwa Mtume wake mtukufu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam).
Ewe ndugu yangu Muislamu! kumbuka kuwa
hapana baada ya haki isipokuwa
upotovu, na uikumbuke kauli ya Imaam ‘Aliy
(Radhiya Allaahu ‘Anhu) aliposema:
"Ifungeni
‘Ashuraa siku ya tisa na ya kumi
akiba ya maneno kwani inafuta
madhambi ya mwaka uliotangulia.” [Mustadrakul-Wasaail 1/594 na Jami’ah Ahaadiythush-Shia 475/9].
Na kutoka kwa Ibni
‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘Anhu) kuwa amesema: "Utakapouona mwezi wa Muharram anza kuhesabu, na itakapotimia ya tisa basi
funga kuanzia asubuhi ya siku
hiyo." Anasema mwenye kuisimulia Hadiyth hii kuwa
aliuliza: "Mtume wa Mwenyezi Mungu
alifunga hivi pia?" Akasema Ibni ‘Abbaas (Radhiya
Allaahu ‘Anhu): "Ndiyo." [Iqbaalul-A’amaal ukurasa
554, Wasailush-Shia 347/7, Mustadrakul-Wasaail
594/1].
Kumbuka pia ndugu yangu
kuwa riwaya zote zilizokuja zenye kuitilia nguvu swaumu hii
zimekuja kwa njia sahihi na
zile zote zenye kuipinga swaumu hii zimekuja
kwa njia dhaifu kama alivyokiri
Ash-Shaykh Al-Hajj As-Sayyid
Muhammad Ridha Al-Hussayn
Al-Hairi katika kitabu chake kiitwacho
Najatlul-Ummah Fiy Iqaamatul-Azaa Li A’al Hussayn Wal-Aimmah ukurasa wa 145, 146 mpaka 148.
Je
ndugu yangu baada ya ushahidi
huu utatanguliza maneno ya watu
wa kawaida
au utatanguliza maneno ya mbora wa
viumbe vyote (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam)?
Tanbiyh:
Mauaji ya Al-Hussayn (Radhiya Allaahu ‘Anhu) ni
mojawapo ya masaibu makubwa waliyokumbwa nayo Waislamu, na kubwa
zaidi ni kuuliwa kwa baba
yake Imaam ‘Aliy bin Abu Twaalib (Radhiya Allaahu ‘Anhu) na kubwa
kupita yote ni kufariki kwa
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam). Muislamu anapokumbwa na
masaibu anatakiwa akumbuke masaibu haya matatu ili
aweze kuona na kuhisi kuwa
masaibu aliyokuwa ndani yake ni
madogo sana akiyalinganisha na hayo.
Hata hivyo Mwenyezi Mungu Ametufundisha katika kitabu chake
kitukufu kuwa Muislamu anapokumbwa na masaibu
aseme: "Innaa liLlaahi wa innaa
ilayhi raaji’uun."
Mwenyezi Mungu Anasema: {{Ambao uwapatapo msiba husema: "Hakika sisi ni wa Mwenyezi
Mungu na kwake Yeye sisi
tutarejea.” Hao juu yao zitakuwa barakah zitokazo kwa Mola
wao na rehema,
na ndio wenye
kuongoka.}} [Al-Baqarah:
156-157]
Na kumbuka kuwa Al-Hussayn (Radhiya Allaahu ‘Anhu) ni shahiyd
aliyeko peponi akineemeshwa na Mola wake, na kwamba
ishapita miaka elfu nyingi tokea
alipouliwa kwa dhulma, na wajibu
wa Muislamu ni kusubiri na
kuomba na sio kutukana na
kukufurisha.
Anasema
At-Tijani ambaye ni mwandishi
maarufu wa kitabu 'Then I was guided' (Thumma
Ihtadayat) kuwa: "Mengi kati ya
wanayofanya watu hivi sasa katika
kuomboleza kifo cha Al-Hussayn (Radhiya Allaahu ‘Anhu) hayakupata kufanywa na yeyote tokea
alipokufa Mtume wa Mwenyezi Mungu
hadi siku hii ya leo
na wala hayakuwahi
kufanywa na Al-Hassan wala Al-Hussayn (Radhiya Allaahu ‘Anhu).”
Anasema kuwa mmoja katika
aliyeshuhudia mauaji hayo yaliyofanyika Karbala amesema: "Nimehudhuria mkusanyiko usiopata kuhudhuriwa na
mtu yeyote, na nikashuhudia kwa jicho langu
yale ambayo hakupata kuyashuhudia mtu yeyote hapo
Karbala alipouliwa baba yangu na ami
zangu na ndugu zangu wote,
na nikaona masaibu yanayoweza kuyaondoa majabali."
Anasema
At-Tijani: "Juu ya yote hayo
aliyoyaona lakini hajapata kufanya haya yanayofanywa siku hizi wala
kuamrisha watu wake kufanya hivyo." [Kitabu cha 'Kullu-l-huluul' ukurasa wa
151].
Anaongeza
At-Tijani: "Hata ajitahidi vipi mwenye kujitahidi, lakini lazima aelewe
kuwa hayo wanayotenda katika kupiga vifua na kuomboleza na kulaani na
kutukana sio katika maamrisho ya diyn hata
kama watatoa fatwa wenye kutowa, lazima
waelewe kuwa hayo ni katika
hisia zinazopindukia mipaka." [Kitabu cha 'Kullu-l-huluul' ukurasa wa 148].